Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

Tunataka watu wenye uweledi kama sabodo. Katika siasa hakuna rafiki au adui wa kudumu.
...Mkuu hawa sisiem huwa hawaeleweki kabisa siku zote wanapenda mambo mazuri yaende kwao tu. Hapo nina uhakika wale akina Chili..., Ma-rope na wengine utasikia tu siku si nyingi wanaanza kashfa!!....
 
kwenye hizi picha huyu mzee anaonekana kama kapalalaizi au ni macho yangu tu?
 


juu mfanyabiashara maarufu na muumini wa maendeleo ya kijamii nchini, bw. Mustapha jaffar sabodo akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 100 mwenyekiti wa taifa wa chadema mh.freeman mbowe aliyeambatana na katibu mkuu wake dr wilibrod slaa leo jijini dar. Chini bw. Sabodo akiongea na mh. Mbowe na dk. Slaa

*asifu umakini wake ndani na nje ya bunge
*awapongeza mbowe na dr slaa
*aahidi kuchangia zaidi


mfanyabiashara maarufu na muumini wa maendeleo ya kijamii nchini, mustapha jaffar sabodo amekichangia chama cha demokrasia na maendeleo-chadema shilingi milioni mia moja ili kuimarisha upinzani na demokrasia nchini.

Bw. Sabodo amekabidhi hundi ya kiasi hicho cha fedha leo jijini dar kwa mwenyekiti wa taifa wa chadema bw. Freeman mbowe aliyeambatana na katibu mkuu wake dr wilibrod slaa na mkurugenzi wa fedha wa chama hicho bw. Antony komu.


akikabidhi hundi hiyo bw. Sabodo amesema pamoja na kwamba yeye ni mwanachama wa chama cha mapinduzi lakini anapenda kuona upinzani na demokrasia vinaimarika nchini huku akikitaja chadema kuwa ni chama makini na safi cha upinzani.


bw. Sabodo amekuwa mmoja wa wazee walio wazi katika kukosoa utendaji wa serikali ya chama chake ccm hasa inapokiuka misingi ya utawala bora iliyojengwa na mwasisi wa tanzania mwalimu julius nyerere.


“mimi ni mwanachama wa ccm lakini napenda kuona demokrasia ikikua huku kambi ya upinzani ikiimarika kwa kuwa na wabunge wengi bungeni ili kushamirisha maendeleo nchini……na nawachangia chadema kwa kuwa natambua umakini wenu katika siasa za hapa nchini na hasa bungeni”, alisema.


bw. Sabodo amesema kuongezeka kwa wabunge wa upinzani bungeni ni jambo la muhimu katika kutoa upinzani kwa ccm na kusukuma maendeleo ya wananchi huku akikitaka chadema kuongeza nguvu zaidi katika harakati zake za kisiasa na kumwelezea dr slaa kuwa ni mwanasiasa mwenye uchungu wa kweli na watanzania.


aidha bw. Sabodo amesema ana mpango wa kuichangia fedha zaidi chadema ili kuimarisha harakati zake za kisiasa na kuahidi kufanya hivyo atakaporejea nchini akitokea india kwenye matibabu.


akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwa bw. Sabodo mtaa wa upanga jijini dar es salaam mwenyekiti wa chadema freeman mbowe ameshukuru na kutaja msaada huo kuwa ni wa kihistoria katika siasa za vyama vingi nchini.


amesema mara nyingi imekuwa ni vigumu kwa wafanyabiashara wakubwa wa kada ya bw. Sabodo kuchangia kwa uwazi tena kiasi kikubwa cha fedha na kutaka hatua hiyo kuigwa na wafanyabiashara wengine nchini.


“kwa kweli tunashukuru sana hii ni historia mpya katika siasa za vyama vingi nchini, ni wajibu wa wafanyabiashara wakubwa kuona umuhimu wa kusaidia vyama vyote makini nchini bili kuwa na ubaguzi wala woga, mzee ameonyesha njia naamini itakuwa ni mfano kwa wengine wenye uwezo, alisema bw. Mbowe.


kwa upande wake, katibu mkuu dr slaa ameshukuru kwa mchango huo na kudokeza kwamba mchango utatumika kwa kadiri ya vipaumbele vitakavyopangwa kwenye kamati kuu ya chama inayotarajiwa kufanyika tarehe 20 julai 2010 ikilenga zaidi katika kutekeleza mipango endelevu ya kuimarisha chama kama operesheni sangara na utekelezaji wa mikakati ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.


