Sababu za kwenda Igunga Mkapa anazo, na sababu za kutokwenda Igunga pia zipo.
Sababu za kwenda: Usalaama wa viongozi waliostaafu lakini wakiwa na kashfa zinazoweza kupelekea kuvuliwa kinga za kushitakiwa, unategemea CCM kudumu kuwa madarakani hadi wafe. Mkapa anatamani sana aiokoe CCM huko Igunga, kwasababu kupoteza jimbo la Igunga ni maandalizi makubwa ya CCM kupoteza majimbo mengi na hata hadhi ya chama tawala. Kwa sababu hiyo sasa hivi Mkapa ana kibarua cha kufanya maamuzi ya kwenda au kutokwenda.
Sababu za kutokwenda: Hakuna mtu anayependa kuumbuliwa, au kukumbusha makosa yake ya siri. Hasa mtu alipata kuwa katika nafasi ya kuheshimiwa, kuabudiwa, kupigiwa makofi, kushangiliwa, kutukuzwa, kuimbiwa nyimbo za sifa, kuongoza vyombo vya ulinzi, nk. Mtu wa namna hiyo huona aibu kuuuubwa sana kuikabili hadhira iliyompa hizo heshima na sasa hadhira hiyo inafahamu kuwa kumbe alikuwa fisadi tu. Inatisha! Inaweza kumuangusha mtu kwa BP na kufa!
Vilevile, tukizingatia kuwa sasa hivi upinzani Tanzania umeshakuwa na nguvu nyingi za kusema na kupata taarifa za siri ili kuthibitisha maelezo yao. Hili linaweza kumtisha mtu yeyote, hata rais Bush mwenye moyo mgumu kujitokeza mbele ya mazingira ya namna hiyo. Kwahiyo, hakuna anayejuwa Mkapa ataamuaje. Ila mwisho wa siku ni yeye ndiye atakayeamua kuokoa chama chake, au kujiepusha na aibu ya kukumbushwa historia yake ama kuibuliwa makubwa zaidi yaliyokuwa yamebakizwa.