Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Sakata la Nape Nnauye na UVCCM

Makubaliano ya awali my foot, hapo walikuwa wanatest zali, kama kungekuwa hamna kelele kiulaini "makubaliano ya wali" hayo ndiyo yangekuwa mkataba. Hii ni spin tu, makubaliano ya awali!
 
Mkataba tayari umeshapatikana, by kesho ninaahidi tutakuwa nao hapa JF, wote kama ulivyo yaani kurasa sita, kwa sasa tunapitia kila kona kuona kama kuna anything, lakini ninaahidi kuwa kesho tutauweka hapa JF!

Na let the chips fall where they may, this is JF where we dare!
 
Mkataba tayari umeshapatikana, by kesho ninaahidi tutakuwa nao hapa JF, wote kama ulivyo yaani kurasa sita, kwa sasa tunapitia kila kona kuona kama kuna anything, lakini ninaahidi kuwa kesho tutauweka hapa JF!

Na let the chips fall where they may, this is JF where we dare!

Mwaga vitu Mzee wa data!
 
Hii ndiyo taabu ya kujichanganya na Maharamia kama Lowassa.
Masikini Makamba, mjanja usoni tu.
Dr Emmanuel Nchimbi na PhD yake FAKE anazidi kujidhihirisha kwamba yeye ni kihiyo kweli kweli.

Hivi nyie CCM umbumbu huo mmeutoa wapi??

Mnakula msosi,ukiisha mnakula mikono yenu huku mkitabasamu kwa maumivu?? Aibu kweli!!!!

Kweli CCM ni Chama Cha Mafisadi

Uzuri wa soo hili ni mmoja;
Safari hii kuchapana bakora ni kati ya wana CCM wenyewe, nasubiri nani atakuwa wa kwanza kuvua au kuvuliwa shati la kijani kwa kuzidiwa na kashfa.

Napenda wawe wote Lowassa na Makamba.
 
Hivi mkataba ni nini? Kwa nijuavyo mimi mkataba ni makubaliano ambayo yanakubalika kwa mujibu wa sheria baina ya pande mbili au zaidi kwa ajili ya kufanya au kutokufanya kitendo fulani. Kama EL na YM walisaini makubaliano fulani na huyo mwekezaji ambayo yanakubalika kisheria, basi hapo kuna mkataba.
 
Hicho alicho saini EL ambacho si mkataba lakini kikawapa jeuri wawekezaji kuanza kujenga kinaitwa nini jamani?
 
Date::8/2/2008
Wagombea UVCCM wawekewa kitanzi cha umri

*Kinawalenga Mnauye Nape, Bhashe
*Mbinu ya kuchomeka wanawake yaiva

Na Mwandishi wetu
Mwananchi

BAADA ya wagombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi kukwepa kitanzi cha kura tatu mwaka 2005, safari hii Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC)ya chama hicho inadaiwa kuwaandalia vijana wa chama hicho zengwe la umri kama njia ya kuengua baadi ya wagombea, Mwananchi Jumapili imeelezwa.

Taarifa mbalimbali zilizofikia gazeti hili zinaeleza kwamba NEC iliamua kwamba kanuni ya wagombea wasiwe wamevuka umri wa miaka 30 itumike kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM).

Zengwe la umri ni kanuni iliyoingizwa kwenye taratibu za uchaguzi wa UVCCM mwaka 2003 wakati Mwenyekiti wa sasa, Dk Emmanuel Nchimbi, anawania nafasi hiyo kwa mara ya pili, ikilenga kumuengua, lakini busara ya Kamati Kuu ya CCM iliiweka pembeni kwa muda.

Kulingana na kanuni hiyo umri wa mwisho wa kugombea ni miaka 30 ili kiongozi husika asizidi miaka 35 akiwa madarakani umri ambao ni wa mwisho wa uanachma wa UVCCM.

Zengwe la umri safari hii linalekea kuwalenga baadhi ya wagombea machachari katika uchaguzi wa UVCCM, ambao ni pamoja na Nape Mnauye, na Hussein Bhashe ambao wamejitosa kuusaka uenyekiti.

Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili, umebaini kwamba kama utaratibu wa kura tatu uliokuwa utumike kuamua nani atakuwa mgombea wa CCM kwenye NEC, ikionekana zaidi kumlenga Rais Jakaya Kikwete, wakati huo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ni dhahiri baadhi ya wakubwa ndani ya chama hawafurahishwi na misimamo ya watu kama Nape na Bhashe.

Habari za ukahakika zanasema kwamba baada ya hoja ya umri wa miaka 30 kuahirishwa mwaka 2003, kabla ya kutumika ilipaswa kwanza kupata baraka za vikao vya UVCCM kunzia kwenye sekretariati, Kamati ya Utekelezaji na mwishowe kwenye Baraza Kuu. Hatua hizi hazikufuatwa ila ni NEC iliagiza tu kuanza kutumika.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa UVCCM ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu wa umoja huo, Francis Isaac, aliambia Mwananchi Jumapili kwamba kanuni ya umri ilipitishwa na Kamati Kuu ya CCM miaka mitano ilyopita.

Isaac alisema haikuweza kutumika katika uchaguzi wa UVCCM uliopita kwa sababu wakati uamuzi unapitshwa wa kanuni hiyo tayari uchaguzi ngazi ya wilaya ulikwisha kufanyika na hivyo kuamuliwa ianze kutumike katika uchaguzi huu.

"Kwa mujibu wa kanuni hiyo mgombea anayefaa kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea ni yule ambaye amezaliwa chini ya Januari mosi, 1978 kama atachaguliwa atamaliza muda wake wa uongozi akiwa na miaka 35," alisema na akaongeza:

"Kanuni hii imeacha majeruhi watu wengi, kuna vijana wazuri sana, tuliwapenda wachukue fomu lakini umri wao wa miaka 32 na 33 umewafanya waende kugombea uongozi kwenye Jumuiya ya Wazazi."

Isaac pia alisema kwamba mchakato wa kutungwa kwa kanuni hiyo ulifuata taratibu zote kuanzia kwenye sekreteriati, Baraza Kuu, Kamati Kuu ya CCM, NEC na baadaye mkutano mkuu wa CCM uliofanyika miaka mitano iliyopita.

Hata hivyo alipotakiwa kueleza ilikuwaje ikashindikana kutumika wakati huo kama ilikuwa imekwisha kutunga na ikalenga kwenye viongozi wa kitaifa tu wa UVCCM mwaka 2003, alisema wakati uamuzi unatolewa uchaguzi ngazi ya wilaya ulikuwa umekwisha kufanyika.

Nape aliyezaliwa Novemba 26, 1977, aliwasha moto ndani ya chama hicho siku amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo, baada ya kulipua bomu kwamba mkataba wa kujenga jengo jipya la UVCCM umegubikwa na ufisadi.

Mbali na Nape, Bhashe amekuwa majeruhi wa siasa za fitina ndani ya CCM, kwani katika uchaguzi wa wajumbe wa NEC ya CCM mwaka 2007 kura wala jina lake havikutokea baada ya kura kupigwa, hali iliyozua maswali mengi.

Bhashe ni mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM mkoa wa Tabora na mjumbe wa Mkutano Mkuu UVCCM. Kama ilivyo kwa Nape, Bhashe naye anapigwa zengwe la umri akiwa amezaliwa Agosti 26, 1978.

Hoja ya umri ikiendelea kuandaliwa kama silaha ya kuwamaliza vijana hao wawili ili majina yao yasipitishwe, makundi kinzani ndani ya chama hicho yanazidi kujiimarisha na kuongeza mikakati ya kumalizana.

Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa mvutano wa makundi haya yanayoongozwa na makanda wa siku nyingi wa chama hicho yanataka kila moja kuweka mgombea wake ili aweze kuibuka mwenyekiti wa umoja huo ambaye kwa nafasi yake ataingia katika vikoa vya juu ya vya chama, kikiwamo kikoa cha Kamati Kuu (CC) ambacho ni muhimu katika maamuzi ya chama.

Katika siasa hizi za makundi, Nape anaonekana kupaniwa zaidi hasa kutokana na uamuzi wake wa kushupalia kashfa ya mkataba wa ujenzi wa jengo la UVCCM unaodaiwa kuwa kufanywa kinyemela.

