Uhakika Bro
JF-Expert Member
- Mar 29, 2022
- 2,398
- 3,070
Je? mtu anaweza kuwa na furaha bila ya kuwajibika. Hapana. Hiyo haipo kabisa. Kwa nini ninasema hivyo? Kabla sijaanza naomba kuanza na ufafanuzi kiasi;
Furaha inahusianishwa na hisia za utulivu na kutosheka na kile kilichopo (what IS). Utulivu wa moyo unakuja pale ambapo mtu anahisi anao uwezo wa kuamua mazingira yake na hata kuyabadili apendavyo. Kimsingi kuyaendesha, yaani mfano anaweza kuamua kujongea au kutulia tu.
Hicho kitendo cha kuyaendesha na kuwa na uwezo wa kutia nia na matakwa binafsi kufanya mambo yatokee ndio inaitwa UWEZO.
Tukizungumzia uwezo,ninafahamu wapo watu wengi tu ikiwamo mdogo wangu mmoja wanaofikiri kwamba hiki ndio kitu cha juu kabisa. Lakini mimi nafikiri kwamba huu ni mwanzo tu. Tena ni wa pili kwa wajibu. Yaani unaanza wajibu halafu ndio uwezo. Mwenye wajibu mkubwa ndio anapata kuwa na uwezo mkubwa!
Hivyo basi uwezo wa kuyafanyia kazi matakwa ya mtu unampa kuendesha mambo na mwisho utulivu wa moyo unaopelekea FURAHA. Tafakari hilo kwa muda, na chukua hiyo point.
Jambo hili linahusiana vipi na furaha;
Mtu hujisikia furaha pale mambo yanapokuwa yanaenda kulingana na matakwa yake. Ikiwa mtu atawajibika na kuchukua jukumu la kuendesha visababishi vingi zaidi basi ataweza kuamua na kuathiri matokeo kwa kutenda impasavyo.
Watu wawili wanaweza kupokea kitu kimoja kiletacho raha, kwa mfano kufaulu alama za juu(A+) katika mtihani. Yule ambaye atakuwa na furaha ya kweli ni yule atakayewaza kuwa alifanya bidii na amewajibika kupata matokeo hayo. Yule aliyeibia mtihani na majibu hatakuwa na furaha ya kweli. Weeh! Subiri kidogo!, Huyo mtu anaweza kuwa na furaha vilevile maana naye pia akifikiri juhudi zake katika kuiba/kuangalizia huko zimempatia hiyo A+. Atakayekosa furaha hapa ni yule tu ambaye kufaulu huko ni kinyume na matakwa yake. Labda malengo yake ilikuwa kufeli.
Mfano nilioutoa juu unaweza ukakuchanganya kiasi, hebu tuangalie mfano mwingine. Mungu anafahamu kabisa kwamba watu watakuwa na furaha zaidi ikiwa watawajibika katika kuleta matokeo. Yeye angeweza kufanya kila kitu lakini bado ameruhusu na ameupa thamani kubwa mchango wa mwanadamu. Tunaomba kisha tunapokea. Tunaishi kisha tunachagua kwenda mbinguni au kufa tu (kupatwa na mauti ya pili). Mbinguni patajawa na mandhari ya furaha kwa sababu patafurika watu wawajibikaji. Kama watu wangebebwa tu na kupelekwa mbinguni bila hili wala lile wasingeiishi furaha ukilinganisha.
Katika kuishi nimejionea. Kwamba hata kama matokeo ni machungu kweli, yule mpokeaji wa athari hizo anaweza asihuzunishwe hata kidogo. Hii ni hususani pale ambapo anajihisi kuwa alitaka mambo yawe hivyo na amewajibika kikamilifu kwa hilo. Hapa watakaoweza kung’amua jambo hili ni wale tu wenye-uwezo-wa-kuhiari.
Pale ambapo mtu mwenye kuwajibika anaumizwa na jambo. Hawezi kuipoteza furaha yake yote na kuwa mwenye huzuni. La. Ataangalia kwenye visababishi vilivyopelekea maumivu. Atatazama ni vipi angeweza kuviendesha na atakavyoviendesha kwa hapo baadaye. Hivyo kimsingi mtu huyu mwisho wa siku atakuwa na furaha kwa sababu amepata funzo UJINGA wake umeshapona sasa.
