Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Kwa kweli hapa kuna spinning ya hali ya juu kabisa.SS kazomewa ukumbini na wajumbe jana wewe unasema alikuwa ni shujaa,tena jk akamwambia hayo matendo yenu yanauwa chama live.Nape anaweza kushinda au kushindwa rufaa yake lakini kumtoa uanachama haikuwa ni nia yetu ya kumkomoa bali agenda yetu ilikuwa wakati wa mchakato hasiwe mwanachama wa uvccm na kwa msingi huo nia ilikuwa ni political assasination kwa muda ili asije kugombea uenyekiti wa vijana....wewe ulizani nia yetu ni uanachama wake,hujui kuona na kama unaona basi utambui....tumempiga nje ya duru kwa uwezo wake mdogo.NINAYO FURAHA KUKWAMBIA KUWA SASA NAPE SIYO MGOMBEA TENA NA THIS WAS OUR ATTENTION.HAHAHAHAHAHAHAH.


Wewe Kijana,nilidhani ulikua unampa back up Nchimbi kwa sababu unataka kuona kanuni zinafuatwa.

Katibu Mbumbu asiyejua hata kujenga hoja? Kama huyo Ndiye katibu anaefuatilia utekelezaji wa ilani ya Chama na ambae ameshirikiana na Mhunzi wa Vyeti Nchimbi ambae ni mwenyekiti wa vijana manaestahili kutetea jumuiya ya vijana na kujenga sera za kuendeleza vijana ndani ya Chama,wamefanya uamuzi wa jazma na kuuvalia njuga lro hii wame-end up kuumbuka mchana kweupe! Wana mawazo mepesi kama karatasi.Yaani hata JK asiye na ujasiri wa kupambana na viongozi vilaza bado amewaona hao jamaa zako ni uchochoro kweli kweli,Sasa sijui wewe utatuambia nini.Yaani wewe mpiga debe ni kama vile uko out of touch,mabosi wako wameshaumbuka lakini bado unabweka tu hapa.

Hapo Makamba na Nchimbi,they are big loosers.
 
My interest ilikuwa ni Nape anakatwa jina ambapo yeye na wewe mlisema kuwa mna imani na vikao vya juu.sisi tumemkata kwa stahili tofauti kabisa na mliodhania nyie.

NINA FURAHA KUKWAMBIA KUWA WALAU KWA SASA nAPE SIO MGOMBEA TENA WA UVCCM.WAPAMBA WAKE WOTE TUMEWAHAMISHIA KWENYE VITA YA KUMUOKOA ASIVULIWE UANACHAMA WA UVCCM NA KUTUACHA TUKIENDELEA NA KUPANGA SAFU YETU YA MWENYEKITI MPYA.....

Marekebisho sio hoja kabisa kwa kuwa ata baraza kuu lilitoa marekebisho na tena yalikuwa ni makubwa zaidi ya hayo yalioletwa na kamati kuu.kwa mjinga yeyote kuangakia karekebisho ya kamati kuu kama ushindi ni kichekesho kikubwa sana kwa kuwa alitegemea kamati kuu hisione cha kurekebisha kabisa.


Labda ungetuambia kwanza kwa nini wewe hukutaka kumuona anagombea! ili niache kukuona mwehu.angalao come up with facts,ili nipate hisia za kukufikiria vile ninavyofikiria
 
My interest ilikuwa ni Nape anakatwa jina ambapo yeye na wewe mlisema kuwa mna imani na vikao vya juu.sisi tumemkata kwa stahili tofauti kabisa na mliodhania nyie.

NINA FURAHA KUKWAMBIA KUWA WALAU KWA SASA nAPE SIO MGOMBEA TENA WA UVCCM.WAPAMBA WAKE WOTE TUMEWAHAMISHIA KWENYE VITA YA KUMUOKOA ASIVULIWE UANACHAMA WA UVCCM NA KUTUACHA TUKIENDELEA NA KUPANGA SAFU YETU YA MWENYEKITI MPYA.....

Marekebisho sio hoja kabisa kwa kuwa ata baraza kuu lilitoa marekebisho na tena yalikuwa ni makubwa zaidi ya hayo yalioletwa na kamati kuu.kwa mjinga yeyote kuangakia karekebisho ya kamati kuu kama ushindi ni kichekesho kikubwa sana kwa kuwa alitegemea kamati kuu hisione cha kurekebisha kabisa.

