Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

The history ni only Mkapa could do that! Hata Mwalimu mwenyewe kwenye hili asingeweza.

MAY I ASK WHY ONLY MKAPA CAN DO THAT?
 
Huyu kijana ni shujaa

Amesema jambo ambalo watanzania wengi lazima walizingatie, CCM na wapinzani

UZALENDO WA TANZANIA.

Uzalendo upite itikadi kwenye nchi, yule ambaye ana nia nzuri kwa nchi yetu tumfuate sio kwa itikadi ya chama chake.

Sio watanzania wengi wana msimamo kama huo.
Unaweza kukuta wengine hata aambiwe chama chake kimefanya vibaya lakini hatathubutu kukikosoa

Sisi ambao hatuna msimamo wa siasa tunaiombea tu nchi yetu ielekee kuzuri.
Wazaliwe wengi kina Nape, Zitto na Kilango na wengineo wanaoitetea Tanzania
 
Akileta mchezo wanamtoa na roho. Be care hawana dogo Mafisadi na Vizee vyao.
 
Mwanakijiji,

Asante sana kwa interview nzuri , ninachoweza kusema ya kuwa Nape yuko deep na CCM inabidi wawe makini kwani wakikurupuka wataumia .Mimi nilikuwa simjui Nape ila kwa yeye kuquestion Status Quo limemjengea sifa kubwa sana ...
 
Mwanakijiji shukrani sana!

CCM waendelee na mpango wao. Napenda sana maamuzi yao. Tuipendao nchi haya ya Nape ni sherehe. Wakimretain sidhani kama watakuwa wamemretain kwa nia njema. Nape awe mwangalifu sana ndani ya hicho chama kwa sasa, asije kudhani vikao vya juu vinampenda sana! Hao watu ni walewale. Yeye kuondoka CCM kwa sasa hakuna mjadala kama anataka future yoyote. Ila asubiri vikao vyote vitende hili kosa ili pasiwepo hata kisingizio. Kusubiri msimamo wa JK ni wishful thinking tu! Tulisubiri sana msimamo wake kwa EPA, Richmond nk lakini tumeishia kuwa kupata vidonda vya tumbo kwa dissappointment, hasa baada ya hotuba yake! Maadamano yale yalinikumbuka watu walivyoandamana wakati mwinyi amefunga chuo kikuu kwa mwaka mzima! Nchi yenye chuo kikuu kimoja tu, rais anakifunga na wanafunzi wanakaa joblessly kwa mwaka mzima wananchi wanamwagika mitaani kumpongeza rais!!!!!! Kweli ndio maana Bush alitushangaa sana, duniani kote akienda anapokelewa kwa mabango ya bush the terrorist, Tanzania watu wanashinda mvuani kumtabasamia! Kweli nchi yetu ni maskini kwa mawazo, hata mwenge wa olympic hivyohivyo, Jamani tuna ulemavu wa akili?
 
Makubwa ni kuwa JK a;ikuwa Dar ,mpaka saa sita na dk 32 mchana alipokuwa anafungua mkutano wa AU pale Kempinski.

Habari ya pili ni kuwa chama kimezidiwa na mafisadi na sasa kinatapatapa na wapo ambao tayari wamemueleza wazi kuwa kama anataka kukigawa chama basi na aingilei mambo ya UVCCM , huku kundi la pili wakiwa tayari kuipambana kwa vyovyote vile wakitaka kuona haki inatendeka .

Vikao vimekua vikiendelea kimakundi kimakundi, na hata imefikia mahali sasa wakuu wa usalama nao wametishika na kukaa na makundi haya mawili kwa kisingizio kilekile kuwa nchi itaingia kwenye mtafaruku wa kisiasa kama mambo hayatawekwa sawa hivi sasa na mvutano kwisha.

Kuna mambo mengi sana yanaendelea mjini Dodoma kwa sasa na mengi yakiwa yako cerntred kwa kijana Nnape , ila huyu ni kama mbuzi wa kafara tuu kwani yeye amejikuta kuwa ni msemaji wa kundi mojawapo lililojeruhiwa na sasa kundi ovu limeamua kuonyesha nguvu zake ndani ya mfumo wa chama .

Mapambano ya kisiasa ambayo yalikuwa yameekwenye chama kimojawapo cha upinzani ili kuhakikisha kuwa kinasambaratishwa yanaonekana kugonga mwamba na haswa baada ya viongozi wa chama hicho kukaa imara na kuweza kuzijua mbinu za mafisadi pamoja na mtandao wao kwa ujumla wake.

