HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,444
- 6,201
- Thread starter
- #41
SIRI
episode 8
Mtunzi. Patrick CK
************
Kumepambazuka Tanzania na
habari kuu iliyotawala vinywani
mwa watu na katika vyombo vyote
vya habari ni hali tete ya
mheshimiwa Edger Kaka.Hali yake
bado iliendelea kuwa siri na
kilichowachanganya zaidi watu ni
taarifa za kusafirishwa kwake
kupelekwa nje ya nchi kwa
siri.Gazeti moja la kila siku
linaloandika habari za kiuchunguzi
lilizipata taarifa za Edger
kusafirishwa kwenda nje ya nchi na
kuandika kichwa kikubwa cha
habari chenye maandishi mekundu. EDGER ASAFIRISHWA NJE YA
NCHI KWA SIRI.Ndivyo
kilivyoandikwa kichwa cha habari
cha gazeti hili pendwa lenye kutoa
habari za kina na
uhakika.Waandishi wa habari wa
gazeti hili walikuwa wamepiga
kambi katika hospitali aliyolazwa
mheshimiwa Edger mpaka usiku
wa manane na kuhakiksha kuwa ni
kweli Edger alisafirishwa nje ya
nchi.Kwa nini asafirishwe kwa siri
namna ile lilibaki ni swali gumu
ambalo hakuna aliyekuwa na jibu
lake.
Spika wa bunge alirejea
Dodoma alfajiri na mapema tayari
kwa kuendelea kuongoza vikao vya bunge.Saa tatu kamili kama
kawaida kikao cha bunge kikaanza
kikiongozwa na Spika ambaye
alianza kwa kusoma dua halafu
akawaruhusu wabunge
waketi.Walipoketi wote Spika
akasimama na kutoa taarifa fupi.
“Waheshimiwa wabunge,jana
katika kikao cha asubuhi mbunge
mwenzetu Edger kaka alipatwa na
ugonjwa wa ghafla.Alikimbizwa
katika zahanati yetu ya bunge lakini
hali yake haikuwa nzuri
,akahamishiwa katika hospitali ya
St Francis hapa Dodoma ambako
madaktari wakashauri kuwa
ahamishiwe katika hospitali kuu ya
moyo iliyoko Dar es salaam.Mheshimiwa Edger
akakimbizwa Dar es salaam jana
mchana na kupokelewa katika
hospitali kuu ya moyo.Madkatari
walijitahidi sana kumuhudumia
mheshimiwa mbunge lakini bado
tatizo lilionekana kukomaa hivyo
wakashauri mbunge ahamishiwe
nje ya nchi.Taratibu za kusafirisha
mgonjwa nje ya nchi nafikiri wote
mnazifahamu isingewezekana kwa
usiku ule kuweza kukamilisha
taratibu zote.Namshukuru
mheshimiwa rais kwa sababu yeye
alitoa maelekezo kuwa Edger
apelekwe nje ya nchi na alitoa
ndege yake itumike kumsafirisha
mheshimiwa Edger kuelekea nchini Israel pamoja naye alikuwepo Dr
Olivia Themba.Bado tunajitahidi
kuwasiliana nao kwa kutumia
ubalozi wetu nchini Israel.Taarifa
zote tutakazopata tutakuwa
tukiwataarifu.Nawashukuru sana
madaktari wote kuanzia madaktari
wetu wa bunge na katika hospitali
zote alikopelekwa mheshimiwa
Edger.Tuzidi kumuombea ili Mungu
amjalie uponaji wa
haraka”akasema spika. Kupitia
taarifa hii fupi ya mheshimiwa
spika,bunge na taifa liliweza kujua
kinachoendelea kuhusu Edger
kaka.Nyoyo za watanzania na hasa
mashabiki wa Edger zilitulia wakati wakisubiri kupata taarifa zaidi za
maendeleo yake nchini Israel.
HAIFA - ISRAEL
Rambam medical center moja
kati ya hospitali kubwa za rufaa
nchini Israel,ilianzishwa mwaka
1938.Ikiwa na vitanda vya
wagonjwa zaidi ya 2000,na
madaktari zaidi ya 700 ,idara za
kila ugonjwa na wafanyakazi
wenye taaluma na
uzoefu,inahudumia watu zaidi ya
milioni mbili.
Toka katika uwanja wa ndege
wa kimataifa wa Haifa moja kati ya
uwanja mkongwe kabisa na wa kwanza kujengwa nchini
Israel,Edger akiwa katika gari la
wagonjwa akawahishwa
hospitalini.Kwa kuwa walikwisha
taariwa juu ya mgonjwa huyu mara
tu gari la wagonjwa lilipofika
hakukuwa na muda wa
kupoteza.Kwa haraka akaingizwa
katika chumba cha wagonjwa
mahututi akaanza kuhudumiwa.
Dr Olivia alikuwa amechoka
kwa kazi kubwa aliyoifanya toka
alipompokea Edger.Akachukuliwa
na daktari mkuu hadi ofisini kwake
na kutoa maelezo ya kina ya
ugonjwa wake.Baada ya maelezo
yale Dr Olivia akachukuliwa na
kupelekwa katika hoteli moja kubwa mjini Haifa iitwayo
Leaonardo Hotel.Hoteli hii iko
katikati ya Mlima Carmel na bahari
ya Mediteranea.Chumba chake
kilikwisha andaliwa tayari na kwa
uchovu aliokuwa nao akajitupa
kitandani na kuanza kutafakari kwa
kina juu ya mshike mshike
alioupata.
“Naomba Mungu amsaidie
mgonjwa wangu aweze
kupona.Kwa hapa tulipofika nina
imani atapona.Mungu yuko upande
wetu” Akawaza Olivia na kupitiwa
na usingizi
Saa kumi na moja za asubuhi
akastushwa na mlio wa simu ya mezani iliyo chumbani.Akainuka na
kuipokea
“Hallo” akaita Dr Olivia
“Dr Jacob ninaongea toka
hospitali ya Rambam.”
“Dr Jacob.Mgonjwa
anaendeleaje?
“Hali ya mgonjwa ndiyo
iliyonifanya nikupigie simu mida
hii.Nakuomba tuonane saa mbili leo
asubuhi” Akasema Dr Jacob.
