SIRI
MTUNZI : PATRICK CK
SEASON 9: EPISODE 1
Gari la Avi Abramson
mkuu wa Mossad ukanda wa
Afrika Mashariki lilikaribia
kufika katika ubalozi wa
Israel jijini Nairobi akatoa
simu na kupiga
akazungumza na mtu simuni
akamtaka azime kamera zote
za ulinzi ubalozini hapo kwa
muda wa dakika kumi na
tano.
Gari lilifika getini na
kwa haraka walinzi
wakafungua geti na kuingia
ndani ya jengo la
ubalozi.Mlinzi wa Avi
akawahi kushuka garini na
kuangaza pande zote kama
kuna hatari yoyote halafu
akamfungulia mkuu wake
mlango wa gari Avi
akashuka.Bila kuonekana
Devotha akabonyeza ile
kamera aliyoivaa katika koti
lake naye akafunguliwa
mlango akashuka.
Mara tu Devotha
alipobonyeza kamera,akina
Gosu Gosu waliokuwa ndani
ya chumba cha hoteli Sadena
wakaanza kupata picha.
“She’s in”akasema Tino
na kuwajulisha akina
Mathew Dar es salaam
waliokuwa wanafuatilia kila
kinachoendelea Nairobi
“Good job” akasema
Mathew
Baada ya kushuka garini
Avi akamuita Devotha
pembeni
“Nimeelekeza kamera
zote zizimwe kwa muda wa
dakika kumi na tano ili
uweze kuonana na
Edger.Sitaki mtu yeyote
afahamu kama nimekuleta
hapa ukaonana
naye.Naomba tusipoteze
muda twe….” Akasema Avi
“Avi kabla hatujaenda
huko una hakika mtu
uliyemuelekeza azime
kamera kweli amezima
kamera zote? Akauliza
“Nina uhakika
amezima.Kwa nini umeuliza?
“Yawezekana akajiuliza
maswali mengi kwa nini
kamera zote katika jengo hili
zizimwe? Anaweza akapata
ushawishi wa kuacha baadhi
ya kamera ili ajue
kinachoendelea.Nakushauri
ufanye uhakiki kama kweli
kamera zote zimezimwa ili
yasije kutokea matatizo kwa
upande wako baada ya mimi
kuondoka” akasema Devotha
“Ninawaamini watu
wangu lakini ulilolisema lina
msingi yawezekana kweli
mtu niliyemuelekeza azime
kamera akataka kuchunguza
kujua nini kinaendelea”
akasema Avi na kumtaka
Devotha amfuate wakaelekea
ofisini kwake akawasha
kompyuta yake.Kulikuwa na
sehemu ya kuweka namba za
siri na Devotha akaielekeza
kamera yake makusudi
katika kompyuta ya Avi ili
wenzake wanaoendelea
kumfuatilia wazione namba
zile za siri atakazoandika
Avi.Huu ulikuwa ni ujanja
wa Devotha kumleta Avi
ofisini kwake ili waweze
kuipata namba ya siri
anayoitumia kuingia katika
mtandao wao.Avi akabonyeza
kompyuta yake na
kujiridhisha kamera zote
zilikuwa zimezimwa.
“Kamera zote zimezima”
akasema Avi huku akizima
kompyuta yake
“Ni vyema
umejiridhisha” akasema
Devotha wakatoka na
kuelekea mahala aliko Edger
kaka
Timu ya akina Mathew
waliokuwa wakimfuatilia
Devotha walikuwa na kazi
kubwa ya kuhakikisha
wanaipata vyema ramani ya
njia ya kupita kuelekea
mahala alikofichwa Edger
Kaka.
Avi alitumia kadi yake
kufungulia mlango mkubwa
wakaanza kushuka ngazi
kuelekea chini ya jengo hadi
walipofika katika lango
lingine kubwa akalifungua
kwa kutumia kadi ile ile
wakatokea katika sebule
nzuri yenye sofa za kuvutia.
“Hapa ndipo anapoishi
Edger Kaka” akasema Avi na
kwenda kuufungua mlango
mwingine akaingia Devotha
akamfuata.Ndani ya chumba
kile kulikuwa na kitanda
kikubwa ambacho alikuwa
amelala mtu mmoja
aliyedhoofu sana.
“Edger
unaendeleaje?akauliza Avi
“Naendelea vyema.Kuna
taarifa zozote
umeniletea?Olivia
amepatikana?akauliza Edger
“Nimekuletea
mgeni.Atajitambulisha yeye
ni nani na kwa nini yuko
hapa” akasema Avi na
kumgeukia Devotha
akamnong’oneza sikioni
“Una dakika tano tu za
kuzungumza
naye,usithubutu kufanya
kitu chochote cha kijinga”
akasema Avi na kutoka
akaufunga mlango.Devotha
akachukua kiti
akaketi.Edger alikuwa
anamshangaa hakuwahi
kumuona hapo kabla
“Edger kaka”akasema
Devotha
“Wewe ni nani?Unataka
nini?akauliza Edger ambaye
bado sauti yake ilikuwa
dhaifu
“Naitwa Devotha
ninatokea Tanzania”akasema
Devotha na kumstua Edger
“Tanzania?akauliza
“Ndiyo” akajibu Devotha
na woga mkubwa ulionekana
machoni pa Edger
“Umefahamuje kama
niko hapa?akauliza Edger
“Ninafanya kazi na
Mossad hivyo ninafahamu
kila kinachoendelea na kwa
nini uko hapa.Nimepewa
dakika tano tu za
kuzungumza nawe hivyo
nataka kujielekeza moja kwa
moja katika suala la msingi
lililonileta kwako” akasema
Devotha na kumkazia macho
Edger
“Hivi sasa nchini
Tanzania shirika la ujasusi
la Israel Mossad,wanaandaa
operesheni kubwa ya
kumtafuta Dr Olivia Themba
ambaye ametekwa na watu
wasiojulikana.Ili uweze
kuwapa Mossad taarifa za
muhimu wanazozitafuta
kuhusu mtandao wenu wa
IS,umeelekeza wahakikishe
wanamtafuta na kumpata
Olivia.Mimi ndiye wakala wa
Mossad nchini Tanzania na
operesheni nzima ya
kumtafuta Olivia
inaniegemea mimi.Katika
uchunguzi wetu wa awali
tumebaini kwamba Olivia
ametekwa na watu wa
mtandao wako wa IS hivyo
nimekuja kwako kukuomba
utoe ushirikiano ili tuweze
kumpata Olivia” akasema
Devotha
“Olivia ametekwa na
watu wa IS?akauliza Edger
“Ndiyo ametekwa na
IS.Kama ulimaanisha
ulichokisema kuwa Olivia ni
mwanamke pekee
unayempenda ,huu ni wakati
wako wa kutoa ushirikiano
mkubwa ili tuweze
kumuokoa kutoka katika
mikono ya IS” akasema
Devotha
“Kwa nini IS wamteke
Olivia Themba?akauliza
Edger
“Mimi siwezi kuwa na
jibu lakini wewe unafahamu
kila kitu kwa nini wamteke
Olivia”
“Sifahamu chochote dada
yangu.Nimekaa mahala hapa
ambapo sijui ni wapi kwa
muda wa miaka mitatu na
sielewi chochote
kinachoendelea huko
nje.Siwezi kujua sababu ya
IS kumteka Olivia”
“Edger umekuwa hapa
kwa muda wa miaka mitatu
na katika muda huo wote
watu wako wa IS hawajui
kama uko hai hivyo hakuna
yeyote
atakayekusaidia.Unapaswa
kuyapigania maisha yako
wewe mwenyewe.Umeanza
vyema kwa kuahidi kueleza
kila kitu japo umetoa
masharti ya kupata Olivia
ninakuahidi tutampata
lakini nataka utupe
ushirikiano mkubwa katika
hilo kwani Olivia kama
nilivyokuelea anashikiliwa
na watu wa mtandao
wako.Nataka unipe orodha
ya watu walio katika
mtandao wa IS nchini
Tanzania ambao unamini
wanaweza kuwa wanahusika
na kutekwa kwa Olivia
Themba” akasema Devotha
“Sifahamu mtu yeyote wa
IS Dar es salaam” akajibu
Edger
“Edger ulikiri mwenyewe
kwamba unampenda
Olivia,huu ni wakati wako
wa kulithibitisha hilo kwa
kutoa taarifa ambazo
zitasaidia
kumpata.Waliomteka ni
wenzako wa IS na
yawezekana lengo lao ni
kumuua.Kama kweli
unampenda Olivia nipe
majina ya watu walio katika
mtandao wa IS nchini
Tanzania ili tuweze
kumuokoa Olivia” akasema
Devotha
“Dada yangu sifahamu
mtu yeyote ambaye
anashirikiana na IS nchini
Tanzania” akajibu Edger na
Devotha akamtazama kwa
hasira
“Edger unaonyesha wazi
kwamba maneno yale
uliyoyasema kwamba
unampenda Olivia si maneno
ya kweli bali ulikuwa ni
uongo.Huna mapenzi yoyote
kwa Olivia kwani kama
ungekuwa unampenda
ungedhihirisha hilo kwa
kutoa taarifa ambazo
zingesaidia kumuokoa
kutoka katika mikono ya
watu ambao hatujui lengo lao
ni nini kwake.Edger Olivia
alikuokoa pale ulipowekewa
sumu kwa sasa yuko
matatizoni ni wakati wako
na wewe kuhakikisha
unamsaidia kuyaokoa
maisha yake kama
alivyofanya kwako” akasema
Devotha.Edger hakujibu kitu
aliendelea kumtazama
Devotha
“Edger muda wangu
unakwisha tafadhali naomba
unijibu ili tuweze kumuokoa
Olivia ambaye hastahili
kupitia mateso kama haya
anayoyapitia hivi sasa”
akasema Devotha lakini bado
Edger aliendelea kuwa
kimya.Mlango ukagongwa.
“Edger muda wangu
umekwisha.Nitakapotoa
mguu wangu ndani ya
chumba hiki bila kupata jibu
lako naomba ufahamu kuwa
hakutakuwa na uwezekano
tena wa kumpata Olivia.IS
are going to kill her !!
akasema Devotha.Bado
Edger aliendelea kuwa
kimya.Devotha akainuka
“Edger nina sekunde
chache zimebaki nieleze
tafadhali! Akasema Devotha
“Sifahamu mtu yeyote”
akajibu Edger.Devotha
akamtazama kwa hasira na
kumfuata pale kitandani
akamshika na kumuinua
lakini kabla hajafanya
chochote Avi akaingia
“Devotha !! akasema Avi
na Devotha akamuachia
Edger
“Muda
umekwisha.Twende
tuondoke” akasema Avi
“Olivia akifariki dunia
damu yake itakuwa juu
yako” akasema Devotha kwa
ukali na kutoka ndani ya kile
chumba
“Muda nilioelekeza
kamera kuzimwa umekaribia
kumalizika hivyo unapaswa
kuwa tayari umetoka ndani
ya jengo pale kamera
zitakapowashwa” akasema
Avi huku wakitembea
haraka haraka kutoka ndani
ya jengo wakaingia katika
gari la Avi na kuondoka
katika ubalozi wa Israel.
Hakukuwa na
mazungumzo garini baada ya
kuondoka katika ubalozi wa
Israel hadi walipofika
Sadena hotel.Avi na Devotha
wakashuka garini
wakaelekea chumbani.
