Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Anza kuaanda mbingu yako mkuu ...ushakua mtu mzima na ufahamu wa kutosha jitegemee sasa.
 
kuna point huwa inanichanganyaga sana mpaka leo sijapata jibu linaloeleweka...!
mungu anajua kuzaliwa kwangu maisha yangu mpaka jinsi nitakavyokufa... na pia kwa uweza wake anajua kama nitakuwa motoni au peponi.. hapa bado sijaelewa inamaana tangu nazaliwa alishanipangia niende wapi...!!!!
nisaidieni wakuu hapo...!
 
2... Mungu yu muwazi kwa watu wake, anakupa ukweli wake na anakuonyesha njia ya dhambi ambayo ukiifata utaangamia...anafanya hayo kila leo kwa watu wote, hivyo adamu alionyeshwa njia zote maana Mungu alijua yupo huyo malaika wake aliyemuasi anaweza kumpotosha adamu, hivyo sio kuwa Mungu aliruhusu adamu ajaribiwe hapana ila ndo hali halisi ibilisi angemshwish tu adamu hivyo Mungu alikuwa muwazi kabisa so ni ujinga wa adamu....kwa wale wakristu twajua hata Yesu alijaribiwa tena akaonyeshwa fahari zote za ulimwengu kuwa kama ukiniabudu mimi(shetani) hivi vyote vitakuwa mali zako....je wanadamu wangapi wa leo wanautafuta utajiri kwa njia za kishetani, hapo napo Mungu tumlaumu! Yeye hajatuficha hata kimoja, ni uamuzi wako wewe na tamaa zako kufata ya shetani.
 
Una mawazo yasiyo na majibu yaliyozidi uwezo wa ubongo wako. Hali hii itakupelekea kuwa kichaa.

Sasa rafiki fanya hivi kabla ubongo wako haujafyatuka fyuzi. Kama una pesa, andaa safari (ni vema ukawa na mtu mnayependana/kuelewana) nenda mahali pazuriiii fanya utalii pumzika, kula na kunywa vizuri, jichanganye usiwaze kabisaaaa futa maswali kichwani mwako. Tafuta mwalimu mwenye uelewa uanze kusoma/kujifunza vitabu kuhusu maswali yako. Kama huna pesa ..... lala muda mwingi na achana kabisa na mawazo uliyonayo. Jione unastahili kuishi upendavyo, fanya kazi kwa bidiii kutafuta chakula na mahitaji yako. Maisha lazima yaendelee bila kujali unakubali uwepo wa Mungu au la.
 
3... Tunamtumikia Mungu kwasababu twatakiwa tumjue, tumpe utukufu wake kwa makuu yake, tumtumikie kwa kufanya kazi yake iendelee na mwisho wa siku zetu tupate kurudisha roho zetu mbinguni ktk furaha ya milele na ufalme aliotuandalia, hivyo twamtumikia Mungu ili atufanye tuwe imara mbele ya majaribu tusije tukashindwa tukapoteza roho zetu, watu wote wanaogopa jehanamu ila kukwepa majaribu ya kukupeleka jehanamu ni ngumu maana yanakuja ktk njia nzuri ya kutamanisha na pasipo Mungu huwezi shinda majaribu maana shetani anajua udhaifu wetu na anajua pa kutushinda ni wapi.
 
4.... Hivi nikuulize swali, serikali za nchi zinaweka jela na vifungo na adhabu zake kwa ajili ya wahalifu, je wewe kama raia mwema ukitenda dhambi si nawe utahesabika kama muhalifu na utaadhibiwa pamoja na majambazi na vibaka na wauaji.... Kutuchoma moto si mpango wetu kwake ila ni kwa shetani na malaika zake, ila we binadamu ukitenda maovu ukawa sawa na hao malaika wa ibilisi hapo hamna budi lazima nawe utachomwa moto.......
 
