Ruling Kuhusu Kesi ya Lema ni Leo!!

Ruling Kuhusu Kesi ya Lema ni Leo!!

Tukisema chama chenu ni cha dini mnalia lia hapa!!

kwani utakuwa wa kwanza kusema...wajinga ni wengi.Baraka hata baba yako anaweza kubariki kwa kukuambia maneno ya kukutakia majaliwa mema.Hata wimbo wa taifa unabariki nchi na watu wake.Nao ni udini?Hutoafautiana sana na avatar yako.
 
Lema Godbless may God bless you! Win the case and let yo'afflictors be put to shame!
 
Iko hivi:Serikali iliweka mapingamizi matatu katika rufaa ya Lema,mahakama katika uamuzi wake mdogo (ruling) ilichokifanya leo baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili,ni kuyatupilia mbali ,mapingamizi mawili(dismissal)na kulikubalia moja(uphold).Matokeo ya kulikubali pingamizi moja ni kwamba to some extent rufaa ya Lema ilikuwa na matatizo lakini yanayorekebishika(curable defects).Hivyo Mahakama kwa kuzingatia misingi ya haki imeamua kuiondoa rufaa ya Lema Mahakamani lakini ikatoa nafasi ya kuirudisha tena(The Court of Appeal has decided to struck out the appeal with leave to re-file).Kwa kuwa ruhusa ya kurudisha rufaa imetolew,mahakama ikaona ni vema zitolewe siku 14 tu ili makosa yaliyobainishwa yarekebishwe na rufaa irudishwe.Rufaa ikisharudishwa mahakamani ndani ya siku 14 itapangiwa tarehe nyingine kwa kuzingatia ratiba ya Mahakama ya rufaa.

======

Umefafania vizuri. Lakini sasa tueleze ina maana gani kwa ubunge wa Lema. Mahakama ilimvua, sasa mahakama ya rufaa kwa uamuzi huu, inamaanisha nini?
 
======

Umefafania vizuri. Lakini sasa tueleze ina maana gani kwa ubunge wa Lema. Mahakama ilimvua, sasa mahakama ya rufaa kwa uamuzi huu, inamaanisha nini?

Uamuzi mdogo(ruling) haukugusa rufaa,yalikuwa ni mapingamizi ya kuzuia rufaa(preliminary objections).Kwa uamuzi wa leo ina maana hakuna mapingamizi kuhusu rufaa,njia ni nyeupe kwa Lema kuleta rufaa iliyorekebishwa kwa nujibu wa uamuzi.Mambo yangekuwa mabaya zaidi kwa Lema kama wangeondoa rufaa moja kwa moja bila kutoa muda wa kuirudisha(striking out with no leave to refile)au kama wangeitupilia mbali(dismissal).Hivyo basi,kwa uamuzi huo,cha kufanya ni kuirudisha rufaa ndani ya muda uliowekwa,na la msingi zaidi ni kwa Mawakili kutorudia tena makosa mengine ambayo kwayo yanaweza kusababisha mapingamizi mengine mabaya zaidi.Hivyo rufaa ya Lema itasikilizwa kama ilivyopangwa.
 
Kukosekana kwa mwakilishi wa wananchi waliomchagua kwa kura nyingi, kwa muda mrefu hivi kwa jiji kama Arusha, nadhani inabidi iwe fundisho kwa chaguzi zijazo. Ni mara ya pili wakimfanyia mbunge wa upinzani faulo, wa kwanza alikuwa Makongoro Nyerere alipochaguliwa kuwa mbunge wa Arusha mjini 1995 kwa kupitia chama cha NCCR-Mageuzi enzi zile kikiwa chama cha upinzani hasa.
Kuna baadhi ya matatizo/kasoro hutokea nyakati za uchaguzi lakini kunapaswa kuwe na angalizo kuwa endapo kuna haja ya kwenda mahakamani, basi muhusika mkuu (mgombea aliyekosa ubunge) ndiye awe shahidi/mlalamikaji wa kwanza mahakamani.
 
Who is Lema kwani?????? Kwanini habar yake ipewe mvuto. KUna mambo mengi sana ya kuandika na yenye uzito..siyo habari kama hii!!

Kama haina uzito imekuwaje ukachangia? basi utakuwa aidha bonge la mnafikia ama hujui unachoandika
 
Big up kamanda kesi hii ni ya kupika haina kichwa wala miguu, as always kimbunga kipo pale pale, hata wapige sarakasi vp.

  • :target:
 
Hatimaye leo ndio leo kwa hukumu kwa aliyekua mbunge wa Arusha Mjini bwana Godbless Lema ni leo na ulinzi mkubwa kuimarishwa kwa wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo ( Chadema)! kwa wale watakao kwenda mahakamani tunaomba mtupe Updates!

Souce: Gazeti la Majira!
unajua kwa nini waliamishia Dar?
 
