Hali ya hewa nzuri, kuna kaubaridi kidogo, kama umetoka sehemu ya joto andaa nguo nzito kidogo
Kuna matope mvua ikinyesha
Kimbulu ndio lugha kuu hata hospitali ukifika au masokoni, unaweza ukawa discussion wakidiscus kwa kimbulu
Wanapenda sana kusoma ,hasa biology na chemistry
Kwakipindi hiki asilimia kubwa watu wapo mashambani , wanalima sana mahindi na maharage,
Pale kwa upande wa siasa HATA WATOTO NA WANAWAKE wanafuatilia sana siasa ukifika kutana na mzee yeyote piga nae story za siasa utajua kweli kuna watu wanajua mambo
Muda wote hata mchana wanaume wanavaa shuka, huo ni mtoko kabisa, pia mara nyingi huvaa bukta zile za shule ya msingi zikiwa na viraka( SIO UMASIKINI) ila ni tamaduni ya jamii hiyo. Tena hivyo viraka vinashonwa na uzi kwakutumia mkono na vinabandikwa kwa nje ( INGAWA SIO WOTE WAPO HIVYO) Na huenda wakawa wanabadilika kutokana na majira
Nguruwe zinafugwa kwa wingi mno
Sio wapenda usafi. Kula yao ,vaa yao, sio watu wakujipenda sana
Miswaki mara nyingi huwa niya miti(SIO KWAMBA MADUKANI HAKUNA ILA NI MAZOEA) ingawa sio wote
Rangi ya udongo ni udongo mwekundu.
Usafiri upo ila mtapangwa kama magunia ya mchele, kama kuna watu wanajua kupanga watu kama viroba vya mizigo utawakuta huko, labda kama unausafiri wako binafsi
Kila mahali utasikia neno SAITA,SAYUU,BARAGAHE,DERO, SHIDIKAH kariri hayo maneno ni comon kwa dongobesh
Ahsante