Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

1....jehanamu iliumbwa kwa ajili ya ibilisi na malaika wake, ila wewe binadamu unapofanya matendo ya ibilisi yaani kuungana na ibilisi nawe unakuwa sehemu yake ibilisi....kumbuka hao malaika hata huyo ibilisi mwenyewe walikuwa malaika wa Mungu
mkuu hivi tofauti ya shetani wa wakristo na waislamu ni ipi au utawatofautisha vipi maana kila dini inataratibu zake kwann shetani awe yuleyule
 
Mungu uishiye mahali pa Juu Mbinguni, usifunge rehema zako juu ya hawa watu.
 
Mungu uliyeumba mbingu na nchi, na vyote vinavyoonekana na visivyoonekana. Mungu umesema ktk 2Mambo ya Nyakati 7:14 kuwa Ikiwa watu wako walioitwa kwa Jina lako wakaja kwako kwa kunyenyekea na kuacha njia zao mbaya hakika utasikia kutoka mbinguni nawe utawasamehe'

Hakika Mungu tumefanya makusudi ya kukutukana ww kwa kusema kwanini umetuumba, kwanini umetupa uhai mpaka sasa tunapumia ikiwa wengine wanatamani warudi duniani watengeneze na ww. Mungu, rehema zako zisikome juu yetu.

Hata dunia nzima tukukatae ww ila bado utabaki kuwa Mungu, hakuna cha kukufananisha na ww wala hapana cha kukiweka kukuringanisha na ww, Mungu uliyetuumba uturehemu.

Kwa kuwa tumekuwa na afya njema, pesa, majumba na kila kitu tumekusahau, tumesahau kuwa ww ndie uliyeruhusu tuwe hivi tulivyo leo, Damu yako Yehova itutakase.

^Mungu uturehemu kwa maneno ya vinywa vyetu tunayoyanena^
 
Unaweza ukaongea au kuelezaje pale Musa alipomtokea YESU walipopanda mlimani na wanafunzi wake!? Musa na Elia,,muelezee zaidi Musa maana alikufa na MUNGU akamzika?Je YESU alikuwa na maana gani kumwambia yule mwizi pale msalabani kwamba leo nitakuwa na wewe mbinguni??? Je YESU atakaporudi mara ya pili na wafu kutoka makaburini na kupaa nae watakuwa ni wafu wapi hao?? Ile habari ya YESU kuelezea maskini na tajiri kufa na maskini kwenda kwa Ibrahim na tajiri kwenda penye shida unaielewaje??? Au ni fiction????


Maswali mazuri sana, lakini yote yanahitaji uelewevu mzuri sana wa Biblia, na yana maelezo marefu. Nikipata muda nitakujibu.

Labda ambalo yana maelezo mafupi ni hili ya Yesu kuelezea masikini na tajiri. Kwa kifupi huo pia ulikuwa mfano, sio jambo halisi. Fikiria, ikiwa ni kitu halisi, huko peponi na motoni ni jirani kiasi watu wanaongea na kuwa na mazungumzo?

Na tuje kwa hili la Yesu kumwahidi yule mwizi wangekuwa wote mbinguni "siku hiyo". Lakini kumbuka kwamba Yesu hakwenda mbinguni "siku hiyo". Alipaa kwenda mbinguni siku 40 baadaye. Na sidhani kama utafikiri kuwa Yesu alienda mbinguni siku hiyo, akarudi tena duniani, kisha akapaa kwenda mbinguni baada ya siku 40.

Kwa hiyo kwa ujumla mambo ambayo tunayachukulia kwa haraka haraka katika Biblia na kufanya conlusion huwa yawa hatari ya kutupeleka kwenye wrong conclusions.

Lakini jambo la msingi kuliko yote ni kwamba ukiona kwamba kuna facts mbili katika Biblia zinazoonekana kupingana, usikate shauri kung'ang'ania moja kuwa ndio kweli na nyingine haifai. Hii mifano uliyonipa haifanyi yale niliyokueleza hapo awali kuwa ya uongo. Yote yanatoka katika Biblia hivyo ni jukumu lako kufanya utafiti wa kina ili upate kuelewa undani wake badala ya kuwa unazikubali sehemu fulani za Biblia na nyingine unaona hazina ukweli. Biblia haijipingi hata siku moja, bali wanadamu ndio wasioielewa na kudhani inajipinga. Haiwezi kusema watu wakifa hawajui wajualo sehemu moja na sehemu nyingine ikasema wanaendelea kuwa na fahamu. Ukielewa hivyo tatizo sio Biblia, ni wewe msomaji. Kila andiko katika Biblia lina pumzi ya Mungu.
 
NNACHOAMINI NI KWAMBA KILA ANAYEKANA UWEPO WA MUNGU UPO MDA UKIFIKA ATAKIRI KUWA MUNGU YUPO.

