Rose Migiro Kafunikwa na Halima Mdee

Rose Migiro Kafunikwa na Halima Mdee

First thing first. Mimi sio mstaarabu na vilevile sio great thinker, but I don't afraid to give people a piece of my mind. This thread of yours stinks for the following reasons.

  • Kama unaleta mada akikisha kuwa kichwa cha mada na kile unachotaka kusema vinaendana. Kina Tundu Lisu and Lipumba wamefuata nini?
  • Vilevile akikisha mada yako ni kamili. Michango ya watu haiji kukamilisha mada kwani sio lazima tuchangie.
  • Pia ni lazima ufananishe vitu vinavyofanana, andazi kwa andazi
  • n.k n.k n.k

Kuna wanaopenda viungo waachie harufu yake, wasiopenda viungo wale vikavu vilivyo.
Hapa JF licha ya kuwa na mada nzitonzito, nyingine pamoja na umuhimu kuna kuweka radha fulani ya watu wanyooshe kidogo mbavu zao katika mapumziko ya weekend. Hatupo kwenye kuweka tesisi ya kuchambuliwa na instructors, kwani hapa ni kilima cha jopo la watu kuchangia mada, nyoosha kile uonacho kinakosekana.

Haijaletwa mada ya kuisoma kama kitabu tu, hapa ni kujadili, kilichopungua ongeza au jazia, hatima ya mada ndio ukamilifu wake, vinginevyo hatungechangia kama kitu kimekamilika.
 
First thing first. Mimi sio
mstaarabu na vilevile sio great thinker, but I don't afraid to give
people a piece of my mind. This thread of yours stinks for the following
reasons.

  • Kama unaleta mada akikisha kuwa kichwa cha mada na kile unachotaka
    kusema vinaendana. Kina Tundu Lisu and Lipumba wamefuata nini?
  • Vilevile akikisha mada yako ni kamili. Michango ya watu haiji
    kukamilisha mada kwani sio lazima tuchangie.
  • Pia ni lazima ufananishe vitu vinavyofanana, andazi kwa andazi
  • n.k n.k n.k

well said
 
Ok. Kwa hiyo kama nimekuelewa vizuri, kigezo ulichotumia hapo juu kuwalinganisha Asha-Rose Migiro na Halima Mdee ni "kiwango cha kutambulika kimataifa", au siyo?


La ajabu, hujaweka wazi mlinganisho wako wa wahusika hao wawili kutumia kigezo kama hicho, na hitimisho lako linaloendana na kigezo chako, zaidi ya kukiri kwamba Halima Mdee ni zaidi ya mkeo!

Kwa ufupi ujipange upya mkuu! Weka kwanza relevant analysis yako ya wahusika kulingana na vigezo au kigezo ulichoamua kutumia pamoja na ushahidi uliyo nao, ikifuatiwa na conclusion statement husika,siyo kukurupuka tu, sawa?

Mkuu!

Yaonekana yamekugusa sana. Tunaona mapovu yanakutoka mtindo mmoja. Hebu tuliza akili na ndio utaona kwamba Asha Migiro ali-proove failure UN. Kumbuka wenzetu kwenye nyanja za kimataifa hawajui kufanya kazi kwa ushikaji. Migiro alishindwa ku-deliver UN ilicho hitaji na hivyo kuamua kuachana na mizigo ya baba Mwanaasha.

Kwa kawaida watu wa UN hawaondoki kwa style ile aliyo ondokea Migiro. Unakwenda kumalizia kipindi chako cha kazi nje ya ofisi yako!!!! Yaani walimuona ile miezi iliyokuwa imesalia ilikuwa mzigo kwao kuwa naye pale UN.

Kifupi hakuwa na wala hana mchango wowote aliotoa ama kimataifa au ndani ya nchi yake na ndiyo maana Mh. Halima Mdee akaibuka kidedea kwa kutetea wananchi wake hasa kwenye eneo la rasilimali ardhi.
 
