Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

umoja1.jpg

umoja2.jpg


Msiniulize Mkataba wenyewe uko wapi. Simo.

Well tuwaachie wanachama wao wenyewe waamue... Binafsi sina maslahi yoyote na mauzo ya majengo yao... hata wakiuza uwanja wa Kirumba poa tu.
 
Well tuwaachie wanachama wao wenyewe waamue... Binafsi sina maslahi yoyote na mauzo ya majengo yao... hata wakiuza uwanja wa Kirumba poa tu.

Kasheshe ni kweli maslahi kwa sasa hatuna, lakini kumbuka hayo majengo ni mali zetu yaliyo nganganiwa na CCM baada ya demokrasia ya vyama vingi, Natamani na naomba Mungu aniweke hai nishuhudie sikumoja urejeshwaji wa malizetu nyingiiii tulizo zijenga kwa michango yetu na wakati mwingine makato ya kulazimishwa enzi za chama kimoja!

Sipendi yawe yameisha wekwa chini ya mikataba ya kinyonyaji kama hii!!.. Naamini ndoto yangu siku moja itatimia, kwani historia i wazi juu ya mali hizi.

Back to the issue,
Inashangaza sana, CCM inavo jizatiti kwa nguvu zote kuhakikisha inalinda mafisadi kiasi hiki, Hivi kwa sahihi hizi zilivyo wazi wanashindwa nini kuwa wajibisha wahusika? am tuseme kuwajibishana ndani ya chama ni MWIKO?
 
Well tuwaachie wanachama wao wenyewe waamue... Binafsi sina maslahi yoyote na mauzo ya majengo yao... hata wakiuza uwanja wa Kirumba poa tu.

Mkuu MMJ,

Heshima mbele kwa kutuwekea hiyo kitu ni ujumbe tosha kwa mafisadi kuwa JF iko mbele siku zote kwenye kuwamulika na ufisadi wao, Lowassa amejaribu sana kujiosha na huu mkataba, sasa unauona ukweli ulivyo wazi kuwa ni yeye aliyesaini na Bwana Mkalla kwa hiisadi wasdihani kuwa wananchi hatujui ufisadi wao, na wasifikiri kuwa kwa sababu utawala wa sasa unawalinda basi wamepona milele, hapana kuna siku tutawafikisha kwenye mkono wa sheria na ushahidi ndio kama tunaendelea kuukusanya,

Mkuu Kasheshe,

Hela zilizojenga hayo majengo na viwanja, ni hela zetu wananchi kuanzia zile walizokatwa wazazi wetu zamani katika mishara yao, na zile zilizokuwa zinachotwa kule Hazina na kina Msuya, bila ya hesabu wala accountability kwa taifa, ni hela zetu wananchi, ni haki yetu kujua wanaziafnyia nini, sio kwa sababu wameligeuza taifa letu kuwa lisilo na sheria, basi wote tunakubali huo ujinga, hapana tutaendelea kukusanya ushahidi na kuna siku huu mkono unaowalinda utalegea.

Mkuu MMJ, bravo kwa huu ushahidi mzito dhidi ya mafisadi.
 
Nimeona majina ya Kiasia you can make a bright guess ni ndugu zake RA!
 
Bila ya kuona mkataba tutaamini nani ? wenye kusema docoment ni mkataba au ni hati ya makubaliano tu?

Kimsingi nilikuwa ninasubiri aliyeanzisha hii thread aendelee kutoa habari ya msingi hasa kwani hizo signature bado hazibebi uzito wa hoja nzima.
 
Mwanakijiji heshima mbele ndugu yangu kwa kutuwekea hiyo kitu. Na hiyo status yako ya "Mwanakijiji is present!" Mimi nakaa mkao wa kula.
 
Kimsingi nilikuwa ninasubiri aliyeanzisha hii thread aendelee kutoa habari ya msingi hasa kwani hizo signature bado hazibebi uzito wa hoja nzima.

