Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Nasikia Nchimbi ni Mshirikina? nasikia ndio aliowauwa Ipyana Malecela etal? Bwana Nchimbi mi simo nauliza tu........
Ushirikina nai imani ambayo imeshamiri sana kwenye nchi masikini.msirikina ni yule anaetenda na anaeamini kama wewe.
 
Aliyekuwepo kwenye kikao sio Nchimbi peke yake, walikuwepo wengi sana, Nape alizisema habari za jengo kwa mara ya kwanza kwenye kikao cha baraza hilo hilo, sasa leo atasemaje kuwa ni waandishi?

Wajumbe hawakusema kwa kauli moja, ilikuwa ni kauli ya Makamba na hela zilizogawiwa na Tom, ndio zilizoimba huo wimbo, wajumbe hawawezi kusema Nape ni lipyoto halafu adhabu yake ipungue, hai-make a sense kwa mtu mwenye akili timamu!

Nchimbi ametumia faulo na hii faulo ilitegemewa, sasa kazi itakuwepo CC ambako Kingunge haingii na Nchimbi ni mtu wa kawaida kama wajumbe wengine, na ambako Makamba ni kichekesho.
Tom wa watu unamsingizia tu bure...amefika ukumbini toka dar saa kumi na moja jioni hizo hela aligawa muda gani.anafika na ajenda ya Nape inaanza,,kaka acha kudandia maneno ya mitaani.
 
1.
mkataba haujapelekwa cc kwa kuwa ni ufisadi bali ni utaratibu wa mchakato wa chama kwenye miradi mikubwa.....kesho kamati kuu inakaa.

Sio kweli, mkataba umevuka ngazi zote muhimu umekwenda moja kwa moja kwa Rais, hilo usijaribu kuli-spin, hapa unachojaribu ku-spin ni kuwa eti huu mkataba kwenda huko CC ni kitu cha kawaida, hilo sio kweli mkataba umekwenda huko baada ya Nape kuupigia kelele, na wala haukwenda huko wenyewe ila ulienda straight kwa Rais,

Jaribu kuwa na aibu kidogo na hizi spin, wadhamini wote wameitwa mbele ya Rais wamekataa kuhusika na mkataba, mawakili wa serikali, CCM, na wa binafsi wamekataa kuidhinisha mkataba sasa unapitishwaje na CC?

Utaratibu wa mchakato wa CCM ungetakiwa kufanywa kabla ya kuupitisha mkataba bro hizo ndio kanuni, huendi kuchakata mkataba baada ya jengo kuanza tayari, mbona unatufanya na sisi hapa kama ni UV-CCM? Hebu kitaje ni chama gani duniani kinachoachia mkataba wa jengo linaanza kwanza halafu ndio kinafanya mchakato?


2.
hakuna atakayejadili kufukuzwa kwa Nape kwenye kamati kuu.Napenda kukwambia wala huna haja ya kupiga kelele hapa.Kesho kabla ya saa kumi jioni CC itakuwa imepitisha mkataba kwa kauli moja....Nape atabaki anangojea hukumu yake.Na nilikwambia Mr Sadist.

1. Acha kujdanganya, ni lazima CC iatoe mapendekezo ya kwenda NEC kuhusu kufukuzwa kwa Nape, hayo maneno ya Nchimbi ya kujifanya anajua sana sio kanuni za CCM, kanuni za CCM ni lazima hii ishu ijadiliwe CC, ndio iende NEC ninaelewa kuwa kwa mawazo yako Nchimbi ni Mungu, lakini kanuni za CCM ni kwamba lazima hii ishu ikatazamwe CC, na ndivyo Nchimbi alivyokuwa ameagizwa na Rais, hiyo ni kanuni ya CCM kuwa lazima CC waiangalie hilo la Nape kufukuzwa, it has nothing to Nchimbi.

