Nimegundua kumbe adui yetu namba moja kama taifa ni ujinga, na ndani ya ujinga huo kimezaliwa kitu kinaitwa udini. Ninavyofahamu ni kuwa jambo la dini ni suala binafsi kati ya mtu na muumba wake( kama ana amini kuwa yupo) ndiyo maana katiba yetu pamoja namapungufu inaelaza wazi jambo hili, Ibara 3 (1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia isiyokuwa na dini..., Ibara ya 19 (2) Kazi ya kutangaza dini,kufanya ibada na kueneza dini itakuwa jambo huru la hiari la mtu binafsi..... .Leo hii tunapoona watu wanaleta hisia za udini kwa nia ya kuwagawa watz tunashindwa kuwaelewa. Jambo hili naliona ni mkakati mahsusi wa baadhi ya vyombo vya dola , ukiwa na nia ya kuwagawa watz kwa misingi ya dini ili wakose nguvu ya pamoja ya kukabiliana na genge la watawala.Natoa wito kwa wapenda nchi wote wasiingie kwenye mtego huu wa kidhalimu. Hakuna mtu yoyote katika nchi hii anayeweza kunufaika kimaendeleo kwa kuwa tu mtu anayetawala ni wa dini yake, tutapata maendeleo tu kwa kupata viongozi wazalendo wenye uchungu na nchi yetu. Watanzania tuamke tuache ulevi wa mawazo ya udini.