Mzee Mwanakijiji,
Naposema wahindi na waarabu wengi wana uraia wa nchi mbili ni kutokana na kile mnachomshutumu Rostam..Hakuna mhindi wala mwarabu mzawa wazazi wake waliyekwenda kuukana uraia wa nchi ambayo walitoka..Hata Nyerere hakwenda kuukana URwandiz ndipo tukawakubali watoto wake.. wala wazazi wake hawakuukana..
Mzee naona haujanipata vizuri. Nyerere hakuhitaji kuukana uraia wa Rwanda (kama alikuwa nao) kwani alikuwa ni raia wa Tanganyika kama Koloni (la uangalizi) la Mwingereza. Vivyo wote watu wote (wahindi na wengine) waliokuwa ndani ya koloni hilo wakiwa raia.
Nimefafanua kuwa sheria ilitangaza kuwa siku ya Uhuru wa Tanganyika wale wote waliokuwa raia wa Koloni la Tanganyika (maana yake ni raia wa Uingereza na Makoloni yake) wanakuwa raia wa Tanganyika. Hii ina maana kwa makusudi sisi tulikataa kuangalia uraia kwa sababu ya rangi au mahali mtu anatoka! Uraia ulikuwa very defined.
Sasa ikiwa hivyo unataka Rostam avuliwe uraia kwa kitu gani?.. kwa maneno ya Mtikila kuwa wazazi wake hawakuwahi kuwa raia?.. Mtikila ambaye hana ushahidi wowote zaidi ya chuki yake binafsi! Sii huyu aliyechukua fedha kwa Rostam!.. inawezekana anachofanya ni blackmail..
Hapana, Mtikila alisema kitu hicho Juni mwaka jana! Katika uchunguzi wetu pembeni ndio tumekutana na jambo hilo hilo na ndio tukarudia kuangalia alichosema Mtikila. Tulichojengea hoja ni kuwa sheria ilifuatwa kumvua uraia Ulimwengu na yule mwandishi wa Zanzibar kwanini isifuatwe kuhusu Rostam?
Mkuu watu kibao wanaifahamu familia ya Rostam toka enzi..Na kama huniamini mimi basi huu mjadala wala hauna maana zaidi ya kutafuta mchawi kwa ramli...Kifupi nenda kwao kafanye uchunguzi wako acha hizi habari za Ki nzi, fika mwenyewe uzungumze na wazee wa maeneo anayodai kisha rudi tupe ujumbe wa kweli na sii kum quote Mtikila..
Mzee hilo wala halina mjadala. Familia ya "Rostam" inafahamika Igunga na ndio nimefuatilia vya kutosha kabisa. Sisi siyo wa kwanza kuhoji hili kwa sababu unaposema "familia" ujue tunanzungumzia nini. Mtu huwi raia kwa sababu familia yako ina "historia" ndefu. Hapana, unakuwa raia aidha kwa kuomba, ndoa, au ya kawaida zaidi kwa uraia wa wazazi wako. Kama kuna mzungu ambaye alizaliwa tanzania, na wazazi waliokuwa Watanzania, mtoto huyo haitaji kuukana uraia wa wazazi wake, yeye ni Mtanzania!
Lakini kama kuna Waingereza wanaoishi Uingereza, halafu mtoto wao alikuja mdogo Tanzania na akakulia Tanzania, akazungumza Kiswahili n.k.. haina maana mtoto huyo ni Mtanzania!
Rostam ana makosa yake, rangi yake haiwezi kutumika kama sababu ya kutafuta Uraia wake kwani angekuwa Mmakonde tungeyasema yote haya ya wazazi wake walitokea Mzambique hawakuukana uraia wa huko...Wangapi weusi wamepimwa kwa kipimo hiki kama kweli huzungumzii rangi na asili ya Rostam?
Mzee hili la rangi ni wewe unalileta. Kuweza kuelewa anachofanya RA kinahusiana moja kwa moja na uraia wake; siyo nje ya hilo. Kama Jenerali (mweusi) alivuliwa uraia, kama Premji (mhindi) alivuliwa uraia, kama Ali Nabwa (mcomoro) alivuliwa uraia wake, kwanini iwe suala la rangi inapokuja Rostam?
Unataka kuniambia kuwa tusiguse uraia wa Rostam kwa sababu ni Muajemi? Yaani tuangalie sura yake kwanza kabla ya kusema si "raia"?
Huu ndio Ubaguzi unaozungumziwa kwani sioni sababu kabisa ya kumtafuta mchawi kwa rangi yake sawa na maamuzi ya kuwaua wazee kwa kudhaina ni wachawi..
Hili halina msingi.
Na unaposema Uraia wa Tanzania hautegemei kuzaliwa kwako ila kwa wazzazi wako una maana gani sikuelewi hata kidogo ikiwa mzazi huyo alikuwa akiishi Tanzania kabla ya Uhuru..Mkuu wangu kama ulivyosema hapo juu, Uraia wa mtu unaanza na siku ya Uhuru... kuzaliwa kwa wazazi wako sii sababu kabisa ikiwa walizaliwa nje au laa..
Nadhani hapa tunazungushana kwa jambo jepesi tu: Kuwa Raia wa Tanzania kunategemea uraia wa wazazi wako (haitegemei kama walizaliwa hapa au la). Kama wazazi wako ni Watanzania, wewe ni Mtanzania, na kama una uraia wa nchi nyingine ifikapo miaka 18 unatakiwa kuukana uraia ule mwingine vinginevyo unapoteza uraia wa TAnzania (ndiyo iliyotumika kwa Ali Nabwa).
Wazazi wa Rostam (sijasema familia, wajomba, shangazi, binamu au wakwe) hawajawahi kuwa raia wa TAnzania au Tanganyika. Sasa yeye Rostam kapata vipi uraia? Hilo ndilo swali unisahihishe. Kusema tusizungumzie, au kudai ni suala la rangi ni kukwepa hoja iliyopo mbele yetu.
Kama una habari kuwa RA wazazi wake ni Watanzania au walikuwa watanzania nisaidie tu kwani itazima mjadala huu mara moja! Je wazazi wa Rostam ni Watanzania? tangu lini?