Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

tatizo hawakuwepo mawaziri wenye uchungu na nchi boara sasa jembe mwakyembe alivyokuwepo ila wasiwasi wangu ni kwamba hapati support ya kutosha kutoka serikali kuu

Mkuu tuko pamoja, ndio maana nikasema hatuna viongozi wenye uchungu na uchumi na nchi, wao wanajali matumbo yao na kujilimbikizia mali tu. Kama kungekuwa na viongozi makini na wanaojitahidi kama anavyofanya Mwakyembe, I believe hata hizo siasa za Uhuru zisingengefanikiwa. Sasa tumekumbuka shuka wakati kumekucha. Bandari ya Dar ni matatizo tupu.

Tiba
 
Mkuu tuko pamoja, ndio maana nikasema hatuna viongozi wenye uchungu na uchumi na nchi, wao wanajali matumbo yao na kujilimbikizia mali tu. Kama kungekuwa na viongozi makini na wanaojitahidi kama anavyofanya Mwakyembe, I believe hata hizo siasa za Uhuru zisingengefanikiwa. Sasa tumekumbuka shuka wakati kumekucha. Bandari ya Dar ni matatizo tupu.

Tiba
kilichobaki tuangalie mbele yaliyopitwa si ndwele uganda na rwanda hatuwezi kuwarudiisha kwenye bandari yetu,hasa kwa uhusiano waliokuwa nao so tuangalie mahali pengine ambapo tunaweza kufanikiwa kuwawin
 
hizo ni njama za Rwanda unajua museven amenunuliwa na kagame hakuna lolote lilishajulikana hili mapema, amelipa kisasi baada ya kuona wahamiji haramu wamerudishwa kwake, pia taharifa zilizopo Kenya, Uganda na Rwanda wanakikao tena mwezi huu kitafanyika Nairobi sasa huoni ni njama zinaendelea? kwanini Tanzania haijitoi EAC? SITA amekaa kimya tu na hao wabunge wa EAC wamekaa kimya hii ni mara ya tatu wanakutana kama jumuia na kuamua mambo yao hamuoni kama sisi wametutoa? Tujithamini sisi wenyewe tuwe na maamuzi ya busara
 
Liwalo na liwe, kama vipi nasi tufunge njia ya RUSUMO tuone bidhaa zao watapitisha wapi
 
kisha mniambie kuwa EAC itarejea kwenye utengamano wake ! THUBUTU, upo mgogoro mkubwa unafukuta, na tusipokuwa waangalifu TUTAUMIA, tutafute marafiki wapya kusini mwa Afrika,

Zambia na Malawi wanatumia bandari yetu ya dar. Burundi na drc nao ni wateja wetu. Kenya wanategemea sana Uganda, Rwanda na sudan kusini. ushindani wa kibiashara upo kila sehemu. bandari ya bagamoyo itakua kubwa sana na huduma zake zitakua za kisasa na za haraka. hao waganda na warwanda watarudi tu. wafanyabiashara wa Rwanda na Uganda bandari zetu za dar na bgmyo zikiimarika watalazimisha serikali zao kurudi. kagame, uhuru na museveni wana tuhuma za uhalifu. uhuru ana kesi hague na kagame na museveni wanatarajiwa kushitakiwa wakiondoka kwenye urais. that's why wameng'ang'ania kwenye madaraka. wameunda utatu wao kwa sababu matatizo yao yanafanana. hivi hujiulizi kwa nini Burundi na kongo wamekataa kujiunga nao? ujio wa marais wa china na marekani nayo ni sababu nyingine. wivu wanatuonea.
 
wasiwasi wangu wasije wakaunda millitary alliance tu hapo ndipo hali itakapokuwa mbaya

Tatizo la watanzania kila saa ni kuogopa kuvamiwa kwa taarifa yako security nzuri dunia ya leo ni kuwa na uchumi imara, watu watakuogopa, hata pale kijijini kwenu mtu aliye na mali anaogopeka, hakuna kibaka kuingia ktk himaya ile the same at the level of a country.Tanzania jengeni uchumi hakuna atakayekuvamia.3Ks they are planning to be super power in the EA economy Tanzania hata katiba imetushinda kila kukicha CDM,majanga kweli
 
wasiwasi wangu wasije wakaunda millitary alliance tu hapo ndipo hali itakapokuwa mbaya

na ndio hatari ninayoiona mimi, tunanze kuimalisha undugu wetu na Malawi, Botswana, Afrika Kusini, Zambia na Namibia ! Integration na hao jamaa zitawatisha hao wapenda vita.
 
