Rugemalila aitaka Benki Kuu iwataje watu wote waliopata mgawo wa Escrow. Gavana asita, aomba ruhusa ya Mahakama awataje

Ruge anatapa tapa
Angejikita katika kupangua kesi yake,ingeweza kumsaidia zaidi kuliko kujaribu ku 'crowd the deck' ili wafe wengi
Kwa hiyo wewe hupendi,acha Mafisadi yote yafikishwe Mahakamani.

Tena wengi wanatoka CCM .
 
FRESHMAN,
Kwa nini alilipwa na pap ilihali huzo pasa zilikuwa ni za Iptl kama mwana hisa , na pap alitoa sh ngapi kuinunua hiyo iptl


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hivi huyu mzee yupo haya magereza yetu kweli. Aliingia amekonda lakini sasa hivi amenenepa!!
 
Siku Lugola naye akiomba kutaja aliyekuwa amemtuma Kukopa hizo tr ndipo tutajuwa maana ya ile kukata mauno mbele ya kadamnasi
 
FRESHMAN,
Basi arudishe hilo hela PAP, maana PAP hawawezi kutoa kisicho chao,
Mengine kwa sababu kesi bado inaendelea na nyamaza
 
Pole Tata Ruge! Kwanini usiuseme ukweli unaoujua juu ya waliochota fedha za wananchi? Sio sahihi sana kukaa na Jambo ambalo wewe unaliona Siri ilihali kwa wengine lipo wazi! Kama Havana wa bot anayajua majina Basi siyo Siri Tena!

Wataje Tena kwa sauti kwani naamini una ushahidi wa kutosha! Huna unaloliogopa Wala kupoteza Bali kuwataja hadharani itakusaidia kuutua mzigo mzito ulioubeba moyoni na huenda ukapata nafuu ya ugonjwa wa moyo! Wataje hata Leo ili historian ikuhukumu kwa haki!
Kwa kisukuma kuna msemo unatumika kuwang'ong'a wale wanaojiona ni miamba wa kuwashauri wenzao wafanye ambalo hata wenyewe hawawezi kulifanya (ISAMILA BANYI).
 
babu M,
Stress wengine huwanenepesha!

Actually mtu mwenye kuwa na stress halafu akanenepa ni hatari zaidi kiafya ukizingatia na umri wake huyo mzee Rugemalira!

Mwenyezi Mungu aendelee kumtia nguvu na kumsaidia kuuvuka huo mtihani salama arudi nyumbani salama anendelee na maisha yake na wajukuu zake.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee kama Ruge na kina Kitilya n.k wanatakiwa kuwa kulelewa na kuwa na diet maalumu yaani wanatakiwa kuwa na milo maalumu kutokana na umri wao hata kama hawatakuwa na changamoto za kuumwa magonjwa yasiyo ambukiza,

sasa sijui kule magerezani huwa wanazingatia hayo?!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kisukuma kuna msemo unatumika kuwang'ong'a wale wanaojiona ni miamba wa kuwashauri wenzao wafanye ambalo hata wenyewe hawawezi kulifanya (ISAMILA BANYI).
Najua unatoka kabila teule na Kanda pendwa! Na usisahau kushauri ni fani na inasomewa ili uwe mbobezi na hata rais anao washauri japo hupuuzia analoshauriwa kwa kiburi na jeuri ya kikabila chake!

Wenye fani za kushauri hatushauri kile tusichokiweza bali yanayowezekana kwa Kila mshauriwa! Ruge ana maamuzi ya kufanyia kazi ushauri anaopewa na sidhani Kama ana kiburi Cha kisukuma!
 
Back
Top Bottom