“Umepata ulichokuwa
unakitafuta kwa Edger
Kaka?akauliza Avi
“Hapana sikufanikiwa
kupata chochote muda
ulionipa wa kuzungumza
naye ni mdogo sana”
akasema Devotha
“Nafahamu ni muda
mfupi lakini ulipaswa
kuutumia kikamilifu na
kuweza kupata taarifa
kutoka kwa Edger.Devotha
hata kama ningekupa masaa
manne ya kuzungumza naye
Edger asingeweza kukueleza
chochote.Kama ameweza
kukaa kwa muda wa miaka
mitatu bila kuzungumza
chochote usingeweza kupata
chochote kutoka kwake kwa
muda wa dakika tano”
akasema Avi
“Edger alikuwa karibu
sana kufunguka.Kwa ajili ya
Olivia yuko tayari kueleza
kitu chochote.Ungenipa
muda zaidi wa kuzungumza
naye nakuhakikishia
ningeweza kupata kile
nilichokuwa nakitafuta
kwake”
“Devotha unapaswa
ushukuru kwa hata dakika
zile chache nilizokupatia
ukaweza kuonana na Edger
Kaka.Kuna watu wako ndani
ya ubalozi wetu hawafahamu
kama kuna mtu anaitwa
Edger ameishi pale ndani
kwa miaka mitatu”
“Ninalifahamu hilo Avi
lakini kama ningeweza
kupata nafasi nyingine ya
kuzungumza naye nina
uhakika mkubwa wa kuweza
kupata kile ninachokitafuta”
“Devotha hakutakuwa na
nafasi nyingine tena ya
kuonana na Edger kaka na
ninaomba hiki tulichokifanya
kibaki kuwa siri kwani
ikijulikana ni mimi nitakuwa
katika matatizo
makubwa.Naomba uitunze
siri hii” akaomba Avi
“Usijali Avi.Ninafahamu
umuhimu wa siri hii kubwa
na ninakuhakikishia
nitakwenda nayo kaburini”
akasema Devotha
“Kwa sasa baada ya
kukosa taarifa kutoka kwa
Edger nini mipango yako ya
kumpata Olivia? Akauliza
Avi
“Bado yapo matumaini
makubwa.Kuna taarifa
fulani tunazifuatilia jijini
Arusha ambako niliwaacha
Fishel na Ehud.Nikitoka
hapa ninakwenda kuungana
nao.Nina uhakika taarifa
hizo zinaweza kutupa
mwanga.Usihofu Avi lazima
tutampata Olivia” akasema
Devotha na kwenda
kumkalia Avi mapajani
“Avi nimemaliza kile
kilichonileta Nairobi japo
sijafanikiwa lakini
nimejaribu.Unataka
tuendelee pale
tulipoishia?akauliza Devotha
huku akikuna kidevu cha Avi
na kumfanya atabasamu
halafu akaanza kumfungua
tai yake akamuinamia na
kumbusu.
“Unasemaje Avi
tuendelee?akauliza Devotha
akiendelea kumbusu Avi
“Mhh ! Avi akaguna
“Unasemaje
Avi?Unahitaji tuendelee pale
tulipoishia?Nataka
nikuonyeshe namna
wanawake wa kiafrika
wanavyoyafahamu mapenzi”
akasema Devotha akiendelea
kumfanyia uchokozi Avi
ambaye tayari damu ilikuwa
inamchemka.Akamvua koti
na kulitupa pembeni
akaanza kumvua shati.Avi
mashetani yake yakampanda
akajikuta akiufungua
mkanda wa suruali yake
akaivua na kuitupa
sakafuni.Akamvuta Devotha
na kuanza kumbusu
akamfungua vifungo vya
koti,Devotha akainuka
akamshika mkono Avi
akamuongoza hadi katika
chumba cha kulala na
kumlaza kitandani akamvua
nguo ya ndani na kuanza
kufanya utundu mkubwa
ikulu kwa Avi kwa kutumia
ulimi wake halafu akambusu
Avi na kusema
“Avi ninahitaji kupata
vinywaji nisubiri dakika
mbili nikachukue kinywaji
nikipendacho halafu
nitarejea” akasema Devptha
“Kwa nini usiwapigie
simu walete kinywaji hicho
hapa hapa chumbani?HUna
haja ya kwenda wewe
mwenyewe” akasema Avi
“Ngoja nikachukue
mwenyewe nirudi
haraka.Wahudumu
wanaweza wakachelewa kuja
na mimi huwa ninapata
starehe sana nikinywa
kinywaji nikipendacho.Nipe
dakika mbili tu” akasema
Devotha na kumbusu Avi
kisha akatoka na kwa
haraka akaingia katika
chumba cha akina Gosu Gosu
“Mambo yanakwendaje
huku? Mmefuatilia kila
kitu?akauliza Devotha
“Devotha umefanya kazi
nzuri.Tumekufuatilia kila
ulichokifanya” akasema Gosu
Gosu na mara katika picha
za kamera Avi akaonekana
akiishika simu yake
“Guys Avi ameishika
simu yake kuweni makini
kufuatilia kile
anachokizungumza” akasema
Mathew na wote wakageukia
runinga kumtazama Avi
“Ongeza sauti tusikie kile
anachokizungumza” akasema
Mathew na Tino akaongeza
sauti
“Hallow Nabil” akasema
Avi baada ya mtu
aliyempigia kupokea
simu.Baada ya sekunde
chache akasema
“Nabil kuna kazi ambayo
nataka uifanye usiku wa
leo.Kuna mwanamke mmoja
ametoka Tanzania nataka
kumkata pumzi usiku wa
leo.Nitakupa maelekezo
baadae kidogo anza
kujiandaa” akasema Avi na
kukata simu.
“Guys Avi
hajafurahishwa na kitendo
cha Devotha kufahamu siri
yao na kuonana na Edger
Kaka na sasa anasuka
mpango wa kumuua.Siri hii
ya Edger Kaka kuwepokatika
ubalozi wao hawataki
ijulikane.Devotha umefanya
kazi nzuri sana.Kwa sasa
wote tuna uhakika Edger
Kaka yuko hai na
tumethibitisha hilo.Baada ya
kufahamu mpango wa Avi
kumuua Devotha kuna
mambo mawili ambayo
lazima tuyafanye”
akanyamaza kidogo na
kusema.
“Tunatakiwa
kuhakikisha Avi,mlinzi na
dereva wake hawatoki
salama ndani ya
hoteli.Tunatakiwa kuwaua
wote.Devotha utarejea ndani
ya chumba chako na
kumtaka Avi awapigie simu
watu wake aliowaacha ndani
ya gari ambao ni dereva na
mlinzi wake ili waweze
kupata kinywaji wakati
wewe ukiendelea
kumstarehesha.Akiwapigia
utawafuata utawachukua na
kuwapeleka katika chumba
cha akina Gosu
Gosu.Wakiingia humo
waueni wote na atabaki Avi
peke yake hiyo itakuwa ni
kazi ya Devotha
kummaliza.Kabla ya saa tatu
usiku wa leo watu hao wawe
wameuawa.Gosu Gosu
unajua namna ya kufanya
baada ya kuwaua watu
hao.Tino ni mwenyeji hapo
Nairobi atakusaidia namna
ya kuihifadhi miili ya watu
hao isionekane” akasema
Mathew
“Sawa Mathew
nimekuelewa”akasema Gosu
Gosu
“Jambo la pili,baada ya
kuwaua hao jamaa,Tino
utachukua gari la Avi na
utakwenda katika ubalozi wa
Israel.Wanalifahamu gari la
Avi wakiliona watakuruhusu
kupita getini na kama
kutakuwa na tatizo lolote
waambie wapige simu ya Avi
ambayo itaunganishwa na
mfumo wetu na Ruby
ataipokea na kuzungumza na
hao jamaa kwa kutumia
sauti ya Avi ambayo
imerekodiwa.Ukivuka geti
tutakuongoza kuelekea
katika ofisi ya Avi kwani
tayari tumeipata ramani
muda ule alipokuwa na
Devotha.Tunataka kuingia
katika mtandao wa Mossad
ili tuweze kupata taarifa zote
za muhimu
zitakazotuwezesha
kufanikisha operesheni
yetu.Ukishaingia katika ofisi
hiyo Ruby atakupa
maelekezo nini cha
kufanya.Nadhani
mmenielewa” akasema
Mathew.
“Tumekuelewa
Mathew,hakuna muda wa
kupoteza mimi ngoja nirejee
chumbani nikamshawishi ili
awapigie simu watu wake
kule garini” akasema
Devotha
“Devotha kuwa makini
sana ili Avi asigundue
kwamba tayari tunafahamu
kile anachotaka kukifanya”
akasema Mathew
“Niko makini usihofu”
akasema Devotha kisha
akatoka katika kile chumba
na kurejea tena chumbani
kwake akamfuata Avi pale
kitandani ambaye alikuwa
mtupu akambusu
“Mbona umerejea bila
vinywaji?akauliza Avi huku
akiuchezea uume wake
“Avi kuna kitu
kimenirudisha”
“Kitu gani?akauliza Avi
“Umewaacha ndani ya
gari mlinzi na dereva wako
wanakusubiri na hawajui
utatoka humu ndani saa
ngapi.Haipendezi wakati sisi
tunastarehe wao waendelee
kupigwa na baridi ndani ya
gari.Itapendeza kama
tukiwatafutia sehemu nao
waweze kupata nafasi ya
kupumzika wakati sisi
tunaendelea na mambo
yetu”akasema Devotha
“Usihofu Devotha
watanisubiri hata kama
nikitoka saa tisa usiku,ni
kazi yao” akasema Avi
“Avi nakubali ni kazi yao
lakini wakati mwingine tuwe
na ubinadamu.Kuna ubaya
gani wakati sisi tukistarehe
wao wakiendelea kupata
kinywaji na chakula cha
jioni?Yawezekana ukatoka
humu saa nne za usiku.Muda
huo wote watakuwa garini
wanakusubiri?Wapigie simu
tafadhali wajulishe kwamba
ninakwenda kuwachukua ili
wapate kinywaji kidogo
wakati sisi tunastarehe.Avi
unajua kunikuna na
ninataka nikupe vitu adimu
sana leo hadi umsahau mke
wako”akasema Devotha na
kumbusu Avi akamletea
simu yake.Avi akaweka dole
gumba simu ikafunguka
akampigia mlinzi wake
akamjulisha kwamba kuna
mtu anakwenda kuwachukua
ili wapate kinywaji kwani
yeye atachelewa kidogo
“Ahsante Avi.Umefanya
jambo jema ninawafuata
sasa hivi ili nao waendelee
kuburudika kwa vinywaji”
akasema Devotha na kutoka
akashuka chini hadi katika
maegesho ya magari
akagonga mlango wa gari
kioo kikashushwa
“Amewapigia simu Avi?
Twendeni mkapumzike
kidogo mpate chakula na
vinywaji kuna sehemu
mmeandaliwa.Avi
atachelewa kidogo” akasema
Devotha wale jamaa
hawakuwa na wasiwasi
kwani wamekwisha pewa
ruhusa na mkuu wao
wakashuka garini na
kumfuata Devotha
wakaelekea ndani.Moja kwa
moja akawapeleka hadi
katika chumba cha akina
Gosu Gosu akakiminya
kitasa na kuufungua mlango
“Karibuni
ndani”akasema Devotha
David Kioko dereva wa
Avi ndiye aliyekuwa wa
kwanza kuingia ndani ya kile
chumba ambamo aliwakuta
Gosu Gosu na Tino
“Karibu kaka” akasema
Tino na kulazimisha
tabasamu usoni.Mlinzi wa
Avi naye akapiga hatua
kuingia ndani ya kile
chumba lakini
alipochunghulia ndani
akasita kuingia.Devotha
aliyekuwa nyuma yake kwa
kasi ya umeme akamrukia
teke kali la mgongo Yule
jamaa akaangukia
ndani.Gosu Gosu aliyekuwa
karibu na mlango alimpokea
Yule mlinzi wa Avi kwa
ngumi nzito iliyompeleka
chini kisha akamtandika
tena teke zito la uso na Yule
jamaa akaanza kutoa damu
mdomoni.Gosu Gosu akatoa
bastora iliyofungwa kiwambo
cha sauti
“Msiniue jamani !
akasema dereva aliyekuwa
akitetemeka lakini Gosu
Gosu hakupoteza muda
akaizinga bastora yake na
kuachia risasi tatu
akimlenga kifuani Yule
mlinzi wa Avi.
“Ndugu zangu msiniue
nawaomba sana” akaomba
Yule dereva lakini masikio
ya Gosu Gosu yalikuwa
yameziba akaachia risasi
kadhaa na Yule dereva
akaanguka sakafuni.Gosu
Gosu akawavuta
akawaingiza chooni
akawapekua na kuchukua
simu zao zote akazizima
kabisa kisha akafuta damu
iliyosambaa pale sebuleni.
“Kazi nzuri Gosu
Gosu,Devotha usichukue
muda mrefu nenda kaendelee
na sehemu yako.Tino jiandae
uelekee katika ubalozi wa
Israel hapo muachie Gosu
Gosu ataendelea kumlinda
Devotha”akaelekeza Mathew.
Devotha akatoka na
kurejea katika chumba chake
“Tayari wanapata
chakula na kinywaji.Sisi
tuendelee”akasema Devotha
akivua koti lake
“Ahsante Devotha una
roho nzuri sana.Ngoja
niwakumbushe wasinywe
kupitiliza sintakawia sana
hapa” akasema Avi na
kuchukua simu yake lakini
Devotha akamshika mkono
na kuichukua simu akaitupa
pembeni.
“Usiwasumbue Avi wale
ni watu wazima wanafahamu
wanachotakiwa
kukifanya.Waache nao
waburudike kidogo” akasema
Devotha na kuanza
kumporomoshea mabusu
mfululizo na taratibu Avi
akazidiwa na kipute
kikaanza.
Tino alitoka chumbani
kwao akaufungua taratibu
mlango wa chumba cha
Devotha na kuingia sebuleni
akapekua mavazi ya Avi
akachukua kadi ya Avi ya
kufungulia milango halafu
akatoka na kurejea
chumbani kwao akachukua
funguo za gari akaenda
maegesho akalitafuta gari la
Avi akaingia na kuondoka
kuelekea katika ubalozi wa
Marekani akiwa ameweka
kifaa cha mawasiliano sikioni
ili aweze kuwasiliana na
akina Mathew
“I’m on move” akasema
Tino
“Tunakufuatilia Tino”
akasema Mathew.Tayari kiza
kilikwisha ingia
Hotelini chumbani kwa
Devotha kipute kilikiwa
kinaendelea na Devotha
alimpeleka Avi vilivyo.Hadi
mzunguko mmoja
ulipomalizika Avi alikuwa
hoi akihema kama mkimbiaji
wa mbio ndefu.Devotha
akamuacha pale chumbani
amelala kitandani akaenda
sebuleni akatazama
kamera.Hii ilikuwa ni ishara
kwa akina Gosu Gosu
“Gosu Gosu hakuna
kupoteza muda ni wakatiwa
kummaliza Avi ” akaelekeza
Mathew na Gosu Gosu
ambaye sura yake ilikuwa
imejikunja kwa hasira
akaificha bastora yake
kiunoni akachungulia nje
hakukuwa na mtu akaenda
katika mlango wa chumba
cha Devotha akakiminya
kitasa taratibu na mlango
ukafunguka akamkuta
Devotha sebuleni akichomoa
bastora yake akanyata na
kuingia chumbani akamkuta
Avi amelala kitandani
hoi.Kijiusingizi kilianza
kumpitia
“Hey ! Gosu Gosu
akamstua
Avi alistuka akainua
kichwa akajikuta
akitazamana na
bastora.Alitaka kuinuka
lakini alichelewa kwani
kidole cha Gosu Gosu tayari
kilikwisha izinga bastora na
risasi zikatoka na kuzama
kifuani kwa Avi.Gosu Gosu
aliyeonekana kuwa na hasira
kali alimchakaza Avi kwa
risasi hadi zilipomalizika
katika bastora.
“Papii imetosha,tayari
amekufa ! akasema Devotha
aliyekuwa amesimama
mlangoni akishuhudia Gosu
Gosu akifanya mauaji yale
“Mfiche bafuni
tutamuondoa baadae”
akasema Gosu Gosu na
kutoka mle chumbani
“Ama kweli safari hii
nimekutana na watu wa aina
yake.Gosu Gosu ni muuaji
hata macho yake
yanaonyesha kwake kutoa
roho ya mtu ni kitu chepesi
mno.Ilitosha kumuua Avi
kwa risasi mbili lakini
amemimina risasi zote
katika bastora yake.Kuna
nyakati hata mimi ninaogopa
sana kuwa karibuna watu
hawa?akawaza Devotha
akamvuta Avi toka kitandani
akampeleka bafuni
akampekua na kuchukua
kila kitu alichokuwa nacho
kisha akatoka na kwenda
chumbani kwa Gosu Gosu.
“Kazi nzuri Devotha.Kwa
sasa tunasubiri Tino aingie
ndani ya ubalozi.Anafanya
jambo la hatari tumuombee
arejee salama”akasema
Mathew aliyekuwa
akishuhudia kila kitu
“Tino tupe mrejesho
tafadhali” akasema Devotha
“Ninakaribia kufika
ubalozini nimechelewa njiani
msongamano mkubwa sana
jioni hii hapa
Nairobi.Nitawajulisha
kitakachoendelea” akasema
Tino
Alikaribia kufika katika
geti la kuingilia ndani ya
balozi akapewa ishara na
walinzi ya kusimama
akapunguza mwendo lakini
walipogundua ni gari la Avi
haraka haraka wakakimbia
kufungua geti.Lilikuwa na
vioo vyeusi hivyo
hawakuweza kuona
aliyekuwa ndani ya gari ni
nani.
“Guys I’m in.Nimepita
getini bila taabu wakidhani
ni Avi.Nahitaji maelekezo ya
kufika katika ofisi ya Avi”
akasema Tino
“Safi sana Tino.Katika
mzunguko fuata njia ya
kushoto halafu utapinda
kulia utaona kibao
kimeandikwa VIP
parking.Huko ndiko
alikoegesha gari Avi wakati
nimekwenda naye” akasema
Devotha na Tino akafuata
maelekezo aliyopewa akafika
katika maegesho
aliyoelekezwa
“Tayari nimefika
maegesho” akasema Tino
“Shuka garini nenda
katika mlango mkubwa
utapitisha kadi mlango
utafunguka utaingia ndania”
akaelekeza Devotha.
