Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

Rwanda, Uganda zajitoa Bandari ya Dar

......................TUJIKUMBUSHE..................
kamau.jpg


Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau, Kenya.

"If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa port would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast," said Mr Kamau.
 
JK ongeza wanajeshi Congo tuwang'oe M23 ilitufanye biashara vizuri na Congo Rwanda is nothing to Tanzania bana acheni uoga ndio maana mnaambia Watanzania waoga tujivunie aridhi yetu na tuitumie tusiwape wageni.
 
Panoni&company,Liberty,Usangu,Dhandoo,lake oil,Riz1 and xxx,wote watakua na hali ngumu,Reli iboreshwe kupunguza hizo kero.Dar,Tanga,Mtwara zinatushinda bado tunakomalia mega project ya Bagamoyo?hii serikali haiwezi tatua hizi changamoto,wamefikia kikomo cha akili zao plus ulafi,Mradi wa bomba la mafuta Dar mwanza mnaukumbuka kweli?
Hapa ndipo namkumbua mch Peter,
 
labda ungeeleza kwa kina chanzo na sababu, si wote pengine tuliosikia habari hiyo.
 
JK ongeza wanajeshi Congo tuwang'oe M23 ilitufanye biashara vizuri na Congo Rwanda is nothing to Tanzania bana acheni uoga ndio maana mnaambia Watanzania waoga tujivunie aridhi yetu na tuitumie tusiwape wageni.

Nusu ya ardhi nzuri kwa sasa inamilikiwa na wageni na hawajaiendeleza,wameuziwa kupitia GPS,subiria mengi yanakuja
 
Mlishangilia kufukuzwa kwa wanyarwanda, ni sawa wanyarwanda walitakiwa kuondoka lakini si kuwashtukiza leo nchi ile inahangaika kuwahifadhio kwa kuwa hatuwaarifu mapema na wao wameamua kumwaga mboga come 1st september, hakuna mizigo kupita DARPORT.
  • Bajeti ya mgimwa majanga,
  • clearing and forwarding companies majanga ina maana itabidi kupunguza wafanya kazi
  • wenye malori ya kusafirisha mafuta majanga no cargo to haul
  • baadhi ya vitengo TRA vitapunguiza wafanyakazi
  • Consumption ya fule nad lubricants kwa malori itashuka na hivyo kuathiri, sector ya nishati
  • Kwa ujumla yako mengi haya yote ni kukosa uvumilivu ktk kuamua, kazi tunayo
 
Jamani naombeni msaada. Binafsi ninfahamu umuhimu wa bandari za Dar na Tanga. Kwa sababu hiyo zikipanuliwa nitaelewa. Sasa bandari ya Bagamoyo itakuwa ina-serve maeneo gani na umuhimu wake ni upi?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Swali lako ni sawa na kuuliza 'kwa nini tunajenga daraja la Kigamboni pale kurasini hali kuna kivuko pale ferry na pia barabara ya Kongowe' jibu ni 'Congestion'

Eneo la bandari limekuwa dogo, unalazimika kubomoa nyumba za wananchi kupanua bandari imeshindikana, tufungua Bandari kavu kibao ambazo ni usumbufu na gharama kubwa kwa mteja. ukiachilia mbali msongamano wa malori ya kuhamisha mizigo bandarini kupeleka bandari kavu.
 
ha ahaaaaaaaaa ngoja nicheke kushusha presha kabla haijaniua kwa majanga ya nchi hii!!!!!

Serikali imelala fofofo mambo ya msingi ilikuwa ni reli na bandari then revenue ingejenga barabara lakini tulianzia mkiani na kuacha kichwa wazi haya ndo majibu sasa!!!!!

Jamani hatuwezi kuweka watu binafsi watuendeshee uti mgongo,tulijikwaa siku nyingi sema tu upepo ulikuwa hauna nguvu now we are taken by wind hatuna pa kushika UBINAFSISHAJI huuuuu ndo unatugharimu sasa!!!!

Hivi tujiulize Watanzania wangapi tumetumia bandari ya Mombasa,???? Mimi mmoja wao kwa sababu ya kero za Dar port,sasa watakuwa wasio Watanzania????!!Tumeyataka haya ngoja yatukute ingawa inaumiza sana!!!

Mtu amabaye kashakuwa waziri na mwanasheria mkuuanataka aandikiwe matatizo ya nchi na wafanyabiashara?????!!!!Kweli kabisa ndo watukomboe watu hawa!!Thubuuutuuuuuu yeeetu tumeliwa...

Ntakesha naandika bure na mapigo ya moyo yanabadilika!!!!!!