6.....wewe kuja hapa duniani ni zawadi mkuu, wewe ukishinda vita hivi hatimaye ukaingia ktk ufalme wake unakuwa mkuu kuliko hata hao malaika maana wao malaika hawana vishawish wala mazingira ya mitihani kama tuikutayo huku duniani, siku ukiwa mshindi utajua na utaona utakavyopata pumziko zuri, labda nikupe mfano, waangali wanafunzi ktk hatua yoyote hasahasa primary na secondary level, wao huteseka sana kipindi cha masomo, huadhibiwa hupata misukosuko ila siku matokeo ya mtihani wa taifa yametoka na kwa waliofaulu hutukuzwa, huthaminiwa, hurinnga na kudeka mbele ya wazazi/walezi wao, husikilizwa hupikiwa chakula wanachotaka na hufanyiwa tafrija na nduguzo au hata na serikali na hupewa zawadi nyingi... Ila hamna ajuaye mateso aliyopata hadi kufika hapo, ila wangekata tamaa na kusema kwann waliletwa shule na kuamua kuacha masomo leo hii wangekuwa wavuta bangi au maskini wa kutupwa..... Hivyo wewe usiyejielewa kaa chini tafakari umuhimu wako kwa Mungu na tambua madhumuni yake ya kukuumba wewe, jua kwann Mungu katuleta hapa duniani, usijaze ujinga huo akilini mwako, nyi ndo mnaishia kujinyonga tu. Tafuta viongizi wa dini wakusaidie kukuelimisha umuhimu wako hapa duniani na wakwamvie yuke aliyekuweka hapa anategemea yapi toka kwako
 
Mungu hayupo so point zako ni invalid.

Kama yupo basi anavyosema ni mwenye rehema na upendo kuliko binadamu yeyote anatudanganya maana angekua nao dunia isingekua kwenye mess hii.

Ana paradox nyingi mno kiasi kwamba his own existence can't be possible in anyway. Anasema anajua yote yatakayokuja na yaliyokuwepo,hehe meaning story ya adam n eve ka ni kweli then anamlaumu eve bure tu maana yeye alijua wazi watakachokifanya na bado akaweka mti pale, kosa ni la kwake 100% ni sawa na mzazi kujua mtoto ukimpa wembe atajikata alafu unampa then anajikata unamtupia lawama na kumuongezea adhabu juu.

Siku nilipoachana na fix za dini akili ilifunguka, kuishi kwa uoga uoga tena hakuna, mtoto ukimjaza kitu utotoni anakishika kama kilivyo, acheni watoto wenu wakue then wachague, hamtobaki na mtu anayeamimi haya maduduwasha
Mungu yupo.Na njia pekee Ni kuamini.Unapoanza kutumia akili yako kung'amua kila kitu it turns to be a paranoid.Because we just can't explain God.Its beyond human intelligence.

Hatuwezi tukazungumzia intelligence iliyotuumba,hatuwezi tukamjadili Mungu Kama specimen.Mungu aliyeumba the universe.Universe Ina Kama galaxies trillion mbili! ambazo technology ya mwanadamu inaweza ikaona,ziko zaidi.Na galaxy yetu Ina mpaka nyota billion 400 na zaidi labda,na Kama sayari billion 100.Galaxy yetu Ina mpaka solar systems 500 na zaidi zinagundulika.

Sisi binadamu kwenye solar system yetu yenye sayari nane na satellites au miezi Kama 150 hivi na nyota moja(jua)…tunathubutu kusema Mungu hayupo?
 
