Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Hata mimi nimeshangaa, hivi tunajadili nini hapa? Tusiangushe hadhi ya JF kiasi hicho.
 
Lakini tukikaa na kufikiria kwa makini tutabaini kuwa mtoa mada anaonekana ni mtu mwenye anayekuza mambo au kuandika habari za kichochezi,tujiulize kwani nape kukaa mlimani city kunjwa serengeti lager yake ndio kushereheka? Watu waliofanya sherehe za mashujaa EL kule arusha na AC kule bariadi baada ya kuachia nyadhifa walizolazimishwa na mkuu wa kaya. Nape ana haki ya kukaa na kukutana na marafiki zake.
 
PROBE ON VIJANA COMPLEX DEAL: The credibility question

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THE credibility of a team appointed by the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) to probe a controversial real estate project being developed by the ruling party's youth wing (VIJANA) in joint venture with a group of local private investors has emerged as a central question following the inclusion of former Cabinet minister Andrew Change in the panel.

Several political commentators have reacted strongly to the appointment of the ex-infrastructure development minister in the probe team, saying he lacks credibility after himself being forced to resign from Cabinet over a corruption scandal.

Chenge, who also chairs the CCM ethics committee, was this week appointed by the ruling party along with two other central committee members -- Dr Abdallah Kigoda and Pindi Chana -- to review the dubious real estate deal between VIJANA and private developers comprising Estim Construction Limited and MMI Steel Mills companies owned by the Patel family business franchise.

''How can Chenge -- a man of questionable integrity who is under a serious corruption investigation himself -- be given the task of investigating possible allegations of corruption in the VIJANA complex deal?'' Queried a senior CCM member on condition of not being named.

He added: ''I don't think its proper at all for a man under corruption investigation to be given the task of investigating possible wrongdoings of other people ... this is a question of credibility.''

Chenge resigned under a bribery cloud in April this year after detectives from Britain's Serious Fraud Office (SFO) investigating the 70bn/- military radar deal questioned him about the origin of more than $1m found in his offshore bank accounts.

The Bariadi North Member of Parliament provided legal advice to former President Benjamin Mkapa's government in 2002 in relation to the purchase of the military radar system from Britain's Serious Fraud Office in his capacity as the then Attorney General.

The Deputy Leader of the Official Opposition in the National Assembly, Dr Wilbrod Slaa, slammed Chenge's appointment in the CCM probe team, saying the integrity of the entire investigation had been undermined.

''This man (Chenge) is still under investigation in the military radar corruption scandal. His integrity is obviously questionable until he is cleared of any wrongdoing,'' he said.

Slaa said it was a shame for the ruling party to completely disregard principles of good governance by appointing Chenge to the probe team.

''How can someone suspected of involvement in corruption be given the mandate to investigate other corruption allegations. This is a shame to the whole nation,'' he charged.

He added: ''What do you expect to come out of investigations headed by a man who is himself the subject of a very serious corruption investigation that forced him to resign as a Cabinet minister?''

Several other independent experts said although every person is presumed innocent under the law until proven guilty, Chenge's inclusion in the probe team was unwarranted.

''You simply cannot give a person under corruption investigation the mandate to investigate other people suspected of wrongdoing. Where will he get the moral authority to do so? That is why former judges and other persons of good public standing are appointed to head committees and probe teams,'' remarked another political commentator close to CCM.

Nalaila Kiula, who is a former Cabinet minister, earlier this year criticized the appointment of Chenge to CCM's ethics committee, declaring that he should step down until cleared of all corruption allegations.

A member of the CCM national executive committee, Nape Nnauye, recently challenged the entire board of trustees of VIJANA to be held accountable over a controversial real estate project being developed in joint venture with the Patel business family.

Nnauye called for the resignation of the VIJANA board of trustees' chairman, former Prime Minister Edward Lowassa, and other senior leaders of the ruling party's youth organization to accept responsibility for mishandling the real estate deal.

The youthful politician, who has emerged as one of the main candidates for the post of VIJANA national chairman in forthcoming elections, said he was not targeting any particular person within the youth organization, but ''the entire leadership.''

His remarks came in the wake of a statement by Lowassa published by a section of the local media, claiming that the VIJANA board of trustees that he (Lowassa) chaired had only signed a Memorandum of Understanding (MoU) with the private investors - not a formal contract.

But according to Nnauye, this statement only served to justify the question of how come the private investors have been allowed to proceed with the construction project adjacent to the VIJANA headquarters building in the city, in the absence of a formal contract.

