Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sikujua kuwa Nchimbi anaweza kuwa na wapiga debe wa nguvu sana kwenye ukumbi huu hadi wanadiriki kutangaza waziwazi kuwa Nape hamuwezi Nchimbi. Yaani inaonyesha wazi kuwa kulikuwa na bifu kali kati ya Nape na Nchimbi na Nchimbi akawa mshindi, at least for now. Hata hivyo nadhani kuwa ushindi huo hauna manufaa kwetu wananchi tuliochangishwa hela nyingi sana kujenga vitega uchumi mbalimbali za CCM likiwemo jengo hilo la vijana linaloleta bifu hili.
 
Sikujua kuwa Nchimbi anaweza kuwa na wapiga debe wa nguvu sana kwenye ukumbi huu hadi wanadiriki kutangaza waziwazi kuwa Nape hamuwezi Nchimbi. Yaani inaonyesha wazi kuwa kulikuwa na bifu kali kati ya Nape na Nchimbi na Nchimbi akawa mshindi, at least for now. Hata hivyo nadhani kuwa ushindi huo hauna manufaa kwetu wananchi tuliochangishwa hela nyingi sana kujenga vitega uchumi mbalimbali za CCM likiwemo jengo hilo la vijana linaloleta bifu hili.

Waache mafisadi wakiue chama chao cha kifisadi. Walidhani wanamkomoa Nape kwa kumfukuza uanachama wa UVCCM lakini hawajui wamempa umaarufu mkubwa nchi nzima. Labda nguvu za Nape zinaweza kukisambaratisha chama hicho cha mafisadi. Kama kuna wenye akili ndani ya chama hicho watajua nani anayestahili kufukuzwa kati ya Nchimbi na Nape.
 
nape naona anawapeleka mchaka mchaka kweli kweli wazee wa ccm .......akumbuke wenzio wameshiba ufisadi, pressure ipo juu asije kuwauwa tu!
 
Of course, we will bring an exclusive uncut, unedited interview with Nape Nnauye on KLHN early in the morning tomorrow. About 15 minutes that will thrill you and make you tap your foot, drop your jaw and say.. I know why!

Safari hii sitakosa intavyuu hii ingawa itakuwa ni usiku sana nyumbani kwangu, lakini nitasikiliza tu; unajua niliamua ku-donate Kidney Foundation ile laptop yangu iliyokuwa hainipi sauti na kujipatia nyingine yenye "Sauti Safi Sauti Kubwa." Kwa hiyo siku hizi sikosi uhondo tena; kwani wacheza na miye kumbe.

LOL! Nyani


Ah! Unajua watu wengi wamekuwabadilisha majina yao hadi inafikia tunashindwa kuunganisha post zao na hulka zao. Je huyu Nyani MacCain ndiye yule Nyani Ngabu?
 
Jamani, sisi humu ndani tuwe objective kidogo na tujaribu kuangalia vitu kwa mapana yake.

Issue hapa sio Nape kabisa, issue kubwa ni kuwa The Powerful duo are playing Chess against our president and they have called checkmate, and we will all know exactly who has won depending on the following::

1) Kama CC na NEC watapitisha mkataba wa jengo la UVCCM, basi JK atakuwa amepigwa bao la mwaka na mimi binafsi ndio itakuwa mwisho wa kupoteza muda kusubiri chochote cha maana toka kwake. Nape amepewa adhabu kwa kusema kuwa Lowassa kahusika na ufisadi wa jengo, jambo ambalo ni wazi na wala halina ubishi, sababu mkataba unazungumzia wazi kuwa gharama za kujenga jengo jipya zitatoka bank kama mkopo against the title ya kiwanja, which means Shubash Patel ( Na partners wake walio wazi) Hawahitajiki kwani hawana capital na ONLY in TZ eti watakuwa na 75% hisa!! Kwa lipi?? UVCCM ni kuchukua tu mkopo CRDB na kujenga hilo jengo na kuown 100%.

2. Nape inajulikana wazi kuwa sio chaguo la JK kuwa mwenyekiti wa UVCCM, kwa hiyo the duo walijua wakimwacha aendelee kugombea watakuwa hawajashinda against JK, so kuforce issue na kumweka JK kwenye wakati mgumu wamemsimamisha Nape uanachama wakitaka public ugomvi. Jiulize mwenyewe kuna haja gani ya kurudia makosa kama yaliyotokea wakati wa kumsimamisha Zitto bungeni?? Hawa mafisadi sio wajinga wanajua kabisa hii issue inapotential ya kuwa disaster lakini wameweigh benefits zitakazokuja kama JK akishindwa kumrudishia Nape uanachama wa UVCCM, na wamekubali kuchukua risk. Nchi nzima itaelewa kuwa mafisadi wana nguvu kuliko Presida kama huu wazimu wa kumsimamisha Nape na mkataba wa Jengo vikiruhusiwa kusimama.

