Safari ya Dongobesh Wilayani Mbulu

Safari ya Dongobesh Wilayani Mbulu

Huko ndio asili nyumbani asili yangu, waarab kama wazungu nusu, kama waethiopia, kuwa makini sana ni warembo mno, ukikosea kuchukua mke au demu wa mtu ukirudi na roho yako au moyo wako omba Mungu, kuwa makini sana, fanya yaliyokupeleka, ukiona warembo sana angalia tu, maana kuna mtu nyuma yake, wanapiga hao watu, nakushauri tena, fanya yaliyokupeleka. Haya, naamini umenisikia
Ndugu yangu kabisa hata Mimi wazazi wangu ni wazaliwa wa huko
 
Karibu sana

Kuna guests nzuri Sunshine na nyingine jirani na Torokauje bei 20000Tsh safi kabisa .Kuku choma Torokauje watam balaa.ITM 1 km from mjini bank NMB na CRDB ..Mpesa ulizia kwa Maziku hapo pia kuna Min supermarket
Vi grosari vya kutosha utakutana na Waarabu wa Dubai na WaEthiopia(wairaqw)...ni kamji katulivu hakuna Kufuatana fuatana bia 24hrs ....wenyeji Wachangamfu sana....pombe kali jamii ya Viroba kwa wingi usishangae kukuta warembo wakipiga hayo makitu...
Mayai ya kienyeji sh 300 moko...kuku wa kienyeji kibao bei nafuu kabisa...mahindi ya kuchoma maharage mabichi msimu mzima.....karoti bora barani Afrika kutoka Tumati

Nenda Mkuu hutajutia.....kuna mrembo anaittwa Pasikii ana kigrosari mtaa wa Mchagaa mchoma nyama maarufu....ukimwona mpe salamu
Ukifika huko usikose kutembelea mnada wa DIRIMU
Pasikii=Paskalina?
 
Shabiby nimetizama kwenye website yao hawana hiyo ruti. Ila Mtei naona wengi wanaisifia.
Ipo shabiby, labda website haijawa updated ila shabiby ipo na wiki hii tu nimetumia kampuni hiyo kusafirisha mizigo kutokea dar-babati

Shabiby anaaminika zaidi ya wote, mtei hawafai, maning nice wako vizuri ila hamfikii shabiby
 
Back
Top Bottom