Kimsingi, unachosema ni sahihi, maana si wengi (ukiwamo wewe) ambaye anajua au anafuatilia kinachoendelea UVCCM kwa sasa. Lakini kwa watu wa aina yako, wanapaswa kusoma thread nyingine zinazohusu UVCCM/ Lowassa/Nape/Subash Patel/Kikwete na jengo la UVCCM. Unaweza kusoma pia thread ya: https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=15649


Kwa ufupi, UVCCM wana jengo na kiwanja katika eneo la katikati ya jiji, mita chache kutoka Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam.

Kwanza kabisa kiwanja hicho wameamua kukikodisha (kukiuza) kwa familia ya Patel (Subash ect). Na jengo wamo mbioni kulikodisha. Mdhamini ni Lowasa lakini amekana kabisa kusaini mkataba bali anasema alichosaini ni MoU... sasa hoja hapa je, anachosema Lowasa ni nini? Kina mantiki? Mbona mwekezaji anafanya kazi?

Nitajadili baadaye hoja ya Mwanakijiji... maana ni NZITO kuliko munavyoiona
 
Kimsingi ni kuwa kilichosainiwa kilimpa mjenzi " a go ahead" ya kuanza ujenzi. NI kitu ambacho kina nguvu ya kisheria. Memorandum of Understanding ni sehemu ya Mkataba. Na kutegemea na lugha iliyotumika ndani yake basi inaweza kuzifunga pande mbili. Hebu fikiria kwa mfano tu:

a. MoU inasema kuwa UVCCM itaingia mkabata kamili baada ya kuona mjenzi ameanza kuinua ukuta na kufikia mambo x,y, na z. Na wakati huo huo Mjenzi anasema ili aweze kunyanyua ukuta anahitaji UVCCM ihamishe watu a,b,c na kuzungusha fence kwenye eneo. Wanakubaliana na kutia sahihi. Huo ni mkataba. Kwa sababu, mkataba ni makubaliano ya hiari yanayozifunga pande mbili au zaidi zenye mamlaka, uwezo, na madaraka ya kuingia mkataba kukamilisha jukumu/majukumu fulani huku ndani yake wajibu wa kila mmoja/pande yakifafanuliwa na adhabu ya kutotekeleza zikianishwa.

Wikipedia inasema hivi:

In some cases, depending on the exact wording, MoUs can have the binding power of a contract; as a matter of law, contracts do not need to be labeled as such to be legally binding. Whether or not a document constitutes a binding contract depends only on the presence or absence of well-defined legal elements in the text proper of the document (the so-called "four corners"). For example, a binding contract typically must contain mutual consideration-a legally enforceable obligations of the parties, and its formation must take place free of the so-called real defenses to contract formation (fraud, duress, lack of age or mental capacity, etc.).

So, kusema kilichosainiwa ni "MoU" na siyo mkataba ni kutojua sheria ya mikataba kwani MoU inaweza kuwa ni mkataba endapo kuna vipengele vinavyomfunga mtu kisheria. Basically, nikipata hiyo MoU naweza kuwaambia na mtu mwingine anaweza kuona mara moja kuwa ni mkataba au si mkataba.

Changamoto kwa UVCCM ni kuweka hiyo MoU hadharani.
 
Kasheshe ni kweli maslahi kwa sasa hatuna, lakini kumbuka hayo majengo ni mali zetu yaliyo nganganiwa na CCM baada ya demokrasia ya vyama vingi, Natamani na naomba Mungu aniweke hai nishuhudie sikumoja urejeshwaji wa malizetu nyingiiii tulizo zijenga kwa michango yetu na wakati mwingine makato ya kulazimishwa enzi za chama kimoja!

Sipendi yawe yameisha wekwa chini ya mikataba ya kinyonyaji kama hii!!.. Naamini ndoto yangu siku moja itatimia, kwani historia i wazi juu ya mali hizi.

Back to the issue,
Inashangaza sana, CCM inavo jizatiti kwa nguvu zote kuhakikisha inalinda mafisadi kiasi hiki, Hivi kwa sahihi hizi zilivyo wazi wanashindwa nini kuwa wajibisha wahusika? am tuseme kuwajibishana ndani ya chama ni MWIKO?

Thank you Rwabugiri!
 
LOW Vs KUB

Low: Ule sio makataba ni makubaliano tu.
KUb: Ule ni Mkataba si mmesainiana.
LOw: wewe wasema hujui kitu hadi Kamati kuu imeshaupitisha
Kub: Hakuna hata Mkuu hamkumshirisha
Low: we umejuaje wewe mchokonoko, kwani Mkuu hakuwepo alikuwa nje ya nchi
Kub: Sasa subiri uone mie nishasema ni mkataba na jamaa keshaweka mjenzi site
Low: Hakuna anaandaa tu site akisubiri tusaini mara ya pili
Kub: Hahahaaaa danganya toto hiyo
Low: We mtoto kaa kimya wakubwa zako wako kazini
Kub: Mhhhh!!
 
Nape mambo mazito

na Martin Malera
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), leo kinaanza kuwachuja vijana wanaoomba kuteuliwa kuwania nafasi za uongozi wa juu ndani ya Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), huku mwombaji anayegusa hisia za wengi kwa mitazamo tofauti, Nape Nnauye, akilazimika kukwepa vihunzi saba vya vikao vya mchujo kutokana na utata wa umri wake.

Ingawa vihunzi hivyo saba vinawahusu wagombea wote, lakini jina la Nape huenda likaumiza vichwa vya wajumbe wa vikao hivyo, kwa sababu kubwa mbili.

Mosi, ni kutokana na utata wa umri wake ambao hadi sasa ana umri wa miaka 30, lakini wakati uchaguzi huo utakapofanyika Desemba mwaka huu, atakuwa na miaka 31, umri ambao kimsingi unamwondolea sifa ya kuwania nafasi hiyo.

Sababu ya pili ni hatua yake ya kulipua bomu la ufisadi linalohusu mradi wa ujenzi wa jengo la makao makuu ya umoja huo, jijini Dar es Salaam, huku akimtaka Mwenyekiti wa UVCCM anayemaliza muda wake, Dk. Emmanuel Nchimbi, Katibu Mkuu, Francis Isaac na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Edward Lowassa, kuwajibika.

Habari kutoka ndani ya CCM ambazo Tanzania Daima imezipata, zinasema Sekretarieti ya UVCCM, ndiyo itakayoanza kufungua pazia la mchujo huo katika kikao chake kinachotarajiwa kufanyika leo, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Katiba ya UVCCM, mwenyekiti wa kikao hicho ni Kaimu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Francis Isaac, ambaye Nape amemtaja kama mmoja wa viongozi wanaopaswa kuwajibika kutokana na kashfa ya ufisadi ya mradi huo wa ujenzi. Isaac pia ni Mkurugenzi wa uchaguzi huo.

Isaac, jana aliithibitisha Tanzania Daima kuwapo kwa kikao hicho na kuongeza kuwa kitafuatiwa na kikao kingine cha Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM, ambacho kitaongozwa na Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Dk. Nchimbi, ambaye Nape amemtaja kama mmoja wa wahusika wakubwa wa mradi huo unaodaiwa kuwa na harufu ya ufisadi na hauna masilahi kwa jumuiya hiyo.

Isaac alisema kikao hicho cha Kamati ya Utekelezaji, huenda kikafanyika mjini Dodoma au Dar es Salaam, na hadi sasa hakijapangiwa tarehe ya kufanyika hadi hapo watakapokutana na Nchimbi, ili kupanga tarehe ya kufanyika kwa kikao hicho nyeti.

Nchimbi aliyekuwa mpinzani mkubwa wa Nape katika uchaguzi uliopita, pia ataongoza kikao kingine cha Baraza Kuu la Umoja huo, ambacho Isaac alisema hakijapangiwa tarehe, lakini kitafanyika mjini Dodoma.

"Kikao cha Kamati ya Utekelezaji na cha Baraza Kuu la UVCCM, bado havijapangiwa tarehe, lakini vitafanyika hivi karibuni na vitafanyika Dodoma. Tunasubiri kukutana na mwenyekiti tujue vikao hivyo vinafanyika lini," alisema Isaac.

