Sakata la DP World na Bandari, Jenerali Ulimwengu asema Serikali imepoteza imani ya wananchi

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,115
49,837
Wakati mjadala wa uhalali wa mkatabva wa uwekezaji katika bandari kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai ukiendelea, Mwandishi nguli nchini Jenerali Ulimwengu, amesema Serikali imepoteza imani ya wananchi.

IMG_7661.jpeg

Mwandishi huyo nguli anaibua hoja hiyo wakati watanzania na wadau mbalimbali wamekuwa wakiupinga mkataba huo wa uboreshaji wa bandari wakisema, una harufu ya unyonyaji kwa kile walichobaini mkataba huo hauna ukomo na umekiuka sheria za nchi.

“Tanzania ni moja, haigawanyiki wala haiuziki. Kwa hiyo ndugu zangu mama ni Mtanzania, maendeleo yetu ndiyo muhimu, kila linalofanyika ni kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania,”amesema Rais Samia mara baada ya kuwasili mkoani Mwanza Juni 14 kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo.

Kwenye mjadala ulioendeshwa leo Juni 19,2023 na Taasisi ya Media Brains jijini Dar es Salaam, ukijadili “Kulinda na kuendeleza umoja wa kitaifa wakati wa mageuzi ya kisiasa na kiuchumi”

Ulimwengu amesema kutokana na usiri ambao umekuwepo wananchi wana haki ya nini kimetokea.

Amesema kwa watu wanaofikiri vizuri na kudodosa mambo Serikali haina ‘Trust’ kubwa ya wananchi. “kuna mtu mmoja alimkaribisha ndugu yake chakula cha mchana akamwambia atamchinjia jogoo, yule bwana akaenda anajua anachinjiwa jogoo bahati mbaya ana ulemavu wa macho haoni, Akaingiza mikono kwenye bakuli akagusa mguu wa kwanza na wapili akasema, yeye kipofu amepewa viwili wao wamekula vingapi,”amesema.

Akizungumzia suala la ubinafsishaji amesema hakuna ukinzaji wa moja kwa moja kati ya ubinafsishaji na utaifishaji kama wale ambao wanachukua mali chini ya Serikali ni raia waliopo ndani ya taifa husika.

Hoja hiyo imekuwa ikipingwa na Serikali huku ikisema huo ni upotoshaji kwani mkataba uliosainiwa ni wa msingi nab ado mikataba ya utekelezaji huku Rais Samia Suluhu Hassan akienda mbali zaidi kujibu kauli za wanaodai Serikali inauza bandari akisema bandari haiuzwi.

Maana yake mali itakuwa imetoka kwenye mikono ya serikali na kuingia kwenye mikono ya wananchi na hiyo ndio maana ya shirika la umma, Ili mashirika yawe ya umma yapewe umma ambao ndio wananchi wenye nguvu ya kufanya kazi na kuendeleza nchi yao kwa mali walizopata.

Amesema suala la uwekezaji wa bandari ya Tanzania si suala la kukataa au kukubali bali ni aina ya uwekezaji unaotakiwa kufanyika.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Kanisa Katoliki Tanzania TEC Padri Dk Charles Kitima amehoji pamoja na aina mbalimbali za uwekezaji uliowahi kufanyika nchini ni kwanini sasa uwekezaji wa bandari unapigiwa kelele…?.

Chanzo: Mwananchi

===

My Take
Serikali achaneni na hili suala, Wadanganyika hawataki regardless of how important privatisation is!
 
Mungu Ibariki Tanzania!

Eee Mungu eeh, Ibariki Tanzania! Njoo huku!

CCM must go!

Pamoja na kuwa mkataba unawapa nyenzo na mamlaka Kampuni ya watu binafsi kuilazimisha Serikali ya Tanzania kufanya maamuzi magumu kama ya 'kuwataarifu' kuhusu hatua zezote zile Serikali itakayochukua, yaani.

Tanzania itaijulisha DPW juu ya fursa zozote zilizopo, na zitakazokuwepo sasa na baadae.

Basi,sasa Wananchi nao kwa sauti moja, watoe na kuitaarifu CCM, kuwa nao, Wananchi watafanya maamuzi magumu na kuwapa taarifa kuwa CCM hawatachagilika hapo baadae.

Sasa, kwa muktadha huo, itakuwa sahihi kwa Wananchi wote waendelee kudumisha amani na utulivu, umoja na mshikamano, kwa kulinda Katiba na maadili na utamaduni zetu na rasilimali zetu kuwajulisha chama cha mapinduzi, kuwa fursa zezote zile walizobakiwa nazo na fursa zezote zile zitakazo kuwepo hapo baadae, kuwa, itawa taarifu Umma/Wananchi, kuwa ifikapo Tarehe itakayotangazwa na uwepo wa Uchaguzi, kuwa, kama Chama kilichopo madarakani, kuwa, kitatota taarifa kuwa Chama kipigiwe kura iwapo tu, kilisharudisha Mkataba bungeni ujadiliwe kwa mapana na marefu, kwamba, kimeondoa vipengele tajwa na tata katika mkataba unaojadiliwa na mijadala yote nchini, na kuwa pia,kitaondoa wingu, jinamizi, laana , shetani, tandabuli la na hofu, waliouleta na kwa, manufaa ya Nchi na Wananchi wake, kuwa, limerudisha matumaini na matamanio ya wananchi kwa Serikali yake, kuwa, kinyume na hayo, kuwa, Mkataba wake na Wananchi utakoma kwa njia ya Kura.