Hivyo sasa nguvu kubwa zimeelekezwa kwewnye hizi chaguzi zndani ya CCM huku mkuu akikubwa na mashinikizo mengi kutoka kwenye makundi yote ndani ya chama , ila kimsingi ni kuwa kundi la mafisadi linaonekana kufanikiwa kuwashawishi wazee wengi ndani ya uongozi ambao wamejikuta wakuwaunga mkono na kutishia uhai wa chama hicho ndo maana JK hana la kusema ama kufanya kwa sasa.
 
Katika CCM yao, Nape ameshakuwa outcast

Na kwa Watanzania wengi sasa hivi Chama Cha mafisadi kimeshakuwa outcast ndiyo maana inabidi waibe kura, watoe rushwa na kuintimidate wananchi ili washinde chaguzi.
 
Uamuzi wa kumfukuza Nape wa jazba - Msuya

2008-09-09
Na Waandishi Wetu, Dar na Dodoma


Waziri Mkuu mstaafu Cleopa Msuya amesema amepigwa na butwaa kusikia habari kwamba Nape Nnauye amefukuzwa uanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na anauona uamuzi huo kama umetolewa katika mazingira ya jazba.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Msuya alisema hataki kuingia ndani juu ya ubaya au uzuri wa tuhuma alizotoa kijana huyo, lakini kilichomshangaza ni ukubwa wa adhabu aliyopewa, na mazingira ya kuendesha kesi hiyo.

Alisema hakutegemea hatua kama hiyo ingechukuliwa na vikao vya CCM ya sasa ambayo alitegemea inayo dhamira ya dhati ya kujenga demokrasia ya mtu kutoa maoni yake.

``Sijui kiundani juu ya tuhuma alizotoa kijana huyo, lakini jinsi suala hilo lilivyoshughulikiwa limenitia wasiwasi na kunishangaza sana,`` alisema.

Alisema hata sababu ambazo zimetolewa za kumfukuza uanachama Nape ni nyepesi na hazina uzito unaostahili.
\"Lakini kwa nini wakakimbilia kumfukuza. Wamemfukuza kwa sababu hizi hizi walizotoa, au kuna nyingine?`` alihoji.

Kiongozi huyo wa siku nyingi, alisema waliochukua hatua hiyo ya kumnyang\'anya Nape haki yake ya msingi katika CCM, wanapaswa waeleze hatua za awali walizomchukulia, ikiwa ni pamoja na kumuonya, au kumsimamisha.

``Wangekuwa angalau wamemsimamisha uanachama wa Umoja wa Vijana tungeshangaa kidogo, lakini kumfukuza! Hii ni ajabu mimi binafsi nimeshangaa,`` alisema.

Msuya alisema hata mapendekezo yaliyotolewa na Baraza hilo kwamba Nape avuliwe nyadhifa zote katika chama, ni uthibitisho mwingine kwamba mazingira ya adhabu dhidi ya kijana huyo yalitawaliwa na jazba.

Alisema Baraza la Umoja wa Vijana lilipaswa pia kutoa sababu kwamba Nape avuliwe uongozi kwa kosa gani. Hata hivyo, kanuni ya umoja wa Vijana inatoa nafasi kwa Baraza kupendekeza adhabu zaidi kutoka vikao vya CCM.

``Wanaposema avuliwe nyadhifa zote wanakusudia nini? Yule ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, kofia hiyo nayo avuliwe? Hapa hoja ni kosa lake la kuhoji mradi wa jengo la UVCCM au kuna jambo jingine? Bila shaka hapa kuna jazba zilitawala,`` alisema.

Msuya ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM ambayo inakutana mjini Dodoma, alisema anasubiri kwa hamu mjadala wa hayo mapendekezo yaliyodaiwa yametolewa na Baraza Kuu la UVCCM la kumnyang\'anya Nape nyadhifa zote.

Alisema baada ya kupitia taarifa za awali, hajapata sababu ya kufikiwa kwa uamuzi huo.

``Labda kama kuna sababu zingine watazileta kwenye vikao, lakini hizi nilizosikia hazina mantiki,`` alisema.

Alisisitiza kwamba inaonekana wazi kwamba ndani ya CCM kuna watu hawajui dhana ya ujenzi wa demokrasia ya kutoa maoni au wanajua ila hawataki kwa malengo yao binafsi.

Katika hatua nyingine, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimelaani uamuzi wa Baraza Kuu la UVCCM wa kumfukuza Nape uanachama kikisema kwamba ni mwendelezo wa vitendo vya umoja huo kutumika kuwalinda na kuwasafisha mafisadi nchini.

Akizungumza na Nipashe jana, Mkurugenzi wa Vijana Taifa wa Chadema, John Mnyika, alisema ukweli wa madai hayo unapata nguvu kutokana na Nape kufukuzwa uanachama baada ya kuibua mjadala wa ufisadi UVCCM, ambao umewagusa baadhi ya vigogo ndani ya umoja huo.

