Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Swali lako ni sawa na kuuliza 'kwa nini tunajenga daraja la Kigamboni pale kurasini hali kuna kivuko pale ferry na pia barabara ya Kongowe' jibu ni 'Congestion'

Eneo la bandari limekuwa dogo, unalazimika kubomoa nyumba za wananchi kupanua bandari imeshindikana, tufungua Bandari kavu kibao ambazo ni usumbufu na gharama kubwa kwa mteja. ukiachilia mbali msongamano wa malori ya kuhamisha mizigo bandarini kupeleka bandari kavu.

Usichekeshe mkuu. Rudi nyuma halafu chungulia ulichokiandika na usome btwn the lines. Hakuna kitu km hicho. Kigamboni bridge is a different case for we do not have other parallel bridges through to Kigamboni. If we had some like the ports we would not hv needed a third or a fourth bridge.
 
Haya ni matokeo ya kikao kilichofanyika kigali kati ya mseven,kagame na uhuru,,,na watakaa kikao kingine tena hivi karibuni,,sijui watakuja na lipi jipya ,,swala la ushuru na forodha sio sababu yawao kutoitumia bandari ya dar,,bali wanataka kujijenga kiuchumi bila kumshirikisha tanzania ,,maana wanampango wakujenga reli itakayopita uganda,kenya na rwanda

The 3Ks wanayo road map yao ambayo ndani ya miezi nane impact itaonekana kwa kudorora kwa uchumi wa nchi.Walimshadadia Kenyatta wakati wa uchaguzi wakidhani wakuwa upande wao.
Ni hivi kenyata ni mjasilia mali anajua wapi pa kuwekeza at the right time, the guy knows sabotage strategies in business na ndicho yule dogo katufanyia leo tunalia na kagame, no ni yule dogo, mfaidikaji wa mgogoro huu ni kenya via MOMBASA PORT.Mtalaumu kagame buuuuuuuuuuuuuuuuuureeeeeee!!! think outside the box, just open the pandora box.Kenya ni wafanya biashara wanajua mikakati ya kibiashara.

Wa-TZ mmeingia Kingi kwa mgogoro wa Rwanda, no Kenya behind the panorama
 
Mnachanganya mambo, someni vizuri mada. Uamuzi wa kupitisha mizigo Kenya si wa Serikali ni wa wafanyabiashara wa nchi hizo mbili. ambao hapa wanasemewa na mtanzania mfanyabiashara wa kusafirisha mafuta, ambaye anajaribukuibana serikali ihararishe uharamia kupitisha ktk barabara zetu magari yake yakiwa na uzito usioruhusiwa kisheria.

Wadanganyika kutokujua tunashabikia maharamia ambao miaka yote ndio wanapenyeza hela zao chafu kwa watendaji serikalini kuchelewesha mipango ya matumizi ya reli ktk usafirishaji mizigo mizito.

Hawahawapaswi kuchekewa!!!
Hayo yanatokea wakati Rwanda ikiendeleza vita yake ya maneno na Tanzania na mfululizo wa matukio ya kuitenga Tanzania kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Viongozi wa Kenya, Rwanda na Uganda walikutana Juni 25, mwaka huu mjini Entebbe, Uganda na kukubaliana kuongeza uhusiano wa kibiashara baina yao.

HAPA KUNA SERIKALI NDANI YAKE.
 
Hii serikali mie sisemi kitu.. we are doomed..

WaTz wote tumekuwa vichwa vya nazi. Pengine hadi kizazi hiki (kizee na kipya) kitoweke ndio nchi itarejea katika mstari. Sote tunaangalia dunia ya leo kwa namna ile ile kama Mhe Dr JK & co wanavyoingalia. Mojawapo ya unazi wetu ni kushindwa kujitoka katika tope la a reactive society na kuwa a proactive society hata kwa vitu ambavyo viko wazi (havihitaji siasa). Tunasubiri matukio ndio tuanze kutenda!! Hakuna aliyeturoga wala kutuhujumu, bali tunajiroga na kujihujumu wenyewe. Evidence: ni maoni ya hapa hapa JF!
 
wengi hapa mtaongelea hili swala kwa kulihusisha na mgogoro hewa kati ya TZ na RWANDA.
lakini kwa mtu yeyote anejua jiografia na usumbufu ulitukuka pale bandarini DSM na kwenye barabara zeu, basi hatabishana na hali halisi.
kwa mfanya biashara, siasa wala haziwezi kumlazimisha kutumia bandari ya MOMBASA kama akipitia bandari ya dsm atapata faida kubwa zaidi.la msingi ni kwamba,bandari ya DSM inatakiwa kubadili mfumo wake wa kutoa huduma ili ziweze kuvutia wateja na kupunguza urasimu
 
Kuja marais watatu mfululizo hapa Tanzania kumetu-cost sana na bado,huku kujipendekeza kwa wazungu nouma.
 
hello! Jf mi naona hapa tunatwanga maji kwenye kinu, mafisadi wamekula hela za bandari hazijawatosha wanataka kuhamia kwenye vitengo vingine, hanspope anasema vikwazo ni ving atwambie ni nani mwenye jukumu la kumaliza matatizo hayo, ili tumpe taarifa kuhusu malalamiko yake, wamelikoroga lazima walinywe

ilo kweli nilakujiuliza,,,kipindi cha nyuma bandari ilikuwa inanuka lakini mh mwakyembe ameisafisha,,eti ndio wanahama na kusingizia ushuru na forodha,,mbona wakati wanaibiwa mafuta kwenye meli hawakuama,,hapa kuna siasa ndani yake
 
kisha mniambie kuwa EAC itarejea kwenye utengamano wake ! THUBUTU, upo mgogoro mkubwa unafukuta, na tusipokuwa waangalifu TUTAUMIA, tutafute marafiki wapya kusini mwa Afrika,
 
Kuna taarifa zinasema kua jk atasaini mkataba na serikali ya marekani kutumia bandari ya tz,na mazungumzo na wachina yanaendelea pia huenda nao wakasign.
 
Kwa wachumi mtanisaidia kidogo, kwani nachanganyikiwa na sirikali reactive.

Maka jana mh.rais alizinDUA KWA MBWEMBWE a five years strategic Plan.mwaka huu ktk bajeti ya nchi imeletwa bila kufuata vipau mbele ktk strategic plan ya nchi, baada ya miezi kadhaa tumeletewa the BIG RESULT NOW nashindwa kuunganisha kipi kinaanza na kipi kinafuata.
Nhi hii kwa MAJANGA kwa kukosa maarifa
 
Hiyo habari imeandikwa kwenye Blog ya Mpekuzi! Lakini mi niseme kitu Haya ni matokeo ya serikali kushindwa kisimamia uchumi wake! Maana serikali Corrupt haiwezi kukusanya kodi, Sio kodi tu! Serikali Corrupt haiwezi kusimamia uchumi wake! Bunge hovyo, utekerezaji wa miradi Kama utanuzi wa Bandari na Miundombinu na kupunguza Mizani katika mabarabara makuu ambayo imekua kero si kwa wageni tu ata kwa wazawa imekua kero sana! Bado huo ukiritimba ambao uko bandarini yani huo ndo kero sana! Niseme tu hapa kwetu kila kitu kimekua hovyo sn! Wakati Kenya, Uganda, na Rwanda wanapanga na kushughulika na maswala ya uchumi Sisi hapa Tanzania, Serikali inafikiria kupambana na Upinzani haswa Chadema!
 
let them Go nothing to worry! kuendelea kulialia na RWANDA&UGANDA kutumia bandari yetu au lah kwetu ni changamoto lakini pia tujue kua ni muda mrefu hawakupenda kufanya hivyo ila kwa sasa ndo wamejidhiirisha roho zao zikoje! Tumshukuru Mungu kwakua na bahari cha msingi apa ndo iwe chachu ya kusimamia na kuanzisha vyanzo vya mapato vingine..leo tunalaumiana lakini tujiulize je nchi ambazo hazina BAHARI chumi zao zinaendeshwaje? Tuwekeje kwenye GAS na italipa tu acha watuondolee Jams na usumbufu

hiv wewe mbona una mawazo mgando! Iwapo bandari ulokua nayo toka mungu kaumba dunia imeshindwa kukunufaisha unategemea gesi ndo itakunufaisha?
 
fast track.............................Uhuru Kenyatta katika ziara yake majuzi nchini China amepata msaada/mkopo wa dolari bilioni 5 kugharimia upanuzi wa bandari ya Mombasa na kujenga reli ya kuunganisha nchi hizo tatu, Kenya, Uganda na Rwanda.
Najua Serikali ya JK wanasema yatapita tu!
 
Hao wasafirishaji kwa nini hawaleti mchanganuo wa kitakwimu....

1. Inachukua siku ngapi kuondosha kontena bandarini (Dsm/Mombasa)
2. Gharama za uondoshaji huo zikoje?
3. Unatumia siku ngapi kusafirisha kontena kwenda Uganda ama Rwanda?
4. Kero za traffic police kwa Tanzania na Kenya zikoje?

Kubwa zaidi hao kina Hanspope watwambie tukiondoa mizani wanatuhakikishiaje kuwa hawatabeba mizigo zaidi ya uzito unaoruhusiwa???

Bila kufanya haya tutakuwa tunapiga siasa tu!!

Kikubwa serikali yetu iongeze ufanisi tu bandarini, barabara ziimarishwe, tufufue reli ya kati jambo ambalo kina Hanspope hawato-support....mwisho wa siku wafanya biashara wa Rwanda na Uganda wataangalia njia ipi inawapa faida!!!!


Mkuu hapo nilipobold, soma hiyo experience ya SeasonedTraveller. Anzia alipoingia bong.


http://www.thenomadiks.com/index.ph...a-seasoned-traveler-s-exposure-to-tanzania#38
 
hizi ni short term impact za mgogro wetu na rwanda pamoja na mkutano wa siri waliokaa uganda,rwanda na kenya inatubidi tungalie impact nyingine ambazo tunweza kuzipata na vipi tunaweza kuziepuka,ili kulinda hhadhi ya nchi yetu!!!
 
Hao wasafirishaji kwa nini hawaleti mchanganuo wa kitakwimu....

1. Inachukua siku ngapi kuondosha kontena bandarini (Dsm/Mombasa)
2. Gharama za uondoshaji huo zikoje?
3. Unatumia siku ngapi kusafirisha kontena kwenda Uganda ama Rwanda?
4. Kero za traffic police kwa Tanzania na Kenya zikoje?

Kubwa zaidi hao kina Hanspope watwambie tukiondoa mizani wanatuhakikishiaje kuwa hawatabeba mizigo zaidi ya uzito unaoruhusiwa???

Bila kufanya haya tutakuwa tunapiga siasa tu!!

Kikubwa serikali yetu iongeze ufanisi tu bandarini, barabara ziimarishwe, tufufue reli ya kati jambo ambalo kina Hanspope hawato-support....mwisho wa siku wafanya biashara wa Rwanda na Uganda wataangalia njia ipi inawapa faida!!!!

Mkuu ule mkutano uliofanyika Uganda kati ya Museveni, Uhuru na Kagame ndio unaelekea kuiua bandari ya Dar Es Salaam. Uhuru kwa kujua kwamba serikali yake soon inawezekana ikawekewa vikwazo vya kiuchumi endapo hatashirikiana na Mahakama ya ICC, alianza mapema kuangalia jinsi ya kuongeza pato la ndani litakaloweza kuziba pengo endapo wahisani watajitoa kuisaidia Kenya. Kumbuka Uhuru aliitembelea bandari ya Mombasa kabla hata ya kuapishwa kuwa Raisi. Pamoja na kukubaliana kujenga reli, Uhuru ameondoa mizani kwa mizigo inayokwenda Uganda na Rwanda, pia amewapa ofisi maafisa wa Uganda na Rwanda kushughulikia mizigo yao wenyewe pale Mombasa. Hii deal iliwafurahisha Museveni na Kagame na sasa tayari wametangaza kuacha kuitumia bandari ya Dar Es Salaam kuanzia Septemba Mosi.

