Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga


Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

.

Mawani yangu yameposuka, hebu mtu asome hapo kwenye bold!
 
Clouds redio waliorusha ya kwenye you tube watakuwa matatani mara baada ya hii ya polisi kuwekwa hadharani , wajiandae kumlipa Lwakatare fidia kutokana na kumdhalilisha mbele ya umma .
Clouds wanalazimisha kujitumikisha...siyo tatizo. Lakini wajitahidi kuwa smart!

Wakipatikana safari hii wasiachiwe, ili siku nyingine washike adabu kutorukia mambo kichwa kichwa.
 
Hongera sana Mh Lissu na team yako. Wanayofanya magamba ni aibu kwa taifa. Ila lengo lao nikupotezea maandamano ya cdm na matokeo feki ya tume ya uchunguzi kushindwa wanafunzi kidato cha 4. Kudhoofisha chama kwa matakwa yao ya kifisadi. Hawana lengo zuri na Tzn, to put it in short.
 
CHADEMA kupitia mgongo wa wanasheria wanaomba huruma ya wananchi, tambueni sheria ni msumeno; Lwakatare karikoroga ni wajibu wake kulinywa
 
Hivi unaamini kuwa bunge ni mhimili unaojitegemea? Wote bunge na mahakama wanaendeshwa remotely toka magogoni.
Bunge la MAKINDA ndo lina issue ila zama za SITTA huwezi leta hoja zako za kipuuzi puuzi ndo maana wakampiga chini ata PM wa kale EL.
Makinda amewekwa so lazima atekeleze matakwa ya waliomuweka which means yeye kama yeye iyo nafasi hakustairi nia kwa hisani tuu
 
Hivi sasa wanasheria wa CHADEMA wanafanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la Lwakatare na makosa ambayo alishitakiwa nayo.

Anaeleza kuwa kama ameshitakiwa kwa ugaidi lazima makosa hayo yawe ni ya kigaidi, ila makosa ya




Kidnapping na abduction ni makosa ya kawaida ya jinai , na kama ili yawe ya kigaidi ni lazima hayo makosa yawe yamefanyika kwa malengo ya kigaidi , na hata hati ya mashitaka haina maelezo ya makosa ya ugaidi .


Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

Tatu, tarehe 29.12.2012 Mwigulu Nchemba , akiwa na Zitto na Mtatiro Star Tv , kipindi cha tuongee asubuhi ndipo alisema kuwa ana mkanda wa viongoz i wa chadema wakipanga mauaji ......sasa haya yote yatajulikana mahakamani.

Ziada .

Maelezo aliyotoa Lwakatare polisi kuhusu maneno yaliyoko kwenye video alisema kuwa yeye anakumbuka siku ya tarehe 28, alikuwa nyumbani kwake na Ludovick ndio alienda kwake , ila picha ya video ni ya kwake , sura ni ya kwake ila baadhi ya maneno yaliyoko sio ya kwake na ameandika hivyo , kwa hiyo kuhusu ukweli wa mkanda majibu ya kina yanatakiwa kutoka polisi , Mwigulu na Denis ndio wanajua nini kipo kwenye mkanda . Hivyo picha limeanza kuonekana , na kwa taarifa zaidi ni kuwa polisi wana video yenye dakika 27.06 na maneno yanatofautiana sana na yaliyoko kwenye You tube iliyowekwa kwenye mitandao .

Sasa polisi nao waliulizwa ni kwanini hawajamkamata aliyeweka hiyo you tube kwenye mitandao walitoa majibu yao na mawakili wanaendelea na uchunguzi wao.


Ni kwa nini huyo Mwiglu Nchemba naye hakamatwi akahojiwa?
 
hii serekali imekaa kijoti joti,ukiangalia na ile kesi ya Lema ya ubunge utugundua dhuluma ni nyingi sana!

Haya kayasema Lissu au ni wewe mkuu, ni vema katika kutoa habari kama hizi za reporting ukatanguliza jina la mtoa habari
 
The more hii issue inakuwa tamu the more Kikwete na CCM wanaaibika na kuzidi kupotea kwenye ramani ya utendaji wa haki.