Wala usichukizwe na vitu vya kukalilishwa.
1.Ulimuona wapi huyo Mungu? Kama kweli yupo,kwa nini wapo wasiomuamini,hasa hizi nchi zilizoendelea?
2.Utaambiwa kwamba injiri ina miaka si zaidi ya 107 sasa.Hii itakupa picha kamili ya kwamba ni mbinu za wazungu kuwarubuni waafrica.
Mwanasiasa moja alisema huko Kenya kwamba waliwaletea biblia,wakawambia wafumbe macho,walipofumbuwa walijikuta wamebaki na zile biblia wale nao wamechukua ardhi zao.
Unayoyapitia,hata wanyama wanapitia,kila unachokiona kinapitia,huwenda ndo mfumo wa uhai wa kila kilichopo.
3.Leo unaambiwa mtu mwenye umri mkubwa duniani hana zaidi ya miaka 130,000. Huyu ukimpata hakujua kusoma wala kuandika.
Sasa swala linakuja je,miaka 2017 wanaihesabu toka kuzaliwa kwa Yesu,waislam,leo hii nadhani wapo kwenye 14.. je,hujiulizi kwa nini hizi hesabu haziendi sawa? Wanakuja watu wanaitwa wanasayansi,watakwambia kuna jamii ya wanyama wamewahi kuwepo miaka zaidi ya milioni 3,na leo mafuvu yao yapo.Je,unakubaliana na hili?

4.Mfano hai mwingine,wanasayansi wanadai (na inavoonekana)hakuna siri duniani kupitia mifumo waliyotengeneza,hata kitu cha ukubwa wa sindano kitapatikana tu.Ndege ya Malaysia na abilia wake wake wapi? Hawa wote walimkosea Mungu huyo na kuamua kuwafanyia unyama?
5.Nasikiaga habari ya majini,uchawi na vitu kama hivyo,nagalia vifo vya kila kukicha, mfano wa wanyarwanda na wayahudi,walioteketezwa na wenzao tena makusudi,Mungu kwa nini aliwaacha waangamie,ukizingatia walikuwemo watoto wadogo ambao hawana kosa mbele yake?!
Hivyo basi,Mungu kama kweli yupo,mafundisho tuyapatayo ni kwamba kutambua uwepo wake ni katika kujali viumbe wake.Leo hii kina Trump na wengine,si wanaapia kwenye Biblia na Quran? Si wanaenda makanisani na misikitini?
Yeye kafanya nini Syria hivi karibuni?
Angalia vikundi vya kigaidi,mbona wanaua hata waislam wenzao? Mbona wanajiunga na wakristo?
Ni mengi sana ya kusemwa, ila kifupi tu wewe,jaribu kuwa mwema kadri uwezavyo,na mfumo huo huo ndo ulelee wanao na uwasihi wawalelee wajukuu zako,kila mtu angefanya hivo amani ingekuwepo,na ukiweza hilo kama kweli Mungu yupo hutakuwa na hatia.
Sasa kama hayupo,kama wanavyosema wengine,mpe mwenzio sawa na kile uachohitaji wewe.
Mtu mwenye utu ana akili,lakini akili zake huchezewa na wenye ujuzi.

Haya unayojiuliza wewe angalia watu wanaokaa vijiji ambavyo ni vya pekee,mambo ya maendeleo hawayajui wakiona gari wanakimbia,ukiwauliza uwepo wa Mungu utapata jibu na hayo majuto yako utaona kwa nini unayo.
Hivyo basi,kwanza kanisa lako au msikiti wako,acha viwe matendo yako.

Sijaema kuwa Mungu yupo au hayupo,kila mtu na imani yake,hayo ni mawazo yangu tu.
 
Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way He is and we have to live with it.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mm nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa ntakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo. So im just keeping it real.
Wewe umezidisha kufuru ndio maana unajiona hauko free kufanya madhambi makubwa kuliko ulio kua nayo .
Allah kisha weka mipaka yake sasa wewe ni kazi kwako TO CUT OR TO SHAVE .

Halafu wewe umekua nani mpaka usimpende MUNGU .
Allah kasema atakae chukia kukutana mimi basi mimi ALLAH sipendi kukutana nae .

Fanya FASTER utubu kwani umesha kufuru sana hauoni hata uzito kutuma UZI kama huu .

Halafu umesha jijibu :

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui.
 
Mungu yupo.Na njia pekee Ni kuamini.Unapoanza kutumia akili yako kung'amua kila kitu it turns to be a paranoid.Because we just can't explain God.Its beyond human intelligence.

Hatuwezi tukazungumzia intelligence iliyotuumba,hatuwezi tukamjadili Mungu Kama specimen.Mungu aliyeumba the universe.Universe Ina Kama galaxies trillion mbili! ambazo technology ya mwanadamu inaweza ikaona,ziko zaidi.Na galaxy yetu Ina mpaka nyota billion 400 na zaidi labda,na Kama sayari billion 100.Galaxy yetu Ina mpaka solar systems 500 na zaidi zinagundulika.

Sisi binadamu kwenye solar system yetu yenye sayari nane na satellites au miezi Kama 150 hivi na nyota moja(jua)…tunathubutu kusema Mungu hayupo?

Ebu tupe vigezo vyako vya unachokiamini hapa.
Je,ina maana wanaoamini kuwa Mungu hayupo ni wajinga?
Hiyo sayari unayoisema na vilivyomo,umevitoa wapi? Si ni vitabu tu umesoma?
Je,sijui umezaliwa lini lakini,wakati unazaliwa,idadi ya madhehebu yaliyopo leo nibtofauti na yaliyokuwepo kipindi hicho,je hawa wanaofanya hivi wamegundua Mungu unayemsema siyo bado wanamsaka wa kweli?
Kosa kubwa tunalolifanya binadamu ni kutaka kukalilisha watu yale tunayoyafikilia.
Mungu gani anayependa upuuzi unaofanywa na hawa wazungu? Mtu anahofia bomu linaloweza kufukia nchi nzima au kuua kila kilicho hai sehemu fulani,huyo Mungu wako basi gaidi,kama hawezi kuokoa aliowaumba.

Sasa basi,wewe tenda mema,ili kama kweli yupo,athamini wema wako,na kama hayupo,wema wako uthaminiwe na watu wenzako.
Kudhibitisha uwepo wake huna vigezo, na kudhibitisha kutokuwepo kwake,vigezo pia huna.
 
Hivi,wasomi ni wengi tu.
Masista wangapi na mapadri waliofundishwa miaka nenda miaka rudi,wameshika imani kweli,af badae,wanageuka na kusalimu amri,wanaoa na kuolewa,ina maana yule Mungu waliyemfata miaka yote kawakimbia?
 
Hata ukimchukia ataacha kukupenda daima ndo maana upo hai hata sasa kwa pumzi ya bure usiyolipia hata sent.Amekujali uwezo wa kumiliki smart phone jiulize wangapi duniani hawana
 
Mpende sana shetani wala usimwache, yeye hana double standard, ni mzuri na ana upendo wa dhati kwa watu wake
Ndo maana tunaishi kama yeye heri ya jana mbele Moto nyuma Moto sukari 3000 unga 2500 hela hakuna kazi hakuna biashara hazitoki
 
Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way He is and we have to live with it.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mm nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa ntakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo. So im just keeping it real.
Pole sana, ila pia bidii hiyo hiyo ya chuki kwa Mungu ungewekeza katika kumpenda ingewezekana pia. Ila kwa kuwa ume-comply na pando la adui niseme tu kuwa Yesu Kristo akutokee kipekee sana ili "UUONE MKONO WA BWANA KATIKA NCHI YAO WALIOHAI" na dhambi inayokutaabisha ilishindwa msalabani, ni wewe tu kuamua kuambatana na huyo aliyeishinda dhambi au kuendelea na huyo anayepanda dhambi.
 
Kama unamchukia Mungu sababu ya jehanum take from me jehanum hakuna iliingizwa kimakosa kwenye biblia kwa rengo LA kuonya watu sasa hawa evangelist wamechukulia kama kitu halisi. So love your God he is there might and good.
 
Back
Top Bottom