Sababu za kufeli kwa zoezi sensa

Udini uliochochewa na unaoendelea kuchochewa na baadhi ya Wanasiasa kwa faida yao wenyewe..Hili CCM hatutalikwepa maana tumekuwa tukifikiria ni mtaji kumbe ni janga la taifa kipindi kifupi kijacho!!!
kwa jinsi zoezi linavyoendelea , napata shak kama takwimu kwenye madodoso zintakuwa sahihi.Pia takwimu ya idadi ya watanzania na shaka kama itakuwa sahihi.
 
Walimu wengi hawakuchukuliwa kwenye sensa, wengi ni form 4 na 6 leavers, wengi wao walikuwa na shida na hizo posho tu sio kazi, baada ya posho ya semina wengi wameingia mitini, waliobaki kati ya nyumba 10 wanakwenda 3, zilizobaki wana pika data. Hivyo tatizo kubwa ni kutohesabiwa kwa watu wengi waliotayari kuhesabiwa na sio mgomo wa waislamu.

Tehe Tehe Hata Mimi sijahesabiwa ila Mkuu wa mkoa wangu alisema tusipo hesabiwa tutakadiriwa tuu kuwa 47-50 million sababu watz tunazaa Saba ikilinganishwa na estenent ya mwazo 45m people mpaka raha
 
Zoezi la sensa limefanikiwa kwa asilimia 90%. (taarifa ya jana)
Hakuna madaktari waliogoma kazi zinaendela vizuri, (taarifa za nyumba)
Walimu wanaendelea na kazi vizuri tu, (Taarifa za nyuma)
Mgomo wa madaktari haukusababisha maafa yoyote hali iliongezeka kuwa nzuri wakati wa mgomo, mochwari zilikuwa na maiti chache kuliko wakati madaktari walipokuwa pale hii ni ishara vifo vilipungua (ilitoka bungeni)

tusipokuwa seriuos jamaa wanatulostisha
 
Limefeli? Ni Maoni yako binafsi ama umeamua kutumia Bundle na time yako vibaya...kweli niamini baadhi ya Watanzania ...mwalimu yeye,Dr. Yeye,Mchumi yeye,Engineer yeye,Mwanasiasa yeye.na Mpuuzi yeye

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

Acha ubishi zoezi limefeli,Mimi ni karani wa sensa, Kilichosababisha ni serikali wamechakachua pesa hakuna madodoso, tumefanyakazi siku tatu madodoso yamekwisha eneo langu bado kama nusu ya watu hawajahesabiwa na siku tatu hatujui kinachoendelea, hapo unabisha kuwa zoezi halijafeli tu acha ukasuku wa kusikia tu bila kupima
 
Mimi nimegoma kuhesabiwa na bado hadi leo makarani hawajafika kwangu, sasa sielewi kuwa walijua nimegoma au ndo niendelee kusubiri ili wakija niwape makavu yao, cha ajabu tunaishi wengi kwenye hiyo nyumba na tuliogoma wachache sasa sijui hao wengine itakuwaje na ofisi za mwenyekiti hawataki kwenda wanasema kunawatu wamelipwa kuwafuata wao nyumbani,
 
Ndugu yangu afadhali ya wewe angalau walikuachia hata hayo mawsali,mie tangu siku ya kwanza ya sensa nimesubiri labda watapita lakini wapi,wakapita nyumba ya jirani kwangu pale hawaja rudi,baada ya kuona siku zinapita,nikawa namtafuta yule karani wa sensa aliyepangwa eneo lile nikaambiwa kashamaliza naamesha kabidhi kazi.Na hiyo imetokea kati kati ya mji.Huko vijijini sijui hali ikoje.

Halafu kituko kingine ni kuweka alama ya vema ktk kujulisha kama hapo makarani wamehesabu kumbe hawajahesabu,hasa wakipita maramoja halafu wasikukute.Walisema walimu watahujumu sensa,sasa sijajua km hiyo siyo hujuma.
Jamani mie kulingana na kazi yangu natoka asubuhi na kurudi jioni na naishi pekeyangu so alipokuja karani wa sensa akanikosa. Wakaacha maswali matatu tu kwa jirani;
1. Jina kamili
2. Tarehe ya kuzaliwa
3. Kiwango cha elimu
Hii imekaa vizuri kweli, kwani kulingana na mkurugenzi wa Takwimu alisema kuna aina mbili ya dodoso;
1. Fupi, yenye maswali 32 na
2. Dodoso ya pili ina maswali zaidi ya 60
 
Hizo fedha za wafadhili mlitaka zirudishwe?
Si kwa sababu SIYO WAISLAM KUGOMA, watu wengi tu hawajahesabiwa!
 
Acha ubishi zoezi limefeli,Mimi ni karani wa sensa, Kilichosababisha ni serikali wamechakachua pesa hakuna madodoso, tumefanyakazi siku tatu madodoso yamekwisha eneo langu bado kama nusu ya watu hawajahesabiwa na siku tatu hatujui kinachoendelea, hapo unabisha kuwa zoezi halijafeli tu acha ukasuku wa kusikia tu bila kupima
Unachosema naweza kukubaliana na wewe aisee; mi ninapoishi niko ndani ya apartment kuna nyumba tatu zenye jumla ya familia 12 sote hakuna aliyehesabiwa; kila nikiuliza wanadai makarani hawajapita; kuna karani mmoja nilikutana naye maeneo ya kijitonyama nika muomba anahesabu akadai kwa vile nakaa Ilala natakiwa niesabiwe hukohuko; kwakweli sikumuelewa na nikabaki najiuliza Sensa ni kwa ajiri makaazi au kujua Idadi ya watu provided sijaesabiwa sehemu yoyote ile: hivyo sikupata huduma na ninapoishi sote hatujaesabiwa. Zoezi la sensa Limefeli kwa kiwango kikubwa.
 
makarani wenyewe hata kuwaona sijawai.

Kumbe tuko wengi, nasikia tu kuna kuhesabiwa. J2 sikutoka nasubiri kuhesabiwa, hadi leo sijawaona kuja. Wanahesabu wapi huko??? Halafu wanasema kuna watu wamegoma kuhesabiwa, sa sie tunaosubiri wanasema imekuwaje? Dah!
 
Hivi unaposema zoezi la sensa halijafanikiwa,unazungumza kwa furaha au kwa uchungu. Kumbuka kuwa hizi takwimu hazitatumiwa na serikali iliyopo madarakani tu,hata kama ikiingia serikali nyingine hapo 2015 mf. Chadema,TLP au NCCR bado hiyo serikali itatumia hizo takwimu. Kwa hiyo tuache chuki za kisiasa ambazo hazina msingi.
Siamini kama kila ambacho kinafanywa na serikali ya CCM ni kibaya. Watanzania sisi ambao tunajiita ni wapinzani tukiwa katika majukwaa au vijiweni ndio ambao tunasema serikali ya CCM haijafanya kitu kwa miaka 50 wakati huo tunampa sifa Mwl Nyerere kuwa alikuwa ni kiongozi aliyetukuka wakati wa kipindi chake. Ndugu wananchi tusiwe tunabeba tu kila ambalo tunaambiwa na wanasiasa,Tupime kauli zao. Mimi sio mwanaccm wala Chadema wala chama chochote cha siasa. Nimeongea kwa mtazamo wangu.
''TUACHE KUWEKA MASLAHI YA VYAMA VYETU MBELE,BALI TUWEKE MASLAHI YA TAIFA LETU MBELE''
 
Hivi unaposema zoezi la sensa halijafanikiwa,unazungumza kwa furaha au kwa uchungu. Kumbuka kuwa hizi takwimu hazitatumiwa na serikali iliyopo madarakani tu,hata kama ikiingia serikali nyingine hapo 2015 mf. Chadema,TLP au NCCR bado hiyo serikali itatumia hizo takwimu. Kwa hiyo tuache chuki za kisiasa ambazo hazina msingi.
Siamini kama kila ambacho kinafanywa na serikali ya CCM ni kibaya. Watanzania sisi ambao tunajiita ni wapinzani tukiwa katika majukwaa au vijiweni ndio ambao tunasema serikali ya CCM haijafanya kitu kwa miaka 50 wakati huo tunampa sifa Mwl Nyerere kuwa alikuwa ni kiongozi aliyetukuka wakati wa kipindi chake. Ndugu wananchi tusiwe tunabeba tu kila ambalo tunaambiwa na wanasiasa,Tupime kauli zao. Mimi sio mwanaccm wala Chadema wala chama chochote cha siasa. Nimeongea kwa mtazamo wangu.
''TUACHE KUWEKA MASLAHI YA VYAMA VYETU MBELE,BALI TUWEKE MASLAHI YA TAIFA LETU MBELE''

