Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

Tatizo tunafanya political discourse iangukie kwenye partisan lines. With sentimentalism kama vile tunaongelea unazi wa mpira. Wakipewa CCM milioni mia moja na wahindi, ufisadi.

Wakipewa CHADEMA, kukua kwa demokrasia. Si sawa hivyo.

Ukweli lazima usemwe, harufu ya ufisadi ni ile ile, iwe CHADEMA au CCM. Kikwete au Mbowe, Makamba au Slaa.

Can you imagine Kikwete na Makamba wangekuwa wanapokea milioni mia moja kutoka kwa muhindi kelele za ufisadi ambazo zingeporomoshwa hapa? Sasa mbona tuna standards tofauti kwa CHADEMA?

Double standards hizi mbaya.


Lakin kiranga huyu Sabodo kidogo yuko tofati na wahindi wengine. Ebu fatilia matangazo yake magazetin harafu uniambie kama huyu bwana ni sawa na sir CHANDE au PATEL na ROSTAM wake. Huyu yuko tofauti na utofauti wake haujaanza jana wala leo. Amekuwaanatoa matangazo kira mara magazetin kukemea ufisadi, na kwa kias flan anachungu. Kama na yeye ana harufu ya UFISAD sijui kwa kweli
 
Last but not least Chadema kinaendelea kuonekana ni chama cha kistaarabu kwa kuzingatia sheria zilizowekwa na bunge, kwa vile kilikuwa na option ya kuamua kupokea kimya kimya na hakuna mtu yeyote angejua.

Huwezi kusifia mtu aliyemtia mwanamke kidole kwa nguvu kwa sababu hajamtia dhakari (ashakum si matusi) katika sehemu ambayo kutia vidole si rape, lakini kutia dhakari ni rape. Halafu unasifia kwamba katia vidole kweupe kwa hiyo ni muwazi. Ningetegemea upige kelele kufanya hata kutia vidole kuwe rape.
Kiranga

Tatizo lako unafikiri hii thread tunajadili kwa ajili yako au inakulenga wewe tu NO, maana inaonekana kila mtu anapotoa hoja unarukia mimi sijasema ....mimi nimesema.......hatuendi hivyo. Hoja hii itajadiliwa hata kama mimi na wewe hatupo au hutuchangii kitu.

Another thing try to use a moderate language when responding to a post, thanks.

Respect
 
Kiranga

Tatizo lako unafikiri hii thread tunajadili kwa ajili yako au inakulenga wewe tu NO, maana inaonekana kila mtu anapotoa hoja unarukia mimi sijasema ....mimi nimesema.......hatuendi hivyo. Hoja hii itajadiliwa hata kama mimi na wewe hatupo au hutuchangii kitu.

Another thing try to use a moderate language when responding to a post, thanks.

Respect

Hhaha labda wewe ndiye unayefikiri thread ni yako kijoka cha mdimu.

And as far as using moderate language, I have never used it and never will.I believe in passionate discussion.
 
Lakin kiranga huyu Sabodo kidogo yuko tofati na wahindi wengine. Ebu fatilia matangazo yake magazetin harafu uniambie kama huyu bwana ni sawa na sir CHANDE au PATEL na ROSTAM wake. Huyu yuko tofauti na utofauti wake haujaanza jana wala leo. Amekuwaanatoa matangazo kira mara magazetin kukemea ufisadi, na kwa kias flan anachungu. Kama na yeye ana harufu ya UFISAD sijui kwa kweli

Ni kweli pia ametangaza scholarship mara nyingi nje ya nchi sina uhakika na wangapi wamezifaidi.

Kwa kutoa msaada huu waziwazi ni trasparency inayotakiwa kuigwa. Hivi kesho na keshokutwa Chadema wakikaa kimya au kutoa favour kwake wananchi tunajua why. Siyo wale washikaji wa 2005 ambao wamekuwa talk of the state na gharama za kuwatunza ziko kwa watanzania bila kujua nini kilitokea ilikuwa ni kiasi gani na makubaliano yalikuwa yapi vyeo, business deals au nini?
 
aya sisi wanainchi ndio wa kupiga kura na kuchagua nani atuongoze
ok na wengine wajitokeze hadharani wachangie basi vyama vya siasa
 
Chukueni muda kidogo kumfahamu huyu Mzee Sabodo kabla ya kutaka kuonyesha kuwa na yeye ni fisadi,

Kumbukeni kuwa huyu hata kwenye mfuko wa Mwl .Nyerere alitoa fedha nyingi kwa ajili ya bahati na sibu ile , na alitoa zaidi ya shilingi milioni mia nane (800) .