Lema Godbless may God bless you! Win the case and let yo'afflictors be put to shame!

si unaona hata majina watu wanayowapa watoto,wengine wanwahita watoto muhahid,wengine maruahani(maruane), na mengine yanayoshangaza.wenzao wana mwita Godbless, kila likiitwa linadariki ukoo na uliyemwita.
 
Je wajua kuwa Jaji RWAKIBALIRA baada ya kuhukumu kesi ya Lema kule Arusha ajawahi kutoka kitandani?Yupo hoi bin taabani Nyumbani kwake...Kapelekwa India olaaaaa.
 
jamani wadau walioko mahakamani 2naomba mtujuze tafadhalini xna


MINJA MAN Fuatilia topic kwa makini, taarifa unayoihitaji iko wazi kama inavyoonekana hapa chini toka kwa Yerico Nyerere.

Ruling tayari, mapingamizi 2 yametupwa, moja limekubaliwa, lakini kwamba in 14 days kasoro irekebishwe na kesi ya msingi iendelee
 
Je wajua kuwa Jaji RWAKIBALIRA baada ya kuhukumu kesi ya Lema kule Arusha ajawahi kutoka kitandani?Yupo hoi bin taabani Nyumbani kwake...Kapelekwa India olaaaaa.
ya kweli aya mkuu au
 
Majaji wanahitaji busara ya kawaida tu kwani kwa namna yoyote Arusha haiwezi kwenda CCM. Wasipomrudishia ubunge wake, wananchi wa Arusha watafanya hivyo, tena kwa kishindo.

Majaji hawaaangalii utashi wa kisiasa wanafuata sheria.
 
Huenda kilio cha Lissu kiko sahihi[/QUOTE

Kama hadi leo wewe ni miongoni mwa watu, ofcourse wachache, wasioelewa na kuona ukweli ktk hoja ya Tundu juu ya uteuzi wa majaji, tena kwa ushahidi mzito ambao hawajaweza kukanusha, basi kuna matatizo makubwa.

So nini kifanyike juu ya hao wateuli wa Rais? Katiba ya nchi inasema nini Rais anaposhindwa kuilinda katiba aliyoaapa kuilinda ?
 
Iko hivi:Serikali iliweka mapingamizi matatu katika rufaa ya Lema,mahakama katika uamuzi wake mdogo (ruling) ilichokifanya leo baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili,ni kuyatupilia mbali ,mapingamizi mawili(dismissal)na kulikubalia moja(uphold).Matokeo ya kulikubali pingamizi moja ni kwamba to some extent rufaa ya Lema ilikuwa na matatizo lakini yanayorekebishika(curable defects).Hivyo Mahakama kwa kuzingatia misingi ya haki imeamua kuiondoa rufaa ya Lema Mahakamani lakini ikatoa nafasi ya kuirudisha tena(The Court of Appeal has decided to struck out the appeal with leave to re-file).Kwa kuwa ruhusa ya kurudisha rufaa imetolew,mahakama ikaona ni vema zitolewe siku 14 tu ili makosa yaliyobainishwa yarekebishwe na rufaa irudishwe.Rufaa ikisharudishwa mahakamani ndani ya siku 14 itapangiwa tarehe nyingine kwa kuzingatia ratiba ya Mahakama ya rufaa.

Mkuu asante kwa kutupa ufafanuzi. inaonekana unafahamu sheria vizuri. Hebu tutolee dondoo kidogo ya hayo makosa na je ni nani ameyafanya au kuyasababisha?
 
IMG-20121108-WA0004_thumb1.jpg
Jopo la Majaji likiwa tayari kuanza kazi
hili si jopo la majaji...majaji hapo walikuwa bado hawajafika nafikiri hao ni mawakili
 
Leo ni leo kusuka ama kunyoa Court of Appeal, DAR kuhusu RULING ya pingamizi zilizotolewa na upande wa mjibu rufaa!

Updates..

Ruling tayari, mapingamizi 2 yametupwa, moja limekubaliwa, lakini kwamba in 14 days kasoro irekebishwe na kesi ya msingi iendelee







IMG-20121108-WA0007_thumb2.jpg
Godbless Lema akiwasili katika viwanja vya Mahakama ya Kuu jijini Dar leo.
IMG-20121108-WA0006_thumb1.jpg
Wapenzi wa Chadema wakimlaki Mhe. Lema mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mahakama leo.
IMG-20121108-WA0004_thumb1.jpg
Jopo la Majaji likiwa tayari kuanza kazi.
IMG-20121108-WA0003_thumb1.jpg
Kutoka kushoto, Henry Kileo, Nuru Ndosi na Mhe. Godbless Lema wakiwa mahakamani leo.
IMG-20121108-WA0002_thumb1.jpg
Henry Kileo akiwa ndani ya ukumbi wa Mahakama Kuu, Dar es Salaam.
IMG-20121108-WA0005_thumb1.jpg



Ish mbona picha ya 4 wamekaa chaggaz tupu. Is it a coicedence or planned
 
Back
Top Bottom