Mkuu Fairplayer,

Huyu ni mtu mwenye kupenda atteintion, kama unakumbuka vizuri kwanza alianza kujiita Aduiwakikwete, since then anahangaika tu majina alipoona hakuna attention akaamua kujipachika majina ya Nchimbi, Toma Mwang'onda, na sasa hili la Fisadi mtoto, sasa ndugu yangu kweli unafikiri ni worthy kujadili naye ishus muhimu za taifa?

Kabla sijaingia jana ameandika maneno mengi sana ya uongo akidai ni kutoka kwenye kikao, sasa nilitegemea kuwa atakuja na kukanusha ninayosema, tizama anavyohangaika, halafu wala asiwadanganye hana lolote gata kwenye payroll ya mafisadi hayumo, ila anajipendekeza tu huko, kuna mtu ameniambia majuzi kuwa sasa hivi anahangaikia kupeleka wazungu kwenye jimbo la Nchimbi,

In the real life jamaa hudai kuwa ni mtoto wa chifu, kwa hiyo siku zote kwake ni lazima awe na something kwenye public cha kumfanya ajiskie yuko on top of others, sasa hili jina na maneno anayoyatumia vinamfanya alale usingizi mzuri sana maana angalau ana some type of attention otherwisae ni waste of time kufikiri unaweza kwua a reasonable debate, lakini tutaendeela kumsaidia tu kuwa hao anaowalilia ni viongozi walioshindwa na wanatakiwa kukaa pembeni, kama yeye!

Jana sliema mkataba umepita, leo anaimba wimbo mwingine tena masikini wa Mungu! ni wa kumsamehe tu! hasa kwa wale tunaomjua vizuri!
 
Nape should go to hell.

Wewe na Nape nani should go to hell? Wewe ndiye unayetakiwa kwenda to hell na you know that tena better than anybody, acha huu uchuro wako Nape bado ni mjumbe wa NEC, mwanachama wa CCM na hajafa kama ile kawaida yenu!

Mikono yenye damu bwana, ndio maana maisha yenu ni fragile wewe kama wao, inaiskitisha sana!
 
Mwalimu alimtaka Salim, akakataliwa na wajumbe wengi wa Zanzibar, Mwalimu hakumkataa Muungwana, alichosema ni kwamba hakuwa tayari ila asubiri mpaka Mkapa atakapomaliza amuachie that is exactly what he said na Mkapa did exactly what he was told,

Mwalimu aliwakataa kabisa Lowassa na Malecela, alisema Lowassa ni mla rushwa na Malecela hawezi kuaminiwa madaraka ya urais kwa sababu ya marafiki zake watamyumbisha, na akamuapisha Mkapa never to let that happen kwa Malecela kushika urais, ashike anything lakini not urais!

Lakini Mnyonge mnyongeni, Jk alipewa baraka na Mwalimu za kuwa rais baada ya Mkapa, JK amelelewa na kukulia mikononi mwa Mwalimu, hata alipokuwa Mlimani alikuwa siku zote akipelekewa hela za matumizi kutoka Ikulu.

Salim hakukataliwa na wajumbe wa Zanzibar,Salim alisema yeye hayuko tayari na anataka kumalizia kazi aliyotumwa at the time OAU kama katibu mkuu wake,nafikiri akiwa na imani kuwa 2005 Mwalimu bado angekuwa hai.Salim alikuwa ni mmoja ya waliomshawishi Mkapa achukue forms,pamoja na Warioba,Butiku na Adam Marwa.Mkapa hata hakujua kuwa Mwalimu angem support.Na alienda kishingo upande.Baada ya kushinda Mwalimu aliwauliza ni wapi wangependa yeye asaidie...CCM wakasema Mkoa wa Kilimanjaro,na Mwalimu alikwenda kupiga kampeni huko.Hakuzunguka nchi nzima kama ilivyosemekana,he didnt have the energy kama wakati ule wa Mwinyi ambapo alizunguka nae nchi nzima na aliwaambia

JK simply alilazimishwa kuchukua forms kwa sababu moja kubwa.Nayo ni kuwa wengi ya waliochukua,kama sio wote walikuwa ni wakristo.Mwalimu hakuwa na interest na Kikwete ila alikuwa na interest ya ku balance.Aliekuwa na nguvu alikuwa ni Lowassa.Chimbuko la mtandao original ni hapo.Lowassa alivyobwagwa,alipeleka nguvu zake zote kwa JK,na ndio kisa cha JK wakati wa kujieleza alisema kuwa Lowassa atakuwa an integral part ya serikali yake kama atafanikiwa.Na hio ndio iliyokuja kum-haunt baadae,2005,kwa sababu walikuwa na makubaliano hayo.

