Rostam awaparamia CHADEMA

Fortunately Rostam naye si muislam! Hili gazeti limetuabisha cc waislam. But why?

Huwa mnasemaga hivyo hivyo mkiona mambo yanakuwa ndivyo sivyo, kwani mnapodai Waislamu sasa wamefikia 1.5bn duniani kwa idadi huwa mnawatenga baadhi yao?
 
lkn mbona mwakyembe hakanushi yanayaonikwa na annur?

Una jinsi ya kukwepa kuwa umetumwa wewe...hivi una haibu kuongea non-sense words...........Hivi Rostam anaweza kukwepa kuwa ni muuhaji wa watu wetu? Nani kakutuma kwenye hii forum...Join January 2011 halafu unaingia na ujinga hapa......
 
May be Max was right to say "..religion is an opium to society"...I'm about to prove this.
 
Hili limekuwa genge la wapumbavu watupu. Mtu hata kichwa cha habari haweki, anaandika hisia zake halafu watu wanadandia. Kama sio upumbavu tuuiteje. Hebu asome mmoja wenu aone kama kuna mahala katetewa Rostam. Tatizo la forum kujaa vitoto vya shule!
 
sipendagi vijikazeti vyo vichochoroni vyenye waandishi pumba na mbumbumbu kama hcho kigazeti,.cpendi hata kukitaja jina ntakuwa naki-advertise eti!.
 
Me muislam bt haka kagazeti kana uhusiano na CUF na km 2navyojua sasa CUF ni CCM B so please al nur muctutie aibu waislamu kwa kununuliwa na fisadi km vipi jitangazeni km uhuru tujue km na nyinyi CCM C
LAANAT ALLHA kwa wale wote wanao watetea wa2 walodhulumu
 
Kawaambie wazazi wako wakufundishe kwanza kujichamba ili usiwe unatembea na kinyesi kisha ndio uje kujadili habari za Madrasa!

whats the reason of dissing my parent here? Ok , back to the topics.. You think is fair for all annur to defend Rostam Aziz? And why? Answer me please and never again put my parent in this discussion because you dont know me . Come on men!!! I wanna hear you .
 
Ama kweli naye haoni shida kabisa na anajigamba nchi jirani ya Kenya na Uganda si ndiyo uko mnapoiga visivyoigika bila kuangalia maendeleo ya nchi yenu,hivi kweli Uganda kuna kitu cha kujifunza kikubwa saana kwa mabadiliko ya Tanzania
Acha kutudanganya kama woote ni majuha
 
lkn mbona mwakyembe hakanushi yanayaonikwa na annur?

ndio hapo sasa. Huyu ndio kazi yake kulia lia, mara o wanamwaga pesa jimboni kwangu mara o wanataka waniuwe, acha tabia ya kujizushia mambo kutafuta huruma za wananchi, kama unaushahidi c upeleke mahakamani au muwahi yeye kabla haja kuwahi, MWAKYEMBE ACHA KULIALIA
 
ASHAWAHI KUDAI KUWA UKOO WAO NI MATAJIRI TANGU MIAKA 1850 A.D. MIAKA HIYO EPA,RICHMOND,KAGODA NA DOWANS HAZIKUWAPO. WALIKUWA NA UTAJIRI GANI ZAIDI YA KUUWA TEMBO NA FARU PAMOJA NA WATUMWA WAKISHIRIKIANA NA BABU YAKE AL ADAWI, TIPU TIPU?:embarassed2:
 
lkn mbona mwakyembe hakanushi yanayaonikwa na annur?

wewe muanzisha thread nawe ni kiazi tu... kwa hoja iliyopo hapo juu kwa nini usiweke hilo gazette la kipuuzi hapa tusome tupambanue wenyewe?? Maana wengine huwa hatuaribu hata THUMNI ya tigo kununua gazette hilo... na wewe uliyelinunua ni mshabiki wa habari hizo.

Kwanza inaonekana na wewe ni mshabiki kwa kuwa inaonyesha hukusoma habari iliyokuwa katika mwanahalisi... ukweli ni kuwa katika njama iliyoainishwa na Mwakyembe HAKUMTAJA MOJA KWA MOJA RA, bali alitaja wamiliki wa magari yaliyotumika na watu wengine kwa majina na siyo RA.