``Hali hiyo inabua maswali kuhusu dhamira ya CCM katika vita dhidi ya ufisadi� Kinachosikitisha zaidi ni kuwa Baraza Kuu la UVCCM limekaa katika kipindi ambacho orodha ya mafisadi imetolewa na mjadala wa ufisadi umeshamiri katika taifa letu,`` alisema Mnyika.

Wakati Mnyika akisema hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe, alisema ameshtushwa, kukerwa na kukasirishwa na uamuzi wa Baraza Kuu la UVCCM kumvua uanachama Nape, huku viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi wakiachwa.

``Nimeshtushwa, kukerwa na kukasirishwa na uamuzi wa Baraza Kuu la UVCCM kumvua uanachama ndugu Nape Nnauye.

Wakati viongozi wa CCM wenye shutuma za wazi za ufisadi wameachwa na kupeta, whistle blowers (wapiga filimbi) wanaadhibiwa,`` alisema Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.

Mnyika alisema kilichotakiwa kufanywa na Baraza Kuu la UVCCM, si kumfukuza Nape uanachama, bali lingetoka na azimio la kutaka watuhumiwa wa ufisadi, wavuliwe uanachama CCM au wavuliwe nafasi za uongozi kama walivyopendekeza kwa Kamati Kuu kuhusu Nape.

``Uamuzi wa UVCCM umeendeleza vitendo vya jumuia hiyo kutumika kuwalinda na kuwasafisha mafisadi. Kama hali hii haitabadilika, wasiwasi wa Watanzania kuwa CCM inageuka kuwa chama cha mafisadi utazidi kushamiri na hatma ya taifa itakuwa shakani kama chama kilicho madarakani kwa wakati huu kitakuwa kinalea vijana wake katika malezi, fikra na maamuzi ya utamaduni wa ufisadi,`` alisema Mnyika.

Mnyika alidai anaamini uamuzi uliochukuliwa na UVCCM dhidi ya Nape, ni shinikizo kutoka kwa kundi la baadhi ya vigogo wa CCM kwa kuzingatia kauli walizozitoa kuhusu mradi wa jengo la Umoja huo, lililoko jijini Dar es Salaam.

Alisema kufukuzwa kwa Nape, kulitanguliwa na kauli ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale-Mwiru hivi karibuni ya kuwakemea wanaoikosoa CCM na viongozi wake dhidi ya ufisadi, lakini pamoja na kwamba hakutoa kauli hiyo ndani ya vikao vya CCM, hakuitwa kuhojiwa na kuadhibiwa kama alivyofanywa Nape.

Kwa upande wake, Nape aliambia Nipashe jana kwamba bado yeye ni mwana-CCM mwaminifu na anatarajia vikao vya juu vitamtendea haki.

``Uamuzi wa Baraza Kuu si mwisho, nina imani na chama kwamba vikao vya juu vitatoa haki,`` alisema Nape.

Nacho Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimeshangaa hatua ya UVCCM kumfukuza uanachama mwanasiasa machachari, Nape kwa kisingizio cha kuvujisha siri za vikao, huku chama hicho kikishindwa kuwachukulia hatua viongozi wengine wanaovujisha siri za vikao hasa katika mjadala wa Zanzibar ni nchi au la.

Kituo hicho kimeeleza kuwa hatua hiyo ya UVCCM haikubaliki katika nchi inayofuata misingi ya utawala bora kwani ni sawa na kuminya demokrasia na uhuru wa mtu kujieleza.

Akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Francis Kiwanga, alisema kitendo alichofanya Nape cha kufichua utata uliopo katika ujenzi wa Jengo la UVCCM ni cha kijasiri na kinachofaa kuungwa mkono badala ya kuadhibiwa.

Alisema kuwa kitendo kilichofanywa na UVCCM kinataka kunyamazisha watu wanaotaka kusema ukweli na waliomstari wa mbele kupambana na rushwa.

``Nape alikuwa akitetea maslahi ya vijana wenzake na hatua iliyochukuliwa dhidi yake inakiuka misingi ya demokrasia, uwazi na uwajibikaji, kunapokuwa na mbinu za kuwabana wanaowajibika ndiko kunakopelekea kupata viongozi wabovu na wasiotetea maslahi ya wananchi na hii ndiyo inayoiharibu nchi hii kabisa,`` alisema Kiwanga ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

Hata hivyo, alimtia nguvu Nape kuwa asivunjwe moyo na uamuzi wa UVCCM, bali umpe ujasiri zaidi wa kutetea haki na kupambana na aina zote za ufisadi na mambo mengine maovu katika jamii.

``Tunamtia moyo Nape japokuwa chama chake kinambana kwa sababu anatetea haki, hii isiwe mwisho wake katika kutetea haki`` alisema.

