Riwaya: Siri

Asanteh kulubule tunasubiri Cha pili!
tatizo huyu jamaa naye anapendaga sana kuitwa itwa mkuu mkuu,tunaomba,tunaomba,kama umeamua kuwapa burudani basi fanya hivyo,kuna watu wakiamua ku post story wanapost kweli×2..any way atakuja na hoja zake naye mara sishindi jamii,mda si mlefu mtasikia mb,,hata mzuka wa kusoma unapotea aiseeee..!!
 
tatizo huyu jamaa naye anapendaga sana kuitwa itwa mkuu mkuu,tunaomba,tunaomba,kama umeamua kuwapa burudani basi fanya hivyo,kuna watu wakiamua ku post story wanapost kweli×2..any way atakuja na hoja zake naye mara sishindi jamii,mda si mlefu mtasikia mb,,hata mzuka wa kusoma unapotea aiseeee..!!
Nimekuita hapa ndugu? Unadhani kila mara niko online usipoweza kusubiri tafuta nyuzi zingine usome
 
Nimekuita hapa ndugu? Unadhani kila mara niko online usipoweza kusubiri tafuta nyuzi zingine usome
honestly this is not good! Kwa nn unatutesa? Yan tuwe tunakuomba omba kila saa kama unazo s uweke tu episodes za kutosha? Sio vizur mkuu hata ungekua wewe ungekwazika na hiki kitu unafanya, saa huo muda ulomjibu hapo s ungeweka hata ngapi basi? Ama kweli bure ghali
 
honestly this is not good! Kwa nn unatutesa? Yan tuwe tunakuomba omba kila saa kama unazo s uweke tu episodes za kutosha? Sio vizur mkuu hata ungekua wewe ungekwazika na hiki kitu unafanya, saa huo muda ulomjibu hapo s ungeweka hata ngapi basi? Ama kweli bure ghali
tulia madame,,hope ungekuwa nayo ww hii,daaaa..........
 
Guys kwa mfano ndio narudi home now Sadeki imenibana kesho nitawapa vigongo
 
SIRI
episode 15
Mtunzi. Patrick CK

Kama maelekezo ya kazi
aliyopewa yanavyompasa kufanya,
baada ya kunasa maongezi kati ya
Edger na Stanley bila kupoteza
muda Judy akayatuma moja kwa
moja kwa Paul mkuu wake wa kazi
nchini Tanzania.Paul akiwa ofisini
kwake akisubiri taarifa toka kwa
vijana wake aliowatumakumfuatilia Damian Mwamba
akapokea faili lililotumwa na Judy
akalifungua na kutoa tabasamu.
“Judu anafanya kazi nzuri
sana” akawaza na kuanza
kuyasikiliza mazungumzo yale ya
Edger na Stanley.Akarudia kwa
mara ya pili kuyasikiliza kwa
makini sana halafu akampigia simu
Donald Nkebo
“Paul kuna habari gani mpya?
Donald Nkebo akauliza baada ya
kuipokea simu ya Paul
“Mr Donald kuna taarifa
nimeipata sasa hivi toka kwa Judy
ambayo ninadhani unapaswa
kuisikiliza.Ninakutumia sasa hivi”
akasema Paul “Sawa Paul.Nitumie sasa hivi
niisikilze halafu nikuelekeze nini
cha kufanya.” Mr Nkebo akajibu
akiwa na shauku ya kutaka kujua
kilichomo ndani ya maongezi hayo
Kwa haraka Paul akamtumia
Donald Nkebo maongezi yale ya
Edger na Stanley. Kama ilivyokuwa
kwa Paul,Dr Nkebo naye
akayarudia maongezi yale zaidi ya
mara mbili halafu akashika kichwa
akitafakari.
