Riwaya: Tutarudi na roho zetu?

Riwaya: Tutarudi na roho zetu?

mkuu malizia hii riwaya mbona imebakia kodogo sana kuisha!?
 
Ahaaa ndo kusema smesusa sio

Kama uko Dar nenda TPH posta hiki kitabu kipo pia nimeona kile kingine cha salamu toka kuzimu ni sh 7, 000

Gharama za bundle kuchungulia huku kila siku ni kubwa kuliko bei ya kitabu. Mi nshamaliza kukisoma
 
SURA TISA



II


Joram na Nuru walitazamana kwa macho yalijaa hisia. Mmoja akatabasamu, mwingine akainama kwa haya. Mmoja akainua mkono na kuutua juu ya paja la mwenzake. Mwingine akaufunika mkono juu kwa kiganja chake, wakaanza kuutomasana kimahaba. Mkono wa pili ukainuliwa na kutua juu ya kifua cha mwenziye, ukitafuta uwezekano wa kupenya, ndani ya mavazi yake. Vijilima viwili, kwa namna ya kupendeza macho. Mkono ukaviacha vijilima hivyo na kuanza kufungua vifungo vya vazi hilo. Mara kimojawapo cha vilima hivyo kikajitokeza, kikimelemeta kwa wekundu na ulaini wake.


Wakatazamana tena. Kisha alikisogeza kinywaji chake na kukifanya kimeze chuchu za kijilima hicho. Mdomo ulipohama kifuani ulienda katika kinywa cha mwingine ambako ulianza kunyonya ulimi uliokuwa ukisubiri. Mara wakaachana na kuanza kuvuana mavazi yao moja baada ya jingine. Tahamaki mara wakawa wamesimama kama walivyozaliwa, kila mmoja akishangazwa au kuridhishwa na uzuri wa mwenzie. Kisha wakakumbatiana kwa nguvu. Mmoja aliguna, mmoja akanong'ona.


"Nuru..."


"Joram..."


Kitanda kiliwalaki na kuwafariji. Hawakuhitaji shuka. Walikuwa kama walivyohitaji kuwa, wakifanya mapenzi kwa namna ambayo walihitaji. Kwa kiwango ambacho hakikadiriki. Vitendo vyao vilifuatwa na maneno ya mapenzi ambayo yalisikika kwa sauti ya kike, mara chache sana yakijibiwa kwa sauti nzito ya kiume.


Kisha ghafla, vitendo na sauti zao vilitoweka machoni na masikioni mwa mtu ambaye alikuwa akishuhudia kila kitendo chao, "Shit", Alifoka mtu huyo aliyeitwa kwa jina na Von Iron. Alikuwa amefuatilia kila kitendo kwa tamaa kubwa, huku akiburudika. Lakini haikuwa burudani rahisi, kwani kuona huko kulimfanya atetemeke mwili mzima na roho kwa uchu wa tamaa, huku jasho likimtoka na damu kuchemka. Alikuwa akijaribu kujifariji kwa kuubembeleza uume wake kwa mkono wake huku macho yake yakiwa yamekazwa kutazama katika mtambo wake. Mkono haukuwa na faraja yoyote; Mara mbili aliutoa na kuufuta kwa leso yake kwa jinsi alivyokuwa amechafuka kwa manii yaliyokuwa yakimtoka kwa wingi.


Alitamani aondoke hapo na kuachana kutazama vitendo hivyo lakini macho hayakuruhusu. Akaendelea kutazama, akiendelea kujifariji kwa mkono wake. Moyo wake ulikuwa ukitutuma na kushindwa kustahimili zaidi. Kichwani alifahamu kabisa kuwa alihitaji kitu zaidi ya mkono kujifariji. Alihitaji mwanamke. Na si mwanamke yeyote isipokuwa yule mwanemke aliyekuwa akimtesa sana. Mwanamke wa Kiafrika Nuru...