Alisema hii si mara ya kwanza kwa viongozi wa CCM kuzungumza nje ya vikao, akitolea mfano mjadala unaoendelea wa Zanzibar ni nchi au la, kuwa kuna baadhi ya viongozi wanatoa matamshi yanayoenda kinyume na chama chao, lakini hakuna hatua zozote zinazochukuliwa dhidi yao na kueleza kuwa kinachoonekana kwa Nape ni kutaka kunyamazisha watu wanaotetea haki na wasema kweli.

Imeandaliwa na Muhibu Said, Simon Mhina, Abdallah Bawazir Dar na Mary Edward, Dodoma.

SOURCE: Nipashe
 
Makamba.... Nape amefungiwa duniani hata mbinguni

2008-09-09 12:01:46
Na Simon Mhina


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, amesema zama za Nape Nnauye kisiasa ndani ya Umoja wa Vijana (UVCCM) zimefikia tamati na haruhusiwi kukata rufaa mahali popote.

Vilevile, Makamba amesisitiza kuwa Nape, mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa mkongwe nchini Marehemu Moses Nnauye, hataruhusiwa kugombea wadhifa wowote ndani ya umoja huo.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana kutoka Dodoma, Makamba alisema Baraza Kuu ambalo lilimvua Nape uanachama wa UVCCM, lina nguvu kikatiba kufanya hivyo.

Alisema baraza hilo linayo mamlaka ya kufanya kazi za Mkutano Mkuu kama kumfuta mtu uanachama.

Alipotakiwa atoe ufafanuzi juu ya haki za kijana huyo akiwa kama kiongozi wa juu wa CCM, Makamba alisema Nape hana pa kwenda.

Alisema kama angekuwa amefutwa uanachama wa CCM, na vikao vya chini, angekuwa na haki ya kukata rufaa vikao vya juu, lakini kikao cha Baraza Kuu la UVCCM kilichomfuta uanachama, hakuna kingine kinachozidi hapo.

``Suala la rufaa halipo, hawezi kuja kwenye Kamati Kuu ya CCM wala Halmashauri Kuu, hayo ni mambo ya UVCCM na kama angefukuzwa na kikao cha chini cha umoja wa vijana, angekuwa na haki ya kukata rufaa kwenye Baraza Kuu, lakini sasa hilo ndilo limemtimua, hana pa kwenda,`` alisema.

Kutoakana na kufutwa uanachama, Makamba alisema moja kwa moja jina la Nape limefutwa kwenye orodha ya wagombea wa uenyekiti wa UVCCM taifa.

``Imeandikwa, katika Biblia kwamba mtakaowafungia duaniani wamefungiwa na Mbinguni,`` alisema na kuongeza: ``Kwa hiyo kwa vile Nape amefungiwa na Baraza Kuu, amefungiwa pia kwenye vikao vitakavyojadili wagombea.``

Makamba alimshauri Nape kwamba iwapo sasa anataka kugombea cheo chochote, labda aende akagombee kwenye Jumuiya ya Wazazi.

Alipotakiwa kuzungumzia madai kwamba kulikuwa na shinikizo kutoka nje ili Nape afukuzwe, Makamba alisisitiza kwamba halikuwepo kwa vile na yeye ni mjumbe.

``Mimi Mwenyewe ni mjumbe wa hilo Baraza, sisi ndio tuliomvua uanachama, hakuna unafiki uliofanyika, ifahamike wazi kuwa nami nilishiriki kumng`oa,`` alisema.

Alipoulizwa kuwa haoni adhabu aliyopewa Nape ni kubwa mno, alisema kwamba siyo, bali anastahili kwa vile amethubutu kukata tawi alilokuwa amekalia.

Kuhusu hatma ya kisiasa ya kijana huyo, Makamba alisema ni jambo linalomhusu Nape mwenyewe.

Juzi Baraza Kuu la UVCCM lilimfukuza uanachama Nape kwa kuvunja kanuni za jumuiya hiyo. Hata hivyo Nape bado ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.

SOURCE: Nipashe
 
Yusuf Makamba said:
``Imeandikwa, katika Biblia kwamba mtakaowafungia duaniani wamefungiwa na Mbinguni,`` alisema na kuongeza: ``Kwa hiyo kwa vile Nape amefungiwa na Baraza Kuu, amefungiwa pia kwenye vikao vitakavyojadili wagombea.``


Hivi Huyu Yusuf Makamba ana Akili Timamu Kweli?
 
Nakumbuka sana ule msemo wa Mzee wetu Nyerere (RIP).... "DHAMBI YA KULA MTU HUWA HAIFI...." sasa huyu Mheshimiwa sana NCHIMBI aka MZEE WAKUTUNDIKA MAKOTI anakumbukumbu ya hiyo hotuba nadhani Mwalimu alikuwa anakipawa cha kuona mbali maana kama mlikuwa mnafuatilia hotuba zake mengi naona yanajitokeza sasa.

Matabaka aliokuwa anayakemea ndani ya chama sasa ndio yameibuka tena kwa kasi ya ajabu, laiti Mwenyezi Mungu angeweza kumrudisha walao kwa mwezi mmoja tu huu ujinga jiinga wa kina Nchimbi usingekuwebo, halafu najiuliza huyu Makamba kwanini wanaendelea kumfuga ndie anayechangia kwa kiasi kikubwa huu uowozo, inamaana CCM imeshindwa kutafuta katibu alie kuwa na vigezo vinavyostahili, Makamba anafaa kuwa DIWANI wa MTAA sio kuoshika nyadhifa hiyo. Naomba mwenye profile la Makamba aliweke tuichambue kwa kina nina wasiwasi na ule U-CAPTAIN wake alionao.

UVCCM mmekosa kabisa wazee wakuwapa hekima kama mnawaitaji kuliko kuwaweka hao kina Kingunge na Kawawa mbona CCM inawazee wako safi na wenye hekima na tija.Tanzania yoteee hiiiiiiiii mmekosa wazeeeeee jamani hebu amkeni. Kina Lowasa ni MAFISADI TU HAWANA CHOCHOTE ZAIDI YA KUWASHAURI JINSI GANI MMFISADI NCHI.

NA MSUBIRI JK TUONE KAMA ATAKUWA NA JIPYA KUHUSU HII ISSUE YA NAPE AU ATAWABEMBELEZA NA KUWAKUMBATIA MAFISADI KAMA KWENYE HOTUBA YAKE YA MWISHO????
 
Kiyama cha Nape CCM leo

Na John Daniel, Dodoma

KAMATI Kuu ya CCM, inayokutana leo mjini hapa, inakabiliwa na mtihani wa kukubali au kukataa mapendekezo ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama hicho (UVCCM) ya kumvua madaraka yote, Bw. Nape Nnauye, kwa kilichoelezwa kuwa ni kuvunja kanuni za Umoja huo.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya wajumbe wa kikao hicho chenye nguvu na kinachotoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama (NEC), kitachofanyika mijini hapa keshokutwa, kuna mgawanyiko huku baadhi yao wakionesha wasiwasi wao kama Bw. Nape ametendewa haki au amehukumiwa kwa sababu za ugomvi kati yake na viongozi wa UVCCM na wadhamini wake.


"Nafikiri bado kuna maswali mengi ya kujiuliza kuhusu huyo Bwana (Nape), inawezekana kulikuwa na shinikizo kubwa kutoka kwa hao wakubwa wake na wadhamini, unajua wana nguvu na ushawishi mkubwa, sasa sijui wajumbe wa CC na NEC watamua vipi," alisema moja wa wajumbe wa Halmashauri Kuu.


Kanuni kwanza


Hata hivyo baadhi ya wana CCM waandamizi waliipongeza hatua ya Baraza la UVCCM dhidi ya Nnauye, wakisema imezingatia kanuni za msingi za Jumuiya hiyo na hivyo kilichotakiwa ni kuzifuata na kuchukua hatua.


"Watu wanaweza kusema mengi kuhusiana na hatua hii, lakini ieleweke kuwa siasa za siku hizi nchini zinaelekea katika watu kutafuta umaarufu na hivyo kujikuta wakivunja kanuni walizokubaliana, lakini wakibanwa huanza kulia na kutafuta visingizio vya kuonewa," alisema kiongozi wa CCM ambaye hakutaka kutajwa jina.


Alisema kimsingi CCM inakubali kukosolewa na kujikosoa, lakini hata hivyo ina kanuni zake na mahali pake pa kutolea ushauri au malalamiko au kukosoa na si popote kama ilivyofanywa na Bw. Nape.


Alisema Bw. Nnauye kiumri alijua kabisa asingestahili kugombea nafasi ya uenyekiti wa UVCCM kwa kuzingatia umri wake, kwani angefikisha miaka 35 akiwa bado mwanachama wa UVCCM wakati anajua kanuni hazimruhusu.


"Sasa alipoona hata yeye kwamba hawezi kugombea, akatafuta upenyo wa kutafuta umaarufu ndipo akachukua fomu kugombea na kuanza kutafuta kinga nje ya kishabiki na kutoa kauli za kupotosha na hata kutukana viongozi, sasa amebanwa analalamika, asubiri uamuzi wa vikao vya juu," alisema.


Uchunguzi uliofanywa na Majira mjini hapa ulionesha kwamba suala la kuondolewa kwa Bw. Nape kumeleta mawazo tofauti huku baadhi yao, wakidai kuwa kumetokana na yeye mwenyewe kuweka mawazo yake mapema kabla ya kufikia hatua ya kuongoza UVCCM, jambo lililosababisha watu kujua mwelekeo wake hivyo kufanya maadui zake kupata mwanya wa kummaliza.