sasa kama mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge ya bajeti ni andrew chenge unategemea watu wako serious kweli na serikali hii?
Yaani ktk watu wote mzee wa vijisent ndio amepewa uenyekiti?
Kazi tunayo

chenge kichwa wewe acha kuwaza kima------
 
Bandari yetu itabaki kuwa bandari ya kushushia shehena ya dawa za kulevya tu na kusafirishia pembe za ndovu, maana ndio biashara tunayoiweza.
 
Ccm blah blah nyingi wacha waende wakafanye yao mpaka tutakapo kuwa serious na juzi uhuru kenyatta alikuwa china kashasaini mkataba wa kupanua bandari!!!!!!! Tanzania tunambwela mbwela tu na chama cha wauza unga!!!!!!!!!!
 
Tatizo la watanzania kila saa ni kuogopa kuvamiwa kwa taarifa yako security nzuri dunia ya leo ni kuwa na uchumi imara, watu watakuogopa, hata pale kijijini kwenu mtu aliye na mali anaogopeka, hakuna kibaka kuingia ktk himaya ile the same at the level of a country.Tanzania jengeni uchumi hakuna atakayekuvamia.3Ks they are planning to be super power in the EA economy Tanzania hata katiba imetushinda kila kukicha CDM,majanga kweli
sijakwambia kwamba naogopa vita nimesema point yangu ni kwammba formation of military aliance huwa zinaanza hivi hivi,by the way hatutarajii vita and i hope haitokuja kutokea
 
kwa kutafakari kwangu Muda mrefu nimeona kuna vita vya kudhoofishana kiuchumi kati ya jk na pk...kuna gari nyingi sana za mafuta tank ninasadikika kuwa za mafisadi mpya mpya zilikuwa zinapelaka sana mafuta kigali mengi yakishukiwa kuwa ya ridhiwan,sasa kukataa kupitisha mizigo hasa hasa mafuta nadhani Pk anataka aioneshe Tz na kupitia hao hao mafisadi adhari za moja kwa moja mifukoni mwao...kurudishwa kwa wanyarwanda 8000 na kupewa hekari 300 za hifadhi ni mwiba kwa Pk na hivyo anataka tu kulipa kisasi,Tungeweza kuwa na uswahiba na museven kila kitu kingekwenda sawa ila hilo limeshakuwa haliwezekani tena....Buriani Jk-Nilikuwa sikukubali kadisa kutoka rohoni wakati ule ulipotengeneza mabango makubwa kama unatangaza bia ya Kibo gold kila mahala (pale nzega stand)ndilo lililokuwa lina nichukiza sana...kwa kuacha kupitisa mizigo wamesha acha mdogo mdogo kitambo hapa tuliokuwa tunawategemea hao transity tushaanza kuonja adha.njaa kali...kagongwa ,tinde,isaka kote tunalia hali ni mbaya na kuanzia sept sijui itakuwaje....lakini poa ngoja iwe ndio death of CCM
 
Hizo ni KELELE ZA MPANGAJI tu.

Wacha wajitoe kwani tulijenga kwa ajili yao. Rwanda ajenge na yeye bandari yake.... poor landlocked counrty!
 
Hizo ni KELELE ZA MPANGAJI tu.

Wacha wajitoe kwani tulijenga kwa ajili yao. Rwanda ajenge na yeye bandari yake.... poor landlocked country!
 
mbona hizo mbwe mbwe tu .... atake asitake bado nchi yake ni "land locked country-rwanda" atake asitake.

Una mawazo finyu sana ya kuona mambo kwa mapana yake, kama Rwanda wa njia mbadala wa kuingiza mizigo yao hatuna jinsi la ni kufuata yale madai yao ya msingi katika kufanya nao biashara ama tutegemee kuathirika kibiashara wakienda bandari ya Mombasa.
 
Back
Top Bottom