Sanda Matuta
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 949
- 142
Salamu na watolea,malenga mlio tukuka.
Javini nimekaribia,pumzi nimeshashusha.
Mwito kuuitikia,Kijijini umetoka.
Sambusa yaleta jaa,mengine nayo kadhalika.
Mbona mna kondeana,wakati vyote chakula?
Bado mna kasumba,vyakula kunyanyapaa?
Mdomoni vyaingia,tumbo kwenda vimbisha.
Chooni enda vitupa,muda ukishafika.
Kula tena tatamani,hamu wala haitoisha.
Sambusa zilizo nona,kwa mafundi wakupika.
Kumi kumi wakikupa,kuvimbilwa si ugonjwa.
Takula tena na tena,hamu haitoisha.
Mihogo nenda chimbua,na jikono kuiweka.
Tia nazi na mafuta,katu shibe haitaleta.
Jaribu ya kuchemsha,au mdomoni kutafuna.
Bara hata Jangombe,kote nenda tafuta.
Matunda yana hadaa,machoni yana pendeza.
Mtini utapopoa,nyumbani nenda vundika.
Utakula kwa madaha,mchanyato ulopendeza.
Tumbo kwenda vuruga,chooni taenda harisha.
Mtabadilisha majina,vyakula mnavikweza.
Shibe ita walevya,njaa itawalegeza.
Vitumbua utatamani,upate japo na togwa.
Sambusa na vinevyo,majina hayo manjonjo.
Javini nimekaribia,pumzi nimeshashusha.
Mwito kuuitikia,Kijijini umetoka.
Sambusa yaleta jaa,mengine nayo kadhalika.
Mbona mna kondeana,wakati vyote chakula?
Bado mna kasumba,vyakula kunyanyapaa?
Mdomoni vyaingia,tumbo kwenda vimbisha.
Chooni enda vitupa,muda ukishafika.
Kula tena tatamani,hamu wala haitoisha.
Sambusa zilizo nona,kwa mafundi wakupika.
Kumi kumi wakikupa,kuvimbilwa si ugonjwa.
Takula tena na tena,hamu haitoisha.
Mihogo nenda chimbua,na jikono kuiweka.
Tia nazi na mafuta,katu shibe haitaleta.
Jaribu ya kuchemsha,au mdomoni kutafuna.
Bara hata Jangombe,kote nenda tafuta.
Matunda yana hadaa,machoni yana pendeza.
Mtini utapopoa,nyumbani nenda vundika.
Utakula kwa madaha,mchanyato ulopendeza.
Tumbo kwenda vuruga,chooni taenda harisha.
Mtabadilisha majina,vyakula mnavikweza.
Shibe ita walevya,njaa itawalegeza.
Vitumbua utatamani,upate japo na togwa.
Sambusa na vinevyo,majina hayo manjonjo.