Sala ya siku 3, je kama nchi tuna nini? Tunaomba huku hakuna juhudi za kupambana na corona? Wenzetu wanasali au wanawekeza kwenye afya?

Mungu hubariki jitihada za mwanadamu pale anapotumia akili, nguvu na afya aliyopewa na mwenyezi Mungu.

Huombi Mungu akupe unga, mchele, au sukari. Wala huombi Mungu akupe flagyl au panadol ila unamwomba Mungu abariki jitihada zako za kilimo au kazi yako ili uwe na uwezo wa kula na kuilisha familia yako.

Unaomba ili dawa unayotumia ikafanye kazi katika mwili wa mgonjwa au Mungu awaongoze matabibu katika kumtafutia mgonjwa wako tiba sahihi, huku wewe ukihangaika kutafuta hela ya kulipia matibabu. Kushindwa kumlipia mgonjwa wako wakati una akili, nguvu na afya njema, ni kushindwa kutimiza wajibu wako. Ni dhambi.

Paulo alikuwa akishona nguo ili kupata hela ya matumizi. Pamoja na miujiza yote Mungu aliyoitenda kwa kupitia Paulo lakini Paulo alifanya kazi ili apate kuishi.

Mungu alimwokoa Nuhu na gharika kwa kumtaka atengeneze mashua. Nuhu aliokolewa na Mungu kwa kufanya kazi.

Mtoto Musa aliokolewa kwa kupitia Mama yake ambaye alitoroka naye. Akamtengenezea kikapu, akamhifadhi kwenye mto ambako binti ya Farao alizoea kwenda. Mama yake Musa ilibidi afanye kazi ili kupokea uokoaji wa Mungu.

Herode alipoamru watoto wote wa kiume wauawe, Mungu alimwambia Yusuf aondoke na Mariam kwenda Misri ili mtoto asiuawe. Mariam na Yusuf walifanya kazi ili kumwokoa mtoto Yesu.

Katika kuwaokoa Waisrael waliokuwa wakiuawa na Goliati, Daud alitengeneza kombeo alilolitumia kurushia jiwe. Na jiwe hilo Mungu akalipatia nguvu, na hata kumwua Goliati. Daud alifanya kazi ili kuwaokoa wana wa Israel.

Wakati mbalimbali Waisrael walipoonewa na maadui zao, waliandaa jeshi lao. Walienda mstari wa mbele. Walipigana, huku makuhani wakiomba. Mungu alibariki jitihada zao, hata wakaweza kushinda vita. Walifanya kazi.

Bikira Maria, alipewa nafasi ya kuwa mbarikiwa kuliko wanawake wote. Na baraka hiyo aliipata baada ya kukubali kubeba mimba, kutembea nayo kwa miguu umbali mrefu mpaka Betlehem, na kwenda kujifungulia kwenye zizi la wanyama. Hakushtukia mtoto yupo mkononi. Alifanya kazi. Alitumia akili pia.

Mungu wetu hutafuta mahali pa kuweka baraka na neema katika jitihada mbalimbali tunazozifanya. Kama hatujapatengeneza mahali pa Mungu kushushia baraka, neema na ulinzi wake, kamwe hatutapata baraka na wala hutapokea neema wala ulinzi wake.

Kutotimiza wajibu wako ni dhambi.

Kama wewe ni kiongozi mkuu wa nchi, wajibu wako mkuu ni upi katika kipindi hiki cha janga la Covid 19? Usipotimiza wajibu huo, unatenda dhambi.

Kama wewe ni kiongozi wa kiimani, wajibu wako kwa wakati huu ni upi? Usipoutimiza wajibu huo ni dhambi.

Kama wewe ni tabibu, wajibu wako mkuu wakati huu ni upi? Usipoutimiza wajibu huo, umetenda dhambi.

Kama wewe ni mfanyabiashara, mkulima, mkuu wa idara, mkuu wa majeshi, Polisi, n.k; wajibu wako ni upi? Usipoutimiza, hutapokea baraka wala ulinzi au neema za Mungu.

Mimi kama mwananchi wa kawaida, mwanataluma, mfanyakazi wa kawaida, mpiga debe wa daladala, mmiliki wa biashara mbalimbali, wajibu wangu ni upi? Usipoutimiza huwezi kupata ulinzi, kupokea neema zake wala baraka zake.