Kwamba, Wananchi watapiga kura yao na kuwaondoa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kuchagiza mkataba hovyo kutokea Nchini kutoka madarakani.

Chagua kwa Uangalifu na Umakini mkubwa 2025.

Amani ikutandae
 
Jambo Hilo Moja hakiwezi iondoa ccm,wachangiaji wote wanasema dosari zirekebishwe so usijifariji,hakuna chama mbadala wa CCM Kwa Sasa hakipo.
 
Tundu Lisu: Azimio la Bunge linaufanya Mkataba uwe sheria

My take; Kuupanda Mchongoma kushuka ndio ngoma
Mwandishi wa habari nguli, mwanasheria na mwanasiasa Jenerali Ulimwengu leo Jumatatu amesema katika suala la uwekezaji kwenye bandari ya Dar es Salaam kama ilivyo kwa DP World na mashirika mengine kutoka nje sio suala la kukataa au kukubali kwani inatakiwa kuangalia inawekeza kwa namna gani.
 
Jambo Hilo Moja hakiwezi iondoa ccm,wachangiaji wote wanasema dosari zirekebishwe so usijifariji,hakuna chama mbadala wa CCM Kwa Sasa hakipo.
Ndio unaona nimemuita Mungu aje huku!

Wacha nijifariji mzungu mwe.

Mbadala upo mumo humo CCM. Ila kwa sasa(uchaguzi ujao) wachukue halftime(waliopo kwenye ngazi za juu) wapate semina ya 'Imani'.

Amani ikutawale
 
Kinachokataliwa ni Mkataba mbovu

Mbona Kilimanjaro Hotel Mwekezaji alikuwa Mwarabu na Ilikuwa fresh tu 😂😂😄

Au akina Abood mbona ni Waarabu na waliuziwa viwanda na Mabasi yanazidi kuongezeka🤣🤣
 
Jambo Hilo Moja hakiwezi iondoa ccm,wachangiaji wote wanasema dosari zirekebishwe so usijifariji,hakuna chama mbadala wa CCM Kwa Sasa hakipo.
Dosari gani kwenye huo mkataba zirekebishwe? Huo mkataba ni wa hovyo haufai kabisa utupwe. Tayari TPA nd DPW wana MoU kwa nini DPW ijifiche nyuma ya nchi yao kwa huo mkataba hovyo (IGA)?

Serikali ikilazimisha uendelee ijue ndio kuchimba kaburi la CCM.
 
Katika mjadala wa kitaifa ulioebdeshwa na Media Brain, Kuna wachangiaji wawili walitoa mwelekeo mzuri sana wa mjadala nao ni Dr Kitima na Jenerali Ulimwengu, na hawakuweka udini au nasaba. Na mojawapo ni Bunge kuwa Butu n.k na serikali kuharibu uaminifu wake na kuwa waongo waongo, na alipochangia Kitila mkombo mchango wake ulielekea kwenye uongo.

Mfano anasema mkataba ni kati ya serikali wakati DPW sio serikali.

Pili kifungu kinacho ruhusu mabadiliko ya mkataba ni tata maana kimesema by "mutual consent" maana yake sisi tuna weza taka hayo mabadiliko wao wakakata.
 
Katika mjadala wa kitaifa ulioebdeshwa na Media Brain, Kuna wachangiaji wawili walitoa mwelekeo mzuri sana wa mjadala nao ni Dr Kitima na Jenerali Ulimwengu, na hawakuweka udini au nasaba. Na mojawapo ni Bunge kuwa Butu n.k na serikali kuharibu uaminifu wake na kuwa waongo waongo, na alipochangia Kitila mkombo mchango wake ulielekea kwenye uongo.
Mfano anasema mkataba ni kati ya serikali wakati DPW sio serikali.
Pili kifungu kinacho ruhusu mabadiliko ya mkataba ni tata maana kimesema by "mutual consent" maana yake sisi tuna weza taka hayo mabadiliko wao wakakata.
jenerali ulimwengu hana lolote la maana,ni mnafiki na ni spent force na wala hana chochote kipya
 
Katika mjadala wa kitaifa ulioebdeshwa na Media Brain, Kuna wachangiaji wawili walitoa mwelekeo mzuri sana wa mjadala nao ni Dr Kitima na Jenerali Ulimwengu, na hawakuweka udini au nasaba. Na mojawapo ni Bunge kuwa Butu n.k na serikali kuharibu uaminifu wake na kuwa waongo waongo, na alipochangia Kitila mkombo mchango wake ulielekea kwenye uongo.
Mfano anasema mkataba ni kati ya serikali wakati DPW sio serikali.
Pili kifungu kinacho ruhusu mabadiliko ya mkataba ni tata maana kimesema by "mutual consent" maana yake sisi tuna weza taka hayo mabadiliko wao wakakata.
Katika watu wa hovyo kuwahi kutokea ni Kitila na sijui ni nani alimwalika.
 
Back
Top Bottom