Kujitokeza hadharani kuichangia CHADEMA kunaonyesha kuwa anafanya biashara halali.

wanaosema eti TRA watamfuata jiulizeni mbona hawajamfuata Mbowe na Ndesamburo ? jambo la msingi ni watu kujifunza kuwa ukifanya biashara halali huwezi kuzushiwa .

Mbowe ni mfanya biashara na Ndesamburo ni mfanya biashara tena mkubwa tuu mbona wao TRA hawaendi ? ukiona anafuatwa jua kuna tatizo kwenye biashara zake.

Mbona CHADEMA kuna Musilm Hassanal naye ni muhindi mfanya biashara hao TRA mbona hawajamfuata?,
 
Yaani CHADEMA wameingia kwenye nyavu za CCM hivihivi. Hivi kuna muhindi gani mwenye jeuri ya kuchangia upinzani na kujitangaza hadharani?. Huyu jamaa katumwa afanye hivi makusudi, na lengo kuu ni kuiondoa hoja ya ufisadi katika uchaguzi huu. Yaani kwa kukubali hili chadema wamejitia kitanzi, upinzani kwisha kazi. Sasa chadema watapigia wapi kelele zao kuwa CCM inafadhiliwa na mafisadi wafanya biashara na wengi wao wenye asili ya asia?.

Haya shuguli imeisha sasa kwa mwenye akili timamu ni kwamba vita ya ufisadi leo ndiyo mwisho na kwa hili ninawaambieni hawawezi tena kuwashinda CCM kwa hoja hii. Shs Mil 100 ni hela ndogo sana kwa mafisadi na CCM kwa ujumla ila kwa wananchi wa kawaida hiyo ni big deal, na vyombo vya habari vimesetiwa kuionesha hii kwa walalahoi ili kuonesha kuwa anayechukua hela za wahindi ni CHADEMA si CCM. Underground CCM wamezikusanya zisizo na hesabu kama hivi ila kuwatega CHADEMA wawe publicized ni bao la kisigino kwa CCM.

Pesa yaweza kuwa ni mtego nami I thought the same lakini swali ni kwamba is this Sabodo naye fisadi ? Kuna mahali anatajwa ama connected to ufisadi ? If not them kafanya jambo jema and the man is heavy weight CCM watalia lia tu.
 
Tatizo tunafanya political discourse iangukie kwenye partisan lines. With sentimentalism kama vile tunaongelea unazi wa mpira. Wakipewa CCM milioni mia moja na wahindi, ufisadi.

Wakipewa CHADEMA, kukua kwa demokrasia. Si sawa hivyo.

Ukweli lazima usemwe, harufu ya ufisadi ni ile ile, iwe CHADEMA au CCM. Kikwete au Mbowe, Makamba au Slaa.

Can you imagine Kikwete na Makamba wangekuwa wanapokea milioni mia moja kutoka kwa muhindi kelele za ufisadi ambazo zingeporomoshwa hapa? Sasa mbona tuna standards tofauti kwa CHADEMA?

Double standards hizi mbaya.

Mkuu tatizo si kupewa hela na muhindi tatizo linaloikumba siku zote CCM na wachangiaji wake, wengi ni wahalifu wanaofahamika mfano RA, Jeetu, Fida, Somaiya etc. Lakini one thing inachotakiwa kujua ni kwamba Sabodo is totally different , ni mchangiaji amabaye so far unaweza kumwita credible! How much anachangia au anpaswa kuchangia that is another subject ambayo ofcourse tunaweza kuifungulia thread nyingine. Juzi juzi tumetangaziwa CCM imekusanya tayari bilioni hamsini of which I doubt kama ni kutokana na mia 2 mia 2. Kuna mkuu alisema is from SMS which is completely impossible.

However I am not trying to say TWO WRONGS CAN MAKE A RIGHT.
 