“nawaomba watanzania wengine wa kada na uwezo mbalimbali kuichangia chadema ili kuondokana na ukiritimba wa chama kimoja kwani ni hatari kwa maendeleo na usalama wa nchi kama michango yote ikielekezwa kwa chama tawala pekee.


"natoa mwito kwa vyombo vya dola kuacha kuwatisha watanzania wenye mapenzi mema wanaochangia vyama mbadala kama chadema kwani kufanya hivyo ni kuhujumu taifa na kukwamisha maendeleo ya nchi”, alisema



imetolewa tarehe 12 julai na:



erasto tumbo

mkurugenzi wa habari na uenezi

chanzo: habari hii imesambazwa na erasto tumbo kwa kushirikiana na john mnyika kwa vyombo vya habari

mh! Interesting tunataka watu kama hawa but why chadema?


*asifu umakini wake ndani na nje ya bunge
 
Last edited by a moderator:


Mfanyabiashara maarufu na muumini wa maendeleo ya kijamii nchini, BW. Mustapha Jaffar Sabodo akimkabidhi hundi ya shilingi milioni 100 Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA Mh.Freeman Mbowe aliyeambatana na Katibu Mkuu wake Mh. Dr Wilibrod Slaa jana jijini Dar.

CCM WASIJE WAKAMSHUHULIKIA HUYU MKEREREKETWA KAMA WANAVYOFANYA KWA WENGINE.

CHONDE CHADEMA PESA YA KUJIHIMARISHA HIYO BANA SI ULAJI .....
 

Attachments

  • sabodo.jpg
    sabodo.jpg
    27.7 KB · Views: 71
Tatizo langu ni kuwa nina imani ndogo sana na hawa watu wenye asili hiyo maana wengi wao wameifisadi nchi vilivyo na bado tunawakumbatia.
vyanzo vya michango yote hiyo ni nini milioni 100 kila kinachochangia mmh! isije ikawa ndio mwenzetu we pweza wala ndio nala! tehe tehe.:A S tongue:
 
Hongereni sana Chadema kwa umakini wenu hadi kumshawidi mzee SABODO kuwa changia kiasi hicho kikubwa cha pesa. ni matumaini yetu watajitokeza wengine wengi tu, nimemjua mzee sabodo kwa muda mrefu kiasi kuwa yeye ni muumini mkubwa wa siasa za mwalimu JK pia ni mmoja wa wadhamini wa mfuko wa mwalimu Nyerere na kwa hakika naamini mzee sabodo ameona mbali na kafanya tafakuli ya muda mrefu hadi kushawishika na kuichangia Chadema, wito wangu kwa wafanyabiashara wengine kama Ole Mangi na wengine changieni Chadema ili tufanikishe maendeleo na demokrasia ya kweli nchini! Chademaaaa! ushindiiii! Hatulali hadi Kieleweke!
 
This requires more than just transparency, we surely need transparency, but we also need caps on these amounts.

The best thieves steal in broad daylight, usidanganyike na show za photo ops.

Tujue kitu kimoja, kwamba bila sheria watu hawalazimiki ku act in the best interest of all, wata act in their own best interest. Bila strict campaign finance laws hawa matajiri pamoja na viongozi wa vyama vya kisiasa hawalazimiki ku act in the best interest of the people, and can easily cut deal consciously or even get into temptations and be trapped unconsciously.

Hata baada ya strict campaign finance laws, inabidi tuwe macho sana tu, sembuse sasa hivi ambako hatuna hata hizo sheria ?

Mimi hii supposed transparency hainipi any level of comfort at all, kwa sababu ukweli unabaki kibopa akichangia shilingi milioni 100 anapata power sana chamani na anaweza kutaka kulipwa fadhila kwa namna yoyote, na CHADEMA wakishaonja utamu wa mamilioni ya michango who is to say how will they react ?