Following Nape's scathing attack of Lowassa and other senior party officials, the outgoing VIJANA leadership recently stripped him of his membership of the youth organization, thus technically ruling him out of the upcoming leadership race.

However, the CCM central committee, which met this week in Dodoma under the chairmanship of President Jakaya Kikwete gave Nape the option of lodging an appeal against the termination of his membership in VIJANA, which is chaired by the current Deputy Minister for Defence and National Service, Emmanuel Nchimbi.

Several respected politicians, including a couple of retired prime ministers (not Lowassa) recently came out in public to defend Nnauye, saying VIJANA erred by stripping him of his membership.

There are concerns among some CCM members that the punitive action against the young politician displayed a lack of tolerance to criticism by the top echelon of power in the CCM's youth organization.
 

Maisha yangu yote ya uanachama wa CCM, sikujua kuwa Chenge ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya CCM, maana sijawahi kuwasikia CCM wakilisema hilo hadharani,


Hapana, waleta habari wa JF wamekosea.

Chenge sio Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya CCM. Ni mjumbe tu.

Na thread nzima ya "WITO: Chenge Jiuzulu Kamati ya Maadili," iliyosema ni Mwenyekiti haikufanyiwa fact checking.

Mwenyekiti wa kamati ya Maadili na Usalama ni Mwenyekiti wa chama Taifa, kwa lazima.


KANUNI ZA UONGOZI NA MAADILI


2.0 Muundo wa Kamati ya Usalama na Maadili


2.2 Ngazi ya Taifa


(a) Mwenyekiti wa CCM – Mwenyekiti
(b) Makamu Mwenyekiti wa CCM; Bara na Zanzibar – Wajumbe
(c) Katibu Mkuu wa CCM – Katibu
(d) Makamu wa Rais – Mjumbe
(e) Naibu Katibu Mkuu wa CCM; Bara na Zanzibar – Wajumbe
(f) Wajumbe wanne wa kamati Kuu, wawili kutoka Bara na wawili kutoka Zanzibar; jinsia ikizingatiwa.

Habari ndio hiyo!
 
B aada ya majungu ya majungu ya magazeti na spinning za kina FMES umoja wa vijana leo umetoa press release yake kueleza kilichojiri katika vikao vyake pamoja na uamuzi wa kamati kuu,dondoo za mambo yaliojiri ni pamoja na yafuatayo:
1.mkataba ulipitishwa na vikao vyote vya jumuhia ambavyo pia Nape ni mjumbe.
2.Wanasheria na wataalamu mbalimbali walipitia,pia tunathamini sana michango ya kubenea katika kuimarisha mkataba huo.
Maamuzi ya kamati kuu ni kama yafuatayo:
{a}kamati kuu haina ubavu wa kuzuia mkataba.uvccm ina full authority.
{b}mkataba umefata maelekezo ya chama
{c}uvccm ijiridhishe mambo yafuatayo kabla ya kuyasaini:
.gharama za mradi ziwe wazi zaidi
.uv iruhusiwe kuongeza hisa
.iwapo mkataba unavunjwa zionyeshwe hatua zake.
.nguvu za mgawanyo wa hisa
.kuwepo na chombo cha pamoja cha kusimamia ubia huo
Wajumbe watatu wa kamati kuu wamewekwa kusaidia ushauri wa kitaalamu.

Swala la Nape:
nape hajaachishwa uanachama kwa kukosoa mradi.bali kwa kusema uongo kuwa hakukuwa na vikao vya kupitisha mkataba huo wakati vilikuwepo na pia alishiriki kufanya maamuzi.katika utetezi wake alikanusha kuwa alisema na kudai ni maneno ya waandishi,alikutwa na hatia.
adhabu zake ni:
kufutwa uanachama wa uvccm
kupendekeza kwa chama wamvue nafasi zake za uongozi

Kwa suala la kuachishwa uanachama mamalaka ya mwisho ni baraza kuu la umoja wa vijana kwa mujibu wa ibara ya 89{e} hivyo chama hakina uwezo wa kumrudishia uanachama wake bali anaweza kata rufaa yake kwenye baraza kuu la taifa na si penginepo.
Kuhusu nafasi zake za uongozi alizoombewa kufutiwa anaweza kata rufaa kwenye chama.