Sorry wanaJF, nimekuwa bize kdg nje ya mji hivyo nikawa outdated kwenye JF. Leo nimefanikiwa kupata internet cafe na kitu cha kwanza nikafungua JF, moja ya thread nilizotarajia kuzikuta ni mtazamo wa wana great thinkers juu ya uamuzi wa mfanyabiashara Sabodo kuchangia CHADEMA milioni 100 na kuahidi zaidi baadae. Najua lazima wanaJF wana maoni tofauti, ila thred yake sijaiona, iko wapi?
 
A%20S%20new.gif
Makamba: Si dhambi kuchangia Chademahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/5-habari-za-siasa/3226-makamba-si-dhambi-kuchangia-chadema


Wednesday, 14 July 2010 08:18
gazeti la mwananchi.


Ramadhan Semtawa

KATIBU mkuu wa CCM, Yusuph Makamba amesema kitendo cha kada wake maarufu na bilionea Mustafa Sabodo kuichangia Chadema, si dhambi kwa kuwa hata "Waislamu huchangia Wakristo" katika shughuli mbalimbali.

Sabodo, ambaye ni mfuasi mkubwa wa falsafa za muasisi wa taifa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere, alitoa hadharani hundi ya Sh100 milioni na kuweka bayana kuwa lengo lake ni kuwezesha wapinzani kupata wabunge wengi zaidi, kitu ambacho si cha kawaida katika duru za kisiasa nchini.

Lakini, akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana Makamba alisema kitendo hicho si dhambi wala cha ajabu kwa sababu Sabodo alitoa fedha kutoka mfukoni mwake na si za CCM.

"Kwani wewe dini gani," alimuuliza mwandishi. "Mimi dini yangu ya Mwislamu, lakini nimewahi sana kuchangia Wakristo. Kwani nilivyochangia Wakristo nilibadili dini kuwa Mkristo?

"Kwani ni kosa gani kwa Mkristo pia kumchangia Mwislamu? Huu ni upendo na ukifanya hivyo haimaanishi umebadili dini bwana weee.."

Akikabidhi fedha hizo, Sabodo alisema: "Kambi ya upinzani ikiimarika na kupata wabunge wengi, itasaidia kuimarisha demokrasia nchini na kuliletea taifa maendeleo ya kweli.”

Akifafanua zaidi, bilionea Sabodo alisema kwamba kuongezeka kwa wabunge wa upinzani bungeni ni jambo la muhimu katika kuweka upinzani kwa CCM na kusukuma gurudumu la maendeleo kwa wananchi wake.

Makamba alisema Sabodo bado ni mwanachama wao na kwamba kitendo chake cha kuisaidia Chadema hakiwezi kufungua mlango wa kutokea kwa wanachama ambao wanaona chama hicho kinakwenda tofauti na misingi iliyowekwa na waasisi.

"Tumeacha misingi ipi bwana mbona unataka kuongeza mambo....! mimi nakwambia hicho ni kitendo cha kawaida tu," alisema.
Alijifariji kwamba Sabodo hatajatangaza kuondoka CCM pamoja na kuichangia Chadema.

"Kwani CCM ni nini na Chadema ni nini? Hivi vyote ni vyama vya siasa kama ilivyo dini, hivyo kuchangia Chadema haimaanishi yuko Chadema," alisisitiza Makamba.

"Kuna sababu kuu za mtu kujiondoa katika chama; moja ni kunyang'anywa kadi au kurudisha kadi, sisi hatujamnyang'anya kadi wala yeye hajarudisha kadi," alisisitiza Makamba.

Kwa mujibu wa Makamba, CCM haina tatizo na mchango huo wa Sabodo kwa Chadema.

Sabodo kwa muda mrefu amekuwa kimya hasa tangu kuingia madarakani serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete.

Katika uongozi wa awamu ya tatu, Sabodo amewahi kushutumu baadhi ya mambo ndani ya serikali na chama ambayo yalikwenda kinyume na misingi iliyowekwa na Nyerere.
-mwisho-



wana jf mnasemaje kuhusu uweledi huu unaooneshwa na bw. sabodo na koment ya katibu mkuu wa chama chake?
 
