Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 617
Sitashangaa sana kama Nape atapitishwa na NEC, watu wengi ndani ya CCM wameanza kuamka na sidhani kama wataona uvivu kotofautiana na Nchimbi. Ningeomba tutumie hii thread kuwajadili hao waliopitishwa na Nchimbi na team yake, apart from Zainab- who are they?
Kana-Ka-Nsungu, umepatia maana hata hii story imepelekwa na Nchimbi huko Mwananchi kupitia kwa mwandishi mmoja mkubwa ambaye hata hivyo sasa anaondoka hapo Mwananchi, ambaye alimpa kijana wake, aliyeandika.
Story hiyo imetolewa na kina Nchimbi kupima upepo kama Nape akiondolewa kutatokea nini na pia kuwakatisha tamaa wafuasi wa Nape na wapiga kura ambao wataambiwa "achaneni naye, mpeni kura .... tumeshamkata jina lake."
Lakini ukweli ni kwamba kikao hicho kilimpa alama hizo hizo uchaguzi uliopita lakini NEC wakampandisha na kumpa alama A kwa kuwa ni mjumbe wa NEC aliyepata kura nyingi na ni mtumishi wa chama, kwa hiyo alama E ni kwamba NEC na CC iliyompitisha na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM hawana akili na CCM kumuajiri pia imekosea maana hafai hata kuwa mjumbe wa nyuma kumi.
Hayo ni matusi kabisa kwa CCM na kwa wana CCM wote. Kwa kuwa NEC ina mseto wa watu mbalimbali, nadhani NAPE atapitishwa tu maana kama Bashe kapitishwa hakuna kigezo cha kumzuia NAPE