2. Mkataba umechunguzwa tayari na mawakili wengi tu tena mpaka independent kwa shinikizo la Rais, unless ameamua kujichanganya mwenyewe, maana juzi almkemea sana Mengi kuhusu maneno kama yako yaliyokuwepo Nipashe, sasa leo rais atageuka na kuupitisha, basi Nchimbi atakuwa ni very powerful man kama unavyoamini, lakini mimi ninaisubiri kesho in this.

3. Ulisema kwa jina la Fisadi Mtoto, sasa sielewi unapsoema ulisema kwa jina hili tena au?
 
Tom wa watu unamsingizia tu bure...amefika ukumbini toka dar saa kumi na moja jioni hizo hela aligawa muda gani.anafika na ajenda ya Nape inaanza,,kaka acha kudandia maneno ya mitaani.

Mbona hukusema toka jana, why saa hizi? Ndio kwanza wamekupigia simu nini? Bwa! ha! ha! ha! ha!

Wewe unayesema leo na mimi niliyekwua ninasema toka jana ya huko ndani nani anyedandia maneno mkuu? Jaribu ku-stick na hoja mbona umeanza vizuri na hoja sasa unaanza kubadilika na wewe una ukweli?
 
Mkuu soma maneno ya kijana hapa chini:-



Na Waandishi Wetu

1. HATUA ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (CCM) kumsimamisha na kupendekeza kumfukuza uanachama,Nape Nnauye, inaelekea kupingwa vikali na vikundi vya kijamii, vikiwemo vyama vya siasa na hata ndani ya kada za vijana wa chama hicho tawala.

2. Aidha, mtoto huyo wa mwanasiasa wa zamani wa CCM, Moses Nnauye amesema vyombo vya juu vya chama hicho vitamtendea haki katika kuamua suala hilo, ambalo alisema bado liko kwenye mkakati.

3. Nape alisimamishwa uanachama katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM kilichofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa wiki, akidaiwa kushindwa kuthibitisha tuhuma alizozitoa dhidi ya vigogo wa chama hicho kuhusu mkataba wa jengo la uwekezaji la UVCCM lililo jijini Dar es salaam.

4. Akizungumza kwa njia ya simu jana, Nnauye alisema Baraza Kuu si kikao cha mwisho kinachoweza kumsimamisha uanachama na kwamba yeye kama mwanachama halali wa umoja huo ana imani haki itatendeka katika vikao vya juu, ambavyo ni Kamati Kuu ya CCM, inayokutana leo, na Halmashauri Kuu itakayokutana kesho.

5. "Uamuzi wa baraza hauniatishi tamaa kwa kuwa vikao vya juu vya chama vinaweza kutengua maamuzi haya na nina imani na vikao hivyo na nina imani kwa chama kuwa haki itatendeka na hatimaye kupata haki yangu," alisema Nape.

6. Hata hivyo, Nape alisema mpaka sasa hajapokea barua rasmi au maelezo yoyote ya kumfahamisha juu ya uamuzi huo zaidi ya kusoma kwenye vyombo vya habari tu.
 
1.

Sio kweli, mkataba umevuka ngazi zote muhimu umekwenda moja kwa moja kwa Rais, hilo usijaribu kuli-spin, hapa unachojaribu ku-spin ni kuwa eti huu mkataba kwenda huko CC ni kitu cha kawaida, hilo sio kweli mkataba umekwenda huko baada ya Nape kuupigia kelele, na wala haukwenda huko wenyewe ila ulienda straight kwa Rais,

Jaribu kuwa na aibu kidogo na hizi spin, wadhamini wote wameitwa mbele ya Rais wamekataa kuhusika na mkataba, mawakili wa serikali, CCM, na wa binafsi wamekataa kuidhinisha mkataba sasa unapitishwaje na CC?