“Huyu kijana anaonekana ana
nia ya dhati ya kugombea urais.Ni
lazima tumdhibiti haraka
iwezekanavyo.Tukimuachia
mwanya hata kidogo anaweza
akatusababishia matatizo makubwa.Anafikiria hata
kuutangazia umma kwamba
aliwekewa sumu na watu kutoka
ndani ya chama chake,hatupaswi
kumuacha akafanya hivi.nadhani
wakati umefika wa
kuwanyamazisha watu hawa
wawili Edger na huyu mwenzake
Stanley anayeonekana kuwa
mshauri wake mkuu.Hii ni kazi ya
haraka ambayo Paul anatakiwa
aifanye haraka sana”akawaza
Donald na kumpigia Paul simu
“Mr Donald” akasema Paul
“Paul nimeyasikiliza
mazungumzo yao.Kwanza kabisa
nimegundua Edger anapata
msaada mkubwa wa kimawazo toka kwa huyu Stanley ambaye
anaonekana ndiye mshauri wake
mkuu.Nataka utumie kila mbinu
unayoijua mpaka leo jioni uwe
umekwisha mfahamu huyo Stanley
ni nani na uanze mara moja
kutafuta namna ya
kumnyamazisha.Edger akimkosa
huyu Stanley atavunjika moyo
kwani yeye ndiye mwenye kusuka
mipango yake yote.Jambo lingine
Edger anaonekana kukubaliana na
ushauri wa Stanley wa kutaka
kuhama chama ili akagombee uraisi
katika chama cha upinzani.Vile vile
anafikiria kuutangazia kwamba
alipewa sumu ili afe na hili si jambo
zuri hata kidogo.Edger anatakiwa adhibtiwe haraka sana kabla
hajatoka hospitali na kuanza
harakati zake za urais.Nataka
mipango ya kumuondoa Edger
ianze haraka sana.Vipi kuhusu
Damiani mmefikia wapi? Akauliza
Donald
“Donald kwanza kuhusu Edger
sishauri kumuondoa kwa
sasa,tuendelee kumchunguza ili
tuufahamu mtandao wake
wote.Huyu Stanley tutamuondoa
haraka sana ili kuzidi kummaliza
nguvu Edger na mipango ya
kumuondoa inaanza haraka
sana.Kuhusu Damiani mwamba
tunaendelea vizuri na leo tunaanza
kupiga hatua ya awali kwa Mr Mwamba.Tunachotaka kukifanya
kwanza ni kutega kifaa maalum
katika simu yake ambacho
kitakuwa kikituonyesha kila
mahala anapokuwa.Nina imani
mpaka jioni ya leo nitakupa taarifa
kamili ya wapi tumefikia kuhusu
Damiani.Vijana wanafanya kazi
usiku na mchana”
“Nanafurahi kusikia hivyo
Paul.Ongeza bidii ili mheshimiwa
rais aanze kusikia hatua
tunazozichukua.”
“Nimekuelewa Mr
Donald,tunajitahidi sana na
ninakuahidi kazi nzuri
itakayomfurahisha hata
Mheshimiwa rais”akasema paul na kukata simu

*******************
Blue Lavender hotel ni moja
kati ya hoteli iliyojizolea umaarufu
mkubwa ndani na nje ya nchi kwa
upikaji wa vyakula vya kila aina na
vya mataifa mbali mbali.Ni hoteli
hii ambayo Damiani Mwamba
hufika mara kwa mara hasa nyakati
za asubuhi kupata supu.Kwa siku
kadhaa sasa amekuwa akifuatiliwa
na vijana wa Paul
wanaomchunguza bila yeye
kufahamu.Moja kati ya vitu
walivyovigundua katika uchunguzi
wao waligundua kwamba Damian anapenda sana kufika katika hoteli
hii kupata supi kila siku asubuhi.
Kama kawaida yake alishuka
garini na kuingia katika ukumbi
mzuri ulioezekwa kwa makuti safi
na kuifanya mandhari ya hapa
kuwa ya kuvutia mno,akaenda
katika meza ambayo imezoeleka
kama meza yam zee Damian akakaa
huku akisoma gazeti wakati
akisubiri supu.Hakuwa na haja ya
kuagiza kwani anafahamika sana
hapa.Imekuwa ni kawaida yake kila
siku kununua magazeti na kuja
nayo hapa na kuyasoma huku
wakati akiendelea kupata supu.
Dakika tatu toka awasili katika
hoteli hii,vijana wawili waliovalia suti safi walioonekana kama
wafanya biashara wakubwa nao
wanawasili na kukaa katika meza
ya karibu kabisa na Damian
Mwamba nao hali kadhalika
wakaagiza supu.Damian akiwa
mezani peke yake hakuweza
kung’amua kuwa vijana wale
wawili waliokuwa wamekaa karibu
yake ni vijana hatari waliokuwa
wakifanya kazi ya kumfuatilia usiku
na mchana na kujua nyendo
zake.Vijana wale waliendelea na
maongezi yao kama kwaida huku
wakipata supu waliyokuwa
wameagiza huku Damiani
akiendelea kusoma gazeti lake.
Akiwa amezamisha mawazo yake katika gazeti lile kubwa
lililosheheni habari mbali mbali za
siasa mara ghafla kikatokea
kishindo kikubwa cha mlipuko wa
kitu na kuzua taharuki kubwa huku
wateja wengine waliokuwepo hapo
hotelini wakianguka kwa
mstuko.Kama umeme kijana mmoja
kati ya wale wawili waliokuwa
wakimfuatilia Damiani Mwamba
akajirusha toka pale mahala
alipokuwa amekaa na kumpiga
kichwa kizito Damian Mwamba
akaanguka na kupoteza
fahamu.Kijana ambaye naye
alianguka chini kwa kasi ya aina
yake akaingiza mkono mfukoni kwa
Mr Damiani na kuitoa simu yake.Akaifungua kwa haraka na
kupachika kidude Fulani kidogo
sana chenye muundo kama karatasi
katika mfuniko wa simu ile
ambacho si rahisi kwa mtu kuweza
kuking’amua kuwa kimepachikwa
hapo.Akaifunga simu ile na
kuirudisha mfukoni mwa Mr
Mwamba.Ni kitendo kilichochukua
sekunde zisizozidi ishirini.Hakuna
mtu yeyote aliyeweza kukishuhudia
kitendo kile kwa sababu watu wote
kwa sasa walikuwa ndani ya
taharuki kubwa kutokana na
kishindo kile cha mlipuko na kila
mmoja alikuwa akijaribu
kujiokoa.Ni kitendo kilichofanyika
kwa haraka,wepesi na umakini wa hali ya juu sana kisha vijana wale
wakatoweka.
