Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 971
- 1,945
Hii hadithi tumeisikia kuanzia Nchi imepata Uhuru. Najiuliza umeme utakasambazwa nchi nzima ndo huu huu unaokatika kila baada ya masaa nane au?
My take suala sio kusambaza umeme swali ni huo umeme unaosambazwa utaweza kukidhi mahitaji ya Watanzania nchi nzima na utakuwa reliable?
=======================
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa nishati ya umeme itasambazwa katika maeneo yote ili wananchi kupata huduma hiyo kwa uhakika zaidi.
Dkt Samia ameeleza hayo leo Jumanne Septemba 9,2025 akiwahutubia wananchi wa Manyoni mkoani Singida katika mwendelezo wa kampeni zake za kusaka kura za urais, akiwa siku ya kwanza mkoani humo.
“Kama kuna vitongoji ambavyo havijapata umeme, tutakwenda kuisambaza nishati hii Tanzania yote,” amesema Dkt Samia huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi wa Manyoni waliofuruka kumsikiliza. Kwa asilimia kubwa Serikali imefanikiwa kufikisha umeme karibu vijiji vyote nchini na hivi sasa wapo katika mchakato wa kumaliza vitongoji.
Katika hatua nyingine, huku akiendelea kushangiliwa na wananchi wa Manyoni, Dkt Samia amewaahidi wakazi wa Singida kuboresha sekta za elimu, afya na maji ili kuhakikisha wanazipata huduma hizo kwa ufanisi zaidi. “Kadri idadi ya watu inavyongezeka na ndivyo mahitaji yanyavyokuwa, mkitupa ridhaa tutahakikisha tunawatumikia watu ikiwemo kupata huduma bora za afya.
“Tulisema tutaanza na bima ya afya kwa wote kwa majaribio ndani ya siku 100, mkitupa kura zenu.Tutaangalia mwenendo unakwendaje, ukiende vizuri tutafungua nchi nzima, nani kama CCM,” aliuliza Dkt Samia huku akiitikiwa na ‘hakuna…’
My take suala sio kusambaza umeme swali ni huo umeme unaosambazwa utaweza kukidhi mahitaji ya Watanzania nchi nzima na utakuwa reliable?
=======================
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa nishati ya umeme itasambazwa katika maeneo yote ili wananchi kupata huduma hiyo kwa uhakika zaidi.
Dkt Samia ameeleza hayo leo Jumanne Septemba 9,2025 akiwahutubia wananchi wa Manyoni mkoani Singida katika mwendelezo wa kampeni zake za kusaka kura za urais, akiwa siku ya kwanza mkoani humo.
“Kama kuna vitongoji ambavyo havijapata umeme, tutakwenda kuisambaza nishati hii Tanzania yote,” amesema Dkt Samia huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi wa Manyoni waliofuruka kumsikiliza. Kwa asilimia kubwa Serikali imefanikiwa kufikisha umeme karibu vijiji vyote nchini na hivi sasa wapo katika mchakato wa kumaliza vitongoji.
Katika hatua nyingine, huku akiendelea kushangiliwa na wananchi wa Manyoni, Dkt Samia amewaahidi wakazi wa Singida kuboresha sekta za elimu, afya na maji ili kuhakikisha wanazipata huduma hizo kwa ufanisi zaidi. “Kadri idadi ya watu inavyongezeka na ndivyo mahitaji yanyavyokuwa, mkitupa ridhaa tutahakikisha tunawatumikia watu ikiwemo kupata huduma bora za afya.
“Tulisema tutaanza na bima ya afya kwa wote kwa majaribio ndani ya siku 100, mkitupa kura zenu.Tutaangalia mwenendo unakwendaje, ukiende vizuri tutafungua nchi nzima, nani kama CCM,” aliuliza Dkt Samia huku akiitikiwa na ‘hakuna…’