Kwa sasa ndio kwanza mapendekezo yamepelekwa chama kwa ajiri ya kujadiliwa hivyo si kweli kuwa chama kimekwisha jadili na kuamua hatima za nafasi zake za uongozi alizoombewa tumnyanganye.AMEN
 
B aada ya majungu ya majungu ya magazeti na spinning za kina FMES umoja wa vijana leo umetoa press release yake kueleza kilichojiri


{b}mkataba umefata maelekezo ya chama
{c}uvccm ijiridhishe mambo yafuatayo kabla ya kuyasaini:
.gharama za mradi ziwe wazi zaidi
.uv iruhusiwe kuongeza hisa
.iwapo mkataba unavunjwa zionyeshwe hatua zake.

Wajumbe watatu wa kamati kuu wamewekwa kusaidia ushauri wa kitaalamu.

1. Mkataba umeshasainiwa au bado ?

2. Na kama UVCCM ndio wenye mamlaka ya maamuzi, nani kaunda Tume ya Chenge, sio kile kikao NEC Taifa ?

3. Na muhimu ninalotaka kujua ni kwamba, kama UVCCM inasema mambo yote yalienda sawa kuhusu Mkataba, na kwamba Nape alitunga uongo kuhusu Mkataba, sasa ni nini kime trigger waunde Tume ya Chenge ?

Maana kama mnaunda Tume ya Chenge kwa ku respond kwenye madai ya Nape ina maada Nape hakuwa mwendawazimu, au ?

Hebu nieleweshe hapo.

Vinginevyo Fisadi Mtoto, umeeleza vizuri sana yaliyomjiri Nape.
 
Fisadi Mtoto,

Kusema kwamba CC haina ubavu wa kuzuia mkataba, huo ni uongo. Kusema kwamba UVCCM ina full authority nao ni uongo, hakuna ambacho huwa kinafanywa na Jumuiya za Chama ambacho huwa hakiendi kujadiliwa CC ama NEC. Tatizo ni kwamba baadhi ya viongozi wa CCM na Jumuiya za Chama wamekuwa wakitanguliza mbele maslahi yao binafsi badala ya kutanguliza maslahi ya Jumuiya.

Kama UVCCM ingekuwa na full authority wala mkataba usingeundiwa tume nyingine ya wajumbe toka CC. Hilo pekee linaonyesha kwamba CC haina imani na uongozi wa UVCCM na ndiyo maana wametoa watu wengine washiriki kurekebisha hizo kasoro zilizo kwenye mkataba na si ajabu hata hizo kasoro ziko nyingi ila kwa kuogopa kuumbuana ndio maana wameamua akina Kigoda waingie kusaidia. Vinginevyo akina Isaac na Nchimbi wangeachiwa wafanye hiyo kazi bila kuingiliwa na mtu.

Mtu akisema mkataba una mapungufu na unatakiwa kuboreshwa ili pande zote ziweze kufaidika, kwa lugha nyepesi anakuwa amekuambia kuna ufisadi ndani yake na ndio maana mkataba unaonekana kupendelea upande mmoja na upande mwingine unaumia.

Kuhusu Nape kila mtu anasema la kwake na wote hao ni vigogo wa CCM. Nchimbi kasema ya kwake ambayo umeyanukuu hapo juu. Makamba kameza matapishi yake na kukiri kwamba kulikuwa na ubabe. Nchimbi amekiri kwamba maamuzi ya Baraza Kuu yalikuwa makali kuliko yaliyopendekezwa na Kamati ya Utekelezaji (hapo anakuonyesha wazi kwamba maamuzi yalikuwa ya jazba na kukomoana). Ndiyo maana Makamba anaona hata aibu kuongelea swala la Nape maana ni kama amevuliwa nguo na kuaibishwa mbele ya wana CCM. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar anasema kwamba jina la Nape halitakatwa na lazima lifike mpaka mwisho wa safari ambako ni kwenye NEC. NEC ndiyo wataamua hatima yake. Hii ni dalili kwamba kuna vurugu ndani ya CCM na kila mtu anasema kile anachokijua yeye. Kuna mengi yatasemwa lakini mwisho wa siku kitajulikana na wewe mwenyewe jana ulisema lengo ilikuwa ni kumchinjilia mbali Nape ili jina lake lisisonge mbele na ndiyo maana vikawa vinaitishwa vikao vya ghafla bila hata kupangwa.

