Sabaya asema alimiliki silaha kwa sababu alikuwa anatishiwa kuuawa

Hii case naona Sabaya anaenda kufungwa, Kwanza maelezo yake yake yanajichanganya, mwanzo alisema alienda kwenye duka la shahadia store akiwa kwenye oparesheni maalum ambayo alitumwa na mamlaka za juu, huku kwenye utetezi anakana kuwa hapajui huko
Atafungwa kwa kuangalia ushahidi wa jamuhuri kama umenyooka na sio yy kubabaika kujibu maswali. Samahani nauliza tena hiyo kwenye avatar ni pic yako og?
 
Lengai Ole Sabaya ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha amefunga utetezi wake leo baada ya mawakili wa jamhuri kumaliza kumhoji huku akiieleza mahakama kuwa anamiliki silaha aina ya Glock-17 kwa ajili ya kujilinda kutokana na kutishiwa kuuawa.


Akihojiwa na wakili wa Serikali mkuu, Tumaini Kweka mbele ya hakimu mkazi mwandamizi, Odira Amworo wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha,Sabaya ambaye alikuwa mkuu wa wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro, amesema silaha hiyo alianza kuimiliki Machi 24, 2021.


Hata hivyo Sabaya kabla ya kutaja aina ya silaha anayomiliki aligoma akidai hawezi kueleza aina ya silaha anayomiliki mahakamani,ndipo wakili wake Mosses Mahuna alipoingilia Kati na kumwamuru aitaje.



Sehemu ya mahojiano hayo alikuwa hivi;


Wakili: Tusaidie katika ushahidi wako wa msingi umeieleza mahakama unamiliki silaha


Sabaya: ni sahihi


Wakili: Unamiliki silaha ya aina gani


Sabaya: Hakimu kwa sababu ni kifaa cha moto sijui kitatumikaje nikieleza kilivyo.


Wakili: Nataka kujua ni silaha




Sabaya: Kwa usalama wa silaha hiyo na kwa sababu nipo gerezani naomba nisieleze silaha gani. Ni silaha ndogo inaitwa Glock 17


Wakili:Utakubaliana na mimi kwa Kiswahili inaitwa bastola




Sabaya: Hapana




Wakili: Ulikua unaimiliki kwa shughuli gani




Sabaya: matumizi ya ulinzi binafsi




Wakili: Unapokuwa wapi




Sabaya: Ninapokuwa Wilaya ya Hai Mkoa wa Kilimanjaro




Wakili: Hai ulikuwa una maadui




Sabaya: Ndiyo mheshimiwa hakimu




Wakili: Ulianza kumiliki lini?




Sabaya: Nilianza kuimiliki Machi 24, 2021


Soma zaidi:Ole Sabaya asomewa maelezo upya, akana




Wakili: Kwenye ushahidi wako wa msingi siku ukiondoka kuja Arusha Februari 9, 2021 uliacha silaha yako nyumbani Bomang'ombe.Ni sahihi siku ile ulikuwa ukimiliki silaha?




Sabaya: Sikuwahi kumiliki silaha ya moto kwa wakati huo nilikuwa na silaha ila haikuwa silaha ya moto




Wakili: Una watoto wangapi




Sabaya:Kwa sababu nimeshasema familia iko kwenye risk. Naomba nisitaje watoto wala idadi




Wakili: Lengai nikurudishe kwenye swali dogo wakati unatoka Hai saa 9 kuja Arusha na hiyo timu yako ulipita wapi




Sabaya: Nilipitia Kia barabara ya Mirerani nikaja Arusha




Wakili: Kwanini ulipita huko usipite barabara ya kawaida Moshi -Arusha




Sabaya: Napitia barabara yoyote kwa usalama wangu kwa sababu natishiwa kuuawa




Wakili: Kwanini ulikuwa unatishiwa kuuawa na wewe ni kiongozi wa watu


Soma zaidi:Sabaya amkana mshirika wake katika kesi




Sabaya: Kwa sababu ya aina ya majukumu niliyokuwa nafanya siasa za Arusha na Hai




Wakili: Umefika Arusha mlipokuwa mnaenea na timu yako alimkuta shahidi wa nne Hajirin Saad Hajirin, ulimuona?