UWE UMEKUFA WAKATI WA HUKUMU AU UPO HAI ILA UKIFIKA MDA KWA KINYWA CHAKO UTAKIRI YUPO MUNGU, NA MAGOTI UTAPIGA KWA HUYO MUNGU UNAYESEMA HAYUPO.

MWANADAMU KUWA MAKINI SANA NA PUMZI NA UHAI ULIONAO.
 
Mkuu Synthesizer Unaposema YESU alipaa mbinguni baada ya Siku 40 una maanisha ahadi aliompa yule mwizi ilikuwa ya uwongo?? Nilichotaka uone ni kwamba yule mwizi pale msalabani walimuua pia na akazikwa lakini YESU aliondoka nae na hakuondoka na mwili wake,,,Kuna andiko linasema Je! Hamjui miili yenu ni hekalu la Roho mtakatifu?!# MIILI yenu/+/=# kuna wewe na mwili wako??? Mwili wako(wewe)
 
Atheists mngetoa uthibitisho wa madai yenu ya kuwa hakuna mungu basi sasa hii mijadala isingekuwepo tena ingekuwa imeshaisha,ila kuendelea tu kukosoa hiki na kile bado haisaidii maana hata wakristo na waislamu huwa wanakosoana,hivyo mnachoendelea kukifanya humu ni kushawishi watu waamini kuwa hakuna mungu na ndiyo maana hamna uthibitisho wa madai yenu.
 
Mkuu Synthesizer Unaposema YESU alipaa mbinguni baada ya Siku 40 una maanisha ahadi aliompa yule mwizi ilikuwa ya uwongo?? Nilichotaka uone ni kwamba yule mwizi pale msalabani walimuua pia na akazikwa lakini YESU aliondoka nae na hakuondoka na mwili wake,,,Kuna andiko linasema Je! Hamjui miili yenu ni hekalu la Roho mtakatifu?!# MIILI yenu/+/=# kuna wewe na mwili wako??? Mwili wako(wewe)

Hapana Mkuu, Yesu hata siku moja hakusema uongo, na wala hakusema uwongo kwa yule mwizi. Na wala hakusema uongo aliposema siku inakuja wale waliomo makaburini (wafu) wataisikia sauti yake na kutoka. Nilichotaka kukuonyesha ni kwamba usomaji wa maandiko bila kuwa makini unaweza kufanya upotoke sana katika kuelewa jambo.

Angalia sentensi mbili hapa chini uniambie ni ipi Yesu alitamka kwa yule mwizi. Angalia sentensi hizi zina maneno sawa kabisa;

1. Amini nakuambia, leo hii utakuwa nami peponi.
2. Amini nakuambia leo hii, utakuwa nami peponi.

Umegundua kitu? Sasa niambie, ni sentensi ipi kati ya hizo mbili Yesu aliitoa kwa yule mwizi?

Ili kuzidisha uthibitisho wa umuhimu wa kusoma na kutafsiri vizuri, maana kutafsiri mara nyingine ndio kinakuwa chanzo cha tatizo, angalia tena sentensi zifuatazo ambazo pia zina maneno sawa;

1. A woman without her man is nothing
2. A woman, without her, man is nothing

Umegundua tena taswira mbili zinazotolewa na hizo sentensi hapo juu?

Basi kwa kusikitisha sana, vitu kama hivi hata vimechngia watu kuzidi kuamini Yesu na yule mwizi siku hiyo walipokufa walienda peponi (paradiso). Na wengine, baada ya kuelewa Yesu alipaa baada ya siku 40, hata wamedhani alitoa ahadi ya uwongo kwa yule mwizi.

Hata hivyo, haimaanishi kwamba Yesu alikwenda mbinguni na yule mwizi baada ya siku 40. Kumbuka Yesu aliahidi "utakuwa nami peponi" kama kitu cha baadaye. Sasa suala la msingi, ni lini yule mwizi alikuja kuwa au atakuwa na Yesu peponi?

Na huwezi kutofautisha mwili na roho katika kupata thawabu ya uzima wa milele au mshahara wa dhambi, kifo. Suala la miili ya damu na nyama linategemea tu makazi yako ni wapi. Ukiwa duniani basi inabidi uwe na mwili wa nyama, na ukiwa na makazi mbinguni utakuwa na mwili wa roho. Angalia Yesu, alikuwa mbinguni akiwa na mwili wa roho, akaja duniani akazaliwa katika mwili wa nyama, akarudi mbinguni akiwa na mwili wa roho. Sasa haina maana katika hizi awamu tatu Yesu alikuwa ni mtu tofauti - alikuwa ni Yesu yule yule, kuonyesha kwamba hii theory ya watu kusema sijui roho inatoka mwili unabaki si ya kweli. Ni mambo mawili - aidha una mwili huu au ule. Sio kwamba inaunganishwa au kutenganishwa. Unakuwa na one form or the other, lakini ni mtu yule yule. Kuna watu walifufuliwa toka mwili wa nyama kurudi mwili wa nyama - mfano Lazaro. Na kuna watu wanafufuliwa toka mwili wa nyama kwenda mwili wa roho - mfano Yesu.

Ila Biblia inasema kwamba Mungu anaweza kukubadilisha kwa kufumba na kufumbua kutoka mwili mmoja kuwa mwingine. Alimdadilisha Yesu toka mwili wa roho kuwa wa nyama kama kiini katika tumbo la Maria. Note kwamba alimbadilisha, hakumuua. Ila katika hali ya kawaida, lazima kifo kitokee ili ubadilike ikiwa unatakiwa ufufuliwe ili ukaishi mbinguni. Ila ikiwa unatakiwa ufufuliwe uishi duniani basi utakufa katika mwili wa nyama na kufufuliwa katika mwili wa nyama - ukiwa na utu wako ule ule. Na kumbuka, whether ni kutoka mwili wa nyama kwenda wa roho au wa nyama tena, katika hali ya kawaida, lazima ufufuo utokee, sio kitendo ambacho ni automatic kwa mtu yeyote anaekufa. Kama wewe sio mtu wa kufufuliwa ukifa ndio basi tena, huendi tena kwenye mwili wa nyama au roho. Ingekuwa kupata mwili wa roho ni automatic mara tu ukifa, basi Yesu asingesubiri siku tatu ili afufuliwe, angekuwa na mwili wa roho mara tu baada ya kufa pale pale alipotundikwa!
 
Kitu Nilichotaka uone ni kwamba mwili ni vazi la roho,,,na Hakuna anaejua ratiba ya YESU baada ya kufa alikuwa anafanya nini,,,ila yeye ndie mfano mzuri sana wa kifo maana baada ya kufa aliendelea kufanya kazi na mwili akiwa kuacha kaburini.Hii ni evidence kwamba kufa kwa mwili sio mwisho wa maisha bado roho itaendelea kuishi.Mwili tu ndio hufa na kuoza.,,,bado nasubiria unijibu kuhusu Musa Synthesizer.
 
Unaeza kujiuliza maswalimengi tuu bila kumchukia Mungu. He is Omniscient, omnipotent, omnipresent, huna haja ya kumshambulia hata. Pia hajakulazimisha Umpende. Chagua hivi leo hii kuwa Neutral. Ukifa hatokuhukumu kwa kuwa Neutral kwani hukumpenda wala kumchukia
 
Inaonekana uko stressed muda huu (point yako ya sita) as if kuna jambo baya umefanya,linakuumiza,unalijutia

Kama iko hivyo kweli ni heri ukatubu kwa imani yako na kuamini sisi binadamu hakuna mkamilifu,wote tunamkosea Mungu

Kwa imani yangu nafahamu Mungu ni pendo na huwa hakusudii baya lolote litutokee
Sasa kama humpendi yeye manake hata ndani yako hakuna upendo

USHAURI
Usipende kumuongelea Mungu kiboya boya kama unawongelea wachumba zako huko

Hayo maswali # 1,2&3 nimeshindwa kuyajibu kwasababu sipo into dini kabisa

wewe Mungu unamjua? na kum uongelea kiboya boya ndio kufanyaje? mungu analipi hasa la maana ambalo wewe unaweza sema unajivunia? uoga wako wa kuogopa moto, na akili yako mgando ya kushindwa kupata majibu ya mambo usio yajua ndio yamekufanya ujitengenezee majibu ya mungu wako na uendelee kujifariji na habari zenu za kizushi kuhusu Mungu....... mtoa mada upo sahihi sana mkuu nakuunga mkono asilimia mia.
 
wewe Mungu unamjua? na kum uongelea kiboya boya ndio kufanyaje? mungu analipi hasa la maana ambalo wewe unaweza sema unajivunia? uoga wako wa kuogopa moto, na akili yako mgando ya kushindwa kupata majibu ya mambo usio yajua ndio yamekufanya ujitengenezee majibu ya mungu wako na uendelee kujifariji na habari zenu za kizushi kuhusu Mungu....... mtoa mada upo sahihi sana mkuu nakuunga mkono asilimia mia.
Mkuu nimekuwa nikizitafakari hizo sababu zinazosemwa kuwa ndiyo zinazofanya watu waamini mungu ambazo nawe umezitaja hapo,nachokiona ni kama hazina uhalisia.