Baada ya Nauye kutoa tuhuma hizo, si tu Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alikosa uvumilivu na kumshambulia kupitia vyombo vya habari, ila ndani kwa ndani kuna mikakati ya kutaka hata kumnyang'ana kadi Nape akidaiwa kwamba amekiuka maadili ya chama kwa kumshambulia Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa UVCCM, Edward Lowassa, anayedaiwa kusaini mkataba unaoelezwa kutokuwa na maslahi kwa chama.

Makamba pia alimtuhumu Nape kwamba amevunja taratibu za uongozi kwani kwa nafasi yake kama mjumbe wa NEC na kiongozi ndani ya UVCCM, alitakiwa kuzungumza mambo hayo kwenye vikao halali vya chama na si barabarani.

Ingawa zengwe hilo linajengwa juu ya umri, hoja pia imekuwa ikielezwa kwamba viongozi hao wawili wanaonekana kuwa wa msimamo mkali ambao watakataa kuwa daraja la watu waliozoea kuutumia umoja huo kwa maslahi binafsi ya kisiasa.

Kutokana na kuweka mikakati huo, kundi linalopingana na Nape na Hussein wanaamini kwamba karata yao inaweza kupita kama pia wakichomeka suala la jinsia, ili kuonekana kwamba wanajali nafasi za wanawake katika ngazi za juu za uongozi kwenye chama. UVCCM haijawahi kuwa na mwenyekiti mwanamke.

Lakini pia nafsi ya mgombea huyo kutoka visiwani hasa wakati huu wa mjadala tete wa hadhi ya Zanzibar, mgombea wa ngazi ya mwenyekiti akitoka huko ni mbinu ya kusaka kuungwa mkono zaidi.

Chanzo kimoja kutoka ndani ya CCM kinaeleza kuwa baada ya kubaini mbinu hiyo , kundi la Nape nalo limeamua kumchukua mgombea mwanamke kutoka Pemba ili kama suala la jinsia litaibuliwa basi anayeweza kukubalika zaidi ni wa Pemba ambako wanachama wa chama hicho wanaeleza kuwa wametengwa.

Baadhi ya wagombea wa kike waliochukua fomu kuwania nafasi hiyo kutoka Zanzibar ni Raha Ahmada Ali na Adila Hilal Vuai, wote kutoka Unguja na Ashura Ismail Abdallah kutoka Pemba.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Umoja huo, Francis Isaac aliiambia Mwananchi Jumapili vikoa vya kuanza kuwajadilia waliochukua fomu vitaanza kufanyika mwezi huu.

Alisema jumla ya wagombea 27 wamechukua fomu za kugombea nafasi hiyo, 18 kutoka Bara na 9 kutoka Zanzibar.

Uchaguzi wa viongozi wa UVCCM nafasi ya wilaya utafanyika Oktoba 25, mwaka huu na ule wa mkoa utafanyika Novemba 4, mwaka huu na kumalizia na wa taifa utakaofanyika Desemba 27, mwaka huu.
 
wale ambao hawatatendewa haki , milango iko wazi wajiunge na vyama vingine au waanzishe vya kwao. kwani ccm ndo mama zao kwamba hawawezi kuiacha?

msituchoshe na chama chenu uchwara hapa. watu tuko hapa tunazungumzia mustakabali wa taifa letu ambalo liko kwenye hali tete
 
Wana ngd zenge fitna ni sehemu ya siasa za nchi hii nilichokiona ktk story iliyopostiwa ni kua nape kweli ilifika Dec atakua amezidi umri kwa siku nne tu najiuliza umri ni factor wakati wa selection or wakati wa kuchukua form ikiwa ni wakati wa kuxhukua form nape alikua ktk umri unao takiwa but ikiwa ni wakati wa selection or election atakua amezid kwa siku chahe na kwa hili hatuahesabu umri wa mtu kwa kusema ana miaka 30 na siku 2 hamna ktu cha namna hiyo.