Sisi kama Watanzania lazima tukubali kwamba tumekosa viongozi wenye ubunifu na wanaoweza kuona mbali kitu ambacho sasa inaelekea kitaugharimu uchumi wetu. Ni kelele ngapi zimepigwa na importers juu ya tabia ya wizi pale bandarini lakini hakuna hatua madhubuti iliyochukuliwa. Mtu unaagiza kagari kako lakini by time hilo gari linatoka bandarini, power window hakuna, radio hakuna, wheel cover hakuna, list ni ndefu. Wakati tukishangaa Uganda na Rwanda kuacha kuitumia bandari yetu, hata sisi Watanzania wengi tayari waliisha ikimbia bandari ya Dar Es Salaam na sasa wanaitumia bandari ya Mombasa kwa sababu hakuna wizi wa bila mpangilio wa mizigo, hakuna urasimu usio kuwa na tija wakati wa kutoa mizigo na hakuna kudaiwa rushwa ovyo ovyo.

Tujifunze.

Tiba
 
kisha mniambie kuwa EAC itarejea kwenye utengamano wake ! THUBUTU, upo mgogoro mkubwa unafukuta, na tusipokuwa waangalifu TUTAUMIA, tutafute marafiki wapya kusini mwa Afrika,
wasiwasi wangu wasije wakaunda millitary alliance tu hapo ndipo hali itakapokuwa mbaya
 
Mkuu ule mkutano uliofanyika Uganda kati ya Museveni, Uhuru na Kagame ndio unaelekea kuiua bandari ya Dar Es Salaam. Uhuru kwa kujua kwamba serikali yake soon inawezekana ikawekewa vikwazo vya kiuchumi endapo hatashirikiana na Mahakama ya ICC, alianza mapema kuangalia jinsi ya kuongeza pato la ndani litakaloweza kuziba pengo endapo wahisani watajitoa kuisaidia Kenya. Kumbuka Uhuru aliitembelea bandari ya Mombasa kabla hata ya kuapishwa kuwa Raisi. Pamoja na kukubaliana kujenga reli, Uhuru ameondoa mizani kwa mizigo inayokwenda Uganda na Rwanda, pia amewapa ofisi maafisa wa Uganda na Rwanda kushughulikia mizigo yao wenyewe pale Mombasa. Hii deal iliwafurahisha Museveni na Kagame na sasa tayari wametangaza kuacha kuitumia bandari ya Dar Es Salaam kuanzia Septemba Mosi.

Sisi kama Watanzania lazima tukubali kwamba tumekosa viongozi wenye ubunifu na wanaoweza kuona mbali kitu ambacho sasa inaelekea kitaugharimu uchumi wetu. Ni kelele ngapi zimepigwa na importers juu ya tabia ya wizi pale bandarini lakini hakuna hatua madhubuti iliyochukuliwa. Mtu unaagiza kagari kako lakini by time hilo gari linatoka bandarini, power window hakuna, radio hakuna, wheel cover hakuna, list ni ndefu. Wakati tukishangaa Uganda na Rwanda kuacha kuitumia bandari yetu, hata sisi Watanzania wengi tayari waliisha ikimbia bandari ya Dar Es Salaam na sasa wanaitumia bandari ya Mombasa kwa sababu hakuna wizi wa bila mpangilio wa mizigo, hakuna urasimu usio kuwa na tija wakati wa kutoa mizigo na hakuna kudaiwa rushwa ovyo ovyo.

Tujifunze.

Tiba
tatizo hawakuwepo mawaziri wenye uchungu na nchi boara sasa jembe mwakyembe alivyokuwepo ila wasiwasi wangu ni kwamba hapati support ya kutosha kutoka serikali kuu
 
Kuna watanzania wengine wanatumia bandari ya Mombasa kwa mambo yao inakuwa bora kuliko kutumia Dar .Tanzania kila kitu ni siasa hata kuwaza kawaisa leo ule nini lazima uingize siasa .Haya endelezeni siasa muone .
 
Back
Top Bottom