Baadhi yao walidai kwamba licha ya kuondolewa kwake katika Umoja huo na kinyang'anyiro cha uenyekiti, lakini bado suala la uchunguzi kuhusu mradi wa UVCCM katika kiwanja namba 1081/2 Dar es Salaam ni muhimu hasa katika kipengele cha uwekezaji na muda wa wawekezaji.


Pamoja na mambo mengine CC katika kikao chake cha leo itajadili na kumteua rasmi mgombea wa CCM katika Jimbo la Tarime iliyoachwa wazi na marehemu Chacha Wangwe.


Habari kutoka ndani ya CCM, ilieleza kwamba jina la mgombea huyo litatangazwa rasmi Septemba 13 mwaka huu, siku mbili baada ya kumalizika kwa kikao cha NEC mjini hapa.


Pia CC itajadili majina yaliyopitishwa na UVCCM kuwania uenyekiti wa umoja huo baada ya Bw. Nnauye kuenguliwa rasmi juzi kwa kuvunja kanuni ya 17(c) na Ibara ya 18(b) ya kanuni ya Umoja huo kwa kuzungumza nje ya vikao halali.


Aapa kuendeleza mapambano


Siku moja baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) kutangaza kumfuta uanachama, Bw. Nape amesisitiza kuwa ataendelea kusimama kidete kutetea anachokiamini kuhusiana na ujenzi wa mradi wa Jumuiya hiyo, wanaripoti Reuben Kagaruki na Said Mwishehe.


Bw. Nape ambaye alikuwa akigombea uenyekiti wa UVCCM kabla ya kufutwa uanachama, alisisitiza kuwa kauli zinazotolewa na viongozi wa umoja huo, kuwa alikana kutoa taarifa hizo, si za kweli bali wanataka kupotosha ukweli.


Akizungumza na gazeti ili kwa simu Dar es Salaam jana, Bw. Nape alisema ataendelea kusimama na kutetea kile alichokisema kuhusiana na ujenzi wa mradi huo.


Alisisitiza kuwa amesikitishwa na kauli iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Bw. Francis Isack, kuwa alipoulizwa kama alitoa taarifa zilikuwa zikiripotiwa na vyombo vya habari, alikanusha.


Jana vyombo vya habari vilimkariri Bw. Isack akisema Bw. Nape alipoulizwa kuhusu taarifa zilizokuwa zikiandikwa kwenye vyombo vya habari, alikanusha kuhusika nazo na kusema magazeti yalilenga kufanya biashara.


Alisema mali za UVCCM zinasimamiwa na Bodi ya Wadhamini hivyo kama kuna matatizo wa kuulizwa ni wao (Bodi).


Alipoulizwa amepokeaje uamuzi wa UVCCM kumvua uanachama, Bw. Nape alisema Baraza Kuu si kikao cha mwisho ndani ya CCM, hivyo ana matumaini vikao vingine vitatoa uamuzi utakaomtendea haki.


Bw. Nape alitaja vikao ambavyo vinaweza kubatilisha uamuzi wa UVCCM kuwa ni Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Kamati Kuu (CC), Kamati ya Maadili na Sekretarieti.


"Bado nina imani na vikao hivi, wao kama vijana wana uhuru wa kutoa uamuzi wao," alisisitiza. Alipoulizwa kama ataendelea kubaki ndani ya CCM iwapo uamuzi utaendelea kama ulivyo, alijibu kuwa kwa sasa ni mapema mno kutangaza hatua atakazochukua.


"Kwa sasa bado vikao vinaendelea, vikishamalizika nitasema ni nini kitafuata," alisema na kuwataka wafuasi wake kuendelea kumuunga mkono, kwani siasa ni lazima mtu avuke milima na mabonde.


Bw. Nape alipoulizwa kama kufutwa kwake uanachama kunatokana na yeye kuwa tishio kwenye kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya uenyekiti, alisema hawezi kujua kilichomo ndani ya moyo wa kila mmoja.


Alisema hadi jana alikuwa hajapewa taarifa za kuvuliwa uanachama kwa maandishi. Alipoulizwa kama alipewa nafasi ya kusikilizwa, Bw. Nape alijibu kuwa juzi aliitwa na Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM na kueleza kile alichokisema na hakukuwa na maswali.


Hivi karibuni, Bw. Nape alikaririwa na vyombo vya habari akiwatuhumu Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la UVCCM, Bw. Edward Lowassa, mbunge wa Monduli na aliyekuwa Waziri Mkuu kuwa anahusika na mkataba tata wa mradi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya umoja huo.