Mwanamke mweusi! Von alikuwa akijishangaa kimoyomoyo. Ana wazimu? Hata hivyo alijua kimoyomoyo kuwa asingestahimili hadi atakapompata. Alijifariji kwa kujiambia kuwa baada ya kutenda naye mara moja tu angemuua, ili yasiyekumpata kama yaliyomkuta hayati baba yake.


Ni tamaa hiyo hiyo iliyomfanya akatae kata kata madai ya wenzake waliomtaka amruhusu Joram na msichana wake wauawe mara moja.


"Ni jambo la hatari lisilo na busara kumwacha hai mtu hatari kama huyo hasa katika kipindi hiki", mwenzake mmoja alikuwa amemwambia. "Japokuwa amekimbia kwao na hawezi kurudi, lakini ni mtu ambaye hafai kuaminika. Kumwacha hai ni sawa na kuishi na nyoka chumba kimoja"


"Atafanya nini?" Von alikanusha. "Hana awezalo kufanya, dado saa chache sana tutamleta katika televisheni atazame jinsi nchi yake inavyoteketea. Baada ya hapo tutamchinja kwa urahisi kama kondoo. Usijali. Waache waishi usiku mmoja zaidi.


Usiku ni kitu alichokuwa akikisubiri kwa shauku kubwa, akikumbuka yale aliyoyaona usiku wa jana. Na ulipowasili hakuwaalika wenzake kwenda kutazama kwa kisingizio cha "Kumchunguza kwa makini". Alikwenda peke yake. Akiburudika kwa faraja unayotesa.


Hivyo ilikuwa kama pigo kwake, vitendo hivyo vilipotoweka machoni kwake. Aliamini kuwa kulikuwa na hitilafu ya mitambo iliyounganishwa na chumba hicho. Lakini kwa vile mitambo hiyo ilikuwa Automatic, na ilitegeshwa kwa namna ambayo ingeweza kukirekebisha yenyewe, alisubiri kwa utulivu.


Katika kipindi hicho cha kusubiri ndipo lilipomjia wazo la kuyafikiria mambo ambayo yangetokea mara tu baada ya usiku huo. Kesho, kesho wakati kama huu bila shaka nchi kadhaa za Kiafrika zitakuwa katika maombolezo makubwa huku majeneza yakiwa yamejaa maiti zilizoungua na hospitali zikishindwa kuhimili idadi ya majeruhi walioponea chupuchupu. Mpango huu ulikuwa umetokana na ubunifu wake, ulikuwa umepita kwa taabu sana baada ya wakubwa kulalamika kwamba ulikuwa wa kikatili mno.


Lakini yeye Von na wenzake wachache walifaulu kuwashawishi na wakaafiki baada ya kuwakumbusha tena na tena kuwa ANC ilikuwa haifanyi mchezo. Ilikusudia kuwapokonya utawala wao, jambo ambalo lingewatia weupe wote mashakani. Chama hicho kinapewa onyo kali, onyo ambalo kamwe lisingeweza kusahauliwa. Dawa ya moto ni mto... Na sasa wakati wa kutumia dawa hiyo, iliyokuwa ikichemshwa kwa muda mrefu na kwa gharama kubwa, ulikuwa unawadia. Lipi lingeweza kumpendeza Von zaidi ya hilo? Nani angeweza kufurahia zaidi yake?.


Mara akasikika kucheka kwa furaha. Alijisikia kusherehekea kila chozi katika uso wa mweusi. Kwani machozi haya kwake yangekuwa faraja ambayo ingemsahaulisha ukatili wa mtu mweusi ambaye alimfanya awe yatima. Kwa ajili ya malaya mmoja mweusi, maelfu ya weusi yatateketea, aliwaza. Watakilipia kifo cha mama yake mpendwa. Pamoja nao Joram Kiango na msichana wake, aliendelea kuwaza. Lakini kabla ya kifo chao lazima awe amempata huyu msichana aitwae Nuru. Aliyokuwa ameyaona kwa macho yake yalikuwa hayastahamiliki. Alihitaji kuyaona kwa vitendo. Alihitaji kuijua siri iliyomo katika ngozi hii nyeusi. Siri ambayo ilimfanya akose mama na baba milele. Baada ya hapo ndipo Nuru angemfuata Joram ahera.


