Rose Migiro Kafunikwa na Halima Mdee

Rose Migiro Kafunikwa na Halima Mdee

images
VS
images

Rose Asha Migiro na Halima Mdee nani zaidi

Tanzania kama kubahatika na kupendelewa tumefanikiwa lakini tumekuwa watu tusioweza kutumia vema nafasi tunazopata, pengine kutokuwa na utambuzi na ufahamu wa kutosha kwa uwajibikaji wa kujituma katika nafasi tulizopewa na kuelewa uzito stahiki unaotakiwa na jinsi werevu na kujituma kwa hali ya juu katika utendaji unaotakiwa katika kutumika nafasi adimu ambayo kwa ulimwengu mzima ni chanda cha dhahabu kwenye kisahani. Wanaopata heshima na sifa ni kutokana na kujituma si mradi kukalia kiti na kutabasamu.

Kwa miaka karibu mitano nimekuwa nikikodolea macho list ya wanawake bora na maarufu duniani kwa kiwango cha kimataifa, pamoja na Rose Migiro kushika nafasi pekee akiwa kama mwanamke wa kwanza UNO kuparamia kiti hicho, lakini hakubahatika hata kushika nafasi ya 100 kati ya 100 bora. Nilijiuliza na kuishia kukaukiwa cha kuandika na kusubiria nafasi nyingine kwa mwaka unaofuata hadi ilipofikia kutompa nafasi kwa ingwe nyingine.

Halima Mdee, hajashika nafasi pekee serikalini zaidi ya ubunge kutoka kambi ya upinzani, lakini bungeni alivyoonyesha ushupavu usio wa kawaida hadi kuwashikisha adabu viongozi waandamizi serikalini imeleta matumaini mapya hadi kushuhudiwa na dunia ambayo imempa tuzo stahiki, na labda mwanamke kama huyu Mdee angepata nafasi ile adimu na ya pekee katika historia ya wanawake katika Umoja wa Mataifa huenda angeweza kuingia bora 100 kwa miaka aliyokaa Migiro United Nation.

Inawezekana tumezoea kuwavimbisha vichwa wengi wetu bila stahili, na wapatapo nafasi inakuwa basi bora muda ukamilike aende, ni kwa haidhuri tu tumekuwa naye ofisini.


images
images

Ibarahim Lipumba na Tundu Lisu


  • Ibrahim Lipumba ameshatikisa dunia kwa kuitwa kuitumika UNO kitengo cha uchumi kwa mwaka mmoja, huku ni kutambuliwa kimataifa kwa utumishi uliotukuka.
  • Tundu Lisu ameshapata tuzo ya Kimataifa

Matukio kadhaa ambayo yametokea kimataifa na kushuhudiwa kutambulika kimataifa kwa baadhi ya watanzania kutoka vyama vya upinzani ni dira inayoleta matumaini makubwa kwamba hawajapata nafasi, wakiipata hata kuongoza nchi hii mapinduzi makubwa kimaendeleo yatatokea. Kwani kufanya mambo kwa mazoea kuna athari zake.

images

Hapa Tundu Lisu
anajaribu kumpa tuition kidogo Lukuvi.

Watu kama Lukuvi ni lazima waishi kwa kujikomba kutokana uwezo wao. Hawa watu jamani wanaendelea kuonesha uwezo mdogo kila muda unavyodogea mbele.
 
mdee amegombania jimbo na kuchaguliwa na huyo mwingine alipewa ubunge wa chu.pi. Huoni utofauti hapo?

Duh! Kumbe hata ubunge alipata ule wa upendeleo wa viti maalum, maana yake hata kumwaga sera majukwaani kwa wananchi hakuzoea na hajui wala kufanyia mazoezi, hata kupambanishwa na wengine katika uringo wa siasa hakufanya, huyo ndio kumpeleka pale UNO? Oh my goodness! Umemwaga mchele kwenye kuku wengi sasa.
 
Tukiondoa mapenzi kibubusa na siasa ukweli ni kwamba Asha Migiro alichemsha. Maana kama angefanya kazi vizuri haikuwapo haja ya kumuondoa kwenye unaibu katibu mkuu kabla ya katibu mkuu kumaliza muda wake. Nafasi hii ingetokea zama za Salim Ahmed Salim stori ingekuwa nyingine. Mlitegemea chaguo la bwana dhaifu liwe bora wakati anachagua watu wake kutokana na sababu anazojua mwenyewe? Hata apigiwe debe vipi hawezi kuwa rais wa Tanzania simply because ni mwanamke. Tumejifunza toka kwa Anna Makinda ambaye alitumiwa na mafisadi kumpiga kibuti Samuel Sitta baada ya kuruhusu bunge kuwa bunge badala ya genge la sasa la CCM ukiachia mbali wapinzani kuzidiwa namba.
diplomasia ya salim katika umoja wa mataifa ni bora hata ya asha Rose migiro aliyechemsha. tanzania ni anti semite state(mchukia wayahudi). siasa zake za nje ni za uwongo uwongo tuu, halafu alipoondoaka hapa nchi aliambiwa na mwanasiasa mashuhuri kuwa ukifika UN kawaeleze Tanznaia hatutaki majeshi ya Uvamizi Iraq,katika mgogoro wa Israel na palestina Tanzania imekaa upande wa waarabu,kila kukicha magazeti huandika matusi kwa wayahudi. Sasa wewe unategemea nini kuhusu tanzanaia kuwa na mwanadiplomasia bora ikiwa malezi aliyoyapata ni ya uwongo matupu kuhusu ukweli wa mambo yaendvyo hapa duniani? kwa sababu nadhani mama migiro alipofika UN alikuta mambo ni kinyume tupu na jinsi huko alikotoka alivyotangaziwa. wewe fikiria tuu, eti tanzania ililaani majeshi ya uvamizi ya USA li;e Iraq, sasa jiulize kwa nini tanzania haikulaani majeshi ya Uganda yalipovamia Congo na kukalia ardhi ya wakongomani? malezi kama haya katu hayawezi kuzaa mwanadiplomasia bora ambaye ataweza kutamba katika vyombo vya kimataifa/
 
nadhani kama alimshawishi Ban Kimoo kuhusu majeshi ya uvamizi huko Iraq, naona Ban Kimoo alimshangaa sana au kama aliwaita wayahudi occupyer wa ardhi ya waarabu sijui Ban Kimoo alimjibu vipi ikiwa majeshi ya rwanda na uganda yaliyo occupy ardhi ya kongo bila ya kukemewa na nachi yetu.
 
Nashindwa kuelewa dr wa sheria anakuwa kilaza aha aha taabu kweli au ndio kuzaliwa kariakooo
asha rose migiro aling'olewa un kwa sababu ya utendaji mbovu!!! Alibebwa tu kikwete lakini alipofika huko akapwaya vibaya sana!!! Aibu!!! Hana lolote la kujivunia!!!
 
Back
Top Bottom