DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan, amewataka wananchi wa Wilaya ya Kondoa kuendelea kuamini chama hicho kwa kuchagua wagombea wake kuanzia ngazi ya urais, ubunge hadi udiwani, na kwamba chama hicho hakiendi na “tone tone,” bali kinamimina fedha.
Akihutubia mkutano wa kampeni leo Jumapili, Agosti 31, 2025, Samia amesema chama hicho kimejipambanua kwa kusimamia maendeleo ya wananchi kwa vitendo, huku akisisitiza kuwa CCM haendi kwa “tone tone,” bali inamimina fedha za maendeleo kwa miradi mikubwa ya kijamii na kiuchumi.
"Ndugu zangu wa Kondoa, hapa tuna mafiga matatu. Kwanza mimi mgombea urais, pia nawaombea kura wabunge wenu ambao ni vifaa vya kazi. Lakini pale tunapomimina fedha ndani ya Wilaya ya Kondoa, kwa sababu sisi hatuendi na tone tone, tunamimina fedha. Kwa hiyo, tunapomimina fedha ndani ya Kondoa, madiwani wenu ndiyo watakaosimamia utekelezaji wake. Kwa hiyo, naomba kura zenu kwa wote," amesema Samia.
Akihutubia mkutano wa kampeni leo Jumapili, Agosti 31, 2025, Samia amesema chama hicho kimejipambanua kwa kusimamia maendeleo ya wananchi kwa vitendo, huku akisisitiza kuwa CCM haendi kwa “tone tone,” bali inamimina fedha za maendeleo kwa miradi mikubwa ya kijamii na kiuchumi.
"Ndugu zangu wa Kondoa, hapa tuna mafiga matatu. Kwanza mimi mgombea urais, pia nawaombea kura wabunge wenu ambao ni vifaa vya kazi. Lakini pale tunapomimina fedha ndani ya Wilaya ya Kondoa, kwa sababu sisi hatuendi na tone tone, tunamimina fedha. Kwa hiyo, tunapomimina fedha ndani ya Kondoa, madiwani wenu ndiyo watakaosimamia utekelezaji wake. Kwa hiyo, naomba kura zenu kwa wote," amesema Samia.