Mawazo hayo yalimpandisha mori hata akakumbuka kuyarejesha macho yake katika screen iliyokuwa ikimwonyesha chumba cha Nuru na Joram. Hakuna chochote. Mitambo ilikuwa bado haifanyi kazi. Von akaitazama saa yake. Ilikuwa ikikaribia saa kumi za alfajiri. Masaa mawili yalikuwa yamepita toka mitambo hiyo ilipokorofisha. Von hakuamini. Isingewezekana mitambo hiyo iwe haifanyi kazi kwa muda wote huo. Ilikuwa imepangwa kuwa ingeweza kujiwasha yenyewe dakika tano tu baada ya kupata hitilafu. Vipi leo ikatae? alijiuliza. Na hasa akiwepo Joram Kiango ambaye pamoja na matatizo yote aliyokuwa nayo ilikuwa imeamriwa kuwa asiachwe huru zaidi ya dakika tano?.


Hima Von aliinua simu na kuzungusha namba za mmoja wa makachero waliokuwa wamepewa jukumu la kuwa macho wakati wote katika jumba hilo alimokuwa Joram. "Sikia", Von alimwambia kwa sauti ya amri, "Tumia kisingizio chochote uingine katika chumba chao. Humo ndani fanya kila hila uone kwanini mashine imegoka kufanya kazi".


Mtu huyo, akiwa anaijua vizuri kazi yake, alivaa ovaliri lake jeupe na kuchukua vifaa vya umeme hadi chumbani kwa Joram. Aligonga mlango kama kawaida. Kisha akagundua kuwa ulikuwa wazi. Akaufungua polepole na kuingia ndani. Macho yake yalidakwa na umbo la Nuru akiwa kavaa vazi la kulalia, jepesi kiasi cha kufichua umbo lake zuri la ndani kwa kiwango cha kutosha. Kando ya Nuru alisimama kijana wa kizungu ambaye alikuwa kavaa nguo zake zote, suti, kama ambaye alikuwa hajalala kabisa. Fundi huo bandia alidhani kuwa kabla ya kubisha hodi mara ya kwanza alikuwa amewasikia wakicheka. Lakini hayo yalimtoka akilini mara alipomwona msichana huyo akiangua kilio huku akisema kwa kwikwi.


"Afadhali umefika fundi nadhani utanisaidia ".


"Kuna nini?" kachero huyo aliuliza.


"Huyu hapa", Nuru alisema akiuelekeza mkono kwa mzungu aliyesimama kando yake kwa utulivu. "Huyo ameingia humu chumbani kwa nguvu akitaka kuninajisi. Mtoe nje tafadhali".


"Yuko wapi bwana wako?"


"Yuko bafuni".


"Anafanya nini huko kwa muda wote huu?" aliuliza fundi huyo bandia huku akizidi kumkodolea macho yenye tamaa Nuru. Mara macho yake yaliuona mfuko uliokuwa wazi kando ya kabati. Akaona vitu vilivyokuwemo. Aligutuka kidogo na kuruka nyuma huku akiupeleka mkono wake mgongoni kuichukua bastola yeke. Alikuwa amechelewa sana. Wakati huo huo kisu kilikuwa kikipenya katika kifua chake. Pigo la pili lilimfanya atelemke sakafuni bila ubishi. "Mzungu" aliyekitumia kisu hicho alikitupa uvunguni na kuifuta mikono yake kwa shuka.


"Fanya haraka Nuru", alihimiza akiirudia maiti na kuilaza vizuri kando ya kitanda.


Dakika chache baadaye mlinzi aliyekuwa akilinda jengo hilo kwa mlango wa nyuma aliwaona vijana wawili wazungu, mvulana na msichana wakimjia. Mikononi walikuwa na mizigo yao ambayo haikuwa chochote zaidi ya mifuko yao midogo midogo.


"Tunawahi uwanja wa ndege", alieleza kijana wa kiume.