Kuhusu Bashe hoja ya umri haimkamati kama nape kwani story iliyopo inaonyesha amezaliwa August 26th 1978 ila la mizengwe na shaka nalo hivi alopoteza jina lake ni nani na alifanya kwa maslahi ya nani haya yanahitaji majibu ili tuweze kuangalia kama walimpiga zengwe hilo wanaweza kupoteza hata jina lake klisirudi kwa wapiga kura.

Mchakato huu unaonyesha kua kuna upinzani mkubwa kati ya NAPE,BASHE,BENO, lakini pia kuna watu wananafasi kidogo kama JERRY,ZAINAB, uwezo wa nape na Bashe unathibitika hata kwa wapiga kura waliopo sasa ambao ni kama 180 ambayo ni saa na asilimia 25% jumua hii imevurugwa na inahitaji maamuzi sahihi ya wapiga kura.

Mizengwe itaimaliza jumuiya hii nape nae aache kuropoka hawa jamaa wanpenda mbumbumbu hao mafisadi anao watukana asubiri apate achukue hatua
 
Namuonea huruma sana Nape..maana wanaweza akawa ndio bye bye jamaa wanakomaliaa sana issue ya umri wamtoe kafara...ila wapiga kura na watoa maamuzi watakuwa wamefanya kosa kubwa sana kutompitisha Nape........ngoja tusubiri tuone.
 
Lowassa aumbuka: Mkataba wake watinga kwa Kikwete

Ni ule wa mradi tata wa UV-CCM

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele
Toleo Na. 108


KUNA ushahidi wa kutosha kwamba Baraza la Wadhamini la Umoja wa Vijana (UV-CCM) chini ya Edward Lowassa limeingiza umoja huo katika mkataba wa utata na bila kufuata utaratibu.

MwanaHALISI limegundua kuwa hati ambayo Lowassa na wenzake walisaini ni mkataba halisi wa kumwezesha mbia kuanza utekelezaji wa mradi.

Utekelezaji huo ni pamoja na kuondoa mara moja wapangaji katika Jengo la Vijana na kuanza ujenzi katika kiwanja Na. 108/2 barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana gazeti likienda mtamboni zinasema mkataba huo sasa umo mikononi mwa Mwenyekiti Jakaya Kikwete na ilitarajiwa utumiwe kufanya maamuzi katika Kamati Kuu (CC).

Kamati Kuu ya CCM ilikuwa ikutane juzi Jumatatu mjini Dodoma. Imeahirishwa hadi tarehe "itakayopangwa baadaye."

Wiki iliyopita gazeti hili liliripoti kuwa Baraza la Wadhamini la UV-CCM chini ya Lowassa limesaini mkataba wenye thamani ya zaidi ya Sh. 30 bilioni, kati yake na makampuni mawili ya uwekezaji, bila wenye chama kujulishwa na kuridhia.

Lakini katika hali ya kushangaza Lowassa amekana kutia saini mkataba huo na kudai kuwa alichosaini yeye na wenzake ni "maelewano tu na siyo mkataba."

Wiki iliyopita Lowassa alitishia kushitaki gazeti hili kwa kile alichoita kuandika uwongo juu yake na "mazoea ya kunichafua."

Gazeti hili limepata nyaraka, ukiwemo mkataba, zinazothibitisha kuwa kilichosainiwa na Lowassa na wenzake, si maelewano kama alivyodai yeye, bali mkataba wenye nguvu ya kuruhusu utekelezaji wa mradi.

Mkataba wa UV-CCM umezua maswali mengi. Kwa mfano, kama Lowassa anasema alichosaini siyo mkataba, nani basi alisaini mkataba?

Kwani mwekezaji tayari ameanza kujenga kabla ya mkataba. Je, kama alichosaini Lowassa siyo mkataba ina maana mwekezaji akamtwe na kufunguliwa mashitaka kwa uvamizi wa kiwanja na jengo la UV-CCM?

Aidha, kama anayeendelea na ujenzi hana mkataba, ina maana ni mbumbumbu kiasi cha kutumbukiza fedha katika eneo ambako hajakubaliwa kuwekeza?

Kauli ya Lowassa inapendekeza kuwa kama alichosaini siyo mkataba, basi ni yeye na baraza la wadhamini waliomhakikishia mwekezaji kuwa "kwa vyovyote itakavyokuwa ni yeye atakayekubaliwa" na hivyo wakaanza kujenga.

