SeliSelina
JF-Expert Member
- Jun 27, 2014
- 418
- 898
View: https://www.facebook.com/share/v/17qxXJt2YN/
kuna video nyingi sana, huo mfano mmoja.
Msikilizeni huyu dada, anaelezea kwa kirefu kiasi gani maandamano yalivyoandaliwa na baadhi ya diaspora wa Tanganyika ili kuiangamiza Tanzania, kisha lawama yote amepewa samia na kmkm, na watu kuwa na visasi kuwa wa zanzibar wamewaua. Na kupandikiza chuki mbaya sana, ili watoke kwenye hii lawama, na kuahidi watalipiza kisasi.
Nimepata mshtuko mkubwa yanayoendelea kwa baadhi ya Tanzania wanaoishi nje ya Tanzania, ambao sio wazalendo hata kidogo.
lmefika watu wamechangisha pesa nyingi kuwaletea baadhi ya hawa vijana ili wafanye uhalifu wa kuichoma Tanzania kweli kweli, yote hayo mtayasikilza mkimfollow huyu dada.
Lakini ubaya zaidi wamemtaja Tundu Lisu, hapo wamemchomea kabisa na chama cha chadema.
kwa kweli hili halikubaliki hata kidogo, kwa walichofanya diaspora ambao kumbe wanashirikiana na Mange Kimambi na diaspora waishio Marekani.
Mimi fikra zangu kuwa tunataka kuiondoa CCM madarakani na nini tunataka, kumbe watu fikra zao ziko kwengine, ndio maana maandamano yakafeli sana na wakafa watu wengi sana, kutokana kutokuwa na nia safi ya nchi yetu. Kuwa na chuki, hasada.
na kuwahusudu pia baadhi ya wa Tanzania wenzetu kwenye mali zao, hii ni sumu kwa kweli.
Tanzania ni nchi yetu tunatakiwa tuipende na tujifaharishe nayo pahala popote, lakini kumbe baadhi ya watanzania wanataka ichomoke kweli kweli
HAWA NI MAGAIDI
MAGAIDI
MAGAIDI
kitendo kilichofanywa kimenikasirisha kweli kweli.
HAWANA TOFAUTI NA HAO CCM AMBAO WANATEKA, WANAUA, WANAPORA, HAWAJALI N.K.
VIPI UTAANDAA MAANDAMANO YA KUITEKETEZA NCHI?
TUSITUKANANE MAANA SIJAMTUKANA MTU NILICHOKIELEZA NI KILE HUYU DADA AMBAE NA YEYE ALIKUWEMO KWENYE HUO MCHAKATO ILA AKAONA WENZAKE WANAENDA NJIA SIO AKAAMUA KUJITOA INAVYOONYESHA, NDIO AKALETA USHAHIDI WOTE KWA WANACHOFANYA WENZAKE AMBAO WANATAKA MAANDAMANO MENGINE.
IT IS VERY SAD
HII PICHA HAIHUSIANI NA NA HAYA MAELEZO,