Pamoja na kwamba walizungumza kiingereza fasaha, mlinzi huyo aliwashuku kutokana na sauti. Hasa akiwa analifahamu jengo hilo lilivyo hakuamini kuwa hao walikuwa wasafiri wa kawaida.


"Naweza kuona vitambulisho vyenu?"



"Bila shaka", alijibu mzungu wa kiume, akiutia mkono wake mfukoni. Ulitoka na kisu ambacho kilididimia katika kifua cha mlinzi huyo. Maumivu makali yaliyoambatana na mshangao vilimfanya afyatue risasi bila shabaha. Mara akaanguka chini na kukata roho.



ITAENDELEA 0784296253


KUMRADHI WASOMAJI WETU, HATUKUWA HEWANI KUTOKANA NA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WETU. KARIBUNI - MPIGANAJI...

cc. Meljons
kiraia [URL="https://www.jamiiforums.com/member.php?u=294409"]Jimena, [URL="https://www.jamiiforums.com/member.php?u=66519"]ADK[/URL][/URL]


 
Milio ya risasi alfajiri hiyo tulivu
iliwashitua watu wengi na kusababisha
hali ya wasiwasi. Zaidi ya wote alikuwa
Von Iron alikuwa ameathirika zaidi. Von
alikuwa ameshtuka sana kiasi cha
kupatwa na kiwewe.
Alikuwa bado ameketi katika chumba kile
kile akisubiri matokeo ya mtu alimtuma
chumbani kwa Joram. Alisubiri kwa muda
ambao aliuona mrefu kupindukia.
Alipojaribu kuwasiliana nae kwa Walkie
Talkie ndogo iliyokuwa imevaliwa kama
saa ya mkono hakupata majibu.
Akaendelea kusubiri. Na katika subira
hiyo ndipo aliposikia milio ya risasi
ambayo hakuitegemea. Akafanya hima
kumtuma kachero wake mwingine ili
aende katika chumba hicho. Mara moja
akapata majibu ambayo yalimfanya
atokwe na jasho jembamba.
Dakika chache baadae Von alikuwa
miongoni mwa maofisa sita wa ngazi za
juu katika BOSS waliosimama ndani ya
chumba hicho mbele ya maiti ya
mwenzao iliyolala sakafuni juu ya dimbwi
la damu nzito. Joram hakuwa ndani ya
chumba hiki tena wala msichana wake
Nuru. Vitu vyao vichache vilikuwepo;
ingawa baada ya kupekuliwa
havikuonekana na chochote cha haja
zaidi ya mavazi na vitabu. Katika vitabu
hivyo kilipatikana kitabu kimoja cha
Physics ambacho kilionekana kuwa
kilisomwa sana kwa jinsi kilivyokuwa
kimepigiwa mistari chini ya maneno
fulani. Baada ya uchunguzi mdogo
ilidhihilika kuwa msomaji alikuwa
akizingatia mambo ya setilaiti na nuklia.
Hilo liliwafanya waunge mbili na kupata
nne.
"Ana wazimu", Von alifoka. "Kama
amekuja hapa akiwa na ndoto ya kutaka
kufahamu chochote juu ya setilaiti yetu
hii maalum wazimu unamsumbua.
Amekuja kuinadi roho yake". Akawageukia
wenzake na kuwatazama kwa jicho lake
kali la kutisha; jicho ambalo lilikuwa
msingi wa kuwafanya wenzake waendelee
wamwogopa na kutomkosoa.
"Mmenisikia, mtafuteni haraka aletwe
kwangu akiwa hai, atakufa taratibu kama
mbwa wenzake walivyokufa.
Kabla hawajatawanyika kutoka chumbani
humo, ziliwafikia habari zingine mbaya
zaidi. Imeonekana maiti ya mmoja wa
walinzi wa jengo hili ikiwa imechomwa
kisu kifuani. Aliuawa kwa aina ile ile ya
kisu ambacho kimetumika kumwua huyu",
alieleza kachero mmoja ndani ya ngome
hiyo ya makaburu.
"Mnaona?", Von aliunguruma mbele ya
wenzake. "Sasa namtaka Joram akiwa hai
ama maiti. Haraka apatikane haraka
iwezekanavyo, tafadhali..."