Lakin kiranga huyu Sabodo kidogo yuko tofati na wahindi wengine. Ebu fatilia matangazo yake magazetin harafu uniambie kama huyu bwana ni sawa na sir CHANDE au PATEL na ROSTAM wake. Huyu yuko tofauti na utofauti wake haujaanza jana wala leo. Amekuwaanatoa matangazo kira mara magazetin kukemea ufisadi, na kwa kias flan anachungu. Kama na yeye ana harufu ya UFISAD sijui kwa kweli

Kama unasoma posts zangu vizuri utagundua tatizo langu kimsingi si Sabodo, mimi siongelei mtu mmoja mmoja, naongelea principles ambazo zina apply kwa watu wote.

Hata kama Sabodo ni safi (debatable by the way) hii loophole ya rushwa ni lazima tukubali kwamba ni kubwa sana kuruhusiwa. Na hata kama mtu ni safi, mtu anaweza kuwa tempted.Katika "The Godfather" Mario Puzo anakwambia "every man has a price" kwa hiyo kwa nini tuachie michango ya kampeni isiyo na regulations au iliyo na lax regulations?

Leo kaja Sabodo na kampa hela Mbowe, suppose wote waminifu, kesho wakija wengine wasio waaminifu je? Huwezi kuacha mwanya wa rushwa uendelee kuwepo na kutumini kwamba watu watakuwa waaminifu, inabidi kuwe na sheria zinazoguarantee at least kwamba mtu akijiingiza katika vitu vyenye mianya ya rushwa anakuwa anavunja sheria.
 
Kama chadema kachanga m100 tena waziwazi hivi,basi ccm usikute alishapeleka billions kadhaa.

Kwa vyovyote vile, Mr Sabodo anastahili pongezi kubwa kutoka kwa wapenda demokrasia wote, including wale walioko ndani ya CCM, kwa kitendo chake cha kutaka kupunguza "one-sidedness" iliyoshamiri nchini kwa zaidi ya nusu karne sasa. Kama anachangia pia CCM isiwe nongwa kwani serikali imekuwa siku zote ikiwachangisha wafanya biashara kwa ajili ya CCM kwa kutumia mbinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mbinu ambazo hazikubaliki katika nchi ya kidemokrasia. Kwa upande mwingine, serikali imekuwa ikiwatisha na kuwahujumu wafanyabiashara kila wakitaka kukichangia chama kingine hata kwa kiasi kidogo. Kama huu siyo "wivu wa kike" ndiyo nini?.

Kitendo cha Sabodo kuchangia CHADEMA hadharani ni mfano mzuri wa kuigwa na wafanyabiashara wengine hasa wale ambao tayari wanachangia CCM, iwe kwa hiari yao wenyewe au kwa kushinikizwa. Hali ya nchi kuwa dominated na chama kimoja kwa kiasi kikubwa na muda mrefu kama ilivyo Tanzania kunaifanya serikali iwe ni ya KIVIVU na ya KIZEMBE hali ambayo haiweki mazingira mazuri kwa maendeleo ya biashara na ukuaji wa uchumi. Wafanya biashara wengi wanajua hilo.

Serikali inawakamulia CCM mabilioni kutoka serikali yenyewe, taasisi zake, mashirika ya uma, mifuko ya pensheni, mamlaka na tume kadha wa kadha ambazo ukifikiria huoni sababu nyingine ya kuanzishwa kwazo isipokuwa kuwakamua wananchi na wafanyabiashara kwa manufaa ya CCM au manufaa ya watu binafsi kwani hela wanazookota zinawekwa kwenye private accounts zilizoko kwenye private banks hivyo kwamba ni vigumu kwa wananchi kujua hela hizo ni kiasi gani na zimetumiwa vipi. Hizo, bila kutaja mabilioni mengine wanayopata kutoka nchi za kikomunisti zenye nia ya kudumisha mfumo wa chama kimoja nchini.

Kama wafanyabiashara wote wanaochangia CCM - iwe kwa hiari yao wenyewe au kwa kulazimishwa - wangechangia chama kingine NUSU tu ya kile kiasi wanachochangia CCM, matokeo yake yatakuwa manufaa makubwa kwa taifa.
 
Wanafiki wataleta maneno ya kukatisha tamaa kuhusu mchango wa Mzee huyu. Tunamfahamu sana kuwa ana uadilifu mkubwa. CCM huwa inaiba halafu inadanganyia kuchangiwa na watu. Waacheni watu wenye nia njema na TZ wachangie vyama vitakavyoleta mabadiliko chanya.