Hilo la JK kuwa anapata pesa kutoka Ikulu,nina mashaka nalo,nimejaribu kuongea na watu waliokuwa karibu na huko wakati huo na sijapata jibu la kuonyesha kuwa that was true
 
Nape should go to hell.

Wewe na Nape nani should go to hell? Wewe ndiye unayetakiwa kwenda to hell na you know that tena better than anybody, acha huu uchuro wako Nape bado ni mjumbe wa NEC, mwanachama wa CCM na hajafa kama ile kawaida yenu!

Mikono yenye damu bwana, ndio maana maisha yenu ni fragile wewe kama wao, inaiskitisha sana!


Mkuu,

Naona amekasirika hadi anatamani kusikia kiaama kinamfikia kijana Nape,hayo ndiyo mawazo ya Jazba yaliyojaa kichwani mwake.

Jana tulimpiga swali,kwanini Nape asivuliwe hata ujumbe wa NEC kama alipita kupitia tiketi ya vijana? It was a tricky question for him,na ujue jinsi alivyo kilaza aliingia mtini hadi leo alipokuja kuibuka huku.

Halafu anakuja kutoa mawazo mepesi huku as if haja-realize kwamba bosi wake Ameshikwa pabaya.Anabweka tu huku na unafiki wake.Always mawazo yake ni ya kitoto.


Nimemuuliza kwa nini anshangilia Nape kushindwa kugombea? Ili tuendelee kujadiliana nae,maanke mkuu hata wewe unatujua huwa sisi tunajadili ishuz za taifa tu hapa,au tunajadili na watu wenye mitazamo inayolenga kulikomboa taifa letu tu and not otherwise.sasa nimemuuliza lakini ametoweka.kimsingi hatuwezi kuuzuia huo upupu wake hapa maanake mwenyekiti wake au bosi wake Nchimbi anatambua hapa lazima pia kuwe na wendawazimu, ili mradi asilete matusi tu,
 
Achebe,

Kumbuka kuwa kuna Limbukeni Nchimbi ambaye anajidai kuwa ana asilimia 80 za hisa UVCCM, Je nape atapona kwake. Mwkjj umekaa kimya sana katika swala hili la nape vp upo kwenye kambi ya beno?
 
1.
Salim hakukataliwa na wajumbe wa Zanzibar,Salim alisema yeye hayuko tayari na anataka kumalizia kazi aliyotumwa at the time OAU kama katibu mkuu wake,nafikiri akiwa na imani kuwa 2005 Mwalimu bado angekuwa hai.Salim alikuwa ni mmoja ya waliomshawishi Mkapa achukue forms,pamoja na Warioba,Butiku na Adam Marwa.Mkapa hata hakujua kuwa Mwalimu angem support.Na alienda kishingo upande.Baada ya kushinda Mwalimu aliwauliza ni wapi wangependa yeye asaidie...CCM wakasema Mkoa wa Kilimanjaro,na Mwalimu alikwenda kupiga kampeni huko.Hakuzunguka nchi nzima kama ilivyosemekana,he didnt have the energy kama wakati ule wa Mwinyi ambapo alizunguka nae nchi nzima na aliwaambia

Mwaka 1985, Salim alikataliwa na kina Natepe, kama alivyokuja kukataliwa tena 1995, lakini Salim akawa mjanja kwa sababu alijua tayari kuwa ameshakataliwa, akagoma kurudi toka Adis kuja kwenye kikao, Wajumbe wengi wa bara walimtumia ujumbe kumatka aje mwenyewe uso kwa uso, akawajibu kwa jeuri kubwa kuwa kama wanamtaka watangaze kuwa wanamuomba arudi, ndio wajumbe wengi wa CC wakasema to hell!

2.
JK simply alilazimishwa kuchukua forms kwa sababu moja kubwa.Nayo ni kuwa wengi ya waliochukua,kama sio wote walikuwa ni wakristo.Mwalimu hakuwa na interest na Kikwete ila alikuwa na interest ya ku balance.Aliekuwa na nguvu alikuwa ni Lowassa.Chimbuko la mtandao original ni hapo.Lowassa alivyobwagwa,alipeleka nguvu zake zote kwa JK,na ndio kisa cha JK wakati wa kujieleza alisema kuwa Lowassa atakuwa an integral part ya serikali yake kama atafanikiwa.Na hio ndio iliyokuja kum-haunt baadae,2005,kwa sababu walikuwa na makubaliano hayo.