Ni maoni tu!!!
 
Fisadi mtoto,

Sio wewe uliekuwa against Nchimbi humu muda flani? imekuwaje mkuu umebadilika?

Kweli TZ hatuna wanasiasa kabisa wengi tunaganga njaa tu!

Ngoja nipate chai yangu hapa!
 
Fisadi mtoto,

Sio wewe uliekuwa against Nchimbi humu muda flani? imekuwaje mkuu umebadilika?

Kweli TZ hatuna wanasiasa kabisa wengi tunaganga njaa tu!

Ngoja nipate chai yangu hapa!

wewe mwenye akili kama zaako ndio unaweza kuwa against mtu hapa ndani.mimi niko against mawazo ya mtu.pale anapokuwa amewaza sahihi namuunga mkono.kwa sasa Nchimbi yuko sahihi kama vile nilivyounga mkono CHADEMA kumsimamisha Marehemu Chacha Wangwe kwa kuvujisha siri za chama na kuongelea matatizo ya ndani kwenye magazeti jambo ambalo linaumiza chama.
 
1

Mkuu nilitaka mimi na wewe twende step by step, of exactly who Nchimbi is tukaona jinsi alivyoshindwa kupasi darasa la Saba na kwenda kusoma Sangu, nikakuuliza Sangu ambayo na wewe ulisoma kama ni shule ya Serikali ya waliopasi hukujibu tena! Sasa kosa langu liko wapi? Haya matuisi ni wewe unayapenda sana eti kwa sababu wewe ni shoga wa Nchimbi basi inakupa power ya kuja hapa na kutukana na jina la mtoto wa fisadi, watu wengine mtaelimika lini jamani?

2.

No clue what is the point here?

3.

Anytime ukiwa tayari kuonyesha elimu nzito na ya halali ya Nchimbi, mimi nitakupa hiyo medali ya Nchimbi, lakini ulikuwa na all the time kufanya hivyo toka juzi sasa tatizo lilikuwa nini? Nani aliyekuzuia na nani anayekuzuia sasa?

4.

1. Hivi kwa nini uantaka kuchanganya ishus, aliyoyafanya Nchimbi jana nani amekataaa? Wote tumekubali kuwa jana Nchimbi amfanya aliyoyafanya kama mwenyekiti wa UV-CCM, hakuna aliyetegemea Nchimbi kufanya tofauti, lakini tunasema kuwa bado ishu itaenda CC, sasa hapa hoja yako ni nini?

2. Mimi unajua vyema ni lini nimewahi kukimbia hapa wala kubadili majina? Sasa leo au kesho cha ajabu kitakuwa ni kipi hicho as far as Nchimbi na CCM mpaka eti nikimbie na kubadili kauli? Sio tabia yangu hiyo hata siku moja mkuu!

I am always here, having a lot of fun and good time na ishus za taifa langu! uwe unawatisha wasiokujua vizuri na wanaoamini kuwa kweli wewe ni mtoto wa fisadi, not me mkuu!

Again Ahsante Sana.
kwanza si kweli kuwa Nchimbi alifeli darasa la saba na kwenda kusoma sangu,bali Nchimbi alikwenda kusoma Uru seminary ambako uko alisoma na kina Dk cyril Chami,ANtony Komu,Josephat Kweka etc...wakwti ule shule za seminary zilikuwa ni bora kuliko za serikali na hata inerview yake watu wajinga kama wewe walikuwa hawawezi kupass.Sangu alihamia akiwa form two.....sawa nimekubali kwamba kwa mtazamo wako ni kwamba Nchimbi elimu aliosoma ya mzumbe i mean undergraduate na masters ya MBA,maana ana MBA ya mzumbe pia. vyote ni fake,hapo sijajua ufake ni chuo au hakuwepo darasani kabisa?????tukimaliza hili twende hatua inayofata.
 
1) Kama CC na NEC watapitisha mkataba wa jengo la UVCCM, basi JK atakuwa amepigwa bao la mwaka na mimi binafsi ndio itakuwa mwisho wa kupoteza muda kusubiri chochote cha maana toka kwake.