Mwaka 2000 Karume alichinjiliwa mbali na akina Komandoo, jina lake liliingilia mlango wa jikoni na akapeta huku chaguo la Komandoo (Dr. Bilal) akibaki anashangaa na kulalamika kwamba Rais wa Zanzibar aliteuliwa na Bara. Katika vyama vinavyojua kuvunja kanuni na kupindisha demokrasia nadhani CCM inaweza kuwa inaongoza. Ili mradi tu mhusika awe anajua namna ya kuchanga karata zake.
 
Sakata la Nape: Kila mmoja CCM anasema lake

Na Michael Uledi, Dodoma

KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) amesema alitangaza kuwa mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Nape Nnauye, kuwa hawezi kukata rufaa "mbinguni na duniani" kwa ubabe.

Wakati akisema hayo, viongozi wa chama hicho wamezidi kutoa taarifa zinazopingana kuhusu hatua ya kumvua Nape uanachama wa UV-CCM, huku mwenyekiti wa jumuiya hiyo ya vijana ya chama tawala akilazimika kutoa taarifa kufafanua jinsi suala lake lilivyoshughulikiwa katika Baraza Kuu la vijana na hatimaye Halmashauri Kuu ya CCM.

Baada ya Baraza Kuu la UV-CCM kutangaza kumvua Nape uanachama na kupendekeza mtoto huyo wa mwanasiasa wa zamani wa CCM, Moses Nnauye avuliwe nyadhifa zake zote kwenye chama hicho tawala, Makamba, akiongea na waandishi kwa nyakati tofauti alisema Nape "hawezi kukata rufaa mbinguni na duniani".

Lakini mwenyekiti wake wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alibatilisha kauli hiyo na kusema Nape, ambaye anagombea uenyekiti wa UV-CCM, anayo haki ya kukata rufaa ili kupigania haki yake na kwamba CCM inamtambua kama mwanachama wake na nyadhifa zake zote anazoshikilia kwenye chama hicho.

Akizungumza na Mwananchi jana, Makamba alionekana kutotaka kuzungumzia suala hilo alipolizungumzia kwa kifupi, akirejea maneno ya Rais Kikwete.

Makamba alisema: "Nape anayo haki kukata rufaa kupinga maamuzi ya Baraza Kuu kwa kuzingatia kanuni na taratibu na katika hali iliyopo anaendelea kuwa mtumishi wa chama katika idara ya Mambo ya Nje," alisema Makamba kabla ya kujibu kwa kifupi swali la mwandishi aliyetaka kujua sababu za kusema kijana huyo hawezi kukata rufaa mbinguni na duniani.

"Ilikuwa ni ubabe," alisema Makamba akizungumzia kauli hiyo iliyosababisha kizaazaa miongoni wapenda demokrasia.

Wakati Makamba akisema hayo, mkurugenzi wa uchaguzi wa UV-CCM, Francis Isaack alikaririwa jana akisema kuwa hata kama Nape atakata rufaa, hataweza kujumuishwa kwenye mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa CCM kwa kuwa wagombea ni lazima wawe wanachama wa umoja huo wakati Nape amevuliwa uanachama.

Isaack alisema mchakato wa uchaguzi utakuwa umefika mbali wakati rufaa ya Nape, ambaye ameripotiwa kupewa alama E na vyombo vya juu vya UV-CCM kumaanisha kuwa hafai kwa kiongozi, itakapotolewa maamuzi iwapo kijana huyo atakata rufaa na hivyo hatarejeshwa kwenye mchakato huo

Lakini jana, naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar, Saleh Radhaman Ferouz aliliambia gazeti hili kuwa UV-CCM haina mamlaka kukwamisha fomu ya mgombea kwa sababu yoyote yule katikati ya mchakato wa uchaguzi, anaripoti Kizito Noya.

Jana Ferouz alisema: "Nape hawezi kuondolewa katika mchakato wa uchaguzi huo na UV-CCM kwa kuwa jumuiya hiyo sio yenye maamuzi ya mwisho juu ya wagombea.

"Hatma ya Nape katika kinyang'anyiro cha uchaguzi kilichokwishaanza, itatolewa na NEC ambayo ndio kikao cha mwisho katika mchakato wowote wa uchaguzi ndani ya chama hicho na jumuiya zake na sio UV-CCM.

"UV-CCM haiwezi kuitupa fomu ya mgombea aliyekwishaingia kwenye mchakato wa uchaguzi kwa sababu yoyote ile, kwani mwenye mamlaka ya mwisho ni NEC."

Alisema Nape ataendelea kujadiliwa katika mchakato huo wote hadi NEC na hata alama anazowekewa katika vikao vya awali vya UV-CCM hazitoshi kumwondoa kwenye uchaguzi huo.