Baada ya chaguo la Mwinyi yaani malecela kugonga mwamba, kambi hiyo iliamua kutafuta alternative kwa sababu they could not trust Msuya, ambaye ni rafiki wa karibu sana na malecela, kwa hiyo usiku huo huo malecela alipokwama, Lowassa na muungwana wakatumiwa ndege haraka sana na hili kundi la Mwinyi na malecela kwenda Dodoma kuwahi fomu na wale wotw waliokuwa wametayarishwa kumpigia malecela waliwa re-direct kumpigia Muungwana baada ya Lowassa kukwama, Mwalimu akamtumia Salmin another malecela friend kuwazima kundi la Mwinyi, ni Salmin aliyewa-betray kwa Mwalimu ili asurvive uchaguzi kule visiwani.

3.
Hilo la JK kuwa anapata pesa kutoka Ikulu,nina mashaka nalo,nimejaribu kuongea na watu waliokuwa karibu na huko wakati huo na sijapata jibu la kuonyesha kuwa that was true

Mkuu ninamjua mpaka mtu wa uwt aliyekuwa akimpeleka pesa huko, ambaye alikuwa na Mwalimu masaa 24, nitafute kwenye pm nitakupa zaidi mengine siwezi kuweka hapa.

Ahsante Mkuu
 
Hii nadhani ni fundisho kwa vijana wengine na wapenda nchi yao. Tusisubili wakati wa kuomba kura ndiyo tupambane na fisadi, hapo unakuwa si mpambanaji bali unafiki kiasi fulani au unatafuta njia ya kukutangaza si vita endelevu.
Nchimbi umezidi hii adhabu ni kali sana kwa huyu kijana


Hapana,
Hii adhabu sio kali kihivyo. Tunachotakiwa kushukuru kupitia adhabu hii ni kile walichotuonesha. Hapa namaanisha utendaji wao wa kila siku, kile wanachoamini, na wanachosimamia which is equal to NDIVYO WALIVYO. Vinginevyo tusingehakikishiwa kirahisi hivyo.
 

Lakini Mnyonge mnyongeni, Jk alipewa baraka na Mwalimu za kuwa rais baada ya Mkapa, JK amelelewa na kukulia mikononi mwa Mwalimu, hata alipokuwa Mlimani alikuwa siku zote akipelekewa hela za matumizi kutoka Ikulu.

Kama nani?

Watoto wa Nyerere wenyewe walikuwa wanaenda kuchukua karo kwa Butiku. Ndugu wa karibu na Nyerere wanasema alipostaafu alisema kwamba anasikitika sana kwamba familia yake aliiweka kwenye back burner. Sembuse stranger Kikwete?

Kwa kweli hawa wanaokusikiliza sijui ni watu hawajui chochote kuhusu Bongo au ni vipi, lakini hakuna kitu kinachonishangaza kuzidi unavyoweza kuchota akili za watu hapa na "dataz" ambazo hazi make sense hata kwa mtoto wa vidudu mwenye kufikiri.

Eti Kikwete na Sitta wamewaambia viongozi wa CCM "wapumbavu na wajinga." !

Halafu watu wazima wanabugia hizo charade! Yani siamini.
 
Warioba ajitosa kumtetea Nape

2008-09-11 10:51:46
Na Simon Mhina


Baada ya mawaziri wakuu wawili wastaafu kujitokeza kumtetea mwanasiasa chipukizi, Nape Nnauye, dhidi ya adhabu ya kufukuzwa uanachama wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jaji Joseph Warioba naye amejitosa kumtetea kijana huyo.

Warioba sasa anaungana na mawaziri wakuu wenzake, Clepa Msuya na Frederick Sumaye ambao wameelezea kushtushwa kwao na adhabu iliyotolewa na Baraza Kuu la Umoja huo dhidi ya Nape.

Baraza Kuu, Jumapili iliyopita lilimfukuza uanachama Nape kwa madai ya kuvunja kanuni za UVCCM. Pia lilipendekeza kwa Kamati Kuu ya chama hicho kumvua mwanasiasa huyo machachari nyadhifa zake zote ndani ya CCM.

Mbali ya kuwa Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM, Nape pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho. Pia ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba.

Warioba ambaye pia alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais chini ya utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi, alisema kama CCM ya siku hizi ukisema ukweli unafukuzwa kama Nape, basi kuna siku naye atafukuzwa, lakini akasisitiza hatishiki.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, kiongozi huyo anayeheshimika nchini, alisema haoni sababu za Nape kufukuzwa kwa kutoa maoni yake, bila kujali ni maoni gani.