Mgogoro uliopo ni kwamba Baraza la Wadhamini la UV-CCM liko chini ya Baraza Kuu la UV-CCM. Hata wajumbe wake wanateuliwa na baraza hilo.

Hivyo Baraza la Wadhamini haliwezi kuchukua maamuzi makubwa kama lililochukua bila kutaarifu Baraza Kuu na kupata ridhaa yake.

Aidha, Baraza la Wadhamini siyo chombo cha utendaji kwa misingi ya kanuni. Hivyo mwenyekiti na baraza lake hawawezi kufikia hatua ya kusaini mkataba, hata kama ni Hati ya Maelewano (Memorandum of Understanding (MoU) kabla ya kuwasiliana na Baraza Kuu.

Kiongozi wa ngazi ya juu katika UV-CCM amesema kazi ya baraza la wadhamini ni "kuangalia na kusimamia mali za umoja huu. Vilevile kuna Kamati ya Utekelezaji ambayo kanuni inasema, "Itaongoza na kusimamia shughuli za kila siku za Umoja wa Vijana chini ya uongozi wa Baraza Kuu."

Kutokana na hali hiyo, hata Kamati ya Utekelezaji inawajibika kwa Baraza Kuu. Na hata wajumbe wake wanachaguliwa na baraza hilo.

Kanuni inaweka wazi kwamba Baraza Kuu litakuwa na jukumu la kuangalia na kusimamia shughuli zote za sehemu zote zinazoongozwa na UV-CCM na ndilo lenye mamlaka ya kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Hii ina maana kwamba ukiondoa Mkutano Mkuu, Baraza Kuu ndilo chombo cha juu kabisa ambacho kimepewa jukumu la kusimamia shughuli zote za UV-CCM.

Hata kama Kamati ya Utekelezaji itakuwa na wazo la kuanzisha mradi wowote wa kiuchumi, inatakiwa kuwasilisha hoja kwanza kwenye Baraza Kuu na baraza ndilo lenye uwezo wa kuidhinisha au kutoidhinisha mradi wowote.

Kwa msingi huu, Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamani haingii katika utendaji wa shughuli za umoja mpaka kufikia hatua ya kusaini mkataba au hata kile ambacho yeye anadai kuwa ni MoU.

Hata hivyo, mkataba huu unamweka Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete katika wakati mgumu hasa baada ya taarifa kwamba wote wawili, Lowassa na Katibu Mkuu Yusuph Makamba wamekuwa hawamwambii ukweli kuhusu suala hili.

Katika hatua nyingine baadhi ya viongozi wa UV-CCM walioongea na MwanaHALISI walihoji uamuzi wa Lowassa wa kupeleka suala hilo kwenye Kamati Kuu ya CCM (CC) wakisema atakuwa ameruka ngazi kwani Baraza la Wadhamini linawajibika kwa Baraza Kuu.

"Kama hivyo ndivyo, basi Baraza Kuu limekiukwa katika mradi huu; iwe Lowassa amesaini mkataba au hati ya maelewano kama anavyodai na anavyotaka umma uamini," amesema kada mmoja wa UV-CCM ambaye sasa ni mkuu wa wilaya.

Alisema, "Lowassa anayajua haya kwa makini. Huyu ni mweledi wa kanuni za jumuiya hii kutokana na kupikwa na kukulia katika umoja wetu na wazazi wake – TANU na CCM."

Baadhi ya wajumbe wa UV-CCM wamesema ni CC ambayo ilimshupalia aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake (UWT) Halima Mamuya na kumlazimisha ajiuzulu kutokana na madai kama haya.

Katika sakata hili nyundo imeelekezwa kwa Lowassa, Makamba, Mwenyekiti wa UV-CCM Emmanuel Nchimbi na Mweka Hazina wa sasa wa CCM Amos Makala.

Waliosaini mkataba ni Edward Lowassa akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini na Makala ambaye wakati huo alikuwa Katibu wa Bodi.