Wengine waliokuwa wametajwa katika tuhuma hizo ni Mwenyekiti wa UVCCM, Dkt.Emmanuel Nchimbi na aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Bw. Amos Makalla, ambaye kwa sasa ni Mweka Hazina wa CCM.


Kutokana na kauli hizo, Baraza Kuu la UVCCM lililokutana juzi liliamua kumvua uanachama kwa kile kinachodaiwa alivunja kanuni ya 17(C) ya umoja huo kwa kutoa taarifa za uongo.


Katika hatua nyingine, uamuzi uliotolewa na UVCCM dhidi ya Bw. Nape umeonekana kuwaudhi baadhi ya viongozi wa CCM na kueleza kuwa umoja huo umekurupuka kwa kuchukua uamuzi wa kumfuta uanachama na kupendekeza avuliwe madaraka aliyonayo chini ya mwavuli wa CCM.


Kiongozi wa CCM aliyezungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa jina, alisema jana kuwa uamuzi uliotolewa na umoja huo unaweza kutafsiriwa vingine na wabaya wa chama hicho.


"Wangeweza kusubiri kwa kuheshimu mawazo yake, leo hii mtu anagombea ndani ya kipindi hicho hicho anaadhibiwa kwa kufutwa uanachama, unadhani hiyo inaleta picha gani?," alihoji


Aliongeza kuwa kauli za Bw. Nape ziligusa chama chote na si UVCCM tu, hivyo walipaswa kusubiri ili chama kitoe uamuzi wake.


Aliongeza kusema kuwa "Mbona wabunge wanawasema mawaziri na wengine wanafikia hatua ya kujiuzulu nyadhifa zao hawachukuliwi hatua za kinidhamu na chama?," alihoji kiongozi huyo na kuongeza kuwa iweje adhabu hizo aanze kupewa Bw. Nape.


Alisema kitendo hicho kinalenga kuonesha kuwa Bw. Nape amefanya kosa kubwa ndani ya CCM. Kiongozi huyo alisisitiza kuwa uamuzi wa UVCCM kumfuta uanachama Bw. Nape, unalenga kufananisha chama hicho na CHADEMA ambacho kilimsimamisha uongozi aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wake marehemu Chacha Wangwe, baada ya kuhoji mapato na matumizi ya fedha za ruzuku.


Kiongozi huyo alisisitiza kuwa umoja huo umekurupuka na unataka kuwapa nafasi wapinzani kukisema vibaya chama hicho.


Kwa upande wao, viongozi wa vyama vya upinzani waliozungumza na gazeti hili, walisema uamuzi wa kumfuta uanachama UVCCM Bw. Nape, unalenga kuonesha jinsi chama hicho kisivyopenda kukosolewa.


Wapinzani wachekelea


Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustino Mrema, alisema CCM imemtoa kafara kijana huyo. "Ufisadi ndani ya CCM umeota mizizi, iweje leo hii wamtoe kafara kijana mdogo kama Nape?," alihoji.


Alisema haiwezekani waliohusika kwenye 'ujambazi' wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa chini ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) wapewe muda wa kulipa fedha walizoiba huku wanaosimama na kutaka mabadiliko ndani ya CCM akifukuzwa.


Alisema inashangaza kuona mtu anayetaka mabadiliko ndani ya CCM akifukuzwa na kuwataka wabunge wa CCM wanaokemea maovu ndani ya Serikali ya chama hicho kuwa makini kwani uamuzi uliotolewa dhidi ya Bw. Nape ni salamu kwao.


"Hii ni message (ujumbe) imetumwa kwa wabunge wa CCM watambue kuwa mtu anayetikisa uhai wa CCM ataishia pabaya," alisema Bw. Mrema na kumtaka Bw. Nape kuhama chama hicho kwani CCM si baba wala mama yake.


"Nape ni kijana mdogo asidhani kuwa akihama CCM ndio mwisho wa maisha yake," alisisiza Bw. Mrema.


Naye Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa, alisema alishawahi kusoma magazeti yakimnukuu Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuf Makamba, akiwataka vijana waache kuchafua chama kwa kusema hadharani.


Alisema kauli hiyo ilikuwa inalenga kuficha uchafu ndani ya chama hicho. "Wanachofanya ni kukigeuza chama hicho cha mafisadi kwa kuwafukuza wanaosema ukweli," alisema.


Alipoulizwa kama chama hicho kitakuwa tayari kumpokea Bw. Nape iwapo atatangaza uamuzi huo alijibu; "Mtu akitoka kwenye Ukristo na kwenda kwa Waislamu huwa anapokewa".
 
Nadhani JK ameondoka mchana huu nimeona msafara wake saa nane ya leo ukielekea Airport
 
Katibu huyo, alisema kufanya hivyo ni sawa na kukiletea chama mauti kwani tabia hiyo inaweza kuibomoa UVCCM na wakati huo huo kudhalilisha chama.