“Sawa Dr Jacob Nitafika mida
hiyo”akasema Dr Olivia na kukata
simu
Dr Olivia akaanza kuingiwa na
wasi wasi mwingi kutokana na
mwito ule wa Dr Jacob. “Inawezekana hali ya mgonjwa
ni tete sana.Nina wasi wasi na
maisha ya mgonjwa.Kama hawa
wakishindwa sijui kama kuna
sehemu nyingine tena ambayo
wanaweza kuutibu ugonjwa ule
usioeleweka” Akawaza Dr
Olivia.Hakuweza kulala tena.Toka
alipopigiwa simu ile akawa katika
mawazo mengi.
Kulipambazuka na kijua
kuanza kuchomoza.Dr Olivia
akasimama dirishani na
kuishuhudia mandhari ya kuvutia
ya mji huu wa Haifa asubuhi
hii.Pamoja na mandhari yote nzuri
na ya kuvutia lakini mawazo ya
Olivia yalikuwa sehemu moja tu,hospitalini kwa mheshimiwa
Edger .Akaingia bafuni kuoga na
ndipo alipogundua kuwa hakuwa
amekuja na nguo zozote za
kubadilisha.Alisafiri na pochi ndogo
iliyokuwa na vitu vyake muhimu
ambavyo huwa anavihifadhi ofisini
kwake kama kadi ya benki ,hati ya
kusafiria n.k.
“Itanibidi leo nizunguke
madukani kununua vitu vichache
vitakavyonisaidia kwa muda wote
nitakaokuwa hapa.”akawaza
Gari maalum la kukodi lilikuwa
tayari likimsubiri.Akapanda na
kuelekea hospitalini ambako Dr
Jacob alikuwepo ofisini kwake
akimsubiri “Karibu sana Dr Olivia.”
“ahsante sana Dr Jacob”
Akajibu Olivia akiwa na shauku ya
kutaka kufahamu alichoitiwa.
“Dr Olivia nimekuita ili nikupe
picha halisi ya hali ya
mgonjwa.Mgonjwa anaendelea
vizuri kwa sasa.Timu ya madaktari
wetu wamemuhudumia toka
alipofika hapa na hali yake kwa
sasa naweza kusema ni tofauti na
ile aliyokuwa nayo wakati anafika
hapa.Hata hivyo kuna kitu
tumekigundua kuhusiana na huyu
mgonjwa.Tumegundua kwamba
mgonjwa huyu alipewa sumu.”
Dr Olivia akapatwa na mstuko
wa ghafla. “Sumu aliyopewa inaitwa
Spaxloxy ambayo ikiingia mwilini
inaweza kuua kwa muda wa masaa
kuanzia saba.Katika uchunguzi
wetu tumegundua kwamba sumu
hii imeingiwa mwilini kwa kupitia
katika ngozi.Tuna wasiwasi
yawezekana amepuliziwa au
ameogea sabuni yenye sumu au
ameshika kitu kilichopakwa sumu
hiyo. Sumu hiyo ikiingia mwilini
huanza kufanya kazi taratibu na
mgonjwa hawezi kuhisi chochote
hadi baada ya masaa manne au
matano ndipo huanza kufanya kazi
kwa kasi na hapo ndipo mgonjwa
asipowahiwa anaweza
akafariki.Imekuwa bahati kwamba dawa alizowahi kupewa mgonjwa
zimemsaidia sana kwani baadhi ya
dawa alizopewa zilikuwa sahihi
kabisa katika kupambana na sumu
ile.Kitakachofuata tutamfanyia
operesheni ili kuondoa baadhi ya
sehemu ambazo zimeharibiwa na
sumu katika mwili wake.Ni
operesheni kubwa lakini nina imani
baada ya operesheni hiyo hali yake
itakuwa nzuri zaidi.Kwa sasa ondoa
shaka kwani hayuko tena katika
hatari kwa sababu tumefanikiwa
kuiondoa sumu yote
mwilini.”akasema Dr Jacob
Dr Olivia akahisi kijasho
kikimtoka baada ya taarifa ile ya Dr
Jacob.Akakohoa kidogo kurekebisha koo lake halafu
akasema
“Dr Jacob nashukuru kwa kazi
kubwa mliyoifanya na kuokoa
maisha ya Edger.Tulifanya jambo la
msingi sana kufanya maamuzi ya
kumleta mgonjwa hapa kwani
tusingeweza kugundua kama
ameathiriwa na sumu.Kwa ufupi tu
ni kwamba huyu mgonjwa ni
mwanasiasa.Ni mbunge ambaye
anapendwa na watu
wengi.Kupendwa huko
kumemfanya awe na maadui wengi
vile vile.Nina imani hata sumu hiyo
iliwekwa makusudi na maadui zake
kisiasa.Dr Jacob naomba
asiruhusiwe mtu yeyote asiye muhusika wa hospitali hii kumuona
mgonjwa zaidi yangu mimi au
nitakayemruhusu kwa sababu watu
hawa waliofanya hivi hawatasita
kumfuata Edger hadi huku .”
“Usihofu kitu Dr Olivia.Hopitali
yetu ina usalama mkubwa na
hakuna mtu yeyote anayeweza kuja
kufanya kitendo chochote kibaya
hapa.Hata hivyo tutafanya kama
ulivyoomba na tutaweka ulinzi
mkali katika chumba cha mgonjwa
na hatutamruhusu mtu yeyote
kwenda kuonana na mgonjwa.Kwa
sasa operesheni inaandaliwa na
baada ya masaa mawili tutakuwa
tumeanza na tutakutaarifu kila kitu
kitakavyokuwa kikiendelea.Naahidi kumshughulikia mgonjwa huyu
kwa kila namna tunayoweza na
atapona.Tumekuwa na mahusiano
mazuri na hospitali yako na
tunakuheshimu sana”akasema Dr
Jacob
Dr Olivia
akatabasamu,akaagana na Dr Jacob
akatoka kuelekea madukani kwa
ajili ya kujinunulia vitu vichache
vya kutumia kwa muda
atakaokuwa hapo Haifa.
