Kwanza ni kwa nini gazeti limeweza kutaja majina ya watu hadi rais wa nchi,lakini likaacha kutaja jina la hoteli yalikofanyika mahojiano hayo? yaweza kuwa ni kwa sababu gazeti limeogopa kushitakiwa kwa kuzushia hoteli,au kuwa gazeti na walio nyuma ya habari hii wataumbuka maana hoteli inaweza kukanusha.pili,ni kwa nini mahojiano yenye kutesa watu hivyo yafanyike hotelini? hotelini ni mahali ambako polisi wanaweza kupaamini zaidi ya vituo vyao wenyewe?,tatu mtu aliyeteswa hadi kupoteza fahamu anazinduka anakuta amekaa kitini??? nne,hii habari ingekuwa kweli tupu,kumbukeni hii ilishaandikwa huko nyuma na gazeti la MAWIO,version hii ina tofauti kidogo tu.je hawa waliotajwa leo walikuwa hawajulikani wakati ule testimony ya kihawa ilipoandikwa na MAWIO?
Kwenye story ya kwanza ya MAWIO huyu kihawa wa dodoma,alisema aliulizwa kama anamfahamu LUDOVICK JOSEPH.huyu dogo chadema wanamtuhumu kutumika na mwigullu.imekuwaje kwenye simulizi ya sasa mtu huyu asitajwe tena,bali wametajwa watu wengine??.tuendelee, je hao vijana waliopigwa shoti kwenye korodani,walibaki salama tu baada ya korodani kupigwa umeme? wanayo majeraha yoyote? je wanasheria wa chadema na viongozi wangeshindwa kutaja haya majina waliyotaja sasa tanzania daima kama kijana vijana hawa walikuwa nayo?
Ningeweza kuendelea tu kuonyesha mashaka kwenye hii kitu.nimalizie na mambo mawili.binafsi kama mapalala sikatai kuwa vijana hawa wanaweza kuwa waliteswa,hata kama hilo ni kweli ninao wasiwasi na extent ya mateso hayo.wanatia chumvi.NYOMBI ni ofisa wa juu sana wa polisi,na pasua kadhalika.sasa hatujaambiwa kuwa walikuwa wenyewe wakitesa au waliamrisha watesaji wafanye huo unyama.pili,chadema ni chama kikubwa sasa.siasa za UHARO zimetapakaa.ndiyo maana Lwakatare alipotoka gerezani akiwa Bukoba alilalamikia majungu ndani ya chama hiki.kwa hiyo,hawa vijana kumbukeni kuwa nao wana maslahi ya kisiasa ndani ya chama chao.inawezekana hao wanaowataja ni maadui wao kisiasa,au ni maadui wa watu wanaowaunga mkono.wanataka kutumia mwanya huo kuumiza wengine ndani ya chadema.mchezo ulee,wa kutoana kafara. na je mwandishi wa habari hii josephat isango ana uongozi gani katika chadema kule singida? hana ugomvi wowote na akina chagulani,matata na akina kisandu? amewahi kutoa tamko la bavicha singida huyu wakati wa sakata la akina mchange na chagulani.je mhariri wa habari hii na gazeti kwa ujumla,ana nafasi gani katika chadema,na hawezi kutumia habari kama hii kutengeneza mambo yake?? na tujaribu kuacha kutawaliwa na ushabiki kwa chadema kiasi hiki.kama tutaendelea hivi,basi chadema kitakuja kuwa chama kiovu kuliko CCM