Utaratibu wa mchakato wa CCM ungetakiwa kufanywa kabla ya kuupitisha mkataba bro hizo ndio kanuni, huendi kuchakata mkataba baada ya jengo kuanza tayari, mbona unatufanya na sisi hapa kama ni UV-CCM? Hebu kitaje ni chama gani duniani kinachoachia mkataba wa jengo linaanza kwanza halafu ndio kinafanya mchakato?


2.

1. Acha kujdanganya, ni lazima CC iatoe mapendekezo ya kwenda NEC kuhusu kufukuzwa kwa Nape, hayo maneno ya Nchimbi ya kujifanya anajua sana sio kanuni za CCM, kanuni za CCM ni lazima hii ishu ijadiliwe CC, ndio iende NEC ninaelewa kuwa kwa mawazo yako Nchimbi ni Mungu, lakini kanuni za CCM ni kwamba lazima hii ishu ikatazamwe CC, na ndivyo Nchimbi alivyokuwa ameagizwa na Rais, hiyo ni kanuni ya CCM kuwa lazima CC waiangalie hilo la Nape kufukuzwa, it has nothing to Nchimbi.

2. Mkataba umechunguzwa tayari na mawakili wengi tu tena mpaka independent kwa shinikizo la Rais, unless ameamua kujichanganya mwenyewe, maana juzi almkemea sana Mengi kuhusu maneno kama yako yaliyokuwepo Nipashe, sasa leo rais atageuka na kuupitisha, basi Nchimbi atakuwa ni very powerful man kama unavyoamini, lakini mimi ninaisubiri kesho in this.

3. Ulisema kwa jina la Fisadi Mtoto, sasa sielewi unapsoema ulisema kwa jina hili tena au?
Mimi ni nakuwa mpole kwa kuwa najua wewe kuwa huwa hukubaliani n a ukweli na ni mbishi....ulisema kama kweli Nchimbi alisimamia ujenzi wa shule utampa nishani,ukasema unamtafuta Kajege.umekimbia kimyakimya....sasa leo umesema kama kesho mkataba utapitishwa basi utaamini kuwa Nchimbi ni most powerful man kuliko JSM....Naomba kesho uonyeshe uungwana kwa kuja na kukiri wazi kuwa humwezi wewe,wala mama yako Kilango na wala Mh Seguyemisi...plz uje na kukubali please.
 
Wewe naamini ni kichaa kabisa na nashangaa kwa nini hawakushauri....Nchimbi alikuulia mama yako mzazi? mnakufa na ukimwi mnasema mnalogwa mbwa wewe.

si lazima uandike vijitusi humu, waweza tukana kwa sauti hapo ulipo bila kupost ingekuwa vyema zaidi.
 
Mbona hukusema toka jana, why saa hizi? Ndio kwanza wamekupigia simu nini? Bwa! ha! ha! ha! ha!

Wewe unayesema leo na mimi niliyekwua ninasema toka jana ya huko ndani nani anyedandia maneno mkuu? Jaribu ku-stick na hoja mbona umeanza vizuri na hoja sasa unaanza kubadilika na wewe una ukweli?
Ni kweli nilikuwa nangojea nipate uhakika wa yaliotokea kutoka vyanzo tofauti vya habari na sio kukurupuka kama wewe.
 
Bila kujali tofauti zetu kisiasa lakini kufukuzana uanachama na uongozi ni tabia za kikomunisti ambazo zimepitwa na wakati.

Kama mtu hafai basi mpeleke kwenye wanachama wakaamue hatima yake na wala sio kagenge ka wapambe kanaamua kufanya maamuzi ya kijinga kama hayo. Inatakiwa kiongozi asimamishwe/afukuzwe na kikao kile kile kilichomchagua na sio vinginevyo.

Nape kama ana umri mkubwa, hana sifa ya kuwa mwenyekiti wa UVCCM. Ila kumfukuza uanachama ni siasa za kizamani na kijinga ambazo haziwezi kujenga taifa.
 