Dakika kama kumi hivi tangu
kishindo kile cha mlipuko
kitokee,gari nne za polisi zikafika
kwa kasi zikiwa zimesheheni askari
wenye silaha waliojizatiti vilivyo
,nyuma yao kulikuwa na gari
kubwa la kuzima moto.Haraka
haraka na kwa umakini wa aina
yake polisi wakaanza kudhibiti hali
ya usalama na kuanza zoezi la
kuwaondoa watu waliokuwamo
hapo hotelini ambao wengine
walikuwa wamejeruhiwa kwa
kukatwa na vitu kama chupa au
kuunguzwa na vitu vya moto.Wapo
watu wachache waliokuwa wamepoteza fahamu kutokana na
kishindo cha mlipuko ule.Gari tatu
za wagonjwa zilikuwa tayari
zimefika na kuwapakia wale
wagonjwa waliokuwa wameumia
na wengine kupoteza fahamu
wakakimbizwa katika hospitali ya
karibu kwa matibabu.Miongoni
mwa watu waliokuwa wamepoteza
fahamu alikuwapo Damiani
Mwamba .
Katika maegesho ya magari
kulikuwa na magari matatu
yaliyokuwa yakiwaka moto na
kikosi cha zimamoto kilikuwa
kikiendelea na kazi ya kuuzima
moto ule ili usije ukasambaa katika
magari mengine na kusababisha maafa makubwa zaidi.Watu wote
walikwisha tolewa mahala hapa
ambapo kwa sasa palionekana
kama si mahala salama .Wataalamu
wa milipuko kutoka jeshi la
wananachi wa Tanzania
wakishirikiana na wale wa jeshi la
polisi waliwasili na kuanza mara
moja kazi ya kuchunguza chanzo
cha mlipuko ule na kuangalia kama
kuna dalili zozote za kutokea
milipuko zaidi.

*******************
Sekunde ambayo yule kijana
,aliweka kile kifaa kilicho kama
karatasi katika simu ya Damian Mwamba,Paul akaiona taa ya kijani
ikiwaka katika mitambo yake
ishara kwamba kifaa kile kinafanya
kazi akatabasamu.Muda huo huo
akachukua simu na kumpigia
Damian Nkebo
“Paul kuna habari gani mpya?
Donald Nkebo akauliza
“Mr Nkebo ,nimeona
nikutaarifu habari nzuri kwamba
dakika kadhaa zilizopita vijana
wangu wamefanikiwa kuweka kifaa
maalum katika simu ya Damian
mwamba ambacho kitakuwa
kikitupa mwelekeo kamili wa kila
mahala anapokuwa Mr
Mwamba.Kama unavyofahamu yule
ni mfanyabiashara mkubwa kwa hiyo kila mahala aendapo ni lazima
awe na simu yake kwa maana hiyo
hivi sasa tutakuwa tukimfuatilia
kwa masaa ishirini na
manne.Tutaweza kujua yuko
wapi,anaongea na nani na
anaongea nini.Nina imani baada ya
muda mfupi ujao tutakuwa
tumepata kitu cha kuweza
kumwondoa kabisa katika
ulimwengu huu wa siasa.”
“Kazi nzuri sana Paul”akasema
Donald Nkebo
“Hata hivyo Mr Donald wakati
wa kutekeleza jambo hilo
tulilazimika kufanya tukio dogo ili
kufanikisha shughuli nzima”
“Tukio dogo? Hebu nifafanulie”akauliza Donald
akionekana kuwa na wasiwasi
kidogo
“Tulilazimika kufanya mlipuko
mdogo ndani ya gari moja
tulilokuwa tumeliegesha pale kwa
zaidi ya siku mbili.Damian
Mwamba ana mazoea ya kwenda
kupata supu katika hoteli ile kila
siku hivyo tukalazimika kufanya
tukio dogo ili kuweza kufanikisha
mpango wetu”
“Paul hakuna madhara yoyote
yaliyotokea?Nina uliza hivyo kwa
sababu lazima uchunguzi
utafanyika.Nataka nipate picha
kamili ili na mimi nije kitu cha
kufanya”akasema Donald “Ulikuwa ni mlipuko ambao
haukusababisha kifo au madhara
makubwa kwa hoteli zaidi ya gari
mbili zilizokuwa karibu na gari letu
lililokuwa limebeba mlipuko ule
kuwaka moto.Vijana wetu wote
wako salama salimini na kwa hivi
sasa wako njiani wanarudi ofisini
baada ya kuikamilisha kazi.Nitazidi
kukupa taarifa kadiri tunavyopiga
hatua.Nimeona nikujulishe ili kama
kutatokea tatizo lolote basi uwe
tayari kulimaliza haraka”
“Sawa Paul,kazi nzuri sana
Paul.Endelea kunipa taarifa ya kila
tukio linalotokea.Na kama una
tatizo lolote lile usisite
kunifahamisha.Ukumbuke katika operesheni hii tunao mkono wenye
nguvu wa mheshimiwa rais kwa
hiyo usiwe na wasi wasi na kitu
chochote kile.”
