SIRI
episode 18
Mtunzi.Patrick CK
sana hadi nikashindwa kujua kama
kuna mtu alikuja hapa
kunitazama.Najiuliza ni nani huyu
mtu sipati jibu.Hakuna
anayenifahamu huku Israel zaidi ya
Olivia na Judy.Au Olivia kuna tatizo
amelipata?akajiuliza Edger na
kubonyeza kitufe pembeni ya
kitanda chake na ndaniya sekunde
chache muuguzi akafika
“Edger kuna tatizo
lolote?akauliza mwanadada yule
muuguzi aliyekuwa na tabasamu
usoni
“Ndiyo nina tatizo.Nahitaji
kujua nani alikuja kunitembelea
jana usiku hapa chumbani?akauliza
Edger
“Sina hakika kwa sababu mimi
nimeingia asubuhi hii.Nitamuuliza
muuguzi aliyekuwepo usiku halafu
nitakupa jibu.Kwa nini umeuliza
hivyo Edger?akauliza yule muuguzi.
“Usijali dada.Kuna kitu kingine
naomba unisaidie.Nataka simu
kuna watu nahitaji kuwasiliana
nao” akasema Edger na muuguzi
akaenda kumletea simu
akaziandika zile akapiga lakini
hazikuwa zikipatikana
“Huyu ni nani anataka
nimpigie huku hapatikani
simuni?akajiuliza Edger.
“Nitajaribu tena
baadae,yawezekana akawa ni mtu
muhimu au anaweza kuwa ni balozi
: wetu hapa Israel anataka
kuzungumza nami ndiyo maana
akanitumia ujumbe huu kunitaka
niwasiliane naye” akawaza na mara
akapata wazo
“Yawezekana akawa ni Sayid
anataka kuzungumza nami.Naamini
atakuwa ni yeye kwani nilimjulisha
kuwa niko hapa.Lazima atakuwa ni
mwenyewe ngoja niwasiliane naye”
akawaza na kuchukua kompyuta
yake akampigia simu Sayid Omar
“Edger vipi maendeleo yako?
Akauliza Sayid ambaye alikuwa
anatumia simu yake ya mkononi
“Ninaendelea vyema
Sayid.Maendeleo yangu si mabaya”
“Nafurahi kusikia
hivyo.Nimekuwa na mawasiliano
na madaktari wa hapo hospitali na
wamekuwa wakinijulisha kila
kinachoendelea kuhusiana na hali
yako”akasema Sayid
“Umekuwa unawasiliana na
madaktari?Edger akashangaa
“Ndiyo Edger.Nimekuwa
nikiwasiliana nao mara kwa mara
kujua maendeleo yako”
Edger akafikiri kidogo na
kuuliza
“Jana usiku ulikuja hapa
hospitali au kuna mtu yeyote
ulimtuma aniletee ujumbe
wowote?akauliza Edger
“Hapana sijafika huko ila
nimekuwa nawasiliana kwa karibu
sana na madaktari wa hapo.Ujumbe
gani huo?akauliza Sayid
“Nimekuta kuna bahasha
pembeni ya kitanda changu na
ndani yake kuna kadi yenye namba
za simu nikaelekezwa kwamba
nipige simu hiyo,nimepiga lakini
simu haipatikani nikahisi labda ni
wewe ulitaka kuwasiliana nami”
“Hapana si mimi Edger.Kama
ningehitaji kuwasiliana nawe
nisingekutumia ujumbe.Nitumie
hizo namba ambazo umeelekezwa
upige” akasema Sayid na Edger
akampatia zile namba
“Nitakupigia tena baadae”
akasema Sayid na kukata simu
“Nani ambaye aliniachia
ujumbe huu niwasiliane
naye?Nilitegemea angekuwa sayid
lakini amekana si yeye.Nadhani
Sayid atanisaidia kujua mtu huyo
ni nani” akaendelea kuwaza.
***************
Saa nne za asubuhi Dr Olivia
akiwa na Judy waliwasili hospitali
kumtazama Edger kama ilivyo
kawaida yake.Kabla hajaingia
katika chumba cha Edger Dr Olivia
akaamua kwenda kwanza kumuona
Chris.Aligonga mlango wa chumba
cha Christopher akaruhusiwa
kuingia.