1.
Mimi ni nakuwa mpole kwa kuwa najua wewe kuwa huwa hukubaliani n a ukweli na ni mbishi....ulisema kama kweli Nchimbi alisimamia ujenzi wa shule utampa nishani,ukasema unamtafuta Kajege.umekimbia kimyakimya

Unakuwa mpole sana ni kweli, ila nilikuomba tuanze na mjadala wa elimu ya Nchimbi kwanza ukakataa, maana hatuwezi kukimbilia shule kabla ya kujua elimu ya Nchimbi, sasa vipi uko tayari kujadili elimu ya Nchimbi kwanza halafu twende kwenye hizo shule alizojenga bila yeye mwenyewe kua na elimu? Ukiwa tayari nifahamishe!

2.
....sasa leo umesema kama kesho mkataba utapitishwa basi utaamini kuwa Nchimbi ni most powerful man kuliko JSM....Naomba kesho uonyeshe uungwana kwa kuja na kukiri wazi kuwa humwezi wewe,wala mama yako Kilango na wala Mh Seguyemisi...plz uje na kukubali please.

1. the fact kwamba huna wazazi na unajaribu kulazimisha kila kiongozi awe mzazi wako, sio kosa langu, mpaka kujifanya mtoto wa fisadi ili uonekane una wazazi viongozi wakati wewe ni masikini hohe hahe kama mimi, ni dalili tosha ya kwamba hapa ninajadili na mtu wa aina gani!

2. Umejaribu kuwarukia Malecela na Mkewe ili uonekane kua mtoto wao, lakini umeshindwa kwa bahati nzuri through mgongo wao na kwenda kujikomba komba Dodoma, badala ya kwenda kwenu kwa ndugu zako, ukaishia kuwajua Nchimbi na Mwakyembe, kwa hiyo ulipofukuzwa kwa Malecela kwa sababu za unafiki, sasa ndio ukarukia kuwa mtoto wa Nchimbi na Mwakyembe, na kwamba sasa wewe ni mtetezi wa Nchimbi na huku bado ukiendelea kujikomba kwa watoto wa Malecela, ambao hawaji hapa wala hawakujui vizuri tabia zako za unafiki, nimewaonya mara nyingi sana kuwa kuna siku utawaletea sumu kutoka kwa huyo bosi wako lakini na wao hawasikii, lakini mzee na mama wamesikia, na ninajua kua Mwakyembe naye hakuelewi vizuri maana na yeye sasa hivi atakufukuza, kama ulivyofukuzwa na yule balozi na makaratasi yako uliyompora Mike kwamba una kiwanda cha mafuta, siku zote mtu wa aibuu tu na kujikweza kweza kwa kutumia watu kumbe huna lolote, siku nyingi unatukana sana matusi! ninakuangalia tu, leo niko kwenye faulo mood bring it on!

Sasa usinitishe na hayo amneno ya Malecela na Mama Kilango, umejikom,ba weee umetumiwa weee, sasa endelea kutumiwa huko kwa Nchimbi maana that is all your life is about huwezi kusimama hata siku moja on your own lazima tu kujikweza kweza, wakati you are no body!

Jana nilikuwepo hapa, na leo nipo hapa nakesho nitakuwepo hapa, siwezi kukimbia kwa sababu eti wewe ni messenger wa Nchimbi hata siku moja bro, ndio maana toka jana ulikuwa kimyaa maana walikuwa kwenye mkutano kwa hiyo ilikwa usubiri mpaka leo wakutumie ujumbe ndio uanze kubadili majina hapa ili utishie watu nonesense! mimi sikuogopi hata siku moja na huo ushambenga wa kutumwa! Ni muda mrefu sasa unalilia Malecela na Mama kilango, sio tatizo langu walikufukuza mkuu! na kwamba sio wazazi wako, na hwanihusu and I could careless kwa yoyote anyejikomba komba kwa viongozi!