T.H White katika "The Once and Future King" aliandika "What is not forbidden is compulsory" . Tusipokataza huu mwanya wa rushwa katika michango ya kampeni, tutawalazimisha wafanyabiashara wote watumie mbinu za michango ya kampeni kwa njia za kutoa rushwa.
wewe unalako jambo! wewe unafikiria bila michango na mali upinzani utasimama hiyo 100 million na mabilioni ya fedha zinazoibiwa tena za misaada (Sitta gave figures some times ago) kipi bora? sometimes it takes to befriend ur enemy to win! haswa ukizingatia jinsi system ilivyo repressive namna hii!
 
wewe unalako jambo! wewe unafikiria bila michango na mali upinzani utasimama hiyo 100 million na mabilioni ya fedha zinazoibiwa tena za misaada (Sitta gave figures some times ago) kipi bora? sometimes it takes to befriend ur enemy to win! haswa ukizingatia jinsi system ilivyo repressive namna hii!

Sijakataa michango, nimeeleza umuhimu wa wanachama kuchangia vyama vyao, nimeeleza umuhimu wa wanachama ku own vyama vyao, nimeeleza hatari ya matajiri wachache kununua influence katika vyama vyetu visivyo na resources.

Mabilioni ya fedha za misaada kuibiwa ni vibaya, lakini kuibiwa huku kwa mabilioni ya fedha hakuhalalishi mianya ya rushwa mingine iachwe. Two wrongs do not make a right, wrong is wrong and will still be wrong.

Not having a tough campaign finance law is wrong. Chama kukubali michango mikubwa kutoka kwa matajiri wachache si sawa, unwaweka matajiri hawa na viongozi wa vyama katika temptation ya rushwa hata kama hawana nia hiyo.

I am not talking about winning or losing, I am talking principle. I bet you can't understand that. We are a nation without principles.

Hata hao wanaopigana against ufisadi hawaoni ubaya kupigwa picha wanapokea mihela kibao kutoka kwa matajiri. Hata hao wanaopinga ufisadi hapa JF wanaupinga ukiwa CCM tu, ukiwa CHADEMA mswano.

CHADEMA inanunuliwa na matajiri polepole, mwisho wake itakuwa haina tofauti na CCM.
 
Sijakataa michango, nimeeleza umuhimu wa wanachama kuchangia vyama vyao, nimeeleza umuhimu wa wanachama ku own vyama vyao, nimeeleza hatari ya matajiri wachache kununua influence katika vyama vyetu visivyo na resources.

Mabilioni ya fedha za misaada kuibiwa ni vibaya, lakini kuibiwa huku kwa mabilioni ya fedha hakuhalalishi mianya ya rushwa mingine iachwe. Two wrongs do not make a right, wrong is wrong and will still be wrong.

Not having a tough campaign finance law is wrong. Chama kukubali michango mikubwa kutoka kwa matajiri wachache si sawa, unwaweka matajiri hawa na viongozi wa vyama katika temptation ya rushwa hata kama hawana nia hiyo.

I am not talking about winning or losing, I am talking principle. I bet you can't understand that. We are a nation without principles.

Hata hao wanaopigana against ufisadi hawaoni ubaya kupigwa picha wanapokea mihela kibao kutoka kwa matajiri. Hata hao wanaopinga ufisadi hapa JF wanaupinga ukiwa CCM tu, ukiwa CHADEMA mswano.

CHADEMA inanunuliwa na matajiri polepole, mwisho wake itakuwa haina tofauti na CCM.

