FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,894
- 109,227
Spika anasema wacheni kupotosha:
--
Spika wa Bunge, Dr Tulia Ackson ametoa ufafanuzi kuhusu taarifa zilizosambaa zikidai kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari limesharidhia Azimio la Bunge kuhusu pendekezo la mkataba wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai ambapo amesema Bunge bado halijaridhia.
Spika Dr. Tulia amesema taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari na mitandao kuwa azimio hilo limesharidhiwa na Bunhe si za kweli kwani azimio husika kwa sasa bado lipo katika ngazi ya kamati ya pamoja kwa mujibu wa kanuni na mara baada ya kamati kumaliza kazi yake azimio hilo limepangwa kuingia Bungeni tarehe 10 June 2023 kwa ajili ya mjadala.
--
Spika wa Bunge, Dr Tulia Ackson ametoa ufafanuzi kuhusu taarifa zilizosambaa zikidai kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tayari limesharidhia Azimio la Bunge kuhusu pendekezo la mkataba wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai ambapo amesema Bunge bado halijaridhia.
Spika Dr. Tulia amesema taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari na mitandao kuwa azimio hilo limesharidhiwa na Bunhe si za kweli kwani azimio husika kwa sasa bado lipo katika ngazi ya kamati ya pamoja kwa mujibu wa kanuni na mara baada ya kamati kumaliza kazi yake azimio hilo limepangwa kuingia Bungeni tarehe 10 June 2023 kwa ajili ya mjadala.