Ulitangazwa msako mkali katika jiji la
Johannesburg. Mitaa yote ilifurika
makachero ambao walikuwa
wakichunguza kila uchochoro. Ilikuwa
siku ngumu sana kwa watumishi weusi
ambao walikuwa wakiwahi makazini
asubuhi hiyo. Wengi wao waliambulia
kuishia katika vituo vya polisi ambako
waliteswa na kusumbuliwa kwa makosa
ambayo hawakuyafahamu. Mtu ama watu
waliokuwa wakitafutwa hawakupatikana.
Badala yake, hadi mapambazuko
kulikuwa na taarifa za vifo vya watu
wanane zaidi.
Watano walikuwa wameuawa kwa visu,
watatu wa risasi za bastola. Wengi wa
marehemu waliouawa walikuwa watu
wakubwa katika ofisi zao au walinzi wa
majumba fulani fulanib yenye umuhimu
mkubwa. Ilikuwa dhahiri kuwa hiyo
ilikuwa kazi ya Joram Kiango.
Von alizidi kupandwa na hasira.
Hakuelewa kabisa dhamira na manufaa
ya mauaji hayo. "Wazimu unamsumbua"
aliwaza. Kisha alihisi kuwa ameelewa.
Joram alikuwa akilipiza kisasi dhidi ya
maafa yatakayozipata nchi za Afrika saa
chache baadaye. Bila shaka alikuwa
akijifariji kwa kumwaga damu zisizo na
hatia. "Anajisumbua", Von alisema,
"Atalazimishwa kutazama kwenye
televisheni, moto utakavyokuwa
unaiteketeza Dar es Salaam. Baada ya
hapo ndipo atakapokufa kifo cha
kusikitisha".
Von akaamuru msaka mkali zaidi
uongezwe. Polisi wote na askari wa jeshi
la ulinzi waliingizwa katika msako huo.
Kila mmoja alikuwa ameagizwa kuhusu
mtu anayetafutwa na akionekana
afanywe nini. "Akileta ubishi ua,
vinginevyo aletwe mbele yangu akiwa
hai".
Pamoja na Von kutegemea habari hiyo
kuwa siri, lakini hakufahamu jinsi
ilivyofika masikioni mwa wana habari.
Alishangazwa na televisheni moja
iliyokatisha matangazo yake ya kawaida
ikaeleza jinsi Joram Kiango alivyotoroka
na mauaji aliyokuwa akifanya. Ikatolewa
picha ya Joram na msichana wake Nuru
ikiwaonyesha jinsi walivyofika Afrika
Kusini kwa ndege waliyoiteka nyara.
Televisheni pia ilionyesha maiti za watu
waliouawa na Joram.
Taarifa zilisambazwa kote kila kona ya
Jiji. Vyombo vya habari viliandika
"Jihadhari sana na mtu huyu, ukimuona
ua kwanza maelezo baadaye", alieleza
mtangazaji mmoja wa televisheni hiyo.
Tangazo hilo lilizua hofu ambayo
haikuwahi kutokea ama kuonekana katika
jiji hilo. Watu walizidi kupatwa na
wasiwasi wakiogopa kuifungua milango
yao ilipogongwa na mtu yeyote. Wapo
ambao hata kazini waliogopa kwenda
wakihofia kukutana na kifo.
Dakika chache baadaye Von alijitokeza
kwenye televisheni na kuwataka
wananchi waache hofu. Kwamba kutoroka
kwa Joram ilikuwa tatizo dogo sana
ambalo vyombo vya usalama vitalimaliza
muda si mrefu. Akiongea kwa kujiamini
sana. Von akawafahamisha kuwa badala
ya hofu leo ingekuwa siku ya sherehe;
kwani Afrika na dunia nzima itaziona
nguvu za Afrika Kusini. "Wote ambao
wamekuwa wakiionea kijicho nchi yetu
leo ndio siku ya kutupigia magoti",
alieleza Von. "Tulieni msiwe na wasiwasi
wowote. Itakapofika saa nne leo fungueni
radio na televisheni zenu muone
kinachotokea...", Von alimaliza.
ITAENDELEA 0784296253
 
Mkuu tunashukuru kama umerudi!maana tulikuwa tushakata tamaa!tukijua umepotea mazima
 
Wakuu mmenifurahisha sana,yaan endeleeni kutupa uhondo huu.
 