Kiranga mimi natofautiana na wewe kuhusu hili la vyama kukubali michango toka kwa matajiri, ni kweli kuwa wakti mwingine matajiri hawa wanaochangia vyama huwa hawana nia njema na vyama hivi lakini kama CHAMA na VIONGOZI wake watakuwa na msimamo juu ya sera na Maamuzi ya CHAMA kamwe hawatayumbishwa na matajiri hawa. Kumbuka hata TANU wakati wa kutadi uhuru ilifanikiwa kwa michango ya matajiri walikuwa na nia njema na mustakabali na ustawi wa nchi, kumbuka watu kama Rupia, Aziz Ally, Sykes na wengine ndio walifanikisha safari ya Mwalimu kule UNO kutoa ile hotuba maarufu iliyopelekea UNO ku grant uhuru kwa Tanganyika. lakini kutokana na msimamo imara wa Mwalimu na viongozi wengine wa TANU, walikataa chama kutumika kwa faida ya matajiri wale na kwa hakika watanganyika wote walifurahi! hata|CCM wakati wa mwalimu kulikuwa na matajiri waliokichangia chama, tatizo linakuja pale tu viongozi wanapokuwa na tamaa na kujali maslahi yao badal ya maslahi ya wale wanaowatumikia na hili lipo CCM, na ninathubutu kabisa kusema SIJALIONA CHADEMA ndio maana sina SHAKA hata chembe ni NIA ya mzee Sabodo kuchangia Chadema na wala sina HOFU kwa Chadema kupokea mchango huo!
 
Kwa kweli huyu mzee amefanya jambo la busara sana, anastahili kuungwa mkono na kila mtu mpenda demokrasia kwani itasaidia sana kuondoa ukiritimba wa chama TAWALA kudhani kwamba wao tu ndio wanaostahili kuchangiwa na wafanya biashara wakubwa.
Naamini kabisa huyu mheshimiwa si miongoni mwa mafisadi kwani angekuwa mmoja wao asingefanya hivyo.
Ahsante sana Mr Sabodo kwa ujasiri uliyouonesha kwa mstakabali wa demokrasia yetu.
 
Kwa kweli huyu mzee amefanya jambo la busara sana, anastahili kuungwa mkono na kila mtu mpenda demokrasia kwani itasaidia sana kuondoa ukiritimba wa chama TAWALA kudhani kwamba wao tu ndio wanaostahili kuchangiwa na wafanya biashara wakubwa.
Naamini kabisa huyu mheshimiwa si miongoni mwa mafisadi kwani angekuwa mmoja wao asingefanya hivyo.
Ahsante sana Mr Sabodo kwa ujasiri uliyouonesha kwa mstakabali wa demokrasia yetu.

Wapenda demokrasia wa kweli hawapendi matajiri wachache kununua influence katika vyama kwa jinsi ambayo inaweza kuzaa rushwa.

Demokrasia maana yake ni utawala wa wengi, wapenda demokrasia wa kweli watapenda sana vyama vya upinzani vikiweza ku raise hela kama hizi kutokana na michango ya wanachama wake in general, sio kutokana na mchango wa tajiri mmoja.

Michango kama hii amabayo kwa juu juu inaonekana kama inakuza demokrasia actually inaweza kuwa inaua demokrasia, in the sense kwamba tunaanza ku create tabaka la matajiri wanaokuwa na influence kubwa sana katika vyama vya siasa, na viongozi wa vyama vya siasa wanaokosa uhuru wa maamuzi kwa sababu ya utegemezi wao mkubwa kwa tabaka fulani dogo la matajiri.

Kwa hiyo wapenda demokrasia wa kweli wangependa kuona campaign finance laws zinawekwa kuondoa mianya ya rushwa, wangependa kuona Tanzania inaongeza GDP per capita, wangependa kuona Wtanzania wanaweza kuwa na disposable income na political awareness ya kutosha kuchangia vyama vyao.

Wapenda demokrasia wa kweli hawawezi kufurahia matajiri wachache kuchangia hela nyingi.Hii ni kualika disaster.
 
Mkuu wewe katika taratibu za kibank hutakuwa hujui hapo inafanyika TT Teregraphic Transfer

Mkuu King of Kings pia inategemea kama wote wako benki moja unaweza kumlipa kiasi chochote kile bila TT.

Wengi kimewauma lakini bado kama kazi watu watapoteza tu!
 
Naona watu hatuelewi maana ya ufisadi ndiyo maana Dr Slaa aliwaambia wapiganaji wa CCM wanapinga kitu wasichokijua ni kama wamedandia train kwa mbele.