Kila mmoja ana wajibu wake. Ndiyo maana ya viungo ni vingi lakini mwili ni mmoja.

Mkuu wa nchi asifanye kazi ya unabii au ukuhani. Mkuu wa mkoa asijifanye mhubiri au mwombaji, daktari asijifanye kuhani. Kila mmoja atimize wajibu wake.

Tatizo letu kwa sasa, kwa kushindwa kutimiza wajibu wetu, kila mmoja anataka awe kuhani, nabii au mhubiri.

Kila mmoja aende kwenye wajibu wake. Maana Mungu atampima kila mmoja kwa wajibu aliomwekea.

Kusali na kuomba wakati wote ni jambo muhimu lakini tunaomba kitu gani?

Tunaomba ili siku moja tukiamka tuone ugonjwa haupo? Mbona haikuwa hivyo kwa ugonjwa wa plague (1720), kipindupindu (1820), Spannish Flu (1920), kifua kikuu, au ndui iliyoua zaidi ya watu 300m.

Sisi tunamwomba Muumba wetu abariki jitihada ambazo kila mmoja anazifanya kupambana na ugonjwa huu kama vike-

Mungu awaongoze wanasayansi wafanikiwe kupata chanjo ili ugonjwa utokomezwe kama ilivyotokomezwa ndui;

Mungu awaongoze wanaofanya tafiti kuujua ugonjwa huu vizuri, wapanuliwe ufahamu ili tujue kuenezwa kwake, kujikinga kwake, na tiba sahihi;

Mungu awajalie neema ya upendo wa kweli wanaowahudumia wagonjwa wetu ili waishi katika upendo na faraja mioyoni mwao wanapowahudumia wagonjwa wetu;

Mungu awajalie ufahamu wale wenye nafasi yoyote ya kusaidia, waongozwe kwenye utayari na kujua njia sahihi za kusaidia.

Mungu hashushi ulinzi na neema kwa watu wajinga. Ndiyo maana anasema, watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Mungu wetu hujivunia watu werevu, wenye bidii na wasiokata tamaa.
Kila baada ya miaka mia.lazima janga kubwa litokee.kuna mtu aliniambia hii habari jana
 
wewe unaona sayansi imefaulu kwenye corona?
sayansi IMESHINDWA.
Na ndo maana wenyewe wanatuambia "STAY HOME FOR US".
Yaani mpaka wenyewe wamekiri kuwa corona imewashinda.
SASA TEGEMEO LINGINE NI LIPI ZAIDI YA MUNGU PEKEE MUWEZA WA YOTE?View attachment 1421462View attachment 1421463View attachment 1421464

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
Kama Sayansi imeshindwa basi fanyeni maombi halafu maisha yaendelee kama yalivyokuwa kabla ya Corona!Maana Sayansi imetueleza namna ugonjwa unavyosambaa na namna ya kujikinga,kama sayansi imeshindwa basi tupilia sayansi pembeni halafu kafanyeni maombi huku maisha yakiendelea kama kawaida!Hapa namaanisha
1.Watalii wawndelee kuingia
2.Daladala kama zamani hakuna cha level seat
3.Hakuna mambo ya kuosha mikono wala sanitizer!
4.No mask

Maana hayo manne hapo juu ni sayansi,tusiyafanye hayo maana yameshindwa tukafanye sala!
 
.
SALA
Tunaposimama mbele za Mungu, tunapaswa kuwa na imani thabiti. Imani kuhusu utendaji wa Mungu na Neema zake.

Mwenyezi Mungu ametuumba kwa upekee sana. Ametupa AKILI na UTASHI, ili tuwe tofauti na wanyama. Neno linasema Tuenende kwa AKILI, kwamba kutumia AKILI sio dhambi.

Mwenyezi Mungu anatumia AKILI alizotupa kuonesha uweza wake na nguvu zake. Kwamba, anatenda kazi zake kupitia sisi viumbe wake. Ni kama anavyotumia UZAZI kuendeleza kazi yake ya UUMBAJI ndio maana tunakemea utoaji mimba.

Sasa tunaingia magotini....

Je, tunaingia magotini kwa kuwa tuna HOFU?
Je, ni kwa kuwa ni 'maagizo' kwamba tusali?
Je, ni kumshirikisha Mungu wakati tunatumia AKILI alizotujalia ili atende kazi?
Je, tunasali kwa kuwa hatutaki tena kuwajibika?
Je, tunatumia sala kama njia ya kuficha uzembe?

Kila mmoja anajua kwa nini aingie magotini.

LAKINI

Nikumbushe, Yesu alisali, na ALITIMIZA WAJIBU.
Aliwapa watu chakula, japokuwa angeweza kutowapa chakula na kuwapulizia nguvu ya Roho Mtakatifu wawe wameshiba. Yesu ALIJIFICHA walipotaka kumpiga mawe... Hakujiachia hapo na kusema MUNGU ANAWEZA..

Wana wa Israeli walipewa mana, na walipaswa KUTOKA NJE ya nyumba zao kwenda kuzichukua...Hawakuketi kusubiri mana zijilete ndani ya nyumba zao. Ndio kusema, walipaswa waoneshe jitihada kupokea msaada wa Mungu.

Sisi WATANZANIA TUNAFANYA NINI?

Pamoja na kuliweka taifa katika maombi ambayo HAYAPASWI KUWA YA SIKU 3, bali maombi ya daima, tunatakiwa kuonesha juhudi katika kukabiliana na tatizo lililopo.

Kila siku unapotoka nyumbani kwako kuingia mtaani, jua kwamba unahatarisha maisha ya wengine. Jua kwamba unamweka muhudumu wa afya katika hatari ya kupoteza maisha.

Tujikumbushe haya kila tupigapo hatua huko mtaani: LEO NAKWENDA KUWAPELEKA WATU KADHAA KARANTINI. LEO NAKWENDA KUJIONGEZEA NAFASI YA KUWEKWA KARANTINI...

SERIKALI.

Pamoja na kuitia jina la BWANA, tujue kwamba juhudi zinahitajika. Kuhakikisha watu wanapata mask, huduma ya maji kwa bei nafuu, na WAHUDUMU wetu wapewe vifaa. Watu wapimwe, na taarifa zitoke.

Huwaambii watu wasali huku hata chai hawawezi kuimudu, au hawawezi kumudu kununua mask na vitakasa...

SALA na JUHUDI, SALA na AKILI, SALA na UKWELI.

Bibi Happy J
IMG-20200417-WA0019.jpeg


Jr
 
Naunga mkono wito wa Rais kuingia kwenye Maombi ya siku tatu, wengine hii ni desturi yetu kuendelea kumwomba Mungu, huku tukichukua tahadhari zote za lazima kujikinga na huu ugonjwa wa COVID-19.

Unapomwomba Mungu zingatia maandiko yafuatayo:-
  • 2 Mambo ya Nyakati 7:14
  • Yona 3:4-10
Huu si muda wa kulaumiana ndugu zangu....tumwombe Mungu
 
Lakini tambua kuwa Rwanda wanafanya testing, sisi hatufanyi. Kwa kuwa hatufanyi, hatujui hata idadi ya walioambukizwa. Tunasuburi mtu aumwe ndiyo apimwe au ahisiwe kuwa ameambukizwa, ndiyo apimwe.

Rwanda wanafanya testing. Wanawagundua walioambukizwa hata kabla ya kuanza kuumwa. Kwa takwimu zilizopo, mpaka sasa hakuna raia wa Rwanda aliyepoteza maisha kwa Covid 19.
Mungu hubariki jitihada za mwanadamu pale anapotumia akili, nguvu na afya aliyopewa na mwenyezi Mungu.

Huombi Mungu akupe unga, mchele, au sukari. Wala huombi Mungu akupe flagyl au panadol ila unamwomba Mungu abariki jitihada zako za kilimo au kazi yako ili uwe na uwezo wa kula na kuilisha familia yako.

Unaomba ili dawa unayotumia ikafanye kazi katika mwili wa mgonjwa au Mungu awaongoze matabibu katika kumtafutia mgonjwa wako tiba sahihi, huku wewe ukihangaika kutafuta hela ya kulipia matibabu. Kushindwa kumlipia mgonjwa wako wakati una akili, nguvu na afya njema, ni kushindwa kutimiza wajibu wako. Ni dhambi.

Paulo alikuwa akishona nguo ili kupata hela ya matumizi. Pamoja na miujiza yote Mungu aliyoitenda kwa kupitia Paulo lakini Paulo alifanya kazi ili apate kuishi.

Mungu alimwokoa Nuhu na gharika kwa kumtaka atengeneze mashua. Nuhu aliokolewa na Mungu kwa kufanya kazi.

Mtoto Musa aliokolewa kwa kupitia Mama yake ambaye alitoroka naye. Akamtengenezea kikapu, akamhifadhi kwenye mto ambako binti ya Farao alizoea kwenda. Mama yake Musa ilibidi afanye kazi ili kupokea uokoaji wa Mungu.

Herode alipoamru watoto wote wa kiume wauawe, Mungu alimwambia Yusuf aondoke na Mariam kwenda Misri ili mtoto asiuawe. Mariam na Yusuf walifanya kazi ili kumwokoa mtoto Yesu.

Katika kuwaokoa Waisrael waliokuwa wakiuawa na Goliati, Daud alitengeneza kombeo alilolitumia kurushia jiwe. Na jiwe hilo Mungu akalipatia nguvu, na hata kumwua Goliati. Daud alifanya kazi ili kuwaokoa wana wa Israel.

Wakati mbalimbali Waisrael walipoonewa na maadui zao, waliandaa jeshi lao. Walienda mstari wa mbele. Walipigana, huku makuhani wakiomba. Mungu alibariki jitihada zao, hata wakaweza kushinda vita. Walifanya kazi.

Bikira Maria, alipewa nafasi ya kuwa mbarikiwa kuliko wanawake wote. Na baraka hiyo aliipata baada ya kukubali kubeba mimba, kutembea nayo kwa miguu umbali mrefu mpaka Betlehem, na kwenda kujifungulia kwenye zizi la wanyama. Hakushtukia mtoto yupo mkononi. Alifanya kazi. Alitumia akili pia.

Mungu wetu hutafuta mahali pa kuweka baraka na neema katika jitihada mbalimbali tunazozifanya. Kama hatujapatengeneza mahali pa Mungu kushushia baraka, neema na ulinzi wake, kamwe hatutapata baraka na wala hutapokea neema wala ulinzi wake.

Kutotimiza wajibu wako ni dhambi.

Kama wewe ni kiongozi mkuu wa nchi, wajibu wako mkuu ni upi katika kipindi hiki cha janga la Covid 19? Usipotimiza wajibu huo, unatenda dhambi.

Kama wewe ni kiongozi wa kiimani, wajibu wako kwa wakati huu ni upi? Usipoutimiza wajibu huo ni dhambi.

Kama wewe ni tabibu, wajibu wako mkuu wakati huu ni upi? Usipoutimiza wajibu huo, umetenda dhambi.

Kama wewe ni mfanyabiashara, mkulima, mkuu wa idara, mkuu wa majeshi, Polisi, n.k; wajibu wako ni upi? Usipoutimiza, hutapokea baraka wala ulinzi au neema za Mungu.

Mimi kama mwananchi wa kawaida, mwanataluma, mfanyakazi wa kawaida, mpiga debe wa daladala, mmiliki wa biashara mbalimbali, wajibu wangu ni upi? Usipoutimiza huwezi kupata ulinzi, kupokea neema zake wala baraka zake.

Kila mmoja ana wajibu wake. Ndiyo maana ya viungo ni vingi lakini mwili ni mmoja.

Mkuu wa nchi asifanye kazi ya unabii au ukuhani. Mkuu wa mkoa asijifanye mhubiri au mwombaji, daktari asijifanye kuhani. Kila mmoja atimize wajibu wake.

Tatizo letu kwa sasa, kwa kushindwa kutimiza wajibu wetu, kila mmoja anataka awe kuhani, nabii au mhubiri.

Kila mmoja aende kwenye wajibu wake. Maana Mungu atampima kila mmoja kwa wajibu aliomwekea.

Kusali na kuomba wakati wote ni jambo muhimu lakini tunaomba kitu gani?