Tino akavuta pumzi
ndefu nakusema
“Pray for me guys”
Akashuka garini na
kuangaza pande zote
kulikuwa kimya na ofisi
chache zilikuwa zinawaka
taa.Alipohakikisha hakuna
tatizo lolote akatembea kwa
kujiamini kuelekea katika
mlango mkubwa akatoa kadi
ya Avi akaipitisha na mlango
ukafunguka akaingia ndani
akakuta kuna lifti nne
“Tayari nimeingia kuna
lifti nne ninaziona” akasema
Tino
“Kuelekea ofisini kwake
panda lifti ya kushoto kwako
hadi ghorofa ya sita ndiko
ziliko ofisi za
Mossad.Ukishuka kwenye
lifti fuata korido hadi
chumba cha mwisho kabisa
kwenye kona hiyo ndiyo ofisi
ya Avi” akasema Devotha na
Tino akaingia ndani ya lifti
hadi ghorofa ya sita
akashuka na kuanza
kutembea kuelekea katika
chumba cha mwisho kama
alivyoelekezwa.Wakati
akielekea katika ofiosi ya Avi
mara mlango wa ofisi moja
ukafunguliwa wakatoka
jamaa wawili lakini Tino
hakuwajali akajiamini na
kupishana nao.Jamaa wale
nao hawakumjali kabisa
waliamini Tino ni mmoja wao
kwani asingeweza kuingia
katika ghorofa ile kama si
muhusika wa Mossad.
Alifika chumba cha
mwisho ambacho ndicho ofisi
ya Avi kwa mujibu wa
maelekezo ya Devotha
akapitisha kadi ile mlango
ukafunguka akaingia ndani.
Mara tu Tino alipoingia
ndani ya ofisi ya Avi,katika
chumba walimo Gosu Gosu
na Devotha simu ya Avi
ikaanza kutoa mlio.
“Tino hebu jaribu kutoka
ndani ya hicho chumba”
akasema Devotha na Tino
akatoka ndani ya kile
chumba
Mara tu Tino alipotoka
ndani ya kile chumba ule
mlio katika simu ya Avi
ukakoma
“Nadhani kuna
muunganiko kati ya ofisi na
simu ya Avi.Ulipofungua tu
mlango simu ikaanza kutoa
mlio ulipotoka ikaacha”
akasema Devotha
“Kuna kitu hata mimi
nimekigundua ambacho si
kawaida katika ofisi
hii.Hakuna hewa na hakuna
kitu chochote kinachowaka
hata taa ya ndani haiwaki”
“Ofisi hiyo” akasema
Ruby akiwa Dar es salaam
“Ina mfumo maalum
ambao unamtambua Avi
pekee na ndiyo maana
wakati ule alipoingia na
Devotha hakukuwa na tatizo
lolote.Akiwa nje ya ofisi na
mlango wa ofisi yake
ukafunguliwa atajulishwa
kwa kutumia simu yake ya
mkononi iliyounganishwa na
mfumo huo.Lazima iko
namna ya kuweza kuufungua
mfumo huo kwa kutumia
simu ya Avi.Tino ingia tena
katika hiyo ofisi na mlio
ukianza katika simu ya Avi
ichukue na ujaribu
kuifungua uizime kengele ”
akasema Ruby
“Sawa nimekusikia
Ruby” akasema Tino na
kufungua tena mlango wa
ofisi ya Avi akaingia ndani
na simu ya Avi ikaanza tena
kutoa mlio.
“Devotha ichunguze simu
hiyo ya Avi kwa haraka
lazima kuna namna ya
kuweza kuufungua mfumo”
akasema Ruby na Devotha
akaichunguza simu ile
akakuta mahala kuna alama
ya kuweka dole gumba Gosu
Gosu akatoka mbio akaenda
chumbani kwa Devotha na
kukata dole gumba la Avi
kisha akaliweka katika ile
sehemu inayohitaji dole
gumba la Avi na mara simu
ikafunguka na Devotha
akapekua akaipata sehemu
iliyoandikwa unlock the
system akaibonyeza na
ofisini kwa Avi taa zikawaka.
“Tino nini kimetokea
hapo?akauliza Devotha
“Taa zimewaka” akasema
Tino
“Good sasa nataka uende
katika kompyuta ya Avi
uiwashe” akaelekeza
Devotha na kwa haraka Tino
akaenda katika kompyuta ya
Avi akaiwasha na kukutana
na sehemu inayomtaka
aingize namba za siri.Ruby
tayari alikuwa na namba za
siri za kufungulia kompyuta
ile ya Avi akamtajia Tino
akaziingiza namba zile na
kompyuta ya Avi ikafunguka.
“Elekeza kamera yako
katika kompyuta ya Avi”
akasema Ruby na Tino
akaelekeza kamera katika
kompyuta ya Avi akaanza
kumuelekeza namna ya
kuiunganisha na kompyuta
ndogo aliyokuwa nayo
Tino.Haraka haraka Ruby
akaanza kazi yake akiwa Dar
es salaam huku
akimuelekeza Tino kufanya
mambo kadhaa katika
kompyuta ile ya Avi.Baada
ya muda wa dakika kadhaa
mafaili yakaanza
kuhamishwa kutoka katika
kompyuta ya Avi kuingia
katika kompyua ya
Tino.Asilimia zilihesabu
haraka haraka namna
mafaili yalivyokuwa
yakihama kutoka katika
kompyuta ya Avi.Ilipofika
asilimia mia moja Tino
akaelekezwa kitu cha
kufanya halafu akaizima ile
kompyuta ya Avi akatoka
ndani ya ile ofisi na
kuufunga mlango akaanza
kutembea kwa tahadhari
hadi katika lifti akashuka na
kuelekea maegesho alikoacha
gari la Avi akaingia na
kuondoka,akafunguliwa geti
bila kuulizwa chochote
walinzi wakidhani ni Avi
ndiye aliyekuwamo ndani ya
gari.
“Nimetoka salama”
akasema Tino
“Kazi nzuri sana sasa
rejea hotelini” akasema
Mathew.
Kabla ya kurejea hotelini
Tino akapita kuchukua
baadhi ya vifaa ambavyo
aliagizwa na Gosu Gosu
kisha akarejea hotelini.
“Mathew tayari nimefika
hotelini salama” Tino
akawajulisha akina Mathew\
“Tino kazi nzuri
sana.Sasa ni wakati wako
Gosu Gosu unajua nini cha
kufanya wakati Ruby
akiendelea kupitia kile
ambacho tumekipata kutoka
katika kompyuta ya Avi.”
akasema Mathew.Gosu Gosu
akachukua vifaa alivyokuja
navyo Tino ambavyo ni shoka
dogo kali,panga na kisu
kikubwa kikali na bila
huruma akaanza kuikata
kata miili ya dereva na
mlinzi wa Avi ikafungwa
vizuri katika mifuko ya
nailoni na kuingizwa ndani
ya masanduku makubwa
akaenda pia chumbani kwa
Devotha na kufanya hivyo
pia kwa Avi halafu usafi
mkubwa ukafanyika kabla ya
miili ile iliyokuwa ndani ya
masanduku kuondolewa mle
hotelini.Gosu Gosu Anita
wakayakokota masanduku
yale matatu hadi katika lifti
wakashuka chini wakatoka
nje ya hoteli hadi katika gari
la Avi.Tino alibaki nyuma ili
kuhakiki usalama wa
wenzake.Baada ya
kuhakikisha wenzake
wameingia garini na yale
masanduku Tino naye
akawafuata akaingia garini
wakaondoka.Walielekea
mtaa Fulani ambako Tino
akawataka Gosu Gosu na
Devotha wabaki garini yeye
akashuka baada ya dakika
kama kumi hivi akarejea
akiwa na watu wengine
wawili wakaingia garini na
safari ikaanza wakaingia
katika kiwanda kikubwa
haraka haraka masanduku
yale matatu yakashushwa
kutoka garini watu wale
wawili wakiongozana na Tino
wakaingia ndani ya nyumba
Fulani Gosu Gosu na
Devotha wakabaki
garini.Dakika ishirini
zikapita Tino akarejea na
wale jamaa wawili wakaingia
garini na kuondoka pale
kiwandani.Safari ilikuwa ya
kimya kimya kurejea
hotelini.
DAR ES SALAAM
“Mathew kupitia haya
mafaili ambayo Tino
ameyachukua katika
kompyuta ya Avi
tumefanikiwa kupata mambo
mengi ya Mossad kwa
ukanda huu wa Afrika
Mashariki.Siri zao nyingi
sasa tunazo.Tunayo orodha
ya majasusi wote wa Mossad
walioko eneo la Afrika
Mashariki na kati na
kusini.Orodha ya operesheni
zao zote ,watu
wanaowafuatilia na mambo
mengine mengi lakini
kikubwa ni kuipata ramani
ya jengo zima la ubalozi na
Israel nchini Kenya ambayo
inaonyesha kila kitu kuanzia
mfumo wote wa ulinzi,njia za
dharura za kujiokoa endapo
kumetokea
shambulio,mahala
zinapohifadhiwa silaha na
mambo mengine mengi”
akasema Ruby baada ya
kumaliza kuyapitia mafaili
ambayo waliyapata kutoka
katika ofisi ya Avi.
“Good job Ruby.Vijana
wamefanya kazi kubwa sana
kule Nairobi.Ramani hii
ndiyo ambayo tulikuwa
tunaitafuta sana na
hatukujua kama tungeweza
kuipata mapema namna hii
hivyo basi usiku wa leo
tunakwenda Nairobi
kumchukua Edger Kaka”
akasema Mathew
“Usiku wa leo?akauliza
Ruby
“Ndiyo.Kila kitu
kitamalizika usiku wa
leo.Hatuna tena muda wa
kuendelea
kusubiri.Avi,dereva wake na
mlinzi wote wameuawa na
siku ya kesho wataanza
kutafutwa na
wasipopatikana tayari
wataanza kuhisi wameuawa
na kufanya operesheni yetu
kuwa ngumu hivyo lazima
tuhakikishe kila kitu
kinamalizika usiku wa
leo.Kikosi cha jeshi cha
operesheni maalum ambacho
tutashirikiana nacho kipo
tayari muda wowote kwa
kazi hivyo sioni sababu ya
kuendelea
kusubiri.Everything ends
tonight and we’ll bring Edger
Kaka home” akasema
Mathew.
“Mathew una hakika
hakuhitajiki maandalizi zaidi
kabla ya kuvamia ubalozi
huo?akauliza Ruby
“Ruby usihofu.Kikosi
ambacho utashirikiana nacho
ni kikosi hatari kabisa na
wao muda wotewapo tayari
kwa kazi hawahitaji
maandalizi.Kikubwa kwao ni
kujua wapi wanakwenda na
kufanya nini.Tunayo ramani
ambayo inatuongoza katika
kila kitu hivyo hakuna haja
ya kupoteza muda kufanya
maandalizi.Tukitaka kuvuta
muda zaidi tutatengeneza
mazingira magumu.Avi ni
mtu mkubwa na shughuli
nyingi za Mossad
zinamtegemea yeye,simu
yake tumeizima na
itakapofika asubuhi bado
hapatikani simuni na
hajulikani alipo wataanza
kuingiwa na wasi wasi na
juhudi za kumtafuta zitaanza
mara moja na wasipompata
hadi kufika kesho mchana
wataamini amepatwa na
jambo baya hivyo basi
tahadhari kubwa
itachukuliwa na kuifanya
kazi ya kumchukua Edger
kaka iwe ngumu ndiyo
maana ninataka usiku wa leo
operesheni hiyo
imalizike.Sisi tuko
tayari,kikosi kiko
tayari,hakuna cha kusubiri”
akasema Mathew na
kuchukua simu akampigia
Dr Evans
“Mathew habari yako
kijana wangu.Umekuwa
kimya sana nini
kinaendelea?akauliza Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais kabla
sijasema chochote nataka
kufahamu kama wale jamaa
wamekupigia simu siku ya
leo” akasema Mathew
“Hawajanipigia simu na
hata mimi nashangaa kwa
ukimya wao.Waliniahidi
kunipigia simu kunipa
maelekezo mengine ya nini
wanakitaka lakini
nashangaa mpaka sasa
hawajawasiliana nami na
hapa nilipo
nimechanganyikiwa sijui hali
ya mwanangu
ikoje.Nimejaribu kupiga
namba zile walizotumia
kunipigia
hazipatikani.Nifanye nini
Mathew? Akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais usiwe
na hofu mwanao atakuwa
salama.Hawatakubali
mwanao afe watahakikisha
kwa kila namna anakuwa
mzima ili waweze kumtumia
katika mabadilishano na
Edger Kaka.Bado wanaamini
kwamba wewe unafahamu
mahala alipo Edger na ndiyo
maana wanamshikilia
mwanao hivyo basi
watahakikisha kwa namna
yoyote ile mwanao anakuwa
salama na ndiyo maana
wakamtaka kwanza Olivia ili
aweze kumtibu virusi vile
alivyomuambukiza” akasema
Mathew
“Mathew ahsante sana
kwa kunipa moyo lakini yule
ni mwanangu lazima niwe na
wasi wasi.Ukimya wao
unanipa mashaka sana
kwamba yawezekana
wanashindwa kuwasiliana
nami kwa kuwa mwanangu
tayari amefariki”
“Tusiombe hayo yatokee
mheshimiwa Rais,nina
uhakika mkubwa kwamba
mwanao atakuwa mzima
kabisa.Nina uzoefu na hawa
magaidi namna
wanavyofanya operesheni
zao na Coletha watakuwa
wanamchunga sana kwa kila
namna wawezavyo.”