Kabla sijachangia lolote labda mnieleze tu huyu Asha Ros Migiro aliwahi kufanya jambo gani la maana? au je aliwahi hata kushind uchaguzi kwa kupigiwa kura na Wananchi, msiniletee habari za viti maalum au teuzi.
 
The world has two kinds of people, the ones with competence but no qualification and the the ones with qualification but no competence.Someone who is competent can perform like Halima Mdee unless Asha Migiro
 
Tukiondoa mapenzi kibubusa na siasa ukweli ni kwamba Asha Migiro alichemsha. Maana kama angefanya kazi vizuri haikuwapo haja ya kumuondoa kwenye unaibu katibu mkuu kabla ya katibu mkuu kumaliza muda wake. Nafasi hii ingetokea zama za Salim Ahmed Salim stori ingekuwa nyingine. Mlitegemea chaguo la bwana dhaifu liwe bora wakati anachagua watu wake kutokana na sababu anazojua mwenyewe? Hata apigiwe debe vipi hawezi kuwa rais wa Tanzania simply because ni mwanamke. Tumejifunza toka kwa Anna Makinda ambaye alitumiwa na mafisadi kumpiga kibuti Samuel Sitta baada ya kuruhusu bunge kuwa bunge badala ya genge la sasa la CCM ukiachia mbali wapinzani kuzidiwa namba.

Wewe acha hizo za hawezi kuwa rais sababu ni mwanamke. That's primitive!
Ni sawa na kusema mwanaume fulani hawezi chaguliwa urais sababu mafisadi papa wote ni wanaume.

Huyu mama mhukumu kwa ukilaza wake na si kwa jinsia yake.
 
Aisee! Rose Migiro vs Halima Mdee ni sawa na Range Rover vs. Toyota.

Sasa kama ni Halima Mdee vs mkeo, nadhani hii itakuwa Toyota vs San-Lg.

Naona hii post hujaielewa sababu Candid Scope hajaweka source yake.
Na wewe ungekuwa msomaji mzuri, ungekuwa na taarifa ya Forbes Most Influential Women in Africa. Tanzania imetoa two women, mmoja wapo ni Halima Mdee.
Forbes wanafahamu ukilaza wa Migiro ndio maana hawakumweka.

Ila tafadhali tuambie jambo hata moja la maana alilofanya Migiro kwa ujasiri wake. Tusaidie ili tusiwe tunamwona muuza sura tu kumbe mpambanaji.
 


Unaweza kunisaidia labda mada yako ilikuwa ina maana nyingine kwa sababu haya maelezo ni kutoka Forbes Magazine.

Mkuu, bora umemuuliza hili swali,manake Halima Mdee nani anayemjua katika medani za Kimataifa??? Mimi naona hii mada ni upuuzi tu! Huwezi kumlinganisha Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa UN na Mbg. wa Kawe. Hivi ni vichekesho!
 
Wewe acha hizo za hawezi kuwa rais sababu ni mwanamke. That's primitive!
Ni sawa na kusema mwanaume fulani hawezi chaguliwa urais sababu mafisadi papa wote ni wanaume.

Huyu mama mhukumu kwa ukilaza wake na si kwa jinsia yake.

Mkuu, wale waliosoma sheria UDSM (Department of Law, by then), na walifundishwa na DR. huyu, inabidi ndo watujuze ukilaza wake.
 
Mkuu, bora umemuuliza hili swali,manake Halima Mdee nani anayemjua katika medani za Kimataifa??? Mimi naona hii mada ni upuuzi tu! Huwezi kumlinganisha Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa UN na Mbg. wa Kawe. Hivi ni vichekesho!

Hawa ndiyo wale wale wanaodamuka asubuhi bila hata ya kwenda kunawa uso ili kutoa matongotongo, badala yake wanakaa kwenye keyboard na kuanza kurusha utumbo kama huu harafu bila hata aibu, wanaanza kuutetea.

Inasikitisha sana.
 
Kwa miaka karibu mitano nimekuwa nikikodolea macho list ya wanawake bora na maarufu duniani kwa kiwango cha kimataifa, pamoja na Rose Migiro kushika nafasi pekee akiwa kama mwanamke wa kwanza UNO kuparamia kiti hicho, lakini hakubahatika hata kushika nafasi ya 100 kati ya 100 bora. Nilijiuliza na kuishia kukaukiwa cha kuandika na kusubiria nafasi nyingine kwa mwaka unaofuata hadi ilipofikia kutompa nafasi kwa ingwe nyingine.

Halima Mdee, hajashika nafasi pekee serikalini zaidi ya ubunge kutoka kambi ya upinzani, lakini bungeni alivyoonyesha ushupavu usio wa kawaida hadi kuwashikisha adabu viongozi waandamizi serikalini imeleta matumaini mapya hadi kushuhudiwa na dunia ambayo imempa tuzo stahiki, na labda mwanamke kama huyu Mdee angepata nafasi ile adimu na ya pekee katika historia ya wanawake katika Umoja wa Mataifa huenda angeweza kuingia bora 100 kwa miaka aliyokaa Migiro United Nation.

Candid Scope uchambuzi wako huu una walakini mkubwa.........................unalinganisha nyanya na vitunguu kwa vipimo ambavyo hata wewe umekiri havina uhusiano.....................umesema Mdee hajabahatika nafasi kama ya Migiro kama wajua hayo sasa wapi na wapi kuwalinganisha? .......na ukaendelea kutoa hisia zako kuwa pengine angelifanya vizuri zaidi....................huna ushahidi wowote ule kwenye hilo zaidi ya kubashiri tu.

Kama unataka kuwalinganisha watajwa basi pitia rekodi zao bungeni tu....kwa vipindi ambavyo wametuhudumia khalafu waweza kuwalinganisha.................

umem'mwagia sifa Mdee kuhusu kuwashikisha adabu viongozi serikalini hujatueleza kivipi walishika adabu yao wakati cdm wanaendelea na maandamano ya kudai dhuluma zikomeshwe..........................kuna mgongano wa huu ujumbe wako na azma za cdm machoni pa umma.............upitie upya ujumbe wako na kurekebisha haya mapungufu ili tuweze kushawishika.....................am sorry about this if i have to mark this paper.......................you will not pass, may be after you have made major alterations.........

.jingine la kujiuliza ni kwanini Bank Moon alimtimua Migiro.....utendaji mbovu na afya yenye mgogoro ni baadhi ya sababu alizozitumia..................................

Kubwa pengine kuliko yote ni vigezo wanavyovitumia katika kupanga safu ya watu 100 mashuhuri duniani ni lazima vieleweke na wao hulenga nini.........na je huenda zoezi zima ambalo unajivunia nalo halitutendei haki nchi dhaifu kiuchumi kama yetu...................

.please do the needful..................our expectations now have gone up in terms of analytical threads like this one...............................ninafahamu presidential succession politics is behind this pithy narrative but let us do justice to all parties........................ninawakilisha mada.
 
Kwakweli kwa Rose Migiro kukosa kuingia kwenye 100 bora imeonyesha kabisa jinsi Tanzania tunavyopeana nafasi kwakuangaliana. Huyu mama tangia amerudishwa sijawahi msikia kitu cha maana amekifanyia jamii zaidi ya kushiriki makongamano ya starehe anayokaribisha.

Migiro na Mdee hawalingani but I bet our super hero Mdee angepata hizo chances za Migiro angeprove kuwa yeye ni nani. Wangapi wameingia bungeni kwamamiaka kibao hawajajituma kama Mdee? Nafikiri umefanya vizuri kumlinganisha ili Migiro ajione jinsi alivyo kiazi kinachosubiria nazi ikibusti kipate ladha
 
Mkuu, bora umemuuliza hili swali,manake Halima Mdee nani anayemjua katika medani za Kimataifa??? Mimi naona hii mada ni upuuzi tu! Huwezi kumlinganisha Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa UN na Mbg. wa Kawe. Hivi ni vichekesho!

Ndio maana kafananishwa kibongobongo, cha muhimu ni kufananisha exposure yake na mambo aliyoyafanya. Mbona ni hesabu ndogo sana
 
Hivi kweli kwenye diplomatic career ya Asha-Rose Migiro, huoni mazuri yoyote aliyofanya zaidi ya yale yanayoweza kukuridhisha nafsi yako? Dude you must have some serious problems, na sijui ni vigezo au juhudi gani alivyofanya Halima Mdee ambavyo vinakufanya hadi umuweke juu zaidi ya mkeo.

Kwako MIGIRO ndo zaidi ya mkeo?
 
Ndio maana kafananishwa kibongobongo, cha muhimu ni kufananisha exposure yake na mambo aliyoyafanya. Mbona ni hesabu ndogo sana

Kwa uchambuzi yakinifu hizi hesabu hazitalingana! hiyo mbona ni mantiki ndogo tu.
 
First thing first. Mimi sio mstaarabu na vilevile sio great thinker, but I don't afraid to give people a piece of my mind. This thread of yours stinks for the following reasons.

  • Kama unaleta mada akikisha kuwa kichwa cha mada na kile unachotaka kusema vinaendana. Kina Tundu Lisu and Lipumba wamefuata nini?
  • Vilevile akikisha mada yako ni kamili. Michango ya watu haiji kukamilisha mada kwani sio lazima tuchangie.
  • Pia ni lazima ufananishe vitu vinavyofanana, andazi kwa andazi
  • n.k n.k n.k

Nionavyo mimi akina mama wa kitanzania pamoja na usomi wao nadhani wana matatizo ambayo mpaka leo najiuliza nashindwa kupata jibu.
Angalia mama Mongera alivyoaibisha kule afrika kusini, mama Tibaijuka kule Kenya na huyu Migiro na hiyo ni mifano michache tu kuna wengine hawajulikani kutokana na kutotambulika machoni mwa watanzania. Nilianza kumjua mama Tibaijuka nikiwa chuo kikuu wkt wa research akawa anatupeleka mkoani kagera pesa nyingi alikuwa anachukua yeye hivyo sikushangaa nilivyosikia kule nairobi. Watu kama Mlama sioni wala simkii pamoja nakuwa vikundi vingi vya sanaa kwa sasa yeye alipashwa awe mstari wa mbele kuwapa mawazo. Bado kazi ipo kwa akina mama. Tafakari
 
Kwa uchambuzi yakinifu hizi hesabu hazitalingana! hiyo mbona ni mantiki ndogo tu.

Sijaua uchambuzi makinifu unaomaanisha zaidi ya kuangalia nchi wanayotoka inahitaji nini na wao wamefanya nini na wamepata umaarufu kivipi. Sasa elimu na uzoefu alio nao Migiro umemnyanyua vipi Mtanzania wa kawaida the same has Mdee. Migiro hajaonyesha kulleta mabadiliko yoyote kwa mtanzania wa kawaida sasa hayo mambo ya mavyeo kukaa UN ni bure kwetu, bora hiyo nafasi angepata Mdee sababu Migiro kakaa bungeni na hajawahi onyesha chochote cha kustua lakini angalia Mdee aliyoyafanya kwa muda mfupi
 
Ndjabu Da [COLOR=#ff0000 said:
Dude[/COLOR];5439885]Jee, mke wako naye kafunikwa na Halima Mdee?

Kweli wewe DUDE. Jazba ya nini? kama hutaki changia si uache tu?
 
Back
Top Bottom