``Unauliza kwamba wanaosema ukweli ndani ya CCM wamewashiwa indiketa? Ni kweli pengine kuna watu wenye lengo hilo, lakini hilo mimi haliniogopeshi kabisa.

Kusema ukweli ndio tabia anayotakiwa awe nayo mwana-CCM. Kiapo chetu cha uanachama kipo wazi kwamba nitasema kweli daima, fitina kwangu ni mwiko,`` alisema.

Jaji Warioba alisema hana haja ya kuingia kwa undani juu ya madai ya Nape yaliyosababisha afukuzwe UVCCM, lakini anachojua ni kwamba taratibu na kanuni za haki za UVCCM zimekiukwa.

Alisema japokuwa yeye ni kijana wa zamani, haamini kwamba kanuni za sasa za UVCCM zinaweza kuruhusu kuvunja demokrasia.

Hata hivyo, alisema anasubiri maamuzi ya vikao vya Kamati Kuu na NEC ili aweze kusema yaliyoko moyoni mwake.

``Ninaamini watatengua uamuzi huo wa ajabu. Wakitoa maamuzi ambayo yanaunga mkono, hapo sasa mnitafute ili nitoe na mimi yaliyo moyoni mwangu. Lakini ngoja kwanza tuwasikilize,`` alisema.

Vilevile, alisema licha ya kupigwa na butwaa aliposikia uamuzi huo, hakuamini macho yake, kwamba uamuzi huo umechukuliwa na jumuiya ya CCM anayoijua yeye.

Jaji Warioba alihoji ni kwa vipi wapinzani wanaoisema vibaya CCM na kuitukana mchana kweupe, wakitangaza kurejea CCM wanapokelewa kwa mbwembwe na kupewa vyeo, lakini waliopo kwenye chama hicho siku zote wakikikosoa chama, wanaonekana wabaya hata kufukuzwa?

``Mtu anakitukana CCM na kukisema vibaya kila siku. Akirudi anatukuzwa na kupewa vyeo. Lakini mwana-CCM akisema yale yale aliyokuwa anasema mpinzani (kama Nape) anafakuzwa, hii maana yake nini?`` Alihoji na kuongeza: ``Sasa kizuri ni kipi, Nape anayesema kwa nia ya kukikosoa na kukisaidia chama chake, au wapinzani wanaosema kwa lengo la kukibomoa CCM?.``

Warioba alisema suala la kumfukuza Nape halikuwa la kidemokrasia na limelenga kuwanufaisha watu wachache kwa lengo la kukiharibia sifa Chama. ``Hii ni aibu kubwa na fedheha kwa chama chetu,`` alisema.

Alisema hata ukiyaweka hayo mambo mawili kwenye mzani wa kawaida, yaani Nape kutoa madai ya ufisadi kwenye mradi wa Jengo la Vijana na Baraza Kuu la UVCCM kumfukuza, utakuta kitendo cha kumfukuza, ndicho kimeharibu sifa ya chama kuliko madai aliyotoa.

``Nimeshangaa kidogo, hivi kati ya Nape na waliomfukuza nani kaharibu sifa ya chama kinachowataka watu wake waseme kweli daima na fitina kwao iwe mwiko?`` Alihoji.

Warioba ni Waziri Mkuu mstaafu watatu kutoa kauli za kupinga hatua ya Nape kutimuliwa UVCCM.

Wa kwanza kutoa maoni yake ni Cleopa David Msuya ambaye alisema mazingira ya kumfukuza kijana huyo yalitawaliwa na jazba.

Alisema adhabu hiyo ni kubwa kwa Nape hata kama kweli alikosea.

Mwingine aliyejitokeza kutoa maoni yake juzi ni Frederick Sumaye ambaye alisema binafsi amesikitishwa na hatua hiyo na amekaririwa akisema atatoa dukuduku lake kwenye vikao vya CCM.

Sumaye alienda mbali zaidi na kusema: ``Kitendo cha kumfukuza Nape aliyekuwa mgombea wa uenyekiti wa taifa wa UVCCM, bila shaka ni njama zilizopangwa na maadui wake wa kisiasa, kwa lengo la kummaliza.``

Chanzo cha Nape kukumbwa na masahibu ya sasa ni hatua yake ya kukosoa mkataba wa ujenzi wa jengo jipya la UVCCM ambao alisema hauna maslahi ya umoja huo wala chama.