"Sio alama E tu, hata akipewa alama Z, bado haitoshi kumwondoa kwenye kinyang'anyiro. Jina lake litapita katika ngazi zote za uchaguzi hadi NEC, ambayo ndio yenye uamuzi wa mwisho," alisema.

Nape aliiambia Mwananchi juzi kuwa bado anatafakari adhabu hiyo ya Baraza Kuu kabla ya kuamua kukata rufaa kwa kuwa bado hajapewa rasmi barua ya kuvuliwa kwake uanachama.

Naye Emmanuel Nchimbi, mwenyekiti wa UV-CCM, ambaye alimshinda Nape katika uchaguzi uliopita, jana alitoa taarifa kwa vyombo vya habari akisema Nape anayo haki ya kukata rufaa na kwamba alisema uongo kuwa mkataba wa uwekezaji wa jengo la makao makuu ya umoja huo haukujadiliwa na vikao halali ndio maana alitimuliwa.

"Baraza Kuu liliridhika kuwa vikao vyote vya UV-CCM vinavyohusika na mchakato huo vilihusika kikamilifu, ikiwemo Baraza Kuu la tarehe 4/8/2007 na kikao kilichopitisha muhtasari wa Baraza Kuu cha tarehe 9/2/2008 ambacho Nape alishiriki," ameeleza Nchimbi katika taarifa yake.

Alisema kuwa Nape alionekana kwenye televisheni akitoa tuhuma hizo kuwa hakukuwa na vikao halali vilivyopitisha mkataba huo, wajumbe wa Baraza Kuu waliridhika kuwa aliwadanganya kwa kukana maneno hayo.

Hata hivyo, Nchimbi anaonyesha katika maelezo yake kuwa uamuzi wa Baraza Kuu ulikuwa mkubwa kuliko mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya Utekelezaji ya UV-CCM, ambayo ilitaka Nape asimamishwe kushiriki vikao vya umoja huo na CCM imchukulie hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu zake. Baraza hilo lilimvua uanachama badala ya kuzingatia mapendekezo hayo.

Kuhusu hatima ya mtoto huyo wa mwanasiasa wa zamani wa CCM, Marehemu Moses Nnauye, Nchimbi alisema Nape anayo haki ya kukata rufaa kwa mujibu wa Ibara ya 89 (e) ya kanuni za UV-CCM.

"Kwa mujibu wa ibara hiyo, suala la uanachama, mamlaka yake ya mwisho ni Baraza Kuu la UV-CCM," anasema Nchimbi katika taarifa hiyo, akipingana na Ferouz ambaye kwake Nape anaweza kugombea uenyekiti iwapo atapitishwa na NEC, licha ya kwamba mamlaka ya mwisho ya suala la uanachama liko Baraza Kuu.

Nchimbi alisema mapendekezo ya kumvua Nape nyadhifa zake zote ndani ya CCM yameshawasilishwa kwa katibu mkuu wa chama hicho tawala na kuongeza: "Uamuzi wa chama katika suala hilo utakuwa wa mwisho."

Source: Mwananchi
 
Hivi UVCCM inaongozwa na kanuni ngapi? Ama ina set tofauti za kanuni ambazo zinatumika kuongoza UVCCM?

JK kwenye kikao cha NEC alisema Nape ana haki ya kukata rufaa vikao vya juu na akasema apeleke, vikao vya juu vitafanya maamuzi.

Nchimbi anasema maamuzi ya kumvua uanachama mwanachama yeyote ya UVCCM yanaishia kwenye Baraza Kuu na hapo ndipo mtu anatakiwa kukata rufaa kwenye baraza hilo hilo. Hicho kipengele naona kina walakini kwa kuwa huwezi kupeleka rufaa yako kwa mahakama ile ile iliyokuhumu awali. Maana hakimu ni yule yule na bado atakushindilia hukumu ile ile ili ku-prove credibility yake, iwapo akitengua hukumu yake ya awali anaweza kuonekana hana msimamo ama alikuwa na dhamira tofauti wakati akitoa hukumu.

Kwa upande mwingine Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM nae katoa version yake ya maelezo ambayo iko tofauti na ya Nchimbi. Alipobanwa zaidi anasema after all hata kama rufaa yake itakubaliwa kurejeshewa uanachama bado atakuwa kachelewa kwa kuwa mchakato utakuwa umeishafika mbali.