Shukrani sana kwa kusukuma gurudumu hili wakuu.
 
SURA YA TISA
IV
Watu hao Joram Kiango na Nuru,
waliokuwa wakitafutwa kwa udi na
uvumba, alfajiri iliwakuta wakiwa
wamesimama mbele ya hoteli moja
ndogo, katika mtaa ambao ulikuwa
umejaa watu waliokuwa wakijadiliana.
Macho yao yaliwatazama raia hao wa
makaburu waliojaa wasiwasi kwa
dhihaka. Kadhalika waliwakebehi na
kuwadhihaki askari wa polisi waliokuwa
wakipita huku na huku katika mitaa na
vichochoro wakiwasaka huku wakiwapita
Joram na Nuru bila hata kuwatupia
macho. Haikuwa rahisi kwa mtu yeyote
kuwashuku. Pamoja na kukesha
wakifanya kazi ya kwenda hapa na pale,
huku wakilazimika kuua na kuua tena,
bado walijitahidi kuwa katika hali yao ya
kawaida kama raia yeyote wa kawaida
katika nchi hiyo. Hali ambayo ilitokana na
mavazi waliyovaa pamoja na rangi yao.


Yeyote aliyewaona Joram na Nuru
aliamini kuwa hao walikuwa vijana
wengine kabisa tena kutoka katika jamii
ya makaburu. Hayo yalikuwa moja ya
matokeo ya shughuli nyingi ambazo
Joram alikuwa amezifanya kwa gharama
kubwa sana alipokuwa akisafiri hapa na
pale katika miji mbalimbali. Alikuwa
amempata mwalimu ambaye alikuwa
amewatengenezea ngozi za bandia
zilizovaliwa usoni, mikononi na kufunika
vichwa vyao kwa nywele za kizungu. Vitu
hivyo ni miongoni mwa mali zake ambazo
Joram alikuwa amezisafirisha kwa hila
akimtumia yule mfanyabiashara wa
Mmarekani More.