Alimlaumu Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la UVCCM, Edward Lowassa, kuwa ndiye aliyeshiriki kusaini mkataba huo ambao haukupitishwa na Baraza Kuu la UVCCM.

Nape alimtaka Lowassa kujiuzulu wadhifa huo kwa kuwa alikuwa ameuingiza umoja huo kwenye mkataba tata.

Kauli ya Nape aliitoa siku ametangaza nia yake ya kuwania uenyekiti wa UVCCM taifa, nafasi ambayo alipewa alama E katika mchakato wa kupitisha majina.


SOURCE:
Nipashe
 
Salim hakukataliwa na wajumbe wa Zanzibar,Salim alisema yeye hayuko tayari na anataka kumalizia kazi aliyotumwa at the time OAU kama katibu mkuu wake,nafikiri akiwa na imani kuwa 2005 Mwalimu bado angekuwa hai.Salim alikuwa ni mmoja ya waliomshawishi Mkapa achukue forms,pamoja na Warioba,Butiku na Adam Marwa.Mkapa hata hakujua kuwa Mwalimu angem support.Na alienda kishingo upande.Baada ya kushinda Mwalimu aliwauliza ni wapi wangependa yeye asaidie...CCM wakasema Mkoa wa Kilimanjaro,na Mwalimu alikwenda kupiga kampeni huko.Hakuzunguka nchi nzima kama ilivyosemekana,he didnt have the energy kama wakati ule wa Mwinyi ambapo alizunguka nae nchi nzima na aliwaambia

JK simply alilazimishwa kuchukua forms kwa sababu moja kubwa.Nayo ni kuwa wengi ya waliochukua,kama sio wote walikuwa ni wakristo.Mwalimu hakuwa na interest na Kikwete ila alikuwa na interest ya ku balance.Aliekuwa na nguvu alikuwa ni Lowassa.Chimbuko la mtandao original ni hapo.Lowassa alivyobwagwa,alipeleka nguvu zake zote kwa JK,na ndio kisa cha JK wakati wa kujieleza alisema kuwa Lowassa atakuwa an integral part ya serikali yake kama atafanikiwa.Na hio ndio iliyokuja kum-haunt baadae,2005,kwa sababu walikuwa na makubaliano hayo.

Hilo la JK kuwa anapata pesa kutoka Ikulu,nina mashaka nalo,nimejaribu kuongea na watu waliokuwa karibu na huko wakati huo na sijapata jibu la kuonyesha kuwa that was true

Nakubaliana na wewe 100%,Mwalimu alikuwa anatumia busara na akili za hali ya juu na kupima uwiano wa kijamii.Bila shaka alikuwa hamwamini huyu bwana JK kipindi kile akiwa na umri wa miaka 45 ambayo ni miaka waliyoingia akina Clinton,Blair na JFK.Alitumia falsafa hakutaka ku-embarass cadres wake bila sababu za msingi,aliachia busara zichukue mkondo wake.

Kuhusu kukataliwa kwa Malecela hakukuwa na uhusiano wowote kuhusu uwezo,Mwalimu alimukataa kwa sababu ya shinikizo la wanasiasa tegemezi akina Kingunge.Hawa walihofia Malecela kuwatosa wakati wao tegemeo lao ni kufanya majungu na ni watu ambao sio tishio kwake kisiasa. Tukumbuke mwalimu alipenda sana kuzungukwa na watu watiifu na wanafiki,ambao ilikuwa rahisi kuwamanipulate sio wenye akili za kujitegemea kama Malecela.

Kingunge wakati anaishi misheni kota ilala alikuwa taarishi wa TANU,alikuwa amemaliza darasa la nane.Marehemu Sekou Toure alimuchukua na kumpeleka Russia kusomea propoganda na mpaka leo hii anaishi kwa kutumia mdomo wake sio akili.
 
Mkuu Kuhani,

Karibu tena mkuu, maana ni muda kidogo ulikuwa umepotea naona uko tayari tena karibu sana, kuhusu malalamiko yako nimekutumia pm kwa jina lako lingine uliloniulizia nalo kuhusu hiyo ishu ya kina muungwana kupewa hela za matumizi na mwalimu.