“Nalielewa hilo Mr Nkebo na
nitakueleza iwapo kuna mahala
tumekwama au la”
Paul akakata simu akaigeukia
mitambo yake.
“Sasa umeingia katika mikono
yetu Damian.Kiama chako
kimefika.Taratibu sana
tutakupoteza katika uwanja wa
siasa” akawaza Paul huku akicheza
na kompyuta

******************** Taratibu Mr Damiani Mwamba
alianza kurejewa na
fahamu.Akapepesa macho ili
kutazama vizuri akagundua
alikuwa katika chumba kilichokuwa
na harufu kali ya dawa.Mara moja
akapata picha kuwa mahala hapa ni
hospitali.
“Mzee mwamba unajisikiaje
sasa? Daktari aliyekuwa pembeni
akauliza baada ya kugundua mzee
Damiani mwamba tayari
amekwisha rejewa na fahamu zake.
“Kichwa kinaniuma
sana.Siwezi hata kukiinua” Akajibu
Mr Mwamba kwa taabu.
“Pole sana.Inaonekana
uligonga kichwa chako katiak sehemu ngumu baada ya mlipuko
kutokea” Daktari na kumbukumbu
ya tukio lililotokea Blue lavender
hotel ikarejea kichwani
“Daktari vipimo vyako
vinaonyesha nimeumia kiasi gani?
Akauliza Damian kwa wasiwasi
“Mr Mwamba vipimo
vinaonyesha kuwa haukuumia sana
zaidi ya kupoteza fahamu baada ya
kugongesha kichwa katika kitu
kigumu na mstuko ule ukakufanya
upoteze fahamu”
“Kwa hiyo ninaweza
kuruhusiwa kurudi nyumbani
leo?akauliza Damian
“Ndiyo Mr
Mwamba.Tutakufanyia tena vipimo kwa mara ya pili na kama
hatutaona tatizo lolote
tutakuruhusu uende
nyumbani”akasema daktari.Damian
mwamba akarejesha kumbu kumbu
hotelini ulikotokea mlipuko ule.
“Kitu gani kilisababisha
mlipuko ule?Lilikuwa ni bomu au ni
mtungi wa gesi? Akajiuliza
“Lakini kishindo kilikuwa
kikubwa sana na sina hakika kama
kishindo kile kilikuwa ni cha
mtungi wa gesi. Yawezekana likawa
ni bomu.Kama ni bomu lilikuwa la
kutegwa?Na kama lilitegwa nini
hasa malengo yake?akaendelea
kujiuliza
“Nisiumize kichwa sana kwa sasa.Nikitoka hapa nitapata ripoti
kamili ya kilichotokea.Nashukuru
Mungu niko salama.” Akawaza Mr
Mwamba
HAIFA - ISRAEL
Baada ya kutoka hospitalini Dr
Olivia akarejea tena hotelini kwake
kupumzika.Alipojilaza kitandani
akaanza kutafakari juu ya
kilichotokea hospitali
“Nahisi Edger hakufurahishwa
na Christopher na ndiyo maana
alionyesha mabadiliko ya ghafla
mara tu Chris alipokuja kukaa nasi
pale bustanini.Wakati
nikizungumza na Chris alikuwa
mkimya na hakutaka kuzungumza chochote,na mara tu baada ya Chris
kuondoka Edger aliomba
nimrudishe ndani na hakutaka tena
kukaa na mimi.Kuna kitu
kinamsumbua yule jamaa” akawaza
Dr Olivia na kutabasamu baada ya
sura ya Christopher kumjia
kichwani
“Christopher ni kijana
mzuri,anayevutia kukaa na
kuongea naye.Amenivutia
sana.Nitajaribu kumshawishi aje
Tanzania. Akikubali nitafurahi
sana” akaendelea kuwaza Dr Olivia
“Lakini kwa nini nisimpigie
simu na kuongea naye sasa
hivi?Nadhani hili ni wazo zuri sana
ngoja nipige simu pale hospitali niombe kuzungumza na
Christopher” Dr Olivia akawaza
huku akiinuka na kuiendea simu
iliyokuwapo pale
mezani,akabonyeza namba za
hospitali ile alimolazwa
Christopher ,na simu ikapokelewa
na mwanadada mwenye sauti nzuri
Olivia akaomba aunganishwe na
chumba cha Christopher.Baada ya
sekunde kadhaa akaisikia sauti
nzuri ya kiume ikiita
“Halloo Dr Olivia”
“Hallo Chris unajisikiaje?