Kile ambacho Lowassa anaita MoU ni maelewano ya awali ya pande zinazohusika juu ya jambo fulani na siyo mkataba (agreement/contract) kama huu aliosaini (angalia kivuli cha mkataba).
 
kubenea naona humpi nafasi hata kidogo Lowasa!
 
Afadhali kubenea ameamua ku-specialise na ufisadi wa Lowassa. So far so good...tunahitaji mwingine awe specialist kwa RA.
 
Hapa utawapata wana CCM wenzio sisi wengine hatuhangaiki na rushwa na ufisadi wenu ndanu ya CCM lenu .Endeleeni hapa wapo watakao kuja kukuhuza lakini hili ni swala lenu huna mtandao wa Kichama ukapeleka huko ? Ama kama una ujumbe mzito zaidi mwaga hapa Mtoto wa JK atakusikia maana anashinda hapa kusoma na kuchukua info kupeleka huko kwa Mzee wake na kwingineko.Lakini unapaswa kuwa jasiri uje kama mimi Lunyungu natumia majina yangu kwa uwazi useme na aelewe kwamba ni wewe unayepinga kauli zake .
Kwamba wewe unatueleza ufisadi na hela wanazo fuja ni za CCM sio za wananchi. Mimi nadhani hoja si uchaguzi wa UVCCM, hoja ni wapi wanpata hiyo mijihela yote na kiburi cha kusema piga uwa galagaza lazima Benno awe Mwnykt
 
Uchaguzi UVCCM: Nape Nnauye adai hoja ya umri ni fitna chafu

Na Joyce Mmasi
Mwananchi
Date::8/9/2008

HOJA ya umri katika kinyang'anyiro cha uenyekiti katika Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), imechukua sura mpya baada ya mgombea wa nafasi hiyo, Nape Nnauye kuwa kikwazo hicho hakitamzuia kugombea nafasi hiyo na kwamba huo ni mchezo mchafu unaofanywa na wapinzani wake.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana, Nape alisema haogopi mchezo mchafu wa wapinzani wake kwa kuwa alipoamua kuchukua fomu alikuwa na akili timamu na akizifahamu kanuni, sheria na katiba ya umoja huo vyema.

"Kati ya wagombea wote zaidi ya 20 mimi ndiye mwenye uzoefu mkubwa katika chama na jumuiya ya vijana, nimekuwa mjumbe wa NEC kwa muda wa miaka sita, Mjumbe wa baraza la kuu la UVCCM kwa miaka sita na Katibu Msaidizi Idara ya Siasa Makao Makuu ya Chama, najua kanuni, sheria na katiba ya chama ya umoja wa vijana" alisema.

Nape alisema, licha ya kuwa yeye ni muombaji na si mgombea, lakini alipoamua kwenda kuchukua fomu ya kuomba nafasi ya uenyekiti wa umoja wa vijana alikuwa akifahamu kanuni na sheria na katiba ya umoja huo, hivyo vijimaneno vinavyoenezwa haviwezi kumkatisha tamaa yeye wala wanaomuunga mkono.

"Nilikuwa nikifahamu nini kinahitajika na kwa kujipima nilijiona nina sifa, ndio maana nilipoenda kuchukua fomu, mkurugenzi wa uchaguzi alinipa fomu kwa kujua kuwa ninazo sifa zinazohitajika," alisema.

Hata hivyo, Nape alisema lipo kundi lenye nia ya kuwavunja moyo watu wanaomuunga mkono na wanaotaka mabadiliko katika umoja huo.

Alisema vijana wa CCM wanajua nani wanayemtaka katika uongozi na akashauri kuwa ni vyema waachwe waamue. "Vijana wa CCM wamekomaa, wanazijua kanuni na sheria, ni vyema wakaachwa waamue" alisema.

Alisema yeye mwenyewe alishiriki katika marekebisho ya kanuni za umoja huo na akasema kama angekuwa anabanwa au angekuwa hana sifa asingethubutu kuchukua fomu za kuomba kugombea, kwa kuwa hapendi kupoteza muda.

"Mimi sipendi mchezo mchafu, nimekaa kwenye CCM nakijua chama kuliko mgombea yeyote, kwa kulijua hilo wapo watu wanajaribu kunipunguzia umaarufu wangu ndani ya chama," alisema na kuongeza;

"Nasikia kuna kundi lina mtu wao wanalalamika eti Nape ameingilia miradi yetu, lakini mimi nasema vita ya ufisadi sio agenda katika uchaguzi."

