Ruling Kuhusu Kesi ya Lema ni Leo!!

Kinachotarajiwa kufanyika leo ni hukumu ya pingamizi lililokuwa limewekwa na wakili wa walalamikaji wa awali(wakili Mughwai wa akina Mussa Mkanga) na si hukumu yenyewe ya rufaa ya Lema.

Ikiwa pingamizi hilo litatupwa, hapo ndipo rufaa itaanza kusikilizwa. Lakini ikiwa pingamizi hilo litakubaliwa, basi hapo ndipo utakuwa mwisho wa rufaa ya Lema, na jimbo la Arusha litakuwa wazi rasmi kwa ajili ya kinyang'anyiro cha uchaguzi mdogo.
 
Haa haa haa Kiatu kikishachakaa hata ukikipiga kiwi hakiwezi kuwa kipya. CCM wakubali kuwa kiatu kimeshachakaa Arusha hawawezi tena kuichukua .
 
Hapa ndipo pailipo na uvumilivu wa watu wa mungu na mwenye masikio na asikie! Kama ikulu haitaingilia maamuzi ya majaji hawa wa 3 basi lema atarudishiwa ubunge wake!
 

Tatizo ni uandishi wako.
 
Wakipindisha tu hukumu basi wameumia.
 
Ukiona ulinzi mkali wa askari ujue, kimenuka. Ulinzi wa kawaida ujue Lema ameshinda. Mungu mkuu.
 
Wanabodi na wanaushirika.

Tujenge utamaduni wa kuheshimu uhuru wa mahakama tukubali hukumu yoyote itakayotolea na mahakama.
 
Leo ni hukumu ya pingamizi ya rufaa ya Lema inayosomwa Dar! Pingamizi likitupiliwa mbali tu basi usikilizwaji wa rufaa ya Lema utaendelea!

Ikiwa pingamizi hili litakubaliwa, basi Lema atakuwa amevuliwa rasmi ubunge, na jimbo litakuwa wazi!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Chadema!
 
Gambas at work! Washindweeeeeee kwa kweli, ol the best lema!
 
Mungu wabari wote watakao sikiliza shauri hili ili haki itendeke..
 
Tunaiman Mungu ataenda kujibu na hatimae Lema atarud kazin. Tukumbuke haki inashinda dhuluma.

........

Leo ni maamuzi ya pingamizi la awali (preminary objection kwa kifupi PO) yaliyowekwa NA wakili wa ccm ''MRUFANIWA'' ....kesi ya msingi itaendelea baada ya maamuzi hayo ila ni kama tu pingamizi hilo litatupiliwa mbali likikubaliwa LEMA UBUNGE NDO BASI TENA MAANDALIZI YA UCHAGUZI MDOGO INABIDI YAANZE
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…