Olivia akauliza
“Najisikia vizuri,maendeleo
yangu ni mazuri sana.Uko wapi
sasa hivi Olivia,hotelini?akauliza Christopher
“Ndiyo niko hotelini
nilikofikia.Sina mtu wa
kuzungumza naye naye nikaona
nikupigie japo tuongee machache
kama sintakuwa nakusumbua.” Dr
Sanda akasema
“Ni kama ulikuwa katika
mawazo yangu Olivia kwani hata
mimi ninajisikia mpweke sana hapa
hospitalini na nilitamani kupata
mtu wa kuzungumza naye.Nafurahi
sana kukutana na waafrika
wenzangu japokuwa hatutoki
katika nchi moja lakini tunaweza
kuishi kama ndugu ndugu
moja”akasema Christopher na
sekunde kadhaa zikapita halafu akasema
“Dr Olivia hoteli ulikofikia ni
mbali sana na hapa
hospitali?akauliza Christopher
“Hapana hakuna umbali mrefu
ni mwendo wa dakika kumi tu.Kuna
nini Christopher?akauliza Dr Olivia
“Olivia kama hutajali,na kama
unayo nafasi kwa nini usije hapa
hospitali tukakaa ,tukaongea na
kufahamiana zaidi kwa sababu
naona kama siku imesimama masaa
hayaendi”akasema Christopher
“Wazo lako zuri Chris.Nitafika
hapo si muda mrefu kwani hata
mimi nimeboreka sana hapa
hotelini”
Dr Olivia akasimama akiwa ni mwingi wa furaha.
“Kwa kuwa Edger alisema
anahitaji kuwa mwenyewe leo
apumzike,ngoja niitumie nafasi hii
kwenda kuongea na Chris.Ni kijana
mchangamfu,anayefurahisha na
ambaye huchoki unapokuwa
naye.Nimeboreka sana peke yangu
hapa hotelini,Judy yeye anapenda
kujifungia chumbani kwake”
Dr Olivia akawaza huku
akifungua mkebe wake wa
vipodozi.Haraka haraka bila
kupoteza muda akajiweka vizuri
halafu akamfuata Judy chumbani
kwake akamuaga kuwa anakwenda
hospitali.
Dakika kumi na tano baadae akawasili hospitalini akaenda
mapokezi akaomba Chris ataarifiwe
kwamba amekwisha fika na
atamkuta bustanini.Dakika tano
baadae Chris akashuka na kukutana
na Olivia
“Nashukuru kwa kufika kwako
Dr Olivia.Siku yangu nahisi kama
ilikuwa imesimama.Sehemu kama
hii ni nadra sana kukutana na mtu
kutoka afrika na ikitokea bahati
umekutana naye inakuwa ni faraja
kubwa sana.Nasikia furaha
kukutana nawe Dr Olivia.Najihisi
kama niko nyumbani”akasema
Christopher
Dr Olivia huku akitabasamu
akajibu “Hata mimi nafurahi sana
kukutana nawe.Mara ya kwanza
kufika hapa nilikuwa mpweke sana
kwa sababu Edger hakuwa na
fahamu na sikuwa na mtu yeyote
wa kutoka nyumbani wa kuongea
naye.Baadae akatumwa Judy kuja
kunisaidia kumuuguza Chris kidogo
nikafarijika” akasema Dr Olivia
“Dr Olivia samahani kwa
kuuliza swali hili je wewe na Edger
mna mahusiano yoyote ya
kimapenzi?
Dr Olivia akacheka tena
kicheko kikubwa kilichomfanya
Christopher atabasamu.
“Kwa nini umeuliza hivyo
Chris? Dr Olivia akacheka huku akitabasamu
“Kwa sababu niliona dalili
Fulani za wivu machoni mwa Edger
wakati nimekaa na ninyi asubuhi ya
leo hapa bustanini.”
Dr Olivia akacheka kidogo na
kusema
“Mimi na Edger,hatuna
mahusiano yoyote ya
kimapenzi.Edger ni mgonjwa
wangu na ni mimi ndiye niliyemleta
hapa Israel kwa matibabu.Sikuwa
nikifahaiana naye hadi alipoletwa
katika hospitali yetu akiwa
mgonjwa hajitambui.Yeye ni
mwanasiasa na mimi ni
daktari”akasema Dr Olivia
“Niliogopa kwa namna Edger alivyokuwa ananitazama nikajual
labda wewe nay eye mna
mahusiano ya kimapenzi.Lini
unategemea kurudi nyumbani
Tanzania?”
“Kurudi nyumbani inategemea
na hali ya ugonjwa wa Edger
inavyoendelea.Iwapo atapata nafuu
kwa haraka basi nitarejea
nyumbani hivi karibuni.Siwezi
kumuacha Edger peke yake wakati
mimi ndiye niliyemleta huku
Israel.Ungependa kuja kutembea
Tanzania siku moja?