Nape alisema hata hivyo hana hofu na mgombea yeyote kwa kuwa anajiamini anazo sifa zote.

Akizungumzia hali hiyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Umoja huo, Francis Issac alisema walikuwa wakitoa fomu kwa kila aliyejiona ana sifa, na kwamba kila muombaji alirejesha fomu yake na vielelezo ili kuthibitishwa kama ana sifa na vigezo vinavyohitajika.

"Sio rahisi kumnyima mtu fomu kwa kumuangalia sura na kutangaza hana sifa au anazo, wengine wana maumbo makubwa kumbe ni wadogo, kikubwa tunaamini kila aliyekuja kuchukua fomu anaamini ana sifa na vigezo vinavyohitajika," alisema.

Alisema ili kuridhika kama mtu anavyo vigezo, anapozirudisha fomu, muombaji hutakiwa kupeleka vielelezo vyote ili vipitiwe na kamati ya uchaguzi kabla ya kutangaza wagombea wenye sifa na wasio na sifa.

Wiki iliyopita Mkurugenzi wa Uchaguzi wa UVCCM ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu wa umoja huo, Francis Isaac, aliambia Mwananchi Jumapili kwamba kanuni ya umri ilipitishwa na Kamati Kuu ya CCM miaka mitano ilyopita.

Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho inadaiwa kuwaandalia vijana wa chama hicho zengwe la umri kama njia ya kuengua baadhi ya wagombea kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM).

Kulingana na kanuni hiyo umri wa mwisho wa kugombea ni miaka 30 ili kiongozi husika asizidi miaka 35 akiwa madarakani umri ambao ni wa mwisho wa uanachma wa UVCCM.

Zengwe la umri safari hii linalekea kuwalenga baadhi ya wagombea machachari katika uchaguzi wa UVCCM, ambao ni pamoja na Nape Nnauye, na Hussein Bashe ambao wamejitosa kuusaka uenyekiti.
 
“Kati ya wagombea wote zaidi ya 20 mimi ndiye mwenye uzoefu mkubwa katika chama na jumuiya ya vijana, nimekuwa mjumbe wa NEC kwa muda wa miaka sita, Mjumbe wa baraza la kuu la UVCCM kwa miaka sita na Katibu Msaidizi Idara ya Siasa Makao Makuu ya Chama, najua kanuni, sheria na katiba ya chama ya umoja wa vijana” alisema.

Maneno mazito sana, saafi sana CCM tunahitaji viongozi wanaoweza kusema maneno yenye busara badala ya kujikita kwenye malumbano yasiyokuwa na faida kwa wananchi, wala taifa

Bravo Nape! na saaafi sana!
 
Maneno mazito sana, saafi sana CCM tunahitaji viongozi wanaoweza kusema maneno yenye busara badala ya kujikita kwenye malumbano yasiyokuwa na faida kwa wananchi, wala taifa

Bravo Nape! na saaafi sana!

Mkuu, huyu kijana ananifurahisha sana. Hana woga wa kuogopa ogopa pale anapoona kuna dalili ya kudhulumiwa haki zake. Tunahitaji vijana kama hawa ndani ya CCM labda wataweza kurudisha hadhi ya chama hicho badala ya hawa mafisadi waliokiteka nyara chama hicho. Na kwa maoni yangu mpaka sasa yeye anaonekana kuwa msema kweli kwenye issue hii ya uchaguzi na ile ya mkataba wa jengo la Vijana. Hongera sana Nape usiogope mtu katika kusema ukweli na pia kuhakikisha kwamba unatendewa haki katika uchaguzi unaokuja wa UVCCM.
 
umoja1.jpg

umoja2.jpg


Msiniulize Mkataba wenyewe uko wapi. Simo.
 
Kweli hapo watatafutana.Kama ndani ya chama kwenyewe kunanuka,je hizi raslimali zetu je? Mbwa anayeiba nyumbani kweli atashindwa kuiba kwa jirani?
 
Back
Top Bottom