Kuhusu kikao cha CC, ni vyema kama una ukweli wa kushinda wa kwangu ukauweka, kuliko kujaribu kutoa mashambulizi yasiyoweza kumsaidia mwananchi yoyote kuelimika, anayekusaidia na hayo maneno yako ni huyu bwana Fisadi Mtoto akiwa amejibadilisha jina, sasa look back kutoka intellectualism zako humu ndani ya JF, mpaka kufikia one side na kina fisadi mtoto! huoni kuwa ni aibu kubwa sana kwa mtu mwenye elimu nzito kama wewe? LAKINI UKISOMA MAGAZETI YA LEO UTAONA KILA KITU TULICHOSEMA JANA KIMO

nilifikiri kuwa utakaporudi utakuwa tofauti angalau kidogo kumbe ni worse kuliko mwanzo? Yaani unasema maneno yangu kuhusu CC kweli ni sawa na kumsingizia Dr. Masau kuwa alikuwa anauwa wananchi wanaokwenda kutibiwa kwake?

Inasikitisha sana mkuu, lakini karibu sana tuvine ngoma hii ya wachawi, si unajua kua I love it!

Nowbring it on, ingawa nina heshima sana na mchango wako kwenye topic ya Picha na historia, lakini wembe wangu ni ule ule tu wa kumkoma nyani!

Marehemu baba wa muungwana alipokuwa anafariki alikuwa mjumbe mashuhuri sana wa NEC, akamkabidhi mwanawe kwa Mwalimu, na hakuwa muungwan tu kuna watu kama magambo walikuwa kwenye hii payroll ya ikulu bila kupitia kwa Butiku, watu kama ole naiko hawakuwa wakisaidia kupitia kwa butiku, naona mkuu unajaribu sana kujiweka kwenye ishus ambaz ni clear huzifahamu vizuri, ni vyema ukauliza uelimsihwe kuliko kuleta matusi ambayo unajua fika kuwa huyawezi, maana wewe ni mzushi tena wa hatari sana, au?
 
2.

Baada ya chaguo la Mwinyi yaani malecela kugonga mwamba, kambi hiyo iliamua kutafuta alternative kwa sababu they could not trust Msuya, ambaye ni rafiki wa karibu sana na malecela, kwa hiyo usiku huo huo malecela alipokwama, Lowassa na muungwana wakatumiwa ndege haraka sana na hili kundi la Mwinyi na malecela kwenda Dodoma kuwahi fomu na wale wotw waliokuwa wametayarishwa kumpigia malecela waliwa re-direct kumpigia Muungwana baada ya Lowassa kukwama, Mwalimu akamtumia Salmin another malecela friend kuwazima kundi la Mwinyi, ni Salmin aliyewa-betray kwa Mwalimu ili asurvive uchaguzi kule visiwani.

3.

Mkuu ninamjua mpaka mtu wa uwt aliyekuwa akimpeleka pesa huko, ambaye alikuwa na Mwalimu masaa 24, nitafute kwenye pm nitakupa zaidi mengine siwezi kuweka hapa.

Ahsante Mkuu

Mkuu FMES,

Nimekuwa busy kidogo lakini naona kuna mengine uliyoandika yanayohitaji tusaidiane kidogo. Nafikiri inawezekana aliyekupatia baadhi ya data ulizozipata hazikutimia au waliokupa wamezipindisha kidogo. Hapa haya mawili naona ujaribu kuyaulizia zaidi.
  1. Enzi za CCM ya Mwalimu hapakuwa na kambi kubwa kubwa kiasi cha mtandao kwa ajili ya kupigania uongozi ndani ya CCM. Hawakuthubutu kufanya wazi maana hiyo ilikuwa ni sawa na kujichongea habari zitakapomfikia Mwalimu. Malecela alijaribu kuupigania wazi uraisi ndipo Mwalimu alipotoa tamko la kuwaogopa kama ukoma wenye kuikimbilia ikulu. Lowassa hakukodishiwa ndege kwenda kuchukua fomu, bali alikodisha yeye mwenyewe kwa pesa yake mwenyewe. JK yeye alipewa lift tu na mshikaji wake Lowassa. Hili la kukodisha ndege pamoja na ile nyumba ya Lowassa aliyokuwa amewakodisha SA Embassy walipofungua ubalozi Dar, ni kati ya mambo ambayo Mwalimu aliyaorodhesha katika kumuondoa Lowassa kwenye kinyang'anyiro akimtaka aelezee huo utajiri ameutoa wapi wakati yeye ni mtumishi wa serikali. Ni kwa sababu hizo hizo ndio maana Lowassa alinyimwa uwaziri na Mkapa kwenye awamu yake ya kwanza, na aliupata tu baada ya Mwalimu kufariki.
  2. Sidhani kama JK alikuwa anahitaji pesa ya matumizi toka kwa Mwalimu kwani wanafunzi wa UDSM miaka ya 70s walikuwa na posho nono sana kiasi cha kuweza kusomesha ndugu zao au hata kuanza ujenzi wa vibanda vyao.
Naomba usiichukulie hii kama ni kijembe bali ni katika kujaribu kuunganisha data zetu tulizonazo ili tuwe sawia. Tuendelee na mjadala.
 