“Lazima nitakuja Tanzania
mara tu baada ya
kupona.Ninaipenda sana Tanzania.”
“Nitafurahi sana kama utafika kutembea Tanzania.lakini
ningefurahi zaidi iwapo ukija
Tanzania ufike katika hospitali yetu
na mimi niwe daktari wako”
Christopher akacheka baada
ya kauli ile ya Dr Olivia
“Hata mimi ningefurahi sana
kama ungekuwa daktari
wangu.Ningejua mapema
kama kuna hospitali nzuri Tanzania
inayotibu maradhi haya ya moyo
nisingepoteza wakati wangu kuja
kutibiwa huku Israel,ningekuja
moja kwa moja Tanzania”
“Muda wowote karibu sana
Tanzania.Nitakuwa mwenyeji
wako”
Maongezi kati ya Chris na Dr Olivia yakaendelea hadi usiku wa
saa nne .Ni mara ya kwanza kwao
kukutana lakini kwa muda huu
mfupi walitokea kuzoeana kupita
kiasi.
 
SIRI

Episode 16

Mtunzi. Patrick CK

Judy alipiga simu hospitali
akaomba kuzungumza na Edger
kaka ambaye alipelekewa
simu.Tayari alikwisha anza
kupitiwa na usingizi akaamka na
kuipokea simu kutoka kwa Judy.
“Hallo Judy” akasema Edger
“Edger samahani kwa
usumbufu ni mimi Judy ninauliza
kama Dr Olivia bado yuko hapohospitali kwa sababu ni saa nne za
usiku na bado hajarejea hotelini”
“Dr Olivia?” Edger akauliza
kwa mshangao.
“Dr Olivia mbona aliondoka
hapa mchana na sijamuona
tena.Hakuniambia kama angerejea
tena hospitalini.”Edger akasema
“Unataka kuniambia hauko
naye hapo hospitali? Mbona
aliniaga kuwa anakuja hospitali?
Judy akauliza
“Mimi sijamuona.Ngoja nipige
simu mapokezi niulize kama alifika
hapa.Nitakujibu baada ya dakika
mbili.”
Edger akaanza kuwa na wasi
wasi mwingi.Akapiga simu mapokezi na kuuliza kama Dr Olivia
alionekana maeneo yale ya
hospitali mchana ule akajibiwa
kuwa Dr Olivia alikuwa bustanini
na mgonjwa toka Zimbabwe
aitwaye Chritopher .Edger akahisi
mwili wake unaloa jasho.
“This can’t be” Akasema huku
akiuma meno.
Edger akainuka na kukaa
kitandani akiwa na mawazo mengi.
“Nilihisi mapema hili
litajitokeza.Niliona namna Olivia
alivyokuwa akiongea na
Christopher pale bustanini
asubuhi.Tayari alikwisha vutiwa na
yule jamaa ndiyo maana amediriki
hata kuja hospitali bila hata kujua maendeleo yangu akaenda kuonana
na Chris.Wanawake !! akawaza
Edger
“Huko bustanini
wanazungumza nini? Ninampenda
Olivia na ninapata wivu mkubwa
kuona anakuwa na ukaribu
mkubwa na Chris kuliko hata mimi
ninayetoka naye nchi moja.Siwezi
kukubali kumpoteza Olivia just
because of a man from
nowhere.Siwezi kukubali hilo
litokee”akawaza Edger akiwa na
hasira akainuka na kuelekea
dirishani kwake akachungulia
nje.Alichoweza kuona ni mji
uliokuwa umejaa mataa mengi
kisha akazama katika fikira nzito. “Kuna kitu nimekuwa
nakifikiria toka mchana ambacho
kinaweza kunisaidia kuwa karibu
zaidi na hatimaye kumpata
Olivia.Nafikiria kurudi nyumbani
Tanzania.Kwa kuwa kwa sasa hali
yangu si mbaya sana ninaweza
kuomba uongozi wa hospitali hii
waniruhusu niweze kurudi
nyumbani na kuendelea kupata
matibabu katika hospitali
anakofanya kazi Dr Olivia.Nafikiri
hii itakuwa ni njia nzuri zaidi ya
kuniweka karibu na Olivia” Edger
akatabasamu baada ya kulipata
wazo lile.