Kutokutulia moyoni, unyonge na huzuni huwa vinaenda pamoja kama tu ambavyo uwajibikaji, uwezo na furaha vinavyoenda pamoja
Furaha inahusianishwa na hisia za utulivu na kutosheka na kile kilichopo (what IS). Utulivu wa moyo unakuja pale ambapo mtu anahisi anao uwezo wa kuamua mazingira yake na hata kuyabadili apendavyo. Kimsingi kuyaendesha, yaani mfano anaweza kuamua kujongea au kutulia tu.
Hicho kitendo cha kuyaendesha na kuwa na uwezo wa kutia nia na matakwa binafsi kufanya mambo yatokee ndio inaitwa UWEZO.
Tukizungumzia uwezo,ninafahamu wapo watu wengi tu ikiwamo mdogo wangu mmoja wanaofikiri kwamba hiki ndio kitu cha juu kabisa. Lakini mimi nafikiri kwamba huu ni mwanzo tu. Tena ni wa pili kwa wajibu. Yaani unaanza wajibu halafu ndio uwezo. Mwenye wajibu mkubwa ndio anapata kuwa na uwezo mkubwa!
Hivyo basi uwezo wa kuyafanyia kazi matakwa ya mtu unampa kuendesha mambo na mwisho utulivu wa moyo unaopelekea FURAHA. Tafakari hilo kwa muda, na chukua hiyo point.
Jambo hili linahusiana vipi na furaha;
Mtu hujisikia furaha pale mambo yanapokuwa yanaenda kulingana na matakwa yake. Ikiwa mtu atawajibika na kuchukua jukumu la kuendesha visababishi vingi zaidi basi ataweza kuamua na kuathiri matokeo kwa kutenda impasavyo.
Watu wawili wanaweza kupokea kitu kimoja kiletacho raha, kwa mfano kufaulu alama za juu(A+) katika mtihani. Yule ambaye atakuwa na furaha ya kweli ni yule atakayewaza kuwa alifanya bidii na amewajibika kupata matokeo hayo. Yule aliyeibia mtihani na majibu hatakuwa na furaha ya kweli. Weeh! Subiri kidogo!, Huyo mtu anaweza kuwa na furaha vilevile maana naye pia akifikiri juhudi zake katika kuiba/kuangalizia huko zimempatia hiyo A+. Atakayekosa furaha hapa ni yule tu ambaye kufaulu huko ni kinyume na matakwa yake. Labda malengo yake ilikuwa kufeli.
Mfano nilioutoa juu unaweza ukakuchanganya kiasi, hebu tuangalie mfano mwingine. Mungu anafahamu kabisa kwamba watu watakuwa na furaha zaidi ikiwa watawajibika katika kuleta matokeo. Yeye angeweza kufanya kila kitu lakini bado ameruhusu na ameupa thamani kubwa mchango wa mwanadamu. Tunaomba kisha tunapokea. Tunaishi kisha tunachagua kwenda mbinguni au kufa tu (kupatwa na mauti ya pili). Mbinguni patajawa na mandhari ya furaha kwa sababu patafurika watu wawajibikaji. Kama watu wangebebwa tu na kupelekwa mbinguni bila hili wala lile wasingeiishi furaha ukilinganisha.
Katika kuishi nimejionea. Kwamba hata kama matokeo ni machungu kweli, yule mpokeaji wa athari hizo anaweza asihuzunishwe hata kidogo. Hii ni hususani pale ambapo anajihisi kuwa alitaka mambo yawe hivyo na amewajibika kikamilifu kwa hilo. Hapa watakaoweza kung’amua jambo hili ni wale tu wenye-uwezo-wa-kuhiari.
Pale ambapo mtu mwenye kuwajibika anaumizwa na jambo. Hawezi kuipoteza furaha yake yote na kuwa mwenye huzuni. La. Ataangalia kwenye visababishi vilivyopelekea maumivu. Atatazama ni vipi angeweza kuviendesha na atakavyoviendesha kwa hapo baadaye. Hivyo kimsingi mtu huyu mwisho wa siku atakuwa na furaha kwa sababu amepata funzo UJINGA wake umeshapona sasa.
Kutokutulia moyoni, unyonge na huzuni huwa vinaenda pamoja kama tu ambavyo uwajibikaji, uwezo na furaha vinavyoenda pamoja