Ni wendawazimu kukejeli hatua hii nzuri ya mzee huyu. Mwenye kukejeli atakuwa yule tu anayefaidika na ufisadi wa CCM. Wenye nia ya dhati wataungana na mzee huyu kuleta mabadiliko ya kweli.
 
Hizo mia amewapa CHADEMA ili wafanyie nini? Hawa si wanachukua ruzuku serikalini, bajeti ya kampeni zao iko wapi ili tuone wamepungukiwa pesa ngapi za kukodi chopa!!!!? Sabodo ni mwanaharakati toka kitambo, lakini mi naona angetoa pesa kwa ajili ya kuelimisha wananchi juu ya haki zao katika uchaguzi (wengi hawajui kuwa wanaweza wakapokea tshirts, kanga na pilau kisha watoe kura kwa mtu wa maana!).
 
Hizo mia amewapa CHADEMA ili wafanyie nini? Hawa si wanachukua ruzuku serikalini, bajeti ya kampeni zao iko wapi ili tuone wamepungukiwa pesa ngapi za kukodi chopa!!!!? Sabodo ni mwanaharakati toka kitambo, lakini mi naona angetoa pesa kwa ajili ya kuelimisha wananchi juu ya haki zao katika uchaguzi (wengi hawajui kuwa wanaweza wakapokea tshirts, kanga na pilau kisha watoe kura kwa mtu wa maana!).
Swali zuri sana nadhani ungelielekeza kwanza kwa CCM waliowazoefu na mabiolioni ya michango ingefaa kuliko Chadema ambayo ndiyo mara yake ya kwanza kupokea.
 
Wanafiki wataleta maneno ya kukatisha tamaa kuhusu mchango wa Mzee huyu. Tunamfahamu sana kuwa ana uadilifu mkubwa. CCM huwa inaiba halafu inadanganyia kuchangiwa na watu. Waacheni watu wenye nia njema na TZ wachangie vyama vitakavyoleta mabadiliko chanya.

Ni wendawazimu kukejeli hatua hii nzuri ya mzee huyu. Mwenye kukejeli atakuwa yule tu anayefaidika na ufisadi wa CCM. Wenye nia ya dhati wataungana na mzee huyu kuleta mabadiliko ya kweli.

Typical myopic one track mind mentality, mtu hawezi kuja kui criticize CHADEMA bila ya kuwa fisadi na kibaraka wa CCM. Check my record hapa uone nani kai criticize CCM zaidi kati yangu na wewe.

Tatizo letu ni kubwa kuliko CCM, tatizo letu ni status quo, na as far as I am concerned uongozi wa CHADEMA upo katika status quo na michango kama hii inauvuta zaidi katika status quo.Wakishindwa kuleta mabadiliko ya kweli wataona at least politics ni a lucrative career and business.

Ukweli unabaki kwamba, CHADEMA kukubali michango mikubwa in particular na Tanzania kutokuwa na strict campaign finance regulations kutaua democracy.

Kwa jinsi hii hata CCM inaweza kuihonga CHADEMA mchana kweupe kwa kutumia mwanachama wake, na watu wanaoabudu fedha wakapiga makofi kushangilia.
 
hao wafanyabiahsra wa asili ya asia ndio walivyo, wnajilinda kwa kujiweka sawa kwa yoyote atayeshinda amlinde
 
Sabodo atawachagulia mwana CCM (a.k.a Mpenda zote) awe mgombea Urais mil.100 mchezo? naona padre slaa anavyozitamani ...kazi kwelikweli njaa kitu mbaya sana?

Poor you!roho itakuuma mwaka huu mpaka basi.Na bado.Poleni kwa kuhisi kuwa Mpendazoe ndiye atakuwa mgombea Urais.Kwa mtazamo wetu Mpendazoe sio material ya Urais kwa CHADEMA kwa sasa may be some years later kama tuandelea kuwa naye..Kwa sasa mgombea Urais atatokana na CHADEMA.Tena mtapigwa na butwaa na mishangao..Ni miongoni mwa vichwa katika Taifa hili.Utalia na roho yako na huyo Lipumbafu wenu.
 
Back
Top Bottom