Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Zengwe la umri ni kanuni iliyoingizwa kwenye taratibu za Uchaguzi wa UVCCM mwaka 2003 wakati Mwenyekiti wa sasa, Dk Emmanuel Nchimbi anawania nafasi hiyo kwa mara ya pili, ikilenga kumuengua, lakini busara ya Kamati Kuu ya CCM iliiweka pembeni kwa muda.


Nilikuwa nathani kipengele cha umri kiliwekwa baada ya Nchimbi kushika madaraka 2003 kumbe ilikuwa ni kabla na yeye ndiye aliyekuwa mlengwa..!!

Ninaimani Nape ana wapiga kura wengi ndani ya UV-CCM walioko mikoani wanaomuunga mkono...hapo mjini Dar wengi ya hao wapiga kura wana mahusiano ya karibu na hao mafisadi, hivyo sioni ajabu kwa wao kumpa alama ya E.

Nape Nnauye is bad news for those who prefers status quo.
 
Ningemshauri Nape kama yeye ni mwanaharakati makini,asiye lenga kujitafutia umaarufu basi ajiunge na wenzetu wakina Mnyika,Zitto etc CCM sio baba au Mungu wa siasa za taifa hili.Ni kwa sababu tu hakuna playing field yenye usawa.Kama kweli kile alichokisema alikimaanisha then ya nini kubaki katika chama kinachomwekea mizengwe?
Hata hongera kwa uamuzi wako wa kugombea.
 
Yameshaanza tena mie yangu macho tusijepata Ipyana mwingine....maana nasikia huyo Nchimbi ameufanya UVCCM kama mali yake! Tena nasikia anayo nia ya kuja kugombea uraisi baadaye.Nape kaza buti ndiyo hivyo tena umeshayavulia maji nguo...
 
Jamani hata hivyo kanuni lazima zifuatwe!

Ila double standards ndio zinaniudhi!
 
It was obvious huyu Nape angetemwa kwani alitukana mamba kabla ya kuvuka mto kwenda ng'ambo ya pili. Nape aling'amua kwamba jengo la kitega uchumi la UVCCM limejaa ufisadi na alitumia mwanya huo kujinadi huku akiwa amesahau kwamba hao hao anaowasema ndiyo watakaokuwa katika mchakato wa kuwachuja wagombea.
 
alitukana mambA KABLA hajavuka mto!!!! he has to pay the price
 
Pamoja na kwamba ningependa Nnauye awe mwenyekiti wa umoja wa vijana lakini kama taratibu zinasema vingine ni lazima zifuatwe.

Nnauye kama alijua hilo kwanini hakufanya juhudi mapema kupinga hiyo sheria kama ni mbovu?

Binafsi nilaani sana hii tabia ya kupindisha sheria au taratibu ili tu kumwokoa/kumsaidia/kumkomoa mtu mmoja.

Labda kama hao wajumbe wanashindwa kuitafsiri sheria lakini kama sheria kweli iko sahihi kuhusu umri, sio sababu za Nnauye kutaka katiba yao ivunjwe ili yeye apate kugombea uenyekiti wa vijana.
 
Nnauye alifanya kosa la kukemea ufisadi ndani ya CCM akiwa nje ya madaraka; alitakiwa aende "kimya" kama yule simba wa kwenye methali....

Ni kweli Mkuu, washauri walimdanganya wakamwambia ukiingia kwa gia kali basi shoo nzima utaiteka wewe, akasahau kuwa alikuwa bado ameshikilia makali na mpini wameshika wenyewe. Lakini anywaya hata sipopita kama ni mtu mwenye si-hasa za kweli basi ataendeleza mpambano hata asipokuwa mwenyekiti au hata asipokuwa ccm.
 
kuna vyama Vingi...naona attention ipo CCM na taasis Tanzu zake..., Kumbe wengi humu ndani we are not ready for change...Kidumu...

Nape akagombee Ubunge...he still has a chance!!!
 
“Vikao vya chini havina mamlaka kukata jina la mgombea, wanachofanya ni kujadili na kuweka alama na mimi waliniwekea alama mbaya ya E ikimaanisha kwamba sifai. Hata hivyo, kikao chenye mamlaka ya kukata jina na Halmashauri Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete,” alisema.

Nafikiri haya maneno ya Nape, yako very clear au ni mimi peke yangu ninayaona tofauti, kwamba ni NEC peke yake ndiyo wenye huu uamuzi na sio Nchimbi na kamati zake, au?
 
ningemshauri nape kama yeye ni mwanaharakati makini,asiye lenga kujitafutia umaarufu basi ajiunge na wenzetu wakina mnyika,zitto etc ccm sio baba au mungu wa siasa za taifa hili.ni kwa sababu tu hakuna playing field yenye usawa.kama kweli kile alichokisema alikimaanisha then ya nini kubaki katika chama kinachomwekea mizengwe?
Hata hongera kwa uamuzi wako wa kugombea.

vyama vyote tulivyonavyo tanzania haviwezi kum-acomodate mtu kama Nape, kwani umesahau ya chacha wangwe alitoka ccm, kuja kupata uhuru zaidi lakini wapi,alipingwa hata sasa kuna hisia hao wana mapinduzi wetu wame mkorimba, so nape apigane humohumo ccm hadi kiendelee, swosigwa hupo ccm,angoje muda tu, ajifunze toka kwa zuma walipiga vita lakini alisimamama na sasa mwanga unaonekana hawa watachinjana siku moja nasi tuta shinda.
 
Mhhh hii ndo CCM alikosea kukomea hadharani angefanya kama Levy Mwanawasa kimya kimya kisha ukiukwaa unageuka kama kinyonga mbona mafisadi wangebanwa mbavu.
Ila Jk akitaka kushinda vita ya mafisadi amwongeze huyu dogo katika mapambano hayo....
 
Nafikiri haya maneno ya Nape, yako very clear au ni mimi peke yangu ninayaona tofauti, kwamba ni NEC peke yake ndiyo wenye huu uamuzi na sio Nchimbi na kamati zake, au?

Tatizo wapiga kura wengi wanatoka Dar na wenye maamuzi ya NEC wanatoka Dar ambao wanalelewa na mafisadi wanalishwa na mafisadi na wanajengewa na mafisadi hapo unategemea huyu Nape atapita kweli hapo?na mafisadi wameapa huyu hapiti wanataka wamweke tabola lasa wawe wana mcontrol wao.
 
Yameshaanza tena mie yangu macho tusijepata Ipyana mwingine....maana nasikia huyo Nchimbi ameufanya UVCCM kama mali yake! Tena nasikia anayo nia ya kuja kugombea uraisi baadaye.Nape kaza buti ndiyo hivyo tena umeshayavulia maji nguo...

Hayo ya Nape tuliyategemea ila wasim-ipyana tu. Nchimbi siku yake inakuja subirini tu.
 
Kama asemayo Nape ni ya kweli kwamba NEC ndiyo wenye kisu chenye makali, basi na tusiende mbali nakutoka nje ya mada, tusubiri tuone NEC wataamua nini.
 
Sitashangaa sana kama Nape atapitishwa na NEC, watu wengi ndani ya CCM wameanza kuamka na sidhani kama wataona uvivu kotofautiana na Nchimbi. Ningeomba tutumie hii thread kuwajadili hao waliopitishwa na Nchimbi na team yake, apart from Zainab- who are they?
 
said Mtanda is the the best from all
 
Back
Top Bottom