Nasema hivyo kwa sababu laiti watu wangekuwa wanaamini mungu kwa uoga wa moto basi wangeishi vile mungu alivyowaamrisha kuishi(kwa madai ya dini) lakini watu hao wenye kuamini mungu wanaishi maisha ya kinyume kwa maana hiyo huo moto wataupata japokuwa wanaamini mungu,hivyo laiti wangekuwa waoga wa vitisho vya moto basi wangefanya na kuacha yale yote waliyoelezwa kwenye dini zao zinazodai kuwa Kuna mungu.

Lakini pia kusema kuwa watu waamini mungu kwa sababu wamekosa majibu ya mambo wasiyoyajua pia sidhani kama ni sawa,maana ni mambo gani hayo ambayo toka enzi hizo hayajapatiwa majibu hadi leo? maana huwa tunasema kwamba enzi hizo kulikwa na ujinga hivyo mambo mengi watu hawakuwa wakiyajua ila sasa mambo mengi yanajulikana ila bado tu watu waanamini mungu.

Kwahiyo mimi nafikiri kuna sababu zengine za watu kuwa bado wanaendelea kuamini habari za mungu hadi leo na sio hizo.
 
Mkuu nimekuwa nikizitafakari hizo sababu zinazosemwa kuwa ndiyo zinazofanya watu waamini mungu ambazo nawe umezitaja hapo,nachokiona ni kama hazina uhalisia.

Nasema hivyo kwa sababu laiti watu wangekuwa wanaamini mungu kwa uoga wa moto basi wangeishi vile mungu alivyowaamrisha kuishi(kwa madai ya dini) lakini watu hao wenye kuamini mungu wanaishi maisha ya kinyume kwa maana hiyo huo moto wataupata japokuwa wanaamini mungu,hivyo laiti wangekuwa waoga wa vitisho vya moto basi wangefanya na kuacha yale yote waliyoelezwa kwenye dini zao zinazodai kuwa Kuna mungu.

Lakini pia kusema kuwa watu waamini mungu kwa sababu wamekosa majibu ya mambo wasiyoyajua pia sidhani kama ni sawa,maana ni mambo gani hayo ambayo toka enzi hizo hayajapatiwa majibu hadi leo? maana huwa tunasema kwamba enzi hizo kulikwa na ujinga hivyo mambo mengi watu hawakuwa wakiyajua ila sasa mambo mengi yanajulikana ila bado tu watu waanamini mungu.

Kwahiyo mimi nafikiri kuna sababu zengine za watu kuwa bado wanaendelea kuamini habari za mungu hadi leo na sio hizo.

zipi?
 
SIKU UTAKAPO KUTANA NA MTOA ROHO.NDO UTAAMINI MUNGU YUPO.ALAFU UTAKUWA UMESHACHELEWA.MAANA KUTOKUAMINI KWAKO MUNGU HAKUTAKUSAIDIA MBELE YA SAFARI MAANA UTAKUTANA NAE TU.HUNA PA KUKIMBILIA.
 
Mtoa Mada
Nijibu

Huyo Mungu unaye mchukia ni Mungu yupi (gani) ?
Maana umeandika kiujumla tu.
Ungetutajia jina la huyo Mungu aliye kuudhi.
Anaitwa nani ?
Maana kuna miungu wengi sana.
Na kuikweli hawahesabiki ni wengi mno.
Wengine wana Mungu Ng'ombe, Sanamu, Mwezi, Jua,
Mke, nk.
Ili tujue ni Mungu yupi unayemtaja ilibidi ututajie JINA lake.
Inawezekana ni kweli huyo mungu wako ana mambo ya kuudhi.
Au huyo unayemwelezea inawezekana hakuumba Mbingu na Nchi, na anajisifia tu kuwa kafanya hivyo na kimbe siye.
Na inawezekana huyo mungu wako anawachukia watu na kuwatendea mabaya.
Tafadhali kabla sijaendelea kusema naomba utueleza bayana.
HUYO MUNGU UNAYE MCHUKIA ANAITWA NANI ?


Pia tueleze
 
Kwa kujibu swali lako kiujumla ni kwamba watu wanaamini mungu kwa sababu ni jambo ambalo linaleta maana na kuingia akilini tofauti na kinyume chake kwamba hakuna mungu,hivyo pamoja na hao watu kutofautiana dini na na wengine hawana dini (hivyo hawaani habari za moto) lakini wote kwa pamoja hukubaliana kuamini mungu kwa sababu ni suala lenye kuleta maana na kuingia akilini.

Utaona kumbe hata wenye kuamini mungu nao wanatofauti zao,sasa tatizo ya mabishano haya ni watu kutumia hizo tofauti kutaka kuondoa hilo wazo uwepo la uwepo wa mungu.
 
Hivi kabla ya wamisionary na waarabu,africa ilikua inaijua biblia au quran?na hasa walikua wanamjua Muumba?
 
Back
Top Bottom