Kuwa na hela nyingi si ufisadi ila channel iliyotumika kuzipata hizo hela ndiyo inaweza ku define ufisadi, ina maana mimi leo nikijitokeza kutoa mil.100 utaniita fisadi hata kama ulikuwa hunijui?

Kitendo cha Sabodo kina faida na hasara kwa upinzani lakini faida ndizo nyingi kuliko hasara, kwanza kimeonyesha kwa wananchi siasa si uadui kimetoa uoga waliokuwa nao hasa ndugu zetu jamii ya kiasia kila wakati uchaguzi unapokaribia.

Kimekijengea chama heshima mbele ya jamii kuwa Chadema haikujengwa kwa misingi ya matabaka watu wote ni sawa hii itafanya baadhi ya jamii ya kiasia kujiunga na kuvisaidia vyama vya upinzani.

Pia chama kime demonstrate sheria mpya ya uchaguzi kwa vitendo 'transparency' endapo kama nchi yetu ingekuwa ya kidemkrasia halisi viongozi waliotia saini sheria hii mpya wangekipongeza kitendo hiki.

Last but not least Chadema kinaendelea kuonekana ni chama cha kistaarabu kwa kuzingatia sheria zilizowekwa na bunge, kwa vile kilikuwa na option ya kuamua kupokea kimya kimya na hakuna mtu yeyote angejua.

Leo watu wanakuja na maoni ya maximum limit kwa vile tu Chadema kimeamua kufuata sheria(to be transparent), unapofuata sheria vizuri ndipo utapokuwa na uwezo wa kugundua mapungufu yake otherwise sheria zisingefuatwa leo tusingekuja na wazo la maximum limit.
 
Wapenda demokrasia wa kweli hawapendi matajiri wachache kununua influence katika vyama kwa jinsi ambayo inaweza kuzaa rushwa.

Demokrasia maana yake ni utawala wa wengi, wapenda demokrasia wa kweli watapenda sana vyama vya upinzani vikiweza ku raise hela kama hizi kutokana na michango ya wanachama wake in general, sio kutokana na mchango wa tajiri mmoja.

Michango kama hii amabayo kwa juu juu inaonekana kama inakuza demokrasia actually inaweza kuwa inaua demokrasia, in the sense kwamba tunaanza ku create tabaka la matajiri wanaokuwa na influence kubwa sana katika vyama vya siasa, na viongozi wa vyama vya siasa wanaokosa uhuru wa maamuzi kwa sababu ya utegemezi wao mkubwa kwa tabaka fulani dogo la matajiri.

Kwa hiyo wapenda demokrasia wa kweli wangependa kuona campaign finance laws zinawekwa kuondoa mianya ya rushwa, wangependa kuona Tanzania inaongeza GDP per capita, wangependa kuona Wtanzania wanaweza kuwa na disposable income na political awareness ya kutosha kuchangia vyama vyao.

Wapenda demokrasia wa kweli hawawezi kufurahia matajiri wachache kuchangia hela nyingi.Hii ni kualika disaster.

Unapoleta ,mambo ya marekani hapa ni sawa na kumumtembeza kichanga wa siku mbili. Tunajua kuwa compaign finance ina umuhimu ila kwa kuwa haipo inabidi tuhakikishe kuwa inakuwapo.

Nilichopenda kuhusu hii ni kwamba imefanyika kwa uwazi kabisa ambayo inatia moyo kwamba at least mtoaji hakuwa lengo baya (sometimes) kwa kuwa angeweza kutoa kwa kujificha kama wanavyofanya wengi tu kwa CCM. Chaa ajabu umesubiri mpaka ametoa Chadema ndiyo unaanza na ngojera za Marekani kama alivofanya Mcain akishirikiana na Faingold(spelling zimenitoka) mara baada ya kushindwa na Bush. Lakini baada ya hiyo campaign finance yake Bush alirise more money that before hiyo campaign finance, Ina shangaza!

Pamoja na hiyo campaign finance yako bado Obama alichangiwa na watu wenye majina ambayo kwa mfano "kiatu kimoja" kwa hiyo compaign finance siyo 100% suluhisho, suluhisho ni kuwa na watu wanaoipenda nchi yao (uzalendo) kama hao wamerekani na raia wenye akili timamu ingalau 2/3 ya nchi hapa kwetu ni kama 16% hivi!
 
Naona watu hatuelewi maana ya ufisadi ndiyo maana Dr Slaa aliwaambia wapiganaji wa CCM wanapinga kitu wasichokijua ni kama wamedandia train kwa mbele.

Kuwa na hela nyingi si ufisadi ila channel iliyotumika kuzipata hizo hela ndiyo inaweza ku define ufisadi, ina maana mimi leo nikijitokeza kutoa mil.100 utaniita fisadi hata kama ulikuwa hunijui?

Kitendo cha Sabodo kina faida na hasara kwa upinzani lakini faida ndizo nyingi kuliko hasara, kwanza kimeonyesha kwa wananchi siasa si uadui kimetoa uoga waliokuwa nao hasa ndugu zetu jamii ya kiasia kila wakati uchaguzi unapokaribia.

Kimekijengea chama heshima mbele ya jamii kuwa Chadema haikujengwa kwa misingi ya matabaka watu wote ni sawa hii itafanya baadhi ya jamii ya kiasia kujiunga na kuvisaidia vyama vya upinzani.

Pia chama kime demonstrate sheria mpya ya uchaguzi kwa vitendo 'transparency' endapo kama nchi yetu ingekuwa ya kidemkrasia halisi viongozi waliotia saini sheria hii mpya wangekipongeza kitendo hiki.

Last but not least Chadema kinaendelea kuonekana ni chama cha kistaarabu kwa kuzingatia sheria zilizowekwa na bunge, kwa vile kilikuwa na option ya kuamua kupokea kimya kimya na hakuna mtu yeyote angejua.

Leo watu wanakuja na maoni ya maximum limit kwa vile tu Chadema kimeamua kufuata sheria(to be transparent), unapofuata sheria vizuri ndipo utapokuwa na uwezo wa kugundua mapungufu yake otherwise sheria zisingefuatwa leo tusingekuja na wazo la maximum limit.

Asante majibu mengine huwa yanafariji. mkuu luteni nashukuru
 
Naona watu hatuelewi maana ya ufisadi ndiyo maana Dr Slaa aliwaambia wapiganaji wa CCM wanapinga kitu wasichokijua ni kama wamedandia train kwa mbele.

Dr. Slaa mwenyewe anapiga lip service. Caesar alisema mke wake si tu hatakiwi kuwa na hatia, bali pia hatakiwi hata kuwa katika mazingira ya kushukiwa kuwa na hatia.Hawa CHADEMA kwa mkwala wao waliokuja nao katika kupinga ufisadi watu tukafikiri watakuwa na code of conduct iliyo over and above what CCM had to offer, kuja kushtuka kumbe wanataka kuwa CCM B tu!

Kuwa na hela nyingi si ufisadi ila channel uliyotumia kuzipata hizo hela ndiyo inaweza ku define ufisadi, ina maana mimi leo nikijitokeza kutoa mil.100 utaniita fisadi hata kama ulikuwa hunijui?

Sijasema kuwa na pesa nyingi ni ufisadi, nimesema mtu mmoja kutoa msaada mkubwa bila regulations za campaign finance kunatoa mwanya mkubwa sana wa rusha.Hawa wafanyabiashara ni binadamu, hawa viongozi wa vyama ni binadamu, wana mawaa kibao, kwa nini tunataka kuwaachia temptations kibao ?

Kitendo cha Sabodo kina faida na hasara kwa upinzani lakini faida ndizo nyingi kuliko hasara, kwanza kimeonyesha kwa wananchi siasa si uadui kimetoa uoga waliokuwa nao hasa ndugu zetu jamii ya kiasia kila wakati uchaguzi unapokaribia.

Wewe wasema, mimi naweza kusema hasara za kufanya vyama viwe tegemezi, visihamasishe wanachama wake vilivyo, athari za kuendeleza utamaduni wa utegemezi kwa ma godfather miongoni mwa wanachama, athari za influence peddling, athari za kuua demokrasia ni kubwa kuliko faida za huu mchango.

Kimekijengea chama heshima mbele ya jamii kuwa Chadema haikujengwa kwa misingi ya matabaka watu wote ni sawa hii itafanya baadhi ya jamii ya kiasia kujiunga na kuvisaidia vyama vya upinzani.

Kufadhiliwa hakuna heshima.CHADEMA kinaingia matabaka, kama watu wote wangekuwa sawa chama kisingekubali msaada mkubwa sana kutoka kwa mtu mmoja, tofauti ya aliyetoa mchango mkubwa na aliyetoa mchango mdogo ingekuwa ndogo. Unaonyesha jinsi gani ulivyo tegemezi kwa waasia ambao ni asilimia ndogo sana ya raia wetu, kwa nini watu wachache wawe na influence kubwa kiasi hiki ?

Pia chama kime demonstrate sheria mpya ya uchaguzi kwa vitendo 'transparency' endapo kama nchi yetu ingekuwa ya kidemkrasia halisi viongozi waliotia saini sheria hii mpya wangekipongeza kitendo hiki.

Sheria mpya ya uchaguzi sheria gani? Tushakubaliana kwamba bongo hamna campaign finance ndiyo maana mtu yeyote anaweza kwenda kununua chama. Unasifia mwizi anakuibia kwa sababu badala ya kukuibia kisiri anakuibia mchana na kukuambia kamba anakuibia? Transparency si kitu ambacho mtu mwenye akili anaweza kusifia, transparency inakuonyesha tu kama kuna kitu cha kusifia au hamna.

Last but not least Chadema kinaendelea kuonekana ni chama cha kistaarabu kwa kuzingatia sheria zilizowekwa na bunge, kwa vile kilikuwa na option ya kuamua kupokea kimya kimya na hakuna mtu yeyote angejua.

Huwezi kusifia mtu aliyemtia mwanamke kidole kwa nguvu kwa sababu hajamtia dhakari (ashakum si matusi) katika sehemu ambayo kutia vidole si rape, lakini kutia dhakari ni rape. Halafu unasifia kwamba katia vidole kweupe kwa hiyo ni muwazi. Ningetegemea upige kelele kufanya hata kutia vidole kuwe rape.

Leo watu wanakuja na maoni ya maximum limit kwa vile tu Chadema kimeamua kufuata sheria(to be transparent), unapofuata sheria vizuri ndipo utapokuwa na uwezo wa kugundua mapungufu yake otherwise sheria zisingefuatwa leo tusingekuja na wazo la maximum limit.

Mimi nitambalasa mtu yeyote mwenye hipocrisy, nishawabalasa CCM sana tu kwa hiyo huwezi kusema nawabalasa CHADEMA tu. Hii transparency imewekwa makusudi ili tuweze ku scrutinize mambo zaidi, kwa hiyo huwezi kusema tuwaachie CHADEMA kwa sababu wako transparent, transparency si goal letu, ingekuwa transparency ndiyo goal letu watu wangekuwa wanauana mchana kweupe in the middle of kariakoo ili kuwa transparent, halafu usiweze kuwashtaki, si wamekuwa transparent bwana?

Transparency ni njia ya kuelekea kweny a responsible society, lakini transparency in itself si goal. Usiongee kama transparency ndiyo pinnacle ya democracy.
 
Asante majibu mengine huwa yanafariji. mkuu luteni nashukuru

Tatizo tunafanya political discourse iangukie kwenye partisan lines. With sentimentalism kama vile tunaongelea unazi wa mpira. Wakipewa CCM milioni mia moja na wahindi, ufisadi.

Wakipewa CHADEMA, kukua kwa demokrasia. Si sawa hivyo.

Ukweli lazima usemwe, harufu ya ufisadi ni ile ile, iwe CHADEMA au CCM. Kikwete au Mbowe, Makamba au Slaa.

Can you imagine Kikwete na Makamba wangekuwa wanapokea milioni mia moja kutoka kwa muhindi kelele za ufisadi ambazo zingeporomoshwa hapa? Sasa mbona tuna standards tofauti kwa CHADEMA?

Double standards hizi mbaya.
 
Angalau amefungua njia ila TRA wiki hii hii watakuwa mlangoni kwake si unajua TZ!
 
Back
Top Bottom