Imenifanya nizidi ku support CHADEMA maana kuishi kwenye nchi ambayo utawala wa sheria unakandamizwa ni hatua ya juu kabisa ya udikteta. Ni matumaini yangu siku CDM wakiingia madarakani hapo 2015 watarudisha heshima ya mahakama kama chombo kikuu cha kutenda haki
 
Mimi naomba ufafanuzi, juzi tu ndiyo nimejua kwamba DPP ni mtu mkubwa sana nchi hii, yaani anaweza kukuweka ndani kwa muda anaotaka yeye au kukutoa lupango muda anaoona unafaa na huwezi kuhoji/ kulalamika/ kushitaki popote pale ndani ya nchi hii. sasa maswali kidogo tu ndugu zangu

je huyu DPP anachaguliwa na nani kwa manufaa gani?

a) Kigezo cha kumpata DPP - hii kazi inaombwaje ombwaje?
b) Kazi zote za DPP zinaratibiwa na nani?
c) Anariport kwa nani in darily basis?
 
CHADEMA kupitia mgongo wa wanasheria wanaomba huruma ya wananchi, tambueni sheria ni msumeno; Lwakatare karikoroga ni wajibu wake kulinywa
mtawawaibisha mapolice na mahakimu bure!! kama mlivyofanya ile kesi ya Lema, yule hakimu anaelewa sheria ila anapidisha ili afuate maagizo ya Mary Chitanda -- ha ha ha

Ningekuwa mimi hakimu siwezi kupidisha taaluma yangu bora niache kazi nikalime mchicha
 
Kwa ushahidi huo hapo juu kwenye main post, huyu naye anastahili kuhojiwa. Anaonekana ni mmoja kati ya watu walioufahamu vizuri mchezo uliokuwa unachezwa. Na hapa akamtaja mtu kwa madai amesikia sauti yake kwenye video. Hii inapatikana hapa:

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...apa-lwakatare-alikuwa-anamaanisha-nini-4.html

Hii ni posti namba 77:
Nasikia sauti ya jamaa mmoja wa chadema anaitwa ludovik akiitikia na kutoa maelezo kwa boss wake mratibu na mtendaji bwana rwakataremmh kweli hii ngoma nzito kwa chadema sijui watatokea wapi

Na hii ni posti namba 87:
hii ngoma nzito sana kwa chadema sasa sijui nayo wataandamana na huyo jamaa anaeitikia hapo na kujibu maswali ya mchora mchoro wa utekaji nyara lwakatare ni jamaa mmoja hivi wa chadema anafahamika na hizo ndizo kazi zake jamaa huyo bwana L kama herufi yake ya mwanzo ya jina lake ilivyo aliwahi somea upadre ila ukamshinda akaacha naye hana pakukwepea katika hili maana kwa wanaomjua vizuri kama mimi hawatosita kumtambua kwamba ni YEYE{KIJANA L]

Posti namba 91 anataka ziwekwe video zote. Anazijua?
Weka zote mkuu hali ya kiusalama ya nchi ni tete lasivyo watatumaliza hawa jamaa
 
Ukweli daima utasimama mwisho wa siku, kama serikali kwa makusudi kabisa wanaamua kutumia pesa za walipa kodi masikini wa Tanzania kwa kufungua kesi za kutunga kwa malengo ya kuiondoa Chadema kwenye ramani ya kisiasa, hakika watafutika wao, maana malipo ya dhambi wanayoitenda sasa ni makubwa sana na hawatakaa waisahau milele.

Tusubiri tuone, kwanza wameonesha ambavyo wasivyo makini kupitia wanasheria wao, hivyo mwisho wa siku huku kudharisha wanakofanikisha kwa Lwakatare as individual person na Chadema kwa kiwango fulani kwao itakuwa disearter very soon, tusubiri yetu macho, acha wanasheria watifuane na tuombe mahakama isimamie haki.
Hili tunasema kwa kiinglish kuwa ni CCM sysmatic calculated mission na haitaishia kwa Lwakatale tu ni vema Chadema wakajiandaa kwa mengi zaidi.
 
Sasa picha limepata stelingi linaanza na picha za unafiki litaishia na picha za aibu.
 
CCM WAACHANE NA HIZI MBINU CHAFU KWA CDM.KILA SIKU STARTEGY ZAO ZINADUNDA.
WAGEUKIE MBINU ZA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO, that is the only strategy.
wakishindwa na hiyo wakabidhi dola kwa amani kujilinda heshima yao
 
Back
Top Bottom