Tunaomba ili siku moja tukiamka tuone ugonjwa haupo? Mbona haikuwa hivyo kwa ugonjwa wa plague (1720), kipindupindu (1820), Spannish Flu (1920), kifua kikuu, au ndui iliyoua zaidi ya watu 300m.

Sisi tunamwomba Muumba wetu abariki jitihada ambazo kila mmoja anazifanya kupambana na ugonjwa huu kama vike-

Mungu awaongoze wanasayansi wafanikiwe kupata chanjo ili ugonjwa utokomezwe kama ilivyotokomezwa ndui;

Mungu awaongoze wanaofanya tafiti kuujua ugonjwa huu vizuri, wapanuliwe ufahamu ili tujue kuenezwa kwake, kujikinga kwake, na tiba sahihi;

Mungu awajalie neema ya upendo wa kweli wanaowahudumia wagonjwa wetu ili waishi katika upendo na faraja mioyoni mwao wanapowahudumia wagonjwa wetu;

Mungu awajalie ufahamu wale wenye nafasi yoyote ya kusaidia, waongozwe kwenye utayari na kujua njia sahihi za kusaidia.

Mungu hashushi ulinzi na neema kwa watu wajinga. Ndiyo maana anasema, watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Mungu wetu hujivunia watu werevu, wenye bidii na wasiokata tamaa.
Kwani tatizo liko wapi,Mhe.Raisi kaomba kipindi cha Siku 3 special tuombe ,siku zingine tunaendelea kuomba huku tukipambana kwa kadri roho wa maarifa atakavyotuongoza.

Tena ningeshauri Bendera zishushwe nusu mringoti ishara ya toba kwa Taifa mpaka gonjwa hili liyeyuke,kila anaeona ishara ya kitaifa anaendelea kuomba toba kimyakimya .Bila Mwenyezi Mungu kuingilia kati maarifa yenu ni bure.Juhudi zinachukuliwa ila mnataka lazima zifanane na za wenzetu ambao bado pamoja na juhud hizo mapgo yanaendelea.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo muoaji wa wanaume unajiona umetukana?

Kijana unahitaji darasa kubwa hujafkia kiwango cha kufanya mjadala na mimi
Ww shoga mjane, sina shaka na kiswahili changu, kuanzia uwezo wa kuongea, kusoma na kukiandika kwa ufasaha. Na sihitaji popote kuthibitishwa na ww, au yoyote kwani niko vizuri sana kwenye lugha hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kule Marekani mnakowategemea Ndio wanaongoza kurudisha jezi

Mimi Marekani kufa siumii maana wanaitesa sana dunia

Na nyie mhamie kule mtuachie Nchi yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnara hautajengeka, waashi wanasambaratika kwa kauli hizi za hovyo, tutasali kwa Mungu yupi kama unaanza kujipambanua kuwa wewe in mwanaccm na wengine vibaraka wa mabeberu, sawa tuseme ni hivyo sawa salini ninyi na vibaraka wasisali kisha tuone Mungu atamsikiliza nani, wote tutakufa. Hebu jiulize huko zilikoanzia dini wao hawajui kusali? Ilipoanza tu mapadri 60 walifariki! Hao watu wa Mungu, je, Mungu hawapendi?
Mimi binafsi unataka kwenda hospitali ya Mbagala Zakhiem kupima macho lakini ninaogopa, hospitali haina vifaa zaidi ya maji makavu, yaani bila sabuni! Watumishi hawana mask! Hali hiyo niliikuta nilipokwenda Mara ya kwanza wiki iliyopita.
Ni vyema tuone michango ya wananchi ikitumika kuleta matumaini ya jitihada za serikali ndipo ije na nyongeza za kusali.
 
Watanzania, Kabla ya kupiga magoti kwa Muumba wetu atuepushie janga hili kwanza tujitathimini kama tumewasamehe wale wote tunaodhani walitukosea na kuwasweka kolokoloni...kuwajeruhi wengine kubakia vilema wa maisha na wengine kuuawa huku tukiacha familia zao zikilia machozi

Tukiyajutia haya kwanza ndipo twende mbele zake tumwombe atuepushie janga hili la corona...

Vinginevyo ni kumkejeli Muumba!! am not part of....!!
 
Back
Top Bottom