“Christopher” Olivia akasema
huku akitabasamu
“Dr Olivia.Karibu sana habari
za toka jana? Chris akajibu uso
wake ukiwa katika tabasamu
kubwa.
“Habari za toka jana nzuri.Vipi
maendeleo yako?
“Ninaendelea vizuri Olivia”
Chris akajibu huku akitabasamu
“Chris nimekuja kumuona
mgonjwa wangu nikaona nipite
kwanza kukujulia hali kabla
sijaenda kumuona
Edger.Nashukuru unaendelea
vizuri” Dr Olivia akasema huku
akisimama na kujiandaa kutoka.
“Nashukuru sana Olivia kwa
kuja kunijulia hali” Chris akasema
huku akionekana kutaka kuuliza
kiuliza kitu.
“Kuna kitu unataka kuniambia
Christopher? Akauliza Olivia
“Naomba dakika zako chache
kuna kitu nataka kukuuliza kama
hutajali” akasema Dick
“Usijali Christopher uliza
chochote unachokitaka” akasema
Olivia
“Dr Olivia naomba usinielewe
vibaya kwa hili
nitakalokuuliza.Wewe ndiye
uliyemleta Edger hapa hospitali.Je
mtu huyu hana familia?Hana mke
au ndugu mwingine ambaye
angeweza kuambatana naye hapa
kuja kumuuguza na wewe ukapata
nafasi ya kuendelea na majukumu
yako mengine?akauliza Dick
“Nakumbuka nilikueleza jana
kwamba mimi na Edger hatukuwa
tukifahamiana.Aliletwa katika
hospitali ninakofanya kazi akiwa
hajitambui na baada ya kumpa
huduma tuliona kama angeendelea
kukaa pale angepoteza maisha
hivyo ikalazimu kufanya mpango
wa kumleta huku kwa matibabu ya
juu zaidi.Mimi ndiye niliyekuwa
daktari wake hivyo ikanibidi
nisafiri naye.Sifahamu chochote
kuhusu Edger ,sifahamu familia
yake wala sijui kama ana mke au
hana” akasema Olivia
“Hujawahi kumuuliza kuhusu
familia yake?
“Hapana sijawahi
kumuuliza.Edger mwenyewe
amekuwa mgumu sana kuongelea
chochote kuhusu familia yake”
akasema Olivia
“Sawa Olivia ahsante sana kwa
kuja kunitembelea” akasema Dick
na Olivia akatoka akaelekea katika
chumba cha Edger
Mara tu Olivia alipotoka,Dick
naye akatoka akiwa na simu
aliyopewa na Yair kwa ajili ya
matumizi kwa muda wote
atakaokuwepo nchini
Israel.Alikwenda kujitenga sehemu
iliyotulia akaandika namba za simu
za waziri mkuu akampigia
“Hallo” akasema waziri mkuu
wa jamhuri ya muungano wa
Tanzania baada ya kupokea simu
ya Dick
“Mheshimiwa waziri mkuu
shikamoo”
“Marahaba
Dickson,unaendeleaje
huko?akauliza waziri mkuu.
“Hukuninaendelea vyema
mzee wangu.Kila kitu kinakwenda
vyema”
“Nafurahi kusikia hivyo
Dickson.Vipi mgonjwa wetu
anaendeleaje?
“Maendeleo yake nimazuri
yanatia moyo.Anapata matibabu
mazuri na anaendelea vyema”
“Ashukuriwe Mungu sana kwa
maendeleo haya
mazuri.Tunamuhitaji sana huyo
kijana hivyo hakikisha anakuwa
salama kwani waliotaka kumuua
hawatafurahi wakisikia kwamba
anaendelea vyema.”
“Mzee kuna jambo nataka
kukuomba unisaidie”akasema
Dickson
“Omba chochote Dickson”
akasema waziri mkuu
“Mzee nataka kufahamu
kuhusu familia ya Edger
Kaka.Nataka kufahamu kuhusu
wazazi wake ni akina nani na wako
wapi,nataka kufahamu kama ana
watoto au hana na kama anao wako
wapi?Nani mke wake? Nisaidie
kupata taarifa hizo mheshimiw
waziri mkuu” akasema Dickson.