CC inakutana kesho na nitakuwa hapa hapa kuchambua uamuzi wake, kama unataka kumtetea Nchimbi nimekuambia siku zote stick na jina moja halafu simamia hoja sio ujinga wa yanga na simba!.

Ahsante Mkuu!
 
Bila kujali tofauti zetu kisiasa lakini kufukuzana uanachama na uongozi ni tabia za kikomunisti ambazo zimepitwa na wakati.

Kama mtu hafai basi mpeleke kwenye wanachama wakaamue hatima yake na wala sio kagenge ka wapambe kanaamua kufanya maamuzi ya kijinga kama hayo. Inatakiwa kiongozi asimamishwe/afukuzwe na kikao kile kile kilichomchagua na sio vinginevyo.

Nape kama ana umri mkubwa, hana sifa ya kuwa mwenyekiti wa UVCCM. Ila kumfukuza uanachama ni siasa za kizamani na kijinga ambazo haziwezi kujenga taifa.
hakuna chama kisicho na maadili.Nape kafukuzwa ni kikao halali kabisa.wajumbe 108 wa baraza kuu la taifa kutoka mikoa 26 ya tanzania.wanachama gani uliotaka wakae zaidi ya hao wawakilishi halali waliopewa nguvu ya kikatiba na ccm ya kuwarudi watu kama nape....futa kauri yako ya wajumbe halali
 
Ni kweli nilikuwa nangojea nipate uhakika wa yaliotokea kutoka vyanzo tofauti vya habari na sio kukurupuka kama wewe.

Wakubwa wako walikuwa kwenye mkutano, mbona ulikuwepo na majina yako mengine, acha utoto na ujinga ujinga you are too old na huu upuuuzi!

Saa hizi ndio wamekupa spin ndio unajtokeza na majina ya kijinga jinga! sio wote hapa ni wajinga, hapa tunakuja kuelimishana na kuhabarishana, sio wote tuko hapa kusubiri orders za Nchimbi!

Mkuu sio lazima ujikombe kombe kwa hawa kina Nchimbi, simama mwenyewe mwanaume wewe! Umemtukana Nchimbi wee hapa JF sasa eti umebadilika na kuwa rafiki wa Nchimbi, wallahi kuna binadamu mlizaliwa, eti wewe sasa ni mtoto wa fisadi? makubwa sana haya!
 
hoja ya elimu ya nchimbi haikuwa na uhusiano na kujenga shule.kwani baba yako akikupeleka chuo kikuu ina maana kuwa yeye pia ni lazima awe amesoma chuo kikuu...sasa ulisema kuwa Nchimbi ka ma ameweza hizo shule ungempa nishani.niko tayari kuingia katika kuonyesha elimu yake kama utakuwa muungwana na kukiri kuwa record yake ni bora kabisa......kesho utajifanya kama sio wewe uliosema kuwa mkataba ukipitishwa basi Nchimbi atakuwa most powerful man....naomba kesho FMES uje na kukiri kuwa yametokea.
 
1
. hoja ya elimu ya nchimbi haikuwa na uhusiano na kujenga shule.

Mkuu nilitaka mimi na wewe twende step by step, of exactly who Nchimbi is tukaona jinsi alivyoshindwa kupasi darasa la Saba na kwenda kusoma Sangu, nikakuuliza Sangu ambayo na wewe ulisoma kama ni shule ya Serikali ya waliopasi hukujibu tena! Sasa kosa langu liko wapi? Haya matuisi ni wewe unayapenda sana eti kwa sababu wewe ni shoga wa Nchimbi basi inakupa power ya kuja hapa na kutukana na jina la mtoto wa fisadi, watu wengine mtaelimika lini jamani?

2.
kwani baba yako akikupeleka chuo kikuu ina maana kuwa yeye pia ni lazima awe amesoma chuo kikuu...

No clue what is the point here?

3.
sasa ulisema kuwa Nchimbi ka ma ameweza hizo shule ungempa nishani.niko tayari kuingia katika kuonyesha elimu yake kama utakuwa muungwana na kukiri kuwa record yake ni bora kabisa.

Anytime ukiwa tayari kuonyesha elimu nzito na ya halali ya Nchimbi, mimi nitakupa hiyo medali ya Nchimbi, lakini ulikuwa na all the time kufanya hivyo toka juzi sasa tatizo lilikuwa nini? Nani aliyekuzuia na nani anayekuzuia sasa?

4.
.....kesho utajifanya kama sio wewe uliosema kuwa mkataba ukipitishwa basi Nchimbi atakuwa most powerful man....naomba kesho FMES uje na kukiri kuwa yametokea.

1. Hivi kwa nini uantaka kuchanganya ishus, aliyoyafanya Nchimbi jana nani amekataaa? Wote tumekubali kuwa jana Nchimbi amfanya aliyoyafanya kama mwenyekiti wa UV-CCM, hakuna aliyetegemea Nchimbi kufanya tofauti, lakini tunasema kuwa bado ishu itaenda CC, sasa hapa hoja yako ni nini?

2. Mimi unajua vyema ni lini nimewahi kukimbia hapa wala kubadili majina? Sasa leo au kesho cha ajabu kitakuwa ni kipi hicho as far as Nchimbi na CCM mpaka eti nikimbie na kubadili kauli? Sio tabia yangu hiyo hata siku moja mkuu!

I am always here, having a lot of fun and good time na ishus za taifa langu! uwe unawatisha wasiokujua vizuri na wanaoamini kuwa kweli wewe ni mtoto wa fisadi, not me mkuu!

Again Ahsante Sana.
 
Very strong words kutoka kwa mkuu Kamende, bravo mkuu, check this out:-

Kamende :Kamende is a Patriotic Tanzanian :Senior Member

Kwa kweli kwa hili nakiri mafisadi wapiga bao. Labda niwahakikishie kuwa wapo wakubwa humu JF ambao kila hoja ya ufisadi zinaposhika kasi wao wanabuni hoja mbadala ya kupoza au kuzima hoja hiyo. Kwa leo nawapongeza sana kwani mmeonyesha umahiri mkubwa. Kama yamkini mafisadi wameajiri watu wa kufanya kazi kama iliyofanyika katika hoja hii ya leo, basi nina uhakika leo malipo yatakuwa makubwa zaidi.


1. Kila dakika moja tunayopoteza bila kuwabana mafisadi nchi yetu inaibiwa mabilioni kutoka kwenye madini, kukwepa kodi, kuingiza bidhaa feki, mikataba ya hovyo, matumizi mabaya ya fedha za serikali, nk. Mpenda nchi hatathubutu kutumia muda wake kujadili noon issues akauacha ufisadi kustawi.

2. Watanzania wanajua kwa uhakika kuwa mafisadi wanatumia media kila mahali kwa lengo la kujisafisha na kuhujumu vita dhidi ya ufisadi. Hata humu JF wapo makuwadi wa kuwasafisha mafisadi pia.

3. Kila mlio wa ngoma huelezea ngozi iliyoiwamba. Yeyote aliye wa kulia kwa ajili ya uchungu wake kwa ajili ya wizi wa rasilimali za nchi tutamwona hapa. Na yule wa kulia kwa kuwa mabwana zake wameguswa tutamwona hapa pia.

Ninawahakikishia makuwadi wa mafisadi kuwa haijalishi mnatekeleza wajibu wenu kwa uhakika, uangalifu na ustadi kiasi gani, lakini bado wapiganaji dhidi ya mafisadi hawataisha wala kupungua.
 
Na Joseph Mwendapole

Mfanyabiashara maarufu wa Zanzibar, Mohamed Ibrahim Raza, ameunga mkono kauli iliyotolewa na Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, ya kukemea kundi la mafisadi linalotaka kudhoofisha watu wanaomuunga mkono Rais Jakaya Kikwete katika vita dhidi ya ufisadi.

Akizungumza na Nipashe jana, Raza alisema endapo Watanzania wataamua kukaa kimya kuhusu suala hilo ni dhahiri madhara yake yatakuwa makubwa.
Alisema yeye binafsi anaunga mkono jitihada zinazochukuliwa na Rais Kikwete katika kushughulikia masuala ya rushwa na ufisadi hivyo aliwataka Watanzania wengine wamuunge mkono.

`` Tusikae kimya hata kidogo, suala la wizi na ufisadi ni janga kubwa, lazima Watanzania tuache woga na tuwe na wajibu wa kuwasema watu wanaotaka kuliangamiza Taifa kwa wizi wa fedha za umma,`` alisema Raza.
Aliongeza kuwa huduma nyingi muhimu kama shule, barabara na hospitali haziwafikii wananchi walio wengi hivyo kuna umuhimu wa kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma.

Alisema udanganyifu wa wazi wazi ulifanyika katika mkataba wa kampuni ya kufua umeme ya Richmond na kuisababishia serikali hasara kubwa.
Alisema fedha hizo zingeweza kutumika kuwaletea maendeleo wananchi ambao wengi hawapati hata huduma ya maji safi.``Kama Mengi anathubutu kusema na sisi Watanzania wengine tusisite kumuunga mkono na tusipofanya hivyo madhara yanakuja kwetu sote kwani huduma muhimu hazitapatikana,`` alisisitiza Raza.

Kadhalika, Raza aliongeza kuwa hivi sasa makampuni mengi yameanza kuingiza chakula kibovu kisichofaa kwa matumizi ya binadamu na kuwauzia wananchi. Alisema jitihada za pamoja zinahitajika kuhakikisha wafanyabiashara hao wasio na uzalendo wanafichuliwa kwa maslahi ya umma. Raza alisema serikali inapaswa kuwafikisha mahakamani watu walioiba fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA) hata watakaporejesha fedha walizoiba.

Hivi karibuni, Mengi alisema limejitokeza kundi la mafisadi na la waongo na vibaraka uchwara lenye nia ya kuhakikisha kwamba ushupavu na uadilifuwa wale wanaomuunga mkono Rais Kikwete katika vita dhidi ya ufisadi unadhoofishwa.

SOURCE: Nipashe
 
Of course, we will bring an exclusive uncut, unedited interview with Nape Nnauye on KLHN early in the morning tomorrow. About 15 minutes that will thrill you and make you tap your foot, drop your jaw and say.. I know why!
 
Nape agoma kung'oka

Martha Mtangoo, Dodoma
HabariLeo;
Monday,September 08, 2008


Siku moja baada ya Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), kutangaza kumvua uanachama kada wake Nape Nnauye kwa madai ya kukiuka maadili na kusema uongo nje ya kikao, mwenyewe amesema yeye bado ni mwanachama na uamuzi uliotangazwa dhidi yake si wa mwisho.

Akitetea kauli yake katika mahojiano na gazeti hili mjini hapa jumatatu, Nape alisema uamuzi huo si wa mwisho bali ni mapendekezo yanayoweza kubadilishwa na vikao vya juu. Kwa mujibu wa taratibu, iwapo amevuliwa uanachama wa UVCCM atakuwa amepoteza nafasi yake ya kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) kwani aliipata kupitia tiketi ya UVCCM.

Alisema; "Mimi bado ni mwanachama wa UVCCM na nitagombea nafasi ya uenyekiti wa CCM… nina imani na chama changu na nitabaki kuwa CCM, nina imani na vikao vijavyo kuwa vitatoa maamuzi ambayo yatanitendea haki kwa hiyo bado nasubiri." Alisema kuwa kazi ya Baraza ni kutoa mapendekezo yanayotakiwa kufanyiwa kazi na vikao vya juu ambavyo vitatoa uamuzi wa mwisho.

Sababu zilizotolewa na UVCCM za kufukuzwa uanachama Nape ni kutokana na kusema uongo kuhusu mradi wa jengo la umoja huo kwenye kiwanja namba 1081/2 mjini Dar es Salaam kuwa haukupitishwa na vikao halali vya UVCCM. "Imethibitika mradi huu ulipitishwa na vikao vyote vya jumuiya na Nape amepatikana na kosa la kusema uongo na hivyo kuvunja kipengele cha 17 cha kanuni ya Umoja wa Vijana wa CCM", ilisema sehemu ya taarifa ya UVCCM iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu, Francis Isaack.

Kosa la pili lililomfanya atimuliwe ni kusema mambo ya jumuiya nje ya vikao halali vya jumuiya ambapo inaelezwa amekwenda kinyume cha ibara ya 18 (b) ya kanuni za umoja huo. Licha ya kuvuliwa uanachama, baraza hilo limependekeza CCM imvue uongozi alionao ndani ya chama hicho. Nafasi alizo nazo mbali na ujumbe wa NEC pia ni mjumbe wa Baraza Kuu, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Dar es Salaam.

Isaack katika taarifa yake, alisema kuwa kabla ya kutolewa maamuzi hayo Nape alipewa nafasi ya kuelezea ukweli wa tuhuma zake ambapo aliieleza Kamati ya Taifa kuwa hajawahi kutoa tuhuma juu ya mradi huo na kuwa yeye amekuwa akiongelea mipango yake kama atachaguliwa kuwa mwenyekiti.

Isaack alieleza kuwa "Nape alipoulizwa kuhusu mradi wa umoja wa vijana alidai kuwa si msemaji hivyo iulizwe Bodi ya Wadhamini na kudai kuwa yeye anaamini vyombo vya habari vimemzushia maneno hayo ili kuuza magazeti." Alisema kuwa baada ya Kamati ya Utekelezaji ya Taifa kutafakari utetezi wake iliridhika kuwa vyombo vya habari havikumsingizia na viliripoti aliyoyasema.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kutoka ndani ya Kamati ya Utekelezaji, alisema kuwa awali uongozi wa juu wa umoja wa vijana ulikubaliana kumsimamisha kutohudhuria vikao lakini baadaye ilipobainika kuwa mradi wa umoja huo ulipitishwa na vikao vyote vya jumuiya wajumbe waliamua avuliwe uanachama.

Hoja hiyo iliyomponza Nape aliitoa wakati anachukua fomu za kuwania nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo ya vijana kushika nafasi inayoachwa na Dk. Emmanuel Nchimbi ambapo alidai kuwa mradi huo uligubikwa na ufisadi. Katika maelezo yake alimshutumu aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini na viongozi wengine wa UVCCM, akiwamo Dk. Nchimbi na Isaack kuwa waliingia katika mkataba usiokuwa na maslahi kwa jumuiya hiyo na kuwataka kuwajibika.

Alisema mkataba huo ulipitishwa kinyemela kabla haujafikishwa kwenye vikao vya juu ambavyo ni Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) ili kupata baraka za mwisho. Alidai mwekezaji aliyepewa mradi huo ataendesha mradi milele huku jumuiya ikipata asilimia 25 na mwekezaji 75 na wabia walihamishwa kabla mradi kuanza hali ambayo ni ukiukwaji wa sheria ya ardhi inayotaka Kabidhi Wasii Mkuu wa Serikali atoe kibali kwa ajili ya uhamisho wa aina hiyo. Mkataba wa mradi huo inasemekana ulisainiwa Januari 2 mwaka jana kati ya UVCCM na kampuni za M.M Integrated Steel Mills (MMISML) na Estim Construction Company Limited (ECCL).
 
Back
Top Bottom