Makamba ana version yake ambayo anaijua mwenyewe na sijui hata kama huwa anasoma kanuni za UVCCM na haya ndiyo matatizo ya kuweka viongozi ambao wanafanya kazi kwa uzoefu na sio kwa kufuata taratibu zilizopo.

Naibu Katibu Mkuu - Zanzibar nae kaja na version yake ya maelezo kuhusu sakata hilo hilo.

Ni aibu Mwenyekiti wa Chama kutofautiana na Katibu Mkuu wake. Pia ni aibu Katibu Mkuu wa Chama kutofautiana na Naibu wake. Wote wanapaswa kuongozwa na katiba/kanuni zile zile ambazo kwao zinatakiwa kuwa misahafu ili waweze kutenda haki.

Je, kitendo cha hawa vigogo 5 kuja na versions tofauti za maelezo kuhusu swala la Nape inaashiria nini?
 
Hivi UVCCM inaongozwa na kanuni ngapi? Ama ina set tofauti za kanuni ambazo zinatumika kuongoza UVCCM?

JK kwenye kikao cha NEC alisema Nape ana haki ya kukata rufaa vikao vya juu na akasema apeleke, vikao vya juu vitafanya maamuzi.

Nchimbi anasema maamuzi ya kumvua uanachama mwanachama yeyote ya UVCCM yanaishia kwenye Baraza Kuu na hapo ndipo mtu anatakiwa kukata rufaa kwenye baraza hilo hilo. Hicho kipengele naona kina walakini kwa kuwa huwezi kupeleka rufaa yako kwa mahakama ile ile iliyokuhumu awali. Maana hakimu ni yule yule na bado atakushindilia hukumu ile ile ili ku-prove credibility yake, iwapo akitengua hukumu yake ya awali anaweza kuonekana hana msimamo ama alikuwa na dhamira tofauti wakati akitoa hukumu.

Kwa upande mwingine Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM nae katoa version yake ya maelezo ambayo iko tofauti na ya Nchimbi. Alipobanwa zaidi anasema after all hata kama rufaa yake itakubaliwa kurejeshewa uanachama bado atakuwa kachelewa kwa kuwa mchakato utakuwa umeishafika mbali.

Makamba ana version yake ambayo anaijua mwenyewe na sijui hata kama huwa anasoma kanuni za UVCCM na haya ndiyo matatizo ya kuweka viongozi ambao wanafanya kazi kwa uzoefu na sio kwa kufuata taratibu zilizopo.

Naibu Katibu Mkuu - Zanzibar nae kaja na version yake ya maelezo kuhusu sakata hilo hilo.

Ni aibu Mwenyekiti wa Chama kutofautiana na Katibu Mkuu wake. Pia ni aibu Katibu Mkuu wa Chama kutofautiana na Naibu wake. Wote wanapaswa kuongozwa na katiba/kanuni zile zile ambazo kwao zinatakiwa kuwa misahafu ili waweze kutenda haki.

Je, kitendo cha hawa vigogo 5 kuja na versions tofauti za maelezo kuhusu swala la Nape inaashiria nini?
Maelezo ya Nchimbi ndio sahihi kwa kuwa ameeleza wazi na kwa kufuata kanuni ya umoja wa vijana ambayo inasema wazi katika ibara ya 89e kuwa baraza kuu ndio lenye uamuzi wa mwisho juu ya uanachama wa mwana uvccm..suala la kauli za JK ni wazi ziko baseless kwa kuwa hajatumia kanuni wala akatiba.hana uwezo wala akili ya kusoma kanuni na kupambanua mambo.ni wazi alilopoka kama mswahili yeyote wa kizaramo.
 
Maelezo ya Nchimbi ndio sahihi kwa kuwa ameeleza wazi na kwa kufuata kanuni ya umoja wa vijana ambayo inasema wazi katika ibara ya 89e kuwa baraza kuu ndio lenye uamuzi wa mwisho juu ya uanachama wa mwana uvccm..suala la kauli za JK ni wazi ziko baseless kwa kuwa hajatumia kanuni wala akatiba.hana uwezo wala akili ya kusoma kanuni na kupambanua mambo.ni wazi alilopoka kama mswahili yeyote wa kizaramo.

Si kweli.

Kwanza, chochote kile kinachoamuliwa na UVCCM kinapingika na kufutika na vikao vya juu.