Ndo tuamke sasa na kujiuliza nini umuhimu wa hoja ya dual citizenship wakati tuna hoja nzito mia na kumi elfu...watu hawana uzalendo na wanataka kuacha shamba la bibi ili wajukuu wafe njaaa!!!!!
 
Congo wapo,Burundi na Zambia hawa Nyang'au Rwanda waende tu.

Kuwepo siyo tatizo, tatizo ni serikali hii singizi maneno mengi utendaji kidogo, inafanya jitihada gani kuhakikisha hizi fursa tunazipata na kuzitumia kabla wajajanja hawaja take chance. Hapa cha msingi ule mradi wa Bandari ya Bagamoyo usitishwe na badara yake pesa itumike kukarabati na kuongeza njia za reli kuelekea mipaka ya nchi jirani.
 
Jamani naombeni msaada. Binafsi ninfahamu umuhimu wa bandari za Dar na Tanga. Kwa sababu hiyo zikipanuliwa nitaelewa. Sasa bandari ya Bagamoyo itakuwa ina-serve maeneo gani na umuhimu wake ni upi?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Bandari hii itamilikiwa na Wachina, kwa namna hii itakuwa very efficient kwani itakuwa inlet/outlet ya bidhaa zao ambazo nyingine ni za Rwanda na Uganda. Wameahidi pia kuimarisha reli ya kati in that case jamaa watarudi tu.
 
Tusirukeruke tutafute chanzo cha yote haya ni nini ??????halafu tutafute suluhu ya tatizo hilo sio badala ya kutafuta mikakati ya kujenga uchumi imara sisi tunahangaika tu kutengeneza mikakati ya kuiua CHADEMA kucha kuchwa,ngoja na zanzibar ijitenge kabisa labda tutajifunza.

Ni kweli na wazi.
 
Ruanda kuna kitu kinamwasha akishapewa atatulia. Mwache ajae kwenye screen vizuri.
 
Haya ni matokeo ya kikao kilichofanyika kigali kati ya mseven,kagame na uhuru,,,na watakaa kikao kingine tena hivi karibuni,,sijui watakuja na lipi jipya ,,swala la ushuru na forodha sio sababu yawao kutoitumia bandari ya dar,,bali wanataka kujijenga kiuchumi bila kumshirikisha tanzania ,,maana wanampango wakujenga reli itakayopita uganda,kenya na rwanda
 
umeelezea shalo saana, ila lazima ujue EAC bila Tanzania hakuna muungano
 
Bandari hii itamilikiwa na Wachina, kwa namna hii itakuwa very efficient kwani itakuwa inlet/outlet ya bidhaa zao ambazo nyingine ni za Rwanda na Uganda. Wameahidi pia kuimarisha reli ya kati in that case jamaa watarudi tu.

Haiendi hivyo GT. Anae-dictate bandari ya kupitishia mzigo ni importing economy na Sio exporting one. Km nchi haina mahusiano mazuri na nyingine basi vikwazo au masharti ya mpokeaji ndio yenye nguvu. Huwezi Tanzania kupeleka cargo US kwa kutumia Meli za Iran. Mzigo hautapokelewa.
 
Swali lako ni sawa na kuuliza 'kwa nini tunajenga daraja la Kigamboni pale kurasini hali kuna kivuko pale ferry na pia barabara ya Kongowe' jibu ni 'Congestion'

Eneo la bandari limekuwa dogo, unalazimika kubomoa nyumba za wananchi kupanua bandari imeshindikana, tufungua Bandari kavu kibao ambazo ni usumbufu na gharama kubwa kwa mteja. ukiachilia mbali msongamano wa malori ya kuhamisha mizigo bandarini kupeleka bandari kavu.
We ni kifaurongo kweli kabisaaaa!!!!

Unaongea huku ukijua kuwa kuna Mtwara na Tanga au umeamua tu kujitoa fahamu???!!!!

Au ndio nyie mliokimbilia kununua viwanja kwa bei kubwa huko!!!Mtalima mananasi tutayanunua tegeta huo mradi ni ununuzi wa jokofu ueskimo!!!!

We have to reach the maximum handling capacity from all ports before the Bagamoyo thing pops into plan!!!!!!

Kuwa na uzalendo hata kwenye keyboard tu kama ni ngumu kuwa halisi
 
chenge.jpg

Na Raymond Kaminyoge,



Dar es Salaam. Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta Tanzania (Tatoa), kimesema Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.

Katibu Mtendaji wa Tatoa, Zacharia Hanspope aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kukutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi hizo zinajitoa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo kwa muda mrefu zimekuwa zikiyalalamikia lakini Serikali haikuchukua hatua.