TANZANIA
Ni saa mbili za usiku ikulu jijini
Dodoma rais wa Tanzania Dr Evans
mwaluba alikuwa na mfanyabiashara mkubwa Donald
Nkebo wakipata chakula cha usiku
huku wakibadilishana mawili
matatu.Ni Donald Nkebo aliyeomba
kuonana na rais Dr Evans Mwaluba
usiku huu.Dr Evans hakuweza
kukataa ombi la Mr Nkebo kwa
kuwa ni mmoja kati ya watu
muhimu na wanaoheshimika
sana,ni mmoja kati ya wafadhili
wakubwa wa chama.Ni kwa sababu
ya kutambua umuhimu wake ndiyo
maana usiku huu rais alitenga
muda ili aweze kuonana na tajiri
huyu mkubwa
“Mheshimiwa rais ni muda
sasa hatujaonana,siwezi
kukulaumu kwani nafahamu majukumu uliyonayo,na hii ndiyo
sababu nimeomba nionane nawe
walau tuzungumze kidogo”
Akasema Donald Nkebo huku
ajimiminia mvinyo katika glasi yake
“Mr Donald ni kweli muda
umepita hatujaonana nimekuwa
natafuta sana nafasi niweze
kukutana na watu wangu lakini
ninakosa,nimetingwa mno na
mambo mengi.Nimekuwa na ziara
nyingi za kitaifa na kimataifa na
ndiyo maana nimekuwa sipatikani
kwa urahisi.Leo nilipopata taarifa
kwamba uko Dodoma na unataka
kuonana nami nilifurahi
sana.Karibu sana Donald.Vipi
biashara zinaendaje? “Mr President hata mimi
ninafurahi sana kuonana
nawe.Kuhusu biashara zinakwenda
vizuri licha ya kushuka kwa
thamani ya shilingi na kuongezeka
kwa bei ya mafuta katika soko la
dunia lakini bado biashara
zinakwenda vizuri” Akasema
Donald Nkebo
“Hilo la kushuka kwa thamani
ya shilingi yetu linatuumiza vichwa
mimi na viongozi wenzangu
serikalini.Tumekwisha anza juhudi
mbali mbali za kuhakikisha shilingi
yetu inapanda thamani.Nina imani
tutafanikiwa”
“Ninakuamini mheshimiwa
rais.Naamini utafanikiwa katika hilo.Watu uliowapa dhamana ya
kulishughulikia suala hilo ni
wachapa kazi hodari.”
Dr Evans akacheka kidogo
akainua glasi yake ya mvinyo na
kupiga funda dogo.
“Mheshimiwa rais upepo wa
kisiasa unakwendaje?Naona
vuguvugu la urais ndani ya chama
limeanza kupamba moto”akasema
Donald
“Upepo wa kisiasa si
mbaya,bado unavuma vizuri
japokuwa kuna changamoto na
vikwazo lakini sina wasi wasi
nimekwisha jiweka vizuri ndani ya
chama”akasema Dr Evans “Mheshimiwa rais hata mimi
sina wasi wasi wowote na nguvu
yako ndani ya chama lakini nina
ushauri mdogo kwako.Usijipe
uhakika sana kwamba hauna
upinzani ndani ya chama”
“Kwa nini unasema hivyo
Donald?
“Kwa hali tuliyoanza kuiona
kwa sasa inaonekana hamasa ya
kuwania uteuzi imeongezeka sana
ndani ya chama.Japo hatujui bado
nani na nani wana nia ya kuwania
uteuzi huo lakini tayari dalili
zimekwisha anza kujionyesha na ni
dhahiri unaweza ukakumbana na
upinzani mkali sana” “Nakubaliana nawe
Donald,upinzani utakuwepo lakini
kwa upande wangu sina wasiwasi
wowote naamini watajitokeza
wengi kuwania uteuzi lakini
nitakayepita ni mimi.Kwa nini
unakuwa na wasi wasi Donald?
Sura ya Donald Nkebo
ikapambwa na tabasamu.Akainua
glasi yake akapiga funda kubwa
halafu akasema.
“Mheshimiwa rais hilo ndilo
hasa ambalo limenifanya nitake
kuonana nawe ili nikupe taarifa
ambazo naamini bado hujazipata”
“Karibu Donald nakusikiliza”
akasema Dr Evans “Mheshimiwa rais tayari ndani
ya chama kuna watu wamekwisha
anza kutengeneza makundi ya
kuhakikisha kuwa wanashinda
katika uteuzi” Kauli ile ikamfanya
Dr Evans kujiweka sawa
“Jana usiku nilipata taarifa
toka katika moja ya vyombo vyangu
vya taarifa kwamba kuna kikao cha
siri kilifanyika katika hoteli ya
Dodoma palace na mwenyekiti
wake alikuwa Damian Mwamba”
akanyamaza kwa sekunde kadhaa
na kuendelea
“Damian Mwamba tayari
amekwisha anza harakati za
kuwania uteuzi ndani ya
chama.Ninazo taarifa zenye uhakika kuwa tayari amekuwa na
uungwaji mkono wa kuridhisha
toka kwa wajumbe.Timu aliyoiteua
ifanye kazi ya kutengeneza
mtandao inafanya kazi yake kwa
umakini na usiri mkubwa na
kusema ukweli hawalali wanafanya
kazi usiku na mchana kuhakikisha
wanatengeneza mtandao
mkubwa.Harakati hizi Damian
amezianza kitambo sana kwa
kujenga jina katika jamii ndiyo
maana hadi sasa jina la Damiani
Mwamba linatajwa sana katika
orodha ya watu wenye sifa na
uwezo wa kuiongoza nchi
hii.Amekuwa akitoa misaada mbali
mbali kwa vikundi vya akina mama na vijana,amejenga
mashule,hospitali na kila
linapotokea suala lolote la kitaifa
amekuwa mstari wa mbele sana.Si
kwamba namuhofia Damiani lakini
kasi anayokwenda nayo ndiyo
iliyonisukuma kutaka kuonana
nawe tujadili kwa kina kuhusu
suala hili”akasema Donald
Rais akavuta pumzi ndefu na
kumuangalia Donald Nkebo
usoni.Alionyesha uoga wa dhairi
kwa maneno yale aliyoambiwa.
Nkebo akaichukua chupa na
kumimina tena mvinyo katika glasi
yake.
“Mheshimiwa rais ,wewe ni
rafiki yangu na mimi ni mmoja wa watu wanaokuunga mkono
sana,mimi na timu yangu
tulikuunga mkono katika awamu ya
kwanza na ukafanikiwa kushinda
na bado tutaendelea kukuunga
mkono.Nadhani unafahamu kuwa
pamoja na makundi yote yaliyomo
ndani ya chama lakini timu yetu
ndiyo yenye nguvu kubwa ndani na
nje ya chama,sisi ndiyo wenye
kuamua nani awe rais wa nchi hii
na nani asiwe.Tunaangalia nani
ambaye atakuwa na manufaa
kwetu na wewe bado unaonekana
kuwa na umuhimu mkubwa kwetu
ndiyo maana nimekuja
kukuhakikishia kwamba bado
tunakuunga mkono na utapita kwa awamu nyingine.Pamoja na yote
mazuri ambayo umetufanyia
mheshimiwa rais lakini kuna jambo
dogo sana umelikosea labda ni kwa
kutokujua”akasema Donald na
kunyamaza
“Jambo gani Donald?akauliza
Dr Evans
“Ni kuhusu yule mbunge Edger
kaka.Mheshimiwa rais kama
umegundua yule kijana ni tishio
kubwa kwako kisiasa.Ugonjwa
wake alioupata ghafla
umetuonyesha ni jinsi gani
anavyopendwa na watu.Sikufichi
mheshimiwa rais yule kijana ana
nguvu kubwa.Nchi yote ilizizima
baada ya taarifa kusambaa kuwa amefariki dunia.Kasi anayokuja
nayo inaleta wasi wasi
mwingi.Naamini bado hajaweka nia
ya kugombea lakini kama akiamua
kutangaza kuwania urais tutakuwa
na kazi kubwa.Naelewa hana
mtandao mkubwa ndani ya chama
lakini anaweza kushawishiwa
kujiunga na chama pinzani ili
agombee urais na kama akifanya
hivyo mheshimiwa rais basi
shughuli itakuwa ngumu.Kuna
uwezekano mkubwa kijana yule
akatwaa nchi” Donald akatulia
akanywa funda kubwa la mvinyo
akaendelea
“Kilichomtokea Edger ni
mkakati mzito wa kumuondoa katika ulingo wa siasa kwani
uwepo wake bungeni na katika
siasa ni hatari kwa watu
wengi.Edger alitakiwa afariki dunia
jana.Mheshimiwa rais kosa
ulilolifanya ni kutoa ndege yako
kumsafirisha Edger kumpeleka
kutibiwa nje ya nchi.”
Rais akatoa kitambaa na
kujifuta jasho lililoanza kumtoka.
“Donald sikujua kama tukio lile
ni makakati maalum na wala
sikuwa nikiifahamu hatari ya huyu
kijana.Kama ningeambiwa kwamba
ule ni mkakati maalum wa
kumuondoa ningeweka nguvu
yangu kubwa na kummaliza haraka
sana lakini sikujua lolote ndiyo maana nikaamua kumsaidia kuokoa
maisha yake.Donald nashukuru
umenifumbua macho kuhusu
mambo yanayoendelea chini kwa
chini ndani ya chama,nakiri hakuna
katika watu wangu wa karibu
aliyekuja kunieleza mambo haya
uliyonieleza.Nashangaa hata
washauri wangu wamekaa kimya
wakati kuna hatari kubwa
inatukabili.Ninaanza kuhisi
yawezekana hata washauri wangu
watakuwa tayari
wamesharubuniwa na ndio maana
wamekaa kimya na kusubiri
kuanguka kwangu.Haiwezekani
wakashindwa kuwa na taarifa za
kinachoendelea ndani ya chama.Ahsante sana Donald kwa
taarifa hii uliyonipa.Imenifumbua
macho” Akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais,usipate
shida yoyote mimi na timu yangu
tupo na tunakuhakikishia nafasi ya
urais ni yako ila nitakuelekeza nini
cha kufanya kama utakuwa tayari
kufuata ushauri wangu”
“Kwa nini nisifuate ushauri
wako Donald wakati wewe ndiye
uliyekuja kunifumbua macho?
Nielekeze nifanye nini.”
“Kama nilivyokwisha kueleza
mheshimiwa rais mimi na timu
yangu tutahakikisha unashinda
katika awamu ijayo lakini kuna
mambo ambayo lazima tuyafanye.Kitu cha kwanza
tunachotakiwa kukifanya ni kuunda
timu ndogo ya watu ambayo
itafanya kazi ya kuchunguza
mwenendo wa siasa na kuangalia
nini tufanye ili tuweze kupata
ushindi ambayo itakubidi
mheshimiwa rais uiwezeshe ili
iweze kufanya kazi zake kikamilifu
bila kugundulika.Timu hii itakuwa
ya watu sita ambao nitakupa
majina yao.Ni watu ambao
inakupasa uwaamini kwa sababu ni
wataalamu katika michezo hii ya
kisiasa.Kitu cha pili ambacho
tutakifanya baada ya kuunda timu
hii ni kuwanyamazisha wale wote
wanaoonekana kuwa na nguvu kisiasa na kuhatarisha urais wako
kwa kipindi kingine.”
Dr Evans akamtazama Donald
Nkebo halafu akauliza.
“Kuwanyamazisha kivipi?
“Mr resident politics is a dirty
game and to win this game you
need to play dirty too” Akasema
Nkebo.
“Bado sijakuelewa Nkebo hebu
nifafanulie vizuri”
“Mheshimiwa rais ninaposema
kumnyamazisha mtu yeyote
mwenye kuwa na nguvu kisiasa
nina maana ya kumpunguzia nguvu
aliyonayo na wakati mwingine
ikibidi hata kumuondoa katika uso
wa dunia hii iwapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.Kazi hii
si rahisi,inahitaji umakini na
wataalamu wa hali ya juu mno
ndiyo maana nikasema inabidi
tuwezeshwe ili kufanikisha
shughuli kama hizi.Kwa
kuanzia,tutaanza na wale ambao
tayari wamekwisha onyesha wazi
dhamira zao za kuwania urais kama
Mr Damian na huyu kijana
Edger.Sisi tutawashughulikia bila
hata ya mtu yeyote kuhisi kuwa
unahusika kwa namna yoyote na
wao.Ninakuhakikishia Mheshimiwa
rais kuwa hakuna mtu atakayejua
nini tunakifanya”
Sura ya rais ikajenga tabasamu
pana baada ya Donald kumchambulia kwa kina jinsi
mambo yatakavyoendeshwa ili
kuwamaliza wabaya wake
kisiasa.Mpaka wanamaliza
maongezi Dr Evans akamkabidhi
rasmi Donald Nkebo jukumu la
kuhakisha kuwa wale wote
wanasiasa wanaoonekana kuwa na
nguvu ndani na nje ya chama na
ambao wanaonyesha dhamira ya
wazi ya kugombea urais
wanamalizwa kimya kimya.Rais
alimuahidi Nkebo kumuwezesha
yeye na kamati yake kwa kila kitu
watakachohitaji,kama vile ulinzi na
fedha.Saa saba za usiku walimaliza
maongezi yao na Donald akaagana
na rais akaondoka .
episode 8
Mtunzi. Patrick CK
************
Kumepambazuka Tanzania na
habari kuu iliyotawala vinywani
mwa watu na katika vyombo vyote
vya habari ni hali tete ya
mheshimiwa Edger Kaka.Hali yake
bado iliendelea kuwa siri na
kilichowachanganya zaidi watu ni
taarifa za kusafirishwa kwake
kupelekwa nje ya nchi kwa
siri.Gazeti moja la kila siku
linaloandika habari za kiuchunguzi
lilizipata taarifa za Edger
kusafirishwa kwenda nje ya nchi na
kuandika kichwa kikubwa cha
habari chenye maandishi mekundu. EDGER ASAFIRISHWA NJE YA
NCHI KWA SIRI.Ndivyo
kilivyoandikwa kichwa cha habari
cha gazeti hili pendwa lenye kutoa
habari za kina na
uhakika.Waandishi wa habari wa
gazeti hili walikuwa wamepiga
kambi katika hospitali aliyolazwa
mheshimiwa Edger mpaka usiku
wa manane na kuhakiksha kuwa ni
kweli Edger alisafirishwa nje ya
nchi.Kwa nini asafirishwe kwa siri
namna ile lilibaki ni swali gumu
ambalo hakuna aliyekuwa na jibu
lake.
Spika wa bunge alirejea
Dodoma alfajiri na mapema tayari
kwa kuendelea kuongoza vikao vya bunge.Saa tatu kamili kama
kawaida kikao cha bunge kikaanza
kikiongozwa na Spika ambaye
alianza kwa kusoma dua halafu
akawaruhusu wabunge
waketi.Walipoketi wote Spika
akasimama na kutoa taarifa fupi.
“Waheshimiwa wabunge,jana
katika kikao cha asubuhi mbunge
mwenzetu Edger kaka alipatwa na
ugonjwa wa ghafla.Alikimbizwa
katika zahanati yetu ya bunge lakini
hali yake haikuwa nzuri
,akahamishiwa katika hospitali ya
St Francis hapa Dodoma ambako
madaktari wakashauri kuwa
ahamishiwe katika hospitali kuu ya
moyo iliyoko Dar es salaam.Mheshimiwa Edger
akakimbizwa Dar es salaam jana
mchana na kupokelewa katika
hospitali kuu ya moyo.Madkatari
walijitahidi sana kumuhudumia
mheshimiwa mbunge lakini bado
tatizo lilionekana kukomaa hivyo
wakashauri mbunge ahamishiwe
nje ya nchi.Taratibu za kusafirisha
mgonjwa nje ya nchi nafikiri wote
mnazifahamu isingewezekana kwa
usiku ule kuweza kukamilisha
taratibu zote.Namshukuru
mheshimiwa rais kwa sababu yeye
alitoa maelekezo kuwa Edger
apelekwe nje ya nchi na alitoa
ndege yake itumike kumsafirisha
mheshimiwa Edger kuelekea nchini Israel pamoja naye alikuwepo Dr
Olivia Themba.Bado tunajitahidi
kuwasiliana nao kwa kutumia
ubalozi wetu nchini Israel.Taarifa
zote tutakazopata tutakuwa
tukiwataarifu.Nawashukuru sana
madaktari wote kuanzia madaktari
wetu wa bunge na katika hospitali
zote alikopelekwa mheshimiwa
Edger.Tuzidi kumuombea ili Mungu
amjalie uponaji wa
haraka”akasema spika. Kupitia
taarifa hii fupi ya mheshimiwa
spika,bunge na taifa liliweza kujua
kinachoendelea kuhusu Edger
kaka.Nyoyo za watanzania na hasa
mashabiki wa Edger zilitulia wakati wakisubiri kupata taarifa zaidi za
maendeleo yake nchini Israel.
HAIFA - ISRAEL
Rambam medical center moja
kati ya hospitali kubwa za rufaa
nchini Israel,ilianzishwa mwaka
1938.Ikiwa na vitanda vya
wagonjwa zaidi ya 2000,na
madaktari zaidi ya 700 ,idara za
kila ugonjwa na wafanyakazi
wenye taaluma na
uzoefu,inahudumia watu zaidi ya
milioni mbili.
Toka katika uwanja wa ndege
wa kimataifa wa Haifa moja kati ya
uwanja mkongwe kabisa na wa kwanza kujengwa nchini
Israel,Edger akiwa katika gari la
wagonjwa akawahishwa
hospitalini.Kwa kuwa walikwisha
taariwa juu ya mgonjwa huyu mara
tu gari la wagonjwa lilipofika
hakukuwa na muda wa
kupoteza.Kwa haraka akaingizwa
katika chumba cha wagonjwa
mahututi akaanza kuhudumiwa.
Dr Olivia alikuwa amechoka
kwa kazi kubwa aliyoifanya toka
alipompokea Edger.Akachukuliwa
na daktari mkuu hadi ofisini kwake
na kutoa maelezo ya kina ya
ugonjwa wake.Baada ya maelezo
yale Dr Olivia akachukuliwa na
kupelekwa katika hoteli moja kubwa mjini Haifa iitwayo
Leaonardo Hotel.Hoteli hii iko
katikati ya Mlima Carmel na bahari
ya Mediteranea.Chumba chake
kilikwisha andaliwa tayari na kwa
uchovu aliokuwa nao akajitupa
kitandani na kuanza kutafakari kwa
kina juu ya mshike mshike
alioupata.
“Naomba Mungu amsaidie
mgonjwa wangu aweze
kupona.Kwa hapa tulipofika nina
imani atapona.Mungu yuko upande
wetu” Akawaza Olivia na kupitiwa
na usingizi
Saa kumi na moja za asubuhi
akastushwa na mlio wa simu ya mezani iliyo chumbani.Akainuka na
kuipokea
“Hallo” akaita Dr Olivia
“Dr Jacob ninaongea toka
hospitali ya Rambam.”
“Dr Jacob.Mgonjwa
anaendeleaje?
“Hali ya mgonjwa ndiyo
iliyonifanya nikupigie simu mida
hii.Nakuomba tuonane saa mbili leo
asubuhi” Akasema Dr Jacob.