Nape ambaye ni mototo wa mwanasiasa mkongwe nchini, marehemu Moses Nnauye, atakutana na kihunzi kingine cha kikao cha sekretarieti ya CCM mjini Dodoma, kinachotarajiwa kufanyika Agosti 20, mwaka huu na kitaongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuph Makamba.

Katika sakata la ufisadi la mradi huo, Makamba alilazimika kumwita Nape na kumsuta mbele ya vyombo vya habari, akielezea kukerwa na hatua ya mwanasiasa huyo machachari kutoa tuhuma hizo nzito dhidi ya viongozi wa CCM, wakati suala hilo limekabidhiwa kwenye vikao vya juu kwa maamuzi.

Katika mtiririko wa vikao hivyo vya mchujo, Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, ataongoza kikao kingine cha tano cha Kamati ya Maadili ya CCM, kitakachofanyika Agosti 21, mjini Dodoma.

Pia Kikwete ataongoza kikao cha Kamati Kuu (CC), kitakachofanyika Agosti 25 mjini Dodoma, na kikao cha mwisho na cha saba ni cha Halmashauri Kuu (NEC), ambacho pia kitakuwa chini ya Kikwete na kitafanyika mjini Dodoma Septemba 2 hadi 3, katika ukumbi wa White House.

"Katika vikao vyote vya mchujo, Nape anakuwa na ahueni kwenye vikao vitakavyoongozwa na rais na anategemea sana busara ya CC na NEC, lakini vingine vyote vinaongozwa na Nchimbi, Francis na Makamba, ambao amewagusa katika kashfa hiyo ya ufisadi. Hapo kweli atachomoka?" alihoji mmoja wa wajumbe wa Baraza Kuu la UVCCM ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.

Mbali ya Nape, waombaji wengine watakaopitia chekeche hilo ni Jerry Slaa, Zainab Kawawa, Hussein Mohammed Bashe, Hamad Masauni, Issa Haji Ussi na Benno Malisa, ambaye anapewa nafasi ya kuteuliwa, kwa madai ya kuwa kipenzi cha baadhi ya viongozi wa juu wa jumuiya hiyo na ndani ya CCM.

Wengine ni Anthony Mtaka, Said Mtanda, Haule Pangisa, Samuel Marero, Stephen Deya, Godfrey Mwankenja, David Manoti, Mussa Mnyeti, Edson Lubua, Mwamini Lusingu, Asmah Kalokola, Marco Zablon Allute, Harold Adamson, Suleiman Muhsein Haji, Adila Hilal Vuai, Ashura Ismail, Rashid Masalaka na Raha Ahamada.

Wanaowania uteuzi wa nafasi ya makamu mwenyekiti ni Happy Mahava, Raha Ahamada Ally, Riziki Pembe Juma, Michael Bundala, Rabia Hamid Shaka, Nuru Mohammed Ahamed na Twaha Ally Muhaji.

Katika hatua nyingine, waombaji 16 wa nafasi ya mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, wamemaliza kihunzi cha awali cha kikao cha sekretarieti ya mkoa, ambapo watoto wa vigogo, Said Ntimizi na Ben Samuel Sitta, wamepata alama nzuri, na sasa wanasubiri uamuzi wa vikao vya juu vya CCM.
 
Naomba tukijadili hiki kipengele:

This Development Agreement is made on this 2ND day of JANUARY 2007 and shall come into force from the date of signing by all Parties and shall remain binding upon the Patries until lawfully terminated or cease or comes to an end naturally

2qd1u6b.jpg
 
Think Big, thanks.. it answers the question.. this was a binding contract!! Ndio maana Lowassa ameshindwa kwenda mahakamani.
 
Nyambala.. alipokuwa Dodoma yeye alijitangazia tu nia yake hiyo kumbe hakuzungumza na wanasheria wake. Wanasheria wake walipopitia ushahidi wakamuambia next time utuambie mapema kabla ya kupiga watu mikwara.
 
Back
Top Bottom