Njilembera
JF-Expert Member
- May 10, 2008
- 1,496
- 607
kwa nini wanamuita gamba?
ina maana ccm wako tayari hata kutumia majambizi kushinda majimbo sio
na huyu Rostam alisema kahacha ccm hapa inakuwaje?./QUOTE]
Ninakubaliana mno na wewe! CCM kuliko wakose lile jimbo, wako tayari kuwatumia mafisadi wahonge wapiga kura! CCM ilikuwa na nafasi kubwa ya kujiondoa katika mitego na makwapa ya mafisadi (magamba) lakini kinara wao, Kiongozi Mkuu na Jemadari wa Taifa hili, ameshindwa na amekwenda kumpigia magoti Rostam amsaidie! Nafasi nzuri CCM inaipoteza kirahisi mno.
Hofu ya kupoteza jimbo mmoja, hofu ya kushindwa na upinzani umempa CCM kizungu zungu naam, na sasa tutaona mengine!
Habari niliyosoma Nipashe ya leo imenipa matumaini! Benjamin Mkapa na mgombea wa CCM wanatuhumiwa tayari kwa kuiangamiza nchi katika mikataba ya uchimbaji madini! Sinema nzuri iko mbioni kuonyesha! SAA YA UKOMBOZI NI SASA! Sikuwahi kuamini usemi huu, lakini naelekea huko sasa.
JF members mchana mwema na Idd Njema