Sabaya: Ndio nilimuoma hapa mahakamani




Wakili: Wewe unafahamaniana naye




Sabaya: Hapana




Wakili: Una ugomvi naye




Sabaya: Kama simfahamu siyo rafiki wala adui




Wakili: Na yule shahidi wa pili kutoa ushahidi wake akasema alikuona Shahidi Store (dukani) una ugomvi naye au unamfahamu?



Sabaya: Simfahamu na hapo Shahidi Store sipafahamu


Sabaya amefunga utetezi wake Leo baada ya kukamilika mahojiano ya upande wa serikali na baadaye upande wa utetezi ,mshtakiwa wa pili Silvester Nyegu anafuatia Kwa ajili ya kujitetea.


Katika shauri hilo la jinai nambari 105/2021 Sabaya anashtakiwa na wenzake wawili Daniel Mbura na Nyegu Kwa makosa matatu likiwemo la unyang'anyi wa kutumia silaha .


Ends...








View attachment 1898082
KESI YA MBOWE NA YA SAYABA NI ZA KISIASA TUTAWAACHIA HURU WOTE SIKU CHACHE ZIJAZO 😂😂😂😂😂😂😂
 
Sabaya anahitaji usaidizi wa kisaikolojia... Amechanganyikiwa

Sent from my Infinix X627 using JamiiForums mobile app
Ni lazima achanganyikiwe. Kuporomoka kutoka u-General Sabaya mwenye kila aina ya mamlaka, pesa na heshima mpaka kuwa mahabusu asiye na uhuru wowote ni lazima zifyatuke. Ila huyu jamaa alikuwa mafia mbaya sana. Hata ukiangalia sura yake tu anaonyesha ni wale watu wenye viburi vya hali ya juu.
 
Hii case naona Sabaya anaenda kufungwa, Kwanza maelezo yake yake yanajichanganya, mwanzo alisema alienda kwenye duka la shahadia store akiwa kwenye oparesheni maalum ambayo alitumwa na mamlaka za juu, huku kwenye utetezi anakana kuwa hapajui huko
The art of questioning is lacking among gov prosecutors
 
Kujua mwenendo wa kesi sasa hivi kwa kusoma kwenye mtandao, source ikiwa haya ma-TV online na mablogu ya kibongo huwezi kujua lolote. Hakuna maripota wenye uwezo wa kuripoti kesi. Kwa wale tuliokuwepo wakati wa kesi ya uhaini enzi za kina Mucadam, Murtaza Lakha etc watakubaliana na mimi. Hawa maripota wa hii kesi ya Sabaya ni vihiyo kabisa. Sijui kama kuna gazeti lenye waandishi wanaojielewa linaloripoti hii kesi. eg Raia Mwema

Kama Sabaya kasema Yes or No unaitaji reporter akutafsirie? Eliminate bure mbaya sana
 
Sabaya anakiri kumiliki silaha, na anasema ameanza kuimiliki kuanzia mwezi March, ushahidi uliotolewa dhidi yake ulidai siku anaenda dukani kwa muhindi akiwa na silaha ilikuwa mwezi wa pili.

Hapo jamaa amejaribu kukwepa umiliki wa silaha wakati akivamia dukani, lakini amekiri kutumia silaha nyingine kabla isiyo ya moto ambayo hajaitaja, sijui kwanini hakuulizwa alimiki silaha gani kabla?

Jamaa anakiri alikuwa na maadui, hawajamuuliza kama aliwahi kuripoti polisi, na hao maadui alikuwa nao kuanzia lini? na ni wakina nani? na ni ipi sababu ya kuwa na uadui nao?
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi ya Wilaya ana access na bunduki/ bastola au hana?
 
Kama Sabaya kasema Yes or No unaitaji reporter akutafsirie? Eliminate bure mbaya sana
Hujui unachoandika. Na pengine wewe ni mmoja wa hawa maripota uchwara. Unadhani kuripoti kesi ni kunakili kila anachosema mshtakiwa tu? Haya mambo yamekuzidi kimo hivyo huwezi kujua.
 
Kivipi hapo. Naomba unipe mwanga
Sioni ushahidi wa kutumia siraha kama utathibitika dhidi yake......
haupo.....
nikionacho hapa ni matumizi mabaya ya ofisi ya dc ......sidhani kama hilo kosa jamuhuri walimshtaki nalo
 
Back
Top Bottom