mkuu hivi tofauti ya shetani wa wakristo na waislamu ni ipi au utawatofautisha vipi maana kila dini inataratibu zake kwann shetani awe yuleyule1....jehanamu iliumbwa kwa ajili ya ibilisi na malaika wake, ila wewe binadamu unapofanya matendo ya ibilisi yaani kuungana na ibilisi nawe unakuwa sehemu yake ibilisi....kumbuka hao malaika hata huyo ibilisi mwenyewe walikuwa malaika wa Mungu
Unaweza ukaongea au kuelezaje pale Musa alipomtokea YESU walipopanda mlimani na wanafunzi wake!? Musa na Elia,,muelezee zaidi Musa maana alikufa na MUNGU akamzika?Je YESU alikuwa na maana gani kumwambia yule mwizi pale msalabani kwamba leo nitakuwa na wewe mbinguni??? Je YESU atakaporudi mara ya pili na wafu kutoka makaburini na kupaa nae watakuwa ni wafu wapi hao?? Ile habari ya YESU kuelezea maskini na tajiri kufa na maskini kwenda kwa Ibrahim na tajiri kwenda penye shida unaielewaje??? Au ni fiction????
Mkuu Synthesizer Unaposema YESU alipaa mbinguni baada ya Siku 40 una maanisha ahadi aliompa yule mwizi ilikuwa ya uwongo?? Nilichotaka uone ni kwamba yule mwizi pale msalabani walimuua pia na akazikwa lakini YESU aliondoka nae na hakuondoka na mwili wake,,,Kuna andiko linasema Je! Hamjui miili yenu ni hekalu la Roho mtakatifu?!# MIILI yenu/+/=# kuna wewe na mwili wako??? Mwili wako(wewe)
Inaonekana uko stressed muda huu (point yako ya sita) as if kuna jambo baya umefanya,linakuumiza,unalijutia
Kama iko hivyo kweli ni heri ukatubu kwa imani yako na kuamini sisi binadamu hakuna mkamilifu,wote tunamkosea Mungu
Kwa imani yangu nafahamu Mungu ni pendo na huwa hakusudii baya lolote litutokee
Sasa kama humpendi yeye manake hata ndani yako hakuna upendo
USHAURI
Usipende kumuongelea Mungu kiboya boya kama unawongelea wachumba zako huko
Hayo maswali # 1,2&3 nimeshindwa kuyajibu kwasababu sipo into dini kabisa
Mkuu nimekuwa nikizitafakari hizo sababu zinazosemwa kuwa ndiyo zinazofanya watu waamini mungu ambazo nawe umezitaja hapo,nachokiona ni kama hazina uhalisia.wewe Mungu unamjua? na kum uongelea kiboya boya ndio kufanyaje? mungu analipi hasa la maana ambalo wewe unaweza sema unajivunia? uoga wako wa kuogopa moto, na akili yako mgando ya kushindwa kupata majibu ya mambo usio yajua ndio yamekufanya ujitengenezee majibu ya mungu wako na uendelee kujifariji na habari zenu za kizushi kuhusu Mungu....... mtoa mada upo sahihi sana mkuu nakuunga mkono asilimia mia.
Mkuu nimekuwa nikizitafakari hizo sababu zinazosemwa kuwa ndiyo zinazofanya watu waamini mungu ambazo nawe umezitaja hapo,nachokiona ni kama hazina uhalisia.
Nasema hivyo kwa sababu laiti watu wangekuwa wanaamini mungu kwa uoga wa moto basi wangeishi vile mungu alivyowaamrisha kuishi(kwa madai ya dini) lakini watu hao wenye kuamini mungu wanaishi maisha ya kinyume kwa maana hiyo huo moto wataupata japokuwa wanaamini mungu,hivyo laiti wangekuwa waoga wa vitisho vya moto basi wangefanya na kuacha yale yote waliyoelezwa kwenye dini zao zinazodai kuwa Kuna mungu.
Lakini pia kusema kuwa watu waamini mungu kwa sababu wamekosa majibu ya mambo wasiyoyajua pia sidhani kama ni sawa,maana ni mambo gani hayo ambayo toka enzi hizo hayajapatiwa majibu hadi leo? maana huwa tunasema kwamba enzi hizo kulikwa na ujinga hivyo mambo mengi watu hawakuwa wakiyajua ila sasa mambo mengi yanajulikana ila bado tu watu waanamini mungu.
Kwahiyo mimi nafikiri kuna sababu zengine za watu kuwa bado wanaendelea kuamini habari za mungu hadi leo na sio hizo.
Kwa kujibu swali lako kiujumla ni kwamba watu wanaamini mungu kwa sababu ni jambo ambalo linaleta maana na kuingia akilini tofauti na kinyume chake kwamba hakuna mungu,hivyo pamoja na hao watu kutofautiana dini na na wengine hawana dini (hivyo hawaani habari za moto) lakini wote kwa pamoja hukubaliana kuamini mungu kwa sababu ni suala lenye kuleta maana na kuingia akilini.zipi?
Mleta mada mwehu Mungu umchukie usimchukie yeye anabaki kuwa MUngu. Hawezi pungua uungu wake sababu kuna mwehu mmoja ambaye aweza kufa kwa kuharisha au kuumwa na mdudu mdogo Kama mbuOk endelea kumchukia