Samia anasema tuna undugu na Waarabu; lakini ni tangu lini tumekuwa na undugu na Waarabu? Kwahiyo hapa anataka kusema kwamba amewapa waarabu wawekeze kwasababu ni ndugu zake!? Kwanini Rais wa hii nchi akili zake zimejaa undugu na nepotism kwenye kufanya maamuzi ya msingi ya nchi !?
Hafai kuwa kiongozi.
Hafai kuwa kiongozi.
- Tunachokijua
- Machi 12, 2026 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan alishiriki katika hafla ya kupokea ripoti ya ya tume ya mgogoro wa ardhi Ngorongoro na kisha kupata nafasi ya kuhutubia.
Madai
Kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram imeibuka grafiki yenye utabulisho wa kituo cha ITV ikiwa na inayodaiwa na nukuu ya Rais Samia akisema kuwa "Ngorongoro tumewapa ndugu zetu waarabu wawekeze.
Uhalisia: Potoshi
Ufuatiliaji umebaini kuwa grafiki hiyo si halisi na haijachapishwa na kituo cha ITV kama inavyoonokeana.
Grafiki hiyo ni ya kughushi na haijachapishwa na ITV na pia maneno hayo hayajatamkwa na Rais Samia katika tukio hilo la kupokea ripoti.
Ufuatiliaji kwa njia ya kidigitali umebaini kuwa hakuna chanzo chochote kilichochapisha taarifa ama nukuu hiyo kama inavyodaiwa.