“It’s a good idea.Lakini ngoja
kwanza niwasiliane na Stanley nijue amefikia wapi katika yale
masuala niliyomtuma
achunguze.Japokuwa Stanley
amekuwa msaada mkubwa kwangu
lakini sielewi kwa nini kila
linapokuja suala la Olivia amekuwa
akinipinga sana.Pamoja na hayo
siwezi kurudi nyuma kuhusu azma
yangu ya kugombea urais wa
Tanzania.Ni lazima nipambane na
genge lile la mafisadi wachache
wanaozifilisi rasilimali za
Tanzania.Nashukuru kwa mawazo
ya Stanley kwamba niwanie urais
kupitia chama cha upinzani kwa
sababu nguvu yangu ndani ya
chama changu ni ndogo kwa hiyo
sintaweza kupewa nafasi hiyo.Ninaamini nguvu yangu katika
umma wa watanzania ni kubwa
kuliko nguvu niliyonayo katika
chama kwa maana hiyo hata kama
nikihamia chama pinzani
watanzania kwa ujumla wao
hawatajali itikadi zao za kisiasa
wanaweza wakaamua kunipa
ridhaa ya kuwatumikia katika
nafasi ya urais” akawaza Edger
akafungua kompyuta ambayo
amekuwa akiitumia kuwasiliana na
Stanley akampigia simu
“Hallow Stanley” akasema
Edger
“Hallo Edger.Unaendeleaje?
Stanley akauliza
“Naendelea vizuri sana.Kila siku afya yangu inazidi
kuimarika.Kuna habari gani huko
nyumbani?Edger akauliza
“Huku nyumbani kwema. Ni
joto la uchaguzi linazidi kupanda”
“Du! Mbona unanitisha
Stanley? Edger akauliza
“Sikutishi Edger ila ni hali
halisi ya mambo ilivyo kwa sasa
hapa nyumbani.Kumekuwa na
mjadala mkubwa kuhusu uchaguzi
mkuu ujao na watu ambao
wameonyesha nia ya kutaka
kugombea urais.Lakini hiyo isikupe
shaka Edger kila kitu kitakwenda
vizuri” Stanley akasema na
kumfanya Edger avute pumzi
ndefu. “Vipi Edger una matatizo gani?
Don’t tell me its Olivia again”
Stanley akauliza.
“Hapana Stanley,it’s not
her.Hebu kwanza nipe habari
umefikia wapi kuhusu ule
uchunguzi niliokutaka uufanye?
Edger akauliza
“Edger nimeifanya kazi ile na
nimegundua kwamba chama
ambacho wewe kinaweza kukufaa
ni chama cha Democratic ambacho
tayari kimepata usajili wa kudumu
na kina wanachama wapatao nusu
milioni nchini kote.Japokuwa
hakina umaarufu mkubwa lakini ni
chama chenye sera safi zinazolenga
kumkomboa mtanzania.Ni chama kinachoamini katika
demokrasia,haki na usawa kwa
wote.Toka kimeanzishwa huu ni
mwaka wake wa tatu na hakijawa
bado na mbunge hata
mmoja.Uchaguzi huu utakuwa ni
uchaguzi wake wa kwanza wao
kushiriki.Kwa mujibu wa dodoso
zangu mpaka sasa hivi bado
hawajapata mtu makini ambaye
anaweza akapeperusha bendera ya
chama chao katika uchaguzi mkuu
ujao.Nafikiri iwapo watasikia
kwamba unahitaji kugombea urais
kupitia chama chao watafurahi kwa
sababu ya mvuto wako katika jamii
ya watanzania kwani chama chao
kitapaa juu kwa ghafla sana..” Edger akatafakari kwa muda
halafu akasema.
“Nimekupata vizuri
Stanley.Chama hiki kinaonekana
kizuri lakini bado kuna kazi kubwa
ya kukijenga.Inavyoonekana ni
wazi bado hakina mtandao
mkubwa wa kuwafikia wapiga kura
hadi vijijini.Unaona hili haliwezi
kuwa tatizo kwangu?
“Hilo haliwezi kuwa tatizo
Edger.Hata kama ukishindwa
uchaguzi huu tayari chama
kitakuwa kimejulikana vya kutosha
na mtaendelea na kazi moja tu ya
kukijenga chama mkisubiri
uchaguzi ujao. Au wewe unaonaje?
“Mawazo yako mazuri Stanley.Kwa sababu nimekwisha
dhamiria kuwania urais wa
Tanzania sina budi kukubali
ushauri wako wa kujiunga na
chama hicho cha upinzani japo hii
ni karata ambayo natakiwa
kuicheza kwa umakini mkubwa
sana kwani inaweza ikanivusha au
ikanizamisha kabisa
kisiasa”akasema Edger
“Safi sana Edger nimeupenda
uamuzi wako.Kitu
ninachokupendea wewe ni mtu
msikivu na mwelewa sana.Kesho
nitakutumia maelezo mbali mbali
ya kuhusu chama hiki ili uweze
kukifahamu kiundani.” Stanley
akasema “Stanley huna haja ya
kunitumia maelezo hayo kwa sasa”
Edger akasema huku akitabsamu
“kwa nini Edger .Au umebadili
mawazo? Stanley akauliza kwa
mshangao
“Hapana Stanley sijabadili
uamuzi.Nia yangu ya kuwa rais wa
Tanzania na kupambana na genge
la mafisadi iko pale pale na ni
lazima niitimize.Nimesema huna
haja ya kunitumia kwa sababu I’m
coming back home”
“What !! “ Stanley akastuka
“Yes.I’m coming back home”
“Mbona sikuelewi Edger
.Umeshapona?