Hii inathibitisha kwamba CCM ni chama cha kifisadi. Yaani wamekosa mtu mpaka wakamchague fisadi Chenge!? Kweli CCM ni muflisi!!

Sasa mkuu mi naona na ss tunamaamuzi ya kijazba. Tunapozungumzia mikataba tunamaanisha mambo yahusuyo sheria, na hapo Chenge ndio mildfielder wetu sasa kosa liko wapi kumweka "askari ktk ulinzi''
 
Mwalimu aliongoza kwa nyakati zake na hata angekuwapo hai Tanzania ilipofika asingeamini macho yake kwani ingemshinda. Huu si muda wa ndiyo mzee ni muda wa uhalisia katika maamuzi na matendo kwa manufaa ya jamii. Wala si muda wa kuwadanganya watanzania.

It over mazee au hamuoni hili.

Sijui lakini!
 
Nape aluta continua vua gwanda lao jichanganye.
Usirudi nyuma achana na hao wanaokumbatia mafisadi............mwisho wao waja ipo siku
 
Mkuu KJ,

1. Nimekusikia sana, ila moja ya sababu za Mwalimu kumpiga vijembe Malecela, lilikuwa ni kundi lake, ambalo kwenye uchaguzi wa 1995 likiongozwa na Mungai, walikwenda mpaka Butiama kumuomba Mwalimu amsamehe Malecela, lakini Mwalimu akawakaribisha shambani alikokuwa akilima, na hakuwapa nafasi kabisa ya kuwasikiliza hoja yao, Mwalimu alikuwa na tatizo kubwa sana na marafiki wa Malecela, kina Mzindakaya, Msabaha na the likes, aliwaona kuwa ni tatizo kubwa sana huko mbele ya safari kwa taifa,

Kingunge na Malecela wamekuwa marafiki wakubwa sana in fact at some of the times walikuwa wakiamini kuwa Mwalimu yuko wrong na idea zake, Malecela

hakujua kuwa Kingunge ni mnafiki anayemdanganya kumbe anmchoma kwa siri kwa Mwalimu, ni mpaka kwenye uchaguzi wa Makamu wa CCM 2000 wakati Kingunge anapiga kampeni za chini chini ndio kwa mara ya kwanza Malecela, akagundua kuwa Kingunge alikuwa akimchezea maisha yake yote ya siasa ukawa ndio mwanzo na mwisho wao!

2. Kuhusu Muungwana na Mlimani na kulelewa na Mwalimu siwezi kusema zaidi ya niliyokwisha sema maana sidhani kama ni masuala yanayotakiwa kuwa wazi.

3. Lowassa, hakukodi ndege alikodishiwa na lile kundi la Mwinyi, ambalo Mwalimu alilijua kwa siku nyingi sana, na alijua kuwa mwenye nguvu kati yao ni Malecela ndio maana alimpiga yeye kwanza na wengine wakatawanyika, kwa sababu kwenye kukodisha ile ndege kunamhusisha na Ole Kambaine aliyekuwa personal wa Malecela na marehemu Chacha kwa muda mrefu sana na wakati huo alikuwa bosi wa ATC, Lowassa na muungwana hawakuwa na hata nia ya kwenda Dodoma, sasa unafikiri ni kwa nini walikurupuka kwenda Dodoma ghafla na huku Mwalimu hawataki? Mwalimu alimktaaa Lowassa kwa sababu moja muhimu nayo ni hela alizochota kwenye kununua magari ya wabunge akiwa ofisini kwa Malecela na kijiji cha myumba za kukodisha alichojenga Lowassa Arusha, mwalimu alimuita sawa na Ochoa mcolombia muuza unga alikuwa na tabia ya kujenga vijiji huko kwao!

iUnafikiri ujeuri wa muungwana kwa nini hakulalamika aliponyimwa urais na mwalimu 1995? Unafikiri ni kwa nini katika miaka 10 mya uwaziri wake wa nje hakuwa na heshima kabisa na mkapa? Naunafikir ni kwa nini mkapa alikuwa siku zote anamuogopa muungwana?

otherwise ahsante mkuu later!
 
Back
Top Bottom