Sensa ya 2002 hakuna mtu au kikundi kilichogomea sensa lakini hadi leo hii hatujui hizo takwimu ziliiisaidiaje serikali kupanga maendeleo ya nchi - maana , mfano mdogo, leo hii katika kipindi cha sensa ya 2012 baadhi ya watoto wa shule za msingi mijini na vijijini bado wanasomea skafuni kama sio chini ya miti au katika vibanda vya makuti (picha zimekuwa kibandikwa humu humu JF). Sasa kama serikali haikuweza kutumia takwimu za sensa ya 2002 angaa kuboresha mazingira ya kuwapatia watoto wadogo elimu, SIONI FAIDA YO YOTE YA SENSA. Hayo madai kuwa takwimu zinaisaidia serikali kupanga na kuleta maendeleo ni political slogans tu kama zilivyo za 'maisha bora kwa kila mtanzania', 'kilimo kwanza', 'malaria haikubaliki', nk. Ninawapongeza wote waliogomea sensa.
 
Tuache ubishi.... LIMEFELI, LIMEFELI kuna vijiji na mitaa mpaka leo hatujahesabiwa i mean sio mtaa wa watu 100 ni watu wengi sana. leo nimejaribu kuwapigia watu wanaoishi jirani zaidi na office za mtaa nao hawaja hesabiwa.... JAMANI tuache kujidanganya zoezi LIMEFELI Hasa mkoa wa pwani


Naunga mkono hoja, mpaka ninavyoandika sijahesabiwa pamoja na baadhi ya watoto waliolala nyumbani kwangu usiku wa kuamkia 26.08.2012. Kila nikitoka naacha maagizo ya kuitwa mara wakifika wahesabuji.... hola... naamini sitahesabiwa katu mimi na jirani zangu.
 
Sensa ya 2002 hakuna mtu au kikundi kilichogomea sensa lakini hadi leo hii hatujui hizo takwimu ziliiisaidiaje serikali kupanga maendeleo ya nchi - maana , mfano mdogo, leo hii katika kipindi cha sensa ya 2012 baadhi ya watoto wa shule za msingi mijini na vijijini bado wanasomea skafuni kama sio chini ya miti au katika vibanda vya makuti (picha zimekuwa kibandikwa humu humu JF). Sasa kama serikali haikuweza kutumia takwimu za sensa ya 2002 angaa kuboresha mazingira ya kuwapatia watoto wadogo elimu, SIONI FAIDA YO YOTE YA SENSA. Hayo madai kuwa takwimu zinaisaidia serikali kupanga na kuleta maendeleo ni political slogans tu kama zilivyo za 'maisha bora kwa kila mtanzania', 'kilimo kwanza', 'malaria haikubaliki', nk. Ninawapongeza wote waliogomea sensa.

Jaribu kufikiri nje ya box,kama watawala wa sasa wameshindwa kutumia takwimu za Sensa kuleta maendeleo,haiondoa umuhimu wa Sensa! Vyama vya siasa vitaingia ktk uchaguzi mkuu miaka 2 na nusu ijayo kugombea kuongoza nchi hii,hawa wanahitaji takwimu wakati kuunda sera na ilani za vyama vyao. Sasa watapata wapi takwimu kama baadhi yetu tunaona jambo muhimu kama hili halina maana?! Mwafrika sijui aliumbwa na kupewa akili za aina gani!!
 
Kumbe tuko wengi, nasikia tu kuna kuhesabiwa. J2 sikutoka nasubiri kuhesabiwa, hadi leo sijawaona kuja. Wanahesabu wapi huko??? Halafu wanasema kuna watu wamegoma kuhesabiwa, sa sie tunaosubiri wanasema imekuwaje? Dah!

Umechukua hatua ya kuonana na mjumbe wa serikali ya mtaa kujua kwanini hujahesabiwa?
 
Naunga mkono hoja, mpaka ninavyoandika sijahesabiwa pamoja na baadhi ya watoto waliolala nyumbani kwangu usiku wa kuamkia 26.08.2012. Kila nikitoka naacha maagizo ya kuitwa mara wakifika wahesabuji.... hola... naamini sitahesabiwa katu mimi na jirani zangu.

zoezi limefeli nadhani wanafanya makadilio sasa
 
Back
Top Bottom