“Tuachane na hayo
nataka kufahamu mmefikia
wapi katika maandalizi
yenu?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
nimekupigia kukujulisha
kwamba timu niliyoituma
kwenda Nairobi kufanya
maandalizi ya
operesheni,imefanya kazi
nzuri na tayari tumefanikiwa
kuipata ramani ya jengo la
ubalozi na tayari
tumefahamu mahala alipo
fichwa Edger kaka na
kikubwa zaidi sote
tumefanikiwa kumuona na
kuthibitisha kuwa ni yeye
japo amedhoofu
mno”akasema Mathew
“Hongera sana Mathew
na timu yako kwa kupiga
hatua hiyo kubwa ndani
muda mfupi.Sikutegemea
kabisa kama mngeweza
kulifanikisha jambo hilo
mapema namna hii” akasema
Dr Evans
“Mheshimiwa
Rais,katika kuifanikisha kazi
waliyotumwa watu wetu
wamelazimika kutoa uhai wa
watu watatu akiwemo mkuu
wa Mossad Afrika mashariki
na kati dereva wake na
mlinzi.Mhshimiwa Rais
naamini tumeupanua zaidi
mgogoro huu lakini
hakukuwa na namna
nyingine ililazimu watu hao
wauawe ili tupate
tunachokihitaji”
“Ni kweli Mathew hiki
kilichofanyika kinaongeza
mafuta kwenye moto lakini
kama ilikuwa lazima watu
hao wauawe ili tupate
tunachokihitaji mimi sina
tatizo.Kwa hiyo nini mipango
yenu baada ya kupata
mlichokuwa mnakihitaji?
“Mheshimiwa Rais
operesheni yetu ya
kumchukua Edger Kaka
inakwenda kufanyika usiku
wa leo”
“Usiku wa leo?akauliza
Dr Evans kwa mshangao
kidogo
“Ndiyo mheshimiwa Rais
lazima tuifanye usiku wa
leo.Aliyeuawa ni mkuu wa
Mossad Afrika Masjhariki
hivyo asipopatikana hasi
asubuhi ya kesho wataamini
ameuawa hivyo kuifanyakazi
ya kwenda kumchukua
Edger kuwa ngumu ndiyo
maana ninataka kila kitu
kimalizike usiku wa leo”
akasema Mathew
“Mathew hatuwezi
kuzungumza suala hili
simuni nataka ufike hapa
ikulu mara moja.Mmoja wa
wasaidizi wangu ambaye
nimemuweka hapo awasaidie
atakuleta hapa ikulu mara
moja” akasema Dr Evans
“Sawa mheshimiwa Rais”
akajibu Mathew na Dr Evans
akakata simu.Mathew
akampigia Tino Nairobi
“Tino mnaendeleaje
huko?
“Tunaendelea vyema
Mathew.Tumetoka kumalizia
kuiteketeza miili ya wale
jamaa”
“Good.Avi ni mtu
muhimu sana kwa Mossad
na lazima atatafutwa,mna
hakika hawataweza
kupatikana na kugundulika
wameuawa?akauliza Mathew
“Haitakuwa rahisi
kupatikana kwani miili yao
imetupiwa katika tanuru
kubwa la moto na hivi
tunavyoongea imekwisha
kuwa majivu.Hakuna hat
mfupa utakaoonekana”
“Good.Tino nataka
kuwapa mrejesho wa kile
ambacho tumefanikiwa
kukigundua kutoka katika
yale mafaili tuliyoyachukua
ofisini kwa
Avi.Tumefanikiwa kupata
siri nyingi za Mossad afrika
mashariki lakini kikubwa
tumefanikiwa kupata ramani
ya jengo la ubalozi yenye
kuonyesha kila kitu.Baada
ya kuipata hiyo ramani
hatuna tena muda wa
kuendelea kusubiri hivyo
basi tunakwenda kumchukua
Edger Kaka usiku wa leo”
“Usiku wa leo?akauliza
Tino
“Ndiyo Tino,usiku wa leo
tutamaliza kila kitu na
kuondoka
Nairobi.Hamtakiwi kuwepo
hapo Nairobi hadi kufika
kesho asubuhi kwani Avi
ataanza na ninyi ndiyowatu
wa mwisho kuonekana naye
hivyo mtakuwa katika hatari
kubwa.Kila kitu kinakwenda
kufanyika usiku wa leo kabla
Avi hajaanza kutafutwa”
akasema Mathew na
kunyamaza baada ya mlango
kufunguliwa akaingia mmoja
wa wasaidizi wa Rais
Mathew akamfanyia ishara
asubiri dakika mbili
“Tino ninakwenda
kuonana na Rais muda si
mrefu ili kupanga namna
tutakavyotekeleza
operesheni hii na baada ya
kutoka huko nitawapa
taarifa nini kinaendelea
lakini kwa muda huu anzeni
kujiandaa na hakikisheni
mkiondoka hapo hotelini
mnaacha kila kitu kiko
salama.Kama kuna kamera
za usalama hapo hotelini
fanyeni kila namna
mnayoweza kufuta
kumbukumbu zote.Tino
wewe unao utaalamu huo”
akasema Mathew
“Sawa Mathew tunaanza
kujiandaa na utakapokuwa
tayari utatujulisha mambo
yanavyokwenda” akasema
Tino na Mathew akakata
simu akamuaga Ruby
ambaye aliendelea kupitia
mafaili yale waliyoyapata
kutoka katika ofisi ya Avi
akaingia katika gari na
kupelekwa ikulu.