2. Nape inajulikana wazi kuwa sio chaguo la JK kuwa mwenyekiti wa UVCCM!!!


...the secret behind mradi wa umoja wa vijana ..mastermind na financer ni SUBASH PATEL....long time friend wa kikwete tangu bagamoyo....na mnajua connections zao nyingine...yeye ndio anajenga pale...sasa rafiki yangu kama unategemea kikwete ni innocent kwenye hilo deal ...mhh...kikwete is a smooth operator....nadhani hata msishangai sababu za nguvu kubwa sana kutumika kumnyamazisha nape..zinatoka wapi.....

...hata kama kikwete akijitoa kwenye hili that will just be political...but utatu wa kikwete,lowassa,MTANDAO[MAFISADI,NCHIMBI,ROSTAM.....] upo pale pale...hadi dawa itakapotafutwa.....
 
ccm ni chama pekee afrika ambapo mafisadi hulindwa kwa nguvu zote na wasema kweli, watetezi na wapinga ufisadi wanapigwa vita.

Mh. Chenge (mzee wa vijisenti) - fisadi ambaye hakuna mtu anapinga kuhusu hilo, kwa aibu rais akamvua uwaziri lakini ccm haijamuonya, kumsimamisha wala kumvua uanachama!

Mh. Karamagi- aibu tupu, alikuwa anatembea na mihuri ya serikali; alisaini mktaba wa kifisadi akiwa london, mh. Zitto aliposema hilo ccm kutumia wingi wa wabunge wake bungeni wakamsimamisha ubunge! Alipokuwa implicated kwenye richmond, rais kwa shingo upande akamvua uwaziri. Ccm bila chembe ya aibu imeendelea kumbeba, hikumpa hata onyo kwa kuitia aibu serikali na chama tawala!

Nape nnauye, bangusilo (kondoo wa kafara) kukemea ufisadi na kupigia kelele mktaba wa uwekezaji uv-ccm imekuwa nongwa; amevuliwa uanachama uv-ccm; ati hana nidhamu ; kwa kuwa hakuukumbatia ufisadi (u-ccm)! Ati ameitia aibu uv-ccm! Haya ndo maajabu ya ccm.

The list is very long.... You cana add and add and add! Aibu tupu.

Ccm, ccm, njia gani umekwenda wewe? Hawa wajumbe wa baraza kuu la uv-ccm hata ahadi za chama chao wenyewe hawazijui. Naomba niwakumbushe
ahadi moja muhimu:

'nitasema kweli daima fitina kwangu mwiko' nimewakumbusha tu; ccm, kumbuka ni wapi ulipoanguka ukatubu!
 
Kwa kauli ya makamba "amefungiwa dunuani mpaka mbinguni" very interesting
 
1. wewe mwenye akili kama zaako ndio unaweza kuwa against mtu hapa ndani.mimi niko against mawazo ya mtu.

2. pale anapokuwa amewaza sahihi namuunga mkono.kwa sasa Nchimbi yuko sahihi

3. kama vile nilivyounga mkono CHADEMA kumsimamisha Marehemu Chacha Wangwe kwa kuvujisha siri za chama na kuongelea matatizo ya ndani kwenye magazeti jambo ambalo linaumiza chama.

Eti this time Nchimbi yuko sahihi? Mkuu Fair Play,

tizama maneno mengine ya huyu mkulu

"....Tusilaumu balozi za kina USA na UK hawa jamaa wanatuelewa watanzania ni watu wa kudanganywa siku zote si viogozi wala raia wa kwaida kubainisha hilo wangalie viongozi weu wanapokutana na viongozi wa nchi kubwa wanakuwa dhaifu... kabisa pili ukiangalia upande wetu wananchi wengi akili hazifanyi kazi hazina upeo amini leo hii kuna watu bado wanamini Mwalimu yupo hai na wanahoji kwanini hajafika kuwatembelea ,kunawengine wanafika viwanja vya ndege kwa imani watafirishwa kwamiujiza hayo yote ni shahidi tosha tumekuwa na majigambo mengi lazimatubadili hali hii"...

Wakuu Ben na Fidel

Huyu bwana ameruhusiwa kwa siku nyingi sana kutukana matusi humu ndani, sasa haya ndio matokeo yake, yake ndio haya mimi this time nimemua kumvulia uvivu, liwalo na liwe, ametukana watu hapa vya kutosha!
 
Fisadi mtoto,

Sio wewe uliekuwa against Nchimbi humu muda flani? imekuwaje mkuu umebadilika?

Kweli TZ hatuna wanasiasa kabisa wengi tunaganga njaa tu!

Ngoja nipate chai yangu hapa!

kunahaja kweli ya kuumiza kichwa na huyu FM mkuu.... we pata chai achana nae
 
Back
Top Bottom