Sasa Makamba hapo mbona kama anajikaanga mwenyewe..haoni kama yeye ndie anaekiletea chama mauti....

Alisema Jumuiya za vijana ndio chimbuko la kupata viongozi wa juu wa Taifa hivyo vijana hawana budi kukipenda chama chao na kuepuka majungu yanayoweza kukibomoa chama hicho.
“Mambo mengine yanayofanywa na vijana ni mauti kwa chama,kuisema Jumuiya ni kuibomoa Jumuiya hiyo na chama kwa ujumla halafu baadaye tutakosa viongozi mahiri wanaoweza kuongoza nchi,”alionya Bw. Makamba

INAWEZEKANA WAKATIA AKIONGEA SAUMU ILIMBANA AKASHINDWA KUELEWA AMESEMA NINI?


Awali akifungua kikao hicho, Mwenyekiti wa UVCCM,Bw. Emmanuel Nchimbi aliwataka wajumbe wa Baraza hilo kuchagua vijana wenye uwezo wa kuongoza badala ya kuangalia sura na jina la mtu.

Alisema ili kupata viongozi wazuri watakaongoza Jumuiya hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, wajumbe hawana budi kuchagua wanachama wenye umri stahili na kupima utendaji wa wagombea hao.
SASA HAPA NCHIMBI ANAONE YEYE UTENDAJI WAKE NI MZURI?

Akifafanua suala la umri, Bw. Nchimbi, aliwataka wajumbe hao kutomwonea haya mgombea yeyote aliyevuka umri kwani lengo la umoja huo ni kuwa na timu nzuri ya Baraza lijalo.
WAKATI YEYE ANAGOMBEA HUO UWENYEKITI ALIKUWA NA UMRI GANI? HAJIONI YEYE KUWA AMEVUKA UMRI " KWELI ULE MSEMO WA WAHENGA NYANI HAONI....

Aliwataka vijana kuwa na mapenzi mema na chama chao badala ya kujenga chuki na ubinafsi jambo ambalo alisema linasababisha makundi yasiyokuwa na msingi ndani ya Jumuiya hiyo na chama kwa ujumla.

HII NI WAZI KABISA YEYE HANA MAPENZI MEMA NA CHAMA ZAIDI YA CHUKI BINAFSI NA UFISADI NDANI YAKE MAANA KULA YAO NDIO IMEINGIA MCHANGA WALITEGEMEA 10% KTK MRADI SASA WAMEUMBUKA.[/QUOTE]
 
Siasa za CCM ndizo zinazodumaza demokrasia nchini.Kwa miaka mingi tumeshuhudia wanasiasa mahiri ndani ya CCM wakipata wakati mgumu pale wanapoamua kuweka mambo hadharani kwa lengo la kuinusuru nchi na siasa chafu za wana CCM walio wengi.

Kauli ya Makamba kuwa vijana wa CCM wasikiseme chama hadharani ni sawa na kuwaambia wasiseme chochote kwa yeyote mahala popote.Ni siasa za kutishana na kulindana.N i mfululizo wa aliyoyasema Kingunge Mwiru hivi karibuni kuwa wapo wana CCM wanaojitafutia umaarufu kwa kuisema CCM.

Hali ni mbaya sana kwa CCM na njia pekee iliyobaki ni kuua nguvu ya upinzani kwa gharama yoyote.Upinzani dhidi ya CCM hautoki nje tu bali hata ndani ya CCM kwa watu kama Nape Nauye.Tutaendelea kushuhudia kauli kama hizi na vitisho kama hivyo.

Siye yetu macho tu
 
Hivi ni kwanini watu machachari huwa hawadumu Bungeni? Hebu tujiulize, wako wapi Benedicto Mutungirehi, Masumbuko Lamwai, Mabhere Marando, Dr Kaborou (alikuwa mbunge wa Kigoma Mjini kupitia CHADEMA). Wanashindwaje kuya-maintain majimbo yao inapofika kipindi cha uchaguzi?

Hii inashiria kwamba hata kina Zitto Kabwe wanaweza kushindwa kwenye uchaguzi wa 2010 kwa staili hiyo hiyo iliyowakumba hao wachache niliowataja hapo juu. Ingekuwa vipi kama hao wote wangekuwa bado wako Bungeni na wakapata nguvu ya ziada toka kwa Dr. Slaa, Zitto na Kilango?

Naanza kupata picha pana zaidi kuhusu ufisadi. ni donda ndugu ambalo si tu linadhoofisha maendeleo ya nchi, bali linadumaza ukuaji wa demokrasia. Mafisadi wanatumia pesa nyingi sana kwenye majimbo ya uchaguzi ambayo yanaonekana ni "THREAT" kwao. TAFAKARI!
 
Back
Top Bottom