“Sawa Dr Jacob Nitafika mida
hiyo”akasema Dr Olivia na kukata
simu
Dr Olivia akaanza kuingiwa na
wasi wasi mwingi kutokana na
mwito ule wa Dr Jacob. “Inawezekana hali ya mgonjwa
ni tete sana.Nina wasi wasi na
maisha ya mgonjwa.Kama hawa
wakishindwa sijui kama kuna
sehemu nyingine tena ambayo
wanaweza kuutibu ugonjwa ule
usioeleweka” Akawaza Dr
Olivia.Hakuweza kulala tena.Toka
alipopigiwa simu ile akawa katika
mawazo mengi.
Kulipambazuka na kijua
kuanza kuchomoza.Dr Olivia
akasimama dirishani na
kuishuhudia mandhari ya kuvutia
ya mji huu wa Haifa asubuhi
hii.Pamoja na mandhari yote nzuri
na ya kuvutia lakini mawazo ya
Olivia yalikuwa sehemu moja tu,hospitalini kwa mheshimiwa
Edger .Akaingia bafuni kuoga na
ndipo alipogundua kuwa hakuwa
amekuja na nguo zozote za
kubadilisha.Alisafiri na pochi ndogo
iliyokuwa na vitu vyake muhimu
ambavyo huwa anavihifadhi ofisini
kwake kama kadi ya benki ,hati ya
kusafiria n.k.
“Itanibidi leo nizunguke
madukani kununua vitu vichache
vitakavyonisaidia kwa muda wote
nitakaokuwa hapa.”akawaza
Gari maalum la kukodi lilikuwa
tayari likimsubiri.Akapanda na
kuelekea hospitalini ambako Dr
Jacob alikuwepo ofisini kwake
akimsubiri “Karibu sana Dr Olivia.”
“ahsante sana Dr Jacob”
Akajibu Olivia akiwa na shauku ya
kutaka kufahamu alichoitiwa.
“Dr Olivia nimekuita ili nikupe
picha halisi ya hali ya
mgonjwa.Mgonjwa anaendelea
vizuri kwa sasa.Timu ya madaktari
wetu wamemuhudumia toka
alipofika hapa na hali yake kwa
sasa naweza kusema ni tofauti na
ile aliyokuwa nayo wakati anafika
hapa.Hata hivyo kuna kitu
tumekigundua kuhusiana na huyu
mgonjwa.Tumegundua kwamba
mgonjwa huyu alipewa sumu.”
Dr Olivia akapatwa na mstuko
wa ghafla. “Sumu aliyopewa inaitwa
Spaxloxy ambayo ikiingia mwilini
inaweza kuua kwa muda wa masaa
kuanzia saba.Katika uchunguzi
wetu tumegundua kwamba sumu
hii imeingiwa mwilini kwa kupitia
katika ngozi.Tuna wasiwasi
yawezekana amepuliziwa au
ameogea sabuni yenye sumu au
ameshika kitu kilichopakwa sumu
hiyo. Sumu hiyo ikiingia mwilini
huanza kufanya kazi taratibu na
mgonjwa hawezi kuhisi chochote
hadi baada ya masaa manne au
matano ndipo huanza kufanya kazi
kwa kasi na hapo ndipo mgonjwa
asipowahiwa anaweza
akafariki.Imekuwa bahati kwamba dawa alizowahi kupewa mgonjwa
zimemsaidia sana kwani baadhi ya
dawa alizopewa zilikuwa sahihi
kabisa katika kupambana na sumu
ile.Kitakachofuata tutamfanyia
operesheni ili kuondoa baadhi ya
sehemu ambazo zimeharibiwa na
sumu katika mwili wake.Ni
operesheni kubwa lakini nina imani
baada ya operesheni hiyo hali yake
itakuwa nzuri zaidi.Kwa sasa ondoa
shaka kwani hayuko tena katika
hatari kwa sababu tumefanikiwa
kuiondoa sumu yote
mwilini.”akasema Dr Jacob
Dr Olivia akahisi kijasho
kikimtoka baada ya taarifa ile ya Dr
Jacob.Akakohoa kidogo kurekebisha koo lake halafu
akasema
“Dr Jacob nashukuru kwa kazi
kubwa mliyoifanya na kuokoa
maisha ya Edger.Tulifanya jambo la
msingi sana kufanya maamuzi ya
kumleta mgonjwa hapa kwani
tusingeweza kugundua kama
ameathiriwa na sumu.Kwa ufupi tu
ni kwamba huyu mgonjwa ni
mwanasiasa.Ni mbunge ambaye
anapendwa na watu
wengi.Kupendwa huko
kumemfanya awe na maadui wengi
vile vile.Nina imani hata sumu hiyo
iliwekwa makusudi na maadui zake
kisiasa.Dr Jacob naomba
asiruhusiwe mtu yeyote asiye muhusika wa hospitali hii kumuona
mgonjwa zaidi yangu mimi au
nitakayemruhusu kwa sababu watu
hawa waliofanya hivi hawatasita
kumfuata Edger hadi huku .”
“Usihofu kitu Dr Olivia.Hopitali
yetu ina usalama mkubwa na
hakuna mtu yeyote anayeweza kuja
kufanya kitendo chochote kibaya
hapa.Hata hivyo tutafanya kama
ulivyoomba na tutaweka ulinzi
mkali katika chumba cha mgonjwa
na hatutamruhusu mtu yeyote
kwenda kuonana na mgonjwa.Kwa
sasa operesheni inaandaliwa na
baada ya masaa mawili tutakuwa
tumeanza na tutakutaarifu kila kitu
kitakavyokuwa kikiendelea.Naahidi kumshughulikia mgonjwa huyu
kwa kila namna tunayoweza na
atapona.Tumekuwa na mahusiano
mazuri na hospitali yako na
tunakuheshimu sana”akasema Dr
Jacob
Dr Olivia
akatabasamu,akaagana na Dr Jacob
akatoka kuelekea madukani kwa
ajili ya kujinunulia vitu vichache
vya kutumia kwa muda
atakaokuwa hapo Haifa.
TANZANIA
Ni saa mbili za usiku ikulu jijini
Dodoma rais wa Tanzania Dr Evans
mwaluba alikuwa na mfanyabiashara mkubwa Donald
Nkebo wakipata chakula cha usiku
huku wakibadilishana mawili
matatu.Ni Donald Nkebo aliyeomba
kuonana na rais Dr Evans Mwaluba
usiku huu.Dr Evans hakuweza
kukataa ombi la Mr Nkebo kwa
kuwa ni mmoja kati ya watu
muhimu na wanaoheshimika
sana,ni mmoja kati ya wafadhili
wakubwa wa chama.Ni kwa sababu
ya kutambua umuhimu wake ndiyo
maana usiku huu rais alitenga
muda ili aweze kuonana na tajiri
huyu mkubwa
“Mheshimiwa rais ni muda
sasa hatujaonana,siwezi
kukulaumu kwani nafahamu majukumu uliyonayo,na hii ndiyo
sababu nimeomba nionane nawe
walau tuzungumze kidogo”
Akasema Donald Nkebo huku
ajimiminia mvinyo katika glasi yake
“Mr Donald ni kweli muda
umepita hatujaonana nimekuwa
natafuta sana nafasi niweze
kukutana na watu wangu lakini
ninakosa,nimetingwa mno na
mambo mengi.Nimekuwa na ziara
nyingi za kitaifa na kimataifa na
ndiyo maana nimekuwa sipatikani
kwa urahisi.Leo nilipopata taarifa
kwamba uko Dodoma na unataka
kuonana nami nilifurahi
sana.Karibu sana Donald.Vipi
biashara zinaendaje? “Mr President hata mimi
ninafurahi sana kuonana
nawe.Kuhusu biashara zinakwenda
vizuri licha ya kushuka kwa
thamani ya shilingi na kuongezeka
kwa bei ya mafuta katika soko la
dunia lakini bado biashara
zinakwenda vizuri” Akasema
Donald Nkebo
“Hilo la kushuka kwa thamani
ya shilingi yetu linatuumiza vichwa
mimi na viongozi wenzangu
serikalini.Tumekwisha anza juhudi
mbali mbali za kuhakikisha shilingi
yetu inapanda thamani.Nina imani
tutafanikiwa”
“Ninakuamini mheshimiwa
rais.Naamini utafanikiwa katika hilo.Watu uliowapa dhamana ya
kulishughulikia suala hilo ni
wachapa kazi hodari.”
Dr Evans akacheka kidogo
akainua glasi yake ya mvinyo na
kupiga funda dogo.
“Mheshimiwa rais upepo wa
kisiasa unakwendaje?Naona
vuguvugu la urais ndani ya chama
limeanza kupamba moto”akasema
Donald
“Upepo wa kisiasa si
mbaya,bado unavuma vizuri
japokuwa kuna changamoto na
vikwazo lakini sina wasi wasi
nimekwisha jiweka vizuri ndani ya
chama”akasema Dr Evans “Mheshimiwa rais hata mimi
sina wasi wasi wowote na nguvu
yako ndani ya chama lakini nina
ushauri mdogo kwako.Usijipe
uhakika sana kwamba hauna
upinzani ndani ya chama”
“Kwa nini unasema hivyo
Donald?
“Kwa hali tuliyoanza kuiona
kwa sasa inaonekana hamasa ya
kuwania uteuzi imeongezeka sana
ndani ya chama.Japo hatujui bado
nani na nani wana nia ya kuwania
uteuzi huo lakini tayari dalili
zimekwisha anza kujionyesha na ni
dhahiri unaweza ukakumbana na
upinzani mkali sana” “Nakubaliana nawe
Donald,upinzani utakuwepo lakini
kwa upande wangu sina wasiwasi
wowote naamini watajitokeza
wengi kuwania uteuzi lakini
nitakayepita ni mimi.Kwa nini
unakuwa na wasi wasi Donald?
Sura ya Donald Nkebo
ikapambwa na tabasamu.Akainua
glasi yake akapiga funda kubwa
halafu akasema.
“Mheshimiwa rais hilo ndilo
hasa ambalo limenifanya nitake
kuonana nawe ili nikupe taarifa
ambazo naamini bado hujazipata”
“Karibu Donald nakusikiliza”
akasema Dr Evans “Mheshimiwa rais tayari ndani
ya chama kuna watu wamekwisha
anza kutengeneza makundi ya
kuhakikisha kuwa wanashinda
katika uteuzi” Kauli ile ikamfanya
Dr Evans kujiweka sawa
“Jana usiku nilipata taarifa
toka katika moja ya vyombo vyangu
vya taarifa kwamba kuna kikao cha
siri kilifanyika katika hoteli ya
Dodoma palace na mwenyekiti
wake alikuwa Damian Mwamba”
akanyamaza kwa sekunde kadhaa
na kuendelea
“Damian Mwamba tayari
amekwisha anza harakati za
kuwania uteuzi ndani ya
chama.Ninazo taarifa zenye uhakika kuwa tayari amekuwa na
uungwaji mkono wa kuridhisha
toka kwa wajumbe.Timu aliyoiteua
ifanye kazi ya kutengeneza
mtandao inafanya kazi yake kwa
umakini na usiri mkubwa na
kusema ukweli hawalali wanafanya
kazi usiku na mchana kuhakikisha
wanatengeneza mtandao
mkubwa.Harakati hizi Damian
amezianza kitambo sana kwa
kujenga jina katika jamii ndiyo
maana hadi sasa jina la Damiani
Mwamba linatajwa sana katika
orodha ya watu wenye sifa na
uwezo wa kuiongoza nchi
hii.Amekuwa akitoa misaada mbali
mbali kwa vikundi vya akina mama na vijana,amejenga
mashule,hospitali na kila
linapotokea suala lolote la kitaifa
amekuwa mstari wa mbele sana.Si
kwamba namuhofia Damiani lakini
kasi anayokwenda nayo ndiyo
iliyonisukuma kutaka kuonana
nawe tujadili kwa kina kuhusu
suala hili”akasema Donald
Rais akavuta pumzi ndefu na
kumuangalia Donald Nkebo
usoni.Alionyesha uoga wa dhairi
kwa maneno yale aliyoambiwa.
Nkebo akaichukua chupa na
kumimina tena mvinyo katika glasi
yake.
“Mheshimiwa rais ,wewe ni
rafiki yangu na mimi ni mmoja wa watu wanaokuunga mkono
sana,mimi na timu yangu
tulikuunga mkono katika awamu ya
kwanza na ukafanikiwa kushinda
na bado tutaendelea kukuunga
mkono.Nadhani unafahamu kuwa
pamoja na makundi yote yaliyomo
ndani ya chama lakini timu yetu
ndiyo yenye nguvu kubwa ndani na
nje ya chama,sisi ndiyo wenye
kuamua nani awe rais wa nchi hii
na nani asiwe.Tunaangalia nani
ambaye atakuwa na manufaa
kwetu na wewe bado unaonekana
kuwa na umuhimu mkubwa kwetu
ndiyo maana nimekuja
kukuhakikishia kwamba bado
tunakuunga mkono na utapita kwa awamu nyingine.Pamoja na yote
mazuri ambayo umetufanyia
mheshimiwa rais lakini kuna jambo
dogo sana umelikosea labda ni kwa
kutokujua”akasema Donald na
kunyamaza
“Jambo gani Donald?akauliza
Dr Evans
“Ni kuhusu yule mbunge Edger
kaka.Mheshimiwa rais kama
umegundua yule kijana ni tishio
kubwa kwako kisiasa.Ugonjwa
wake alioupata ghafla
umetuonyesha ni jinsi gani
anavyopendwa na watu.Sikufichi
mheshimiwa rais yule kijana ana
nguvu kubwa.Nchi yote ilizizima
baada ya taarifa kusambaa kuwa amefariki dunia.Kasi anayokuja
nayo inaleta wasi wasi
mwingi.Naamini bado hajaweka nia
ya kugombea lakini kama akiamua
kutangaza kuwania urais tutakuwa
na kazi kubwa.Naelewa hana
mtandao mkubwa ndani ya chama
lakini anaweza kushawishiwa
kujiunga na chama pinzani ili
agombee urais na kama akifanya
hivyo mheshimiwa rais basi
shughuli itakuwa ngumu.Kuna
uwezekano mkubwa kijana yule
akatwaa nchi” Donald akatulia
akanywa funda kubwa la mvinyo
akaendelea
“Kilichomtokea Edger ni
mkakati mzito wa kumuondoa katika ulingo wa siasa kwani
uwepo wake bungeni na katika
siasa ni hatari kwa watu
wengi.Edger alitakiwa afariki dunia
jana.Mheshimiwa rais kosa
ulilolifanya ni kutoa ndege yako
kumsafirisha Edger kumpeleka
kutibiwa nje ya nchi.”
Rais akatoa kitambaa na
kujifuta jasho lililoanza kumtoka.
“Donald sikujua kama tukio lile
ni makakati maalum na wala
sikuwa nikiifahamu hatari ya huyu
kijana.Kama ningeambiwa kwamba
ule ni mkakati maalum wa
kumuondoa ningeweka nguvu
yangu kubwa na kummaliza haraka
sana lakini sikujua lolote ndiyo maana nikaamua kumsaidia kuokoa
maisha yake.Donald nashukuru
umenifumbua macho kuhusu
mambo yanayoendelea chini kwa
chini ndani ya chama,nakiri hakuna
katika watu wangu wa karibu
aliyekuja kunieleza mambo haya
uliyonieleza.Nashangaa hata
washauri wangu wamekaa kimya
wakati kuna hatari kubwa
inatukabili.Ninaanza kuhisi
yawezekana hata washauri wangu
watakuwa tayari
wamesharubuniwa na ndio maana
wamekaa kimya na kusubiri
kuanguka kwangu.Haiwezekani
wakashindwa kuwa na taarifa za
kinachoendelea ndani ya chama.Ahsante sana Donald kwa
taarifa hii uliyonipa.Imenifumbua
macho” Akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais,usipate
shida yoyote mimi na timu yangu
tupo na tunakuhakikishia nafasi ya
urais ni yako ila nitakuelekeza nini
cha kufanya kama utakuwa tayari
kufuata ushauri wangu”
“Kwa nini nisifuate ushauri
wako Donald wakati wewe ndiye
uliyekuja kunifumbua macho?
Nielekeze nifanye nini.”
“Kama nilivyokwisha kueleza
mheshimiwa rais mimi na timu
yangu tutahakikisha unashinda
katika awamu ijayo lakini kuna
mambo ambayo lazima tuyafanye.Kitu cha kwanza
tunachotakiwa kukifanya ni kuunda
timu ndogo ya watu ambayo
itafanya kazi ya kuchunguza
mwenendo wa siasa na kuangalia
nini tufanye ili tuweze kupata
ushindi ambayo itakubidi
mheshimiwa rais uiwezeshe ili
iweze kufanya kazi zake kikamilifu
bila kugundulika.Timu hii itakuwa
ya watu sita ambao nitakupa
majina yao.Ni watu ambao
inakupasa uwaamini kwa sababu ni
wataalamu katika michezo hii ya
kisiasa.Kitu cha pili ambacho
tutakifanya baada ya kuunda timu
hii ni kuwanyamazisha wale wote
wanaoonekana kuwa na nguvu kisiasa na kuhatarisha urais wako
kwa kipindi kingine.”
Dr Evans akamtazama Donald
Nkebo halafu akauliza.
“Kuwanyamazisha kivipi?
“Mr resident politics is a dirty
game and to win this game you
need to play dirty too” Akasema
Nkebo.
“Bado sijakuelewa Nkebo hebu
nifafanulie vizuri”
“Mheshimiwa rais ninaposema
kumnyamazisha mtu yeyote
mwenye kuwa na nguvu kisiasa
nina maana ya kumpunguzia nguvu
aliyonayo na wakati mwingine
ikibidi hata kumuondoa katika uso
wa dunia hii iwapo kutakuwa na ulazima wa kufanya hivyo.Kazi hii
si rahisi,inahitaji umakini na
wataalamu wa hali ya juu mno
ndiyo maana nikasema inabidi
tuwezeshwe ili kufanikisha
shughuli kama hizi.Kwa
kuanzia,tutaanza na wale ambao
tayari wamekwisha onyesha wazi
dhamira zao za kuwania urais kama
Mr Damian na huyu kijana
Edger.Sisi tutawashughulikia bila
hata ya mtu yeyote kuhisi kuwa
unahusika kwa namna yoyote na
wao.Ninakuhakikishia Mheshimiwa
rais kuwa hakuna mtu atakayejua
nini tunakifanya”
Sura ya rais ikajenga tabasamu
pana baada ya Donald kumchambulia kwa kina jinsi
mambo yatakavyoendeshwa ili
kuwamaliza wabaya wake
kisiasa.Mpaka wanamaliza
maongezi Dr Evans akamkabidhi
rasmi Donald Nkebo jukumu la
kuhakisha kuwa wale wote
wanasiasa wanaoonekana kuwa na
nguvu ndani na nje ya chama na
ambao wanaonyesha dhamira ya
wazi ya kugombea urais
wanamalizwa kimya kimya.Rais
alimuahidi Nkebo kumuwezesha
yeye na kamati yake kwa kila kitu
watakachohitaji,kama vile ulinzi na
fedha.Saa saba za usiku walimaliza
maongezi yao na Donald akaagana
na rais akaondoka .