KATIBA YA CHAMA CHA MAPINDUZI, 2005

106 (3) : Kazi za Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa zitakuwa zifuatazo:-


Kuthibitisha, kubadili, kukataa au kuvunja uamuzi wowote uliotolewa na kikao chochote cha chini yake au na mkuu yeyote wa CCM.


La pili, hata Mwenyekiti wao UVCCM hawajiteulii wenyewe. Iwapo atarudishwa uanachama, Nape anaweza kukata rufaa aumuzi wa kumuengua ugombea kwa kigezo cha miaka mbele ya Kikao cha juu.

108 (13) (i) Kazi za Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa zitakuwa zifuatazo:

Kufanya uteuzi wa mwisho wa majina ya Wanachama wa CCM wanaogombea Uenyekiti wa Mkoa, Uenyekiti wa Taifa na Ukatibu Mkuu wa kila Jumuiya ya Wananchi inayoongozwa na CCM, na majina ya Wanachama watakaochaguliwa kuiwakilisha kila Jumuiya katika vikao vya CCM vya Mkoa na Taifa.

110 (6) (g) Kazi za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa zitakuwa zifuatazo:


Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa juu ya Wanachama wa CCM wanaoomba nafasi za uongozi katika Jumuiya za Wananchi zinazoongozwa na CCM, ngazi ya Mkoa na Taifa, ambazo uteuzi wake wa mwisho hufanywa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa.

La tatu, hata mambo na taratibu za UVCCM zinasimamiwa na vikao vya juu.

113 (e ). Kazi za Idara za Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa:-

Kusimamia Katiba, Muundo, Kanuni na Taratibu za Chama na Jumuiya zinazoongozwa na CCM.


Kwa hiyo, Kikwete alikuwa sahihi aliposema Nape anaweza kukata rufaa vikao vya juu. Kikwete ni kada wa Chama tokea wengi wetu humu hatujaanza vidudu. Tunaposema alichosema kuhusu kanuni za CCM "ni baseless" tuwe makini. Urais umemshinda lakini atakapopatia tusiseme kakosea. Habari ndio hiyo.
 
Maelezo ya Nchimbi ndio sahihi kwa kuwa ameeleza wazi na kwa kufuata kanuni ya umoja wa vijana ambayo inasema wazi katika ibara ya 89e kuwa baraza kuu ndio lenye uamuzi wa mwisho juu ya uanachama wa mwana uvccm..suala la kauli za JK ni wazi ziko baseless kwa kuwa hajatumia kanuni wala akatiba.hana uwezo wala akili ya kusoma kanuni na kupambanua mambo.ni wazi alilopoka kama mswahili yeyote wa kizaramo.

Fisadi Kijana,

Mwenyekiti wako ameishajichanganya tayari. Kama Baraza Kuu lina uamuzi wa mwisho kuhusu uanachama wa UVCCM, iweje aseme kwamba Nape anaruhusiwa kukata rufaa? Hapo ni sawa na kusema kwamba Mahakama ya Rufani inaweza kusikiliza rufaa ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya rufani ile ile, kitu ambacho siyo sahihi. Kwa hiyo hata Mwenyekiti wako nae anaonekana hajui kanuni.

Ninachokiona na kilicho wazi ni kwamba uongozi wa UVCCM umechanganyikiwa na ndiyo maana wanatoa kauli ambazo zinapingana na kanuni zao wenyewe na wao wenyewe maelezo yao yanapingana. Hawajiamini kwamba kile walichofanya kilikuwa sahihi. Kama kingekuwa sahihi wala kusingekuwa na matamko mengi sana kuhusu kitu kimoja. Kila anayetoa tamko anaonekana kachemka anakuja mwingine kufafanua na badala ya kufafanua ndiyo anaongeza maswali zaidi ambayo hawezi kuyajibu.

Kitu kingine muhimu ni kwamba kanuni za Jumuiya za Chama zote zinaongozwa na Katiba ya CCM. Kwa hiyo lolote linalofanyika kwenye Jumuiya ya Chama mwenye final say ni CC na NEC. Kama kanuni yenu ya 89(e) itachemka basi CCM kama Chama itaingilia kati na kutoa suluhisho la huo mgogoro kwa kufuata katiba ya CCM kwa kuwa hiyo inameza hizo kanuni za Jumuiya za Chama.
 
Mkuu Kuhani,

Wakati ninamjibu Kijana Fisadi sikuwa nimeona bandiko lako. Nadhani lina ufafanuzi wa kutosha sana kuhusu huu mkorogano.
 
