Sam Mahela adai Kikwete alitoa mil 20 kila Kijiji

Ki Mun

JF-Expert Member
Oct 6, 2014
3,443
4,384
Wanahabari wa TZ hakika ni kichefuchefu...usiku huu katika kipindi cha DK.45 cha ITV, presenter wa kipindi hicho Sam Mahela amedai kuwa wakati wa JK kulikuwa na mpango wa kutoa mil. 20 kwa kila kijiji Tanzania Bara - amechapia hilo wakati akimhoji Bi.Bengi Issa ambaye ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji kuhusu Mpango wa kutoa mil.50 kwa kila kijiji; hoja yake ilikuwa ni kwamba kama Mpango wa JK wa "mil.20 kwa kijiji" ulishindwa, Magufuli atabadili nini ili mil.50 kwa kila kijiji nao usiwe ni mpango hewa.

Siku ya Kupatwa Jua watangazaji wa kipindi cha Jahazi cha Clouds Media walihangaika mno kuelezea jinsi kupatwa kwa jua kunavyotokea...ajabu pamoja na kuonekana wazi hawaelewi chochote kuhusu hilo tukio lakini walijitia kujua na wakaishia kupotosha. Sasa mimi nauliza swali, kwanini mtu usifanye utafiti wa kutosha na kujielimisha kabla ya kusikika kwenye mass media kujadili mada asiyoijua na kuishia kupotosha?

Ajabu eti hawa ndo baada ya siku chache unasikia kateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, au Mwandishi wa hotuba za Rais, au Mkurugenzi wa Jiji...huu kama si uchochezi wa wazi wazi ni kitu gani?
 
....mwingine alimhoji mjiolojia kutoka wakala wa jiolojia tz juu ya tetemeko la bukoba alafu mwishoni anakazia kwa kusema hiyo ni ripoti ya kwanza kutoka mamlaka ya hali ya hewa tz!.
 
In every general rule, there are always an exception to the general rule! .Hivyo ni kweli wengi wa waandishi wetu wa habari ni majanga, ila pia tunao waandishi wachache wazuri and are doing a good job!. Usiwahukumu waandishi wote kwa kutumia hukumu ya tenga la samaki kwamba mmoja akioza, wote wameoza! .
Pasco
 
In every general rule, there are always an exception to the general rule! .Hivyo ni kweli wengi wa waandishi wetu wa habari ni majanga, ila pia tunao waandishi wachache wazuri and are doing a good job!. Usiwahukumu waandishi wote kwa kutumia hukumu ya tenga la samaki kwamba mmoja akioza, wote wameoza! .
Pasco
Ceritis peribus
 
Mkorogo unamuathiri....halafu nae pia ni binadam,ameona wenzake walioimba pambio wameula ukurugenzi, nae analazimisha ili akumbukwe...
 
....mwingine alimhoji mjiolojia kutoka wakala wa jiolojia tz juu ya tetemeko la bukoba alafu mwishoni anakazia kwa kusema hiyo ni ripoti ya kwanza kutoka mamlaka ya hali ya hewa tz!.
Ina maana hakujua anamhoji nani ama???
 
In every general rule, there are always an exception to the general rule! .Hivyo ni kweli wengi wa waandishi wetu wa habari ni majanga, ila pia tunao waandishi wachache wazuri and are doing a good job!. Usiwahukumu waandishi wote kwa kutumia hukumu ya tenga la samaki kwamba mmoja akioza, wote wameoza! .
Pasco


Nashukuru hapo kwenye RED
 
Mnawalaumu waandishi bure wapo wengine wapo vizuri kama tasnia zingine tuu mbona hata maprofesa nao wengi vihiyo tuu mwingine juzi kasema Deni kubwa la Taifa sio mzigo kwa Taifa au kwa kuwa ni Prof mnaona sawa tuu...vivyo hivyo wanasheria,wahasibu,mainjinia kote huko kuna vihiyo hakuna sehemu iliyo salama...
 
Bora hata huyo Sam Mahela, kuna vituo hivi ni balaa kuna vihiyo kuliko kawaida aisee:-
1: Clouds media
2; Uhuru media
3: TBC
 
Back
Top Bottom