“Nitakusaidia kupata taarifa
hizo Dickson lakini nataka
kufahamu je kuna sababu yoyote ya
kutaka kupata taarifa hizo?akauliza
waziri mkuu
“Ndiyo mzee.Kuna mambo
yametokea ambayo yamenifanya
intake kupata taarifa hizo.Baada ya
kuzipata na kuzifanyia kazi
nitakujulisha ni kwa nini
ninazihitaji” akasema Dickson
“Sawa Dickson.Nitamuelekeza
spika wa bunge akutumie taarifa
hizo zote katika barua pepe yako na
kama kuna kitu chochote
unakihitaji usichelewe kunijulisha”
akasema waziri mkuu na kuagana
na Dickson.
*****************
Dr Olivia baada ya kutoka
chumbani kwa Dick alielekea katika
chumba cha Edger akaingia bila
hata kugonga hodi akamkuta Edger
akizungumza na Judy.
“Edger unaendeleaje? Dr Olivia
akamsalimia Edger ambaye
alimtazama na kwa sauti ya
unyonge akasema.
“Naendelea vizuri Olivia,habari
za toka jana?
“Habari nzuri.Vipi hali yako
kwa jumla?
“Kwa ujumle ninaendelea
vizuri na kama hali ikiendelea
namna hii,nitaomba kurejea
nyumbani haraka sana”akasema
Edger na kumstua Dr Olivia
“Kurejea nyumbani? Dr Olivia
akashangaa
“Ndiyo Olivia.Ninahitaji
kurejea nyumbani.Maendeleo
yangu ni mazuri na sina sababu ya
kuendelea kukaa hapa,nina mambo
mengi yanayonisubiri
nyumbani.Mbona
umeshangaa?hutaki kurudi
nyumbani? Hakuna shughuli
zinazokusubiri kule?” Edger
akauliza
“You must be kidding Edger”
Olivia akasema huku akicheka
“Sitanii Olivia.Nimeamua
kurudi nyumbani”
“Hujanipa bado sababu za
msingi za kuamua kurudi
nyumbani ukiwa bado haujapona
vizuri”akasema Dr Olivia
“Olivia ninaendelea vizuri kwa
sasa na ninaweza kurudi nyumbani
na kuendelea na matibabu katika
hospitali za serikali.Unaonaje wazo
hili? Edger akauliza
Dr Olivia akamtazama Edger
usoni halafu akasema
“Edger naomba
unisikilize.Suala la kurudi
nyumbani kwa sasa ni
gumu.Utarudi nyumbani pale
utakapokuwa umepona.Mimi ndiye
niliyekuleta huku na ndiye
nitakayekurudisha.Mimi ni daktari
na ninafahamu kwamba bado
hujapona” Dr Olivia akasema
“Olivia nashukuru sana kwa
kuyaokoa maisha yangu kwa
kunileta huku Israel.Najua
umetumia muda mwingi na
gharama kubwa lakini kwa hapa
nilipofika nadhani niko salama na
ninaweza kurudi nyumbani.Kwa
nini hutaki kurudi nyumbani? Kitu
gani kinakufanya upende kukaa
huku katika nchi za watu?
Edger akasema huku uso wake
ukiwa umeanza kuonyesha dalili
Fulani za hasira.
“Hapana Edger hautarudi
Tanzania hadi pale utakapokuwa
umepona kabisa.Lakini kama
umeamua kwa hiari yako kurudi
Tanzania sikukatazi.Unaweza
kurudi lakini mimi bado
nitaendelea kubaki hapa hapa hadi
hapo nitakapoamua kurudi
nyumbani.” Dr Olivia akasema huku
naye uso wake ukionyesha hakuwa
na masihara tena.
“Nitarudi nyumbani
Olivia.Utake usitake ni lazima
nirudi nyumbani.You can’t control
me..” Edger akafoka.Dr Olivia
akabaki akimshangaa.Judy aliona
hali ile iliyoanza kujitokeza mle chumbani akatoka nje na kuwaacha
Edger na Olivia
“Whats going on Edger ? Dr
Olivia akauliza
“I want to go home,that’s all”
Edger akajibu
“I’m tired of being alone in
here” Akasema tena
“Alone? Dr Olivia akauliza kwa
mshangao
“Yes alone.No body cares for
me here.Kila mtu yuko hapa kwa
mambo yake!! Akasema Edger na
kumfanya Dr Olivia kucheka
kidogo.
“Edger Please stop.Don’t ever
say that again.Hakukuwa na mtu
yeyote aliyeyajali maisha yako zaidi
yangu mimi ndiyo maana
nikajitolea kufa na kupona ili
kuhakikisha ninakufikisha hapa.
Ninakujali na ndiyo maana
nimeacha shughuli zangu zote kwa
ajili ya kukuhudumia wewe tu. I’m
here for you.”
Edger hakujibu kitu
akaendelea kutazama chini.
“Edger nieleze nikufanyie kitu
gani ili ujue kwamba ninakujali? Dr
Olivia akauliza tena
“Ulikuwa wapi jana usiku?
Edger akauliza
“Jana usiku? Dr Olivia akauliza
kwa hamaki
“Ndiyo jana usiku ulikuwa
wapi?”
“Kwa nini unauliza hivyo? Dr
Olivia akauliza
“Judy alinipigia simu na
kuniuliza kama niko na wewe kwa
sababu ulimuaga unakuja hospitali
kuonana nami lakini sikukuona
kabisa jana usiku hapa
hospitali.Ulikwenda wapi?
“Nilikuwa hotelini” Dr Olivia
akajibu kwa haraka na kwa ufupi
“Usinidanganye Olivia.Kama
ungekuwepo hotelini Judy
asingepiga simu
kukuulizia.Ninafahamu kwamba
jana ulikuja hapa hospitali ulikuwa
na Christopher” Edger akasema .Dr
Olivia akamuangalia kwa jicho kali.
“Ulikuwa
unanifuatilia?akauliza Dr Olivia
“Nilitaka tu kufahamu uko
wapi na ndiyo maana nikauliza
mapokezi kama umeonekana
maeneo haya wakasema kwamba
ulikuwa bustanini na Christopher”
Edger akasema
“Edger masuala yangu binafsi
yanakuhusu nini? Dr Olivia akauliza
kwa ukali.
“Ni kwa sababu ninakujali
Olivia.Nilipatwa na wasiwasi kama
uko salama”
“Edger please ! Don’t ever try
again to do that.Who am I to you?
Am I your wife or girlfriend?
Sikutegemea Edger kama unaweza
ukafanya kitu kama hiki.For the
records I don’t like
this.……”akasema Dr Olivia kwa
ukali
“Dr Olivia let me explain”
Edger akasema
“You have nothing to explain
Edger.Niliona toka jana
tulipotambulishwa kwa
Christopher,ulimchukia ghafla.Kwa
nini humpendi Chris? Olivia
akauliza kwa ukali
“He’s good for nothing
Olivia.Don’t fall for that man from
nowhere,he’s not good for you!!
Edger naye akajibu kwa sauti yenye
ukali ndani yake
“Good for nothing? Akauliza Dr
Olivia
“A good for nothing is you
Edger !! Huwezi kujilinganisha na
Chris.He is a gentleman” Dr Olivia
akajibu kwa sauti kali
“I am a gentleman Olivia.I care
about you! Edger akasema
“You care about me? Olivia
akauliza
“And why do you care? Dr
Olivia akauliza tena
“Because I love you…….!!”
Edger akajikuta akitamka kwa
nguvu.
Dr Olivia akashika kiuno huku
akimshangaa Edger.Hakuamini
alichokuwa amekisikia toka kwa
Edger.
“Stupid……………!!” Akasema
Olivia akanyakua mkoba wake na
kutoka kwa kasi mle chumbani.
“Olivia..I’m sorry” Edger
akasema baada ya kuona Dr Olivia
akiondoka mle chumbani akiwa
amekasirika.Dr Olivia hakugeuka
nyuma akaufunga mlango na
kuondoka.Edger akajishika kichwa
na kujilaumu
“Its true..I’m a stupid..How
could I do something like that?
Edger akajilaumu akiwa ameweka
mikono kichwani.
“Wivu umepelekea haya yote
kutokea.Nilipaswa kuwa mvumilivu
lakini sasa nimemkasirisha
Olivia.Badala ya kumuweka Olivia
karibu sasa nimemsogeza mbali
zaidi.Itanigharimu kumrejesha
karibu zaidi kwani tayari nimempa
tiketi ya kuwa karibu zaidi na
Christopher.I hate this guy!!