So Ar nuul sijui Al nuri na wewe wote wale wale.
 
ndio hapo sasa. Huyu ndio kazi yake kulia lia, mara o wanamwaga pesa jimboni kwangu mara o wanataka waniuwe, acha tabia ya kujizushia mambo kutafuta huruma za wananchi, kama unaushahidi c upeleke mahakamani au muwahi yeye kabla haja kuwahi, MWAKYEMBE ACHA KULIALIA

Natilia shaka upeo wako... ile habari iliyoandikwa katika mwanahalisi, ni barua iliyoandikwa kwa IGP. so kwa mantiki hiyo siyo kukurupuka tu, bali kafuata right channels... Wewe naona unafuata ushabiki tu... sina hakika umelipwa sh ngapi ila ningeweka hapa malipo yako watu wajue... lakini tambua utakula hiyo hela leo na itaisha kesho mpaka ukamlambe miguu tena huyo bwana wenu.
 
RA amesema yeye ni mwanasiasa makini na kamwe hababaishwi na wanasiasa uchwara.

Amesema maisha magumu kwa watanzania hayatokani na CCM, bali mfumo wa kidunia unaoendana na hali halisi ya sasa.

SOURCE: MWANANCHI PG2
Complete article.

MBUNGE wa Igunga,mkoani Tabora, Rostam Aziz amesema yeye ni mwanasiasa makini na kamwe hababaishwi na wanasiasa uchwara , ambao wamekua wakieneza maneno ya uongo na uzushi dhidi yake.

Akizungumza na wananchi wa mjini Igunga katika Viwanja vya CCM mjini Igunga jana, Rostam alisema kuna wanasiasa ambao kila kukicha, wamekuwa wakitoa maneno ya kuchafuana na kupakana matope.

Alisema hata hivyo , wanasiasa hao hawambabaishi.

Alisema mwanasiasa makini ni yule anayetoa hoja za ukweli na si anayetoa maneno ya kuhamashisha wananchi wafanye vurugu.

Aliwata wananchi wa jimbo hilo kuwaepuka watu hao kwa kuwa ni hatari kwa nchi.

"Hivi karibuni kumekuwa na chama cha siasga kinachoendesha propaganda na kupiga domo kwa kuwahadaa wananchi kwamba maisha magumu yanatokana na wao kuichagua CCM," alisema Rostam.

Aliongeza "watu hao ni waongo kwani maisha magumu hayatokani na CCM, bali mfumo wa kidunia unaoendana na hali halisi ya sasa."

Alisema kupanda kwa bei ya sukari na mafuta nchini, hakutokani na CCM na kwamba chama hicho hakina kiwanda cha sukari wala hakiagizi mafuta kutoka nje ya nchi.
Alisema hata nchi jirani Kenya na Uganda, nazo zimekumbwa na mfumuko wa bei ya bidhaa hizo ambapo bei ya sukari katika nchi hizo ni Sh2,000 kwa kilo sawa na Tanzania.

Alisema propaganda za kisiasa zinazoendeshwa na chama hicho ambacho hakukitaja kwa jina, zinalenga katika kuwapotosha watu.

Hata hivyo aliwataka wananchi kuyapuuzia maneno ya wanasiasa wa chama hicho kwa madai kuwa ni uongo.

Alisisitiza kuwa viongozi wa chama hicho ni waongo kuhusu madai wanayoyatoa.

"Nilikutana na Dk Wilibrod Slaa katika uwanja wa ndege wa Mwanza nikamuuliza kuwa nilisikia wakati ukihutubia wananchi wa Musoma kwamba Chadema mkichukua nchi mfuko mmoja wa saruji utauzwa Sh5,000 tu, lakini hakujibu," alisema Rostam.

Alisema kwa mtazamo huo aligundua kwamba maneno wanayozungumza Chadema ni ya kudanganya wananchi ili wawape ridhaa ya kuongoza nchi na si kuwaletea maendeleo kama walivyokuwa wakijinadi.

Alisema katika kipindi hiki kigumu, amegundua kwamba wananchi wa Igunga wana hali mbaya ya chakula na kwamba atahakikisha kuwa hawafi kwa njaa. Mbunge huyo aliwaomba wananchi wa Igunga kumuunga mkono ili afanikishe malengo yake ya kuwaletea maendeleo.

anajificha kwenye kichaka cha mchicha huyo
 
Back
Top Bottom