Kwa ujumla Joram aliona kuwa mambo
yote yalikwenda vizuri kama
yalivyopangwa, ingawa kiasi yalianza
ghafla kuliko alivyotegemea. Joram
alikuwa amesitushwa sana na taarifa ya
jana alipomsikia kiongozi wa BOSS
akisema kwamba leo saa nne wangeilipua
Dar es Salaam na miji mbalimbali ya nchi
za Kiafrika wakitumia ile silaha ya hatari
iliyofungwa angani. Hivyo Joram hakuwa
na simile tena moyoni. Ndipo alipoamua
kufanya mapenzi ya hali ya juu na Nuru,
akiwa na uhakika kuwa anatazamwa
kupitia mtambo wao ambao alikwisha
uona mapema. Alifanya vile ili
kuwapumbaza watazamaji hao.
Baada ya hapo ndipo alipofanya hila
kuukorofisha mtambo huo. Katika kipindi
hicho cha kutoonekana kupitia mtambo
huo, Joram aliondoka kwa kupenyapenya
kwa hila katika vichochoro hadi nyumbani
kwa More ambako alibisha mlango na
kufunguliwa na Moore mwenyewe. Joram
alipoomba mzigo wake Moore alikanusha
kabisa kuwa hakuwa amechukua mzigo
wa mtu kama huyo. Lakini ngumi mbili
tatu nzito kutoka kwa Joram zilimfanya
Moore amuongoze ghalani ambako
Joram alimfunga mikono na miguu kwa
kamba maalumu, kisha akachukua vitu
vile vya muhimu tu. Akarudi haraka hadi
chumbani kwake ambako alisaidiwa na
Nuru, walipekuapekua na kupata ramani
walizokuwa wameziandaa, pesa na vitu
vingine vingine. Ni wakati Joram
alipomaliza kujivika kozi hizo za bandia
zilizomfanya aonekane kama alivyo sasa,
yule kachero wa kwanza alipoingia, hila
aliyotumia Nuru ya kujifanya kwamba
alikuwa akipambana na 'Mzungu'
aliyetaka kumnajisi ilimsaidia sana.
Ndipo kachero huyo alipopata kile
alichostahili kupata. Nae akafanya haraka
kumsaidia Nuru kuvaa 'Uzungu' wake na
alipokamilika walivichukua vitu vyao
muhimu na kuingia mitaani.
Wakiwa wameikariri vizuri ile ramani
kikamilifu, kazi waliyoifanya mitaani
humo ilikuwa ya kuyafuata yale majengo
waliyoyakusudia na kutega vile vigololi
vilivyopatikana kwa Chonde na
kuvitegesha katika kipindi cha saa tatu
kamili. Walikuwa wameifanya kazi hiyo
kwa ukamilifu kuliko walivyokuwa
wametegemea wenyewe. Watu wachache
waliolazimika kupoteza maisha ni wale
ambao waliwashuku ama kuwazuia
kufanya kazi yao kwa makini. Wakiwa
hawajui kuwa wanapambana na nani
watu hao walikufa kwa utulivu kabisa,
isipokuwa yule ambaye kifo
kilimtetemesha hata akaamu kuruka
dirishani kutoka ghorofa ya nne akiwa na
kisu kifuani.
Sasa kazi ya kutega vigololi ikawa
imekwisha. Joram alimtazama Nuru na
kumnong'oneza. "Awamu iliyobaki ni
ngumu sana, itakuwa kazi yangu peke
yangu. Ni lazima niingie katika mtambo
wao na kuulipua. Nikiweza kuulipua kabla
ya madhala tuliyoyaandaa katika jiji hili
kutokea litakuwa jambo jema sana.
Nikishindwa, mioto itakapoanza nenda
pale ambapo nimekuonyesha katika
ramani unisubiri".
"Hatuwezi kwenda wote?", Nuru akahoji.
"Haiwezekani, tumelijadili hilo mara nyingi
sana", Joram akamwambia.
Wakakubaliana.
Kisha Joram akajiingiza kuwa miongoni
mwa watu waliokuwa wakipita katika
mitaa hiyo akaelekea ilikomwelekeza
ramani yake. Mwendo wake ulikuwa wa
haraka na uhakika, ingawa aliufahamu
kikamilifu ulinzi mkali uliokuwa
umeuzunguka mtambo huo. Matumaini ya
kurudi ilikuwa ndoto isiyo na uhakika.
Hata hivyo hakujali. Asingejali kufa
endapo kifo hicho kingemtokea baada ya
kufanikiwa kutega mabomu yake katika
mtambo huo. Aliamini kuwa ikitokea
amekufa katika dhoruba hiyo, Nuru
asingeshindwa kurudi Tanzania baada ya
msukosuko mkubwa utakaoutokea mji
huo saa mbili na nusu baadaye.
Nuru alikuwa amemwacha Joram
aondoke kwa hatua chache. Mara Joram
alipoondoka na kuamini kuwa hawezi
kugeuka tena kumtazama, Nuru nae
alianza kumfuata nyuma. Hakujua kuwa
yeye pia alikuwa akifuatwa na watu
wengine wanne wenye silaha kali
mikononi na mioyo yenye hofu na hasira
dhdi yake...
ITAENDELEA 0784296253
 
Kaka hapo ndo patamu asee!!thanks mkuu tupo wote hizi simulizi nilikuwa nazitamani kuzisoma.so sasa naenjoy sana mkuu!!
 
Back
Top Bottom