Akawaza Edger na kwenda
kuchungulia dirishani
“Sikupaswa kufokeana na
Olivia ambaye ndiye aliyeyaokoa
maisha yangu. Kama kweli
ninampenda na ninataka kuwa
naye maishani ninapaswa
kumuomba msamaha haraka
iwezekanavyo.” Edger akawaza.
“Hapana hili si wazo zuri kwa
sasa kwani bado ana
hasira.Nitazungumza naye hasira
zikipungua” Akawaza Edger Dr
Olivia alipoondoka pale hospitali
alielekea moja kwa moja hotelini
“Kumbe Edger ametokea
kumchukia Chris kwa sababu
ananipenda,so stupid.!!.Siwezi
kuwa na mahusiano na
mwanasiasa.Uhusiano wangu naye
utabaki wa mgonjwa na
daktari.Hajafanya vibaya kuweka
wazi hisia zake kwangu lakini
hakutumia busara.Alitakiwa atafute
njia nyingine ya kuelezea hisia zake
kwangu na si kwa kuanza
kunifuatilia nyendo
zangu.Ameniudhi sana kwa hili
alilolifanya” Dr Olivia akawaza
“Wanaume!!..yaani
kumuonyesha kumjali katika
kipindi hiki kifupi tayari
ananitaka.!!! Dr Olivia akawaza na
kwa mara ya kwanza toka ametoka
hospitalini akatabasamu.
“Edger ni kijana
mzuri,mwenye sura
nzuri,anapendwa na watu wengi
lakini kwangu mimi atabaki kuwa
rafiki yangu na si zaidi ya hapo.Sijui
kwa nini moyo wangu unastuka
kila nikimfikiria Chris.Ni mapema
sana kusema lakini nahisi kuna kitu
Fulani kati yetu ndiyo maana
namuwaza namna hii.Toka
nimeonana naye hazipiti dakika
bila kuiwaza sura yake yenye
tabasamu la kupendeza.Is he the
one I’ve been looking for? Anaweza
kuyatibu majeraha ya mapenzi
moyo wangu uliyoyapata toka kwa
Nickson? Siwezi kumsahau
baradhuli yule kwa jinsi
alivyonitenda.Alinilaghai na mimi
nikaridhika kwamba ananipenda
kumbe hana lolote.Niliumia sana
.This time I don’t want to get hurt.I
need someone special for me
only.Kwa funzo nililolipata toka
kwa Nickson sitakiwi kuwa na
haraka na Chris.Nahitaji muda
mwingi wa kumfahamu vizuri
zaidi” Dr Olivia akawaza
Akiwa bado katika mawazo
mengi juu ya kilichotokea muda
mfupi uliopita aliamua kumpigia
simu Stanley.Akawasha kompyuta
na kumtafuta Stanley akampigi
simu
“Edger habari yako? Akasema
Stanley
“Habari si nzuri Stanley”
akasema Edger
“Kuna matatizo gani tena ?
Stanley akauliza akionekana kuwa
na wasi wasi
“Nimekwaruzana na Olivia
asubuhi hii alipokuja
kunitazama.Nilipomuona
nilishindwa kujizuia nikajikuta
nikisema maneno mabaya ambayo
yamemuudhi sana .Ameondoka
kwa hasira nyingi .Hapa nilipo
nimechanganyikiwa sijui hata
nifanye kitu gani” akasema Edger
“Edger ndugu
yangu,nimekwisha kuonya mara
nyingi kuhusu huyo Olivia.Ukitaka
kufanikiwa katika mambo yako
achana naye kabisa.Uhusiano wako
naye ubaki wa mgonjwa na daktari
na si vinginevyo.Hebu tulia akili
Edger na ufikirie mambo ya
msingi.Una mambo ya muhimu
sana yanakukabili ambayo
inakubidi uelekeze nguvu zako
huko na si kupoteza muda mwingi
kumuwaza Olivia ambaye hana
msaada wowote kwako”Stanley
akasema
“Olivia ni mtu muhimu sana
katika maisha yangu.Hata kama
nikifanikiwa ndoto zangu lakini
sintakuwa na furaha kamwe kama
sintakuwa naye.Tuachane na hayo
nipe habari za huko” Akasema
Edger
“Habari za huku nzuri.Jana
usiku nimezungumza na Mathew
Lazaro ambaye mwenyekiti wa
chama cha Democratic,nimeongea
naye kwa kirefu sana kuhusu
mpango wako na amefurahi kupita
kiasi.Ameniambia kwamba nimpe
siku ya leo na kesho ili aitishe
mkutano wa dharura wa kamati
kuu walijadili suala hili halafu
watatoa jibu.Lakini uwezekano wa
kukubali ugombee urais kupita
chama chao ni mkubwa sana kwa
sababu walikuwa wakikuna vichwa
katika kutafuta mgombea mwenye
sifa anayeweza kupeperusha
bendera ya chama chao katika
uchaguzi huu.Kwa hiyo tusubiri
majibu yao halafu tuone tutafanya
nini.” Stanley akasema
“Stanley umefanya vyema japo
umekwenda haraka sana.Lengo
langu kubwa lilikuwa ni
kukifahamau vyema hicho chama
kama kinaweza kunifaa”
“Edger hatuna muda wa
kusubiri.Ngoja ngoja unaweza
ukajikuta umebadili
mawazo.Mambo lazima yaanze
haraka sana na moto huu ulioanza
hautazimika” akasema Stanley
“Vema Stanley utanijulisha jibu
watakalokupa lakini hata mimi
ninataka kuonana na daktari
niombe ruhusa ya kurejea
nyumbani nikaendelee na matibabu
katika hospitali za serikali.Sitaki
kuendelea kukaa huku.Maendeleo
yangu ni mazuri sasa hivi.” Edger
akasema.
“Edger wazo la kurejea
nyumbani si wazo baya kama
madaktari wataona inawezekana
litakuwa jambo jema” Stanley
akasema.
“Nitakujulisha itakavyokuwa
Stanley” akasema Edger na kukata
simu
TANZANIA
Saa sita za mchana Damian
Mwamba akiwa ameongozana na
dereva wake waliwasili mjini
Morogoro.Moja kwa moja
wakaelekea City 5 stars hotel moja
kati ya hoteli kubwa na nzuri
ambako alipatiwa chumba na kwa
kuwa hakuwa na mizunguko
mingine hapo Morogoro yoyote
akaamua kujipumzisha chumbani
kwake.Alijitupa katika kitanda
kikubwa kilichokuwemo mle
chumbani na mara sura ya Sintah
ikamjia akilini na kumfanya
atabasamu.
“This girl is driving me
crazy.Nina mipango mikubwa sana
na mizuri juu yake pindi
akishamaliza masomo yake ya
kidato cha sita.Binti kama yule
anatakiwa kuwekwa katika sehemu
nyeti kama benki kuu au sehemu
yoyote ile yenye hadhi
kubwa.Ngoja nimpigie simu
nimtaarifu kuwa nimeshafika
Morogoro” Akawaza Damian
Mwamba huku akizitafuta namba
za Sintah katika simu yake akapiga
“Hallo darling” Ikasikika sauti
tamu ya Sintah.
“My baby,how are you?
Akasema Damian Mwamba huku
akitabasamu.
“I’m fine baby.How are you?
Akasema Sintah kwa sauti nyororo
iliyomsisimua Damian.
“Wewe mtoto hiyo sauti yako
kila nikiisikia inanitoa jasho”
Akasema Damian huku akicheka
“Ouh Darling I love
you.Umefika wapi sasa hivi?
Akauliza Sintah
“Mimi tayari niko
Morogoro.Niko hapa City 5 stars
hotel chumba namba 127.”
“wow..kumbe umeshafika?
“tayari nimefika malaika
wangu.Ninakusubiri,saa ngapi
utakuja? Kumbuka nimevuruga
ratiba zangu na kuamua kulala
hapa Morogoro kwa ajili yako.”
“Nashukuru sana darling kwa
kunijali.Kila kitu tayari nimekiweka
sawa hapa shuleni.Nitaondoka
hapa saa moja na nusu wakati
tayari kuna giza nitafika hapo
kuanzia saa mbili za usiku.”
“Usikose kuja kwa sababu nina
hamu sana na wewe.Unanipa vitu
adimu na kunifanya kijana kila
ninapokuwa nawe.” Akasema Mr
mwamba huku akicheka.
“Usijali Darling,mimi ni wako
leo hadi asubuhi.Mwaaaahh.”
Sintah akamalizia na busu zito
halafu akakata simu.
Damian Mwamba aliendelea
kutabasamu ,akainua simu ya mle
chumbani na kuomba aletewe
mvinyo.
*****************
Paul alikuwa makini akifuatilia
maongezi kati ya Damian Mr
Mwamba na Sintah kupitia
mitambo yake iliyoyanasa
maongezi yale moja kwa moja
kupitia chombo kidogo
kilichowekwa katika simu ya
Damian.Baada ya simu kukatwa
akavua spika za masikioni
alizokuwa amevaa ,akatabasamu.
“Finaly Damian Mwamba is
going down” Akasema huku
akitabasamu.
Akiwa bado anatabasamu
akainua simu yake na kumpigia
Donald Nkebo
“Hallo Paul habari yako?
“Habari yangu nzuri Mr
Nkebo.Nimekupigia nina taarifa
muhimu kwamba leo ni siku ya
historia kubwa kwani mmoja kati
ya wanasisasa wakubwa wa nchi hii
Damian Mwamba anakwenda
kupotea kabisa katika medani za
siasa.” Paul akasema na kumfanya
Mr Nkebo kutoa kicheko kikubwa.
“Niambie Paul nini
kinaendelea?akauliza Donald
Nkebo
“Damian Mwamba yuko
Morogoro tayari amefikia City 5
star hotel chumba namba
127.Ametoka kuwasiliana na Sintah
muda mfupi uliopita na
wamepanga kukutana saa mbili
usiku wa leo ambapo Sintah atalala
na Damian hotelini hapo hasi
asubuhi ya kesho.Kwa kuwa
tulikiwisha fahamu kuhusu mpango
huu,tayari vijana wangu
wanakaribia kufika Morogoro
ambako watakutana na wazazi wa
Sintah na kuwaeleza kila kitu
anachokifanya Damian Mwamba
halafu wataambatana hadi katika
hoteli alikofikia Damian
Mwamba.Vijana wangu
wamefuatana pia na waandishi wa
vyombo vikubwa vya habari hapa
nchini ambao wataripoti tukio hilo
la Damian mwamba kufumaniwa na
mwanafunzi wa sekondari.Kuanzia
usiku wa leo habari kubwa
itakayokuwa ikitawala anga za
habari ni kuhusu fumanizi la Mr
Mwamba.Nitakupigia tena simu saa
nne za usiku baada ya mambo
kukamilika” Paul akasema.Huku
akicheka Donald Nkebo akasema
“Paul una akili sana.Vipi
kuhusu Edger mipango
inakwendaje?
“Kuhusu Edger tunaendelea
kusubiri taarifa kutoka kwa Judy.
Nitakutaarifu nitakapopata kitu
chochote kutoka kwake” Paul
akasema
“Ahsante sana Paul.Tuendelee
kuwasiliana.Nimepanga kuonana
na mheshimiwa rais baadae. leo,naamini atafurahi sana kusikia
hatua mliyofikia.Kazi njema Paul”
akasema Donald Nkebo na kukata
simu.
HAIFA – ISRAEL
Dickson Kipuma alipokea
barua pepe kutoka kwa spika wa
bunge ambayo ilikuwa na taarifa
zote za mbunge Edger kaka.Taarifa
ile ilieleza Edger ni mtoto yatima
ambaye wazazi wake wote
walikwisha fariki.Taarifa ile bado
iliendelea kuonyehsa mpaka wakati
ule mbunge Edger alikuwa bado
hajaoa na hana familia.
“Hii inazidisha ukakasi.taarifa
zinaonyesha Edger kaka hana
wazazi,wote wamekwisha fariki
lakini usiku wa jana nilipompigia
simu yule mwanamke Habiba alijua
anazungumza na Edger na
akamuita “mwanangu”.Alikuwa na
maana gani kumuita Edger
mwanae?Ni mwanae
kivipi?akajiuliza Dickson.