“Sijapona ,ila nieamua kurudi nyumbani.I’m much better now
kwa hiyo siwezi kuendelea kukaa
huku wakati kuna mambo mengi
yanayonikabili”
Stanley akanyamaza kidogo
halafu akasema
“Edger ni lazima kuna sababu
ya kuamua kurudi
nyumbani,usinifiche tafadhali
nieleze kama una tatizo “
“Sina tatizo Stanley ,nimeamua
tu kurudi nyumbani”
“Nakufahamu vizuri
Edger,kuna kitu unanificha.Please
tell me” Stanley akasisistiza
Edger akafikiri kwa sekunde
chache halafu akasema
“Stanley to be honest, it’s because of her.Siwezi kukuficha
Stanley I love this woman with all
my heart lakini ninashindwa
kumwambia.Sijui nitaanzaje
kumweleza kwamba nimetokea
kumpenda na ningetaka awe
mpenzi wangu.Tatizo lililonifanya
mpaka nifikirie kurudi nyumbani ni
kwamba leo hii amekutana na
jamaa mmoja toka nchini
Zimbabwe anaitwa Christopher
Mpaka usiku huu yuko naye
bustanini sijui wanaongea
nini.Nimeamua kurudi nyumbani ili
niweze kuwa karibu na Olivia kwa
sababu najua iwapo nikirudi
nitakuwa nikitibiwa katika
hospitali yake na hilo litanifanya kuwa karibu naye zaidi” akasema
Edger.
“Kaka yangu Stanley
nakuomba tafadhali usione kama
vile ninataka kuingilia masuala
yako binafsi lakini ninakupa
tahadhari kwamba kama unataka
kufanikisha azma yako ya kuwania
urais wa Tanzania basi haraka sana
achana na Olivia.I’m sorry to say
this lakini Olivia ni hatari kuwa
naye kwa sasa.Sitaki kuongea sana
lakini rafiki yangu kabla
hatujasonga mbele zaidi nataka
uamue kitu kimoja kwamba
unataka kugombea urais au
unamtaka Olivia? Fanya maamuzi
halafu utanitaarifu umeamua nini” Stanley akakata simu.Edger akabaki
ameushikilia mkono wa simu akiwa
amepigw ana butwaa.
“Stanley ana nini na huyu
mwanamke?Kwa nini suala la
kutaka kuanzisha mahusiano na
Olivia linamuumiza sana? Kwa nini
hataki kuniweka wazi kama kuna
kitu kibaya anakifahamu kuhusu
Olivia?Hata hivyo Olivia
ninampenda na siwezi katu
kumuacha” akawaza Edger.
Bustanini Dr Olivia na Dick au
Christopher akam alivyokuwa
akitambulika kule Israel,waliagana
na Dick akarejea chumbani
kwake.Kulikuwa kimya
sana,wagonjwa wengi walikuwa wamelala.Toka alipofika hapa
hospitali Dick alikuwa anafanya
uchunguzi wake namna hospitali
hii ilivyokaa na ndani ya muda huu
mfupi aliweza kufahamu mambo
mengi ya hospitali hii.
Chumba chake na chumba
alimolazwa Edger vilikuwa karibu
sana akaingia chumbani kwake
akalifungua sandukua akatoa
kichupa Fulani kidogo sana kilicho
na muundo kama chupa za uturi
akatoka mle chumbani akaangaza
pande zote kama kuna mtu maeneo
yale ya karibu lakini hata wauguzi
nao walikwisha jipumzisha katika
vyumba vyao,akaenda katika
chumba cha Edger akausukuma mlango mkubwa wa kioo.Baada ya
kuufungua mlango ule akakipulizia
kichupa kile kidogo alichokishika
mkononi katika chumba cha Edger
halafu akafunga mlango na kurejea
chumbani kwake.
“Ndani ya dakika kumi na tano
naamini atakuwa amelala na mimi
nitakwenda kufanya kazi yangu”
akawaza Dick na kuanza kuandaa
vifaa vyake.
Baada ya dakika kumi na tano
kama alivyokuwa amepanga Dick
akatoka katika chumba chake
akachungulia kamakuna mtu
yeyote karibu lakini kulikuwa
kimya,akaenda katika chumba cha
Edger akausukuma mlango na kuingia ndani Edger alikuwa
amelala fofofo kitandani, akamfuata
akajaribu kumuita lakini Edger
hakuitika.Bila kupoteza muda
akaanza kufunga kamera ndani ya
kile chumba.Ni zoezi lililochukua
muda mfupi kisha akatoka na
kurejea chumbani kwake akawasha
kompyuta yake na baada ya muda
akaanza kupata picha kutoka katika
chumba cha Edger
“Sasa mambo yanakwenda
vyema.Nitaweza kujua kila
kinachoendelea katika maisha ya
Edger hapa hospitali” akawaza
Dick.
**************************
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom