Rostam, Mkapa kuungana kampeni za CCM Igunga

Rostam, Mkapa kuungana kampeni za CCM Igunga



*Wadai anakwenda kuvuna fedha
*Wakumbusha yaliyomtokea Temeke


Na Gladness Mboma

SIKU moja baada ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa CCM kumpitisha Rais Mstaafu Bw. Benjamin Mkapa kwenda kuzindua kampeni za chama hicho katika jimbo la Igunga, viongozi wa vyama vya upinzani vinavyoshiriki kinyang'anyiro hicho wamesema kiongozi huyo mstaafu anakwenda jimboni humo kuvuna aibu na yatampata kama yale yaliyompata Jimbo la Temeke kwenda kumnadi Bw.Cisco Mtiro mwaka 1996.

"Mkapa hana ubavu wowote wa kufanya aende Igunga kuzindua kampeni za CCM, kwa kuwa mikataba yote mibovu ya madini imesainiwa chini ya uongozi wake wakati mgombea anayeenda kumnadi Dkt. Dalaly Kafumu ambaye ni Kamishna wa Madini wa Wizara ya Nishati na Madini alikuwepo pia katika kipindi hicho.

"Mwaka 1996 Bw. Mkapa alienda Temeke wakati wa uchaguzi mdogo kumpigia debe Bw.Mtiro aliyekuwa anagombea na Bw. Augustino Mrema, lakini aliishia kuzomewa huku Mrema akiitwa ndiye Rais," alisema msemaji wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Erasto Tumbo.

Katika uchaguzi huo Bw. Mrema aliibuka kuwa mshindi kupitia tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi.

Naibu Katibu Mkuu Bara wa CUF, Bw. Julius Mtatiro na Msemaji wa CHADEMA, Bw. Erasto Tumbo wakizungumza kwa nyakati tofauti walisema kuwa Bw. Mkapa ushawishi wake uko kwa watu wa kimataifa na si kwa watu wa kawaida.

"Kwenda kwake Igunga ni kwenda kusafisha aibu ya CCM, lakini ningekuwa ni mimi ningekataa kupokea zigo ilo kwa vile wanakwenda kujitia aibu na kwa nini aende maali CCM hawatakiwi haoni kama anaenda kuaibika,"alihoji, Bw. Tumbo.

Alisisitiza kwamba kama Bw. Mkapa amekubali kwenda Igunga anatakiwa awe tayari kukabiliana na aibu atakayoikuta kuanzia yeye na serikali yake ya CCM.

"Leo Mkapa analetwa kuja kumnadi Dkt. Kafumu. Kafumu yuko Wizara ya Nishati na Madini kwa hiyo hawezi kukwepa lawama za kuua sekta ya madini na kuwafanya Watanzania wawe masikini ndani ya nchi yenye rasilimali nyingi," alisema.

Alisema Dkt. Kafumu kashindwa kutetea hata wafanyakazi wa Tanzania wanaofanya kazi kwenye makampuni ya madini huku wakilipwa sh. 600,000 wakati wafanyakazi wa kigeni wakilipwa mamilioni ya fedha kwa kutumia dola.

Bw. Mtatiro alisisitiza kwamba Bw. Mkapa kama alivyo Kafumu wote ni sehemu ya uongozi uliofikisha sekta hiyo ya madini maali pabaya kwa muda mrefu na wamechangia kudhoofisha uchumi wa nchi, hivyo hawawezi kuwadanganya wana Igunga.

Bw. Mtatiro alimtupia tuhuma nyingine kwa kudai kuwa wakati wa uongozi wake hakuchukua hatua dhidi ya biashara zisizo salama na hatari kwa usalama wa urais Ikulu na nchi, ambapo alitolea mfano kashfa kama ya Meremeta, TANGOLD na Kiwira na kusisitza kwamba siyo msafi.

Alisema kuwa CCM ni wanafiki walimshinikiza Bw. Rostam Azizi ajiuzulu ati kwa sababu anahusishwa na ufisadi, baada ya Bw. Rostam kujiuzulu wanampeleka Bw. Mkapa kujenga heshima ya CCM.

Juzi Kamati Kuu y CCM ilimteua Dkt.Kafumu kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo hilo la Igunga katika kikao kilichofanyika chini ya Mwenyekiti Rais Jakaya Kikwete, ambapo kamati hiyo ilimteua Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Bw. Benjamini Mkapa kuzindua kampeni za uchaguzi huo.


 
Mzee wa kokoto ndani ya Igunga, tusubiri tuone, asije akageuzwa vumbi
 
Nina wasi wasi Mkapa badala ya kuokoa jahazi atalizamisha huyu, maana si msafi hata kidogo.
 
Hiki chama kama hakitaangaliwa kwa macho mawili na watanzania kitasababisha vurugu sana 2015. kipo tayari kutumia mbinu yoyote chafu ili kushinda kura. kimeamua kumtumia fisadi waliyeMfukuza wenyewe na fisadi naye yuko tayari kutumika kama toilet paper na wakimaliza kumchambia wanamfurash na kuendelea tena na kampeni za kujivua gamba.

Kwa hiyo kwa msimamo huu Nepi hatakiwi Igunga na ndiyo mwisho wake wa kuwangolea mafisadi na ndiyo mwisho wa kujivua gamba tena.

Nadhani kwa uchafu huu chadema wa focus zaidi kwenye harakati za kuwaelimisha watu juu ya dhuluma wanazofanyiwa na ccm kwa kundanganywa kwa chmvi na kanga za msimu. Wamchane tu huyu fisadi kwa kuwaelezea namna alivyopata huo utajiri kwa wizi wa mali zetu kupitia ccm. Haijalishi hata kama cdm itashindwa huu uchaguzi lakini matunda yake yatapatikana 2015
 
Mkapa1(12).jpg

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa​


headline_bullet.jpg
Aambiwa ni mchafu asiyestahili kusimama jukwaani
headline_bullet.jpg
Kafumu naye apigwa kombora lake, ajibu mapigo
Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemteua Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, kwenda Igunga kuzindua kampeni za chama hicho za uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo hilo unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2, mwaka huu, Chama Cha Wananchi (CUF) kimesema kiongozi huyo mstaafu amezingirwa na kashfa nyingi hivyo si mtu sahihi kusimama jukwaani katika kampeni hizo. jana kutoka Igunga, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Tanzania Bara, Julius Mtatiro, alisema Mkapa ni kati ya marais walionufaika na sekta ya madini, inayosimamiwa na mgombea wa CCM katika kinyang’anyiro hicho, Dk. Peter Kafumu, ambaye pia ni Kamishna wa Madini nchini.

Mtatiro alisema tambo za CCM katika kinyang’anyiro hicho, zinaonyesha namna ambavyo kisivyokuwa makini kwa kuwa Mkapa kama kada wa CCM, alijimilikisha kinyemela mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira kwa bei ya kutupa. Mkapa anadaiwa kuuchukua mgodi huo kwa kulipa Sh. milioni 70, badala ya Sh. milioni 700 alizotakiwa kulipa.Hata hivyo, taarifa zaidi zinaeleza kwamba wakati Mkapa akijimilikisha kwa bei chee, mgodi huo ulikuwa na thamani ya zaidi ya Sh. bilioni nne. Mkapa anadaiwa kujimilikisha mgodi huo kupitia kampuni ya ANBEN kwa kushirikiana na aliyekuwa waziri wake wa Nishati na Madini, Daniel Yona. Hata hivyo, Julai mwaka 2009, Serikali ilitangaza kuuchukua mgodi wa Kiwira na kwamba ingeanza mchakato wa kupata utaratibu wa kuuendesha mradi huo kama ilivyokusudiwa, ikiwamo kuingia mkataba wa uendeshaji na kampuni itakayopewa mamlaka ya kujenga na kuundesha.