“Naanza kupata picha kuna
mambo ambayo hatuyafahamu
bado kuhusiana na Edger
kaka.Kuna mambo yamejificha sana
ambayo lazima
tuyafahamu.Anafahamiana na
Habiba ambaye ana mafungamano
na mtandao wa IS.Who is this
guy?akajiuliza Dick
“Nimemuona anatumia sana
kompyuta yake kuwasiliana.kwa
bahati mbaya nilikosea kutega
kamera hivyo nashindwa kupata
sauti kujua anazungumza na nani
na anazungumza nini.Nitalazimika
kuipata kompyuta ile niweze
kuchunguza mawasiliano yake”
akawaza Edger na kumpigia simu
Yair
“Yair kuna msaada wako
ninautaka wa haraka sana”
“Sema unachokitaka Dickson”
“Nimepokea barua pepe
kutoka Dar es salaam yenye
maelezo yote ya kuhusina na Edger
kaka.Maelezo yanaonyesha Edger
hana wazazi.Wote wamekwisha
fariki.Vile vile mpaka sasa hana
mke wala mtoto.Nikiunganisha
taarifa hii na kile kilichotokea jana
Habiba kumuita Edger mwanae
ninazidi kupata hamu ya kuendelea
kumchunguza huyu jamaa kwani
inaonekana kuna mambo mengi ya
siri ambayo hatuyafahamu kuhusu
huyu mtu”
“Unataka kufanya nini
Dickson?Yair akauliza
“Nataka Edger atolewe
chumbani kwake ili nikaichukue
kompyuta yake ambayo ndiyo
anaitumia sana katika
mawasiliano.Nataka kujua
anawasiliana na akina nani.Fanya
mpango daktari aje amchukue na
kumtoa chumbani” akasema Dick
“Sawa Dick naomba unipe
muda mfupi nilishughulikie hilo
suala” akasema Yair
Baada ya dakika kumi Yair
akampigia simu na kumtaka aende
katika chumba cha Edger kwani
tayari amekwisha chukuliwa
amepelekwa kwa daktari.Bila
kupoteza muda Dickson akaingia
katika chumba cha Edger na
kuikuta kompyuta juu ya meza
akaifungua na haraka haraka
akaanza kutafuta rekodi za
mawasiliano yote ya Edger katika
kompyuta ile.Akazipata na
kuzihifadhi katika kifaa chake
kidogo cha kuhifadhia kumbu
kumbu halafu akatoka na kurejea
chumbani kwake akamjulisha Yair
kwamba tayari amekwisha toka
chumbani kwa Edger na
amefanikiwa kupata kile
alichokuwa anakitafuta.
Dick akachomeka kifaa kile cha
kuhifadhi kumbu kumbu katika
kompyuta yake na kuanza kupitia
kumbu kumbu zote za mawasiliano
ya Edger.Kwa kutumia kompyuta
yake Edger alikuwa amewasiliana
na watu wawili tu mmoja ni Stanley
na mwingine ni Sayid Omar ambaye
amewasiliana naye mara mbili.
“Sayid Omar hili si jina geni
kulisikia” akawaza Dickson na
kujaribu kuvuta kumbu kumbu ni
wapi amewahi kulisikia jina lile
lakini akashindwa kukumbuka
“Kumbu kumbu haziji lakini
jina hili si geni masikioni mwangu”
akawaza na kumpigia Yair
“Yair huyu jamaa
amewasiliana na watu wawili tu
ambao ni mtu anaitwa Stanley
ambaye naamini atakuwa
mtanzania na mwingine anaitwa
Sayid Omar ambaye amewasiliana
naye mara mbili” akasema Dickson
“Umesema Sayid
Omar?akauliza Yair akionekana
kustuka
“Ndiyo.Inaonyesha amempigia
simu kwa kutumia mtandao wa
skype mtu anaitwa Sayid Omar” “Dickson kama utakumbuka
jana nilikueleza kwa kirefu kuhusu
Habiba mwanamke tajiri sana
ambaye alikuja kumuona Edger
Kaka hapo hospitali,nikakueleza pia
kwamba mshirika mkubwa wa
Habiba anaitwa Sayid Omar na
huyu ndiye ambaye amekuwa
mfadhili mkubwa wa kikundi cha IS
kwa sasa.Kama Edger kaka
anafahamiana na anawasiliana na
Sayid Omar ni wazi atakuwa
anafahamiana pia na Habiba Jawad
na hii inazidi kuongeza kigugumizi
kuhusu Edger.Je naye ana
mahusiano na kikundi cha
IS?Ninauliza hivyo kwa sababu
hainiingii akilini amefahamiana vipi