Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

Sabodo aichangia CHADEMA milioni mia moja

Lets be transparent
SABODO kawa kigugumizi kwa wanachama.
1-Sabodo anasaidia watu wengi sana bila kubagua rangi na itikadi zao.
2-amechangia chama cha upinzani makelele angechangia chama tawala makelele binadamu hatuna shukrani.
3-nani aijuaye biashara ya huyu jamaa ameshaitwa mfisadi kesho nawe ukisha tajirika mfisadi na hatma hata Mengi ataitwa mfisadi.(kwa ujumla wafanya biashara na matajiri wote bila kujali rangi zao ni mafisadi )
4-Tumeona mawaziri mafisadi je !?
 
Ni muhimu sana, sasa hivi bila kuwa na upizani wenye nguvu tusahau maendeleo
 
Mzee Sabodo anijiita retired debt and hedge fund specialist. Ndiye aliyefadhili ile bahati nasibu ya CCM kupitia Mwalimu Nyerere Foundation. Yeye ni muwazi na haogopi kuitupia madongo serikali, CCM au hata mtoto wake wa kumzaa kupitia full page za magazeti ! Huyo ndio Sabodo kwa wasiomjua!
 
Usishangae tukiambiwa kesho kuwa Sabodo si raia!,Hiyo ndo serikali yetu1
 
Basi nanyi Chadema msianze ugomvi kwa sababu tu ya hiyo 100m!
 
Mengi yayolisemwa kuhusu sheria za kuchangia kampeini za uchaguzi yana ukweli. Ila kwa sasa tunahitaji kuchangia vyama vya siasa, tena vile vya upinzani visivyo na dola walu uwezo wa kuiba toka hazina ili viweze kujiendesha, kujiimarisha na kushiriki uchaguzi. Je, tunafayanya hivyo? Nadhani watanzania kama hatatuona huo umuhimu basi tunakosa uhalali wa kumlaumu mtu yeyote atakayechangia vyama vyetu iwe kwa siri au hadharani.
 
Asante sana Mustapha Sabodo kwa kuonesha mfano wa kuigwa kwa wote wenye mapenzi mema na nchi yetu. Hakika tunakushukuru kwa hilo na kuwaomba watanzania waendelee kuchangia harakati hizi kwa kadri ya uwezo wao.
DSC09396.JPG
 
Naona watu wameanza kupanick hapa na bado! Kwa mtizamo wangu ukiona fisadi anasupport chama chenye nia ya kutokomeza ufisadi basi ujue amechoka na ufisadi. Watu wengi wanafanya ufisadi sio kwa kupenda bali ni njisi ya limfumo hili la CCM lilivyolea watu. Na nilazime tuwape watu nafasi za kutubu. Huyu mzee simjui vizuri lakini Mungu ambariki sana. Hii 100M inaweza kuwa ni wabunge kumi.

Subirini Jamani
 
Mengi yayolisemwa kuhusu sheria za kuchangia kampeini za uchaguzi yana ukweli. Ila kwa sasa tunahitaji kuchangia vyama vya siasa, tena vile vya upinzani visivyo na dola walu uwezo wa kuiba toka hazina ili viweze kujiendesha, kujiimarisha na kushiriki uchaguzi. Je, tunafayanya hivyo? Nadhani watanzania kama hatatuona huo umuhimu basi tunakosa uhalali wa kumlaumu mtu yeyote atakayechangia vyama vyetu iwe kwa siri au hadharani.

Na iwe hivyo!
 
Unamaanisha nini? Kwamba kuna chembe ya ufisadi? Kuwa wazi mkuu!
 
Sikuwahi kumsikia Sabodo yupo kwenye kundi la mafisadi. Halafu ikumbukwe kwamba huu ni mchango tu sawa na nyie CCM mnavyochangisha kwa sms tena kwa watu masikini ambao baada ya kuingia madarakani mtawatia umaskini zaidi ili muendelee kupata kura zao.
 
Namsifu huyo mzee kwa kuonyesha ujasiri
 
sabodo.jpg
Kweli Vangi, mie pia sikuwahi kumsikia Sabodo katika kundi la Mafisadi sasa kama Maralia Sugu anadata za mahusiano ya Sabodo na R. A kiasi cha msaada alioutoa auite ni msaada wa R. A.Group atuletee hapa ili tuchambue.
 
nilisikia watu kama wale wenye asili ya huko, wakitoa mchango huhitaji kitu hapo. sasa sijui nao huwakumbatia

Wachangiaji wakubwa wa CCM ni watu wenye asili hiyo, akina abood, shabiby, RA, Manji nk nk. Kwa hiyo unataka kutuambia kila baada ya kupokea michango yao CCM huwa na yenyewe inatoa kitu kikubwa zaidi kwa hawa wote? Kumbee!!
 
Ni upepo unaanza kuonekana kuwa unavuma katika mawimbi ya mabadiliko, leo Sabodo ameaza kufungua njia kwa Watanzania tena wanaCCM kuwa hata wao wanaweza kuchangia vyma vya upinzani, hii imenivutia sana na kuonyesha njia ya kuelekea Demokrasia ya kweli.
 
Hebu wapenzi tutajieni makampuni anayo miliki huyu SABODA kwanza kabla ya kuendelea kumjadili kama ni fisadi au la.

hilo la vyama kupokea michango mikubwa kutoka kwa watu binafsi/makampuni linatakiwa kutungiwa sheria haraka. Huyu katoa Milioni 100, akija mwengine akitoa milioni 300 nae sawa?

isitoshe vyama vinapokea pesa bila ya kutaka kujua kama pesa ni halali au imepatikana kwa njia za mkato.....tusifurahie kwa kuwa wamepewa Chadema au kwa kuwa Chadema kuna Slaa hawawezi kufanya makosa.

Slaa anaweza badilika au kufa vile vile .............
 
Hakika amekuwa mfano wa pekee kwa wapenda demokrasia na mageuzi nchini maana wengi hawakuamini hapo jana walipoangalia kupitia luninga.Kwa waafidhina wa C.C.M ni pigo kwao maana kwa muda mrefu wamekuwa wakikejeli wapinzani kana kwamba ni maadui.Hivyo wajiandae kwa kampeni kabambe wakiwa tayari kujibu ahadi walizozitekeleza kwa wananchi pasipo kutumia ghiliba maana kwa njia hiyo itawagharimu.Kila la kheri CHADEMA
 
Back
Top Bottom