Maelezo ya Nchimbi ndio sahihi kwa kuwa ameeleza wazi na kwa kufuata kanuni ya umoja wa vijana ambayo inasema wazi katika ibara ya 89e kuwa baraza kuu ndio lenye uamuzi wa mwisho juu ya uanachama wa mwana uvccm..suala la kauli za JK ni wazi ziko baseless kwa kuwa hajatumia kanuni wala akatiba.hana uwezo wala akili ya kusoma kanuni na kupambanua mambo.ni wazi alilopoka kama mswahili yeyote wa kizaramo.

Eheeee vipi tena kamanda. Sikujua kama wazaramo ni waropokaji!
 
Wakuu Kuhani na Keil,

Saafi sana, naona mnampatia kijana darasa zito sana kuhusu nafasi ndogo walioynayo UV-CCM ndani ya Chama CCM taifa, hamna la kuongeza tena.
 
Fisadi Kijana,

Mwenyekiti wako ameishajichanganya tayari. Kama Baraza Kuu lina uamuzi wa mwisho kuhusu uanachama wa UVCCM, iweje aseme kwamba Nape anaruhusiwa kukata rufaa? Hapo ni sawa na kusema kwamba Mahakama ya Rufani inaweza kusikiliza rufaa ya hukumu iliyotolewa na mahakama ya rufani ile ile, kitu ambacho siyo sahihi. Kwa hiyo hata Mwenyekiti wako nae anaonekana hajui kanuni.

Ninachokiona na kilicho wazi ni kwamba uongozi wa UVCCM umechanganyikiwa na ndiyo maana wanatoa kauli ambazo zinapingana na kanuni zao wenyewe na wao wenyewe maelezo yao yanapingana. Hawajiamini kwamba kile walichofanya kilikuwa sahihi. Kama kingekuwa sahihi wala kusingekuwa na matamko mengi sana kuhusu kitu kimoja. Kila anayetoa tamko anaonekana kachemka anakuja mwingine kufafanua na badala ya kufafanua ndiyo anaongeza maswali zaidi ambayo hawezi kuyajibu.

Kitu kingine muhimu ni kwamba kanuni za Jumuiya za Chama zote zinaongozwa na Katiba ya CCM. Kwa hiyo lolote linalofanyika kwenye Jumuiya ya Chama mwenye final say ni CC na NEC. Kama kanuni yenu ya 89(e) itachemka basi CCM kama Chama itaingilia kati na kutoa suluhisho la huo mgogoro kwa kufuata katiba ya CCM kwa kuwa hiyo inameza hizo kanuni za Jumuiya za Chama.

Mkuu,

Si wameshasema wenyewe huko kwao CCM kuna wendawazimu..mimi sioni tatizo tena.
 
Mkuu,

Si wameshasema wenyewe huko kwao CCM kuna wendawazimu..mimi sioni tatizo tena.

Na kweli CCM ina wendawazimu wengi na inabidi washughulikiwe kama alivyojisema Nchimbi mwenyewe.

Maneno mengine hata kuyatamka yanatia kinyaa. Hivi kweli Mjumbe wa NEC, Mkutano Mkuu wa CCM na Baraza Kuu la UVCCM anaweza kuwa mwendawazimu? Ina maana hata waliomchagua kuchukua hayo madaraka nao ni wendawazimu.

Hilo lilikuwa ni tusi kwa wana UVCCM na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM ambao huchagua wajumbe wa NEC. Hizi siasa nyingine ni za maji taka kwa kweli.
 
Eheeee vipi tena kamanda. Sikujua kama wazaramo ni waropokaji!

Maji yamezidi unga inabidi waanze kugeukana, maana kuna dalili zote za kupata uji badala ya ugali wakati watu walishakaa mkao wa kupata la mwidebe!

Ni kwa kuwa JK alitamka maneno ambayo Fisadi Kijana hakupenda kuyasikia. Ila yale aliyosema Makamba na baadaye kukiri kwamba aliropoka haikuwa kuropoka kwa kuwa alikuwa anawa-support viongozi wa UVCCM na Baraza Kuu.
 
Kama kawaida ya kiburi chao, kundi la akina Nchimbi, Makamba, Lowassa n.k., walifikiri kuwa chama ni chao na hakuna atakayewapinga as long as JK ndie mwenye kigoda.

These fisadis should not underestimate a growing number of CCMers, who are now willing to voice out their ops openly or even sacrifice their positions in support of fairness/democracy within the party or probably just to be against the unpopular Lowassas & co.
 
Back
Top Bottom