Hanspope alisema ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ni baadhi ya vikwazo ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa kwa muda mrefu na wafanyabiashara mbalimbali wa nchi hizo.

“Serikali ipunguze gharama za ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ili kuwa na ushindani sawa na bandari nyingine na hivyo kuzivutia kutumia Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Hanspope.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo alikataa kuzungumzia lolote kuhusu suala hilo akisema halina mantiki yoyote kwake.... “Hivi hilo jambo unaloniuliza lina sense (mantiki) yoyote? Mie siwezi kujibu lolote nenda ukamuulize mwenyewe (Hanspope) maana wakati akisema mimi sikuwepo.”

Alisema kujitoa kwa Rwanda na Uganda kuitumia Bandari ya Dar es Salaam hakutakiathiri chama hicho tu, bali uchumi wa taifa kwa ujumla.

Hayo yanatokea wakati Rwanda ikiendeleza vita yake ya maneno na Tanzania na mfululizo wa matukio ya kuitenga Tanzania kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Viongozi wa Kenya, Rwanda na Uganda walikutana Juni 25, mwaka huu mjini Entebbe, Uganda na kukubaliana kuongeza uhusiano wa kibiashara baina yao.



Kamati ya Bajeti

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge alisema katika kikao kijacho cha Bunge, kamati hiyo itaibana Serikali kuhusu mikakati inayofanywa kukabiliana na ushindani wa kibiashara katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Alisema sababu ya Rwanda na Uganda kujitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam ni vikwazo katika barabara ikiwamo mizani mingi ya kupimia mizigo.

“Mizani ni mingi pia kuna usumbufu katika kupima mizigo yao na kwamba hali hiyo inawaletea usumbufu wafanyabiashara wengi,” alisema.


Alisema vitendo vya askari wa usalama barabarani kudai rushwa pia ni miongoni mwa vikwazo pamoja na urasimu mkubwa katika utoaji wa mizigo bandarini ikilinganishwa na bandari nyingine.

“Ni lazima tujifunze kwa majirani zetu Msumbiji, upanuzi wa haraka wa Bandari ya Beira umekuwa kikwazo kwetu, kampuni nyingi zimeanza kuitumia bandari hiyo,” alisema.

Chenge alikitaka chama hicho kuiandikia kamati hiyo mapendekezo yake ikiwa ni hatua ya kunusuru uchumi wa nchi ili waweze kuijadili bungeni.



Umoja wa nchi tatu

Marais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda na mwenyeji wao Yoweri Museveni walikutana mjini Kampala, Uganda na kuamua kuitumia Bandari ya Mombasa kwa shughuli zao.

Waliahidi kuimarisha ufanisi katika huduma za Bandari ya Mombasa ili kuhakikisha bidhaa zinafika mapema Uganda na Rwanda.

Pia walikubaliana kujenga reli mpya ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka Mombasa kwenda Kenya na Uganda.

Viongozi hao walikubaliana pia kushirikiana katika sekta ya nishati hasa ikizingatiwa kuwa Uganda imegundua mafuta.

Nchi hizo tatu ambazo zimeruhusu kwa raia wao kusafiri kwa vitambulisho pale wanapotembelea nchi tatu miongoni mwao, zitakutana tena Kenya mwezi huu.

waende zao huko kwani wanafkili sisi bila wao hatuishi! Wanakungutwa nini?!
 
Bandari hii itamilikiwa na Wachina, kwa namna hii itakuwa very efficient kwani itakuwa inlet/outlet ya bidhaa zao ambazo nyingine ni za Rwanda na Uganda. Wameahidi pia kuimarisha reli ya kati in that case jamaa watarudi tu.


Wewe MAJANGA kwelikweli yaani na usomi wako unategemea CHINA wakujengee uchumi POOR tANZANIAN.Tumeshindwa nini kujenga reli kabla ya barabara.Tumekubali kuimba single ya magufuli, ambaye wengi tumeshasema magufili ni kaputi.anapiga kelele watu wanamuona wa maana.Huyu ndiyo kachangi kwa kiwango kikubwa kuwauza viongozi wenzake kwa kushikia bango barabara na kuiacha reli ambayo ingetoa mizigo mingi kwa wakati na barabara ingetoa assistance to the rail system, yaani kule ambko reli hajapita ndiyo barabara zingeimarishwa.serikali DHAIFU imetufikisha hapa.SASA tutakachovuna ni migogoro na majirani huku uchumi HOI
 
Back
Top Bottom