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alitangaza uamuzi huo bungeni, huku akieleza kuwa chini ya mkataba wa uendeshaji, mkandarasi atapewa jukumu la kujenga uwezo wa mashirika ya Shirika la Madini la Taifa (Stamico) na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ili yamiliki na kusimamia mradi. Serikali ilitangaza pia kuanza mazungumzo na Serikali ya China iliyoanzisha na kuendesha mradi huo, ili kupata mkopo wa kufufua mradi huo na kuhakikisha uzalishaji wa umeme wa megawati 200 ungeanza mapema, lakini hakuna uwekezaji uliofanyika hadi sasa.
Hata hivyo, serikali haikukanusha wala kugusia tuhuma zinazomwandama Mkapa kwamba alikuwa mmiliki wa mgodi huo.
Badala yake, ilielezwa kwamba baada ya kampuni ya TanPower Resources (TPR), kuendesha mgodi wa Kiwira chini ya jina la KCPL, mwanahisa mmoja kati ya watano ambaye ni ANBEN Limited yenye hisa 200,000 alijitoa. ANBEN ilidaiwa kumilikiwa na Mkapa na mkewe ambayo nayo ilishatangazwa kufilisiwa. Wanahisa wengine waliokuwa na hisa TPR ni DevConsult International Limited, Universal Technologies Limited, Choice Industries Ltd na Fosnik Enterprises Ltd.

Ujenzi wa mgodi wa Kiwira ulifanyika kati ya mwaka 1983 na 1988 kwa gharama ya Sh bilioni 4.29 kwa ushirikiano wa Tanzania na China na Oktoba 1988 iliundwa kampuni ya KCML, ikiwa ni kampuni tanzu ya Stamico kwa ajili ya kuendesha mgodi huo. Makaa ya mawe yalitumika kuzalisha umeme kwa mgodi wenyewe na kuuzwa kwa kiwanda cha saruji cha Mbeya na cha karatasi cha SPM Mgololo huku ziada ya umeme ikiuzwa Tanesco.

“Mkapa ni kati ya marais waliotumia sekta ya madini kujinufaisha yeye mwenyewe kama rais wa nchi na kujijengea utajiri kupitia madini ya Watanzania,” alisema Mtatiro.Mtatiro alifafanua kwamba: “Leo Mkapa analetwa kumnadi Dk. Kafumu ambaye ni mmoja wa watu wanatumika kuua sekta ya madini na kuwafanya Watanzania wawe maskini wa kudumu ndani ya nchi yenye rasilimali hizi nyingi.”

Alimshambulia Dk. Kafumu kwamba ameshindwa kuisimamia vyema sekta hiyo kwa manufaa ya Watanzania na badala yake, imeendelea kuwanufaisha wageni. “Mkapa si msafi kama alivyo Kafumu, wote wametumika kuua uchumi wa nchi hawawezi kuwadanganya watu wa Igunga,” alisema Mtatiro. Alisema hata mishahara ya baadhi ya wafanyakazi wa Kitanzania wanaofanyakazi migodini ni midogo ikilinganishwa na ile ya wageni wanaolipwa kwa Dola ya Marekani, jambo ambalo kama Kamishna wa Madini ameshindwa kulisimamia.
Tangu alipozushiwa tuhuma hizo na Mbunge wa zamani wa Vunjo (CCM), Aloyce Kimaro, Mkapa aliamua kukaa kimya hadi leo.

DK. KAFUMU AMJIBU MTATIRO

Dk. Kafumu alipoulizwa na NIPASHE kuhusiana na tuhuma zilizotolewa na Mtatiro dhidi yake, alisema hazina msingi wowote kwa kuwa majukumu ya Kamishna wa Madini, ni kusimamia sheria zinazoongoza sekta hiyo, sera, kutoa leseni, biashara ya madini na kumshauri waziri.
“Unapozungumzia ajira hilo ni suala ambalo lipo nje yangu kabisa, wala mikataba mimi hainihusu, mimi nasimamia sheria kuhakikisha zinafuatwa na wale wanaowekeza kwenye madini, labda Kamishna wa Madini anaweza kuingia kwenye tuhuma hizo kama sheria za nchi zitabadilishwa na kumwongezea majukumu,” alisema Dk. Kafumu.

Alisema kuna tuhuma zimeandaliwa dhidi yake na kwamba ni mambo anayoyategemea hasa kutoka kwa wapinzani wake wa kisiasa, lakini akatahadharisha kwamba waelewe kwanza majukumu ya kazi yake. Uchaguzi wa Igunga unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Rostam Aziz, aliyejiuzulu wadhifa huo pamoja na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya taifa (NEC) ya CCM kupitia Mkoa wa Tabora Julai 13, mwaka huu, kwa kile alichoeleza kwamba ni kuchoshwa na siasa uchwara, fitina na kuandamwa ndani ya chama hicho. Kampeni za uchaguzi huo zinatarajiwa kuanza Septemba 7, mwaka huu baada ya kufungwa kwa zoezi la kuchukua fomu za kugombea litakalositishwa Septemba 6.

Kamati Kuu ya (CC) ya CCM ilikutana jijini Dar es Salaam juzi chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, na kumteua rasmi Dk. Kafumu kugombea kiti hicho na pia kumkabidhi Mkapa jukumu la kuzindua kampeni za CCM za kumnadi mgombea huyo. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC ya CCM, Nape Nnauye, alisema kuwa CCM ilimpa Mkapa heshima hiyo kama Mwenyekiti Mstaafu wa chama hicho.

IPPMedia


 
Mkapa hawezi kwenda huko....kawanyamazia kwa muda mrefu,wamem-humiliate kwa muda mrefu,na alibaki kusema "wanadhani kuongoza nchi ni lemama",sasa yamewakuta ndo wanamhitaji...kamwe hawezi kwenda!
 
Kwa sababu alijenga barabara kwa kiwango cha lami akichanganya na politics.wananzengo watapigia CCM
 
Kwa mtazamo wao CCM walifikiri Mkapa ndiye msafi na kukabidhiwa dhamana ya kuipeperusha vema bendera ya CCM Igunga lakini hali imeshaanza kukwaa kisiki.
 
Hiyo ndo siasa ya tanzania. Ataweza kwenda na wote tukabaki midomo wazi.ila akienda atakuwa amejidhalilisha sana maana kama wengine waliotangulia wamesema naye si msafi. Tulishaanza kusahau mabaya yake kwa kujaribu kulinganisha na madudu ya ****** na kudhani ya mkapa yana afadhali. Hivyo kwa kuonekana kwake igunga itakuwa ni kujidhalilisha tuu mzee huyu. Nakumbuka alisha wahi kusema kuwa hataki kujihusisha na siasa na aachwe apumzike. Sasa kulikoni anarudi ulingoni.
Laiti ningekuwa mkapa nisingedhubutu kuonekana igunga.
 
Huo ni unafiki wa CCM, na wanakula matapishi yao tena yale yaleee, du hii nchi chini ya CCM hakuna maendeleo kabisa shime wananchi tuachane na CCM hii. Hata hawa watu ambao bado wanashabikia CCM siju hamnazo
 
Ccm ni wanafiki. Wanaogopa kivuli cho.
 
kwa taarifa zilizopatikana hivi punde mkapa haendi igunga'kazi ipo
 
Yaani kweli haya magamba nibalaa huyo ndio msafi huko kwao,mbona wanachemka?
 
Mnafik ni wewe, RA anapendwa Igunga kuliko kiumbe yoyote. Kafanya makubwa huko kuliko mbunge yeyote wa Tanzania.

Heri mfungo umeisha. Inaelekea ulikuwa hupati glucose ya kutosha mwilini. Hivyo ubongo ulikuwa umetindia!! Labda baada ya Ramadhani akili itakuja kidogo!!
 
Dr kafumu hawezi siasa.wapinzani wakishindwa hapa basi tena.ila ndo demokrasia
 
Masikini Mzee MKapa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa nini ameamu kuingia kwenye huu mtifuano kati ya wananchi na genge la mafisadi sugu nchini?????????? Hivi atatoka salama kweli huko bila ya Wana-Igunga kumtifulia mbovu kweli?????????

Duuhhhhhhhhhhh, hebu subiri kwanza ya zamani yaliyolala yatakavyoamshwa upyaaaaaaaaa tena hapa.Mimi nisingemshauri akaingie kuogelea haya maji mtifuano ya sasa, mara mia angejipumzikia tu mzee wa watu!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom