Riwaya: Siri

SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 4
Simu ya Dr Evans iliita
na kumfanya ahisi
baridi.Alizifahamu namba
zile alizoziona katika kioo
cha simu yake.Ni namba
alizopigiwa na wale magaidi
waliofanya shambulio katika
hospitali ya Mtodora na
kumteka mwanae.Mikono
ilimtetemeka alipoishika ile
simu
“Ee Mungu naomba
ujasiri wa kulikabili hili
jambo” akaomba kimya
kimya na kuipokea ile simu
“Hallow” akasema Dr
Evans
“Nilikuahidi kukupigia
baada ya dakika thelathini
muda umefika.Nataka kujua
umetekeleza maelekezo
yetu?akauliza yule jamaa
“Ndiyo ninaye mtu
mnayemtaka.Kabla sijawapa
mtu mnayemtaka nataka
kujua namna
nikatakavyompata
mwanangu” akasema Dr
Evans
“Si rahisi hivyo kama
unavyodhani mheshimiwa
rais.Mwanao utampata
lakini kwa wakati ule
tunaotaka sisi na kama
utaendelea kutekeleza kila
kile
tutakachokuelekeza.Usihofu
bado tutakuwa na
mazungumzo marefu mimi
na wewe lakini kwa sasa
nataka Olivia apelekwe
Mkumbira mtaa wa Binti
Kassim.Nyuma ya soko la
mfenesini kuna msikiti na
mbele kidogo ya msikiti kuna
miembe mitatu ambako kuna
gari limeegeshwa
hapo.Nataka Olivia aingizwe
katika gari hilo.Gari
litakalomleta Olivia mahala
hapo nataka awepo mtu
mmoja pekee
ndani.Tunafuatilia na kama
tukiona kuna watu wawili
ndani yake au kuna gari
linafuata utamkosa
mwanao.Kuwa makini sana
wakati huu” akasema yule
jamaa
“Vipi kuhusu
mwanan………….” Dr Evans
akataka kuuliza lakini tayari
simu ilishakatwa.
“Bastard !! akasema Dr
Evans na kuitupa simu
kitandani akashika kiuno
“Natamani nitume kikosi
kikawasambaratishe hawa
magaidi lakini ninasita
kufanya hivyo kwa sababu ya
mwanangu kwani
anaumwa.Wameshika mpini
hawa jamaa ninatakiwa
kufanya kile
wanachokitaka.Ngoja nitoe
maelekezo Olivia apelekwe
mahala walipoelekeza”
akawaza Dr Evans na
kumpigia simu yule mtu
wake ambaye alimtuma
kumchukua Olivia Kitalu 2
akampa maelekezo ya
mahala kwa kumpeleka
Olivia
SAA TATU ZILIZOPITA
“Devotha umekosea sana
kubishana na
Mathew.Unatakiwa
kumfahamu Mathew vyema
kama unataka kufanya naye
kazi.Hapendi
kubishana.Hata kama kuna
kitu unataka kumuelekeza
tafuta namna nzuri ya
kumuelekeza na si kufanya
kama ulivyofanya wewe.Hata
mimi sikufurahi namna
ulivyojibizana naye” Ruby
akamwambia Devotha mara
tu alipomaliza kuzungumza
na Mathew simuni.Devotha
akamtazama na kuuliza
“Umefanya kazi na
Mathew kwa muda gani?
“Nimekuwa nafanya kazi
na Mathew kwa muda mrefu
sasa.Kwa nini umeuliza?
“Unaonekana u mtiifu
sana kwake na ndiyo maana
umeweza kufanya naye kazi
muda mrefu.Mimi sijazoea
kupewa amri kama
alivyofan…” akasema
Devotha na kunyamaza
baada ya kuhisi mtetemo
katika mkono wake wa
kushoto.
“Excuse me ! akasema
Devotha na kutoka
akaelekea bafuni akavua ile
glovu ambayo amekuwa
akivaa mkononi.Devotha
hakuwa na vidole viwili
katika mkono wake wa
kushoto hivyo basi huvaa
glovu maalum ambayo
imewekewa vidole vya
bandia na kumfanya
aonekane ana vidole
vilivyokamilika.Kutoka
ndani ya ile glovu akatoa
kidole kimoja akakifungua
na kutoa kitu Fulani mfano
wa kadi ndogo halafu akavaa
tena ile glovu akatoka na
kumfuata Ruby
“Ruby naweza kutumia
simu yako?akauliza Devotha
“Hii simu Mathew
ameiweka maalum kwa ajili
ya kuwasiliana sisi kwa sisi
katika operesheni yetu na
hatutakiwi kupiga namba
tofauti zaidi ya ile ya
Mathew au Gosu Gosu”
“Nataka kumtafuta
Saada.Huyo ndiye alitusaidia
tukaweza kumuokoa Mathew
lakini mpaka sasa hakuna
anayejua mahala alipo”
akasema Devotha.Ruby
akasita
“Nisaidie Ruby.Saada ni
mtu muhimu sana
kwangu.Lengo langu ni
kufahamu kama ni mzima na
yuko wapi” akasema Devotha
na Ruby akampatia ile simu
akatoka akaenda chooni
“Simuamini huyu
mwanamke.Anaonekana ana
jambo hata ukimuona usoni
macho yake yanaonyesha
wasi wasi.Au amepatwa na
wasiwasi baada ya
kumueleza kuwa alifanya
kosa kubishana na Mathew?
Nahisi hivyo kwa sababu
alionyesha kupata mstuko
wakati tukilizungumzia
suala hilo.Anataka
kuwasiliana na nani? Ni
kweli anataka kuwasiliana
na huyo mtu wake kujua
mahala alipo? Kama kweli
anataka kuwasiliana na huyo
mtu wake kwa nini
amekwenda kujificha
chooni?Hapa kuna kitu
anakificha” Akawaza Ruby
na kuinuka akanyata
kumfuata Devotha kule
chooni.
Devotha akaingia chooni
akajifungia na kufungua ile
simu ya Ruby akaweka ile
kadi ndogo aliyoitoa katika
glovu yake kisha akawasha
simu na ujumbe ukaingia
katika simu ile
akausoma.Kilichoandikwa
katika ujumbe ule ni namba
ambazo alihitaji kuwasiliana
nazo.Devotha akapiga simu
katika zile namba
alizotumiwa
“Hallow” akasema
Devotha
“Your Identification
number please! Ikasema
sauti ya mwanamke upande
wa pili
“BRAVO 15E 361 A”
Akasema Devotha
“Thank you Devotha,wait
for three seconds” ikasema
sauti ya yule mwanamke
“Nilijua tu huyu
mwanamke
anatudanganya.Ngoja
niendelee kusikiliza nijue
mtu anayewasiliana naye”
akawaza Ruby aliyekuwa
amesimama mlangoni
akisikiliza kila
alichokizungumza Devotha
“Devotha”ikaita sauti
upande wa pili
“Hallo Dr Yonathan !
akasema Devotha
“Nahitaji kuonana nawe
usiku huu” akasema Dr
Yonathan
“Kuna nini Dr
Yonathan?akauliza Devotha
“Ninakusubiri ofisini
kwangu.Fika haraka sana”
akasema Dr Yonathan
“Sawa ninakuja hapo
ubalozini mud..” Devotha
akastuka baada ya kuhisi
kuna mtu
mlangoni.Akasogea mlangoni
na kuufungua akachungulia
nje hakuona mtu akaufunga
tena ule mlango
“Dr Yonathan nitakuja
hapo muda si mrefu”
akasema Devotha na kukata
simu akaichomoa ile kadi
“She was listening to me
!! akawaza Devotha
akairejesha ile kadi ndogo
katika kile kidole ndani ya
glovu halafu akajitazama
katika kioo.
“She’s such a pretty lad
but she’s forcing my hand !!
akawaza Devotha na
kuikunja sura yake halafu
akatoka mle bafuni akarejea
chumbani alikokuwa Ruby
na kumrejeshea simu yake
“Umefanikiwa kumpata
uliyekuwa
unamtafuta?akauliza Ruby
na Devotha akawa kimya
kwa muda halafu akasema
“Ruby mimi
unanionaje?akauliza Devotha
“Kwa nini unauliza hivyo
Devotha?
“Just answer me Ruby !
akasema Devotha
“Nakuona wa kawaida
tu” akajibu Ruby akiendelea
na kazi yake katika
kompyuta
“Umekosea sana Ruby
mimi siko kawaida kama
unavyodani.Mimi ni
binadamu lakini waweza
niita binadamu
mashine.Unionapo hapa nina
jicho moja linalofanya kazi
lakini wengi hawalifahamu
hilo.Mwili wangu uliwahi
kuharibiwa vibaya sana kwa
bomu na nilifanyiwa
operesheni Zaidi ya
thelathini na nane hadi
mwili wangu ukawa hivi
unavyoniona leo.Ninaposema
ninao utofauti na wanadamu
wengine ninamaanisha
hivyo.Nikupe mfano mdogo
tu kwamba ninao uwezo
mkubwa sana wa kusikia
kuliko uwezo wa
mwanadamu wa
kawaida.Ninaweza kusikia
hata sisimizi akipita kitu
ambacho katika hali ya
kawaida
hakiwezekani.Nilitengenezw
a hivi kwa sababu maalum
ndiyo maana ninasema mimi
ni binadamu mashine”
akanyamaza na kumtazama
Ruby ambaye alionekana
kuwa na wasiwasi
“Nilipokuwa maliwatoni
nilikusikia ukiwa
umejibanza mlangoni
ukisikiliza kile
ninachozungumza.Sikufurahi
shwa na kitendo kile.Kwa
nini ukanifuatilia kusikiliza
mazungumzo yangu?akauliza
Devotha
“Hapana sijakufuatilia
Devotha” akasema Ruby na
Devotha akamnasa kofi kali
lililombabatiza Ruby kabla
hajakaa sawa akapigwa teke
kali lililompeleka hadi
chini.Devotha akaichukua
bastora iliyokuwa juu ya
meza.
“Ulikuwa na wasi wasi
na mimi? Ulitaka kufahamu
ninafanya nini? Ulikosea
sana.Umejitafutia kifo chako
wewe mwenyewe.I’m sorry
Ruby !! akasema Devotha na
kuizinga bastora akaachia
risasi tatu zilizompata
Devotha.Akachukua simu ya
Devotha pamoja na
kompyuta yake akaviweka
katika mkoba wake na
kutoka.Alijaribu kufungua
geti akashindwa kwani
lilihitaji namba maalum za
kufungulia ambazo
hakuzifahamau akarejea
ndani akachukua kiti na
kukiweka ukutani akaruka
na kushika kingo za ukuta
akapanda na kujirusha
nje.Akabaki pale chini
akigugumia kwa maumivu
makali sehemu ile ya bega
alikokuwa na jeraha la
risasi.Akapeleka mkono
akahisi maji maji,jeraha
lilikuwa linatoa
damu.Akainuka na kuanza
kupiga hatua za haraka
kisha akaandika namba
Fulani katika simu ile ya
Ruby na kupiga.
“Anthony naomba uje
mara moja unichukue
nimekwama sehemu Fulani”
akasema Devotha akimpigia
dereva taksi ambaye
humtumia katika manunuzi
ya vitu mbali mbali
akamuelekeza sehemu ya
kumkuta.
“Natakiwa kuwahi
kumuokoa Bella na wanae
kabla Mathew Mulumbi
hajafika hapo na
kuwachukua.Japokuwa
sijamuelekeza mahala
wanakoishi lakini naamini
lazima atatfuta mbinu
nyingine hadi
apafahamu.Yule jamaa ana
macho ya kikatili mno
anaweza akachinja wale
watoto” akawaza Devotha
“Licha ya kwamba sitaki
watoto wale wapate msuko
suko wowote kutoka kwa
Mathew lakini nahitaji
kutumia jambo hili kama
njia ya kunikutanisha tena
na Kaiza.Ninahitaji tena
kujenga mahusiano kati
yangu naye ili niweze
kumpata Olivia.Kaiza
amechukua nafasi yangu na
ndiye anayeaminiwa na Rais
hivi sasa na kikubwa zaidi
anafahamu alipo Olivia hivyo
basi lazima nitafute namna
ya kuwa karibu naye na
kumfanya aniamini”
akawaza Devotha
“Mossad wana nini hadi
watake kuonana nami usiku
huu? Haijawahi kutokea
nikaitwa usiku namna hii
lazima litakuwa ni suala
muhimu mno la
dharura.Ngoja
nikawasikilize” akawaza
Devotha
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 5
Gari jeusi aina ya BMW
lilifika katika soko la
Mifenesini katika mtaa wa
binti Kassim likapunguza
mwendo..
“Naliona gari moja
linakaribia sokoni nina wasi
wasi ndilo linalomleta Olivia”
akasema jamaa mmoja
aliyekuwa na redio ndogo ya
mawasiliano akiwa juu ya
mti mkubwa wa mwembe.
“Abbas unaweza
ukatazama ndani kuna watu
wangapi?akauliza mtu
mwingine
“Linakaribia kufika hapa
nilipo nitaangalia na
kuwajulisha” akasema
Abbas.
Gari lile lililokuwa
linakwenda taratibu sana
lilifika katika ule mwembe
aliokuwa amejificha
Abbas.Akajitahidi
kuchungulia ndani kwa
kutumia hadubini ndogo
aliyokuwa nayo
“Abbas unaona chochote?
“Idris gari lina vioo
vyeusi kiasi kwamba ni
vigumu kuona ndani” akajibu
Abbas
Gari lile lilipita na
kuelekea eneo la msikiti
“Amefika msikitini”
akasema Isa aliyekuwa
amejificha katika pembe
moja ya ukuta uliozunguka
msikiti.
“Unaweza kuona ndani
kuna watu wangapi?akauliza
Idris
“Namuona dereva peke
yake sioni mtu mwingine”
akajibu Isa.
Gari lile liliupita msikiti
likaelekea katika miembe
mitatu ambako kuna gari
lilikuwa limeegeshwa.
“Anakaribia miembe
mitatu.Mlioko eneo hilo
hakikisheni mtu
anayeshushwa ni Olivia”
Idris mkuu wa operesheni ile
akasema
Gari lile lilifika katika
miembe mitatu na kuegesha
nyuma ya gari moja
lililokuwa limeegeshwa
pale.Baada ya dakika mbili
mlango wa dereva
ukafunguliwa akashuka
jamaa mmoja na kwenda
kufungua buti ya gari.Muda
huo wote alikuwa
anaangaliwa na watu
waliojificha sehemu mbali
mbali za eneo lile na mara tu
alipofungua buti ya gari
wakatokea watu watano na
kumtaka dereva wa lile gari
kusogea pembeni wakamtoa
mtu aliyekuwa ndani ya buti
akiwa amefunikwa mfuko
kichwani wakamvua ule
mfuko na kummulika mmoja
wao akatoa picha na
kuifananisha akatikisa
kichwa kuwaelekeza
wenzake kuwa yule ni
Olivia.Haraka haraka
wakamshusha kutoka katika
ile gari na kumpakia katika
gari lao na kumuamuru
dereva yule kuondoka haraka
eneo lile.Alifuatiliwa hadi
alipoondoka kabisa ndipo
gari nyingine nne zilizokuwa
zimefichwa maeneo yale
zikajitokeza na wale wote
waliokuwa wamejificha
sehemu mbali mbali
wakajitokeza wakaingia
katika magari na kuliweka
kati kati gari lile aliokuwa
amewekwa Olivia
wakaondoka.Idris kiongozi
wa operesheni ile akampigia
simu Fahad mkuu wao
“Fahad tayari
tumempata Olivia” akasema
Idris
“Kazi nzuri sana
Idris.Hakukuwa na tatizo
lolote?akauliza Fahad
“Hakukuwa na tatizo
lolote.Rais ametekeleza kila
kitu kama ulivyomuahidi”
akajibu Idris
“Sawa
tunawasubiri.Chukueni
tahadhari kuhakikisha
Olivia hajawekewa kitu
chochote
kitakachowawezesha
kumfuatilia na kujua mahala
alipo” akasema Fahad
“Tayari tumekwisha
mchunguza na hatujapata
kitu chochote alichofungwa”
akajibu Idris
Baada ya kuzungumza
na Idris,Fahad akampigia
simu Dr Evans
“Umeanza vyema kwa
kutekeleza kile
tulichokuelekeza.Tumempata
Olivia na mwanao ana nafasi
kubwa ya kuendelea kuwa
hai”
“Mmekwisha pata
mlichokuwa
mnakihitaji.Naombeni
mnipatie mwanangu”
akasema Dr Evans
“Tunakwenda taratibu
mheshimiwa rais.Utampata
mwanao lakini si rahisi
namna hiyo.Endelea
kututegea sikio nitakuja
kuzungumza nawe tena
lakini narudia tena
kukuonya endelea kuwa
mkimya na jambo hili
ulifahamu wewe peke yako”
akasema Fahad na kukata
simu huku akitabasamu na
kupiga simu kwa Habiba
Jawad.
“Fahad habar za
huko?akauliza Habiba
“Huku kwema Habiba
tunaendelea vizuri”
“Kuna taarifa gani
Fahad?
“Ninazo taarifa njema
kwamba tumefanya
shambulio usiku huu katika
hospitali kuu ya Mtodora na
tayari tunao Coletha mtoto
wa Rais pamoja na Olivia
Themba” akasema Fahad
“Hizo ni taarifa nzuri
sana Fahad.Hongereni mno
kwa kazi hii kubwa.Huu ni
ushindi mkubwa sana”
akasema Habiba
“Mama ninawataka
msiwe na hofu tutampata
Edger muda si mrefu sana
kwa sasa kinachoendelea ni
kumtibu mtoto wa Rais
kwani hali yake si nzuri sana
kisha tutazungumza na rais
kumtaka atuonyeshe mahala
alipo Edger.Kwa sasa
tumembana kwenye kona na
atatueleza kila kitu
tunachokitaka kwa kuwa
tayari tunaye mwanae hana
ujanja.Tuanze maandalizi ya
kumpokea Edger kwa sababu
uhakika wa kumpata ni
mkubwa sana” akasema
Fahad
“Fahad nataka nikuombe
kitu kimoja.Tafadhali
usimuue Olivia kama
alivyoelekeza Khalid
Radwan.Muhoji taratibu
sana ufahamu ukweli sababu
ya kutekwa kwake.Siamini
kama kweli anatumiwa na
serikali ya Tanzania kuchota
siri zetu.Jambo lingine
unalopaswa kulifahamu ni
kwamba Seif anampenda
sana Olivia.Endapo
akipatikana na akijua
mwanamke ampendaye
tumemuua hatafurahi hata
kidog😵livia amemfanyia
Seif mambo mengi hivyo basi
muhoji taratibu kujua
ukweli.Nisikilize mimi na si
Khalid.Umenisikia
Fahad?akauliza Habiba
“Ndiyo mama Habiba
nimekuelewa nitafanya
kama ulivyoelekeza”
“Ahsante sana nawatakia
kila la heri katika
kufanikisha mpango
huu.Nijulishe tafadhali kila
kinachoendelea ili na sisi
tujiandae” akasema Habiba
na kuagana na Fahad.
“Sasa uhakika wa
kumpata mwanangu Seif ni
mkubwa sana.Kama tayari
wamefanikiwa kumpata
mtoto wa Rais pamoja na
Olivia basi muda si mrefu
Seif atapatikana.Tunatakiwa
kuanza maandalizi mara
moja ya kumpokea Seif.Sijui
nitafanya sherehe gani kwa
kumuona tena mwanangu”
akawaza Habiba na
kumpigia Sayid Omar simu
akampa taarifa zile halafu
akampigia simu Khalid
Radwan akamjulisha kuhusu
taarifa zile alizozipokea
kutoka kwa Fahad
“Hizo ni habari njema
sana Habiba.Nilijua tu njia
pekee ya kumpata Seif ni
kwa kumshikilia mtoto wa
rais na sasa atatueleza
mahala aliko Seif.Nimefurahi
pia kusikia kwamba yule
msaliti Olivia
amepatikana.Ametufanyia
jambo baya na mpaka sasa
hatufahamu ni mambo gani
amewaeleza serikali ya
Tanzania kuhusu
sisi.Kitakachompata
kitakuwa ni fundisho kwa
wengine wenye tabia kama
hii ya usaliti.Wakati
mwingine Habiba
usiwaamini watu kwa
haraka kama ulivyofanya
kwa Olivia.Hakupaswa
kabisa kufahamu chochote
kuhusu sisi.Kwa kuwa
amepatikana adhabu yake ni
kumuondoa kichwa!
Akasema Khalid
“Khalid nilimuamini
Olivia kwa kuwa ni mtu
mwenye msaada mkubwa
kwetu.Bila yeye tusingefika
hapa tulipofika.Ni kwa
sababu yake Seif hakupoteza
maisha alipowekewa
sumu.Ni kwa sababu yake
tuna uhakika leo kwamba
Seif yuko hai.Hatupaswi
kuamini kwa haraka hivyo
kwamba Olivia alikuwa
anatumiwa na
serikali.Tunatakiwa
kumuhoji taratibu kuupata
ukweli na ndivyo
nilivyomuelekeza
Fahad.Olivia tumetoka naye
mbali ninamfahamu vyema
na sina hakika kama
anaweza kuwa anatumiwa
na serikali kutuchunguza
kama unavyodai.Ushauri
wangu ni kumfanyia
mahojiano na kumchunguza
kama kweli anatumiwa na
serikali
kutuchunguza.Tukijiridhisha
kama kweli anatumiwa basi
nitaridhia auawe lakini
endapo hatutagundua
chochote kuhusu kutumiwa
na serikali Olivia bado ni
mtu muhimu sana kwetu”
akasema Habiba
“Habiba mimi sijawahi
kukutana na Olivia hivyo
siwezi kubishana nawe kama
unahisi Olivia hawezi kuwa
msaliti ufanyike uchunguzi
kama ulivyoelekeza na
endapo watu wetu
wakijiridhisha kwamba hana
mahusiano na serikali mimi
sina tatizo naye kabisa lakini
nina uhakika mkubwa
kwamba amekuwa
akitumiwa na serikali na
ninaamini uchunguzi wa
kina ukifanyika mtagundua
hilo.Tukiweka pembeni hilo
suala la Olivia kuna jambo
ambalo nataka lifanyike kwa
haraka ikiwezekana usiku
huu.Nataka Coletha na
Olivia waondolewe
Tanzania.Nataka wapelekwe
nchini Kenya ambako tunazo
nyumba zetu kadhaa
wakahifadhiwe huko na kila
kitu kitaendelea kutokea
kule sitaki tuendeshe
operesheni kutokea Dar es
salaam kwani kuna
uwezekano mkubwa
wakafahamu mahala
walikofichwa Olivia na mtoto
wa Rais.Pale Dar es salaam
watabaki watu
wachache.Rais
atakapoelekeza mahala alipo
Seif watu wetu ambao
watakuwa katika utayari
watamchukua haraka sana
na kumpeleka nchini Kenya
na kutokea pale
atasafirishwa kuja
huku.Nitakapomaliza
kuzungumza nawe nitampa
maelekezo Rashid kule
Kenya afanye maandalizi ya
kuwapokea watu hao
muhimu na kuhakikisha
wanakuwa salama.Habiba
huu ni ushindi mkubwa sana
tumeupata.Tumehangaika
sana kuingia Tanzania na
kuijenga himaya yetu na seif
ni mtu pekee ambaye
tulimjenga na kumtegemea
sana kwa ajili ya kuishika
Tanzania lakini likatokea hili
jambo lililotokea na
kuvuruga mipango yetu
yote.Kwa sasa baada ya
kuwa na uhakika wa
kumpata Seif tunatakiwa
kuendelea na mipango yetu
ya kuhakikisha tunampata
Rais ambaye atakuwa na
mahusiano nasi ambaye
atatusaidia kujenga mtandao
wetu.Tukifanikiwa kujenga
mtandao wetu Imara nchini
Tanzania tutakuwa
tumeliteka bara zima la
Afrika.Tanzania ni kioo cha
Afrika na tukifanikiwa
kujiotesha pale kusambaa
kwenda katika nchini
nyingine Afrika ni jambo
jepesi sana” akasema Khalid
“Mawazo yako ni mazuri
Khalid hata mimi
nakubaliana nawe kuhusu
kuwahamisha Olivia na
mtoto wa Rais kuwapeleka
nchini Kenya.Naamini kila
kitu cha kuwawezesha
kuwahamisha watu hao
kutoka Tanzania kwenda
Kenya wanacho hivyo basi
kama kuna uwezekano zoezi
hilo lifanyike kabla
hakujapambazuka Afrika
Mashariki.Kama kuna
chochote kitahitajika kutoka
kwangu nijulisheni haraka”
akasema Habiba
“Kila kitu cha
kuwawezesha kufanya hilo
zoezi wanacho.Tumewekeza
sana katika tawi letu la
Nairobi kwani ndiyo makao
makuu kwa nchi za Afrika
mashariki na kati.” Akasema
Khalid kisha akaagana na
Habiba akampigia simu
Rashid ambaye ni mkuu wa
IS tawi la Afrika Mashariki
anayeishi Mombasa.
“Rashid kuna taarifa
njema.Ile timu uliyoituma
kwenda Dar es salaam
wakishirikiana na wenzao
waliowakuta pale
wamefanikiwa kuwapata
mtoto wa Rais pamoja na
yule mwanamke aliyetusaliti
Olivia.Hii ni dalili njema
kuwa tumekaribia sana
kumpata Seif”akasema
Khalid
“Mungu ni mkubwa
sana” akasema Rashid
“Kufuatia ushindi huo
mkubwa ninataka ufanye
yafuatayo.Tuma boti haraka
sana iende Dar e salaam
nataka Olivia na huyo mtoto
wa Rais wahamishiwe nchini
Kenya.Kuendelea kuwaweka
nchini Tanzania ni hatari
wanaweza wakagundulika
mahala walipo na
tukawapoteza na
tukiwapoteza tutakuwa
tumeharibu operesheni
nzima.Baada ya
kuwaondosha Tanzania kila
kitu kitaendeshwa kutokea
Kenya.Rashid narudia tena
kukukumbusha kwamba
operesheni hii ni muhimu
mno.Tunamuhitaji Seif na
tuko karibu sana kumpata
na nina uhakika yawezekana
usiku wa leo au kesho
tukafahamu mahala
alipo.Nadhani umenielewa
Rashid” akasema Khalid
“Nimekuelewa
Khalid.Kila kitu
kitakamilika usiku wa leo”
akasema Rashid
“Naamini kila kitu
mnacho cha kuwawezesha
kukamilika opresheni
hii.Kama kutakuwa na tatizo
au mtahitaji chochote
tujulisheni haraka sana”
“Khalid kila kitu tunacho
na kama tukihitaji chochote
tutawajulisha” akasema
Rashid.
Baada ya kuzungumza
na Rashid nchini Kenya
Khalid akampigia simu
Fahad nchini Tanzania na
kumjulisha kuhusu mpango
wa kuwahamisha Olivia na
Coletha kuwapeleka Kenya
na maandalizi yakaanza
haraka.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 6
Kaiza alifika nyumbani
kwake na kuwakuta watu
wake aliowatuma
kumchukua Devotha wakiwa
wamejipanga kuimarisha
ulinzi kuhakikisha hakuna
mtu yeyote anayetoka au
kuingia ndani ya nyumba ile
“Devotha bado yuko
ndani? Kaiza akamuuliza
Ayoub
“Ndiyo mkuu bado yumo
ndani”
“Familia yangu pia imo
ndani?Wapo salama?akauliza
Kaiza kwa wasiwasi
“Wote wako salama
kabisa” akajibu Ayoub
“Good.Ninakwenda ndani
jiwekeni sawa nikiwapa
ishara mtavamia chumbani
haraka sana na kumchukua
Devotha” akasema Kaiza na
kuelekea chumbani kwake
akaufungua mlango na
kuingia ndani akawakuta
Devotha na Bella wakiwa
wamekaa wanazungumza
wakionekana hawana tatizo
lolote baina yao.Kaiza
akawatazama
“My love karibu”
akasema Bella akiinuka na
kumfuata mume wake
akamshika mkono na
kumketisha sofani.Macho ya
Kaiza aliyaelekeza kwa
Devotha
“You are such a
devil.Hujatosheka na watu
uliowaua hadi ukaifuata
familia yangu?Sikujua kama
una roho ya kikatili namna
hii Devotha.Watoto wangu
wamekosa nini hadi
uwafuate na kuhatarisha
maisha yao?Huna hata
huruma na hawa malaika
ambao hawafahamu
chochote?akauliza Kaiza kwa
ukali lakini Devotha
hakumjibu kitu
“Love,punguza hasira na
usubiri Devotha azungumze
nawe.Hayuko hapa kwa
ubaya au kuhatarisha uhai
wa watoto wetu.She’s here to
save us.Tafadhali msikilize”
“Bella kitu gani
amekuambia huyu
mwanamke hadi
ukamuamini.Huyu ni shetani
hana hata chembe moja ya
huruma.She’s not who you
think she is.Usikubali hata
kidogo akaingia ndani ya
kichwa chako na kukupa
maneno mazuri
ukamuamini.She’s a …..”
“Enough !! akasema
Devotha kwa ukali na
kusimama.Kaiza naye
akasimama.
“What !! You want to kill
me now? Akauliza Kaiza kwa
ukali.
“Love,relax !! akasema
Bella akimpiga piga mumewe
mgongoni.
“We need to talk
Kaiza.Bella give us a
room.Take out the twins”
akasema Devotha.Bella na
yule mtumishi wake
wakawabeba watoto
wakawatoa nje ya kile
chumba na kuwaacha Kaiza
na Devotha
“Sit down ! akasema
Devotha
“No I can’t.Huna tena
uwezo wa kuniamuru
chochote.Kama kuna
chochote unataka kuniambia
make it quick na wala
usijidanganye kwamba
utatoka hapa
salama.Ninakupa muda wa
dakika tano kueleza kile
unachotaka kunieleza!
Akasema Kaiza
“Look Kaiza ,I’m not here
to harm your
family.Ninawapenda watoto
wako na kamwe siwezi
kuwadhuru! Akasema
Devotha
“So why are you here ?
akauliza Kaiza kwa ukali
“I’m here to save them !
akajibu Devotha
“You are here to save my
children? Akasema Kaiza na
kutoa kicheko kidogo.
“Wewe Devotha unaweza
kumuonea huruma mtu?
Mambo uliyoyafanya leo
hakuna anayeweza
akakuamini tena.I don’t trust
you anymore.Nilikuwa
nakuamini kuliko watu
wote.Nilifuata kila
ulichonieleza lakini kwa yale
uliyoyafanya leo mauaji
makubwa ya bila huruma
siwezi kukuamini
tena.You’ve become a devil.I
don’t know you anymore !
You are not Devotha I know !
akasema Kaiza
“I’m sorry for what
happened today !! Hata mimi
inaniumiza kwa yale
niliyoyafanya lakini ilikuwa
lazima niyafanye.I did that
for a reason” akasema
Devotha
“You betrayed us.Sisi ni
rafiki zako,ndugu zako
tumekuwa pamoja kwa muda
mrefu lakini
umetusaliti.Umeua marafiki
zako,umeua ndugu
zako.Hakuna sababu
inayoweza kukufanya
ukamwaga damu nyingi
vile.You are a killer
Devotha!! Akasema Kaiza
kwa ukali akatazamana na
Devotha
“Saada ambaye
ulimchukua akusaidie katika
mambo yako amejirusha toka
ghorofani na kufariki dunia
kwa sababu yako.Huna
chochote cha kunieleza
Devotha.Nina hasira na kila
mmoja wetu ana hasira kali
mno na wewe kwa mambo
uliyoyafanya.Natamani hata
hapa nitoe bastora
nikuchakaze kwa risasi”
akasema Kaiza
Devotha akamtazama
kisha akatoa bastora na
kumpatia Kaiza
“Take the gun.Fanya kile
ambacho kinaweza
kukuondolea hasira ulizo
nazo juu yangu” akasema
Devotha na kusimama mbele
ya Kaiza ambaye uso wake
ulikuwa umejikunja kwa
hasira akainua mkono ule
ulioshika bastora
akamnyooshea Devotha
“Shoot me !! akasema
Devotha kwa ukali.Kaiza
akaendelea kumtazama
Devotha kwa hasira huku
akihema kwa kasi
“Kaiza don’t you know
how to shoot? Akauliza
Devotha kwa ukali
“Aaaagghh !! akasema
Kaiza kwa hasira
“Shoote me Kaiza.Maliza
hasira zako.Hii ni nafasi
pekee umeipata na
ukishindwa kuitumia hii
nafasi hautapata nafasi
nyingine tena ya kuniua.So
let us end this.Kill me now !!
akafoka Devotha
Mara Kaiza akaushusha
mkono uliokuwa na bastora
na kujishika kiunoni.
“Umeipata nafasi ya
kuniua na kumaliza kabisa
hasira zako umeshindwa
kuitumia na hautaipata
tena.Sasa ni wakati wangu”
akasema Devotha huku
Kaiza akiendelea
kumtazama kwa hasira.
“Devotha wewe ni
shetani kabisa
!.Nilik…………….” Kaiza
akataka kusema lakini
Devotha akamzuia
“Stop Kaiza ni wakati
wangu.Nilikupa nafasi
ukashindwa kuitumia na
sasa naomba unisikilize”
akasema Devotha Kaiza
akatoa kitambaa na kufuta
jasho lililomjaa usoni
“I’m sorry for what
happened today!Nafahamu
nimewaumiza sana watu
wote.Tumekuwa pamoja
kama ndugu na hata mimi
sikutegemea kama siku moja
kungeweza kutokea jambo
kama hili”akasema Devotha
na Kaiza akatikisa kichwa
“Siamini hata neno moja
utakalonieleza
Devotha.Wewe ni shetani”
akasema Kaiza
“Tafadhali nisikilize hadi
nitakapomaliza” akasema
Devotha
“Una haki ya kuniita
majina yote unayotaka lakini
nataka ufahamu sababu ya
kufanya hivi
nilivyofanya.Olivia tayari
amekwisha ingiwa na itikadi
za kigaidi na hakuna namna
ambayo tungeweza
kumfanya ili atupe taarifa za
mtandao wa IS hivyo
nikaamua kujifanya
ninakuwa upande wake ili
aniamini.Lengo kuu likiwa ni
kutaka kuufahamu mtandao
wao na nini hasa malengo
yao hapa nchini.Nilianza
kwa kudukua simu ya rais ili
nifahamu kama ana uhusika
wowote na kile alichokisema
Olivia kwamba Rais
anafahamu mahala alipo
Edger kaka.Sikufanikiwa
kupata chochote kutoka
katika simu ya Rais kwani
niligunduliwa haraka na
kuanzia hapo nikafungiwa
kila kitu na wewe ukachukua
nafasi yangu.Niliposhindwa
kupata chochote katika simu
ya rais nikaamua kurejea
tena kwa Olivia lakini
sikumkuta tayari ulikwisha
muondoa na kumpeleka
mafichoni.Baada ya kumkosa
Olivia nikakumbuka tunaye
Mathew Mulumbi ambaye
ana mahusiano na Olivia
nikaandaa mpango wa
kwenda kumtoa pale kitalu
1.Tayari nilikwisha ondolewa
katika nafasi yangu ya
ukurugenzi wa idara na
nilikuwa natafutwa hivyo
basi hakuna ambaye
angeweza kuniruhusu
kuingia ndani ya kitalu 1
ndiyo maana nikalazimika
kuingia kwa nguvu na ndipo
yakatokea yale yaliyotokea
lakini kwa namna yoyote ile
ilikuwa lazima nimpate
Mathew Mulumbi”akasema
Devotha na kumtazama
Kaiza ambaye bado sura
yake ilikuwa imejikunja
akimtazama Devotha kwa
hasira kali.
“Hili ni tukio ambalo
katu sintaweza kulisahau
katika maisha yangu.Licha
ya watu wangu kuuawa
lakini hata mimi
nimenusurika kifo” akasema
Devotha na kufungua shati
lake na kumuonyesha Kaiza
jeraha ambako alipigwa
risasi.
“Kitendo cha kumtoa
Mathew Mulumbi kitalu 1
kilimfanya aniamini kwamba
mimi ni mwenzao na
nikapata nafasi ya kuwa nao
karibu na kuwasoma vyema
na hicho ndicho kitu
nilichokuwa nakitaka”
“Kuwa karibu yao?Wako
wangapi?akauliza Kaiza na
ile mistari iliyojikunja usoni
ikatoweka
“Mathew Mulumbi ana
watu wake anaofanya nao
kazi”
“IS?akauliza Kaiza
“Nimegundua kwamba
Mathew Mulumbi hana
mahusiano na kikundi cha IS
bali ana mahusiano na Olivia
Themba.Mathew
hakufahamu kama Olivia
ana ushirika na kikundi cha
IS”
“How come you trust him
so easily? Mathew na Olivia
ni wote ni washirika wa IS”
akasema Kaiza
“Hata mimi niliamini
hivyo mwanzoni na ndiyo
maana nikataka kuufahamu
ukweli na nikatumia njia hii
ya kuwa karibu nao ili
niweze kufahamu kila kitu
kutoka kwao na ndipo
nikagundua kwamba
Mathew hana mahusiano
yoyote na IS na wala hakujua
kama Olivia ana
mashirikiano na IS.Baada ya
kuufahamu ukweli kuhusu
Olivia na IS Mathew na watu
wake ..” akasema Devotha na
Kaiza akamkatisha
“Mathew na watu wake
akina nani?akauliza Kaiza
“Mathew aliwahi kufanya
kazi katika idara ya ujasusi
na kwa sasa anashughulika
na mambo yake binafsi ya
biashara.Pamoja na
kuachana na mambo ya
ujasusi lakini kutokana na
ujuzi wake mkubwa
amekuwa akitumiwa wakati
mwingine na serikali katika
operesheni kadhaa hivyo
anao watu wake
anaosaidiana nao katika kazi
zake.Yupo mmoja anaitwa
Gosu Gosu huyu anadai ni
mwanajeshi amewahi
kupigana vita ya msituni
kwa miaka mingi na
mwingine anaitwa Ruby
alikuwa ni mtaalamu
mkubwa sana wa
kompyuta.Sijawahi
kukutana na mtu
anayeifahamu kompyuta
kama yeye”
“Unasema alikuwa
mtaalamu where is she?
“I shot her.I killed her !!
akasema Devotha
“Kwa nini ulimuua?
“Nilimuua kwa sababu ya
kuikoa familia yako”
“Kwa ajili ya kuiokoa
familia yangu kivipi?akauliza
Kaiza
“Kuna mtu alipiga simu
mchana nyumbani kwa
Mathew akimtafuta Mathew
akadai kwamba anazo taarifa
za kumuhusu Olivia.Kwa
msaada wa Ruby
walifanikiwa kujua mahala
mtu yule alipokuwa wakati
akipiga ile simu ,Mathew na
Gosu Gosu wakaenda na
kukuta kuna watu watano
wameuawa na kufichwa
garini vile vile wakagundua
kuna nyumba ya chini
ambayo hutumika kwa ajili
ya kutesea watu”
“Jesus Christ ! Kaiza
akasema kwa mstuko
“Nilikwambia Ruby ni
mwanamke hatari ambaye
anaifahamu kompyuta kuliko
aliyeigunudua hivyo aliweza
kufanikiwa akiwa mbali
kupata kumbukumbu za
kamera zilizozunguka
nyumba ile na kila kitu
kikawa wazi.Tuliona kila
kitu kilichofanyika katika
nyumba ile.We sawa you
Kaiza.Tulikuona toka
ulivyofika pale na
ukamuingiza Olivia ndani ya
nyumba na mateso yote
uliyompatia.” Akasema
Devotha baada ya Kaiza
kutoa kitambaa mfukoni na
kufuta jasho
“Baada ya mateso mengi
ulionekana kupitia
Kamera,ukimuingiza Olivia
garini akiwa hajitambui na
kuondoka.Wewe ndiye mtu
pekee unayefahamu mahala
alipo Olivia.Mathew
Mulumbi baada ya kumkosa
Olivia alitaka kufahamu
mahala unakoishi.Nilitaka
kufahamu sababu ya kutaka
kujua mahala unakoishi
akadai kwamba anataka
kuiteka familia yako
kukushinikiza ueleze mahala
alipo Olivia.Sikuwa tayari
kwa hilo kwa kuwa nilibaki
na Ruby pekee ndipo
nilipoamua kufanya jambo ili
kuja kuwaokoa familia
yako.Nilimpiga risasi Ruby
ili niweze kupata nafasi ya
kutoka mahala pale na ndipo
nilipokuja mpaka hapa
kuwahi kuwachukua watoto
wako na kuwapeleka sehemu
salama.Hivyo ndivyo
ilivyotokea” akasema
Devotha
“Kaiza naomba uniamini
kwamba haya yote
niliyoyafanya ni kwa ajili ya
kuutafuta ukweli wa kuhusu
Olivia.Kwa sasa baada ya
kuwa na uhakika kuwa
Mathew hana mahusiano na
IS tunabaki na Olivia pekee
ambaye tunapaswa
kuhakikisha tunamlinda kwa
kila namna tuwezavyo kwani
Mathew na wenzake lengo
lao kubwa ni kumpata na
wanatumia kila uwezo walio
nao kuhakikisha
wanampata.Kaiza hili suala
la Olivia si suala dogo.Ipo siri
kubwa ndani yake.Shambulio
lililotoka leo usiku katika
hospitali ya Mtodora ni
mwanzo tu wa mipango ya IS
hapa nchini na kubwa ni
kumshinikiza rais Dr Evans
aweze kuwaonyesha mahala
alipo Edger Kaka.Jengo
lililolipuliwa alikuwa
amelazwa mtoto wa rais na
inawezekana shambulio lile
lilimlenga yeye.Haya yote
Olivia anayafahamu na
kama tukijiweka karibu yake
anaweza akatueleza kila kitu
lakini ili atueleze kuhusu
mipango yao yote lazima
tupate kwanza taarifa za
kumuhusu Edger Kaka na
sehemu pekee ambako
tunaweza kupata taarifa za
Edger ni kwa kumchunguza
rais Dr Evans.Msisitizo huu
unaowekwa na IS kwa Rais
kuonyesha alipo Edger
unatoa picha kwamba Rais
analifahamu jambo hili na
ndiyo maana nilidukua simu
yake kuutafuta ukweli.Olivia
yuko tayari kueleza kila kitu
lakini hadi akipata taarifa za
mahala alipo Edger”
akasema Devotha na
kunyamaza kidogo
akamtazama Kaiza halafu
akaendelea.
“Kaiza kazi yetu ni ..”
“Devotha don’t say
we.Sisi si washirika
tena.Toka ulipoamua
kutusaliti na kufanya mambo
yako peke yako you are not
one of us anymore”
“Kaiza nimejaribu
kukueleza kwa kirefu sababu
ya mimi kufanya hivi
nilivyofanya”
“Lakini mpango wako
haujazaa matunda yoyote
Zaidi ya kusababisha vifo
kwa watu wetu” akasema
Kaiza
“Kaiza tafadhali naomba
unielewe.Tuyaweke pembeni
yote yaliyopita na tuungane
tena kuweza kuzuia
mashambulio Zaidi ambayo
IS wamepanga
kuyafanya.Naamini
mashambulizi Zaidi yatakuja
na sisi tunao uwezo wa
kuzuia yasitokee hivyo
lazima tufanye kila lililo
ndani ya uwezo wetu
kuhakikisha tunaifahamu
mipango ya IS na
kuizuia.Thats what we’ve
been doing for years.Nchi iko
salama kwa sababu hatulali
tukihakikisha hakuna vitisho
vyovyote vya amani yetu na
ndivyo tunavyotakiwa
kufanya hata
sasa.Tuhakikishe hakuna
tena damu ya mtanzania
itamwagika lakini hatuwezi
kufanya hivyo kama
hatutaweza kuungana na
kufanya kazi kwa
pamoja”akasema Devotha
“How can I trust you
again Devotha?
“Niamini kama
ulivyokuwa unaniamini
zamani.Usiwe na wasi wasi
na mimi”
“Natamani kukuamini
Devotha lakini nashindwa.Is
this is one of your games?
“A game? This isn’t a
game.Ingekuwa ni mchezo
ninataka kuucheza
nisingemuua Ruby kwa ajili
ya kuwaokoa familia
yako.Hivi sasa Mathew na
wenzake naamini
wananitafuta kwa kumuua
mwenzao.Pamoja na hilo
nililolifanya kwa familia
yako you still don’t trust
me?akauliza Devotha
“Please trust me
Kaiza.Tumepata nafasi
tuitumie vyema” akasema
Devotha.Kaiza akazama
mawazoni kwa muda halafu
akauliza
“Devotha hata kama IS
wana mipango ya kufanya
mashambulio mengine hapa
nchini tutawezaje kujua?
“Kwa nini unauliza hivyo
Kaiza?We have a
solution.Olivia.Yeye ndie
ambaye atatuongoza
kufahamu mipango yote ya
IS hapa nchini na kama kuna
mashambulio mengine
yanapangwa lakini
atatueleza hayo yote kama
tukifanikiwa kupata taarifa
za kumuhusu Edger Kaka”
akasema Devotha.Kaiza
akamtazama kwa macho
yaliyoonyesha kukata tamaa
“Kuna nini Kaiza?
Akauliza Devotha
“Devotha,Olivia is gone”
“What? She’s gone?
Devotha akashangaa
“Where is she?Is she
dead?akauliza
“Hajafa ni mzima kabisa
ila amechukuliwa na rais”
“Rais
amemchukua?How?akauliza
Devotha akiendelea
kushangaa na Kaiza
akamueleza kila kitu
kilichotokea kuhusu Olivia
“I can’t believe this.Rais
anataka kumpeleka wapi
Olivia?akauliza
“Kuna kitu alikitamka
kwamba haridhishwi na
namna tunavyofanya kazi
zetu na akadai kwamba
ataifuta idara yetu naamini
hata kitendo cha kumchukua
Olivia ni kutokana na
kupoteza imani na sisi”
akasema Kaiza.Devotha
akafikiri kidogo na kusema
“Hapana Kaiza.Rais
anatuamini sana.Toka idara
hii imeanzishwa tumekuwa
tukifanya kazi zetu kwa
weledi mkubwa sana na
hatujawahi
kumuangusha.Nilichokifanya
mimi hakimaanishi kwamba
idara nzima ni mbovu hadi
akatishia kuifuta.Kuna kitu
ninakihisi.Usiku huu
magaidi wamevamia
hospitali alikokuwa
amelazwa mwanae na nina
uhakika mkubwa kwamba
mlengwa mkuu wa uvamizi
ule alikuwa
mwanae.Ninaamni
shambuluo lile ni
muendelezo wa shinikizo la
IS kumtaka Rais awaonyeshe
mahala alipo Edger kaka.”
“Nini unakimaanisha
Devotha?akaulizia Kaiza
“Ninamaanisha kwamba
kama magaidi walivamia
hospitali na katika jengo
moja tu alilokuwa amelazwa
mtoto wa Rais hii ina maana
kwamba walichokuwa
wanahitaji ni kumpata mtoto
wa Rais.Kwa kuwa hakuna
taarifa rasmi hadi hivi sasa
kuhusiana na watu wangapi
wamefariki katika shambulio
hilo kuna mambo mawili
ambayo yananijia
kichwani.Kwanza kuna
uwezekano mkubwa magaidi
wakawa wamemteka mtoto
wa Rais na kwa sababu hiyo
basi Rais akamtaka Olivia ili
aweze kuzungumza naye na
kumtumia ili kumpata mtoto
wake.Pili yawezekana
magaidi tayari wanaye mtoto
wake na wamemshinikiza
rais awapatie Olivia ambaye
ni mtu wao.Yote haya mawili
yanawezekana hivyo basi
kitu cha kwanza kufahamu
ni kama mtoto wa rais
ambaye alikuwa amelazwa
katika jengo lililoshambuliwa
yuko wapi.Je ni mzima au
amekufa? Jibu tutakalolipata
litatuongoza kufahamu kwa
nini Rais amemchukua
Olivia” akasema Devotha
“Hapo ndipo kwenye
tatizo Devotha”
“Usihofu Kaiza kila kitu
niachie mimi.Ninachohitaji
kutoka kwako ni ushirikiano
wako na uniamini.” akasema
Devotha
“Devotha tafadhali huu
usiwe ni moja ya michezo
yako.Naomba suala hili liwe
la kweli na tushirikiane
kuwapata hawa watu ambao
wanatishia amani ya nchi
yetu”akasema Kaiza
“Tutawapata
Kaiza.Ninakuhakikishia
lazima tutawapata” akasema
Devotha na ukimya ukapita
wakaendelea
kutazamana.Devotha
akakumbuka kitu
“Ninahitaji kwenda
sehemu Fulani na
nitakaporejea hapa nitakuwa
na jibu la wapi tuanzie”
akasema Devotha
“Vipi kuhusu Mathew
Mulumbi unadhani ataweza
kufika hapa kama
alivyokuwa
amepanga?akauliza Kaiza
kwa wasiwasi
“Hata kama akifika hapa
tayari unao watu wa kutosha
kukulinda lakini sina
uhakika kama anaweza
akafika hapa kwani mtu
pekee ambaye walikuwa
wakimtegemea awape
maelekezo ya mahala
unapoishi ni mimi na
hawataweza kunipata.Kwa
usiku huu watakuwa na
mstuko wa kifo cha mwenzao
Ruby” akasema Devotha
“Devotha yule mtu
ameweza kuua watu kumi na
tatu ambao tuliwaamini na
kuwategemea sana katika
operesheni mbali mbali nina
hakika akifahamu mahala
nilipo hawa vijana nilionao
hawataweza katu
kumzuia.I’m so scared”
akasema Kaiza
“Usiwe na wasiwasi
Kaiza.Kwa kuwa tayari
umekwisha fahamu kuna
hatari waelekeze watu wako
wajipange vyema kuikabili
hatari yoyote ile
itakayokuja.Kaiza suala hili
la mimi na wewe kuonana ni
siri kubwa kati yetu na
waelekeze vijana wako
wasifungue midomo yao kwa
kile walichokiona humu”
akasema Devotha
“Nitafanya hivyo
Devotha” akasema Kaiza
“Kama hakuna lingine
niruhusu niondoke kwa
muda nitarejea baadae”
“Kuna jambo moja
nataka kulifahamu ulitaka
kuwapeleka wapi familia
yangu ambako ulidai ni
salama?akauliza Kaiza
“Hakuna haja ya
kuwapeleka huko tena kwa
kuwa tayari umekwisha
fika.Sina gari naweza
kutumia gari lako?” akauliza
Devotha.Kaiza akasita
kidogo halafu akaongoza ana
Devotha hadi katika gari
lake akampa funguo na
Devotha akaondoka.
“Naamini sijafanya kosa
tena kumuamini
Devotha.Kama huu ni moja
ya mchezo wake naapa
sintomsamehe kamwe!
Akawaza Kaiza wakati
Devotha akitoka getini na
gari lake
“Nimemaliza upande
mmoja.Haikuwa rahisi
kumshawishi Kaiza akubali
kuwa upande wangu lakini
nashukuru ameniamini sasa
ngoja nielekee ubalozi wa
Israel nikajue Mossad
wanataka kitu gani”
akawaza Devotha akiwa
katika mwendo mkali
“Dr Evans kwa nini
amemchukua
Olivia?Anataka kumpeleka
wapi?akajiuliza
“Kwa namna yoyote ile
lazima kumpata Olivia.Bila
kumpata haya yote
niliyoyafanya leo yatakuwa
ni kazi bure.Damu yote
iliyomwagika leo itakuwa
imemwagika bure” akawaza
Devotha
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 7
“Wakati ninamsubiri
Sasha anipe jibu ngoja
nirejee maskani nikajue hali
ya Ruby kwani sifahamu
itamchukua Sasha muda
gani kupiga
tena.Yawezekana naye yuko
katika shughuli zake”
akawaza Mathew akiwa bado
katika bustani ya Kiembe
kavu na kuingia garini
akaondoka
“Nitakesha usiku wa leo
nikimtafuta Devotha na
nikimpata atajuta kunitoa
ndani ya lile shimo” akawaza
Mathew na kuvuta kumbu
kumbu namna alivyohojiana
na Devotha na hadi
alivyoongoza operesheni ya
kumkomboa
“Aliua watu wa idara
yake kwa ajili ya
kunikomboa mimi kwa nini
sasa ametugeuka? I was so
stupid to trust her ! Kama
ningechukua tahadhari ya
kutosha mapema haya yote
yasingetokea na Ruby
asingekuwa katika
hatari.Yeye mwenyewe
alinusurika kupoteza maisha
kwa kupigwa risasi wakati
akinikomboa nini hasa
lilikuwa lengo lake?Alitaka
kuwa upande wetu na kujua
mipango yetu? Akajiuliza
“Majibu yote nitayapata
pale nitakampomtia
mikononi” akaendelea
kuwaza Mathew akiendelea
kukanyaga mafuta.
Hadi alipowasili katika
makazi yao bado Sasha
hakuwa amempigia simu
kumpa jibu la namba
zilizowasiliana na simu ile ya
Ruby aliyotoroka nayo
Devotha.
“Mambo yanakwendaje
hapa?akauliza Mathew
baada ya kuingia katika
chumba alimolazwa Ruby
“Kila kitu kinakwenda
vyema.Mpaka sasa sijaona
tatizo lolote kwa Ruby
mifumo yake yote inakwenda
vyema na pale dawa ya
usingizi itakapokwisha basi
atazinduka.Msiwe na wasi
wasi wowote” akasema Dr
Hiran
“Dr Hiran nakushukuru
sana kwa msaada huu
mkubwa”
“Usihofu Mathew hii ni
kazi yangu hata hivyo
marafiki lazima tusaidiane
naamini iko siku na mimi
nikiwa na tatizo utakuwa
tayari kunisaidia” akasema
Dr Hiran
“Wewe ni rafiki wa kweli
Dr Hiran muda wowote
ukiwa na tatizo usisite
kunieleza nami nitakusaidia”
akasema Mathew akiwa
ameyaelekeza macho yake
kwa Ruby
“Unadhani itamchukua
muda gani kuzinduka kutoka
usingizini?akauliza Mathew
“Sina hakika lakini
atazinduka tu msiwe na
hofu” akasema Dr Hiran
kisha Mathew akamuita
Gosu Gosu wakaenda katika
chumba cha kusomea
“Gosu Gosu yule
mwanamke anacheza na
akili zetu.Alifahamu kwa
alichokifanya lazima
tutamfuatilia na akacheza
mchezo wa kutuchanganya
akili zetu tushindwe sehemu
ya kuanzia kumtafuta lakini
nakuhakikishia lazima
atapatikana.Kama si usiku
wa leo basi haitavuka kesho
lazima
atapatikana.Ninaamini simu
hii hakuichukua kwa ajili ya
kwenda kuitelekeza pale
bustanini bali alikuwa na
kazi nayo.Ninasubiri jibu la
Sasha kujua ni namba zipi
ambazo Devotha aliwasiliana
nazo baada ya kutoka hapa”
akasema Mathew
“Mathew nina wazo kwa
nini usimpigie tena simu
huyo Sasha? Yawezekana
amekwisha sahau kama
unasubiri jibu toka kwake”
akashauri Gosu Gosu
“Ni wazo zuri ngoja
nimpigie” akasema Mathew
na kumpigia simu Sasha
“Mathew nisamehe sana
nilikwisha sahau kama
nilikuahidi kukupigia”
akasema Sasha baada ya
kupokea simu
“Usijali Sasha nafahamu
majukumu yako”
“Mathew nimefuatilia ile
simu nitakutumia namba
mbili za mwisho kuwasiliana
nayo” akasema Sasha na
kumtumia Mathew namba
ambazo ziliwasiliana na ile
simu aliyoondoka nayo
Devotha
“Sasha nashukuru sana
kwa msaada huu mkubwa”
“Karibu tena Mathew”
akasema Sasha na kukata
simu
“Gosu Gosu ulikuwa
sahihi kabisa.Tayari Sasha
alikwisha
nisahau.Amenitumia namba
hizi mbili ambazo
zimewasiliana na simu hii ya
Ruby ninaamini ni Devotha
aliyepiga” akasema Mathew
na kuzitazama zile namba
halafu akaipiga namba ya
kwanza ikaanza kuita na
baada ya muda ikapokelewa
“Your Identification
number please! Ikasema
sauti ya mwanamke upande
wa pili wa simu na Mathew
akakata simu
“Nimeulizwa namba ya
utambulisho.Naamini ni
Devotha aliyetakiwa kutaja
namba yake ya utambulisho”
akasema Mathew
“Yawezekana labda
alipiga simu katika idara
yao” akasema Gosu Gosu
“Yawezekana lakini
ukumbuke tayari
amewasaliti wenzake na
anatafutwa” akasema
Mathew
“Kama si idara yake ni
nani hawa wanaohitaji
namba ya utambulisho?
Akauliza Gosu Gosu
“Ninavyofahamu mimi
mifumo kama hii yenye
kuhitaji namba za
utambulisho huwa ni katika
mashirika ya kijasusi au
taasisi nyingine za usalama”
akasema Mathew na kuipiga
ile namba ya pili ikaita na
baada ya muda ikapokelewa
“Hallow” ikasema sauti
ya mwanaume
“Hallow habari yako
ndugu yangu” akasema
Mathew
“Nzuri kabisa habari
yako”
“Salama.Nikusaidie nini?
“Nahitaji kukufahamu
ndugu yangu nimekuta
namba yako katika simu ya
mpenzi wangu”
“Mpenzi wako
nani?akauliza yule jamaa
kwa ukali kidogo
“Devotha.Unamfahamu?
“Ouh kumbe
Devotha.Ninamfahamu sana
amekuwa ananituma kazi
nyingi mara kwa mara kama
kwenda kumfanyia
manunuzi mbalimbali.Mimi
ni dereva taksi naitwa
Antony” akasema
“Nafurahi kukufahamu
Anthony.Unapatikana
sehemu gani?
“Mimi hupatikana hapa
Queen tower hotel”
“Sawa Anthony imekuwa
vizuri nimekufahamu ila
kuna kitu nataka kuuliza”
“Uliza usihofu”
“Devotha amekupigia
simu usiku huu kuna kazi
yoyote alikutuma umfanyie?
“Mbona una wasiwasi
kaka? Kuna tatizo
lolote?akauliza Anthony
“Hakuna tatizo Antony
kuwa na Amani”
“Devotha aliponipigia
simu usiku huu hakunituma
kazi bali alinitaka nimpeleke
sehemu Fulani”
“Unaweza ukanipeleka
mahala hapo?akauliza
Mathew na Antony akasita
“Usihofu
Antony.Nitakulipa kiasi
kizuri cha pesa.Labda kwa
kukudokeza tu ni kwamba
nimepanga kumvisha
Devotha pete ya uchumba
lakini
sijamwambia.Nimetoka
safari nje ya nchi usiku huu
na ninataka kumshangaza
kwa kumfuata mahala alipo
kumvisha pete ya
uchumba.Nataka kumfanyia
sprise.Nisubiri hapo
tafadhali ninakuja ndani ya
dakika kumi na tano”
akasema Mathew na kukata
simu
“Sasa jibu
limepatikana.Baada ya
kutoka hapa Devotha
aliwasiliana na Anthony
ambaye ni dereva taksi
akamtaka ampeleke sehemu
Fulani.Naamini Antony
atakubali kutupeleka mahala
alikompelelka
Devotha.Tujiandae tuelekee
huko” akasema Mathew
“Vipi kuhusu Ruby?
“Atabaki hapa na Dr
Hiran.She’ll be fine.Naamini
mahala alipo Devotha hivi
sasa atakuwa na ulinzi hivyo
tunahitaji kwenda sote
wawili” akasema Mathew na
kumfuata Dr Hiran
“Dr Hiran mimi na Gosu
Gosu tunatoka kwa muda
kuna sehemu tunaelekea
kisha tutarejea.Ninakuomba
endelea kumuhudumia Ruby
na hakikisha anakuwa
salama.Kama kuna kitu
chochote kitatokea nijulishe
haraka sana” akasema
Mathew
“Usiwe na wasi wasi
Mathew.Nafahamu
umuhimu wake kwenu hivyo
nitafanya kila
kinachowezekana
kuhakikisha anakuwa
salama” akasema Dr Hiran
“Ahante sana Dr Hiran”
akasema Mathew wakatoka
na kuingia garini
wakaondoka.
“Mathew una hakika
Ruby atakuwa salama hapa
peke yake? Nina wasiwasi
sana na Devotha kwani
anapafahamu mahala hapa
na kama lengo lake lilikuwa
kutuchunguza sisi anaweza
akawaleta wenzake hapa”
akasema Gosu Gosu
“Tumkabidhi Mungu
atamlinda lakini hatuna
namna ya kufanya,Devotha
ni muhimu sana kupatikana
kwa sasa” akasema Mathew
Walitumia chini ya
dakika ishirini kufika Queen
tower hotel kutokana na
mwendo mkali ambao
Mathew alikuwa
anaendesha.Baada ya kufika
katika maegesho Mathew
akatoka ndani ya gari na
kumpigia simu Antony
“Antony tayari nimefika
hapa Queen Tower
hotel.Nielekeze mahala ulipo
tafadhali” akasema Mathew
baada ya Antony kupokea
simu kisha akamuelekeza
mahala alipo.
“Gosu Gosu ninamfuata
Antony,wewe utatufuata kwa
nyuma na kama kuna hatari
yoyote unaiona utanijulisha”
akasema Mathew na
kutembea kuelekea mahala
zinakoegeshwa taksi
akampata Antony
“Karibu sana kaka”
akasema Antony akionekana
kuwa na wasiwasi.
“Ahsante
Antony.Nashukuru
kukufahamu.Naomba
unipeleke ile sehemu
tafadhali” akasema Mathew
huku akifungua mlango na
kuingia garini.Antony
akawasha gari na kuondoka
kumpeleka Mathew mahala
alikompeleka Devotha.
****************
Devotha aliwasha taa ya
kushoto ya gari na kukata
kona akaifuata barabara
inayoelekea katika ubalozi
wa Israel nchini
Tanzania.Toka akiwa mbali
akawashiwa taa ya
kumuashiria apunguze
mwendo wa gari na
apunguze ukali wa
taa.Alipunguza mwendo na
kuendesha gari taratibu hadi
alipokaribia getini
akasimamishwa na walinzi
wenye silaha
akajitambulisha kwamba
ana miadi ya kukutana na
balozi wa Israel nchini
Tanzania.Gari la Olivia
likakaguliwa kama lina
hatari yoyote kama vile
mlipuko akakutwa na
silaha.Mmoja wa walinzi
wale akapiga simu ndani ya
ubalozi kumjulisha balozi
kwamba mgeni wake
amekwisha fika na akatoa
maelekezo aruhusiwe
kuingia ndani.Kabla
hajaruhusiwa Devotha
akatakiwa kwanza kuacha
silaha yake kwa walinzi
halafu akaingia
ndani.Anaifahamu ofisi ya
balozi kwani si mara ya
kwanza amefika hapa lakini
kabla hajaingia katika
chumba cha lifti akamkuta
mlinzi mmoja aliyevaa suti
nyeusi akamuelekeza aingie
katika chumba kimoja
akakaguliwa na mashine
kama ana hatari yoyote
halafu akaruhusiwa kupita
moja kwa moja akaelekea
katika ofisi ya balozi na
kugonga mlango
akaruhusiwa kuingia
ndani.Hakuwa peke yake
ndani ya ile ofisi alikuwa na
watu wengine wawili
“Dr Yonathan” akasema
Devotha
“Devotha karibu sana”
akasema Dr Yonathan
akainuka na kwenda katika
meza iliyokuwa na chupa
kadhaa za mvinyo
akamimina katika glasi na
kumpatia glasi moja Devotha
“Nashukuru Dr
Yonathan lakini kwa leo
sintatumia kinywaji kwani
ninatumia dawa”
“Unaumwa nini?akauliza
Dr Yonathan
“Ni matatizo ya
kawaida.Habari za
hapa?akauliza Devotha na
Dr Yonathan akagugumia
mvinyo wote uliokuwemo
katika glasi halafu
akamtazama Olivia
“Samahani kwa
kukusumbua usiku huu
lakini nashukuru kwa
kufika”
“Usijali Dr Yonathan”
akasema Devotha
“Devotha kama
unavyoona humu ndani
ninao wageni wawili ambao
ni Fishel” akasema Dr
Yonathan na Fishel akatikisa
kichwa huku akitabasamu
“Mwingine ni Ehud”
Ehud naye akatikisa kichwa
baada ya kutajwa
“Ehud na Fishel kutaneni
na Devotha Adolph ni wakala
wa Mossad hapa Tanzania”
akasema Dr
Yonathan.Devotha
akasimama na kuwapa
mikono majasusi wale
“Nimefurahi kukutana
nanyi.Karibuni sana
Tanzania” akasema Devotha
“Sisi pia tumefurahi
kukutana nawe” akajibu
Fishel
“Devotha baada ya
kufahamiana sasa tuelekee
moja kwa moja katika kile
kilichotukutanisha hapa
usiku huu” akasema Dr
Yonathan na kunyamaza
kwa muda halafu akaendelea
“Fishel na Ehud
wametokea Tel Aviv
wametumwa na Mossad hapa
Tanzania kwa ajili ya kazi
maalum na wewe ukiwa
kama wakala wa Mossad
hapa Tanzania ni jukumu
lako kuhakikisha kwamba
wanafanikiwa kile
kilichowaleta hapa
Tanzania” akasema Dr
Yonathan na ukimya mfupi
ukapita
“Ningependa kufahamu
nini hasa kilichowaleta hapa
Tanzania?akauliza
Devotha.Fishel akakohoa
kidogo kurekebisha koo
halafu akasema
“Tumekuja kwa ajili ya
kufanya maandalizi ya
operesheni kabambe ya
Mossad itakayofanyika hapa
Tanzania siku chache zijazo”
akasema Fishel na
kunyamaza kidogo
“Operesheni gani ambayo
Mossad wanataka kuifanya
hapa Tanzania?akauliza
Devotha
“Operesheni ambayo
Mossad wanataka kuifanya
hapa Tanzania ni kumtafuta
mtu anaitwa Olivia Themba”
akasema Fishel na Devotha
akapatwa na mstuko
mkubwa
“Olivia
Themba?!akauliza
“Ndiyo,Olivia Themba”
akajibu Fishel
“Nimestuka kidogo
kusikia Mossad wanamtafuta
Olivia Themba” akasema
Devotha
“Tunafahamu kwamba
Olivia ametekwa nyara na
watu wasiojulikana mpaka
sasa hajapatikana wala
hajulikani alipo na ndiyo
maana tumekuja sisi
kuandaa operesheni ya
kumtafuta” akasema Fishel
“Nini hasa sababu ya
Mossad kumtafuta
Olivia?akauliza Devotha
“Swali hilo hatutaweza
kukujibu Devotha.Jukumu
lako kama wakala wetu ni
kuhakikisha unatusaidia sisi
kuweza kuandaa na
kufanikisha operesheni yetu
na kumpata Olivia” akasema
Fishel na Devotha akajikuta
amekosa neno la kuongea
“Devotha wewe ni
mkurugenzi wa idara ya siri
ya usalama wa ndani wa nchi
naamini kabisa kwamba
mara tu baada ya tukio hili
kutokea idara yako imekuwa
inashughulikia suala hili
kwa karibu sana.Nataka
kufahamu namna tukio hili
la kutekwa Olivia
lilivyotokea na mwisho
nataka kufahamu ni wapi
idara yako imefikia hadi sasa
kufahamu waliomteka Olivia
ni akina nani na mahala
alipo” akasema
Fishel.Devotha akameza
mate kulainisha koo kwani
alihisi kama sauti
inashindwa
kutoka.Akawatazama
majasusi wale kwa zamu
ambao walikuwa
wamemkazia macho
“Pamoja na ujasiri wangu
lakini hapa nimegonga ukuta
hawa jamaa wamenibana
kwenye kona.Sikujua kama
Mossad nao wanamtafuta
Olivia.Najuta kuamua kuwa
wakala wao hapa
Tanzania.Hata hivyo
sintawaeleza ukweli kuhusu
Olivia.Siko tayari wampate
Olivia kwani ni mtu muhimu
sana ambaye hata mimi
ninamsaka kwa udi na
uvumba”akawaza Devotha
“Devotha !! akaita Dr
Yonathan baada ya kumuona
Devotha amezama mawazoni
“Nilikuwa natafuta
namna ya kuanza kulieleza
suala hili” akasema Devotha
“Olivia alitekwa katika
geti la nyumbani kwake
alipokuwa akitoka jijini
Kinshasa”akasema Devotha
na Ehud akamkatisha
“Mnazo taarifa zozote za
nini alikwenda kufanya
nchini Congo DRC?akauliza
Ehud
“Taarifa tulizonazo ni
kwamba alikwenda jijini
Kinshasa kwa shughuli zake
za kiutafiti.Olivia ni daktari
ambaye anaendesha kituo
cha utafiti wa magonjwa
mbali mbali ya wanadamu na
wanyama.Zilikutwa sampuli
za damu katika gari lake na
baada a kuzipima
zikagundulika ni damu za
wanyama Sokwe ambazo
alizikusanya kwa ajili ya
kuzifanyia utafiti katika
kituo chake” akasema
Devotha.Ukimya mfupi
ukapita Fishel akasema
“Endelea Devotha”
“Watekaji walikuwa
wamejiandaa vyema
walitumia helkopta
kuusimamisha msafara wake
na kufanya mashambulizi
wakaua walinzi wa Olivia
kisha wakamchukua na
kuondoka naye.Helkopta
iliyotumika katika utekaji
huo ilipatikana imetelekezwa
na ikabainika watekaji
waliiba helkopta ile
wakaitumia katika shughuli
yao ile kisha wakaitelekeza
mahali nje kidogo ya
jiji.Vyombo vyote vya
uchunguzi hapa nchini
vinashirikiana katika
kumtafuta Olivia na mpaka
sasa hakuna taarifa zozote za
nani aliyemteka Olivia wala
mahala alipo.Idara yangu
mimi ni ya siri na hata
shughuli zake pia
zinafanyika kwa siri bila
kushirikisha idara yoyote ya
serikali lakini hata sisi
mpaka sasa bado hatujapata
ufumbuzi wowote wa jambo
hili.Tunachohisi waliofanya
jambo hili ni watu kutoka nje
wakisaidiwa na watu kutoka
ndani ya nchi”
“Nina swali Devotha”
Akasema Ehud
“Uliza usihofu”
“Umesema kwamba
watekaji waliua walinzi wa
Olivia.Mmefuatilia na kujua
kwa nini Olivia alikuwa na
walinzi wa kumlinda?Alihisi
kuna hatari yoyote
inamkabili hadi akaamua
kuajiri walinzi wa
kumlinda?akauliza Ehud
“Kumekuwa na matukio
ya utekaji nyara kwa siku za
hivi karibuni ndiyo maana
wengi wa matajiri hasa
waliopo hapa Dar es salaam
wameajiri walinzi kwa ajili
ya kuwalinda na ndivyo
alivyofanya Olivia”
“Mmechunguza kama
walinzi wa Olivia walikuwa
ni watu wa aina gani? Je
walipitia mafunzo ya ulinzi?
Ehud akauliza
“Hilo
hatujalifanya.Hatukuwa
tumeliwekea uzito wowote”
akajibu Devotha
“Endelea
Devotha.Ulisema mnahisi
waliomteka Olivia ni watu
kutoka nje ya nchi
wakisaidiwa na watu wa
hapa nchini.Kwa nini
mnahisi hivyo?akauliza
Fishel
“Kwa namna tukio lile
lilivyotekelezwa limefanywa
na watu wenye ujuzi
mkubwa sana ambao
tunaamini wametoka nje ya
nchi.Tunaamini ni watu wa
kutoka nje ya nchi kwa
sababu kumekuwa na
mfululizo wa matuko ya
utekaji wa watu matajiri
hapa nchini kwa siku za hivi
karibuni na watekaji
wamekuwa wakifanya hivyo
kwa ajili ya kujipatia
kipato.Kwa mujibu wa jeshi
la polisi mtandao wa
watekaji wa watu umeanzia
nchini Afrika kusini na
Nigeria na kwa sasa
wameanza kusambaa katika
nchi za Afrika mashariki
ambako matukio kama haya
hayajazoeleka.Katika
matajiri watatu waliotekwa
hivi karibuni na kupatikana
baada ya kutoa kiasi
kikubwa cha fedha ilibainika
wateka walitoka nchini
Afrika kusini na ndiyo
maana hata tukio hili
tunaamini watekaji
wametokea nje ya
nchi.Tunaamini sababu kuu
ya kumteka Olivia ni
kujipatia kipat😵livia
anatoka katika familia ya
mabilionea Agrey na Lucy
Themba.Olivia pia ana
utajiri mkubwa na watekaji
wamelenga kujipatia fedha
nyingi kutoka kwa familia ya
Olivia”
“Mna mawasiliano na
wazazi wa Olivia kujua kama
watekaji wamewasiliana nao
kudai kiasi cha fedha?
akauliza Fishel
“Tuna wasiliana mara
kwa mara na mpaka sasa
bado hawajapata simu yoyote
kutoka kwa watekaji lakini
naamini watekaji hao lazima
watawasiliana nao na
wameahidi kutujulisha pindi
wakipokea simu yoyote
kutoka kwa watekaji”
akasema Devotha
“Unaweza
ukatukutanisha na familia
ya Olivia tukazungumza
nao?akauliza Fishel na swali
lile likambabaisha kidogo
Devotha
“Devotha unaweza
ukatukutanisha na familia
ya Olivia tukazungumza
nao? Fishel akauliza
“Familia ya Olivia ni
watu wa karibu sana na Rais
hivyo baada ya kutokea kwa
tukio hili ulinzi mkali
umewekwa kuilinda familia
hiyo na si rahisi kuonana
nao.Kuna watu wachache na
maalum ambao
wanaruhusiwa kuonana nao
hata hivyo nitajaribu
kufanya mipango ili muweze
kuonana nao.Nini sababu ya
kutaka kuonana
nao?akauliza
“Kuna mambo tunataka
kuyafahamu kutoka
kwao”akasema Fishel
“Sidhani kama hilo ni
wazo zuri.Familia hii wana
ukaribu mkubwa sana na
rais na ninyi mko hapa
Tanzania hamna kibali cha
kufanya operesheni yenu
taarifa zinaweza kumfikia
Rais na kila kitu
kikaharibika.Ninawaomba
muwe watulivu na mfuate
kile
nitakachowaelekeza.Mimi
ndiye wakala wenu hapa
Tanzania na nitasaidiana
nanyi kuhakikisha
mnampata Olivia lakini
msijaribu kutaka kufanya
kitu chochote ambacho
kinaweza kuhatarisha
usalama wenu hapa
Tanzania na kinachoweza
kuniweka mimi pia katika
hatari.Hakuna anayefahamu
kama mimi ni wakala wa
Mossad hapa Tanzania”
akasema Devotha.
“Sawa Devotha sisi
tunakusikia wewe ambaye
ndiye wakala wetu lakini
tunataka kufahamu namna
utakavyotusaidia kuandaa
operesheni yetu na hatimaye
tuweze kumpata Olivia”
akasema Ehud
“Ninaomba mnipe muda
hadi asubuhi ili niweze
kuandaa mpango mzuri wa
namna ya kuwasaidia
kutekeleza operesheni yenu”
akasema Devotha.
“Hakuna tatizo Devotha
nenda katuandalie mpango
mzuri ambao utatuwezesha
kufanikisha operesheni yetu
hapa Tanzania.Kikubwa
tunachokihitaji ni kupata
walau fununu za mahala
alipo Olivia ili majasusi wetu
waweze kuingia hapa nchini
na kumchukua.Timu ya
majasusi iko katika utayari
wakisubiri kupata taarifa
muda wowote kutoka kwetu
ili waweze kuingia hapa
nchini” akasema Fishel
“Msihofu kila kitu
kitakwenda vizuri” akasema
Devotha.Hakukuwa na
mazungumzo Zaidi Devotha
akaagana na balozi
Yonathan akaondoka.
“Nimepatwa na mstuko
mkubwa sana ambao
sikuutegemea kiasi kwamba
nahisi kama ile sehemu
niliyoshonwa inaanza
kuachia” akawaza na
kupeleka mkono mahala
penye jeraha akagusa maji
maji
“Hili jeraha sitakiwi
kulifanyia mzaha linaweza
kuniletea matatizo
makubwa.Nahitaji kulitibu
haraka kabla halijaleta
madhara.Kwa hali ya mambo
inavyokwenda nahitaji kuwa
na afya njema” akawaza na
kuvuta pumzi ndefu
“Sikuwahi kupatwa na
mstuko kama nilioupata leo
baada ya kusikia kwamba
Mossad nao wanamtafuta
Olivia.Sikujua kama suala
hili la Olivia lingekuwa
kubwa kiasi hiki kiasi cha
kuwafanya shirika kubwa la
ujasusi Mossad nao kutaka
kufanya operesheni ya
kumtafuta.Kwa nini Israel
wanamtafuta Olivia?
Wamekuwa wagumu kueleza
sababu ya kumtafuta
Olivia.Kama ningejua
mapema alichoniitia Dr
Yonathan ni suala hili la
Olivia katu nisingekwenda
kuonana naye” akawaza
Devotha
“Nimewadanganya
sikutaka kuwaeleza
ukweli.Siko tayari wampate
Olivia ambaye ana siri
kubwa tunayohitaji
kuipata.Endapo Mossad
watampata Olivia
hatutaweza tena kuipata siri
hiyo ambayo Olivia
aliniambia atanieleza pale
nitakapokuwa nimepata
taarifa za mahali alipo Edger
Kaka.Kuna siri kubwa
imejificha hapa katika suala
hili la Edger Kaka na kubwa
ni ushiriki wa IS katika
suala hilo.Mpaka sasa
hakuna anayefahamu IS
wanahusikaje na Edger
Kaka? Limebaki ni fumbo
lakini mtu pekee mwenye
majibu ya fumbo hili ni
Olivia Themba ambaye
hatujui mahala aliko hadi
hivi sasa.Hatujui Rais
amempeleka wapi.Mossad
hawapaswi kumpata Olivia
kabla yetu.Nitahakikisha
hakuna operesheni yoyote ya
Mossad itakayofanyika hapa
nchini kabla hatujampata
Olivia.Nimefanya mambo
makubwa ikiwemo kutoa
uhai wa watu wangu kwa
ajili ya kutaka kuifahamu
siri aliyonayo Olivia hivyo
siwezi kuwapa nafasi Mossad
wakampata Olivia kabla
yangu” akaendelea kuwaza
Devotha na kuongeza ubaridi
ndani ya gari kwani ubaridi
uliokuwepo haukutosha bado
alihisi joto.
“Kwa sasa ngoja nielekee
nyumbani kwangu.Tayari
nimekwisha elewana na
Kaiza hakuna tena kitu cha
kuhofia.Nahitaji kuwasiliana
na Mary aje anitazame hili
jeraha” akawaza Devotha
akielekea nyumbani kwake
“Kuna kitu
nimekigundua kwa Devotha
sijui kama na ninyi
mmekigundua” akasema
Ehud baada ya Devotha
kuondoka
“Kuna kitu hata mimi
nimekiona” akasema Fishel
“Devotha kuna kitu
anatuficha hataki kutueleza
ukweli.Baada ya kuombwa
atukutanishe na familia ya
Olivia kwanza alistuka na
kisha akasema hilo
haliwezekani.Ameonyesha
wasi wasi mkubwa baada ya
kusikia tunataka kuonana na
wazazi wa Olivia.Binafsi
mstuko huu aliouonyesha
Devotha unanifanya niwe na
wasiwasi kama maelezo haya
aliyotupa yana ukweli ndani
yake.Nina uhakika mkubwa
sana kuna jambo Devotha
analificha” akasema Ehud
“Kama mna wasiwasi na
Devotha anaweza asiwezeshe
operesheni yenu kufanikiwa
nini mnashauri
kifanyike?akauliza Dr
Yonathan
“Kwa upande wangu
nakubaliana na Ehud
kwamba Devotha hawezi
akatueleza kila kitu na
ushauri wangu ni kwamba
tusimtegemee sana katika
operesheni yetu ila tuwe na
mpango mbadala lakini papo
hapo tuendelee kuwa nyuma
yake na tumuonyeshe
tunamtegemea sana yeye ili
asiwe na wasiwasi wowote na
sisi kwamba kuna mambo
tunayafanya nyuma
yake.Sehemu ya kwanza
ambako nashauri tuanzie
kufanya uchunguzi wetu kwa
siri ni kwa familia ya
Olivia.Tukionana nao
wanaweza wakatupa picha
pana Zaidi ya suala hili la
kutekwa kwa Olivia.Kuna
mambo ambayo tunaweza
kuyapata yakatusaidia sana
kufahamu nani kamteka
Olivia na pengine kufahamu
hata mahala alipo” akasema
Fishel
“Mawazo ya Fishel ni
mazuri sana na yatatusaidia
kuweza kupata taarifa za
kutekwa Olivia” akasema
Ehud.Walifanya majadiliano
kisha wakapelekwa katika
sehemu walikoandaliwa
kupumzika.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 8
Hakukuwa na maongezi
mengi garini kati ya Mathew
na Anthony hadi walipofika
katika nyumba ambako
Antony alimpeleka Devotha.
“Nilimleta katika
nyumba hii” akasema Antony
“Una uhakika ni
hapa?akauliza Mathew
“Ndiyo nilimleta
hapa”akasema Mathew na
kutoa kitita cha noti kwa ajili
ya kumpa Antony ghafla
akatokea jamaa mmoja
akipiga hatua kubwa
kuelekea gari la akina
Mathew.Hatua kadhaa kabla
hajalifikia gari la akina
Mathew akaanguka chini na
bastora ikaanguka pembeni
yake.Antony akastuka sana
baada ya kuiona bastora ile.
“Ana bastora !! akasema
huku akitazama nyuma ili
aweze kuondoa gari.
“Relax don’t panic”
akasema Mathew baada ya
kujua ile ilikuwa kazi ya
Gosu Gosu aliyekuwa katika
gari la nyuma
yao.Akamkabidhi Antony
kitita cha fedha na kujiandaa
kushuka lakini ghafla
wakatokea watu watatu
wakiwa na bastora.
“Antony ondoa
gar…………”kabla Mathew
hajamaliza risasi zikaanza
kuvuma.Mathew akamvuta
mkono Anthony kumlaza
chini ya kiti lakini alichelewa
kwani risasi nyingi zilipigwa
upande ule wa dereva.Kwa
kasi ya aina yake Mathew
akafungua mlango na
kuruka nje.Akazama chini ya
uvungu wa gari akatambaa
na kuchungulia aliwaona
watu wale watatu wakiwa
wamelala chini wakivuja
damu.Ilikuwa ni kazi ya
Gosu Gosu aliyewazimisha
wote kwa risasi
Kutokea pale chini ya
uvungu wa gari Mathew
akailenga taa kubwa iliyokua
getini iliyokuwa na
mwangaza mkali
ikasambaratika na eneo lile
la nje likawa na mwangaza
hafifu kutoka kwa taa
zilizokuwa ndani ya jumba
lile.Mathew akarejea garini
kumtazama Antony hakuwa
na uhai tayari alikwisha
fariki.
“Mathew ! Gosu Gosu
akamuita Mathew kwa sauti
ndogo
“He’s gone” akasema
Mathew na kutoka ndani ya
ile gari
“Tayari wanajua tuko
hapa na kama kuna wengine
ndani watakuwa
wanajipanga kutusubiri
tuingie ndani” akasema Gosu
Gosu
“Vyovyote itakavyokuwa
lazima tuingie ndani na
kumpata Devotha.She’s in
there.Hata kama litakuja
jeshi zima
tutapambana.Kama ni kufa
tufe tukijaribu” akasema
Mathew.
“Kitu cha kufanya ili
kutusaidia tuweze kuingia
ndani kiurahisi ni kulifanya
eneo liwe na giza.Tuziondoe
zile taa kubwa zinazoleta
mwangaza mkubwa pale
ndani ili tupate nafasi ya
kuing…..” Kabla Mathew
hajamaliza sentensi yake taa
zote zikazimika
“Kama vile walikuwa
katika mawazo yetu”
akasema Mathew
“Usihofu Mathew uko na
mwanajeshi.Huu ni mchezo
mdogo sana.Nimepambana
kwa miaka mingi vita ya
usiku.Nifuate
mim……..aaagghh..!! Gosu
Gosu akatoa mguno na
kuanguka chini.
“Gosu Gosu are you
okay?akauliza Mathew
“Nimekoswa na risasi
imenikwaruza
shingo.Usihofu I’m okay
Mathew”akasema Gosu Gosu
“Kuna
wadunguaji.Tayari
wametuona mahala
tulipo.We need to do
something ! akasema
Mathew
Mathew akaingia ndani
ya lile gari la Antony
akamtoa na kisha akaligeuza
kulielekea geti na Gosu Gosu
akaleta jiwe Mathew
akaliweka katika pedeli ya
mafuta gari lile likaanza
kutembea huku Mathew na
Gosu Gosu wakiwa nyuma
yake.Mivumo ya risasi
ikasikika na vioo vya gari
vikivunjwa kwa risasi.Hii
iliwapa nafasi akina Mathew
kufahamu kirahisi mahala
walipokuwa wamejificha
watu waliokuwa ndani ya
nyumba na kuwapa urahisi
wa kuwaondoa.Mara milio ya
risasi ikakoma baada ya
kulikaribia geti.Lile gari
halikuwa na dereva
likagonga geti na kishindo
kikasikika.Mathew na Gosu
Gosu wakajibanza kusubiri
kama kuna mtu yeyote
ambaye atajitokeza baada ya
kusikia kishindo kile cha geti
kugongwa na gari lakini
zilipita dakika mbili bila
hatua ya mtu kusikika Gosu
Gosu akausukuma mlango
mdogo wa geti wakaingia
ndani.Kulikuwa kimya sana
na hakukuwa na dalili za
kuwepo mtu.
“Kuko kimya sana
yawezekana kuna watu
wamejificha wakisubiri
tujitokeze.Cover me !
akasema Mathew na kuanza
kukimbia kuelekea katika
kibaraza.Alipofika
akajibanza nyuma ya
sanamu kubwa ya kifaru
iliyokuwa katika kibaraza
cha nyumba ile.Gosu Gosu
naye akakimbia kumfuata
Mathew hakukuwa na mlio
wowote wa risasi tena.Eneo
lote la nyumba ile lilikuwa
giza kulikuwa na mwangaza
hafifu kutoka katika taa za
nyumba za jirani.
“Umeme katika nyumba
hii ulizimwa makusudi
kabisa.Katika nyumba nyingi
kifaa cha kukata a kuwasha
umeme huwekwa sebuleni
naamini hata humu
itakuwepo sebuleni.I’m going
to look for it cover me”
akasema Mathew wakaingia
sebuleni.Mathew akajibanza
na kuangaza pande zote
kama kuna mtu yeyote
ataonekana lakini kulikuwa
kimya hakukuwa na mtu
yeyote.Mathew akawasha
tochi ya simu yake na
kuanza kuchunguza ukutani
na kama alivyokuwa amehisi
akafanikiwa kukiona kifaa
cha kuwashia na kukatia
umeme akawasha na taa zote
zikawaka wakachukua nafasi
haraka haraka kuangalia
kama kuna mtu yeyote
atakayejitokeza kisha
wakaanza kupanda ghorofani
wakiingia katika chumba
kimoja baada ya
kingine.Walishangaa kwa
ukimya uliokuwepo
“Wamekwenda wapi
watu wote?akauliza Gosu
Gosu
“Hata mimi
nashangaa.Au yawezekana
tumewamaliza wote?
Akasema Mathew
Chumba cha mwisho
walichoingia ni chumba
kikubwa cha kulala ambacho
kilikuwa kitupu hawakukuta
mtu yeyote.
“Tumemkosa !! akasema
Gosu Gosu
“She was here.Lazima
kuna namna
ametoroka.Wakati ule
ilipozimwa taa ndipo
alipoweza kutoroka”
akasema Mathew wakashuka
na kuanza kufanya
uchunguzi wakagundua
kulikuwa na mlango wa
nyuma uliokuwa wazi.
“Lazima atakuwa
ametoroka kupitia mlango
huu” akasema Mathew
“Hata kama ameondoka
hatakuwa mbali
sana.Tukifuata njia hii ya
huku nyuma tunaweza
kumpata” akasema Gosu
Gosu
“Hatutaweza
kumpata.Tayari
ametuponyoka.!! akasema
Mathew na kumtaka Gosu
Gosu warejee ndani.
“Tuchunguze nyumba hii
kwa makini yawezekana
kuna kitu tunaweza
kukipata kinachoweza
kutusaidia kumpata
Devotha” akasema Mathew
wakarejea ndani moja kwa
moja katika kile chumba cha
kulala.Katika meza
iliyokuwemo mle chumbani
kulikuwa na picha
zimeangushwa.Mathew
akachukua picha moja
akaitazama na kustuka.
“This is Kaiza” akasema
na kuchukua tena picha
nyingine akamuona Kaiza
akiwa na mwanamke mmoja
wakitabasamu.
“Hapa ni nyumbani kwa
Kaiza?akajiuliza na kuzipitia
picha zile na zote zilikuwa za
Kaiza.Akamuita Gosu Gosu
aliyekuwa katika chumba
kingine
“Kuna kitu
nimekigundua.Hapa ni
nyumbani kwa Kaiza yule
ambaye alikuwa na
Olivia.Tazama hizi zote ni
picha zake” akasema Mathew
na Gosu Gosu akazipitia zote
“Devotha na Kaiza tayari
walikwisha ingia katika
mgogoro mkubwa baada ya
Devotha kuwasaliti wenzake
na kuungana
nasi.Imewezekanaje Devotha
akaja kuonana na
Kaiza?akauliza Gosu Gosu
“She played us.Huyu
mwanamke ni mjanja sana
ametumia akili nyingi
kujifanya anakuwa upande
wetu ili kutuchunguza lakini
kumbe bado anashirikiana
na idara yake na ndiyo
maana katika ile namba ya
simu ya kwanza niliyopiga
nilitakiwa kutaja namba ya
utambulisho.Naamini namba
ile ni ya mtandao wa idara ya
akina Devotha.Nini hasa
alichokuwa anakitafuta
kwetu hadi afanye yale
yote?akauliza Mathew
“Sasa nimepata jibu kwa
nini alikuwa mgumu
kuelekeza mahala anakoishi
Kaiza kwa kuwa alifahamu
kuwa bado ni mwenzake na
hakutaka kuiweka familia
yake katika hatari na ndiyo
maana baada ya kutoka pale
kwetu alikuja moja kwa moja
hapa na ninaamini alikuja
kumuonya Kaiza kwamba
familia yake iko katika
hatari.Lakini hizi zote ni
mbio za sakafuni hatafika
mbali” akasema Mathew
“Nini kinafuata? akauliza
Gosu Gosu
“Twende tukajipange
upya” akasema Mathew
wakatoka na kuelekea katika
gari lao wakaondoka
“Mathew nimepata wazo”
akasema Gosu Gosu
“Mchana wakati
tukijiandaa kuja
kukukomboa nilihitaji
silaha,Devotha akanichukua
hadi nyumbani kwake na
kuniingiza katika chumba
cha silaha nikachukua kila
nilichokihitaji.Ninapakumbu
ka mahala anapoishi,kwa
nini tusimfuate huko?
Yawezekana tukampata na
vile vile tunahitaji silaha pia”
“Wazo zuri twende huko”
akasema Mathew na Gosu
Gosu aliyekuwa katika
usukani akaongoza njia
kuelekea nyumbani kwa
Devotha
Muda mfupi baada ya
akina Mathew kuondoka
nyumbani kwa
Kaiza,mfuniko wa moja ya
shimo kati ya mashimo
manne ya maji machafu
ukafunuliwa na mtu mmoja
akatokeza kichwa
akachungulia halafu akatoka
na kuelekea ndani
akachunguza nyumba yote
kama kuna mtu halafu
akarejea tena katika lile
shimo
“It’s clear ! akasema na
watu wakaanza kutoka ndani
ya lile shimo ambalo
halikuwa shimo la kuhifadhi
maji machafu bali
lilitengenezwa maalum kwa
ajili ya kujificha pale
inapotokea hatari.Kaiza
akawasaidia mke wake na
watoto kutoka ndani ya lile
shimo wakarejea ndani
“Devotha alikuwa
anasema kweli kuhusu wale
jamaa kuja kuvamia na
kuwachukua watoto
wangu.Sehemu hii
imekwisha kuwa
hatari.Hakuna haja ya
kuendelea kukaa hapa wale
jamaa wanaweza wakarejea
tena.Siwezi kuacha familia
yangu wawe katika hatari.I
need to take them to safe
place” akawaza Kaiza na
kuwapa maelekezo vijana
wake wawili aliokuwa nao
ndani ya lile shimo
wakusanye miili ya wale
wenzao waliouawa kisha
waipeleke kitalu 1.Yeye
akaingia gereji akachukua
gari la mke wake akaiingiza
familia yake na kuondoka
haraka
“Tunaelekea wapi
Kaiza?akauliza Bella ambaye
bado alikuwa
amewakumbatia watoto
wake
“To the safe place”
akasema Kaiza
“Devotha yuko wapi? Will
she be safe?
“Sifahamu yuko wapi
hana simu hivyo hatuwezi
kujua kama yuko salama au
vipi” akasema Kaiza
“Please Kaiza don’t leave
us again.Tuko katika hatari
na tunakuhitaji sana” Bella
akasisitiza.Kaiza hakujibu
kitu alikuwa katika mawazo
mengi
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 9
Wakiwa njiani kuelekea
nyumbani kwa Devotha,simu
ya Mathew ikaita alikuwa ni
Dr Hiran.
“Dr Hiran anapiga”
akasema Mathew kwa
wasiwasi akamtazama Gosu
Gosu halafu akaipokea ile
simu
“Hallow Dr Hiran”
akasema Mathew
“Mathew nimekupigia
kukujulisha kwamba
mgonjwa wetu
amezinduka”akasema Dr
Hiran na Mathew akashusha
pumzi
“Thank you Lord!
Akasema kwa sauti ndogo
“Vipi maendeleo
yake?akauliza Mathew
“Anaendelea
vyema.Lakini kuna maneno
ambayo amekuwa
anayatamka kwa kuyarudia
rudia nimeyaandika nikihisi
pengine yanaweza kuwa na
maana”
“Anatamka maneno
gani?akauliza Mathew
“BRAVO 15E 361 A”
akajibu Dr Hiran
“Dr Hiran nashukuru
sana endelea kuandika kila
anachokitamka tuko njiani
tunarejea sasa hivi” akasema
Mathew na kukata simu
“Gosu Gosu we need to go
back”
“Kwa nini Mathew?Kuna
mabadiliko katika hali ya
Ruby?
“Ruby amezinduka na
kwa mujibu wa Dr Hiran
anaendelea vyema lakini
kuna maneno amekuwa
anayatamka kwa kuyarudia
rudia BRAVO 15E 361 A”
akasema Mathew
“This looks like some
codes” akasema Gosu Gosu
“Ndiyo inaonekana ni
namba Fulani ya siri.Ruby
ameitamka namba hii kwa
kuirudia rudia kwa sababu
ndicho kitu kikubwa
anachokikumbuka kwa
sasa.Tunatakiwa kufahamu
amezipata wapi namba hizi?
Akasema Mathew.Gosu Gosu
akageuza gari na kushika
njia ambayo inaelekea
nyumbani kwao
“Vipi kuhusu
Devotha?akauliza Gosu Gosu
“Baadae tutamtafuta
lakini kwa sasa hili ni la
muhimu sana” akasema
Mathew
“Yule mwanamke ana
maisha marefu kama
paka.Hata hivyo atapatikana
tu hana sehemu ya kujificha”
akaendelea kuwaza Mathew
Iliwachukua saa moja na
na dakika ishirini kuwasili
katika makazi ya
Mathew.Mathew alishuka
garini haraka haraka kabla
hata gari halijasimama
vizuri akakimbilia ndani
“How’s she! Akamuuliza
Dr Hiran
“Relax
Mathew.Anaendelea
vyema.Kwa sasa ametulia
ameacha kuweweseka”
akasema Dr Hiran
“Aliendelea kuzungumza
maneno
mengine?Umeyarekodi?akaul
iza Mathew
“Maneno pekee ambayo
ameendelea kuyatamka ni
yale yale
niliyoyaandika.Alikuwa
anayarudia hadi pale
alipotulia” akajibu Dr Hiran
“Dr Hiran naweza
kuzungumza naye?akauliza
Mathew na Dr Hiran akawa
kimya
“Please Dr Hiran ni
muhmu sana.Anazo taarifa
za muhimu ambazo natakiwa
kuzipata kutoka kwake”
akasema Mathew
“Anatakiwa kuachwa
apumzike lakini kama ana
jambo la muhimu unaweza
ukazungumza naye”
akasema Dr Hiran na
kuongozana na Mathew hadi
katika kitanda cha Ruby
“Ruby…Ruby !! akaita
Mathew na Ruby akafumbua
macho
“It’s me Mathew”
“Ma..ma…” Ruby
akataka kutamka lakini
akaanza kukohoa
“Easy.Easy Ruby”
akasema Mathew
“Mathew nadhani
tumuache kwanza
apumzike”akasema Dr
Hiran.Ruby akamfanyia
Mathew ishara asogee
karibu.Mathew akainama ili
kumsikiliza Ruby
“The codes !! akasema
Ruby kwa sauti ndogo.
“What codes?akauliza
Mathew
“BRAVO 15E 361 A”
“Umezipata wapi hizi
codes? Akauliza Mathew
“Devo…”
“Devotha” akasema Ruby
kwa sauti ndogo
“Umezipata kwa
Devotha?akauliza Mathew
“She made the
call…follow the codes!!
Akasema Ruby
“Ruby this is very
important.Please tell me
everything”
Ruby akakohoa kidogo na
kusema
“She shot me ! Before
that she made the call.I
heard her mention that
codes.Please find her !!
akasema Ruby na macho
yake yakajaa machozi
“Pole sana
Ruby.Yamekwisha,you are
safe.I’ll protect you” akasema
Mathew na kumfuta Ruby
machozi
“Mathew promise you’ll
find her! Akasema Ruby
“I promise you pretty
angel I’m going to find her.I’ll
get her” akasema Mathew
“Thank you
Mathew.Thank you for
saving my life.” Akasema
Ruby
“Ruby wewe ni mtu
muhimu sana kwangu hivyo
yeyote anayecheza na maisha
yako ananigusa moja kwa
moja hivyo nitamuonyesha
Devotha kwamba alikosea
mno kucheza na maisha
yako.Pumzika Ruby daktari
yuko hapa ataendelea
kukuangalia.Mimi na Gosu
Gosu pia tuko hapa.Hakuna
chochote kitakachokutokea
tena” akasema Mathew na
kumbusu Ruby katika paji
lake la uso akatoka nje na
kumkuta Gosu Gosu akiwa
na Dr Hiran.
“Dr Hiran thank you so
much .Naomba tafadhali
uendelee kumuangalia Ruby
usihofu kuhusu malipo”
akasema
“Mathew niko hapa hadi
kutakapopambazuka na
sintafumba jicho langu
kuhakikisha Ruby anakuwa
salama.Mpaka hapa hayupo
tena katika hatari hivyo
msihofu” akasema Dr Hiran
na Mathew akamuita Gosu
Gosu wakaenda katika
chumba cha kusomea
“Ruby amenieleza
kwamba Devotha alipiga
simu na alimsikia akitaja zile
namba ambazo Dr Hiran
alitutumia.Naamini namba
hizi za siri Devotha
alizitumia katika ile namba
ambayo nilipiga na kutakiwa
kutaja namba ya
utambulisho.Ni wakati wa
kufahamu alikuwa
anawasiliana na nani”
akasema Mathew na
kuchukua ile simu ya Ruby
akapiga zile namba ambazo
alitumiwa na Sasha
“Simu inaita” Mathew
akamwambia Gosu Gosu na
kuiweka simu ile katika
sauti kubwa
“Your Identification
number please! Ikasema
sauti ile ile ya mwanamke
aliyoisikia mwanzo alipopiga
simu.
“BRAVO 15E 361 A”
Akasema Mathew.Baada ya
sekunde mbili sauti ile
ikasema
“Thank you Devotha,wait
for three seconds”
Baada ya sekunde tatu
kama alivyoahidiwa sauti ile
ya mwanamke ikasema
“Devotha Dr Yonathan
amenituma nikwambie yuko
kwenye kikao muhimu na
wale wageni kutoka Tel Aviv
atakutafuta baada ya nusu
saa”ikasema sauti ya Yule
mwanamke na Mathew
akakata simu.
“Dr Yonathan ! who is
he? Akauliza Gosu Gosu
“Kuna mambo mawili
hapa yamejitokeza.Kwanza
ni Dr Yonathan na pili ni
wale wageni kutoka Tel
Aviv.Kwa kauli hii ya huyu
mwanamke inaonekana
Devotha anawafahamu watu
hao waliotoka Tel
aviv.Tunatakiwa
kumfahamu huyo Dr Nathan
kabla ya kuwafahamu watu
hao waliotoka Tel Aviv wana
mahusiano gani na Devotha”
akasema Mathew
“Ruby was here and I
hope she heard everything”
akasema Mathew na kutoka
mle ndani Gosu Gosu
akamfuata nyuma
wakaelekea katika chumba
alimo lala Ruby.Dr Hiran
alikuwa na sindano mkononi
akitaka kumchoma Ruby
“Dr Hiran subiri
kidogo.Nahitaji kuzungumza
naye kuna jambo la muhimu
mno” akasema Mathew na
kuwafanyia ishara Dr Hiran
na Gosu Gosu watoke mle
ndani.Mathew akakaa katika
kitanda cha Ruby
“Ruby nimekuja tena
kuomba msaada
wako.Nataka unieleze kila
kitu ulichokisikia
akikizungumza Devotha”
“Umezipata namba
alizopiga Devotha?
Umetumia zile namba
nilizokupa?
“Ndiyo Ruby na ndiyo
maana nimerudi tena
kwako.Nimetumia zile
namba na tumegundua ni
namba za utambulisho za
Devotha.Baada ya muda
tukapewa jibu kwamba Dr
Yonathan hawezi
kuzungumza na Devotha
kwa sasa yuko kwenye kikao
na wageni wale kutoka Tel
Aviv.Tunataka kumfahamu
huyu Dr Yonathan ni nani?
Nini ulisikia
wakizungumza?akauliza
Mathew.Ruby akafumba
macho
“Ruby ! akaita Mathew
kwa sauti ndogo
“Baada ya kutaja zile
namba nilimsikia Devotha
akizungumza na Dr
Yonathan na ilionekana
kama vile huyo Dr Yonathan
alimtaka Devotha waonane
usiku huu na nikamsikia
Devotha akimjibu kwamba
atafika ubalozini muda si
mrefu.Niliishia kusikiliza
hapo kwani alihisi
ninamsikiliza nikaondoka”
“Kwa maelezo haya
uliyoyasikia inaonekana
kama vile huyu Dr Yonathan
ni mtu mwenye wadhifa na
yupo katika ubalozi Fulani
hapa Tanzania.Inawezekana
huyo Dr Yonathan akawa ni
balozi” akasema Mathew na
kusimama
“Ruby thank you.Endelea
kupumzika” akasema
Mathew na kutoka mle ndani
haraka akamtaka Gosu Gosu
warejee katika ofisi yao
akamueleza kila kitu
alichoelezwa na Ruby
“Gosu Gosu nahisi huyu
Dr Yonathan akawa ni
balozi.Njia rahisi ya kuupata
ukweli ni kutafuta
mtandaoni” akasema
Mathew na kukaa katika
kompyuta akaingia
mtandaoni na kutafuta
orodha ya mabalozi wote
wanaoziwakilisha nchi zao
nchini Tanzania.Mara
akastuka baada ya kuliona
jina Dr Yonathan Cohen
akiwa ni balozi wa Israel
hapa Tanzania
“Israel !! akasema
Mathew kwa mshangao
“Devotha ana mahusiano
na Israel na mtu aliyekuwa
anazungumza naye Dr
Yonathan Cohen ni balozi wa
Israel hapa nchini.”
“Cette affaire deviant
plus belle et plus
grande”akasema Gosu Gosu
kwa sauti ndogo kwa lugha
ya kifaransa akimaanisha
suala hili linazidi kuwa
kubwa
“Kuna ushirikiano gani
kati ya Devotha na balozi wa
Israel hapa nchini? Kadiri
tunavyoendelea na hili suala
ndivyo tunavyozidi
kuchimbua mambo
zaidi.Mwanzo ilikuwa Olivia
na IS sasa ni Devotha na
Israel”akasema Mathew
“Tunafanya nini
Mathew?akauliza Gosu Gosu
“Kitu pekee cha kufanya
hapa ni kumfuata balozi Dr
Yonathan.Ni yeye pekee
mwenye kuweza kutusaidia
kumpata Devotha na vile vile
atatueleza kinachoendelea
kati ya ubalozi wake na
Devotha hadi wakutane
usiku huu tena kwa
mawasiliano
maalum”akasema Mathew
akainamisha kichwa
akafikiri kidogo na kusema
“Gosu Gosu I have to be
honest with you brother”
akasema Mathew na
kumtazama Gosu Gosu
“Tunachoenda kukifanya
ni kitu cha hatari kubwa na
kinaweza kusababisha hata
mvutano mkubwa baina ya
nchi hizi mbili lakini pamoja
na hatari yake bado ni jambo
la muhimu sana ambalo
lazima
tulifanye.Ninakutegemea
sana lakini kama haujisikii
kushiriki katika operesheni
hii you can stay I’ll go there
alone I’m not
scared”akasema Mathew
“Mathew I’m a
soldier.Nimekuwa napigana
vita toka nikiwa
mdogo.Muziki niliouzoea
masikioni mwangu ni milio
ya risasi na mabomu.Hivyo
basi siogopi na sintoogopa
chochote.Nitume kokote
nitaenda.Hata kama
nitashindwa kupita lakini
nitakufa nikijaribu.I’m with
you Mathew.This is our
country and this is our
war.We must fight” akasema
Gosu Gosu
“Thank you Gosu
Gosu.Tunachokihitaji sasa ni
silaha kwani balozi Yule
analindwa na ulinzi
mkali”akasema Mathew na
kunyamaza kidogo halafu
akasema
“I know where we can get
weapons.Tujiandae
tuondoke” akasema Mathew
na kurejea katika chumba
alimo Ruby ambaye tayari
alikuwa amelala Mathew
akambusu katika paji la uso
“You’ll be safe Ruby”
akasema na kumuaga Dr
Hiran wakaondoka
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 10
Baada ya kutoka
nyumbani kwao Kaiza
alielekea moja kwa moja
nyumbani kwa Devotha
ambaye aliwapokea na
kuwakaribisha ndani
“Karibuni
sana.Sikutegemea kuwaona
hapa usiku huu” akasema
Devotha na kustuka baada
ya kuziona sura za akina
Kaiza zikiwa zimejaa
wasiwasi mkubwa
“Nini
kimetokea?akauliza.
Kaiza akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Ulikuwa sahihi
Devotha”
“Kuhusu nini?
“Kuhusu Mathew
Mulumbi.Ni kweli amevamia
nyumbani kwangu usiku huu
akiitafuta familia yangu”
Kaiza akamueleza kila kitu
kilichotokea na namna
walivyoweza kujiokoa.
“Poleni sana”akasema
Devotha
“Devotha nimeamua
kuileta familia yangu hapa
nikiamini ni sehemu
salama.Nina uhakika
mkubwa lazima Mathew
atarajea tena.Pale nyumbani
kwangu si salama tena kwa
familia yangu kuwepo”
akasema Kaiza
“Usihofu Kaiza hapa ni
nyumbani kwako na familia
yako watakuwa salama”
akasema Devotha na
kuwataka wamfuate akaenda
kuwaonyesha chumba cha
kulala.Nyumba ile ya
Devotha ilikuwa na vyumba
vya kutosha vya
kulala.Devotha na Kaiza
wakaenda sebuleni
kuzungumza
“Kaiza usihofu tena
familia yako iko
salama.Mathew hapafahamu
mahala hapa” akasema
Devotha
“Nashukuru sana
Devotha.Utanisamehe kwa
maneno yale yote machafu
niliyokutamkia sikuwa
nikielewa chochote”
“Kaiza tuyaweke
pembeni yote yaliyotokea na
tujielekeze katika suala moja
la muhimu sana ambalo ni
kumpata Olivia” akasema
Devotha
“Devotha Olivia
amechukuliwa na rais kama
nilivyokueleza”akasema
Kaiza
“Kaiza we must find
her.Kwa namna yoyote ile
lazima tumpate Olivia.Ni
muhimu sana” akasema
Devotha
“Nafahamu umuhimu wa
kumpata Olivia lakini namna
ya kumpata ndiyo
changamoto”
“Sikiliza Kaiza kwa sasa
una ukaribu na Rais.Mpigie
simu na muulize kama Olivia
amefika salama na muulize
saa ngapi atarejeshwa ili
tupate walau picha ya
kinachoendelea kati yake na
Olivia” akasema
Devotha.Kaiza akafikiri
kidogo halafu akatoa simu
yake ambayo huitumia kwa
mawasiliano na Rais
akampigia
“Kaiza kunani usiku
huu?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
samahani kwa usumbufu
lakini ninataka kufahamu
kama Olivia amefikiswa
salama”
“Usijali amefika salama”
akajibu Dr Evans kwa ufupi
“Mheshimiwa Rais
ninataka kufahamu vile vile
atarudi saa ngapi kwani niko
na timu yangu tunamsubiri
ili tuendeleze mahojiano
naye” akasema Kaiza
“Kaiza nitakujulisha
atakapokuwa tayari kurejea
kwenu lakini kwa sasa
endeleeni na operesheni
nyingine ya kuwatafuta
Devotha na Mathew
Mulumbi” akasema Dr Evans
na ukimya mdogo ukapita
“Kaiza kuna
lingine?akauliza Dr Evans
“Hakuna mheshimiwa
Rais ni hayo tu niliyotaka
kuyafahamu” akasema Kaiza
“Basi wekezeni nguvu
kubwa katika kuwatafuta
Devotha na Mathew”
akasema Dr Evans na
kukata simu.Kaiza
akashusha pumzi
“Umesikia jibu
alilolitoa.Atanijulisha pale
Olivia atakapokuwa tayari
kurejea kwetu” akasema
Kaiza
“Maneno haya ya Rais
yanatoa picha ya wazi
kwamba Olivia hatarejea
tena.Tutafute namna
nyingine ya kujua mahala
alipo” akasema Devotha
“Devotha ushauri wangu
mimi tuachane na hili suala
litatuweka katika matatizo
makubwa”
“Usiwe muoga Kaiza.Hii
ni kazi yetu kuhakikisha
nchi inakuwa salama hivyo
lazima tuhakikishe kwa kila
namna Olivia anapatikana”
akasema Devotha
“Hilo nalifahamu
Devotha lakini ugumu ni
namna ya kumpata Olivia”
“Kuna njia moja tu ya
kuweza kufahamu mahala
alipo Olivia nayo ni
kumchunguza Rais”
“Una maana kudukua
mawasiliano yake?akauliza
Kaiza kwa wasi wasi na
Devotha akatingisha kichwa
kukubaliana naye
“Hapana
Devotha.Hatuwezi kufanya
hivyo hilo ni jambo la hatari
kubwa sana.Tazama
kilichokutokea wewe
ulipojaribu kudukua simu ya
rais.Sitaki jambo hilo
linitokee na mimi pia”
akasema Kaiza
“Kaiza hatuna namna
nyingine ya kufanya.Kama
tunataka kufahamu mipango
yote ya IS hapa nchini na
kama tunataka kuzuia
mashambulio mengine
yaliyopangwa na IS basi ni
lazima tumpate Olivia.Mtu
pekee ambaye anafahamu
mahala alipo Olivia ni Rais
hivyo lazima tutafute kila
mbinu kuhakikisha tunapata
taarifa kutoka kwake za
mahala alipo Olivia.”
akasema Devotha na
kunyamaza akamtazama
Kaiza ambaye alikuwa na
wasi wasi mwingi
“Kaiza hili ni suala dogo
ambalo haliwezi
kutushinda.Tumesoma na
tunazifahamu mbinu mbali
mbali hivyo lazima
tuhakikishe tunafahamu
alipo Olivia.Are you with me
or not?akauliza Devotha
“I don’t know
Devotha.Rais ni mtu mwenye
nguvu kubwa na sitaki
kuingia katika mgogoro
naye.Unafahamu amri
aliyoitoa kuhusu wewe na
Mathew Mulumbi.Shoot to
kill !! akasema Kaiza kisha
wakatazamana
“Uko hai mpaka sasa
kwa sababu nimetaka iwe
hivyo na hiki nilichokifanya
ni usaliti mkubwa kwa Rais
na akigundua kwamba nina
shirikiana nawe hata mimi
nitakuwa katika matatizo
makubwa.Devotha naomba
tusiingie tena katika
matatizo na Rais.Kama ni
kumtafuta Olivia tutafute
namna nyingine ya kuweza
kumpata lakini si kwa
kudukua mawasiliano ya
Rais ni hatari sana” akasema
Kaiza
“Niambie ni njia ipi
unadhani inaweza
kutusaidia kumpata
Olivia?akauliza Devotha
Kaiza akabaki kimya
“Niambie Kaiza kama
kuna njia yoyote unaifahamu
inayoweza kutusadia
kumpata Olivia” akasema
Devotha akionekana kuanza
kukasirika
“Tell me ?! akauliza Kwa
ukali
“Devotha wewe ni mtu
mwenye akili nyingi na
unazo mbinu nyingi
ninaamini hujaishiwa mbinu
nyingine ya kufanya ili
kufahamu mahala alipo
Olivia zaidi ya hii ya
kudukua simu ya
Rais.Tafuta mbinu nyingine
Devotha na mimi nitakuwa
nyuma yako” akasema Kaiza
“Kaiza hadi nimefikia
maamuzi haya ni kwamba
tayari nimekwisha tafuta
kila namna ya mbinu
nimekosa” akajibu Devotha.
“Hata kama ukisema
tudukue simu ya Rais how
are we going to do
it?Tulikuwa na mtu mmoja
tu ambaye alikuwa na ujuzi
na uwezo mkubwa katika
udukuaji ambaye tayari
amekwisha fariki.Devotha
huu mpango umekwisha
kwama tutafute namna
nyingine” akasema Kaiza
“Aaaagghhh ! akasema
Devotha kwa hasira
“Kaiza unaniudhi
unavyonikatisha tamaa!!
“Sikukatishi tamaa
Devotha ninazungumza
uhalisia.Ni wazi mpango huu
hauwezekani kabisa”
akasema Kaiza.
“Hapana Kaiza.Siwezi
kukubali kushindwa kirahisi
namna hiyo.Sijawahi kukata
tamaa katika maisha
yangu.Nitapata mbinu
nyingine ya kufahamu
mahala alipo Olivia.Nahitaji
kumfahamu mtu aliyekuja
kumchukua Olivia pale
Kitalu 2”
“What?akauliza Kaiza
“Ulikuwepo kitalu 2
alipokuja Yule jamaa
aliyetumwa na Rais
kumchukua Olivia.Nahitaji
kumfahamu mtu
huyo.Elekeza watu wako
wakutumie kumbu kumbu za
kamera za kitalu 2” akasema
Devotha
“Devotha ndiyo maana
nikakwambia kwamba huu
mpango hauwezekani kwani
wewe na watu wako
mliharibu mfumo wetu wote
wa kuhifadhi kumbu kumbu
za kamera kutoka katika
vitalu vyetu hivyo basi
hakuna kumbu kumbu
yoyote tunayoweza kuipata”
akasema Kaiza na Devotha
akamtazama kwa hasira
“Kaiza naona unajaribu
kufanya kila uwezalo
kuhakikisha mpango wangu
haufanikiwi.Why are you
doing this to me?akauliza
Devotha
“Devotha usinielewe
vibaya lakini ninajaribu
kukueleza kitu cha
kweli.Tukubali kwamba
suala hili la Olivia liko nje ya
mikono yetu kwa sasa hivyo
tujielekeze katika mambo
mengine.Nadhani suala la
msingi kwa sasa ni kuanza
kutafuta namna ya
kuhakikisha unakuwa
salama.Ushauri wangu ni
kuondoka hapa nchini
haraka.Devotha Rais ana
hasira kubwa na wewe na
anaisaka roho yako sana
hivyo njia pekee ya wewe
kuendelea kuwa salama ni
kuachana na suala hili la
Olivia na kuondoka
nchini.Nitakusaidia katika
hilo.Nenda ukakae nje ya
nchi kwa muda halafu
utarejea hapo baadae wakati
Rais amekwisha maliza
muda wake.Ninas……”
“Kaiza !! akasema
Devotha kwa hasira na Kaiza
akanyamaza
“Kaiza unanifahamu
vyema mimi ni mtu wa aina
gani pale
ninapokasirika.Umenikasiris
ha sana Kaiza sikutegemea
kabisa kusikia maneno hayo
kutoka kwako.Bahati yako
mkeo na watoto wako hapa
lakini ningeweza kukifumua
kichwa chako kwa risasi sasa
hivi !
“Devotha nilichokueleza
ni kitu cha ukweli
kabisa.Nataka nikusaidie
kuondoka hapa nchini wakati
bado ninao uwezo kwani
sifahamu nini kitatokea
kesho.Wewe ni rafiki yangu
kubali nikusaidie” akasema
Kaiza.Devotha akamtazama
kwa macho yaliyojaa hasira
na kusema
“Go to hell you witch !
akasema huku akianza
kupiga hatua halafu
akageuka
“Sikufahamu kama u
mwoga kiasi
hiki.Nitakuonyesha nguvu
yangu.Utaiona nguvu ya
mwanamke” akasema
Devotha na kupanda ngazi
kuelekea chumbani kwake
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 7
EPISODE 11
Mathew na Gosu Gosu
walifika eneo la Manziki.
“Sijawahi kufika eneo
hili.Kunaitwaje
huku?akauliza Gosu Gosu
“Kunaitwa Manziki”
akajibu Mathew na
kusimamisha gari nje ya
nyumba moja kubwa ambayo
ujenzi wake ulikuwa
unaendelea.
“Nani anaishi
hapa?akauliza Gosu Gosu
“A friend of mine”
akajibu Mathew na
kuchukua simu akampigia
Tino
“Mathew” akasema Tino
baada ya kupokea simu
“Tino samahani sana
kwa usumbufu usiku
huu.Nina shida kubwa kaka”
akasema Mathew ukapita
ukimya Tino akasema
“Uko wapi Mathew”
“Niko hapa nje ya
nyumba yako?
“C’mo Mathew acha
utani”
“Seriously niko hapa nje”
akasema Mathew.Baada ya
dakika tatu mlango
ukafunguliwa akatoka
Tino.Mathew akafungua
mlango wa gari
akashuka.Tino akamfuata.
“Mathew ni mara ngapi
unataka nikuonye kuhusu
namna unavyokuja kwangu?
Nimekwisha kueleza
kwamba sipendi njia
unayotumia kuja kwangu !
akasema Tino akionekana
kutokufurahishwa na ujio ule
wa Mathew
“Ninafahamu Tino lakini
nina shida na sina namna
nyingine ya kufanya ni
kwako pekee ninakoweza
kupata msaada.Tafadhali
usinifungie milango Tino
nimekwama na ninahitaji
sana msaada wako” akasema
Mathew.Tino akamtazama
na mara mlango wa gari
ukafunguliwa akashuka
Gosu Gosu.Tino akamtazama
Mathew kwa hasira
“Who is he?akauliza
“Niko naye.Anaitwa Gosu
Gosu”akajibu Mathew.
“Come inside” akasema
Tino wakaingia ndani
“What do you
want?akauliza Tino
“Nahitaji silaha”akajibu
Mathew kwa ufupi
“Bado hujafanikiwa
kumpata Yule mtu
wako?akauliza Tino
“Mpaka sasa sijafanikiwa
kumpata.Jambo hili
limekuwa kubwa tofauti na
nilivyodhani.” akasema
Mathew.
“Kama mpaka sasa
hujafanikiwa kumpata
mpenzio basi suala hili ni
kubwa.Ninavyokufahamu
Mathew Mulumbi ukisema
suala ni kubwa basi ni
kubwa kweli.Anyway
unahitaji silaha zipi?akauliza
Tino
“Nipeleke kwenye
chumba cha silaha
nikachague” akasema
Mathew na Tino akainuka
wakamfuata hadi katika
chumba anakohifadhi silaha
zile nyeti kabisa anazoziuza
kwa magenge ya waalifu nje
ya nchi.Gosu Gosu
akatabasamu baada ya
kuingia ndani ya kile
chumba wakachagua silaha
na vifaa wanavyovihitaji
“Mathew chukua kila
unachokihitaji sitaki uje tena
hapa.Wewe ni mtu mwenye
maadui wengi na hujui kwa
sasa nani anakufuatulia
hivyo kuja kuja hapa
kunaweza kuniletea hata
mimi matatizo.Ukiwa na
tatizo ni bora ukanipigia
simu kuliko kunifuata
nyumbani” akasema Tino.
“Nimekuelewa
kaka.nashukuru sana kwa
msaada huu mkubwa”
akasema Mathew huku
akisimama Tino akamtaka
aketi
“Nini hasa
kinachoendelea huko na
kusababisha hadi sasa
ushindwe kumpata huyo mtu
wako?akauliza Tino.
“Tino suala hili ni pana
sana na nikianza kukueleza
litachukua muda mrefu
kidogo.Kuna sehemu
muhimu tunakwenda usiku
huu na nikipata nafasi
nitakuja kukueleza kila kitu”
“Mathew nimeuliza ili
nipate picha ya namna suala
hili linavyokwenda and may
be I can help” akasema
“Tatizo ni kwamba suala
hili hadi serikali wana
mkono wake na si serikali tu
hata nchi za nje nao wana
mkono wao katika jambo
hili.Kwa mfano tukitoka
hapa tunakwenda kuvamia
makazi ya balozi wa Israel
hapa nchini.Kuna mtu
muhimu sana ambaye
tunamtafuta.Nadhani hadi
hapo umekwisha pata picha
namna suala hili lilivyo
kubwa” akasema Mathew
“How many are
you?akauliza Tino
“ Just the two of us”
akajibu Mathew
“Only you two?akauliza
Tino na kutoa kicheko kidogo
“Mathew usinifanye
nicheke.Ninyi wawili pekee
mnataka kwenda kuvamia
makazi ya balozi wa
Israel?akauliza Tino
“Kaka unaonekana tayari
umekwisha nisahau mimi ni
nani.Ukiacha uwezo wangu
ninaye Papii Gosu Gosu
ambaye ni sawa na jeshi la
mtu mmoja” akasema
Mathew.Tino akafikiri kidogo
na kusema
“I’m coming with you”
akasema
“Tino hapana.Huko
tuendako ni hatari
sana.Please stay ! akasema
Mathew
“Mathew wewe ni rafiki
yangu siwezi
kukuacha.Nitakuunga
mkono”
“Tin….”
“Don’t say anything
Mathew.Tunakwenda wote”
akasema Tino na kuelekea
chumbani kwake
“Tino aliwahi kuwa
komandoo jeshini alifukuzwa
kazi baada ya kufanya
vurugu kubwa za kupiga
watu na toka wakati huo
amekuwa akijishughulisha
na biashara ya silaha.Si
biashara halali lakini ni mtu
anayefahamika na kila mkuu
wa chombo cha usalama.Ni
mtu ambaye anawasaidia
kupata taarifa nyingi za
kiusalama kwa sababu
anafahamiana na wahalifu
wengi wa ndani na nje ya
nchi.Kila linapotokea tukio
kubwa la uhalifu hapa nchini
Tino huwa wa kwanza
kuulizwa kama
anawafahamu waliofanya
uhalifu huo.Amekuwa ni
chanzo kikubwa cha taarifa
kwa vyombo vya usalama.”
Mathew akamweleza Gosu
Gosu
“Kwa jeshi hili la watu
watatu tunaweza hata
kupindua nchi”akasema
Gosu Gosu na kuta kicheko
kidogo.Tino akatokea akiwa
amevaa tayari kuingia katika
mapambano.
“I’m ready” akasema Tino
na kuzunguka nyuma ya
nyumba na kutoa gari dogo
lenye muundo wa
basi.Wakaingiza silaha zao
katika gari lile kisha
wakaondoka.
Walikaribia kufika eneo
la Kilimani kilipo kijiji cha
mabalozi wanaoziwakilisha
nchi zao hapa nchini.Tino
akasimamisha gari
“Mlikuwa mmepanga
kuingia vipi katika nyumba
ya balozi wa Israel?akauliza
Tino
“Tukifika
tutajitambulisha kama
mafundi wa kutengeneza
viyoyozi.Tutadai tumepigiwa
simu kuna shida ya viyoyozi
katika nyumba ya
balozi.Lengo ni kutafuta
nafasi ya kuwadhibiti walinzi
ili tuweze kuvuka kuingia
ndani.Please don’t kill the
cops” akasema Mathew.
“What if they….”
Akataka kusema kitu
Tino,Mathew akamzuia
“We’re killing only
terrorists not cops.Polisi
wanafanya kazi kubwa ya
kujitolea kulinda maisha ya
watu we have to respect
them.Ni wenzetu katika
ulinzi wa taifa hivyo
tutawadhibiti kwa muda ili
kupata nafasi ya kuingia
ndani.Are we clear?akauliza
Mathew
“Hakuna tatizo” akasema
Gosu Gosu.
“Tino are we
clear?akauliza Mathew
“We’re clear” akajibu
Tino
“Good” akasema Mathew
“Gari langu hili
limekamilika ni maalum kwa
operesheni kama hizi.Lina
vifaa vyote vya
ujasusi.Naamini lazima kuna
kamera za ulinzi zimefungwa
huko t uendako hivyo
nitazima zote kama zipo ili
wasiweze kufuatilia na
kufahamu ni akina nani
waliofanya uvamizi huu”
akasema Tino.
“Good.Kila kitu kiwekwe
tayari” akasema Mathew na
gari likawashwa safari
ikaendelea.Walikuta bango
kubwa likiwa na maandishi
kijiji cha mabalozi.
“Tumekaribia ni kilometa
moja kutoka hapa” akasema
Mathew.
Kwa mbali wakaliona
geti na mara wakajitokeza
watu wawili wakiwa na tochi
kubwa zenye mwanga mkali
wakamulika gari like na Tino
aliyekuwa katika usukani
akapunguza mwanga wa
taa.Gosu Gosu akachukua
hadubini na kutazama
“Nimeona askari polisi
wanne.Wawili wana
silaha.Vile vile kuna mbwa
mmoja.Inaonekana kuna geti
kabla ya kuvuka kwenda
katika nyumba za
mabalozi”akasema Gosu
Gosu
“Damn it.Nimewahi
kufika hapa muda mrefu
kidogo na wakati huo
hakukuwa na geti.Nilijua
tunavuka moja kwa moja
kwenda katika nyumba ya
balozi.Hata hivyo
hakijaharibika kitu tutavuka
lazima tufike nyumbani kwa
balozi” akasema Mathew.
Askari mmoja
akanyoosha mkono kumtaka
dereva asimamishe gari.
“Get ready” akasema
Mathew huku wakiwasoma
wale askari namna
walivyokaa.Tino
akasimamisha gari na
kushusha kioo.Askari
aliyekuwa amemshika mbwa
akasogelea gari na mmoja
akasogelea kioo
“Wakuu habari zenu”
akasema Tino
“Mnaelekea wapi usiku
huu?akauliza askari
aliyesogea dirishani
“Tunaelekea kwa balozi
wa Israel.Tumetoka kampuni
ya kurekebisha
viyoyozi.Tumepigiwa simu
kwamba kuna shida katika
nyumba ya balozi viyoyozi
vyote havifanyi kazi”
“Mmeitwa na
balozi?Mbona hajatupa
taarifa zozote kama kuna
watu watakuja usiku
huu?Utaratibu wa hapa
kama balozi ana wageni
wake hutoa taarifa kwetu ili
tuwaruhusu wageni wake”
“Nimekuelewa afande
nadhani ni yeye mwenyewe
amekosea ngoja nimpigie
simu nimjulishe kwamba
tayari tuko hapa” akasema
Tino na mbwa akaanza
kubweka.
“Kuna nini ndani ya
gari?akauliza Yule askari
“Ni vifaa vya
matengenezo” akajibu Tino
“Shukeni wote ndani ya
gari” akasema Yule
askari.Alikosea sana
kuwataka akina Mathew
washuke garini.Kufumba na
kufumbua Tino aliupiga teke
mlango ule ukampiga askari
Yule aliyekuwa akimuhoji
akaanguka chini.Mathew na
Gosu Gosu wakaufungua
mlango mkubwa kama
umeme wakaruka nje
wakiwa na silaha.Tino
akaruka nje na kumuwahi
Yule askari aliyepigwa na
mlango na kumkaba
kabali.Lilikuwa ni tukio
lililotokea kwa ghafla mno na
ambalo askari wale
hawakuwa wamelitegemea
“Wekeni silaha zenu
chini!! Akaamuru Mathew.
“Hatuhitaji kuua askari
yeyote.Tafadhali wekeni
silaha zenu chini haraka
sana!! Akafoka
Mathew.Mmoja wa askari
aliyekuwa na silaha
akaiweka chini na mwingine
naye akafanya vile vile.Gosu
Gosu akatoa pingu katika
sanduku lao la silaha pamoja
na kamba akawafunga askari
wale na kuwaziba midomo
wasiweze kupiga kelele kisha
wakafungua geti na
kuwaficha katika kichaka
cha maua kilichokuwa karibu
na geti mbwa akafungwa
katika mti kisha wakaingia
garini na kuingia katika kijiji
cha mabalozi.Kulikuwa na
vibao vilivyoelekeza kila
nyumba ya balozi wakafuata
kibao kilichoelekeza ilipo
nyumba ya balozi wa
Israel.Kulikuwa na askari
mmoja katika geti la
nyumba ya balozi
akalisimamisha gari .Tino
akasimamisha gari na
kushusha kioo
“Habari yako Afande”
akasema
“Nzuri habari yako”
“Sisi ni mafundi wa
viyoyozi tumekuja hapa mara
moja baada ya kupigiwa
simu na balozi”
“Mmepigiwa simu na
balozi?Mbona hajanijulisha
chochote?
“Tayari amekisha
wasiliana na geti kubwa
ndiyo maana wakaturuhusu
kupita”
Wakati Tino
akizungumza na Yule askari
Gosu Gosu alitoka garini
taratibu kwa kutumia kioo
cha upande wa pili na
kuingia chini ya uvungu wa
gari.Miguu yake yenye nguvu
mithili ya chuma ikamkata
mtama askari Yule
akaanguka na kabla hajajua
kilichomuangusha tayari
Mathew alikwisha ruka nje
“Usithubutu kupiga
kelele” akasema Mathew na
kuchukua silaha yake.Gosu
Gosu akamuinua na
kumtandika kichwa kizito
akapoteza fahamu.
“Good job Gosu Gosu”
akasema Mathew
wakampakia Yule askari
katika gari lao.Tino akatoka
katika kiti cha dereva
akachukua kamera ndogo ya
kuruka juu akairusha huku
akiifuatilia katika kompyuta
yake.Aliizungusha kamera
ile katika nyumba yote na
kugundua kulikuwa na
kamera nne za ulinzi katika
kile upande wa nyumba.
“Tayari nimekwisha
ziona ni kamera za aina
gani” akasema Tino na
kuanza kucheza na
kompyuta yake na baada ya
muda akasema
“We can go now.Kamera
zote zimezima” akasema
Kila mmoja akachukua
silaha yake na vifaa,Gosu
Gosu akawa wa kwanza
kupanda geti akaingia ndani
na kulifungua Mathew na
Tino wakaingia kisha
wakanyata kuelekea katika
mlango.Kulikuwa na gari
mbili katika banda la
kuhifadhia magari.
Katika mlango kulikuwa
na kifaa maalum kwa ajili ya
kupiga kelele pale mlango
unapokuwa
umefunguliwa.Mathew
akatoa kifaa Fulani kidogo
katika begi na kukibandika
mlangoni akabonyeza namba
Fulani halafu akachukua
vifaa vingine na kuchokonoa
kitasa mlango ukafunguka
na kifaa kile hakikutoa sauti
yoyote wakaingia ndani.Taa
zilikuwa zimezimwa ndani
kulikuwa na mwangaza
hafifu uliotoka katika taa za
nje.
Walitembea kwa kunyata
wakikitafuta chumba cha
balozi.Kulikuwa na ukimya
mkubwa katika nyumba
hii.Katika moja wapo ya
chumba walichofunga
wakamkuta msichana mmoja
akiwa amelala akataka
kupiga kelele Gosu Gosu
akamuwahi na kumziba
mdogo
“Usipige kelele
hatutakudhuru”akasema
Mathew
“Tuonyeshe chumba cha
balozi” akasema Mathew
.Gosu Gosu akamuinua Yule
msichana huku akiwa
amemziba mdomo
akawaongoza hadi katika
chumba cha balozi Dr
Yonathan Cohen.Mathew
akatumia vifaa vyake
akachokonoa kitasa cha
mlango wa chumba cha
balozi kikafunguka
akakinyoga taratibu na
kuingia ndani.Sauti ya
mlango kufungulia ikamstua
Dr Yonathan aliyekuwa
amelala kitandani na mke
wake akawasha taa
iliyokuwa pembeni ya
kitanda na moyo ulitaka
kumpasuka baada ya
kuwaona watu wenye silaha
wakiwa wameingia mle
chumbani.
“Amkeni haraka sana!!
Akaamuru Mathew.Dr
Yonathan huku akitetemeka
akamuasha mke wake.
“Ninyi ni akina
nani?Mnataka
nini?Mmewez……” Dr
Yonathan aliuliza maswali
lakini Mathew akamtaka
anyamaze na kumuelekeza
Gosu Gosu awafunge kamba
“Nini mnahitaji kutoka
kwetu?Niambieni tafadhali
nitawapatia chochote”
akasema Dr Yonathan.Mke
wake alikuwa analia
“Balozi muda wetu ni
mdogo sana wa kuwepo
hapa.Tunachohitaji kutoka
kwako ni ukweli.Endapo
utatupa ukweli wa kile
tunachokihitaji wewe na mke
wako mtakuwa salama lakini
endapo utaamua
kutudanganya basi wewe na
mke wako safari yenu ya
maisha itaishia
hapa.Tutawaua.Umenielewa
?akauliza Mathew
“Mnahitaji kufahamu
nini?Chochote mnachokitaka
nitawaeleza tafadhali
msituue”akasema balozi
“Usiku wa leo
umewasiliana na mwanamke
mmoja anaitwa Devotha
ambaye namba yake ya
utambulisho ni BRAVO 15E
361 A” Sura ya balozi Dr
Yonathan ilibadilika
alipomsikia Mathew
akitamka namba zile za
utambulisho za
Devotha.Mathew akauona
mstuko ule wa balozi halafu
akaendelea
“Nataka kufahamu
kilichowakutanisha usiku
huu na vile vile nataka kujua
mahala alipo” akasema
Mathew.Balozi Dr Yonathan
alikuwa anatetemeka
“Umeulizwa swali jibu
haraka sana! Akasema Gosu
Gosu aliyekuwa nyuma ya
balozi na kumsindikiza na
kofi zito la shingo balozi
akaanguka chini.
“Balozi hatuna haja ya
kuwaumiza au hata kuwatoa
uhai lakini mkitulazimisha
tufanye hivyo hatutasita
kuwatoa roho zenu hapa
hapa.Utakapotupa majibu
tunayohitaji tutawaacha
mkiwa salama salimini”
akasema Mathew
“Simfahamu mtu
anayeitwa Devotha” akasema
Dr Yonathan na sura ya
Mathew ikabadilika
“Humfahamu Devotha?
“Ndiyo simfahamu mtu
huyo.Kama kuna mtu
aliyewaambia kwamba
nimeonana naye
amewadanganya.Simjui na
sijawahi kukutana naye”
akasema Dr Yonathan
` “Dr Yonathan
ninafahamu kila
kitu.Umekutana na Devotha
usiku huu ubalozini
kwako.Nakuuliza kwa mara
ya mwisho nini
kilichowakutanisha usiku
huu? Yuko wapi hivi
sasa?akauliza Mathew
“Simfahamu mtu
huyo.Mmekosea kuja
kwangu mimi sina
mahusiano yopyote na huyo
Devotha.Kwanza ni nani
huyo mwanamke?akauliza
Dr Yonathan.Mathew
akamtazama kwa macho
yaliyojaa hasira halafu
akasema
“Dr Yonathan kwa mara
ya mwisho kabisa naomba
unieleze ukweli wa kile
nilichokuuliza.Sitaki
nikutendee ubaya wowote
ule.Nipe majibu ya kile
ninachokitaka na
ninakuahidi nitakuacha hai
wewe na mke wako” akasema
Mathew
“Vijana nawaeleza ukweli
mtupu simfahamu huyo
Devotha
mnayemzungumzia.Aliyewae
lekeza kwangu
amewadanganya” Dr
Yonathan akaendelea
kusisitiza
` “Gosu Gosu huyu mzee
bado hajatufahamu vyema
anatulazimisha kufanya kile
ambacho hatukuwa
tumekusudia kukifanya”
akasema Mathew na
kumuangalia tena Dr
Yonathan halafu
akamgeukia Gosu Gosu
“Ondoa kidole kimoja
kimoja katika mikono ya mke
wake hadi pale atakapokuwa
tayari kutupa majibu”
Mathew akasema na bila
kupoteza muda Gosu Gosu
akachomoa mkasi mdogo
mgumu katika mfuko wa
suruali.Dr Yonathan macho
yakamtoka.Alipatwa na woga
mkubwa.Bila huruma Gosu
Gosu akakishika kiganja cha
mkono wa mke wa Dr
Yonathan na kwa nguvu
akakikata kidole kimoja.Mke
wa Dr Yonathan akaanguka
chini akigala gala kwa
maumivu makali.Gosu Gosu
akachukua kitambaa na
kumfunga mdomoni asiweze
kutoa sauti.Dr Yonathan
akiwa amefungwa mikono
akapandwa na hasira
akataka kusimama kumvaa
Mathew lakini Tino tayari
alikwisha muona akamuwahi
kumtandika teke kali
akaanguka chini.
“Kwa nini mnatutenda
hivi?Kwa nini mnamtesa
mke wangu kiasi hiki nyie
wanyama?akauliza Dr
Yonathan huku akitetemeka
kwa hasira baada ya
kumuona namna mke wake
alivyokuwa anagala gala
chini kwa maumivu.
“Dr Yonathan sisi ni
wanyama sana kama
ulivyosema na hapa bado
haujauona unyama
wetu.Nakuhakikishia
kwamba tutamkata mke
wako kiungo kimoja kimoja
na atakata roho kwa mateso
makali sana huku
ukishuhudia.Nataka
uniambie uko tayari
kuzungumza au tuendelee na
zoezi letu?akauliza Mathew.
“Aaaagghh !! akasema
kwa hasira Dr Yonathan.
“Gosu Gosu endelea”
akasema Mathew na Gosu
Gosu akakishika kwa nguvu
kiganja cha mkono wa mke
wa Dr Yonatha na kukikata
kidole cha pili.Ni maumivu
makali sana aliyoyapata
mwanamama Yule lakini
sauti ya kilio cha uchungu
haikuweza kusikika kwa
kuwa alikuwa amefungwa
kitambaa mdomoni.
“Mashetani ninyi kwa
nini mnamtesa mwanamke
huyu asiye na kosa
lolote?Kama ni kunitesa
niteseni mimi.Kwa nini
mnakuwa wakatili kiasi
hiki?akauliza Dr Yonathan
kwa hasira huku
akimtazama mke wake
namna alivyokuwa
anagalagala kwa maumivu
makali.
“Uko tayari
kuzungumza? Akauliza
Mathew lakini bado Dr
Yonathan aliyaelekeza
macho yake kwa mke
wake.Gosu Gosu akamnasa
kofi kali
“Jibu ulichoulizwa !
akasema kwa ukali
“Dr Yonathan nakuuliza
kwa mara ya mwisho.Uko
tayari kuzungumza?akauliza
Mathew
“Tafadhali naombeni
mumuache mke wangu.Kwa
nini mnamtenda hivi?Nani
kawatuma mtufanyie
hivi?akauliza Dr
Yonathan.Mathew
akapandwa na hasira
akamfuata mke wa Dr
Yonathan akamuinua
akachomoa kisu na kukiweka
chini ya jicho.
“Ninaliondoa jicho la
mkeo kama hautakuwa
tayari kuzungumza!!
Akasema Mathew kwa ukali
na taratibu kisu kile
kikaanza kukata ngozi damu
ikaanza kuchuruzika
“Basi ! basi ! nitawaeleza
kila kitu.Tafadhali
msiendelee kumuumiza mke
wangu!! Akapiga kelele Dr
Yonathan.Mathew
akamsukuma mwanamama
Yule akaanguka chini halafu
akamfuata Dr Yonathan
“Haraka sana nieleze kila
kitu kuhusu Devotha.Kwa
nini mlikutana naye usiku
wa leo?akauliza Mathew
“Tafadhali naombeni
kwanza mumsaidie mke
wangu asiendelee kupoteza
damu” akasema Dr Yonathan
“Nieleze kwanza kile
ninachokitaka halafu
tutamshughulikia mke wako
kama ukishindwa kuwa
mkweli mkeo atapoteza
damu nyingi na atafariki
dunia huku ukishuhudia”
akasema Mathew.
“Tafadhali kuweni na
huruma.Nitawaeleza kila
kitu” akaomba Dr
Yonathan.Mathew
akamuelekeza Gosu Gosu
amuhudumie Yule mama.
“Wakati mke wako
anaendelea kupatiwa
matibabu kuzuia damu
kuendelea kumwagika
endelea kunipa maelezo!
Akasema Mathew.Dr
Yonathan akainama akafikiri
kwa sekunde kadhaa na
kusema
“Ni kweli nilikutana na
Devotha usiku huu baada ya
kuelekezwa kufanya hivyo na
makao makuu ya Mossad Tel
Aviv”akaanza kutoa maelezo
Dr Yonathan
“Devotha ana mahusiano
gani na Mossad?akauliza
Mathew
“Devotha ni wakala wa
Mossad kwa hapa Tanzania
na kila pale Mossad
wanapokuwa na jambo lao la
kufanya hapa Tanzania
humshirikisha yeye.Namba
ile uliyoitaja ndiyo namba
yake ya utambulisho”akajibu
Dr Yonathan
“Endelea” akasema
Mathew
“Mossad wanaandaa
operesheni hapa Tanzania
ndiyo maana nilimuhitaji
Devotha usiku huu ili aweze
kukutana na watu
waliotumwa na Mossad kuja
kuandaa operesheni
hiyo”akasema Dr Yonathan
na kugeuka kumtazama
mkewe ambaye alikuwa
anabubujikwa machozi
“Operesheni gani ambayo
Mossad wanaiandaa hapa
Tanzania? Mathew akauliza
“Mossad wanamtafuta
msichana mmoja ambaye
ametekwa siku chache
zilizopita na watu
wasiojulikana anaitwa Olivia
Themba.Wametuma watu
wao kuja kufanya uchunguzi
na kuandaa namna
operesheni hiyo
itakavyofanyika kabla ya
kutuma kikosi kuja
kumtafuta Olivia” akasema
Dr Yonathan
“Umesema Olivia
Themba?Mathew akauliza
“Ndiyo anaitwa Olivia
Themba”akajibu Dr
Yonathan
“Olivia Themba ana
mahusiano gani au ana
umuhimu gani kwa Mossad
hadi waandae operesheni ya
kuja kumtafuta?
“Sifahamu zaidi ya
hapo.Maagizo niliyopewa ni
kumtafuta Devotha na
kumkutanisha na majasusi
hao wa Mossad sifahamu
sababu ya kumtafuta Olivia”
“Dr Yonathan
tulikubaliana utatutueleza
ukweli wote lakini umevunja
makubaliano yetu na
umeniudhi.Nitakuomba kwa
mara ya mwisho unieleze
kila kitu kuhusiana na Olivia
na Mossad”
“Naomba mniamini
jamani hayo niliyowaeleza
ndiyo
ninayofahamu.Msiendelee
kututesa tafadhali sifahamu
zaidi ya hapo” akasema
balozi
“Balozi kwa kuwa
umevunja makubaliano yetu
nakuomba umuage mkeo
kwa mara ya mwisho”
akasema Mathew
“Tafadhali naomba
msimuue mke
wangu.Nimekwisha waeleza
kile mlichotaka kukifahamu
na sifahamu zaidi” akalia
machozi Dr Yonathan
“Tunaondoka na mke
wako na hautamuona tena
katika maisha yako.Naomba
umtazame mkeo kwa mara
ya mwisho na umuage”
akasema Mathew
“Jamani msitufanyie
hivi.Niko chini ya miguu
yenu nawaomba” akasema
Dr Yonathan huku akilia
machozi
“Gosu Gosu mfunge huyo
mwanamke tunaondoka
naye” akasema Mathew na
bila kupoteza muda Gosu
Gosu akamuinua mke wa Dr
Yonathan na kumuweka
begani.
“Kwa heri Dr Yonathan”
akasema Mathew na
kugeuka kuanza kuondoka
na alipofika mlangoni Dr
Yonathan ambaye mikono
yake ilikuwa bado
imefungwa kwa nyuma
akamuita
“Mrejesheni mke wangu
nitawaeleza kila kitu”
akasema Dr
Yonathan.Mathew akageuka
na kumtazama
“Hii ni nafasi ya mwisho
ninakupa !! akasema Mathew
na kumtaka Gosu Gosu
amrejeshe mke wa balozi
chumbani akambwaga
kitandani
“Hatuna muda wa
kupoteza balozi nieleze kila
kitu” akasema Mathew
“Ipo sababu kubwa
ambayo Mossad
wanamtafuta Olivia Themba”
akasema Dr Yonathan na
kuvuta pumzi ndefu halafu
akaendelea
“Miaka mitatu iliyopita
mtu mmoja aliyefahamika
kama Edger Kaka aliyewahi
kuwa mbunge wa bunge la
jamhuri ya muungano wa
Tanzania alipatwa na
ugonjwa wa ghafla akiwa
bungeni na kupelekwa Dar
es salaam katika hospitali
kuu ya moyo alikopokelewa
na Dr Olivia Themba na
baadae hali yake ilipozidi
kuwa mbaya Dr Olivia
akafanya mpango na Edger
akapelekwa nchini Israel
ambako iligundulika
kwamba alipewa sumu ili afe
na kitendo hicho kilimlazimu
waziri mkuu wa Tanzania
wakati huo atume mlinzi
maalum wa kwenda
kumlinda Edger kwa siri bila
yeye kujua kama
analindwa.Mlinzi huyo kwa
kushirikiana na mmoja wa
majasusi wa Mossad
waligundua kwamba
mwanamke mmoja
anayeitwa Habiba Jawad na
mtu mwingine anaitwa
Sayid Omar walifika
hospitali usiku kumtembelea
Edger.Watu hawa wawili
wanatajwa kuwa ni wafadhili
wakubwa wa kikundi cha IS
ambacho kwa kushirikiana
na vikundi vingine vidogo
vidogo vya wanamgambo
wamekuwa wakifanya
mashambulio katika ardhi ya
Israel na kuua
waisrael.Serikali ya Israel
imekuwa ikiwatafuta kwa
muda mrefu hasa Habiba
mwanamama tajiri bila
mafanikio.Mara moja ilianza
mipango ya kumpata Edger
ili aweze kusaidia kuwapata
Habiba na Sayid Omar na
ndipo ilipotengenezwa ajali
wakati Edger akirejea nchini
kutokea Israel na Mossad
wakafanikiwa kumchukua
Edger wakati huku Tanzania
ikiamini Edger alikufa
katika ile ajali”
“Edger kaka hajafariki
dunia?! Akauliza Mathew
kwa mshangao
“Edger yuko hai lakini hii
ni siri kubwa sana ya
Mossad” akajibu Dr
Yonathan
“Kumbe Olivia alikuwa
sahihi aliposisitiza kwamba
Edger hajafa” akawaza
Mathew
“Rais wa Tanzania
anahusika kwa namna
yoyote ile na ajali hiyo
iliyotengenezwa na
Mossad?Anafahamu
chochote?akauliza Mathew
“Ilikuwa ni operesheni ya
siri na ambayo serikali ya
Tanzania hawajui chochote
ndiyo maana mpaka sasa
wanaamini Edger alifariki
dunia.Rais wa Tanzania
hafahamu chochote”akasema
Dr Yonathan
“Kwa nini Mossad
wanamtafuta Olivia?
Mathew akauliza
“Kwa miaka mitatu
Edger kaka amewekwa
mafichoni akiteswa ili
kumfanya aweze kutoa siri
za maficho ya Habiba
Jawad.Kufuatia mfululizo wa
mauaji ya waisrael
yanayoendelea hivi sasa
kutoka kwa vikundi vya
wanamgambo wa kipalestina
majasusi wawili wametumwa
kumuhoji Edger Kaka ili
kufahamu namna ya
kumpata Habiba Jawad
lakini Edger aligoma kueleza
chochote hadi pale
atakapomuona Olivia mbele
ya macho yake.Amekiri
kwamba Olivia ndiye
mwanamke pekee
anayempenda kuliko wote
hivyo kama Mossad
wanataka awaeleze kila kitu
wanachokitaka yuko tayari
kuwaeleza lakini hadi
atakapomuona tena Olivia
ndiyo maana Mossad
wanataka kufanya
operesheni ya kumtafuta
Olivia.”
“Damn it ! akasema
Mathew na kugonganisha
mikono kwa hasira
“Tayari nimewaeleza kila
mnachokitaka naomba
mtimize ahadi yenu mtuache
huru” akasema Dr Yonathan
“Devotha yuko wapi?
“Sifahamu alipo kwa
sasa”
“Unafahamu namna ya
kumpata?
“Hap….Ndiyo ! akajibu
Dr Yonathan baada ya
kumuona namna Mathew
alivyokuwa amebadilika
“Katika mkono wake wa
kushoto Devotha ana
upungufu wa vidole viwili
hivyo huvaa glovu ambayo
imetengeneza maalum kama
chombo cha
mawasiliano.Ndani ya glovu
hiyo kuna vidole vya bandia
na mojawapo ya kidole hicho
kina kadi maalum ambayo
humtumia ujumbe kama
ninataka kumuona.Ujumbe
ukiingia hutoa mtetemo
ambao yeye Devotha
anaufahamu kisha huitoa
kadi ile akaiweka katika
simu na kuusoma ujumbe”
akasema Dr Yonathan
“Mtumie ujumbe haraka
sana” akasema Mathew na
kumfungua Dr Yonathna
ambaye aliichukua simu
yake akatuma ujumbe katika
ile kadi ya Devotha na baada
ya muda akasema
“Ujumbe
hajaupokelewa,kidole kile
kimezimwa inaonekana
ameweka katika
chaji”akasema Dr Yonathan
na Mathew akaichukua ile
simu
“Edger kaka yuko
wapi?Amefichwa
wapi?akauliza Mathew
“Sifahamu mahala
alipo.Ni siri ya Mossad.Mimi
ni balozi tu na jukumu langu
ni kutekeleza maelekezo
ninayopewa na viongozi
wangu” akasema Dr
Yonathan
“Hao majasusi ambao
wamekuja kuandaa
operesheni ya kumtafuta
Olivia wako wapi?
“Wako ubalozini kuna
chumba wameandaliwa”
“Utatupeleka huko
ubalozini waliko hao jamaa”
akasema Mathew
“Vipi kuhusu mke
wangu?
“Tunaondoka naye
tunakwenda kumtibu”
akasema Mathew na
kumuelekza Gosu Gosu
ambebe mke wa Dr Yonathan
wakatoka mle mle ndani
haraka.Wakaingia katika
gari lao na kumshusha yule
askari ambaye bado hakuwa
na fahamu wakamuwekea
bunduki yake pembeni na
kuondoka.Dr Yonathan bado
alikuwa katika mshangao
mkubwa sana.
“Mke wangu
mnampeleka kutibiwa
wapi?akauliza Dr Yonathan.
“Nyamaza !! akafoka
Gosu Gosu.Safari ikaendelea
kimya kimya na baada ya
muda Dr Yonathan akauliza
“Nyie ni akina nani?Nini
hasa mnachokihitaji
kwetu?Mnafahamu athari za
hiki mlichokifanya?
“Nimekwambia
unyamaze.Kama hautaki
kutii nitakufunga mdomo
kama mke wako” akasema
Gosu Gosu.
Kutoka nyumbani kwa
balozi wa Israel walielekea
moja kwa moja katika
makazi yao.
“Dr Hiran anaendeleaje
Ruby?akauliza Mathew
“Anaendelea vyema .Kwa
sasa amelala”
“Ahsante sana.Dr Hiran
kuna mgonjwa mwingine
tumekuja naye nitakuomba
umuhudumie ameumia sana”
akasema Mathew na Dr
Hiran akaenda kumtazama
mke wa balozi na kutoa wazo
apelekwe hospitali.
“Hospitali atakwenda
lakini naomba kwanza
apatiwe huduma ya kwanza
hapahapa” akasema Mathew
na kumgeukia balozi
“Mke wako atabaki hapa
atapatiwa huduma na
daktari na baadae ndipo
atapelekwa hospitali”
“Hapana.Mke wangu
ameumizwa sana hawezi
kubaki hapa”
“Balozi tafadhali fuata
kile ninachokuelekeza ili
wewe na mke wako
muendelee kuwa salama”
akasema Mathew na
kumtaka balozi atoke nje
akaingia garini,kabla
hawajaondoka Mathew
akamfuata Dr Hiran.
“Dr Hiran tfadhali
usimpe mwanamke huyu
nafasi ya kutoka humu
chumbani au kuwasiliana na
mtu yeyote hadi
nitakaporejea” akasema
Mathew na kukimbilia
katika gari wakaondoka
Safari ilikuwa ya kimya
kimyakimya hadi walipofika
katika ubalozi wa
Israel.Wakasimamishwa na
walinzi Dr Yonathan
akatokeza kichwa na
kujitambulisha kwamba yeye
ni balozi wa Israel na
amekuja ofisini kwake kwa
dharura.Geti likafunguliwa
wakaingia ndani.Wakashuka
garini na Dr Yonathan
akawaongoza kuelekea
katika jengo lenye vyumba
walikolala wale majasusi
wawili.
“Ni katika chumba kile
pale ndipo walipo hao jamaa”
akasema Dr
Yonathan.Mathew
akawafanyia ishara wenzake
wajihadhari akamsogeza
balozi hadi pale mlangoni na
kumpa maelekezo agonge
mlango na azungume kwa
lugha ya kiingereza ili
wamuelewe anachokisema.
“Nani wewe? Ikauliza
sauti kutokea ndani ya kile
chumba
“Ni mimi balozi Dr
Yonathan.Kuna dharura
imetokea ndiyo maana
nimekuja ghafla kuja
kuwaona” akasema Dr
Yonathan na baada ya ya
dakika mbili mlango
ukafunguliwa na mtu mmoja
aliyekuwa kifua wazi na
mkononi akiwa na bastora.
Mara tu alipotokeza
mkono wake uliokuwa
umeshika bastora ukapigwa
teke kali na bastora ile
ikamponyoka,akataka kurudi
ndani na kuubamiza mlango
lakini Tino akaurukia teke
zito mlango ukafunguka
akarukia ndani.Gosu Gosu
naye akachumpa kama nyani
na kurukia ndani.
“Tulieni hivyo hivyo”
akasema Tino.
“Weka silaha yako chini !
Tino akamuamuru Fishel
aliyekuwa kitandani
akijiandaa kuamka na
mkononi akiwa na
bastora.Taratibu Fishel
akaiweka bastora chini na
kuisukuma kuelekea kwa
Tino.Mathew akaingia ndani
akiwa na balozi.Ilikuwa ni
kama ndoto kwa wale jamaa
hawakuwa wametegemea
jambo kama lile
kutokea.Mathew
akampigisha magoti balozi
pamoja na akina Fishel na
Ehud halafu akasema
“Sina muda wa kupoteza
hapa kuna jambo moja tu
ambalo ninataka ninyi
watatu mnijibu ! akasema
Mathew
“Nataka mniambie wapi
alipo Edger Kaka?Akauliza
Mathew lakini wote wakawa
kimya
“Nauliza tena wapi aliko
Edger Kaka? Akauliza tena
Mathew lakini wale jamaa
wakaendelea kuwa
kimya.Mathew akamuendea
mmoja wao na kumuelekezea
bastora
“Jina lako nani?
“Fishel” akajibu
“Fishel wapi alipo Edger
Kaka?Nijibu ili ujiokoe”
akasema Mathew ambaye
macho yake yalionyesha
ukatili mkubwa
“Sifahamu alipo Edger
Kaka” akajibu Fishel
“Fishel sihitaji mchezo
wowote wa kupotezeana
muda.Nitakuuliza kwa mara
ya pili wapi alipo Edger
Kaka? Akauliza Mathew
“Sifahamu alipo Edger
Kaka” akajibu Fishel.Mkono
wa Mathew ulikuwa mwepesi
sana akaizinga bastora yake
yenye kiwambo cha sauti na
kuachia risasi Fishel
akaaguka chini ubongo
ukasambaa sakafuni.
“Nimewaambia sihitaji
mchezo ninachohitaji ni
majibu!! Akasema Mathew
kwa ukali akamuendea Ehud
“Zamu yako.Nataka
unieleze aliko Edger Kaka!
Akasema Mathew
“Sifahamu ! akajibu
Ehud bila woga
“Narudia kwa mara ya
pili wapi alipo Edger
Kaka?akauliza Mathew
“Sifahamu” akajibu Ehud
Kama alivyomfanya
Fishel,Mathew akaachia
risasi mbili na Ehud
akaanguka chini.Mathew
akamgeukia balozi Dr
Yonathan.
“Ni zamu yako
sasa.Umeona kilichowapata
wenzako?Sina utani hata
kidogo nieleze haraka
mahala alipo Edger Kaka”
akasema Mathew
“Sifahamu alipo Edger
Kaka” akasema Dr Yonathan
“Nitahesabu mpaka
tano,kama usiponipa jibu na
wewe yatakukuta kama
yaliyowakuta hawa wenzako”
akasema Mathew
“Nakuhakikishia
kwamba sifahamu chochote
kuhusu mahala alipo Edger
kaka”
“Tano ! akaanza
kuhesabu
“Nasema kweli jamani
sifahamu chochote! Akalia
balozi
“Nne !
“Jamani mtafanya
makosa makubwa sana kama
mtaniua.Israel na Tanzania
ni nchi marafiki na hiki
mlichokifanya kitakuwa na
athari kubwa sana kwa nchi
yenu.Nawasihi msiniue na
nitawasaidia msiingie katika
matatizo makubwa” akasema
Dr Yonathan
“Tatu ! akasema Mathew
kwa ukali
“Nawaomba vijana
wangu msifanye
hivyo.Msiniue tafadhali !
akasema balozi
“Mbili ! akasema
Mathew.maneno
aliyoyatamka balozi
hayakuonekana kumuingia
kabisa
“Moj…..”
“Msiniue tafadhani
nitasema ukweli” akasema
balozi.Uso wake ukiwa
umeloa jasho.
“Wapi alipo Edger
Kaka?akauliza Mathew kwa
ukali
“Edger Kaka amefichwa
katika ubalozi wa Israel
nchini Kenya”
“Una hakika?
“Ndiyo nina
uhakika.Edger Kaka yuko
katika ubalozi wa Israel jijini
Nairobi” akajibu balozi Dr
Yonathan.Mathew
akamuangalia na kumtaka
anyanyuke wakatoka na
kurejea katika gari lao
wakaondoka.
“Mathew mimi nitaishia
hapa.Msaada wangu ulikuwa
kuwasaidia kuingia salama
nyumbani kwa balozi wa
Israel operesheni
iliyofanikiwa.Ninaomba
mnirejeshe nyumbani na
ninyi mtaendelea na mambo
yenu.Mtakaponihitaji muda
wowote niko tayari kutoa
msaada” akasema Tino
“Tino tunakushukuru
sana kwa msaada wako
mkubwa.Bado tutaendelea
kuhitaji msaada wako”
akasema Mathew .
Walimrejesha Tino
nyumbani kwake halafu
wakachukua gari lao
waliloliacha pale
wakaendelea na safari hadi
nyumbani kwa Mathew.Mke
wa balozi alikuwa
amehudumiwa na alikuwa
amelala baada ya kupewa
dawa ya kumfanya alale ili
asiendelee kuhisi maumivu
makali aliyokuwa
anayapata.Dr Yonathan
akafungiwa katika chumba
kimoja na Mathew akamtaka
Gosu Gosu waelekee katika
chumba cha kusomea
wanachokitumia kama ofisi
yao.
“Gosu Gosu tumefanya
jambo kubwa na la hatari
sana kuvamia makazi ya
balozi wa nchi nyingine na
kumteka yeye na mke wake
na kama haitoshi tumevamia
ubalozi wa Israel na kuua
watu wawili.Hili ni suala
kubwa na linaloweza kuleta
mgogoro mkubwa wa
kidiplomasia baina ya nchi
zetu hizi mbili.Kwa namna
yoyote ile serikali ya Israel
lazima wataitaka serikali ya
Tanzania itutafute na
kuhakikisha tunapata
adhabu stahiki kwa jambo
tulilolifanya.Kwa upande
wangu sijutii kile
tulichokifanya kwani
ilitulazimu kukifanya na
tumeweza kugundua kitu
kikubwa sana.Tumepata
uhakika Edger Kaka hajafa
na ajali ile ilikuwa ya
kutengenezwa na waliofanya
hivyo ni Israel wakitumia
shirika lao la kijasusi la
Mossad.Olivia alikuwa sahihi
kusisitiza kuwa Edger hajafa
nadhani tayari alikuwa na
taarifa.Kitu ambacho
hakuwa sahihi ni
kumuhusisha Rais na tukio
lile.Kwa mujibu wa Dr
Yonathan,operesheni ile ya
kumteka Edger ilikuwa ya
siri na serikali ya Tanzania
hawakufahamu chochote na
hata Rais hajui
chochote.Sifahamu kwa nini
OIivia ameendelea kusisitiza
kwamba Rais anafahamu
mahala alipo Edger
Kaka.Usiku wa leo
tumegundua pia kwamba
Edger Kaka ana mahusiano
na watu wanaofadhili
kikundi cha kigaidi cha IS na
hii inamuhusisha moja kwa
moja na kikundi hicho.Kwa
maelezo ya balozi ninahisi
Edger ndiye
aliyemuunganisha Olivia na
kikundi cha kigaidi.Kwa nini
mtu kama Edger Kaka
ambaye alikuwa ni mbunge
mwenye heshima kubwa
ajiunge na magaidi?Kwa nini
ameyaharibu maisha ya
Olivia kwa kumuunganisha
na magaidi?Atanieleza hili
nitakapomtia mikononi”
akasema Mathew na
kunyamaza akiwa na hasira
nyingi
“Edger Kaka anadai eti
anampenda Olivia.Huu ni
upuuzi mkubwa sana.Huko
aliko aombe kwa miungu
yake yote asiingie katika
mikono yangu.Ameyaharibu
maisha ya Olivia kwa
kumuunganisha na magaidi
na kwa hili atajuta kwa nini
alikuja duniani!! Mathew
akatolewa mawazoni na
Gosu Gosu
“Mathew pamoja na yote
tuliyoyagundua usiku huu
lakini bado tunarudi pale
pale kwamba tunamuhitaji
sana Olivia” akasema Gosu
Gosu.Mathew akafikiri
kidogo na kusema
“Kuna jambo moja
ambalo tunatakiwa
kulifanya” akasema Mathew
na kunyamaza kidogo
“Jambo gani
Mathew?akauliza Gosu Gosu
“Tunatakiwa kuonana na
Rais kabla ya mapambazuko”
“Rais? Gosu Gosu
akastuka
“Ndiyo Gosu
Gosu.Tunatakiwa kuonana
na Rais.Edger Kaka
anashirikiana na magaidi
hivyo kwa kila namna lazima
tumpate.Olivia anatafutwa
hivi sasa na Mossad na Rais
hana taarifa hizi hivyo kama
tukionana naye na
tukamueleza itakuwa rahisi
sisi kumpata.Jambo lingine
ni hiki tulichokifanya usiku
wa leo kuvamia makazi ya
balozi na kumteka nyara pia
kuwaua majasusi wawili wa
Mossad.Kwa hiki
tulichokifanya Israel
hawatatuacha
salama.Tunahitaji kinga na
mtu pekee anayeweza
kutusaidia katika suala hili
ni Rais”
“Mathew nimeshangazwa
kidogo na maamuzi ya
kutaka kuonana na
Rais.Huyu Rais ndiye
aliyeelekeza idara ya siri ya
usalama wa mambo ya ndani
ya nchi wakuteke.Mpaka
sasa Rais anaamini wewe pia
ni mmoja wa watu
wanaoshirikiana na
magaidi.Kitendo cha Devotha
kukutoa katika jumba lile
kinazidi kumfanya Rais awe
na hasira nawe zaidi.Una
hakika anaweza
akakubaliana nasi?
“Tumegundua jambo
kubwa sana na Rais lazima
atusikilize.Nitakwenda ikulu
kuonana na Rais usiku huu
huu.Wewe utabaki hapa
ukiwalinda balozi na mke
wake.Hatutawaachia hadi
nitakapokuwa nimeonana na
Rais”
“Mathew I’m so scared !
“Me too.I’m scared.I’m
not sure about this but it is
the only option we have right
now.Kama sintarejea mpaka
itakapofika saa mbili
asubuhi hakikisha balozi
unaendelea kumshikilia
kwani ni yeye
atakayeniokoa.Mtumie yeye
kumshinikiza Rais aniachie
huru lakini ninaamini
mambo yatakwenda
vyema.Nitaonana na Rais na
atanielewa.Mlinde sana
Ruby,hakikisha anakuwa
salama” akasema Mathew
“Mathew utatumia njia
gani kuonana na Rais usiku
huu? Akauliza Gosu Gosu
“I don’t know yet but I’ll
find a way.Lazima nionane
na Rais usiku huu” akasema
Mathew na kuagana na Gosu
Gosu akaingia garini na
kuondoka.
“Mungu mlinde Mathew
arejee salama.Hiki
anachokifanya ni kitu cha
hatari kubwa” akaomba Gosu
Gosu.
- MATHEW NA
WENZAKE
WAMEMTEKA
BALOZI WA ISRAEL
NA MKEWE NA
KUUA MAJASUSI
WAWILI WA MOSSAD
NINI KITATOKEA?
- MATHEW ANAAMUA
KWENDA KUONANA
NA RAIS
KUMUELEZA KILE
ALICHOKIGUNDUA
KUHUSU EDGER
KAKA..JE LENGO
LAKE
LITAFANIKIWA?ATA
REJEA SALAMA?
MPENZI MSOMAJI
USIKOSE SEHEMU
IJAYO YA SIMULIZI
HII…
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 1
“Lazima nionane na Rais
usiku wa leo.Mambo haya
makubwa tuliyoyagundua
usiku huu anapaswa
kuyafahamu tatizo ni namna
ya kuweza kuonana naye
kama atakuwa tayari
kunipokea na
kunisikiliza.Mimi na yeye
tayari tumekwisha jenga
ukuta mkubwa kati yetu na
hadi hivi sasa anaamini
kwamba mimi na Olivia
tunashirikiana na kikundi
cha kigaidi cha IS.Pamoja na
hayo lakini kwa umuhimu
wa jambo hili lazima nifanye
kila mbinu hadi nihakikishe
nimeonana naye usiku huu
wa leo kabla ya
mapambazuko” akawaza
Mathew akiwa katika
mwendo mkali baada ya
kuondoka nyumbani kwake
“Siri tuliyoigundua ni
kubwa hadi mwili
unanisisimka.Edger Kaka
ambaye alikuwa mbunge
aliyejizolea umaarufu
mkubwa sana kutokana na
umahiri wake wa kupinga
rushwa na mafisadi kumbe
anashirikiana na kikundi cha
kigaidi cha
IS.Imewezekanaje kwa muda
huu wote aliokuwa mbunge
vyombo vyetu vya usalama
vimeshindwa kumfuatilia na
kufahamu kuwa
anashirikiana na
magaidi?Ninaanza kupata
picha kwamba yawezekana
hayuko peke yake lazima upo
mtandao.Kwa siku za
karibuni IS wamekuwa
wanajitanua sana barani
Afrika hususan katika
ukanda huu wa Afrika
Mashariki na kati.Ninahisi
yawezekana zile harakati
zake zote za kupambana na
mafisadi zilikuwa ni kwa ajili
ya kuficha mambo yake
aliyokuwa anayafanya
nyuma ya pazia
akishirikiana na IS.Nini
hasa malengo yao? Je Edger
alijiunga na IS kwa ajili ya
fedha au kuna sababu
nyingine? Akajiuliza Mathew
“Kibaya zaidi
kinachonifanya niwe na
hasira naye,ni kumuingiza
Olivia katika kikundi cha
magaidi.Ameyaharibu
maisha ya Yule
mremb😵livia hastahili
kuishi maisha ya namna
hii.Pamoja na kuyaharibu
maisha yake bado
ameendelea kudai kwamba
anampenda na anawataka
Mossad wamtafute ili
awaeleze kile wanachokitaka
kutoka
kwake.Mwendawazimu huyu
hatafanikiwa kumuona tena
Olivia katika maisha
yake.Nitampata Olivia na
kumuondoa katika maisha
haya aliyoingia” Mathew
akaendelea kuwaza na
alipokumbuka kuhusu
Mossad akahisi baridi
“Mossad ni mojawapo ya
mashirika makubwa ya
ujasusi duniani ambalo
nimeingia nalo katika
mgogoro mkubwa.Nimeua
majasusi wao wawili na
kama haitoshi nimemteka
balozi wa Israel hapa
nchini.Hili si jambo
dogo.Huu ni mgogoro
mkubwa sana wa
kidiplomasia na taifa la
Israel hata hivyo siogopi
kwani wao ndio walioanza
uchokozi wao kwa kuingia na
kufanya operesheni kwenye
ardhi yetu wakaua Rais na
kumteka Edger.Kama
walikuwa wanamuhitaji
Edger Kaka wangewasiliana
na mamlaka za hapa
Tanzania wakashirikiana
kumpata na si kuingia katika
ardhi yetu wakafanya
watakacho na kuondoka kwa
vile tu wao ni taifa lenye
uwezo mkubwa wanadhani
wana haki ya kuingia katika
nchi yoyote na kufanya
watakacho.Hii ni dharau
kubwa kutoka kwa haya
mataifa yaliyoendelea na
lazima tuwaonyeshe kwamba
japokuwa sisi hatujaendelea
kama wao lakini tunao
uwezo mkubwa kama
wao.Sijali kitakachotokea
lakini ninachokitaka mimi ni
kumpata Edger Kaka”
akawaza na kuongeza
mwendo wa gari akalipita
gari kubwa la mafuta
“Kama mbunge wa bunge
la jamhuri ya muungano wa
Tanzania ameweza
kushirikiana na magaidi wa
IS bila kujulikana kuna
ulazima mkubwa wa
kuwachunguza kwa kina
viongozi wetu kabla ya
kuwachagua au kuwapa
nyadhifa.Wengine wanakuwa
ni mamluki wanatumiwa
kwa maslahi ya mataifa na
vikundi vilivyoko nje.Sijui
watanzania hasa wale
waliokuwa wafuasi wakubwa
wa Edger Kaka
watazipokeaje taarifa za
kuwa mbunge wao,kiongozi
wao anashirikiana na
kikundi cha kigaidi cha
IS.Naamini zitakuwa ni
taarifa mbaya sana kwao na
wengi hawataamini.Kitu
kingine ambacho nakifikiria
ni kwamba huyu Edger
hakuwa peke yake kuna
watu ambao amekuwa
akishirikiana nao hapa
nchini na nina uhakika
mkubwa tayari IS
wamekwisha jenga mtandao
wao ndani ya Tanzania na
ndiyo maana ukitazama
shambulio la leo katika
hospitali ya Mtodora
linaoneka na kufanyika kwa
wepesi sana.Ninaapa
kuufumua kabisa mtandao
wote wa IS hapa nchini”
akawaza Mathew
Kichwa cha Mathew
Mulumbi kilijaa mawazo
mengi akiwa
barabarani.Aliendesha gari
hadi nje ya nyumba Fulani
nzuri iliyozungushiwa ukuta
wa rangi nyeupe na pembeni
ya ukuta kukiwa na maua
mazuri.Mlinzi aliposikia
muungurumo wa gari
akafungua dirisha dogo
akachungulia halafu
akafungua mlango mdogo wa
geri akatoka nje.Mathew
akashuka garini
“Habari yako kaka”
Mathew akamsalimu Yule
jamaa
“Habari nzuri.Nini shida
yako hapa usiku
huu?akauliza Yule mlinzi
ambaye alionekana akutoka
usingizini
“Ninaitwa Mathew
Mulumbi nimekuja kuonana
na mzee Meshack.Ni
muhimu sana
tafadhali”akasema Mathew
“Unataka kuonana na
mzee usiku
huu?Haitawezekana ndugu
subiri hadi kesho
asubuhi.Muda huu amelala
na hapendi usumbufu akiwa
amepumzika”
“Nalifahamu hilo ndugu
yangu lakini naomba
umjulishe kwamba Mathew
Mulumbi yuko hapa na
ataruhusu nikaonane
naye”akaomba Mathew
“Ndugu yangu naomba
unisikilize.Ondoka hapa
urejee asubuhi.Hakuna
namna ninayoweza
kukuruhusu usiku huu
ukaonane na mzee” akasema
Yule mlinzi.Mathew
hakutaka kubishana naye
akarejea garini.
“Nimegonga
mwamba.Huyu mlinzi
hataweza kuniruhusu
kuonana na Meshack Jumbo
na sitaki kutumia vurugu
kuingia ndani.Ninasita
kumpigia simu Meshack
kwani namba zake
sizikumbuki vyema lakini
ngoja nijaribu” akawaza
Mathew na kuziandika
namba katika simu yake
akapiga.Hakuwa na uhakika
na zile namba
“Sina uhakika kama
namba hizi ni sahihi lakini
lazima nijaribu” akawaza
Mathew wakati simu ile
ikiita ikakatika bila
kupokelewa akazitazama
tena zile namba na kupiga
simu ikaanza kuita na baada
ya sekunde kadhaa
ikapokelewa.Akashusha
pumzi baada ya kuitambua
sauti ile iliyopokea simu.
“Ahsante Mungu”
akasema Mathew Mulumbi
kwa sauti ndogo
“Hallow ! ikasema sauti
ya upande wa pili ambayo
Mathew aliitambua ni ya
mzee Meshack Jumbo
mkurugenzi wa zamani wa
idara ya ujasusi
“Mzee Jumbo samahani
kwa kukusumbua usiku huu
ni mimi Mathew”
“Mathew ! Jumbo
akashangaa
“Ndiyo mzee.Samahani
sana kwa kukusumbua usiku
huu”
“Una tatizo gani
Mathew?akauliza mzee
Jumbo huku akiinuka
kitandani
“Mzee nimekuja nina
tatizo niko hapa nje ya geti
lako”
“Uko hapa nyumbani
kwangu?
“Ndiyo mzee lakini mlinzi
wako amenizuia amegoma
hata kukupigia simu”
akajibu Mathew
“Sawa ninampigia mlinzi
akuruhusu uingie
ndani.Hajakosea anafuata
maelekezo yangu niliyompa”
akasema Meshack Jumbo na
kukata simu.Hazikupita
sekunde kumi Mathew
akamuona mlinzi akitoa
simu mfukoni akaipokea
halafu akafungua geti na
kumruhusu Mathew aingie
ndani.Mathew akaegesha
gari na kushuka,mlango wa
sebuleni ukafunguliwa
Meshack Jumbo akatoka
akiwa amevaa mavazi ya
kulalia
“Mathew karibu sana”
akasema Meshack na
kumkaribisha Mathew ndani
“Habari za hapa
mzee.Samahani sana kwa
kukusumbua usiku huu”
akasema Mathew
“Bila samahani Mathew
kuwa na amani.Kwema huko
utokako?
“Huko nitokako si kwema
mzee wangu ndiyo maana
nimekuja kwako usiku huu”
akasema Mathew
“Nini kimetokea?Ni
kuhusiana na shambulio
lililotokea usiku wa leo
katika hospitali ya
Mtodora?akauliza Meshack
“Hilo nalo linahusiana na
kile kilichonileta hapa.Mzee
kwa kuwa muda si rafiki
sana nitakueleza kwa ufupi
kile kinachoendelea”
“Mathew Mulumbi
unanifahamu mimi sipendi
kufahamu mambo kwa
kifupi.Nataka unieleze jambo
kwa kirefu ili nielewe na
hata kama unahitaji msaada
wangu nijue nitakusaidia
vipi.Nieleze kwa kirefu kila
kitu” akasema Meshack
Jumbo na Mathew akaanza
kumuelezea kila kitu toka
alivyokutana na Olivia
Themba hadi yale
waliyoyagundua usiku ule.
“I think I need a drink”
akasema Meshack Jumbo na
kutoka baada ya dakika
chache akarejea akiwa na
chupa kubwa ya mvinyo
akamimina katika glasi
akanywa funda kubwa.
“You need some?akauliza
“No thank you! Akajibu
Mathew
“Mathew sijui nianzie
wapi kusema chochote kwa
hiki ulichonieleza.Nimestuka
sana.Kwanza kwa magaidi
kuweza kupiga hatua kubwa
kiasi hiki na kufanya kila
wakitakacho.Kuna udhaifu
katika vyombo vyetu
vinavyohusika na kudhibiti
ugaidi hapa nchini ndiyo
maana magaidi wameweza
kupata mwanya wa kufanya
kile wakitakacho.Pili ni
kuhusu Edger Kaka.Huyu
alikuwa ni mbunge mwenye
jina kubwa hapa nchini na
alifanya kazi kubwa ya
kufichua ufisadi mkubwa
uliokuwa unafanywa na watu
mbali mbali hususan
viongozi walioko
serikalini.Alijijengea
umaarufu mkubwa sana
kwani aliweza kuwataja
mafisadi hadharani bila
woga.Aliaminiwa mno na
alikuwa mmoja wa
wanasiasa vijana
waliotabiriwa kufika mbali
sana katika uongozi lakini
taarifa kwamba anahusiana
na kikundi cha kigaidi cha IS
imenistua sana.Sikutegemea
kabisa.Kwanza kusikia
kwamba yuko hai ni mstuko
mkubwa kwangu.Sote
tunaamini alifariki katika ile
ajali kumbe ulikuwa ni
mchezo tu.Kwa kweli sijui
niseme nini” akasema
Meshack Jumbo na
kumimina tena mvinyo
katika glasi akanywa
“Mzee kwa hapa
nilipofika nimekwama
ninahitaji msaada ndiyo
maana nimekuja kwako”
“Sema Mathew unahitaji
nikusaidie nini?
“Nahitaji kuonana na
Rais usiku huu.Kama
nilivyokueleza Rais anaamini
mimi na Olivia wote
tunatumiwa na kikundi cha
IS na hivi sasa idara ya siri
ya mambo ya ndani ya nchi
wananisaka kila kona
wakiamini ninashirikiana na
magaidi hivyo siwezi kupata
nafasi ya kuonana na Rais
ndiyo maana nimekuja
kwako ili utafute namna ya
kunikutanisha na Rais usiku
huu niweze kuzungumza
naye ayafahamu haya
tuliyoyagundua.Hata yeye
mwenyewe haufahamu
ukweli wa hili suala hivyo
nataka nimueleze kwa kina
ajue namna suala hili
lilivyokaa.Kingine
ninachohitaji kuonana na
Rais ni kuhusu Olivia.Yeye
anafahamu mahala alipo
Olivia na kama tukiweza
kumpata basi atatusaidia
kufahamu mambo mengi
kuhusiana na mtandao wa IS
na mipango yao hapa
nchini.Jambo lingine ni
kwamba tayari tumeingia
katika mgogoro mkubwa wa
kidiplomasia kwa kuvamia
makazi ya balozi wa Israel
na kumteka vile vile kuwaua
majasusi wawili wa Mossad
waliotumwa hapa nchini
kuandaa operesheni ya
kumtafuta Olivia ili
wamtumie katika
kumlazimisha Edger Kaka
awaeleze mahala walipo
watu ambao wanafadhili
kikundi cha IS ambao yeye
Eger anawafahamu na
walikwenda kumtembelea
alipokuwa amelazwa
hospitali nchini Israel.Huu ni
mgogoro mkubwa na Rais
lazima aufahamu kwani ni
yeye anayeweza
kutusaidia.Jambo lingine
mzee tunahitaji kumpata
Edger Kaka ambaye
anashikiliwa katika ubalozi
wa Israel jijini Nairobi.Hii ni
operesheni kubwa na nzito
na mimi sina uwezo wa
kuitekeleza mwenyewe
ninahitaji msaada mkubwa
na mtu pekee anayeweza
akaniwezesha ni Rais hivyo
mzee ninaomba unisaidie
niweze kuonana naye kwa
usiku huu” akasema
Mathew.Meshack Jumbo
akainamisha kichwa
akafikiri kwa muda na
kusema
“Mathew jambo hili ni
kubwa sana na Rais wa nchi
lazima alifahamu lakini
tatizo ni namna ya kukutana
na Rais.Siwezi
kukudanganya kijana wangu
nimekuwa serikalini kwa
miaka mingi na nimekuwa
na ukaribu na marais karibu
wote waliopita lakini huyu
wa sasa sina ukaribu naye
kabisa na hata mawasiliano
naye sina” akasema Meshack
Jumbo
“Mzee hatuwezi
kukwama.Tafuta namna ya
kuniwezesha kukuonana na
Rais naamini huwezi
kushindwa kupata mbinu
yoyote” akasema Mathew na
Meshack akazama katika
tafakari halafu akasema
“Nimepata wazo.Mke
wangu anaye mdogo wake
ameolewa na aliyekuwa
mkuu wa idara ya usalama
wa taifa ambaye amestaafu
miaka mitatu iliyopita.Huyu
anaweza akawa na ukaribu
na Rais na anaweza
akatusaidia kuonana naye
lakini lazima naye
tumshirikishe alifahamu
jambo hili.Anaitwa Joel
Mshana” akasema Meshack
Jumbo
“Hakuna tatizo mzee
ninachohitaji mimi ni
kuonana na Rais” akasema
Mathew na Meshack Jumbo
akainuka akaenda chumbani
kwake na kumkuta mke
wake akiwa amekaa
kitandani
“Kuna nini
Meshack?Nimekusikia
ukizungumza na mtu
sebuleni.Kuna mgeni?
“Kuna mgeni
amekuja.Sikutaka
kukuamsha usingizini lakini
mgeni mwenyewe ni Mathew
Mulumbi”
“Kuna tukio
gani?Mathew hawezi kuja
usiku huu kama hakuna
tukio limetokea”
“Nitakueleza baadae
lakini kwa sasa nataka
kuzungumza na shemeji
Diana”
“Diana? Mke wa Meshack
Jumbo akastuka aliposikia
mumewe anataka
kuzungumza na mdogo wake
usiku ule
“Diana amefanya nini?
“Ninataka kuzungumza
na mumewe” akasema
Meshack
“Kuna tatizo gani
Meshack?Nieleze tafadhali
kama mdogo wangu yuko
kwenye hatari”
“Hakuna hatari yoyote
usihofu.Ninataka
kuzungumza na mume
wake.Mathew ana shida ya
kuonana na Rais na amekuja
kwangu ili nimsaidie
kumkutanisha naye lakini
sina ukaribu na Rais huyu
wa sasa ndiyo maana
ninataka kuomba msaada wa
Joel yeye amestaafu kazi si
miaka mingi na nina
uhakika mkubwa atakuwa
ana mawasiliano ya karibu
na Rais”
“Una uhakika ni hilo tu
na Diana hayuko katika
hatari?
“Niamini darling si
Diana wala mume wake
walio katika hatari.Tunataka
kutafuta njia ya kumsaidia
Mathew kuonana na Rais”
akasema Meshack na
kuchukua simu yake akatoka
akarejea sebuleni halafu
akazitafuta namba za simu
za shemeji yake Diana
akampigia.
“Mzee Meshack” akajibu
Diana baada ya kuipokea
simu
“Umeniogopesha sana
kwa simu hii ya usiku.Kuna
tatizo lolote huko?akauliza
Diana kwa wasi wasi
“Diana naomba
unisamehe sana kwa simu
hii ya usiku.Huku kwema
kabisa hakuna tatizo lolote”
“Haujawahi kunipigia
simu usiku mwingi namna
hii ndiyo maana nimestuka
sana”
“Usihofu Diana.Nimepiga
simu usiku huu ninataka
kuzungumza na Joel na mimi
sina namba zake za simu”
“Kuna tatizo lolote?
Akauliza Diana
“Hakuna tatizo usihofu
ila kuna suala nataka
kuzungumza naye la
muhimu” akajibu Meshack
Jumbo
“Sawa subiri kidogo”
akasema Diana na kumpatia
simu mume wake
“Hallow Meshack”
akasema Joel Mshana
“Joel samahani sana kwa
kukuamsha usiku huu”
“Usijali Meshack.Vipi
huko kwema?
“Joel ninahitaji
kuzungumza nawe jambo
Fulani.Kama hutajali
naomba nije hapo kwako
usiku huu kuna suala la
muhimu sana”
“Suala gani
Meshack?Kuna tatizo hapo
nyumbani?
“Ni suala linalohusiana
na usalama wa nchi.Naomba
tafadhali nije hapo kwako
tuzungumze” akasema
Meshack
“Meshack unaniogopesha
kidogo.Unaweza ukanieleza
japo kidogo tu suala hilo
linahusiana na nini?
“Usijali Joel nitakuja
kukueleza nikifika si suala la
kuzungumza simuni.Ndani
ya dakika arobaini naamini
nitakuwa nimefika hapo
kwako” akasema Meshack
“Sawa karibu sana
Meshack ninakusubiri hapa”
akasema Joel na Meshack
akakata simu.
“Joel
amekubali.Tusipoteze muda
twende tukaonane naye”
Meshack akamwambia
Mathew akaenda chumbani
akamuaga mke wake
wakaingia katika gari la
Mathew na kuondoka
kuelekea nyumbani kwa Joel
Mshana
“Mathew bado natafakari
kuhusu Edger Kaka.Taarifa
kwamba anashirikiana na
magaidi imenistua sana.Nini
hasa malengo yake ya
kushirikiana kwa siri na
watu hawa?akauliza
Meshack Jumbo
“Kwa maelezo
niliyoyapata kutoka kwa
balozi wa Israel Dr Yonathan
Cohen,Edger Kaka akiwa
hospitali alitembelewa na
watu wawili ambao
wanatafutwa sana na
serikali ya Israel kwa
kufadhili kikundi cha kigaidi
cha IS pamoja na vikundi
vingine vya wanamgambo wa
kipalestina wanaoua
waisrael hivyo basi kitendo
hicho kinaonyesha moja kwa
moja kwamba lazima ana
mahusiano ya karibu na
watu hao wawili na ndiyo
maana Israel wakamteka na
kutufanya tuamini kwamba
amekufa lengo lao ni
kumuhoji kupata taarifa za
watu hao
wanaowatafuta”akasema
Mathew
“Kama watu hao
wanaotafutwa na serikali ya
Israel waliweza kuvuka
mpaka na kuingia Israel
wakaenda kumuona Edger
hospitali inaonyesha wazi
kuna watu ndani ya serikali
ya Israel ambao
wanawasaidia katika
kutekeleza mipango yao.Huu
Lazima ni mtandao
mkubwa.Nadhani ni wakati
wa Israel sasa kuyaachia
maeneo ya wapalestina
inayoyakalia kimabavu ili
kumaliza vita hii ambayo na
sisi pia tumejikuta tukiingia
bila kutaka.Wafadhili hao wa
ugaidi wanafadhili vikundi
ambavyo vinafanya
mashambulio katika makazi
ya waisrael na kuipelekea
serikali ya Israel kufanya
operesheni ya kimya kimya
ndani ya nchi yetu na
kumchukua Edger Kaka na
huu ni mgogoro
mmoja.Mgogoro mwingine ni
pale ambapo balozi wao
ametekwa na watu wao
wawili kuuawa.Kama
kusingekuwa na mapigano
haya ya waisrael na
wapalestina haya yote
yasingekuwepo ndiyo maana
ninasema kwamba ninadhani
ni wakati muafaka kwa
serikali ya Israel
kuwarejeshea wapalestina
maeneo yao wanayoyakalia
kimabavu ili kuumaliza huu
mzozo”akasema Meshack
Jumbo
“Mzozo wao
hautuhusu.Kinachonipa
hasira ni dharau za mataifa
haya yaliyoendelea kwa
mataifa yetu yenye uchumi
mdogo.Wameingia hapa
nchini kwetu wakafanya
operesheni yao kimya kimya
na kumchukua raia wetu bila
sisi kufahamu na kama
haitoshi bado wana mipango
ya kuja tena kufanya
operesheni nyingine ya siri
hapa nchini ya kumtafuta
Olivia wamchukue kama
walivyomchukua Edger
Kaka.Hii ni dharau kubwa
sana kwani hata kama Edger
Kaka ana mahusiano na
magaidi serikali yetu
ilipaswa kujulishwa lakini
hawakufanya hivyo.Mgogoro
huu wameuanzisha wao
wenyewe na sasa ni zamu
yetu kuwaonyesha kwamba
hata sisi tunao uwezo
mkubwa kama wao na
tunaweza kufanya mambo
kama wanayoyafanya
wao.Watashangaa namna
tutakavyokwenda
kumchukua Edger Kaka
katika ubalozi wao.Sijali
kitakachotokea lakini kitu
cha muhimu ni kuhakikisha
nchi yetu inakuwa salama”
akasema Mathew
akionekana kuwa na hasira
“Huyu mwanamke Olivia
kuna chochote unachotaka
kunieleza kuhusu
yeye?akauliza Meshack
“Najua unachotaka
kukifahamu mzee.Urafiki
wetu ulikwenda mbali
zaidi.Nadhani tayari
umekwisha nielewa”
“Lakini Mathew wewe
una mke wako kwa
nin………..”
“Mzee naomba
tusizungumzie masuala
hayo.Tujielekeze katika
jambo linaloikabili nchi kwa
sasa” akasema Mathew
Safari iliendelea kukiwa
na maongezi machache hadi
walipofika nyumbani kwa
Joel Mshana ambaye
walimkuta anawasubiri.
“Karibu sana Meshack”
akasema Joel
Mshana.Meshack na Mathew
wakaingia sebuleni
“Joel awali ya yoite
naomba uniwie radhi sana
kwa usumbufu huu mkubwa
niliowapa usiku huu”
akasema Meshack Jumbo
“Usihofu
Meshack.Naamini lazima
kuna sababu ya msingi hivyo
ondoa hofu kabisa” akasema
Joel
“Ahsante sana Joel.Kabla
hatujaendelea naomba
nikutambulishe huyu ni
Mathew Mulumbi.Amewahi
kufanya kazi katika idara ya
ujasusi wakati wangu”
akasema Meshack Jumbo
“Mathew Mulumbi !
Huyu si mgeni
kwangu.Ninamfahamu japo
sina hakika kama naye
ananifahamu na ndiyo
maana nilipokuona naye
nikajua lazima kuna jambo
kubwa” akasema Joel
“Joel ni kweli kuna jambo
kubwa na tumekuja hapa
kwa ajili ya kuomba msaada
wako”
“Ulinieleza ni suala
linalohusiana na usalama wa
Taifa.Ningependa
kulifahamu suala hilo na
msaada upi
mnauhitaji?Kama utakuwa
ndani ya uwezo wangu
ninawaahidi kuwasaidia”
akasema Joel Mshana.
“Joel kumekuwa na
mfululizo wa matukio yasiyo
ya kawaida kwa siku za
karibuni kwa mfano matukio
ya utekaji nyara.Alitekwa
Olivia Themba na baadae
akatekwa baba yake mzee
Agrey Themba.Wakati bado
jitihada za kuwatafuta
zikiendelea usiku wa leo
kumetokea shambulio la
kigaidi katika hospitali ya
Mtodora na mpaka sasa idadi
kamili ya vifo na majeruhi
bado haijatolewa.Usiku wa
leo amenifuata Mathew na
kunifumbua macho
kuhusiana na haya mambo
ambayo yamekuwa
yanaendelea hapa nchini
kuanzia utkwaji wa Olivia na
hili la usiku wa leo katika
hospitali ya Mtodora.Ni
mambo mazito sana.Lengo la
Mathew kuja kwangu
alinitaka nimsaidie aweze
kuonana na Rais ili amueleze
masuala haya makubwa
lakini mimi sina mahusiano
ya karibu na Rais ndiyo
maana nikaona tuje kwako
utusaidie kwa hilo.Naamini
wewe na Rais mna
mahusiano ya karibu na
itakuwa rahisi kuonana naye
kupitia kwako” akasema
Meshack Jumbo.Joel Mshana
akafikiri kidogo na kusema
“Hujakosea
Meshack.Japokuwa
nimestaafu kazi lakini bado
nina mahusiano ya karibu na
Rais na hata yalipotokea
matukio haya hasa la usiku
wa leo nimempigia nikampa
pole kwa kile kilichotokea
katika hospitali ya
Mtodora.Uwezo wa
kuwasaidia kuonana na Rais
ninao lakini siwezi kufanya
hivyo bila kufahamu sababu
hasa ya kutaka kuonana
naye.Rais ni mtu mkubwa na
ili niweze kuwasaidia
kuonana naye nataka
kufahamu sababu”akasema
Joel
“Mzee Joel,ninazo taarifa
nyeti sana za kuhusiana na
kile kinachoendelea hivi sasa
hapa nchini ninazotaka
kuzifikisha kwa Rais usiku
huu.Muda wetu ni mfupi na
siwezi kukueleza kila kitu
lakini kuna mambo nyeti
sana ambayo Rais anapaswa
kuyafahamu kuhusiana na
shambulio lililotokea usiku
huu na kile kinachoendelea
hapa nchini”akasema
Mathew
“Mathew nahitaji
kufahamu ni taarifa gani
ulizonazo ili na mimi nipime
kama zina uzito wa kuonana
na Rais.Usihofu kuhusu
mimi nimewahi kuwa mkuu
wa idara ya usalama wa
Taifa na nimestaafu miaka
mitatu iliyopita.Nieleze
tafadhali taarifa ulizonazo”
akasema Joel
“Mzee Joel nakufahamau
wewe ni nani na
ninakuamini lakini Rais
anapaswa kuzisikia taarifa
hizi kwanza kabla
yako.Naomba umuamini
mzee Meshack Jumbo na
utusaidie kwenda kuonana
na Rais na utasikia kila kitu”
akasema Mathew
“Mathew nasikitika
kwamba nitashindwa
kukusaidia ombi lako bila
kufahamu sababu ya kutaka
kuonana na Rais.Hamuwezi
kwenda peke yenu lazima
niwapeleke mimi na ili
niwapeleke huko lazima niwe
ninafahamu kile ambacho
kimewapeleka.Lazima iwe ni
sababu kubwa ili
nimshawishi akubali
kuonana nawe” akasema
Joel.Meshack Jumbo
akakohoa kidogo na kusema
“Joel mimi na wewe
tunafahamiana
vyema,tumekuwa marafiki
kwa muda
mrefu,tumeshirikiana katika
mengi na isitoshe sisi ni
ndugu kwani tumeoa
nyumba moja naomba
uniamini katika hili
ninalokuomba
utusaidie.Mathew ana
mambo ya muhimu sana
ambayo anataka kuyafikisha
kwa Rais.Kama ningekuwa
na ukaribu na Rais
nisingekujak ukusumbua
usiku huu lakini sina
ukaribu naye ndiyo maana
ninakuomba utusaidie Joel”
“Meshack sina tatizo
lolote nawe.Wewe ni ndugu
yangu lakini tatizo ni
kwamba nitamueleza nini
Rais akitaka kujua sababu
ya kutaka kwenda kuonana
naye usiku huu?Ni hicho
pekee ambacho ninataka
kukifahamu”
“Mweleze ni suala
muhimu kwa usalama wa
Taifa” akasema Mathew.Joel
akageuka na kumtazama
Meshack Jumbo
“Tusaidie tafadhali Joel”
akasema Meshack na Joel
akainamisha kichwa
“Meshack mmenipa
mtihani mgumu sana”
“Usihofu Joel ninaamini
hata Rais mwenyewe
atakushukuru kwa hiki
atakachokwenda kuambiwa
na Mathew” akasema
Meshack Jumbo.
Joel akaenda chumbani
kwake akachukua simu na
kurejea sebuleni akazitafuta
namba za Rais akapiga.
“Hallow Joel” akasema
Dr Evans baada ya kupokea
simu
“Mheshimiwa Rais
samahani sana kwa
kukusumbua usiku huu”
akasema Joel
“Bila samahani
Joel.Nimemaliza kikao na
wakuu wa vyombo vya
usalama muda mfupi uliopita
hivyo usihofu kitu kazi
zinaendelea” akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais
nimekwisha kupa pole awali
lakini naomba nikupe tena
pole kwa mara ya pili kwa
suala lililotokea leo”
“Nashukuru sana Joel”
“Mheshimiwa Rais
pamoja na kukupa pole
lakini simu hii ni kwa ajili ya
jambo lingine kabisa”
“Nakusikiliza Joel”
“Mheshimiwa Rais
japokuwa tumestaafu kazi
lakini kwa nyakati kama hizi
ambazo taifa letu linapitia
wakati mgumu tunalazimika
kuvaa tena gwanda kuingia
katika uwanja wa
mapambano.Yawezekana
hatuwezi kushika bunduki
na kupambana lakini tunao
uzoefu mkubwa sana katika
masuala haya ya usalama
ambao tunaweza
tukautumia”
“Uko sahihi Joel,kama
Taifa tunapitia wakati
mgumu sana na kila
mzalenzo wa taifa hili
ambaye anadhani anaweza
kuwa na msaada wa
kuwafahamu hawa
waliofanya matukio haya
maovu tunamkaribisha.Mtu
kama wewe Joel uzoefu wako
unahitajika sana kwa wakati
kama huu” akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais hilo
ndilo hasa ambalo
limenipelekea nikupigie simu
usiku huu.Naomba pia
utambue kwamba niko hapa
na Meshack Jumbo”
“Meshack
Jumbo?akauliza Dr Evans
“Ndiyo.Ni mkurugenzi
wa zamani wa idara ya
ujasusi”
“Mheshimiwa Rais
tunataka kuja kuonana nawe
usiku huu kuna jambo la
muhimu sana tunataka
kuzungumza nawe
linalohusiana na haya
mambo yanayoendelea hivi
sasa hapa nchini” akasema
Joel na ukimya mfupi
ukapita
“Mheshimiwa Rais”
akaita Joel
“Nafahamu huu si
utaratibu na sisi kama
wastaafu wa tuliokuwa
vyombo vya usalama
tunafahamu taratibu zilivyo
lakini tunaomba utukubalie
ombi letu la kutaka kuonana
nawe usiku huu mheshimiwa
Rais.Nimuhimu
sana”akasema Joel
“Sipati kigugumizi
kukutana nanyi Joel lakini
suala hilo mnalotaka
kunieleza haliwezi
likaahirishwa hadi kesho
asubuhi tukaonana
mkanieleza?Muda mfupi ujao
nitakuwa na kikao kingine
tena ndiyo maana
ninawaomba kama
ikiwezekana tuonane
asubuhi” akasema Dr Evans.
“Mheshimiwa Rais suala
hili ni muhimu sana na
haliwezi kusubiri hadi
asubuhi ndiyo maana
tunataka kuonana nawe
usiku huu huu kabla ya
mapambazuko”Joel
akasisitiza
“Joel unaweza
ukanigusia suala hilo ni
kuhusu nini?
“Mr President it’s the
matter of national security so
I can’t tell you on phone”
akasema Joel
“Joel kwa kuwa wewe ni
mtu ambaye tumefanya kazi
vizuri ninakufahamu vyema
nitaahirisha kwa muda kikao
ambacho kilikuwa kifanyike
muda mfupi ujao kwa ajili ya
kuja kuonana
nanyi.Mtahitaji usafiri
nitume vijana wangu waje
wawachukue mahala
mlipo?akauliza Dr Evans
“Tunashukuru
mheshimiwa Rais lakini
tutatumia usafiri
binafsi.Tunashukuru sana
kwa kukubali kuonana nasi
tutafika hapo ikulu si muda
mrefu sana kutoka sasa”
“Ninawasubiri” akasema
Dr Evans na kukata
simu.Joel Mshana akavuta
pumzi ndefu
“Rais amekubali kuonana
nasi kwa sababu ananiamini
mno.Nimekubali kuubeba
mzigo huu kutokana na
namna ninavyomuamini
Meshack Jumbo.Naamini
asingeweza kufika hapa
kwangu usiku huu kama
kusingekuwa na suala nyeti
hivyo nawaomba ndugu
zangu heshima yangu kwa
Rais isishuke kama hamna
jambo zito ambalo linastahili
Rais kuahirisha kikao
muhimu kulisikiliza”
akasema Joel
“Usihofu Joel” akasema
Meshack.Hawakupoteza
muda wakaingia katika gari
la Mathew na safari ya ikulu
ikaanza huku ndani ya gari
kukiwa na mazungumzo
machache.Kila mmoja
alionekana kuzama katika
mawazo.
Iliwachukua dakika
hamsini kufika ikulu na kwa
kuwa tayari taarifa zao
zilikwisha wasilishwa kwa
walinzi wa ikulu
waliruhusiwa kupita baada
ya kukaguliwa na bastora ya
Mathew kubaki kwa
walinzi.Walipokewa na
walinzi wawili na kuigizwa
ndani aliko Rais.Mara tu
walipoingia Rais akasimama
kuwasalimu.
“Joel Mshana karibu
sana.Nimefurahi kukuona
tena mzalendo wa kweli”
akasema Dr Evans
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais” akasema
Joel wakapeana mikono
kusalimiana
“Mheshimiwa Rais
kutana na Meshack
Jumbo,mkurugenzi mstaafu
wa idara ya ujasusi”
“Mzee Jumbo karibu
sana.Nimefurahi kuonana
nawe” akasema Dr Evans
“Hata mimi nimefurahi
sana kukutana nawe
mheshimiwa Rais”
Mara Rais akastuka
kama ameona dude la
kutisha
“I think I know this man
! akasema Dr Evans kwa
mshangao kidogo.Tayari sura
yake ilikwisha badilika
“Yes Iknow this this
man.Joel what’s the meaning
of this ?! akauliza Dr Evans
akwa ukali
“Mr Pres…………..” Joel
akataka kusema kitu lakini
Mathew akamzuia
“Mheshimiwa Rais
naitwa Mathew Mulumbi !
akasema Mathew na Dr
Evans akapandwa na hasira.
“Joel what is this?! What
is your plan? Akauliza Dr
Evans kwa ukali
“Mheshimiwa Rais ..”
akataka kusema kitu
Meshack Jumbo lakini Dr
Evans akamzuia.
“This man is a
terrorist.Huyu ni mshirika
mkubwa wa magaidi na
hapaswi kuingia katika
nyumba hii yenye heshima
kubwa.Joel na huyo
mwenzako nani sijui
sikutegemea kabisa kwa
namna ninavyokuamini
ukafanya hivi ulivyofanya
kumleta gaidi ikulu.Watu
wengi wamepoteza maisha
usiku wa leo katika
shambulio la kigaidi na
mpaka sasa mwanangu
hajulikani kama ameuawa
ama yuko wapi.Huyu ambaye
mmeongozana naye
anahusika moja kwa moja na
tukio lile.Oh my God !!
akasema Dr Evans na
kuelekea katika simu
iliyokuwa mezani akainua
mkono wa simu.
“Mheshimiwa Rais kabla
hujapiga hiyo simu kuwataka
walinzi wako waje
wanikamate naomba unipe
dakika tatu nizungumze
nawe na baada ya hapo
nitajisalimisha kwako na
walinzi wako watanikamata
na kunipeleka sehemu yoyote
utakayo” akasema Mathew
“Mheshimiwa Rais
umekubali kuonana nasi
kutokana na imani yako
kubwa kwangu.Ninaomba
uniamini mimi na umsikilize
huyu kijana anachotaka
kukueleza.Tafadhali
mheshimiwa Rais niko chini
ya miguu yako” akasema Joel
Mshana.
“Joel sikutegemea
kabisa.Narudia tena
sikutegemea kabisa kama
ungeweza kumleta huyu
gaidi katika nyumba hii
tukufu”
“I’m not a terrorist !
akafoka Mathew na Meshack
Jumbo akamzuia
“Mathew please.Kuwa
mvumilivu” akasema
Meshack kwa sauti ndogo
“Joel na mwenzako ninyi
ni watu wenye heshima
kubwa sana katika nchi hii
kwa nini mmekubali
kuivunja heshima yenu kwa
kuungana na huyu gaidi?
Akauliza Dr Evans kwa ukali
“Mheshimiwa Rais
naomba unisikilize.Mimi ni
Meshack Jumbo nimewahi
kuwa mkurugenzi wa idara
ya ujasusi kwa miaka ishirini
na tatu.Ni mimi
niliyempokea Mathew
Mulumbi katika idara yangu
na kufanya naye kazi na
alikuwa mmoja wa majasusi
wa kuaminiwa mno na
amekwisha fanya mambo
mengi makubwa kwa nchi hii
ambayo sitaki kupoteza
muda wako
kuyataja.Ninamuamini
Mathew Mulumbi
sana.Tafadhali nakuomba
umsikilize.Ana jambo la
kukueleza” akasema
Meshack Jumbo
“Hakuna chochote
mtakachonieleza
kitakachonibadili msimamo
wangu.Huyu ni mtu ambaye
ninamtafuta kwa udi na
uvumba.Tena
ninawashukuru kwa
kunirahisishia kazi yangu ya
kumtafuta na
ninawashukuru vile vile kwa
kunipotezea muda
wangu.Sikutegemea kabisa
Joel kama ungew..….”
“Mheshimiwa Rais
tafadhali” akasema Joel
Mshana na kupiga magoti
“Mr Mshana please stand
up! Akasema Mathew kwa
ukali
“Usipige magoti.Tuko
hapa kwa ajili ya kulipigania
taifa letu lakini mtu ambaye
tumempa dhamana ya
kuwaongoza watanzania
hajali maisha ya watanzania
yanavyopotea.Let him do
whatever he wants to do.Go
ahead Mr president make
the call.Lakini kabla
haujapiga hiyo simu naomba
usikie haya
machache.Ninafahamu
unanitafuta kwa udi na
uvumba na maamuzi yangu
ya kuja kukuoan hayakuwa
rahisi na nilifahamu fika
kwamba ninakuja mwenyewe
kwenye mdomo wa mamba
na sintaweza kutoka salama
lakini sikuogopa kwa kuwa
kilichonileta hapa ni
kulipigania taifa langu.Kesho
asubuhi kama sintaonekana
mtaani taarifa zitaanza
kusambaa katika mitandao
yote ya jamii hapa nchini
kuhusiana na kutekwa kwa
Olivia Themba na baba yake
Agrey Themba.Watanzania
wote watafahamu nani aliye
nyuma ya utekaji
ule.Unataka watu wafahamu
nani aliye nyuma ya tukio la
kutekwa Olivia Themba na
baba yake Agrey?akauliza
Mathew na Dr Evans
akabaki kimya
“Answer me Mr
President !! akasema
Mathew kwa ukali
“Mheshimiwa Rais
naomba tusifike huko
Mathew anakotaka
tufike.Mambo haya ni nyeti
mno na tusianze kuanika siri
za taifa hili na kuuweka
usalama wetu
mashakani.Ninakuomba
mheshimiwa Rais mpe
dakika chache umsikilize kile
anachotaka kukueleza”
akasema Meshack Jumbo.Dr
Evans akamtazama Mathew
kwa macho yaliyojaa hasira
“You want to challenge
me young man?! Akauliza
“Mheshimiwa Rais siko
hapa kushindana nawe na
sina uwezo wala nguvu ya
kushindana nawe.Niko hapa
kwa ajili ya kukupa taarifa
muhimu kwa usalama wa
nchi hivyo naomba
unisikilize kile ninachotaka
kukueleza na baada ya hapo
utaamua wewe mwenyewe
kitu cha kufanya” akasema
Mathew
“Mheshimiwa Rais
msikilize tafadhali Mathew
kile anachotaka
kukueleza.Kama kuna
tofauti yoyote baina yenu
tuziweke kando kwa muda
na tuyaweke mbele maslahi
ya taifa” akasema Meshack
Jumbo
“Ninyi nyote hamjui
mnachokiongea.This man is
a threat to this country.Ni
mtu mbaya sana huyu na
sifahamu amewaeleza nini
hadi mkakubali kuacha
usingizi wenu na
kumsindikiza hapa kwenye
nyumba tukufu ya
watanzania !! Akaendelea
kufoka Dr Evans
“Mheshimiw Rais
naendelea kukuomba
niamini mimi niliyemleta
Mathew hapa kwako na
umsikilize japo kwa dakika
chache na baada ya hapo
utaamua kitu cha kumfanya
yeye pamoja na sisi ambao
tumemleta hapa
kwako.Naomba sana
mheshimiwa Rais” akasema
Joel.Dr Evans akamtazama
Mathew kwa dakika zipatazo
mbili akiwa na sura
iliyojikunja akionyesha
hasira za wazi kisha
akasema
“Nieleze hicho
unachotaka kunieleza lakini
wakati unanieleza andaa
majibu yote kuhusiana na
mtandao wenu na mahala
alipo mwanangu Coletha.Bila
kupata majibu hayo I swear
I’m going to eat you alive!!
akasema Dr Evans kwa ukali
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais” akasema
Mathew na kushusha pumzi
“Mheshimiwa Rais
ninaitwa Mathew
Mulumbi.Niliwahi kufanya
kazi katika idara ya ujasusi
na huyu hapa mzee Meshack
Jumbo ndiye aliyekuwa
mkurugenzi wangu hadi
nilipoachana na kazi hizo na
kwa sasa ninajishughulisha
na biashar…………….”
“Tafadhali sitaki
unipotezee muda wangu nina
kazi nyingi za kufanya usiku
huu kuhakikisha taifa
linakuwa salama hivyo sitaki
hadithi.Ninakufahamu
tayari wewe ni nani hivyo
nenda moja kwa moja katika
kile kilichokuleta hapa !!
akafoka Dr Evans
“Mheshimiwa Rais bado
hujanifahamu mimi ni nani
na yawezekana taarifa
ulizonazo hazijakupa picha
halisi ya kuhusiana na mimi
hata hivyo sitaki kupoteza
muda ngoja nijielekeze moja
kwa moja katika suala la
msingi lililonileta
hapa”akanyamaza kidogo na
kuendelea
“Siku moja nikiwa katika
klabu ya usiku nilikutana na
mwanamke mmoja ambaye
alijitambulisha kwangu
kama Olivia Themba na
tukawa marafiki
wakubwa.Katika urafiki
wetu nilibaini kwamba kuna
jambo lililokuwa
linamsumbua Olivia na siku
moja nilipomdadisi
akanieleza kwa ufupi
kwamba ana matatizo na
watu Fulani ambao hakutaka
kuniweka wazi ni akina
nani.Kwa kuwa ni mtu
wangu wa karibu nilichukua
jukumu la kuhakikisha
anakuwa salama hivyo
nikampa namba Fulani
ambazo nilimtaka azipige
wakati akihisi hatari au
akiwa katika hatari na
kupitia namba hizo mimi
nitafahamu mahala alipo
kisha nitakwenda
kumsaidia.Nikiwa jijini
Arusha katika mkutano wa
wadau wa maziwa nchini
nikapokea ujumbe kutoka
katika zile namba nilizompa
Olivia na baada ya muda
nikapata taarifa kwamba
Olivia Themba ametekwa na
watu wasiojulikana.Kupitia
program ile niliyompa Olivia
niliweza kugundua mahala
namba zili zilipopigwa hivyo
nikalazimika kuondoka
Arusha haraka na kurudi
Dar es salaam kwa ajili ya
kwenda kumuokoa
Olivia.Kabla ya kwenda
kumuokoa nililazimika
kuonana kwanza na wazazi
wake nikawaeleza
ninachotaka kukifanya na
wakaniruhusu nikamuokoe
binti yao.Nilipofika mahala
ambako niliamini Olivia
alikuwa amefichwa nikakuta
ameondolewa na nikakutana
na kikosi cha watu
walioandaliwa kwa ajili ya
kunimaliza.Nilifanikiwa
kupambana nao na
kuwashinda.Baada ya
kuondoka mahala hapo
nilipigiwa simu na Lucy
Themba mama yake Olivia
akanijulisha kwamba mume
wake Agrey Themba
amepigiwa simu na mtu
aliyejitambulisha kuwa ni
mimi na akadai kwamba
amempata Olivia na
kumuelekeza sehemu ya
kukutana.Nilistuka kwa
taarifa ile ikanilazimu kufika
mahala ambako mtu huyo
alitaka akutane na Agrey
lakini nilichelewa kwani
tayari Agrey alikwisha
tekwa.Nilimtaka Lucy
Themba anieleze kama kuna
mtu yeyote ambaye
walimueleza kuhusu mimi
kwenda kumuokoa Olivia
akadai hakuna mtu yeyote
waliyemueleza.Asubuhi Lucy
alinipigia simu na
kunijulisha kwamba
anahitaji kuniona kuna
jambo muhimu anataka
kunieleza.Nilipofika
nyumbani kwake kumbe
ulikuwa ni mtego nikatekwa
na kupelekwa mahala
nisipopafahamu”
akanyamaza akamtazama
Rais halafu akaendelea
“Nikiwa mahala hapo
nilipofungwa baadaya
kutekwa alikuja
mwanamama mmoja
akajitambulisha kwangu
anaitwa Devotha ambaye ni
mkurugenzi wa idara ya siri
ya usalama wa ndani wa nchi
akanieleza kwamba
wameniteka baada ya
kubaini ninashirikiana na
kikundi cha IS.Alinihoji
maswali mengi na
nikamueleza kila kitu
kuhusu mimi na Olivia
akaridhika kwamba sina
mahusiano yoyote na IS
lakini akanieleza kwamba
Olivia anashirikiana na
kikundi cha IS na kwa kuwa
mimi ni mtu wake wa karibu
waliamini lazima na mimi
nitakuwa mmoja
wao.Sifahamu nini
kiliendelea lakini baadae
nilikuja kukombolewa na
Devotha akiwa na mmoja wa
marafiki zangu.Nilimuuliza
sababu ya kuniokoa
akanieleza kwamba anataka
kuutafuta ukweli na
amenitoa ili nimsaidie
kuupata ukweli wa kile
alichokieleza
Olivia.Alinieleza kwamba
Olivia alitoa madai yakuwa
mbunge Edger Kaka ambaye
alifariki katika ajali ya gari
miaka mitatu iliyopita yuko
hai na kwamba wewe Rais
unalifahamu jambo hili na
unafahamu mahala alipo
ndiyo maana mwanao
akaambukizwa virusi hatari
ili kukushinikiza
uwaonyeshe alipo Edger
Kaka. Devotha anadai kuwa
Olivia alimuhakikishia anayo
siri kubwa na angempatia
siri hiyo endapo angemsaidia
kupata taarifa za mahala
alipo Edger Kaka.Kutokana
na msisitizo aliouonyesha
Olivia,ilimlazimu Devotha
kuamua kufanya uchunguzi
wa suala hili ili kubaini
ukweli na ndipo alipoamua
kudukua simu yako
kuchunguza kama
unalifahamu jambo hili
lakini hakufanikiwa kupata
chochote kwani alibainika
haraka.Aliposhindwa
kudukua simu yako akaenda
kuonana na Olivia akakuta
amehamishwa na ndipo
alipobaini kuwa amefungiwa
kila kitu kuanzia simu hadi
kadi zake zote na hivyo
kumlazimu kufanya
maamuzi magumu ya kuja
kunitoa kutoka mahala
nilikokuwa
nimefichwa.Haikuwa kazi
nyepesi kunitoa na ililazimu
watu kadhaa kupoteza
maisha.Baada ya kufanikiwa
kunitoa nilianza
kushirikiana na Devotha
kuutafuta ukweli kuhusu
Edger Kaka lakini wakati
tukiendelea kuna jambo
lilitokea.Devotha alimpiga
risasi mmoja wa watu wangu
halafu akatoweka na mpaka
sasa sijajua sababu ni nini na
ninaendelea kumtafuta”
akanyamaza akamtazama
Rais na wale wazee wawili
wote walikuwa kimya
wakimsikiliza
“Nimekusikia unataja
watu wako.Una jeshi,kikosi
au ni watu wako wa
IS?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
naomba niweke wazi
kwamba mimi si gaidi!!
Akasema Mathew
akionekana kukerwa na
maneno yale ya Rais
“Endelea Mathew”
akasema Meshack kwani
anamfahamu Mathew
akikasirika mambo
yanaweza
kuharibika.Mathew na Rais
wakatazamana kisha
akaendelea
“Nilianza kumsaka
Devotha kujua kwa nini
alimpiga risasi Ruby na
katika harakati za kumsaka
nikagundua kwamba
Devotha alikutana na Dr
Yonathan Cohen balozi wa
Israel hapa nchini” Mathew
akanyamaza baada ya kuona
sura ya Dr Evans
imebadilika.Wale wazee
wawili mle ndani nao
wakatazamana
“Kwa kuwa lengo langu
lilikuwa kumpata
Devotha,nililazimika
kumfuata balozi Dr
Yonathan nyumbani kwake
kufahamu mahala alipo
Devotha na sababu ya
kukutana naye usiku huu”
Mathew akakatishwa na
Rais
“Una maanisha ulivamia
nyumbani kwa balozi wa
Israel? akauliza Dr Evans
“Ndiyo mheshimiwa Rais
nililazimika kumvamia Dr
Yonathan katika makazi
yake”
“Jesus Christ ! akasema
Dr Evans na kumtazama
Mathew kwa hasira zaidi
midomo ikimtetemeka
alishindwa kutamka kile
alichotaka kukisema
“Mheshimiwa Rais”
Mathew akaendelea
“Kuna mambo
niliyagundua kutoka kwa
balozi Dr Yonathan.Kwanza
ni kuhusu Devotha”
akanyamaza tena kidogo na
kuendelea
“Devotha ni wakala wa
shirika la ujasusi la
Israel,Mossad”
“What?Dr Evans
akastuka
“Devotha ni wakala wa
shirika la ujasusi la Israel na
namba yake ya utambulisho
ni BRAVO 15E 361 A”
Uso wa Dr Evans
ulionyesha mstuko mkubwa
“Unamzungumzia
Devotha yupi?akauliza Dr
Evans
“Devotha Adolph
mkurugenzi wa idara ya siri
ya usalama wa ndani wa
nchi” akajibu Mathew na
Joel Mshana akastuka.
“Wait ! akasema na
kumtazama Mathew
“Unasema kuna kitu
kinaitwa idara ya siri ya
usalama wa ndani wa nchi?
“Ndiyo mzee.Kuna idara
hiyo” akajibu Mathew
“Inashangaza nimekaa
ndani ya serikali kwa miaka
mingi na sijawahi kusikia
kitu kama hicho.Kazi zake ni
zipi hasa hiyo idara? Nani
anaiongoza?Imeanzishwa
kwa sheria gani?akauliza
Joel
“Joel achana na mambo
hayo kwanza tujielekeze
katika suala la msingi
lililotuleta hapa” akasema
Meshack Jumbo
“Endelea Mathew”
akasema Meshack.Dr Evans
alikuwa kimya kabisa.
“Israel kupitia shirika
lake la ujasusi la Mossad
wamekuwa wakimtumia
Devotha katika mipango yao
ya kijasusi hapa
nchini.Usiku wa leo Devotha
aliitwa kwenda katika
ubalozi wa Israel kuonana na
majasusi wawili waliotumwa
na Mossad kuja Tanzania
kufanya maandalizi ya
kumtafuta Olivia Themba”
“Olivia Themba?!! Dr
Evans akastuka
“Ndiyo mheshimiwa
Rais.Mossad wanamtafuta
Olivia Themba na wametuma
watu wao wawili kuja
kufanya maandalizi kabla ya
kutuma kikosi cha majasusi
kuja Tanzania kumtafuta
Olivia na Devotha ndiye
anayewasidia katika
kuandaa operesheni hiyo”
“Oh my God ! kwa nini
kila mahali ni usaliti tu?
Devotha nilimuamini sana
lakini kumbe anashirikiana
na nchi za nje !! akasema Dr
Evans na kutikisa kichwa.
“Hao Mossad kwa nini
wanamtafuta Olivia?akauliza
Dr Evans
“Kuna historia fupi
hapa.Miaka mitatu iliyopita
mbunge wa bunge la jamhuri
ya muungano wa Tanzania
Edger Kaka alipatwa na
ugonjwa akiwa bungeni na
akapelekwa nchini Israel
ambako aliambatana na
Olivia”
“Ninafahamu hilo na
mimi ndiye niliyetoa ndege
impeleke huko
Israel”akasema Dr Evans
“Akiwa nchini
Israel,iligundulika kwamba
aliwekewa sumu kwa kusudi
la kumuua.Waziri mkuu wa
wakati huo alituma mtu
maalum wa kumlinda Edger
kwa siri akihofia kwamba
wale waliotaka kumuua
Tanzania wangeweza
kumfuata kule Israel na
kummalizia.Kachero huyo
wakati akiendelea na
shughuli zake za ulinzi kwa
siri aligundua watu wawili
waliofika kumtembelea
Edger hospitali usiku wa
manane.Ilimlazimu
kumshirikisha rafiki yake
kutoka Mossad na
wakagundua kwamba watu
wale ni Habiba Jawad na
Sayid Omar ambao
wamekuwa wakitafutwa na
serikali ya Israel kwa
kufadhili vikundi vya
wanamgambo wa kipalestina
ambao wamekuwa wakifanya
mashambulio kwa raia wa
Israel.Kitendo cha Edger
kutembelewa na watu hao
wawili kilimfanya awe ni
mtu muhimu sana kwa
Mossad na wakapanga
mipango ya
kumteka.Waliandaa
operesheni kabambe na
kumchukua Edger hapa
Tanzania.Walitengeneza
ajali ambayo sote tuliamini
kwamba ndiyo iliyochukua
uhai wa Edger Kaka lakini
ukweli ni kwamba Edger
Kaka hajafariki dunia.Yuko
hai bado” akanyamaza baada
ya kuona sura za Dr Evans
na Joel Mshana zimebadilika
“No this is not true !
Edger Kaka is dead !!
akasema Dr Evans
“Hapana mheshimiwa
Rais.Wote tuliamini hivyo
lakini ukweli ni kwamba
Edger Kaka bado yuko hai”
akasema Mathew.Ukapita
ukimya.
“Una uhakika gani kwa
hili unalotueleza
Mathew?akauliza Dr Evans
“Nimehakikishiwa na
balozi Dr Yonathan Cohen
kuhusu suala
hili.Nilimuuliza kama
unafahamu jambo hili au
kama unahusika kwa namna
yoyote ile akakiri kwamba
hufahamu chochote kuhusu
jambo hili kwani ni siri
kubwa ya Mossad.Kwa hiyo
mheshimiwa Rais madai ya
Olivia na IS kwamba
unafahamu mahala alipo
Edger Kaka si ya kweli
nimelithibitisha hilo”
akasema Mathew na Dr
Evans akashusha pumzi
“Thank you God !
akasema Dr Evans
“Olivia na kundi lake
walinituhumu kwamba
ninafahamu mahala alipo
Edger Kaka na
wakamuambukiza
mwanangu Coletha virusi
hatari ili kunishinikiza
niweze kuwaonyesha mahala
alipo Edger kitu ambacho
sikuwa nakifahamu
kabisa.Mimi na watanzania
wote tuliamini kwamba
Edger Kaka tayari
amekwisha fariki dunia
katika ajali kumbe ajali ile
ilikuwa ya
kutengeneza.Mathew kwa
mara ya kwanza
nakushukuru sana kwa
kuutafuta ukweli” akasema
Dr Evans na kumtazama
Mathew huku macho yake
yakionyesha kama yanataka
kulengwa na machozi.
“Where is Edger Kaka
now?akauliza Dr Evans
“Baada ya kumteka
Edger Kaka walimpeleka
nchini Kenya katika ubalozi
wa Israel ambako amekaa
kwa miaka mitatu akiteswa
na ndipo walipoamua
kutuma majasusi wawili
kutoka Tel Aviv kuja
kumuhoji ili awaeleze
mahala walipo Habiba Jawad
na Sayid Omar.Edger Kaka
aliwaambia majasusi wale
wa Mossad kama wanataka
awaeleze kila kitu
wanachokitaka basi
wamtafute na wampeleke
Olivia Themba”
“Why Olivia
Themba?akauliza Dr Evans
“Edger Kaka anadai
kwamba Olivia ni
mwanamke anayempenda
kuliko wote na yuko tayari
kuwaeleza Mossad kila kitu
wanachokitaka kama
wakimpata Olivia.Hiyo ndiyo
sababu ya Mossad kutaka
kutaka kufanya operesheni
hapa nchini kumtafuta
Olivia”Mathew akanyamaza
na kumtazama Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
nimemaliza kile nilichotaka
kukueleza.Sasa
ninajisalimisha kwako niko
tayari kwa ajili ya
kuchukuliwa hatua zozote
unazoona zinafaa” akasema
Mathew na kumsogelea Dr
Evans.Joel na Meshack
Jumbo wakabaki
wanashangaa.Dr Evans
akamtaza Mathew kwa muda
halafu akasema
“Take a sit ! akasema Dr
Evans na Mathew akaketi.
“Mathew Mulumbi
naomba toka ndani ya moyo
wako unisamehe sana kwa
yale yote niliyokufanyia bila
kujua.Mathew kijana wangu
sijui niseme nini unielewe
kwamba nilifanya yale yote
bila kujua nikiamini wewe ni
mmoja wa IS lakini naomba
unisamehe sana.Mambo
niliyokufanyia ni
makubwa.Ni mimi ndiye
niliyeagiza ukamatwe na
uwekwe kizuizini pale kitalu
1.Ni mimi ndiye .oh my God
!! Dr Evans akashindwa
kuendelea na kutazama
chini.Mathew akasimama
“Mheshimiwa Rais
ninasubiri amri yako.Niko
tayari kwa hatua zozote
utakazozichukua dhidi yangu
kwa yale yote niliyoyafanya!
Akasema Mathew Mulumbi
“Please Mathew take a
sit ! akasema Dr Evans
lakini bado Mathew
aliendelea kusimama
akimuangalia
“Mr
Presid…………...”Mathew
akataka kusema kitu lakini
Meshack Jumbo akamzuia.
“Mathew obey the order
please !! akasema Meshack
Jumbo kwa sauti kali
Mathew akageuka
akamtazama halafu
akaketi.Joel Mshana bado
aliendelea kushangaa kama
vile yuko ndotoni mambo
aliyoyasikia yalimshangaza
sana
“Mathew please listen to
me” akasema Dr Evans
“Kwa mambo
niliyokufanyia una haki ya
kuwa na hasira juu
yangu.Sistahili kabisa
msamaha wako hata kama
ningeomba mara elfu
moja.Kitu kimoja ambacho
nataka niweke wazi kwamba
nilifanya mambo haya bila
kujua na bila kufanya utafiti
wa kutosha kama kweli
unahusiana na mtandao wa
IS kama wote tulivyokuwa
tunaamini.Hata hivyo
Mathew narudia tena
kukuomba
msamaha.Naamini
haitakuwa rahisi
kunisamehe lakini kwa sasa
taifa letu linapitia kipindi
kigumu mno.Mpaka sasa
bado hatujapata idadi kamili
ya wale waliopoteza maisha
katika shambulio la bomu
lililofanywa katika hospitali
ya Mtodora na bado kuna
vitisho vya kuwepo kwa
mashambulio zaidi.Kama
Rais wako,kama mzazi,kama
mtanzania mwenzako
ninataka nikuombe tuweke
pembeni kila kitu
kilichotokea na tuungane
katika kuliondoa taifa letu
katika hatari hii
kubwa.Watu wameingiwa
hofu na usalama wa maisha
yao na jukumu letu ni
kuhakikisha tunaiondoa hofu
hiyo na waishi kwa amani”
akanyamaza kidogo halafu
akasema
“Mathew licha ya
vikwazo vyote
ulivyokumbana navyo
hukukata tamaa bali
umeendelea kupambana na
kuutafuta ukweli.Ulijua
ninakutafuta lakini bado
ulitafuta kila njia hadi ukaja
kuonana name kunifikishia
taarifa hizi nyeti
mno.Mathew wewe ni mtu
wa pekee na nchi yetu
imebarikiwa sana kukupata
mtu kama wewe.Nakuomba
Mathew Mulumbi jambo hili
uliloligundua na kuamua
kuja kunieleza lisiishie hapa
bali uhakikishe unalifikisha
mwisho.Nataka nikukabidhi
rasmi jukumu hili ulibebe na
ulimalize wewe mwenyewe
kwa namna unavyojua.Mimi
nitatoa kila aina ya msaada
unaohitajika.Naomba sana
Mathew” akasema Dr
Evans.Mathew akafikiri
kidogo na kusema
“Mheshimiwa Rais siku
zote katika maisha yangu
nimekuwa nikitanguliza
kwanza nchi yangu na ndiyo
maana kila pale linapotokea
suala ambalo linanihitaji
mimi kuwepo huwa sijiulizi
mara mbili kulifanya kwa
ajili ya nchi
yangu.Mheshimiwa Rais
licha ya yote yaliyotokea
lakini bado mimi na wewe
tunaweza kufanyakazi
pamoja na kuiondoa nchi
katika hatari.Nimelipokea
ombi lako na ninakuahidi
kuhakikisha ninatumia ujuzi
na uzoefu wangu wote
niliojaaliwa kulifikisha
mwisho.Ninachohitaji ni
ushirikiano mkubwa na
kuaminiana” akasema
Mathew
“Mathew nashukuru
sana kwa kukubali ombi
langu.Ninakuahidi
ushirikiano mkubwa sana na
kukupatia kila kile
utakachokihitaji.Wazee
wangu Joel na Meshack
ninawaomba msamaha sana
kwa maneno niliyowatamkia
hapo awali.Ni kweli nilikuwa
na hasira na Mathew na
ndiyo maana nikajikuta
nikitamka maneno yale bila
kujua.Nisameheni sana
wazee wangu ninahitaji sana
ushauri wenu katika jambo
hili naomba tuungane
pamoja tulivushe taifa katika
wakati huu mgumu.”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa Rais sisi
tumestaafu utumishi katika
taasisi lakini si kulitumikia
taifa.Bado tuna nguvu na ari
ya kulitumikia taifa letu na
kila pale itakapotulazimu sisi
tuko tayari kufanya kila lililo
ndani ya uwezo wetu
kuhakikisha nchi inakuwa
salama.Tuko tayari
kuungana nawe mheshimiwa
Rais pamoja na kijana wetu
Mathew katika kuhakikisha
tunamaliza kitisho hiki cha
usalama hapa nchini kwetu”
akasema Joel Mshana
“Nawashukuru sana
wazee wangu kwa kukubali
kwenu.Ninawaomba sasa
wote tuelekee katika chumba
cha mazungumzo ya faragha
ili tuweze kulijadili suala hili
kwa kina” akasema Dr
Evans.
Waliinuka wote
wakamfuata Rais
wakaelekea katika chumba
cha vikao vya faragha
“Karibuni sana” akasema
Dr Evans na baada ya wote
kuketi akasema
“Muda unakwenda kasi
sana hivyo bila kupoteza
muda tuanze mazungumzo”
akasema Dr Evans
“Mathew alizungumzia
jambo lililomstua sana Joel
Mshana kuhusiana na idara
ya siri ya mambo ya ndani ya
nchi.Ni kweli idara hii ipo
lakini inafanya kazi zake
kwa siri kubwa ndiyo maana
hata ndani ya serikali
haifahamiki.Idara hii iko
chini yangu na mimi ndiye
ninayeisimamia kwa kila
kitu.Idara hii niliiunda mimi
kwa siri kwa ajili ya
kunisaidia katika
kuhakikisha nchi inakuwa
salama na kuniwezesha
kutekeleza vyema majukumu
yangu ya kuongoza
nchi.Mtashangaa kwa nini
niunde idara hii licha ya
kuwa na majeshi na vyombo
vingine vya usalama lakini
idara hii ni muhimu sana
kwangu mimi kama
Rais.Hakuna fungu lolote la
bajeti kutoka serikalini ni
mimi mwenyewe ndiye
ninayejua fedha za
kugharamia idara hii
ninazipata wapi.Idara hii
imekuwa na mchango
mkubwa sana katika
kufanikisha shughuli
zangu.Naomba nisiendelee
zaidi kuizungumzia idara hii
ya siri bali tujikite katika
kile kilichotukutanisha usiku
huu” akanyamaza Dr Evans
baada ya sekunde chache
akaendelea
“Nilipokea mjumbe
maalum kutoka kwa Rais wa
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo ambaye aliniletea
ujumbe kwamba kuna raia
wangu mmoja ameonekana
jijini Kinshasa akifanya
mazungumzo na mtu
anaitwa Seif Almuhsin
ambaye anatoka kikundi cha
IS na kazi yake kubwa ni
kukusanya vijana kutoka
katika ukanda huu wa Afrika
Mashariki na Kati na
kuwapeleka katika kambi
zao za mafunzo
kuwafundisha
ugaidi.Nilionyeshwa picha za
mtu huyo nikamtambua
kuwa ni Olivia
Themba.Ilikuwa rahisi
kumtambua Olivia kwa kuwa
Mimi na baba yake Agrey
Themba ni marafiki
wakubwa toka tukiwa
vijana.Nilishangazwa sana
na Olivia kukutana na Yule
gaidi hivyo nikaelekeza idara
yangu ya siri kufanya
uchunguzi kujua sababu ya
Olivia kukutana na Yule
mtu.Uliandaliwa mpango na
Olivia akatekwa nyara
aliporejea nchini akitokea
Kinshasa.Naomba niwaweke
wazi wazee wangu kwamba
idara yangu ya siri ndiyo
waliofanya tukio lile la
utekaji wa Olivia lakini kwa
nia nzuri ya kutaka
kufahamu Olivia ana
mahusiano gani na IS.Katika
upekuzi akagundulika pia
amekuwa na mawasiliano na
mtu anaitwa Sayid Omar
huyu anatajwa kuwa mmoja
wa wafadhili wa
IS.Alipohojiwa zaidi
akawadanganya kwamba
atawaelekeza mahala alipo
Sayid Omar na akawapa
namba ambayo aliwataka
wapige akidai ni ya Sayid na
walipopiga tu mfumo wote
wa mawasiliano wa idara
hiyo ya siri ukajifunga.Olivia
alipotakiwa aufungue akadai
lazima aonane kwanza na
mimi.Nilijulishwa nikaenda
kuonana naye na akakiri
kwamba anashrikiana na IS
akaenda mbali zaidi kwamba
wamemuambukiza mwanagu
Coletha virusi hatari na
atapoteza maisha kama
nisipowaeleza mahala alipo
Edger Kaka.Olivia alisisitiza
kwamba Edger Kaka
hajafariki dunia na mimi
ninafahamu mahala
alipo.Nilidhani Olivia ana
matatizo ya akili lakini
aliendelea kuliwekea jambo
hili msisitizo
mkubwa.Baadae nilipata
taarifa kutoka kwa Agrey
Themba kwamba kuna mtu
amekwenda nyumbani
kwake anaitwa Mathew
Mulumbi na anadai kuwa
anafahamu mahala alipo
Olivia na alikuwa mbioni
kwenda kumuokoa.Ni kweli
mahala alikosema Mathew
ndiko alikokuwa
Olivia.Nikatoa maelekezo
Olivia ahamishwe na haraka
kabla Mathew hajafika na
kiwekwe kikosi maalum ili
kumkamata mara tu
atakapofika hapo,kwa bahati
mbaya Mathew aliweza
kupambana nao
akawamaliza na alinusurika
mtu mmoja pekee.Jithada za
kumuhoji Olivia zilionekana
kugonga mwamba
nikaelekeza baba yake Agrey
Themba atekwe ili
kumshinikiza Olivia aongee
lakini bado
haikusaidia”akanyamaza
akameza mate na kuendelea
“Kwa kushirikiana na
idara hiyo ya siri na mke wa
Agrey Themba tuliweka
mtego na kumkamata
Mathew Mulumbi ambaye
tuliamini anashirikiana na
Olivia na wote wako katika
mtandao wa IS.Niliagiza
ahojiwe tujue kila kitu.Kama
alivyoeleza Mathew
nilifahamishwa na watu
wangu kwamba kuna watu
wanajariku kudukua simu
yangu.Baada ya kufuatilia
nikagundua ni
Devotha.Nilishangaa sana
kwa nini aamue kufanya vile
ndipo nikaamua kumtoa
kabisa katika nafasi yake ya
ukurugenzi wa idara ya siri
na kuelekeza akamatwe
lakini kwa bahati mbaya
akaponyoka na baadae
nikapata taarifa kuwa
amemtorosha Mathew
Mulumbi.Nilikasirika sana
na kuelekeza kwamba kokote
wawili hawa
watakapoonekana wapigwe
risasi na kuuawa”
akanyamaza
“Nimeamua kuweka wazi
kila kitu ili tufungue
ukurasa mpya.Nilimkabidhi
Kaiza kazi ya kumuhoji
Olivia lakini hadi ilipofika
jioni hakuwa amepata
chochote na hali ya Olivia
haikuwa nzuri nikaelekeza
apelekwe shambani kwangu
akahudumiwe.Wakati Olivia
akiendelea kupatiwa
matibabu likatokea
shambulio la Mtodora.Katika
hospitali hiyo alikuwa
amelazwa mwanangu
Coletha na jengo
lililolipuliwa ndimo
alimokuwa amelazwa.Muda
mchache baada ya shambulio
lile kutokea nilipigiwa simu
na mtu ambaye alinijulisha
kwamba yeye ni kiongozi wa
kikundi kilichotekeleza
shambulio lile katika
hospitali ya Mtodora na
kwamba wanamshikilia
mwanangu Coletha”
akanyamaza baada ya nyuso
za Meshack na Joel
kuonyesha mstuko.
“Walinionya kwamba
nisithubutu kumueleza
yeyote suala hili wala
nisijaribu kuelekeza vikosi
vya usalama viwasake kwani
wangemuua mwanangu
Coletha.Walinitaka nifuate
maelekezo watakayonipa ili
mwanangu awe
salama.Walinitaka niwapatie
Olivia Themba”
Sura ya Mathew
ikaonyesha mstuko
“Uliwapa
walichokihitaji?akauliza
Mathew
“I’m so sorry
Mathew.Nakiri kwamba I
was stupid and
coward.Sikuyatanguliza
mbele maslahi ya Taifa na
nikaamua kuwapa kile
walichokitaka.I gave them
Olivia”
“Oh mon Dieu ! (Oh
Mungu wangu) akasema
Mathew kwa lugha ya
kifaransa na kusimama
“How could y…………”
akasema Mathew lakini
Meshack Jumbo akamzuia
“Mathew ! Respect !
akasema Jumbo kwa sauti
kali
“I’m sorry” akasema
Mathew na kuketi
“Mathew una kila haki
ya kuwa na hasira kwa hili
nililolifanya lakini naamini
hata kama ungekuwa wewe
mahala pamgu ungefanya
kama nilivyofanya
mimi.Mwanangu anateseka
hana kosa lolote na siko
tayari apoteze maisha ndiyo
maana nikawa tayari
kutekeleza maelekezo
waliyonipa” akasema Dr
Evans
“Nini kilifuata baada ya
kuwapa Olivia
Themba?Walimrejesha
mwanao?Mathew akauliza
“Hapana
Mathew.Sijapewa
mwanangu.Nimeambiwa
niwe mvumilivu bado kuna
mazungumzo kati yangu
nao.Nahisi kuna vitu vingine
watahitaji”
“Damn it !! akasema
Mathew kwa hasira
“Mathew I was alone and
scared.I didn’t know what to
do.Nilichokuwa nakihitaji ni
kumpata mwanagu akiwa
salama na ndiyo maana
nikafuata kila walichokitaka
wale jamaa.Nimeyaweka
haya mbele yenu nikiamini
kwamba tunaanza upya na
mwanangu atapatikana.Nina
imani kubwa nawe Mathew
kwamba utampata
mwanangu Coletha akiwa
mzima ndiyo maana
ninakubali kwamba
nilikosea”akasema Dr Evans
na kumtazama Mathew
“Mathew ninakuomba
unisaidie kumtafuta
mwanangu Coletha na
umuokoe pia Oliv…..”
“Ni hivi mheshimiwa
Rais” akasema Mathew na
kumkatisha Dr Evans
“Olivia alikuwa mtu
muhimu sana na ndiyo
maana watekaji hao
walimtaka kwa haraka kabla
ya kitu kingine
chochote.Tayari anafahamu
mipango yote ya IS hapa
nchini hivyo basi lazima na
sisi tuhakikishe tunamsaka
na kumpata kabla Mossad
hawajampata kwani nao vile
vile wanamtafuta
sana.Ninataka unipe
maelekezo yote namna
walichomchukua” akasema
Mathew na Dr Evans
akamueleza kila
kitu.Mathew akakuna
kichwa.
“Mheshimiwa Rais kwa
maelezo hayo ni wazi
itakuwa vigumu kujua
mahala alipo Olivia lakini ipo
namna moja tu ya kuweza
kumpata Olivia na Coletha
kutoka kwa hao watekaji”
akasema Mathew
“Nakusikiliza Mathew”
“Tayari tumekwisha
fahamu kwamba Edger Kaka
yuko hai na mahala
alipo,jambo lingine zuri ni
kwamba IS hawafahamu
mahala alipo bado
wanaamini yupo hapa
Tanzania kumbe yuko
Nairobi Kenya.Tunatakiwa
kuvamia ubalozi wa Israel
nchini Kenya na kumchukua
Edger Kaka kimya
kimya.Tukifanikiwa kwa hilo
tutakuwa na uhakika
mkubwa wa kuwapata Olivia
na Coletha” akasema
Mathew
“Kuvamia ubalozi wa
Israel na kumteka Edger
Kaka ?! akaulzia Dr Evans
“Huo ni mgogoro
mkubwa sana wa
kidiplomasia tunataka
kuuanzisha Mathew.Israel ni
marafiki zetu wa muda
mrefu na wamekuwa
wakitusaidia sana katika
mambo mbali mbali hatuwezi
kuingia katika mgogoro nao”
akasema Dr Evans
akionyesha wasiwasi
“Mheshimiwa Rais tayari
tupo kwenye mgogoro
mkubwa kati yetu nao”
akasema Mathew na Dr
Evans akaonyesha woga
“Kwanza kabisa ni wao
waliovamia ardhi yetu
wakafanya operesheni
wakaua na kumteka raia
wetu.Hata kama Edger
alikuwa na taarifa za
muhimu za watu
wanaowatafuta
hawakupaswa kufanya
walichokifanya.Walipaswa
kuishirikisha serikali ya
Tanzania katika jambo hilo
lakini kwa makusudi kabisa
waliingia katika ardhi yetu
na kufanya walichotaka
kukifanya.Mheshimiwa Rais
walichokifanya Israel ni
kitendo cha dharau kwa nchi
yetu hivyo uchokozi
waliuanzisha wao
wenyewe.Kama haitoshi hivi
sasa wanajiandaa kuja
kufanya operesheni nyingine
ya kimya kimya ndani ya
ardhi yetu kumtafuta Olivia”
akasema Mathew
“Mheshimiwa Rais
anachokisema Mathew ni
sahihi kabisa.Israel
walifanya makosa kuja
kufanya operesheni ndani ya
ardhi yetu wakaua watu
wetu na kumchukua mateka
raia wetu.Hiki ni kitendo cha
uchokozi mkubwa na bado
wanataka kurejea tena
kufanya operesheni ndani ya
ardhi yetu kimya
kimya.Kitendo hiki
hakivumiliki kabisa”
akasema Joel Mshana
“Usiku huu wa leo
nimevamia makazi ya balozi
wa Israel nikamteka nyara
yeye na mkewe pamoja na
kuwapa mateso hasa mkewe
ili kutafuta taarifa za Edger
Kaka.Kama haitoshi
nimekwenda pia katika
ubalozi wa Israel na
nimewaua majasusi wawili
ambao walitumwa kuja
kuandaa mpango wa
operesheni ya kumtafuta
Olivia.Huu ni mgogoro
mkubwa taya……”
“Unasema umeua raia
wawili wa Israel?!! Akauliza
Dr Evans
“Ndiyo mheshimiwa Rais
nimeua raia wawili wa Israel
ambao ni majasusi
waliotumwa kuja nchini
kuandaa operesheni ya siri
ndani ya ardhi yetu”
“Kwa nini umefanya
hivyo Mathew?Unafahamu
athari za hicho
ulichokifanya?akauliza Dr
Evans
“Mzee bila kufanya vile
nisingeweza kufahamu
mahala alipo Edger Kaka !
akajibu Mathew
“Hili jambo mbona
linakuwa kubwa na gumu
kulitatua? Naamini mapema
asubuhi nitapigiwa simu na
waziri mkuu wa Israel
akimuulizia balozi wake na
sintakuwa na jibu la kumpa”
“Mheshimiwa Rais
naomba unisikilize” akasema
Mathew
“Tunahitaji kufanya
operesheni kubwa katika
ubalozi wa Israel nchini
Kenya na kumchukua Edger
Kaka.Tulipaswa kuifanya
operesheni hiyo usiku huu
huu lakini tayari
tumekwisha chelewa kwani
yanatakiwa maandalizi ya
kutosha.Nashauri operesheni
hiyo ifanyike usiku wa kesho
au kesho kutwa hivyo basi
inatakiwa siku ya leo
kusivuje taarifa zozote za
kutekwa kwa balozi wa
Israel hapa nchini wala wale
majasusi wawili waliouawa
ndani ya ubalozi wa Israel
wasijulikane.Tukifanikiwa
kwa hili tutapata nafasi
nzuri ya kujiandaa kwa ajili
ya operesheni ya kumtwaa
Edger Kaka kutoka katika
ubalozi wa Israel nchini
Kenya”akashauri Mathew
“Mathew bado napatwa
kigugumizi namna hilo
unalolishauri
litakavyotekelezwa.Balozi
ametekwa na raia wawili
wameuawa.Oh God !
akasema Dr Evans
akionekana kukata tamaa.
“Mheshimiwa Rais jambo
hili linahitaji sana nguvu
yako kulimaliza” akasema
Mathew
“Hebu nielekezeni kitu
gani ninatakiwa
kukifanya?Kichwa changu
kimechoka” akasema Dr
Evans
“Ili tuweze kuingia
katika makazi ya balozi Dr
Yonathan ilitulazimu
kuwadhibiti kwanza askari
waliokuwa getini”
“Mliwadhibiti vipi?
Mliwaua? akauliza Meshack
Jumbo
“Tuliwafunga ili
wasiweze kutuzuia kufanya
kazi yetu.Wamefungwa
katika kichaka cha maua
karibu na geti.Vile vile yuko
mmoja ambaye alikuwa
amepoteza fahamu huyu
alikuwa analinda geti la
nyumba ya balozi.Hawa
askari wote wanatakiwa
waondolewe pale haraka
sana na wapelekwe sehemu
wakahifadhiwe hadi pale
tutakapokuwa tumemaliza
operesheni yetu hiyo
kesho.Jeshi la polisi
hawapaswi kufahamu
chochote kuhusu kutekwa
kwa balozi kwa sasa.Baada
ya kuwadhibiti kwanza
askari wale atafuata balozi
Dr Yonathan.Huyu kwa sasa
anashikiliwa katika makazi
yangu lakini nitamrejesha
nyumbani kwake ili asubuhi
aweze kwenda kazini.Lengo
la kufanya hivi ni kuzuia
watu wasijue chochote
kilichotokea usiku
huu”akasema Mathew
“Una hakika gani
kwamba balozi hatasema
chochote kwa serikali
yake?akauliza Dr Evans
“Hataweza kwa sababu
tunamshikilia mke
wake.Tutampa masharti
ayafuate na kama akienda
kinyume tutatishia kumuua
mke wake.Jambo la tatu
usiku huu kabla ya
kupambazuka tunatakiwa
kuiondoa miili ile miwili ya
wale majasusi wawili
waliouawa ndani ya ubalozi
wa Israel.Haya yanatakiwa
kufanyika kabla ya
mapambazuko.Tukisha
yakamilisha haya ndipo
tuanze kuandaa operesheni
ya kuvamia ubalozi wa Israel
nchini Kenya” Akasema
Mathew
“Mheshimiwa Rais
Mathew ameeleza vizuri
sana namna mambo
yanavyotakiwa kufanyika na
hata mimi ninakubaliana na
mawazo yake.Nguvu yako
inatakiwa sana katika suala
hili”akasema Meshack
Jumbo
“Sina kipingamizi katika
yale yote aliyoyaeleza ili
mradi tu awe na uhakika
kwamba yakitekelezwa
yatakuwa na manufaa”
“Mheshimiwa Rais hii ni
hatua ya kwanza ya kuondoa
mgogoro unaoweza kutokea
kati yetu na Israel wakati
tunajiandaa kwenda
kuvamia ubalozi wao nchini
Kenya.Nina uhakika
mkubwa kama tukikamilisha
haya niliyoelekeza kila kitu
kitakwenda vyema” akasema
Mathew
“Basi hakuna muda wa
kupoteza tuanze kwanza na
hawa askari waliokuwa
wanalinda geti la kijiji cha
mabalozi” akasema Dr Evans
na kuchukua simu
akampigia simu mkuu wa
jeshi la polisi
“Mheshimiwa Rais”
akasema mkuu wa jeshi la
polisi
“Afande IGP kuna jambo
nahitaji msaada wako wa
haraka sana” akasema Dr
Evans
“Ndiyo mheshimiwa
Rais”
“Katika kijiji cha
mabalozi kuna askari
wanalinda katika geti
kuu.Kuna kazi Fulani
niliwatuma vijana wangu
wakaifanye usiku huu pale
ndani na ikawalazimu
kuwadhibiti wale askari
lakini wote wako salama na
silaha zao zote
zipo.Ninawataka askari wale
waondolewe haraka sana
eneo lile na waletwe hapa
ikulu.Nataka wasiulizwe
chochote kuhusu kilichotokea
na simu zao zote zichukuliwe
ili wasiweze kuwasiliana na
mtu yeyote” akasema Dr
Evans
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais
ninatakakufamu je ni askari
wale tu wanaolinda geti kuu
au askari wote wanaolinda
kijiji cha mabalozi?
“Kwani ulinzi ukoje
katika kijiji cha
mabalozi?akauliza Dr Evans
“Kwa kawaida kuna
kuwa na askari watano
katika geti kuu la kuingilia
kijijini,wawili wanakuwa na
silaha wengine wawili
hawana silaha na mmoja
anakuwa na mbwa.Ukiingia
ndani pia kuna kuwa na
askari mmoja katika kila
nyumba ya balozi”
“Basi ninawataka wale
walioko geti kuu na Yule
anayelinda katika nyumba
ya balozi wa Israel”
“Sawa mheshimiwa Rais
nimekuelewa”
“Afande fuatilia suala hili
ili litekelezwe haraka kama
nilivyoelekeza” akasema Dr
Evans
“Sawa mheshimiwa Rais”
akasema mkuu wa jeshi la
polisi na Rais akakata simu
“Hilo la kwanza
limemalizika.Askari wale
wataletwa hapa na
nitaelekeza wapelekwe
katika nyumba ya
mapumziko wakapumzike
huko hadi kesho kutwa ndipo
watakapoachiwa huru.Nini
kinafuata baada ya
hapo?akauliza Dr Evans
“Kinachofuata ni kwenda
kumchukua balozi na
kwenda naye ubalozini ili
kuichukua ile miili ya wale
majasusi wawili waliouawa
na kisha tutamrejesha balozi
nyumbani kwake ili kuondoa
wasi wasi kwani
asipoonekana asubuhi
kutakuwa na tatizo.Katika
hilo la balozi tunahitaji
sehemu salama kwa ajili ya
kumuhifadhi mke wake pale
katika makazi yangu si
salama sana kwani tayari
Devotha anapafahamu na
anaweza akafanya
chochote.Tunahitaji sehemu
ambako tutamuhamishia
mke wa balozi ambako ni
salama zaidi” akasema
Mathew
“Kuhusu makazi salama
hakuna tatizo nina
mashamba mawili na yote
yana nyumba.Tutatumia
nyumba yangu iliyoko katika
shamba la Mikindu ambako
huitumia kama sehemu
yangu ya mapumziko”
akasema Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
ahsante kwa hilo.Nadhani ni
wakati wa kwenda kuanza
utekelezaji kwani muda
unakimbia sana.Tutaendelea
na majadiliano zaidi baada
ya kuhakikisha tumelimaliza
hili jambo” akasema Mathew
na kusimama
“Mathew ni vipi kama
wale magaidi wakinipigia
simu?akauliza Dr Evans
“Usiwe na hofu
mheshimiwa
Rais.Hawataweza kumuua
mwanao kwani wanaamini
wewe unafahamu mahala
alipo Edger Kaka hivyo basi
wakikupigia simu jitahidi
kutafuta namna ya kuvuta
muda ili tujipange kwanza
tumteke mtu wao na hapo
ndipo mchezo utakaponoga”
akasema Mathew
“Mathew una hakika
hawatweza kumuua
mwanangu hawa
jamaa?akauliza Dr Evans
“Niamini mheshimiwa
Rais,mwanao atakuwa
salama.Hawataweza
kumfanya kitu chochote”
akasema
Mathew.Akashikana mkono
na Rais wakaagana
“Mathew kabla
hujaondoka” akasama Dr
Evans na kumpatia Mathew
namba zake za
mawasiliano.Meshack Jumbo
na Joel Mshana wakapewa
gari la kuwarajesha
majumbani ili kumpa nafasi
Mathew ya kuwahi
kutekeleza jukumu lake
kabla ya mapambazuko.
“Mungu ameniwekea
roho ya ubishi ndani
mwangu na kutokukata
tamaa katika jambo lolote
lile na kuna nyakati
ninakuwa na ujasiri
uliopitiliza.Nina wasiwasi
siku moja roho hii ya ubishi
na kutokubali kushindwa
itaniweka katika matatizo
makubwa.Kitendo
nilichokifanya leo kilikuwa
cha hatari
kubwa.Nilijipeleka mimi
mwenyewe katika mdomo wa
Mamba.Ni vipi kama Rais
angekataa
kunisikiliza?Ningekuwa
katika hatari kubwa.Hata
hivyo ninashukuru Rais
amenielewa japo haikuwa
rahisi.Kwa sasa baada ya
kuweka mambo sawa
kinachofuata ni kupambana
na magaidi kuhakikisha
ninawafyekelea mbali wote
na kumpata Olivia akiwa
salama pamoja na
Coletha.Lakini kubwa zaidi
ni operesheni ya kuvamia
ubalozi wa Israel nchini
Kenya kumchukua Edger
Kaka.Hili halitakuwa jambo
rahisi na itakuwa ni
operesheni inayohitaji
maandalizi ya aina yake.Kwa
namna yoyote ile lazima
Edger Kaka apatikane!
Akawaza Mathew akiwa
garini akirejea katika makazi
yake baada ya kutoka ikulu
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 2
Mathew aliwasili katika
makazi yake na kumkuta
Gosu Gosu akiwa
amejiimarisha sawa sawa
kiulinzi.Hakuamini kumuona
Mathew akirejea akiwa
mzima.Akainua mikono juu
akamshukuru Mungu
“Ahsante Mungu kwa
kumrejesha salama
Mathew.Sikujua kama
ataweza kurejea salama”
akasema Gosu Gosu na
kumfuata Mathew aliyekuwa
anashuka garini
“Mambo yanakwendaje
hapa?akauliza Mathew
“Hapa ni salama kabisa
hakuna tatizo lolote” akajibu
Gosu Gosu
“Vipi maendeleo ya
wagonjwa?
“Wote wanaendelea
vyema.Vipi huko
utokako?Kuna
mafanikio?akauliza Gosu
Gosu
“Mungu
mkubwa.Mafanikio yapo
makubwa” akasema Mathew
na kuelekea ndani akaenda
kwanza kumtazama Ruby
ambaye bado alikuwa
amelala.Dr Hiran alikuwa
amejilaza sofani aliposikia
mlnago ukifunguliwa
akaamka
“Mathew”
“Dr Hiran mgonjwa
wangu anaendeleaje?
“Anaendelea vyema.Wote
wawili hawana tatizo
lolote.Yule mwingine
aliyekatika vidole
nimempatia huduma ya
kwanza lakini anahitaji
matibabu zaidi” akasema Dr
Hiran
“Ahsante sana Dr Hiran
kwa msaada huu
mkubwa.Naomba usinichoke
kila pale itakapokuwa
ninakuhitaji.Kesho
nitakuandikia hundi yako ya
malipo” akasema Mathew
“Mathew kitu cha
muhimu ni wagonjwa wetu
wawe wazima usiwaze sana
kuhusu malipo” akasema Dr
Hiran.Mathew akamchukua
Gosu Gosu wakaelekea
katika chumba cha kusomea
ambacho wanakitumia kama
ofisi yao
“Gosu Gosu huko
nilikotoka mambo ni mazuri
japo muda ni mfupi
kukuelezea kila kitu lakini
mambo yamekwenda vyema
kabisa.Nimetoka ikulu
kuonana na Rais”
“Dah ! Mathew wewe ni
kiumbe wa ajabu sana na
kuna nyakati
ninakuogopa.Umewezaje
kupenya hadi ukaingia ikulu
kuonana na Rais?akauliza
Gosu Gosu
“Naweza kusema ni
maongozi ya Mungu tu kwa
sababu kuna mambo
mengine yanatokea ambayo
hata mimi nakuwa
siyatarajii.Kwa ufupi
nimefanikiwa kuonana na
Rais.Haikuwa rahisi lakini
nimemueleza kile
tulichokipata katika
uchunguzi wetu na
kumfanya aingiwe baridi.Ni
mambo makubwa ambayo
hakuwa ametegemea
kuyasikia.Kuokoa muda ni
kwamba Rais yuko upande
wetu sasa na tumeufungua
ukurasa mpya.Tuko timu
moja sisi na yeye” akasema
Mathew
“Ashukuriwe Mungu”
akasema Gosu Gosu
“Amenieleza kila kitu
kilichotokea tukayaacha
yaliyopita yaende na kuamua
kuanza upya.Hata hivyo
kuna mambo yametokea
ambayo tusingeweza
kuyafahamu kama
nisingeonana naye.Kwanza
ni kuhusu shambulio la
Mtodora.Kama tulivyokuwa
tunahisi shambulio lile
lilimlenga mtoto wa
Rais.Muda mfupi tu baada ya
shambulio lile kutokea Rais
alipigiwa simu na kiongozi
wa kikundi kile kilichofanya
shambulio lile hospitali na
akamweleza kwamba
wamemchukua mwanaye
akamtaka afuate maelekezo
watakayompa.Rais
hajamueleza mtu yeyote
jambo hili kwani ni moja ya
masharti aliyopewa na
watekaji hao ili mwanae
aweze kuwa salama.Baada
ya hapo watekaji hao ambao
naamini ni IS walimtaka
Rais awapatie Olivia.Ili
kuhakikisha mwanae
anakuwa salama Rais
akalazimika kutekeleza kile
walichokitaka na akawapatia
Olivia.Mipango yetu
imekwama kwani Olivia
tayari yuko katika mikono ya
magaidi.Njia pekee iliyobaki
ni kumpata Edger
Kaka.Tukifanikiwa kumpata
huyu tutaweza kufahamu
mahala walipo Olivia na
Coletha pamoja na mambo
mengine mengi kuhusiana na
mtandao wa IS.Ili kumpata
Edger lazima tuvamie
ubalozi wa Israel nchini
Kenya.Hii ni operesheni
kubwa ambayo inatupasa
kujipanga vilivyo.Tutaitumia
siku nzima ya leo kujipanga
na kama ikiwezekana na
usiku wa leo au kesho
tutavamia ubalozi huo na
kumchukua Edger.Ili kupata
nafasi nzuri ya kufanya
maandalizi yetu tunapaswa
kuhakikisha kwamba
hakuna taarifa yoyote
itakayovuja kuhusiana na
hiki kilichotokea usiku huu
kuvamiwa kwa balozi wa
Israel na vile vile kuuawa
kwa wale majasusi.Mambo
haya yanapaswa kubaki siri
Israel wakijua kila kitu
kitaharibika na tutamkosa
Edger.Hivi sasa
tunamchukua balozi na
tunakwenda ubalozini
ambako tutachukua miili ile
ya wale watu wawili
tuliowaua na kuondoka nayo
kwenda kuificha mahali ili
kuondoa kabisa ushahidi
halafu tutamrejesha balozi
nyumbani kwake kujiandaa
kwa shughuli za leo na
kutakapopambazuka ataenda
ofisini kwake ili watu
wasijue kama kuna tatizo
lolote limetokea.Mke wake
tutaendelea kumshikilia na
tutamuhamishia katika
nyumba ya Rais ambako Rais
ametutaka tufanyie kila kitu
huko kutokana na usalama
kuwa ni mkubwa sana
mahala hapo”akasema
Mathew kisha wakaenda
katika chumba alimo
balozi.Gosu Gosu
akamfungua pingu
“Mke wangu
anaendeleaje? Ninaomba
nikamuone tafadhali”
akasema Balozi
“Usihofu balozi mkeo
utamuona lakini kwa sasa
tuna mazungumzo muhimu
na wewe” akasema Mathew
“Kitu gani zaidi
mnachokihitaji kutoka
kwangu? Taarifa zote
mlizozitaka nimewapa
mnataka nini tena?Tafadhali
naomba mtuachie mimi na
mke wangu tuondoke”
akasema Dr Yonathan
“Dr Yonathan suala hili
si rahisi kama
unavyodhani.Tayari
umeingia katika matatizo
makubwa sana na nchi
yako.Umetoa siri za taifa
lako lakini ulifanya hivi kwa
nia nzuri ya kujilinda wewe
binafsi na kumlinda mke
wako pia.Serikali ya Israel
wakifahamu hiki
ulichokifanya hawatakuacha
salama.Maisha yako yote
yaliyobaki utaishia gerezani.
Hawataangalia ulitoa siri za
nchi katika mazingira gani
lakini watakachokitambua
wewe ni msaliti kwa taifa la
Israel na haufai kuwa
kiongozi na utaishia gerezani
na yawezekana ukapotea bila
hata familia yako kujua na
huo ukawa ni mwisho
wako.Dr Cohen tunataka
kukusaidia ili haya yote
yaliyotokea usiku wa leo
yabaki kuwa siri na
tutakaofahamu ni sisi
pekee”akasema Mathew na
kumtazama Dr Yonathan
“Nini hasa
mnachokitafuta kwangu nyie
vijana?Mmenilazimisha
nikatoa siri za nchi na sasa
bado mnataka
kunilazim……..”
“Hatukulazimishi Dr
Cohen tunataka uamue wewe
mwenyewe kama unataka
suala hili libaki kuwa siri au
unataka serikali ya Israel
wafahamu kwamba ni wewe
uliyetupa taarifa zote za
kuhusu Edger Kaka ambaye
ni mtu muhimu sana kwa
serikali ya Israel na
walitumia gharama kubwa
kumpata.Tunakupa nafasi
hii ili uweze kuamua hatima
ya maisha yako.Muangalie
mkeo,itazame familia yako
na ufanye maamuzi
sahihi.Dr Cohen hakuna
mkamilifu hapa duniani kila
mtu anakosea lakini wewe
umelisaliti taifa lako kwa
ajili ya familia yako hivyo
basi usikubali familia yako
ikateseka pale
utakapokwenda
gerezani.Tunataka
kukusaidia Dr Cohen”
akasema Mathew.Dr
Yonathan akafikiri kwa
muda na kusema
“Hakuna namna
mnavyoweza kulifanya suala
hili likawa siri.Mliua askari
wanaotulinda katika makazi
yetu na kubwa zaidi mkaua
wale majasusi wawili wa
Israel tena ndani ya ubalozi
wetu.Jambo hili haliwezi
kubaki siri lazima
lijulikane”akasema
DrYonathan
“Sikiliza Dr
Yonathan.Askari wale
wanaowalinda katika makazi
yenu hawakuuawa bali
walidhibitiwa tu na tunao
uwezo wa kuwaziba midomo
yao na tukio lile likabaki
kuwa siri.Tunahitaji
ushirikiano wako Dr Cohen
ili jambo hili lisijulikane kwa
serikali ya Israel.Uko tayari
kushirikiana nasi?
“Nini hasa mnataka
kukifanya?akauliza Dr
Yonathan
“Tunataka utupeleke
ubalozini usiku huu kabla ya
mapambazuko tunakwenda
kuichukukua miili ile ya
wale majasusi waliouawa na
kuificha.Baada ya hapo
utarejea nyumbani kwako na
utaendelea na shughuli zako
kama kawaida ili asigundue
mtu yeyote
kilichotokea.Utawajulisha
Tel Aviv kwamba majasusi
wale wawili wanaendelea
vyema na maandalizi ya
operesheni yao na hakuna
tatizo.Saa nne za asubuhi
utaondoka ubalozini na
utakwenda mahala
nitakapokuelekeza.Mke wako
tutakuwa naye na kama
utafanya kinyume na
maelekezo yetu hautamuona
tena lakini ukifanya kama
tunavyotaka basi suala hili
litaendelea kubaki siri na
utaungana tena na
mkeo.Yeyote atakayekuuliza
kuhusu mkeo mjibu
amekwenda nje ya Dar es
salaam kwa
dharura.Usijidanganye
tafadhali kufanya jambo
lolote la
kijinga,tunakufuatilia.Umeni
elewa? akauliza Mathew
“Nimekuelewa lakini
mke wang…”
“Usihofu kuhusu mkeo
atapatiwa huduma zote na
atakuwa salama.Tekeleza
kile ninachokuelekeza na
mkeo utampata.Narejea
kukuonya kama ukifungua
mdomo wako na kusema hiki
kilichotokea hautamuona
tena mkeo.Nadhani
tumeelewana.Sasa inuka
tunaelekea
ubalozini.”akasema Mathew
na kumfuata Dr Hiran
“Dr Hiran tunaondoka
tena nitakuacha hapa
ukiendelea kuwahudumia
hawa wagonjwa wetu
wawili.Usihofu uko salama
na endapo kutatokea hatari
yoyote unijuze mara moja”
akasema Mathew
“Usihofu Mathew mimi
niko hapa hadi
kutakapopambazuka”
akasema Dr Hiran
Mathew akamuelekeza
Gosu Gosu kukusanya vifaa
vote watakavyovihitaji
katika kazi ile kisha
wakamchukua Dr Yonathan
wakaingia garini na
kuondoka kuelekea katika
ubalozi wa Israel.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 3
Gari tatu ziliwasili
katika geti la kuingilia kijiji
cha mabalozi.Hakukuwa na
mlinzi yeyote pale
getini.Mkuu wa jeshi la polisi
alikuwa amefika katika kijiji
cha mabalozi kutekeleza
agizo la Rais.Alifunguliwa
mlango akashuka eneo
likakaguliwa kisha
wakaanza kuwatafuta askari
walipo.Mbwa aliyekuwa
amefungwa katika mti ndiye
aliyewasaidia kufahamu
mahala walikokuwa
wamefungwa askari
wale.Pembeni kidogo ya
mahala alikofungwa mbwa
walikuwepo askari watano
wakiwa wamefungwa na
kubandikwa gundi midomoni
mwao ili wasiweze kupiga
kelele.Haraka haraka
wakafunguliwa na
kuhakikiwa kama wote ni
wazima wakapelekwa ndani
ya gari.Hawakuulizwa
chochote kilichotokea.Silaha
zao zilikuwa pembeni yao
nazo zikachukuliwa na
kuwekwa katika gari
lingine.Mkuu wa jeshi la
polisi akaelekeza afuatwe
askari mwingine ambaye
alikuwa analinda nyumba ya
balozi wa Israel.Gari
lilimfuata na baada ya muda
naye akaletwa
akaunganishwa na
wenzake.IGP akatoa
maelekezo ya kupelekwa kwa
walinzi wengine haraka sana
kuchukua nafasi za wale
askari kisha wakaondoka
kuelekea ikulu kama
alivyoelekeza Rais.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 4
Gari la Mathew
lilisimamishwa katika geti la
kuingilia ubalozi wa
Israel.Balozi Dr Yonathan
akashuka na kujitambulisha
kwa walinzi wakaruhusiwa
kupita.Moja kwa moja
wakaegesha gari katika
nyumba ambayo hutumiwa
na wageni maalum
wanaotembelea ubalozi
huo.Gosu Gosu akashuka
akiwa na masanduku mawili
makubwa wakaingia ndani
ya nyumba ile moja kwa
moja hadi katika chumba
ilimo miili ya majasusi wale
waliouawa.Bila kupteza
muda Gosu Gosu akatandika
turubai chini halafu
akachukua vifaa walivyokuja
navyo shoka dogo,panga na
kisu kikubwa kikali na
kuanza kuikata miili ile
vipanda vipande.Dr
Yonathan akafumba macho
asione kile kilichokuwa
kinaendelea mle chumbani
mara akaanza
kutapika.Hakuwahi
kushuhudia kitu cha namna
ile kwa macho yake ilikuwa
ni mara yake ya kwanza
kushuhudia mwili wa mtu
ukikatwa vipande vipande
kama nyama
“Nimeingia katika
mikono ya watu makatili
mno wasio na huruma hata
chembe.Sipaswi kuwafanyia
mchezo watu hawa ni
wanyama na
wauaji.Wanakata kata
wanadamu wenzao kama
nyama.Huu ni ukatili
mkubwa uliovuka mipaka”
akawaza Dr Yonathan
Gosu Gosu
hakumuangalia mtu usoni
aliendelea na zoezi lake la
kuikata ile miili alipomaliza
mwili wa Fishel akaviweka
vipande vyote katika mfuko
mkubwa wa nailoni halafu
akauweka kwenye sanduku
akalifunga akauchukua
mwili wa Ehud na kuufanya
vile vile kisha akaufunga
katika sanduku.Akakusanya
vifaa vyake akafanya usafi
mle ndani.Walihakikisha kila
kifaa chenye damu
wamekiondoa na baada ya
kujiridhisha kwamba hakuna
wasiwasi wowote mle ndani
wakayachukua masanduku
yale mawili wakayakokota
hadi katika gari lao
wakaondoka.Bado Dr
Yonathan alikuwa
anatetemeka mwili kwa
kitendo alichokishuhudia.
“Dr Yonathan ahsante
sana kwa ushirikiano wako
mkubwa.Suala hili
tumelimaliza na hakuna
yeyote atakayefahamu
kilichotokea.Itabaki kuwa
siri yetu na wewe utaendelea
kuwa salama.Tutakurejesha
nyumbani kwako ujiandae
kwa ajili ya siku ya leo
usionyeshe utofauti wowote
fanya kazi zako kama vile
hakuna kitu chochote
kilichotokea.Hakikisha
umewasiliana na Tel Aviv
ukawajulisha kuwa huku
mambo yanakwenda vyema
ili wasiwe na wasi wasi
wowote.Saa nne za asubuhi
nitakupigia simu na
kukuelekeza sehemu
utakayotakiwa
uende.Tafadhali naomba
ufanye kila nilichokuelekeza
ili wewe na mkeo muwe
salama.Sisi sio watu wabaya
lakini ukitulazimisha
tutakuwa wakatili
sana.Umenielewa
balozi?akauliza Mathew
“Nimekuelewa” akajibu
Balozi Dr Yonathan
“Safi” akasema Mathew
na kuelekea moja kwa moja
katika makazi yake.
“Gosu Gosu wewe
utashughulikia kuihifadhi
hiyo miili isigundulike mimi
ninamrejesha balozi
nyumbani kwake kwani
mapambazuko
yanakaribia.Tutakutana tena
hapa kwa ajili ya awamu ya
pili.Kama kuna tatizo lolote
nijulishe haraka sana
tafadhali.Tumia gari la Dr
Hiran” akasema
Mathew.Gosu Gosu
akashusha yale masanduku
yenye miili ya watu na
kuyapakia katika gari la Dr
Hiran.Mathew hakupoteza
muda pale nyumbani
akageuza gari na kuondoka
kumrejesha Dr Yonathan
nyumbani kwake.
“Jamani naombeni mnipe
nafasi walau nimuone mke
wangu nijue maendeleo
yake.Nimekubali kufanya
kila mnachokitaka kwa
sababu yake niruhusuni
walau nimtazame”akaomba
Dr Yonathan
“Usihofu balozi,mkeo ni
mzima na anaendelea
vyema.Fuata maelekezo
yangu na utaonana naye
tena lakini ukienda kinyume
na ninavyotaka hautamuona
tena mkeo” akasema Mathew
akiwa makini katika usukani
“Watu hawa ni akina
nani?Kitu gani
wanakitafuta?Wamewezaje
kufahamu kuhusu
mawasiliano yangu na
Devotha?Naanza kuhisi
yawezekana hawa jamaa
wakawa ni magaidi wa IS
ambao wanamtafuta Edger
Kaka” akawaza Dr Yonathan
na kugeuza shingo
akamtazama Mathew kwa
jicho la wizi
“Hawa lazima ni
magaidi.Inaniumiza sana
kuwapa siri mahala alipo
Edger Kaka ambaye nchi
yangu imetumia gharama
kubwa kumpata na ambaye
anategemewa sana
kuonyesha mahala alipo
Habiba Jawad mfadhili wa
vikundi vya ugaidi.Lakini
sikufanya hivi kwa kupenda
bali kwa ajili ya kuokoa
maisha yangu na maisha ya
mke wangu.Kama
nisingefanya vile wangeweza
kutuua sote kama
walivyowaua na kuwakata
kata akina Fishel na Ehud
bila huruma.Hawa si watu
wa kufanyia mchezo hata
kidogo.Ukatili wao umevuka
kile kiwango cha ukatili.Hata
wanyama si wakatili kiasi
hiki.Ninachomuomba Mungu
ni siri hii isijulikane kwamba
ni mimi ndiye niliyewaeleza
mahala alipo Edger
Kaka.Maisha yangu
yataishia
gerezani.Nimelitumikia taifa
langu kwa uaminifu kwa
miaka mingi lakini nimekuja
kuharibu mwishoni wakati
karibu ninastaafu.Nitafanya
kila linalowezekana ili jambo
hili lisijulikane” akawaza Dr
Yonathan.
Hakukuwa na
mazungumzo ndani ya gari
hadi walipofika katika geti la
kuingilia katika kijiji cha
mabalozi ambako
walisimamshwa na askari
balozi akajitambulisha
wakaruhusiwa kupita hadi
katika nyumba yake ambako
alikuta tayari amekwisha
letwa askari
mwingine.Mambo haya
yakaendelea kumshangaza
sana Dr Yonathan.
“Dr Yonathan umefika
nyumbani kwako utaendelea
na ratiba zako kama kawaida
asubuhi hii na usionyeshe
kama kuna kitu chochote
kimetokea.Kumbuka saa nne
nitakupa maelekezo ya
sehemu unakotakiwa uende
na ufanye hivyo haraka
sana.Unaweza kwenda”
akasema Mathew na Dr
Yonathan akafungua mlango
akashuka akaenda chumbani
kwake akamfungua
mtumishi wao wa ndani
ambaye alikuwa amefungwa
kamba
“Nyamaza usilie
Mariana.Mambo
yamekwisha”
“Balozi watu wale ni
akina nani?Mama yuko
wapi?akauliza Mariana
“Usihofu Mariana jambo
lile limekwisha tayari
tumekwishamalizana na
wale watu nimewapa
wanachokihitaji na sasa tuko
salama.Mama yuko hospitali
anapatiwa matibabu kwa
majeraha aliyoyapata”
akajibu balozi.Bado Mariana
aliendelea kulia
“Mariana naomba
unisikilize” akasema Balozi
Mariana akafuta machozi
“Hiki kilichotokea hapa
usiku wa leo kitabaki kuwa
siri ya hapa sitaki kivuke nje
ya mipaka ya nyumba
hii.Hatakiwi mtu yeyote
kufahamu.Hata akija mtu
yeyote kukuhoji usimueleze
chochote sema kwamba
hakujatokea
kitu.Atakayemuuliza mama
mwambie amesafiri kwa siku
chache atarejea.Umenisikia
Mariana?
“Nimekusikia”
“Vizuri
sana.Nitakuongeza
mshahara wako na
ninakuahidi nitakapoondoka
hapa Tanzania pale muda
wangu utakapokuwa
umemalizika nitaondoka
nawe kwenda kukutafutia
kazi huko nchi za Ulaya ili
uwe na maisha mazuri lakini
itunze siri hii asiifahamu
mtu yeyote” akasema balozi
Dr Yonathan na sura ya
Mariana ikajenga tabasamu.
“Sasa nenda kapumzike
kwa ajili ya kujiandaa
kuikabili siku” akasema Dr
Yonathan na Mariana
akatoka mle chumbani.
“Ee Mungu naomba
umlinde mke wangu huko
aliko awe salama hadi pale
tutakapoungana tena”
akaomba Dr Yonathan akiwa
amekaa kitandani akiwa
mwingi wa mawazo.Picha ya
kile alichokifanya Gosu Gosu
ubalozini ikamjia akakimbia
chooni kutapika
Mara tu Mathew
alipotoka katika kijiji cha
mabalozi akachukua simu na
kumpigia Rais
“Hallow Mathew”
akasema Dr Evans baada ya
kupokea simu
“Mheshimiwa Rais
nimekupigia kukupa taarifa
kwamba tayari tumemaliza
kazi kwa upande wa balozi
na hivi ninavyozungumza
nawe nimetoka kumrejesha
nyumbani kwake anajianda
kwa ajili ya kuanza shughuli
zake za siku”
“Kazi nzuri Mathew.Vipi
kuhusu wale jamaa
mliowaua kule ubalozini?
“Nako tayari pia
tumekwisha iondoa miili ile
na hakuna tena kitu cha
kuhofu.Vipi kuhusu wale
askari?
“Askari wale tayari
wamekwisha ondolewa na
nimeelekeza wapelekwe
katika nyumba ya
mapumziko na wakae huko
hadi tutakapokamilisha
operesheni yetu”
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais”
“Baada ya hatua hii ya
kwanza kukamilika nini
kinachoendelea?akauliza Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais,baada
ya awamu ya kwanza
kukamilika nitahitaji kuwa
na mazungumzo nawe ili
kupanga mikakati ya namna
ya kulitekeleza hili suala
lakini kabla ya kuonana
tunahitaji kuhamishia ofisi
yetu ya muda katika shamba
lako kama ulivyosema kwani
mahala tulipo sasa si
salama”
“Sawa Mathew
nitamtuma mtu wangu
atakufuata mahala ulipo na
ndiye atakayewapeleka huko
shambani kwangu.Kitu gani
kingine unakihitaji?
“Nitahitaji daktari nina
wagonjwa wawili ambao
wanahitaji kuendelea
kupatiwa matibabu”
“Sawa Mathew lakini
ningeomba tukutane asubuhi
kabla ya saa tatu kwani
nitakuwa na vikao vingi siku
ya leo hivyo jitahidi tukutane
mapema.Nadhani ingekuwa
vyema wewe ukaja kuonana
nami kwanza na hao
wagonjwa wako watapelekwa
shambani na watu wangu na
baada ya kutoka huku
utakwenda kuungana nao”
akasema Dr Evans
“Sawa mheshimiwa
Rais.Vipi kuhusu wale jamaa
wamekupigia tena simu
kutaka kitu
chochote?akauliza Mathew
“Hapana hawajanipigia
bado lakini naamini
watapiga asubuhi” akajibu
Dr Evans
“Kama tulivyokubaliana
mheshimiwa Rais endapo
wakipiga simu jitahidi
kuvuta muda ili tuweze
kupata nafasi ya kumaliza
kwanza operesheni yetu”
“Nitafanya hivyo Mathew
usiwe na shaka” akasema Dr
Evans na kuagana na
Mathew akakata simu
Tayari ni saa kumi na
moja za asubuhi Mathew
alipowasili katika makazi
yake.
“Dr Hiran wagonjwa
wangu wanaendeleaje?
“Wanaendelea vizuri
Mathew.Wote tayari wako
macho na maendeleo yao ni
mazuri sana” akasema Dr
Hiran
“Nakushukuru sana Dr
Hiran.Umenifanyia jambo
kubwa sana na fedha peke
yake haitoshi kulipia wema
huu ulionisidia.Umekesha
nami usiku kucha
ukiwahudumia wagonjwa
wangu.Nashukuru sana”
“Usijali Mathew kama
daktari ni jukumu langu
kuhakikisha wagonjwa
wanapona bila kujali kwanza
masuala ya pesa”
“Tayari kumepambazuka
ni wakati wako wa kwenda
kupumzika.Hundi yako
italetwa baadae ofisini
kwako na kama nitakuhitaji
tena nitakujulisha”
“Muda wowote Mathew
ukihitaji msaada wangu
mimi nipo tayari kukusaidia
kama rafiki yako hivyo kuwa
na amani”
“Ahsante sana Dr
Hiran.Utatumia gari langu
kwa muda,gari lako
aliondoka nalo Gosu Gosu
baadae atalirejesha kwako”
akasema Mathew na Dr
Hiran akaenda kuwaaga
wagonjwa Ruby na mke wa
balozi kisha akaingia katika
gari la Mathew na
kuondoka.Baada ya Dr Hiran
lkuondoka Mathew akaeleka
katika chumba alimo Ruby
“Mathew ! akasema
Ruby.Mathew akamfuata
pale kitandani akamuinamia
na kumbusu katika paji la
uso
“Unaendeleaje Ruby”
“Namshukuru Mungu
sijambo.Ahsante kwa
kuyapigania maisha
yangu.Siamini kama
ninaendelea kuvuta pumzi”
akasema Ruby
“Ruby sijui nimshukuruje
Mungu kwa muujiza huu
mkubwa.Nilimlilia sana
asiichukue roho yako kwani
bado ninakuhitaji sana
Ruby.Mungu amesikia ombi
langu na amekurejeshea tena
uzima.Ashukuriwe sana aliye
juu” akasema Mathew
“Mathew pamoja na
kumshukuru Mungu lakini
napaswa kukushukuru sana
wewe kwa namna
ulivyopambana kuhakikisha
ninapona.Ulifanikiwa
kumpata Yule shetani
Devotha? Akauliza Ruby
“Mambo mengi
yamefanyika usiku wa
leo.Yameibuka mambo
mengine ambayo hatukuwa
tunayafahamu.Nitakueleza
kila kitu pale utakapokuwa
katika hali nzuri kwa sasa
endelea kupumzika”akasema
Mathew
“Mathew I’m fine.Nieleze
kila kitu kilichotokea.Tell me
you killed that witch”
akasema Ruby
“Relax Ruby.Kwa hali
yako ya sasa unahitaji
mapumziko.Usiwaze sana
kuhusu haya masuala
yaliyotokea”
“Mathew that devil
almost killed me ! She shot
me three times.Tell me
you’ve killed her” akaendelea
kusisitiza Ruby na macho
yake yakaonyesha machozi
“Ruby kama
nilivyokueleza kwamba
yametokea mambo mengi
usiku wa kuamkia leo hivyo
sikuweza kufanikiwa
kumpata Devotha lakini
nitampata.Nakuhakikishia
kwamba lazima nitampata
na atalipa kwa hili
alilolifanya.Hataweza
kukwepa”
“Nini hasa kimetokea
usiku kilichosababisha
ukashindwa kumpata
Devotha?akauliza Ruby
“Nitakueleza baadae
Ruby”
“No Mathew tell me now
!! akasema Ruby na kutaka
kuinuka ili akae akagugumia
kwa maumivu
“Easy Ruby ! Easy”
akasema Mathew na
kumsaidia Ruby kukaa.
“I’m fine Mathew.Nieleze
kila kitu” akasema Ruby na
Mathew akalazimika
kumsimulia kila kitu
kilichotokea kwa usiku
mzima.
“Pole sana Mathew kwa
kazi kubwa uliyoifanya usiku
wa leo.Mambo
uliyoyagundua sikuwa
nimewahi hata kuyaota
ndotoni.Sikutegemea kama
suala hili lingekuwa kubwa
namna hii na hata
kuhusiana mataifa mengine”
akasema Ruby
“Hata mimi nilipoanza
kulichunguza hili suala
sikutegemea kama lingeweza
kuwa kubwa kiasi
hiki.Sikutegemea kusikia
Olivia anajihusisha na
mtandao wa kigaidi wa
IS.Sikutegemea kama suala
hili litamuibua Edger Kaka
ambaye nchi nzima
wanafahamu alifariki katika
ajali miaka mitatu iliyopita
lakini kumbe yuko
hai.Sikutegemea kama suala
hili lingeniingiza katika
mgogoro na Israel,katika
mgogoro na Mossad”
akasema Mathew
“Mambo yaliyoibuka hasa
usiku wa leo ni makubwa
sana.Nini kinachoendelea
sasa kuhusiana na suala
hili?akauliza Ruby
“Kikubwa ambacho
ilikuwa lazima tukifanye ni
kuhakikisha kwamba yale
yote yaliyotokea kwa usiku
wa leo yanabaki kuwa
siri.Serikali ya Israel
hawapaswi kufahamu kitu
chochote kuhusiana na
kuvamiwa kwa balozi wao na
wala kuuawa kwa majasusi
wao wawili na jambo hilo
tumelikamilisha na
kilichotokea kitabaki kuwa
siri.Baada ya kukamilisha
hatua ya kwanza
kinachofuata ni kuvamia
ubalozi wa Israel nchini
Kenya na kumchukua Edger
Kaka.Huyu ndiye
atakayetusaidia kuwapata
Olivia na Coletha.Vile vile
atatusaidia sana katika
kufahamu mipango yote ya
IS waliyoipanga hapa nchini”
akasema Mathew
“Kuvamia ubalozi wa
Israel?! Ruby akashangaa
“Ndiyo.Lazima tuvamie
ubalozi wa Israel na
kumchukua Edger Kaka
ambaye anahifadhiwa
ubalozini hapo”
“Hii ni operesheni kubwa
sana Mathew na ya hatari”
akasema
“Ndiyo ni operesheni
kubwa na ya hatari lakini
lazima tuifanye.Lazima
tumpate Edger Kaka kwa
gharama zozote zile na ili
tumpate lazima tuvamie
ubalozi wa Israel jijini
Nairobi” akasema Mathew
“Operesheni yenyewe
itakuwaje?akauliza Ruby
“Ninakwenda kujadiliana
na Rais asubuhi ya leo
namna ya kuunda timu ya
watu kwa ajili ya operesheni
hii”
“Tafadhali na mimi
niweke katika hiyo timu”
akasema Ruby
“Ruby ! akasema Mathew
“Mathew ninaomba na
mimi uniweke katika hiyo
timu.Unanihitaji sana”
akasema Ruby
“Ni kweli ninakuhitaji
sana Ruby lakini bado
unatakiwa kuendelea kukaa
kitandani ukiuguza
majeraha”
“Usihofu Mathew
nitakuwa salama.Nilikuja
hapa Tanzania kufanya kazi
na si kulala kitandani.Ni
kweli nina maumivu lakini
hayaweza kunizuia kufanya
kazi.Naomba Mathew
tusiweke mjadala katika
hilo.Ninao uwezo wa kufanya
kazi hata kama niko
kitandani” akasema Ruby na
Mathew akamtazama
“Nafahamu unachotaka
kukisema na tafadhali
usikiseme Mathew kwani
mimi ninao uwezo wa
kufanya kazi hata nikiwa
nimelala
kitandani.Operesheni kama
hii inanihitaji mno” akasema
Ruby
“Sawa Ruby kwa kuwa
umesisitiza mimi sina
kipingamizi
chochote.Nitakujum…………
…” akanyamaza baada ya
Gosu Gosu kuwasili
“Vipi mambo
yamekwendaje huko?
Akauliza Mathew
“Kila kitu tayari.Safari
yao imekwisha na
wapumzike kwa
amani.Hakuna
atakayewaona tena”
akasema Gosu Gosu
“Good job.Sasa nenda
kaoge ujiweke tayari muda
wowote tutaondoka hapa
kuelekea katika shamba la
Rais ambako ndiko ofisi yetu
itahamia”
“Tunaondoka
hapa?akauliza Ruby
“Ndiyo Ruby tunaondoka
hapa tunakwenda sehemu
salama zaidi” akajibu
Mathew.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 5
Kijua kilikwisha
chomoza wakati gari mbili
zilipofunga breki katika geti
la nyumba ya Mathew.Hawa
walikuwa ni watu
waliotumwa na Rais.Mathew
akawapokea na
kuwakaribisha ndani
akapewa maelekezo ya Rais.
“Gosu Gosu utaongozana
na hawa jamaa wawili mimi
natakiwa kuwahi ikulu sasa
hivi kuonana na
Rais.Nitakapotoka huko
nitakuja moja kwa moja
kuungana nanyi.Gari langu
utaondoka nalo” Mathew
akampa maelekezo kisha
akaingia katika mojawapo ya
zile gari mbili akaondoka
akiwaacha akina Gosu Gosu
wakijiandaa kuondoka
kuhamia katika makazi
mapya.
Hakukuwa na
mazungumzo katika gari ile
alilopanda Mathew hadi
walipofika ikulu akapelekwa
moja kwa moja kuonana na
Rais
“Mathew karibu sana
nimefurahi kukutana nawe
tena.Pole kwa kazi kubwa
uliyoifanya usiku wa
leo”akasema Dr Evanbs
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais” akasema
Mathew na Rais
akamuelekeza kiti aketi
“Mathew leo ni siku
itakayokuwa ndefu sana
kwangu,ratiba yangu
inaonyesha nitakuwa na
mfululizo wa vikao ndiyo
maana nimeona nizungumze
nawe kwanza kabla ya
mambo mengine
yoyote.Kabla hatujaendelea
una hakika kila kitu
kimekwenda kama
tulivyokubaliana? akauliza
Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
tumejitahidi sana
kuhakikisha kila kitu
kinakwenda sawa.Nakutoa
hofu mheshimiwa Rais
hakuna tatizo litakalotokea”
“Yule balozi una uhakika
naye hataweza kuwaeleza
watu wake kile kilichotokea?
“Hapana mzee hataweza
kwani mke wake
tunamshikilia sisi na
nimekwisha muonya kama
akifanya ujinga wa aina
yoyote ile hatamuona tena
mke wake.Kingine ambacho
kitamlazimisha asiweze
kutamka chochote ni woga
hataki Israel wagundue
kwamba yeye ndiye aliyetupa
siri zote kuhusiana na Edger
Kaka.Usiwe na hofu na
balozi mheshimiwa Rais
lazima atatupa ushirikiano
wa kutosha”
“Sawa Mathew kama una
uhakika hakutakuwa na
tatizo lolote ninakuamini”
akasema Dr Evans
“Ahsante sana
mheshimiwa Rais”
“Sasa tujielekeze katika
jambo hili
linalotukabili.Nimekuachia
wewe kila kitu ukiendeshe
katika suala hili nataka
kusikia namna ulivyojipanga
kulimaliza hili suala na
hatimaye mwanangu na
Olivia wapatikane” akasema
Dr Evans
“Mheshimiwa Rais kama
nilivyokueleza usiku kwamba
ili kulimaliza suala hili
tunatakiwa kumpata Edger
Kaka ambaye amefichwa
katika ubalozi wa Israel jijini
Nairobi”
“Mathew suala hili bado
linanipa ukakasi
mkubwa.Ninataka kumpata
Edger Kaka lakini si kwa
kuvamia ubalozi wa
Israel.Hili ni suala zito
Mathew na ninasita hata
kulikubali lifanyike kwani
endapo ikijulikana basi
kutakuwa na mzozo mkubwa
wa kidiplomasia na
tutakuwa tumepoteza rafiki
mzuri sana wa nchi
yetu.Hicho kinanipa hofu
sana Mathew” akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais Israel
wanamshikilia Edger Kaka
kwa sababu wanaamini ana
mahusiano na kikundi cha IS
na ndiyo maana walifanya
operesheni ile kubwa ya siri
na kumchukua wakaenda
kumficha Nairobi katika
ubalozi wao.Waliomteka
Coletha ni mtandao huu wa
akina Edger Kaka na tayari
wanafahamu kuwa Edger
Kaka yuko hai.Ili kuwapata
Coletha na Olivia lazima
tumpate Edger Kaka na
hakuna namna nyingine ya
kumpata Edger zaidi ya
kuvamia ubalozi wa
Israel.Hili ni suala kubwa
mheshimiwa Rais ni sawa na
kuvamia nchi lakini hatuna
namna nyingine ya kufanya
lazima tumpate Edger Kaka
kwa gharama zozote zile.Ni
mtu muhimu sana kwetu na
kuna maswali mengi ambayo
anapaswa
kuyajibu.”akasema Mathew
“Mathew hicho
ulichokisema ni kitu
ambacho kimenistua sana
hata mimi kusikia kwamba
Edger Kaka ana mahusiano
na magaidi.Hakuna
anayeweza kuamini jambo
hili kwani Edger alikuwa
mmoja wa wanasiasa vijana
aliyejizolea umaarufu
mkubwa sana hasa katika
mapambano ya
ufisadi.Alikuwa mstari wa
mbele katika kuanika ufisadi
na aliwataja mafisadi bila
woga wowote.Inashangaza
mno kusikia kwamba mtu
kama huyu ambaye
alionekana kama mkombozi
wa taifa kumbe
anashirikiana na magaidi.Ni
kweli kuna mambo mengi
ambayo tunahitaji
kuyafahamu kutoka kwa
Edger Kaka.” akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais
nadhani umeona umuhimu
wa kumpata Edger Kaka
kwa gharama zozote”
akasema Mathew
“Nakubaliana nawe
Mathew kwamba Edger ni
mtu muhimu sana lakini njia
ambayo umependekeza
kuitumia kumpata ndiyo
inayonipa hofu”
“Mheshimiwa Rais kuna
njia yoyote nyingine ambayo
unadhani inaweza
kutusaidia kumpata Edger
Kaka?akauliza Mathew.Dr
Evans akafikiri kidogo na
kusema
“Njia nyingine ya
kufanya kumpata Edger ni
kwa kufanya majadiliano na
serikali ya Israel” akasema
Dr Evans
“Hapana mheshimiwa
Rais hatuwezi kufanya
hivyo.Israel hawapaswi
kabisa kujua kama tayari
tunafahamu Edger yuko hai
ndiyo maana nashauri
tufanye operesheni ya kimya
kimya bila wao
kujua.Mheshimiwa Rais
operesheni hii si operesheni
rahisi lakini lazima tuifanye
na ninakuhakikishia
nitaiongoza mimi mwenyewe
na tutarejea hapa nchini
tukiwa n Edger
Kaka.Ninachohitaji ni
ruhusa yako mheshimiwa
Rais”
“Mathew ninaomba
nikueleze ukweli kijana
wangu ninatamani sana
kuruhusu operesheni hii
ifanyike lakini bado ninahofu
kubwa.Kwanza tunavamia
ubalozi wa nchi nyingine
ndani ya nchi ya jirani..Dah !
Dr Evans akashika kichwa
“Mheshimiwa Rais muda
unakwenda na mwenye
maamuzi ya mwisho ni
wewe.Mimi sina namna
nyingine ya kuweza kumpata
Edger Kaka na ninaomba
ufahamu kuwa bila kumpata
Edger Kaka itakuwa vigumu
sana kwetu kuwapata
Coletha na Olivia Themba”
akasema Mathew na kumpa
nafasi Dr Evans akatafakari
halafu akasema
“Mathew let us do it”
akasema Dr Evans lakini
bado macho yake yalionyesha
woga
“Ahsante mheshimiwa
Rais najua haya ni maamuzi
magumu umeyafanya lakini
yana faida kubwa kwa nchi”
“Tell me how’re you going
to do it?akauliza Dr Evans
“Mheshimiwa Rais
operesheni hii ni kubwa
mimi na watu wangu
hatuwezi kuifanya peke
yetu.Tunahitaji kuongezewa
nguvu”
“Nguvu ya namna gani
unaihitaji?
“Nahitaji watu mahiri”
“Watu wa aina gani
unawahitaji
Mathew?akauliza Dr Evans
“Ninahitaji watu wenye
mafunzo ya hali ya juu na
uwezo wa kupambana kwani
hii ni vita hivyo lazima watu
wanaokwenda kufanya
operesheni hii wawe na ujuzi
mkubwa katika mapambano”
“Nitakupa kikosi maalum
cha wanajeshi ambao
hutumiwa katika operesheni
maalum.Unadhani watu
wangapi watatosha katika
operesheni hii?akauliza Dr
Evans
“Naomba niongezewe
watu kumi ukijumisha na
watu wangu nilionao jumla
tutakuwa watu kumi na
nne.Tunatosha kabisa
kuvamia ubalozi wa Israel na
kumchukua Edger
Kaka.Operesheni itakuwa
namna hii.Tutatanguliza
kwanza majasusi kwenda
nchini Kenya kufanya
uchunguzi namna jengo lile
la ubalozi wa Israel
lilivyo,namna tunavyoweza
kuingia ndani na mahala
alipo Edger Kaka.Tukipata
ramani nzima ya jengo hilo
na tukifahamau namna
ulinzi ulivyo basi tutafanya
mazoezi namna ya kuweza
kuingia ndani ya hilo jengo
na kumchukua
Edger.Tutahitaji helkopta
mbili za kijeshi ambazo
hazitoi mlio na hazionekani
katika rada na zoezi la
uvamizi litafanyika usiku wa
manane” akasema Mathew
na kunyamaza baada ya
simu ya Rais kuita akaitoa
mfukoni na kuipokea
akazungumza halafu
akamgeukia Mathew
“Mathew nimetaarifiwa
kuwa nina wageni ambao
napaswa kuonana nao muda
huu.Mpango wako
nimeusikia ni mzuri na mimi
niko tayari kutoa kila aina ya
msaada unaohitajika.Kwa
kuwa bado maandalizi
yanaendelea nitakuomba
tukutane tena jioni hapa
hapa ikulu ili tuwe na
mazungumzo mapana zaidi
na unijuze mahala
mlikofikia.Nafahamu
operesheni hii inahitaji fedha
hivyo basi nimeandaa kiasi
Fulani cha fedha kwa ajili ya
kuanzia kazi” akainuka
akafungua kabati na kutoa
sanduku jeusi
“Humu kuna milioni mia
mbili thelathini na tatu.Hizi
ni kwa ajili ya kugharamia
operesheni hii hivyo basi
sehemu yoyote inayohitaji
kutumia fedha msisite
kutumia fedha na kama
ikimalizika mniambie nitatoa
nyingine.Mathew
ninakukabidhi kila kitu na
ninaamini kwamba mambo
yote yatakwenda vyema na
mwisho wa operesheni hii
nataka Coletha na Olivia
wapatikane.Naomba
nisikucheleweshe nenda sasa
hivi mkaanze maandalizi
kwa ajili ya operesheni
hii.Jioni tutakutana hapa
nataka uje na taarifa ya vifaa
vyote utakavyovihitaji ili
nivifanyie maandalizi”
akasema Dr Evans na
kuagana na Mathew
wakatoka ndani ya kile
chumba cha mazungumzo ya
faragha.Moja kwa moja
Mathew akaelekea katika
gari lililomleta na kuondoka.
“Nadhani hii itakuwa ni
moja kati ya operesheni
zangu kubwa kabisa kuwahi
kufanya tangu nimeanza
kazi hii ya ujasusi” akawaza
Mathew
“Katika operesheni hii
namuhitaji vile vile Tino.”
akaendelea kuwaza Mathew
na kumuelekeza dereva wa
lile gari sehemu ya kwenda
halafu akatoa simu na
kumpigia Tino
“Mathew kuna habari
gani?akauliza Tino
“Tino ninakuja hapo
nyumbani kwako
kukuchukua”
“Kuna nini
Mathew?akauliza Tino kwa
wasi wasi
“Usiogope Tino muda si
mrefu nitafika hapo ni kwa
ajili ya ile kazi imekuwa
kubwa zaidi kidogo” akasema
Mathew na kukata simu.
Kwa maelekezo ya
Mathew dereva wa lile gari
alifika hadi nyumbani kwa
Tino Mathew akashuka na
kuingia ndani
“Karibu sana
Mathew.Kuna tatizo
gani?akauliza Tino akiwa
amesimama akionekna kuwa
na wasiwasi
“Usihofu Tino hakuna
tatizo lolote lakini kuna
operesheni nyingine
imejitokeza ambayo
ninakuhitaji uwepo”
“Unanihitaji mimi?
“Ndiyo Tino.Nakuhitaji
sana katika operesheni hiyo”
“Inahusiana na nini hiyo
operesheni?
“Sitaki kuzungumzia
hapa lakini kwa ufupi tu ni
kuhusiana na kwenda
kumchukua Edger Kaka
kutoka katika ubalozi wa
Israel jijini Nairobi” akasema
Mathew na kumtazama Tino
“Tino hii ni operesheni
nzito na ya hatari sana hivyo
nahitaji sana msaada
wako.We need to do this for
our country”
“Mathe……”
“Tino please don’t say no!
I need you in this brother !
Tino akafikiri kidogo na
kusema
“Fine ! akaenda
chumbani kwake akavaa
shati na kutoka wakaingia
katika gari wakaondoka.
Mathew na Tino
walipelekwa moja kwa moja
katika nyumba ya
mapumziko ya Rais iliyoko
nje kidogo ya jiji.Tayari
akina Gosu Gosu walikwisha
fika.Kulikuwa na wahudumu
wawili wa kike na mmoja wa
kiume na tayari daktari
alikwisha wasili alikuwa
anawahudumia Ruby na mke
wa balozi
“Karibuni” akasema
Gosu Gosu wakaelekea ndani
“Kila kitu kiko vizuri
mahala hapa? Akauliza
Mathew
“Nimekagua kila kitu
kiko safi.Kuna watumishi
watatu hapa ndani kwa ajili
ya kutuhudumia na vyumba
vipo vya kutosha.Kuna ofisi
mbili ambazo tunaweza
kuzitumia zenye vifaa vya
kutosha ambazo huzitumia
Rais.Vile vile kuna chumba
cha tiba hapa ndani chenye
vifaa vingi ambacho unaweza
kukiita ni hospitali ndogo hii
ni kwa ajili ya Rais endapo
atapatwa na ugonjwa wakati
akiwa hapa.Humo ndimo
wanamohudumiwa akina
Ruby hivi sasa kwa ujumla
naweza kusema kwamba
nyumba hii imekamilika ina
kila kitu ambacho
kitatuwezesha kufanya kazi
zetu bila wasi wasi” akasema
Gosu Gosu na kumzungusha
Mathew kwa haraka haraka
katika nyumba ile halafu
wakarejea sebuleni Mathew
akamtaka Gosu Gosu awaite
watumishi wa ile nyumba
wakafika mara moja
“Ndugu zangu samahani
kwa kuwatoa katika kazi
zenu lakini nimewaiteni
hapa kwa ajili ya
kufahamiana.Yawezekana
mkawa mnajiuliza maswali
mengi kuhusiana na sisi ni
akina nani.Mimi naitwa
Mathew Mulumbi huyu
mwenzangu hapa anaitwa
Papii Gosu Gosu na huyu
hapa anaitwa Tino.Tuko
hapa kwa ajili ya kazi
maalum tuliyotumwa na Rais
na tutakuwepo hapa kwa
muda wa siku kadhaa kisha
tutaondoka.Naomba
kuwajulisha kwamba kuna
zoezi litakuwa linaendeshwa
hapa kwa siku hizo chache
tutakazokaa hapa hivyo
msiwe na wasi wasi pale
mtakapoona watu wakiingia
na kutoka humu ndani
ambao hamuwajui,msiwe na
wasi wasi mkisikia mtu
anapiga kelele za maumivu
au mkiona mtu akipigwa au
hata mkisikia mlio wa
risasi.Mko salama na
msihofu kitu.Endeleeni na
shughuli zenu kama
kawaida.Kama kutakuwa na
lolote la kuwajulisha
tutawajulisheni lakini
ninawaomba jambo
moja.Usiri.Chochote kile
mtakachokiona ndani ya
nyumba hii hakipaswi
kutoka nje.Naamini tayari
mnalifahamu hilo” akasema
Mathew na kuwataka wale
watumishi wakaendelee na
majukumu yao kisha
akawachukua akina Gosu
Gosu wakaenda katika moja
ya ofisi ya Rais
“Ni muhimu kuwaweka
sawa watumishi hawa ili
wafahamu kile
kinachoendelea na wasistuke
siku wakiona mtu anakatwa
kichwa humu
ndani.Tuachane na hayo
tuendelee na mambo
yetu.Nimetoka kuonana na
Rais tumezungumza japo si
kwa urefu sana kwani ratiba
yake kwa siku ya leo
imembana mno.Kitu
kikubwa ambacho Rais
alitaka kusikia kutoka
kwangu ni namna
tulivyojipanga kuhakikisha
tunawaokoa mwanae na
Olivia kutoka katika mikono
ya magaidi wanaowashikilia
hivi sasa.Nilimuweka wazi
Rais kwamba njia pekee ya
kuwapata watu hao ni
kwanza tumpate Edger Kaka
ambaye ana mahusiano na
watu hao na kumpata Edger
Kaka lazima tuvamie ubalozi
wa Israel nchini Kenya
ambako ndiko
amefichwa.Ndugu zangu
kuvamia ubalozi wa nchi
nyingine tena ndani ya nchi
nyingine ni jambo ambalo
lina athari kubwa sana
kidiplomasia lakini hatuna
namna nyingine ya kufanya
kumpata Edger Kaka zaidi
ya kuvamia ubalozi
huo.Baada ya
majadiliano,Rais akakubali
tufanye operesheni hiyo
lakini akatoa angalizo
kwamba tujitahidi kuifanya
kwa umakini mkubwa sana
na yeye yuko tayari kutoa
kila aina ya ushirikiano
kuhakikisha operesheni hii
inafanikiwa.Ameahidi
kutupatia makomandoo wa
kikosi maalum cha jeshi
ambao hutumiwa katika
operesheni maalum hivyo
tutakuwa na nguvu ya
kutosha.Tutakuwa jumla
watu kumi na nne kwani
Ruby naye ameomba
ajumuishwe katika
operesheni hii lakini yeye
atakuwa na kazi yake
maalum kama mnavyojua
yeye ni mtaalamu wa
kompyuta kwa hiyo atakaa
katika idara ya
mawasiliano.Tutatumia
helkopta za kikosi cha jeshi
kinachohusika na operesheni
maalum ambazo ni za kisasa
hazina mlio wala haziwezi
kuonekana katika rada”
akanyamaza kidogo
“Kitu kikubwa cha
kwanza ambacho tunatakiwa
kufanya ni kulifahamu
vyema jengo hilo la ubalozi
namna lilivyo ili tuweze
kujipanga namna ya kuingia
na kumchukua
Edger.Tunatakiwa kuipata
ramani ya jengo
zima,kufahamu mfumo
mzima wa ulinzi ulivyo ndani
na nje ya jengo na jambo la
tatu kubwa ni kufahamu
mahala alipofichwa Edger
Kaka.Hii ndiyo kazi kubwa
ya kwanza tunayotakiwa
kuifanya ambayo itatupa
urahisi wa kuweza kuingia
ndani ya jengo hilo” akasema
Mathew
“Uko sahihi Mathew
operesheni nzima
inategemea sana kama
tutafaulu kulifahamu jengo
hilo namna lilivyokaa na
mpangilio wote wa ulinzi”
akasema Tino.
“Kufuatia nchi ya Kenya
kuandamwa na mfululizo wa
matukio ya kigaidi mara kwa
mara ulinzi katika balozi
mbali mbali hasa za nchi
ambazo zimekuwa
zikipambana na vikundi vya
kigadi kwa muda mrefu
kama Marekani na Israel
umeimarishwa sana.Naamini
jengo hilo litakuwa na
teknolojia ya hali ya juu sana
ya ulinzi hivyo ili tuufahamu
mfumo mzima wa ulinzi
hatuwezi kuwakwepa
Mossad.Lazima tupate mtu
ndani ya Mossad ambaye
anaweza akatusaidia kutupa
taarifa zote za mfumo mzima
wa ulinzi ulivyo katika
ubalozi huo” akasema Tino
“Tino jambo unalolisema
ni sahihi na ninakubaliana
nalo lakini upo ugumu wa
kumpata mtu ndani ya
Mossad ambaye anaweza
akatusaidia kupata taarifa
nyeti kama hiyo.Ukumbuke
Edger amehifadhiwa pale
hivyo ni sehemu ambayo
wanaitazama kwa macho
matano” akasema Mathew
“Kwa nini tusipandikize
mtu ndani ya Mossad
ambaye atatumika kama
kirusi cha kuchota taarifa?
akauliza Gosu Gosu.
“Hilo nalo ni wazo
zuri.Kama hatuwezi
kumpata mtu ndani ya
Mossad basi tupandikize wa
kwetu” akasema Tino
“It’s not that simple guys
na inahitaji muda wa
kutosha hadi mtu huyo
kufanikiwa kumpandikiza
mtu huyo ndani ya Mossad
na sisi hatuna muda huo”
akasema Mathew
“Mathew nadhani
nimepata jibu.Devotha”
akasema Gosu Gosu
“What?! Akauliza
Mathew kwa ukali kidogo
“Mathew najua hili
halipenyi vyema katika
masikio yako lakini tunaye
mtu ambaye tunaweza
kumtumia katika operesheni
hii na akatusaidia sana
ambaye ni Devotha” akasema
Gosu Gosu.Mathew akatoa
kicheko kidogo
“Gosu Gosu umetoa wapi
wazo kama hilo?Yaani
tumshirikishe tena Devotha
katika mipango yetu?That
woman is a devil.She shot
Ruby three times,she nearly
killed her nitawezaje
kumsamehe mtu kama
huyu?Nitawezaje tena
kumjumuisha mtu kama
huyu katika timu
yangu?Hakuna namna
ninayoweza kufanya naye
kazi tena na nimeweka kiapo
popote nitakapomuona
Devotha I’ll kill her !
akasema Mathew
“Mathew wewe ni kaka
yangu ni kiongozi wangu na
ninakuheshimu
sana.Sijawahi kukupinga
katika jambo lolote,kila
ulichonielekeza
nimekifanya.Nafahamu unao
ujuzi mkubwa sana katika
mambo haya zaidi
yangu.Mimi ni mwanajeshi
tu na kazi yangu ni kupigana
vita lakini kwa mara ya
kwanza naomba unikubalie
na mimi hiki ninachokisema
ambacho ninaamini
kinaweza kuleta mchango
mkubwa katika operesheni
hii.Nafahamu alichokifanya
Devotha kinaumiza sana na
hata mimi nina hasira naye
lakini tunaweza kuweka
pembeni tofauti zetu kwa
muda na tukaungana
kufanya kazi pamoja kwa
manufaa ya nchi na baada ya
kumaliza kazi ndipo
tukaendelea na mambo yetu
binafsi.Samahani Mathew
kama nitakuwa
nimekukwaza kwa mawazo
haya” akasema Gosu Gosu
“Nadhani Papii amesema
kitu cha msingi sana.Kama
mwanamke huyo
anayemzungumzia anaweza
akawa na msaada katika
operesheni hii basi nashauri
ajumuishwe kama
itaonekana inafaa.Hii
operesheni ni kubwa sana na
kila ambaye anaweza kuwa
na msaada hata wa kupeleka
karatasi muhimu sehemu
Fulani basi atumike.Mathew
naungana na Papii
kukuomba kama utaona
inafaa mwanamke huyo
ajumuishwe katika
operesheni hii” akasema Tino
“Kwa nini alitaka
kumuua Ruby?Alimkosea
nini?Hili jambo limeniumiza
sana na kumfanya Devotha
awe ni adui yangu
mkubwa.Ruby hakustahili
kufanyiwa ukatili mkubwa
kama ule” akasema Mathew
“Mathew ninayafahamu
haya yote na unayo haki ya
kuwa na hasira na Devotha
hata mimi nina hasira naye
sana lakini kwa sasa lazima
tukubali kwamba
tunamuhitaji sana.”
Akasema Gosu Gosu na
Mathew akamtazama kwa
macho makali
“Gosu Gosu kwa nini
unadhani tunamuhitaji
Devotha katika operesheni
hii?akauliza Mathew
“Devotha ni wakala wa
Mossad hivyo itakuwa rahisi
kwake kuweza kuchota
taarifa za mfumo wa ulinzi
ulivyo katika ubalozi wa
Israel pamoja na mahala
alipo Edger Kaka ndani ya
ubalozi huo.Hivi ndivyo
tutakavyomtumia.Tutamtum
a Devotha kwenda
Nairobi.Akiwa kule Devotha
ataomba kuonana na mkuu
wa Mossad pale Kenya na
hapo ndipo atakapotumia
ujuzi na uzoefu wake kuchota
taarifa zile
tunazozihitaji.Simfahamu
vyema Devotha lakini kwa
namna nilivyofanya naye
operesheni ile ya kuja
kukukomboa ni mwanamke
mwenye uwezo mkubwa
sana” akasema Gosu
Gosu.Ilimchukua Mathew
zaidi ya dakika mbili
akitafakari halafu akasema
“Sawa nimekuelewa
Gosu Gosu.Japo moyo wangu
haufurahii jambo hili lakini
inabidi tulifanye kwa
manufaa ya taifa.Kama
tukitaka kumpata Devotha
lazima tumtumie balozi Dr
Yonathan.Yeye amekuwa
akiwasiliana naye kwa
kutumia mfumo wao wa
mawasiliano.Baadae saa nne
ninakwenda kukutana na
balozi Samawati beach
hotel.Pale pametulia sana na
ninafahamika ni hoteli ya
mmoja wa marafiki
zangu.Nitamuelekeza balozi
amjulishe Devotha naye afike
hapo hotelini kabla yeye
hajafika hapo na akishafika
tutamalizana naye.Tino
wewe utakwenda
kushughulikia tiketi tatu za
ndege ya saa saba mchana
inayoelekea
Nairobi.Mtasafiri nyote
watatu wewe,Gosu Gosu na
Devotha” akasema Mathew
“Hakuna tatizo katika
hilo” akajibu Tino.Mathew
akachukua simu na kupigia
Samawati beach hotel
akaweka oda ya chumba
akapewa chumba namba 98
halafu akampigia balozi Dr
Yonathan
“Hallow Mathew”
akasema Dr Yonathan baada
ya kupokea simu
“Dr Yonathan
nimekupigia kukukumbusha
kwamba saa nne za asubuhi
natakiwa kukutana nawe
Samawati beach hotel”
“Ninakumbuka Mathew
kwamba nina miadi ya
kuonana nawe mida hiyo”
“Vizuri sana kama
unakumbuka.Jambo lingine
ninamuhitaji Devotha”
akasema Mathew
“Devotha? Dr Yonathan
akauliza kwa mshangao
“Ndiyo namuhitaji
Devotha.Nataka utumie njia
zako mnazotumia
kuwasiliana na umtake afike
Samawati beach hotel
chumba namba 98 saa tatu
na nusu mwambie una
mazungumzo naye”
“Sawa Mathew nitafanya
hivyo.Vipi mke wangu
anaendeleaje?
“Usihofu anaendelea
vyema kabisa hana tatizo
lolote anapatiwa huduma
nzuri” akajibu Mathew na
kukata simu.
“Tino wewe utakwenda
kushughulikia hizo tiketi
mimi na Gosu Gosu
tutakwenda Samawati beach
hotel kuonana na balozi na
Devotha.Utatumia gari
langu,sisi tutatumia gari la
hawa wasaidizi wa Rais”
akasema Mathew na kwenda
katika chumba walimo Ruby
na mke wa balozi.Kilikuwa
ni chumba kikubwa ambacho
kilionekana kama hospitali
ndogokwani kulisheheni
vifaa vya kila aina vya
matibabu
“Ruby” akasema Mathew
akitabasamu baada ya
kumkuta Ruby akiwa
amekaa kitandani.Mathew
akasalimiana na Daktari
Yule aliyekuwa
anawahudumia akina
Ruby.Mke wa Dr Yonathan
alipomuona Mathew
alipatwa na mstuko mkubwa
akashindwa kujizuia kuanza
kulia.Mathew hakumjali
akamfuata Ruby
“Unaendeleaje
Ruby?akauliza
“Ninaendelea vizuri
Mathew kama unavyoniona”
“Sawa Ruby endelea
kupumzika ninatoka kidogo
nitakaporejea nitakuwa na
mazungumzo marefu nawe”
akasema Mathew
“Mathew unakwenda
wapi?Hapa ni wapi
tulipoletwa?
“Hapa ni sehemu salama
sana kwa wakati huu Ruby
usiwe na hofu yoyote hata
nisipokuwepo” akasema
Mathew
“Mathew tayari
umempata Yule
shetani?akauliza Ruby
“Usihofu Ruby mambo
yanakwenda vyema
nitakaporejea nitakuw na
mengi ya kukueleza”
akasema Mathew akambusu
Ruby katika paji la uso
akamuaga na kutoka mle
chumbani akimuacha mke
wa balozi
akitetemeka.Mathew
akazungumza na walinzi
akawataka wahakikishe
hakuna mtu yeyote kati ya
Ruby au mke wa balozi
anatoka ndani ya nyumba
ile.Wakaingia garini na
kuondoka
“Hili wazo la
kumshirikisha Devotha
katika operesheni hii
litamuumiza sana Ruby hata
hivyo kama Devotha
ataonekana kuwa na msaada
kwetu hakuna ubaya
tunaweza kumtumia halafu
mimi na yeye tutamalizana
baada ya operesheni hii
kumalizika” akawaza
Mathew wakiwa garini.
******************
Boti tatu ndogo za
mwendo kasi zilikaribia jiji la
Mombasa.Tayari ilikaribia
saa tatu za asubuhi.Boti hizi
zilikuwa zinatokea Pemba
nchini Tanzania ambako
walikwenda kwa ajili ya kazi
maalum.Hiki kilikuwa ni
kikosi kilichotumwa kwenda
Tanzania kuwachukua Olivia
Themba na
Coletha.Mawasiliano
yalikuwa makubwa kati ya
wale jamaa waliokuwa
katika zile boti na wenzao
waliokuwa wanawasubiri
sehemu Fulani kabla ya
kufika jiji la
Mombasa.Sehemu Fulani nje
ya bahari walikuwepo watu
kadhaa wakiwasubir wenzao
waliokuwa wakija na zile
boti.Kwa kufuata maelekezo
waliyokuwa wanapewa na
wenzao watu wale
waliziongoza boti zao
kuelekea ufukweni halafu
boti zikasimama wakashuka
watu na kuwashusha
wanawake wawili waliokuwa
wamefunikwa mifuko
kichwani.Wakawatoa nje
wakawakabidhi wanawake
wale kwa wale jamaa
waliokuwa nje wakiwasubiri
na bila kupoteza muda
wanawake wale wakaingizwa
katika helkopta iliyokuwa
mita chache kutoka
ufukweni.Watu wawili
kutoka katika zile boti nao
wakaingia katika helkopta
ile ikapaa na kuondoka
kuelekea Nairobi
TANZANIA
Gosu Gosu aliyekuwa
amejibanza sehemu fulani
katika hoteli ya Samawati
aliyaelekeza macho yake
katika maegesho alimuona
mwanamke mmoja mwenye
umbo lenye la kumtoa
udenda rijali yeyote akishuka
kutoka ndani ya gari na
kuanza kuelekea katika
jengo la hoteli.Haraka
haraka akachukua simu na
kumpigia Mathew
“Gosu kuna chochote
huko?akauliza Mathew
“Devotha amefika tayari
na anapanda huko juu”
“Good” akajibu Mathew
Devotha aliingia katika
lifti na kuelekea ghorofa ya
nne kilipo chumba namba
98.Gosu Gosu naye akatoka
katika mahala alipokuwa
amejificha akaenda kupanda
lifti nyingine naye akaelekea
ghorofa ya nne alipo Mathew.
Milango ya lifti
ikafunguka ghorofa ya nne
na Devotha akashuka kisha
akaanza kutembea huku
akiangalia namba za vyumba
akikitafuta chumba namba
98.Siku hii alikuwa amevaa
sketi ya jeans rangi nyeupe
iliyomkaa vyema na fulana
nyepesi ya rangi nyeupe
iliyoubana mwili wake na
kukifanya kifua chake kizuri
kionekane vyema.Alikuwa
amependeza sana.Alifika
hadi chumba 98 akabonyeza
kengele.Mathew aliyekuwa
ndani ya chumba
akachungulia katika kitundu
kidogo kilichopo mlangoni
akamuona Devotha.Mwili
wote ukafura kwa
hasira.Kwa kasi ya umeme
akaufungua mlango na
kumvuta ndani Devotha
ambaye hakuwa amejiandaa
kwa lolote akiamini kwamba
anakwenda kukutana na Dr
Yonathan,Mathew akaupiga
mlango teke ukajifunga
halafu akamkaba shingo
Devotha akamgandamiza
ukutani.
“Hatimaye nimekupata
shetani wewe !! akasema
Mathew kwa hasira akiwa
ameiweka bastora kichwani
kwa Devotha ambaye mwili
wote ulikuwa unamtetemeka.
“Mathew ! akaita Gosu
Gosu baada ya kuingia mle
ndani na kumkuta Mathew
akiwa amembana Devotha
ukutani huku bastora ikiwa
kichwani
“Mathew please brother !
akasema Gosu Gosu
“I promised to kill this
witch and I have to fulfill my
promise !! akasema Mathew
akiwa ameuma meno kwa
hasira.Gosu Gosu aliingiwa
na hofu kubwa kwa hasira
alizokuwa nazo Mathew.
“Mathew ukimuua
tutakosa kila kitu.We need
her so much.Please don’t kill
her ! akaomba Gosu
Gosu.Mathew akamtazama
halafu akamuachia Devotha
akainama akikohoa
mfululizo.Gosu Gosu
akamfuata
“Take a deep breath !!
akamwambia Devotha
ambaye alivuta pumzi ndefu
haraka haraka.Bado Mathew
alikuwa amesimama kati
kati ya kile chumba akiwa na
hasira.
“Take a sit ! Gosu Gosu
akamuelekeza Devotha aketi
halafu akamsogelea Mathew
“Mathew nadhani
tungemalizana kwanza na
Devotha kabla ya balozi
hajafika” akasema Gosu
Gosu kwa adabu.Mathew
aliyekuwa amegeukia
dirishani akageuka na
kumtazama Devotha kwa
hasira
“Ulifikiria nini Devotha
kumpiga risasi Ruby
?Alikukosea nini? Ulifikiri
sintakupata? Devotha
nakuhakikishia njia pekee ya
kunikwepa mimi ni
kufa.Kama uko hai ndani ya
dunia hii nikiamua kukusaka
ni lazima nikupate.Anyway
tuyaweke pembeni hayo
kwanza tuzungumze mambo
ya msingi.” Akasema
Mathew na kuiweka bastora
yake pembeni.
“Sifahamu nianzie wapi”
akasema Mathew na
kumtazama Devotha
ilionyesha wazi kwamba
hakuwa ameridhika
kumuacha Devotha bila
kumfanya chochote.
“Edger Kaka ni kweli
yuko hai” akasema Mathew
na mstuko ukaonekana usoni
kwa Devotha
“Yuko hai?akauliza
“Ndiy😵livia alikuwa
sahihi kabisa.Edger Kaka
yuko hai”akasema Mathew
huku hasira zikionekana
kuanza kupungua
“Hata mimi nilihisi
hivyo.Msisitizo aliouonyesha
Olivia ni mkubwa.Yuko wapi
Edger?Tayari mnafahamu
mahala alipo?akauliza
Devotha
“Ndiyo tunafahamu
mahala alipo” akajibu
Mathew
“Good.Sasa sikiliza
Mathew.Nilizungumza na
Olivia na akanihakikishia
kwamba ana siri kubwa
ambayo atanieleza endapo
nitampa taarifa za mahala
alipo Edger Kaka nadhani
sasa ni wakati wa kuifahamu
siri hiyo kubwa”akasema
Devotha
“I’m sorry Devotha
unaonekana uko nyuma ya
wakati sana.We don’t have
Olivia”akasema Mathew
“Olivia alichukuliwa na
Rais jana usiku na tuk…”
“Olivia hayuko kwa Rais”
akasmea Mathew na
kumkatisha Devotha
“What do you
mean?akauliza Devotha
“Nadhani unafahamu
jana usiku magaidi walifanya
shambulio katika hospitali
ya Mtodora.Mlengwa mkuu
wa shambulio lile alikuwa ni
Coletha mtoto wa Rais
ambaye walifanikiwa
kumchukua na kuondoka
naye.Rais alipigiwa simu
akajulishwa juu ya jambo lile
na akaonywa afuate kila
atakachoelekezwa ama sivyo
mwanae atapoteza
maisha.Kitu cha kwanza
walichokihitaji magaidi wale
ni Olivia Themba.Rais kwa
kuwa alihitaji kumpata
mwanae akalazimika
kuwapatia kile
walichokihitaji hivyo Olivia
Themba yuko katika mikono
ya magaidi hivi
tunavyozungumza na hatujui
yuko wapi”
“Bastard !! akasema
Devotha kwa hasira
“Kwa nini Rais akafanya
jambo kama hilo?Kwa nini
akawakubalia magadi kile
wanachokitaka?akauliza kwa
ukali
“Hakuwa na namna
nyingine ya
kufanya.Anahitaji kumuokoa
mwanae na mtu yeyote
angekuwa mahala pake
angefanya kama vile
alivyofanya Rais” akasema
Mathew
“So what’s going on
now?akauliza Devotha
“Devotha nataka kwanza
utambue tayari tunafahamu
kuwa wewe ni wakala wa
Mossad hapa nchini”akasema
Mathew
Uso wa Devotha
ulionyesha mstuko mkubwa
sana
“Mmef..fah…Oh my God !
Devotha akababaika
“Jana usiku ulikwenda
kuonana na balozi wa Israel
Dr Yonathan Cohen katika
ubalozi wa Israel hapa nchini
na kikubwa kilichokupeleka
kule ni kwenda kukutana na
majasusi wawili wa Mossad
waliotumwa Tanzania kwa
kazi maalum ya kuandaa
operesheni ya kumtafuta
Olivia na wewe kama wakala
wao wanakutumia katika
kuwasaidia kuandaa
operesheni hiyo” akasema
Mathew bado sura ya
Devotha ilikuwa katika
mshangao.Hakutegemea
kama akina Mathew
wangeweza kufahamu jambo
lile.
“It’s not true ! akasema
Devotha.
“BRAVO 15E 361 A ndiyo
namba yako ya
utambulisho.Devotha we
know everything about
you.Hakuna siri
tena.Naomba tusipoteze
muda kubishana jambo
hilo.Ninachotaka unieleze ni
je majasusi wale walikueleza
sababu ya kumtafuta Olivia
Themba?akauliza
Mathew.Zilipita sekunde
kadhaa Olivia akasema kwa
sauti ndogo
“Hapana
hawakunieleza.Niliwahoji
sababu za kumtafuta Olivia
lakini hawakutaka kuniweka
wazi kwa nini wanamtafuta”
akasema Devotha
“Sawa.Hawakutakakuku
weka wazi kwa sababu
anayemuhitaji Olivia ni
Edger Kaka”
“What? Sijakuelewa una
maanisha nini Mathew”
“Japokuwa wewe ni
wakala wa Mossad lakini
hulifahamu jambo hili.Akiwa
katika matibabu nchini
Israel Edger Kaka
alitembelewa na watu wawili
ambao wanatafutwa na
Mossad kwa muda mrefu
kwa kufadhili kundi la IS na
vikundi vingine vinavyofanya
mashambulizi katika ardhi
ya Israel na kuua
watu.Mossad ndio
waliotengeneza ajali ile
ambayo ilituaminisha
kwamba Edger amefariki
dunia lakini kumbe bado
yuko hai” akasema Mathew
“Oh my God ! akasema
Devotha akionekana
kushangazwa sana na taarifa
zile
“Baada ya kumchukua
Edger Kaka usiku ule
walimpeleka kumuhifadhi
katika ubalozi wa Israel
nchini Kenya ambako yuko
hadi hivi sasa.Kufuatia
mfululizo wa matukio ya
kurusha maroketi
yanayofanywa na vikundi
vya wanamgambo wa
kipalestina katika ardhi ya
Israel ambayo
yamesababisha vifo vya
wanafunzi kadhaa na
walimu,walitumwa majasusi
wawili kwenda nchini Kenya
kumuhoji Edger kwani
wamemuweka pale kwa
muda wa miaka mitatu bila
kumuhoji chochote.Katika
mahojiano hayo Edger Kaka
alikuwa tayari kuwaeleza
Mossad kila kitu
wanachokihitaji kwa sharti
la kuhakikisha wanampata
Olivia.Anadai kwamba
anampenda Olivia na ndiye
mwanamke anayetaka kuishi
naye.Hiyo ndiyo sababu ya
Mossad kuja kumtafuta
Olivia nchini
Tanzania”akasema Mathew
“Binafsi sikuwa tayari
kuwasaidia Mossad kumpata
Olivia kwani ninafahamu
umuhimu wake kwetu na
hata taarifa nilizowapa
hazikuwa za
kweli.Niliwaahidi
kuwasaidia lakini sina
mpango huo wa kuwasaidia
badala yake ninatafuta
namna ya kufanya ili
mpango wao huo usifanyike
hapa nchini”akasema
Devotha
“Huna haja ya kuwa na
wasiwasi nao tena.They’re
gone” akasema Mathew
“Gone?Where?akauliza
Devotha
“Dead.We killed them”
“Jesus Christ ! You killed
them?
“Yes we did” akajibu
Mathew
“Ahsanteni sana kwa
jambo hilo kubwa
mlilolifanya ila hili ni
tangazo la vita.Mossad
watawawinda usiku na
mchana hadi wahakikishe
wamewapata watu
waliowaua majasusi
wao.Mathew mmeingia
katika hatari kubwa
sana”akasema Devotha
“Tunajua,lakini
hawatafahamu chochote
kuhusiana na suala hilo
kwani tayari limekwisha
shughulikiwa kikamilifu”
“Mathew samahani
naomba nipewe nafasi ya
kuuliza swali.Mmewezaje
kufahamu mambo haya yote
hadi kuwaua wale
majasusi?Ni vipi mtafanya ili
Mossad wasiweze kugundua
kama majasusi wao
wameuawa? Ninauliza hivyo
kwa sababu mimi kama
wakala wao lazima
nitaulizwa mahala walipo
Fishel na Ehud.Moja kwa
moja tayari na mimi
nimekwisha ingia katika hili
jambo japo sikufanya mauaji
hayo” akasema Devotha
“Devotha hayo mambo
mengine hayana umuhimu
mkubwa.Akili na nguvu zetu
zote tuapaswa kuvielekeza
katika kuwatafuta Olivia na
Coletha ambao hatujui
mahala walipo hadi hivi
sasa.Ili kuwapata akina
Olivia lazima kwanza
tuhakikishe tumempata
Edger Kaka.Kuna njia moja
tu ya kumpata Edger Kaka
nayo ni kwa kuvamia ubalozi
wa Israel nchini Kenya
ambako ndiko amefichwa”
“Mathew mnataka
kuanzisha vita ! akasema
Devotha
“Thay started this
war.Tunachokifanya sisi ni
muendelezo wa kile
walichokianzisha
wao.Waliingia katika ardhi
yetu wakaua na kuteka raia
wetu wakiamini jambo hili
litabaki siri na
hatutalifahamu.Edger Kaka
ni raia wetu ambaye
ametekwa hivyo kila aina ya
mbinu itatumika kumrejesha
nyumbani na mbinu pekee
ambayo inatakiwa kutumika
kwa sasa ni kuvamia ubalozi
wa Israel nchini Kenya na
kumchukua na hapo ndipo
wewe unaingia” akanyamaza
Mathew akamtazama
Devotha kisha akaendelea
“Tunaandaa kikosi
kabambe kitakachofanya
operesheni ya aina yake ya
kumchukua Edger.Kitu
kikubwa kabla ya yote
ambacho kitatuwezesha sisi
kufanikisha operesheni hiyo
ni kupata ramani ya jengo
hilo lilivyo na vile vile
kufahamu mfumo mzima wa
ulinziulivyo na tatu
tunatakiwa kufahamu alipo
Edger Kaka ndani ya ubalozi
huo.Tulihitaji kupandikiza
mtu ndani ya Mossad lakini
muda tulio nao ni mfupi sana
ndiyo maana tukaamua
kukutumia wewe ambaye
tayari una mahusiano na
Mossad” akasema Mathew.
“Nini mnataka
nikifanye?akauliza Devotha
“Unakwenda
Nairobi.Nataka ukatafute
ramani ya jengo la ubalozi
wa Israel nchini
Kenya,mfumo wote wa ulinzi
wa ubalozi huo na mahal
alipofichwa
Edger.Tumekuchagua wewe
kwa kuwa tayari ni mtu wao
wa karibu unawasiliana nao
hivyo ni rahisi kuweza
kuingia kati kati yao na
kupata taarifa
tunazozihitaji.Naomba
ufahamu Devotha kwamba
katika operesheni hii
tunakutegemea
sana.Ukishindwa kufanikiwa
utakuwa umetuangusha
sisi,umemuangusha Rais na
umewaangusha pia
watanzania kwani
operesheni hii tunaifanya
kwa ajili ya Tanzania hivyo
nakuomba ufanye kila
unaloweza kulifanya ili
kupata taarifa hizo.Naomba
utambue vile vile kwamba
Rais Dr Evans ndiye aliyetoa
kibali cha kufanyika kwa
operesheni hii hivyo utaona
namna ilivyo muhimu.Rais
yuko pamoja nasi na
ametutuma tuifanye kazi hii
kwa niaba ya watanzania”
akasema Mathew
“Ni kweli mimi nina
ukaribu na Israel kupitia
shirika lao la ujasusi la
Mossad na ninawaahidi
kufanya kila linalowezekana
kuhakikisha ninazipata
taarifa hizo.Makao makuu ya
Mossad kwa ukanda huu wa
Afrika Mashariki yapo katika
ubalozi wao nchini Kenya na
ninafahamiana sana na Avi
mkuu wa Mossad kwa
ukanda huu.Nimekuwa
nikiwasiliana naye mara kwa
mara.Ninaamini kupitia
kwake tutaweza kupata kila
kitu tunachokihitaji.Mawazo
yangu bado ni kwa wale
majasusi wawili
mliowaua.Nina wasiwasi
kukosekana kwao kunaweza
kuharibu kila kitu ninaweza
kuulizwa maswali kuhusu
wao nikashindwa
kujibu”akasema Devotha
“Usihofu Devotha.Balozi
wa Israel Dr Yonathan
Cohen yuko na sisi katika
operesheni hii”
“Yuko nasi?Kivipi?
“Ni hadithi ndefu lakini
fahamu kwamba yuko
upande wetu.Yeye ndiye
atakayesimamia suala la
wale majasusi wawili kila
taarifa zao
zitakapotakiwa.Wewe
ukiulizwa utasema kwamba
kuna tetesi kwamba Olivia
baada ya kutekwa
amepelekwa jijini Arusha
hivyo basi majasusi hao nao
wamekwenda jijini Arusha
kufanya uchunguzi.Balozi Dr
Yonathan yeye ataendelea
kuwahakikishia Mossad
kwamba ana mawasiliano ya
mara kwa mara na majasusi
hao wakiwa jijini Arusha
hadi pale tutakapomaliza
operesheni yetu ambapo
balozi atadai kuwa
mawasiliano yamekatika
ghafla na hajui kama
majasusi hao wako salama”
“Mmewezaje kumuingiza
balozi Dr Yonathan katika
suala hili?akauliza Devotha
“Utafahamu hapo baadae
lakini kwa sasa kama
nilivyokueleza awali kwamba
tujielekeze katika
kuhakikisha operesheni hii
inafanikiwa” akasema
Mathew.
“Sawa Mathew mimi niko
tayari.Lini ninatakiwa
kwenda huko Nairobi?
“Unaondoka baadae
leo.Utaambatana na Gosu
Gosu na Tino”
“Tino?Who is he?
“Utamfahamu
baadae.Kwa pamoja
mtaunda timu ambayo
mtahakikisha mnafanikiwa
kuipata ramani hiyo ya jengo
la ubalozi wa Israel na
mtakuwa mkiwasiliana nasi
huku Dar es salaam kwa kila
mnachokifanya.Tino ni
mtaalamu sana wa
mawasiliano na
atatuunganisha sisi na ninyi
huko Nairobi” akanyamaza
Mathew baada ya simu yake
kuita.Alikuwa ni balozi Dr
Yonathan
“Hallo balozi”
“Mathew tayari nikefika
hapa hotelini uliponielekeza
tuonane” akasema Dr
Yonathan
“Njoo moja kwa moja
chumba namba 98 ghorofa ya
nne” akaelekeza Mathew
“Devotha kabla sijasahu
naihitaji ile kompyuta
ambayo uliichukua kutoka
kwa Ruby” akasema Mathew.
“Guys I don’t know how
to say this but I’m
sorry.Nilichokifanya ni kitu
kibaya na hata mimi
mwenyewe
ninakijutia.Sifahamu akili
yangu ilikuwa inawaza nini
hadi nikafanya kitendo
kile.Naombeni sana
mnisamehe” akasema na
kumtazama Mathew
“Is she….”
“She’s not
dead.Tumepambana kwa kila
tulivyoweza na Mungu
amesikia maombi yetu na
kumrejeshea uhai ila tayari
alikwisha chungulia kaburi”
“Please forgive me
Mathew”
“Sifahamu nitaanzia
wapi kukusamehe Devotha
kwa hiki
ulichokifanya.Umeniumiza
sana.Hujui ni kwa namna
gani Ruby alivyo mtu wangu
wa muhimu.Lakini hayo yote
tuyaweke pembeni kwanza
naomba ukafanye kazi
niliyokuag…………” Mlango
ukagongwa na Mathew
akanyamaza.Gosu Gopsu
akainuka kwenda
kuufungua,alikuwa ni balozi
Dr Yonathan.Devotha
akatazamana na Dr
Yonathan
“Huyu Mathew ni mtu
wa kuogopwa
sana.Amewezaje kumdhibiti
balozi na kumfanya afanye
kila
anachomuamuru?Sikutegem
ea kabisa kama angeweza
kugundua jambo kama hili la
mimi kuwa wakala wa
Mossad lakini tayari
anafahamu kila kitu hadi
namba yangu ya
utambulisho.Licha ya hilo
ameweza vile vile kuwaua
Ehud na Fishel.Huyu si mtu
wa kawaida napaswa
kumuogopa sana.Tayari
amekwisha niandika kwa
kalamu nyekundu hivyo
napaswa kuwa makini sana
kufuata maelekezo yake
vinginevyo he’s going to kill
me ! akawaza Devotha
“Balozi karibu
sana.Ahsante umefika kwa
wakati
tuliokubaliana.Nataka
kufahamu huko utokako nini
ninaendelea?Kuna tatizo
lolote kuhusiana na kile
kilichotokea jana? akauliza
Mathew
“Mpaka sasa kila kitu ni
shwari kabisa.Hakuna tatizo
lolote.Nimewasiliana na
mamlaka za juu na
kuwajulisha kwamba huku
kila kitu kinakwenda
vyema”akajibu balozi
“Vipi kuhusu wale
majasusi wawili?akauliza
Mathew
“Ehud na Fishel
walipofika hapa nchini
walifikia katika hoteli na
baadae ndipo wakaja
ubalozini ambako tuliwapa
nyumba inayotumiwa na
wageni wanaofika ubalozini
hapo hivyo hawakuwa
wamerudisha vyumba
vyao.Wakati ninakuja huku
nimepita katika hoteli
walikofikia kuwafahamisha
kwamba wageni wale
hawatarejea tena pale
hotelini na nikalipa kiasi
chote cha fedha walichokuwa
wanadaiwa.Viongozi wa
Mossad niliwasiliana nao
asubuhi ya leo nikawajulisha
kwamba watu wao
wanaendelea na maandalizi
ya operesheni na
wameelekea Arusha”
akasema Dr Yonathan
“Vizuri.Nafurahi kama
mambo yamekwenda vyema”
akasema Mathew
“Vipi mke wangu
anaendeleaje? Akauliza
balozi
“Yuko vizuri usihofu”
akajibu Mathew
“Balozi nimekuita hapa
kuna mambo ambayo
tunataka utusaidie”akasema
Mathew na kumtazama
balozi halafu akaendelea
“Israel kwa kutumia
shirika lao la ujasusi la
Mossad walivamia ardhi yetu
wakaua na kuteka raia wetu
wakampeleka
mafichoni.Walifanya kitendo
kibaya sana na kama
haitoshi wanajiandaa tena
kuvamia ardhi yetu na
kufanya operesheni nyingine
ya kumteka raia mwingine
wa Tanzania na kumtorosha
na hatujui katika operesheni
hiyo watanzania wangapi
watapoteza maisha
yao.Israel ni marafiki zetu
lakini kwa hiki
walichokifanya
hatukubaliani nacho hata
kidogo.Mheshimiwa balozi
tunamuhitaji mtu wetu
aliyetekwa na Israel na
kwenda kufichwa katika
ubalozi wenu nchini
Kenya.Hatuhitaji
majadiliano yoyote kwani
wao wakati wakimchukua
hawakujadiliana nasi hivyo
na sisi tunataka kumchukua
kama wao walivyomchukua
yaani kimya kimya”
akanyamaza akamtazama
balozi aliyekuwa kimya
akimsikiliza halafu
akandelea
“Nafahamu umuhimu wa
Edger Kaka kwa Israel lakini
huyu ni raia wa Tanzania na
tunamuhitaji vilevile hasa
kwa wakati huu hivyo basi
tunaandaa operesheni ya
kwenda kumchukua mahala
alikohifadhiwa jijini Nairobi
katika ubalozi wenu na
tunahitaji msaada wako”
Dr Yonathan alijitahidi
kuficha woga alioupata lakini
vidole vyake vilikuwa
vinatetemeka.Mathew
aliligundua hilo lakini
hakumjali
“Devotha ambaye ni
wakala wa Mossad
anakwenda jijini Nairobi
ambako atakutana na mkuu
wa Mossad katika ukanda
huu wa Afrika Mashariki na
kati ndugu Avi.Tunamtuma
Devotha kwa kazi maalum
katika ubalozi huo hivyo
atahitaji msaada wako pale
atakapohitaji”akanyamaza
tena akamtazama balozi
“Devotha atamjulisha Avi
kwamba majasusi wale
wawili wa Mossad wako jijini
Arusha na Avi akikuuliza
utamthibitishia hivyo
kwamba kweli wako
Arusha.Ukumbuke bado
tunakufuatilia Dr Yonathan
na kosa moja utakalolifanya
litagharimu uhai wa mke
wako na wewe pia.Hii ni
operesheni ya kitaifa na
lazima ifanikiwe kwa
gharama zozote zile na
kumrejesha Edger Kaka
Nyumbani.Umenielewa?
akasema Mathew
“Kwa upande wangu nina
wasiwasi mkubwa na hicho
mnachotaka
kukifanya.Ninawashauri
msikifanye kwani ni hatari
kubwa na kitazidi kuyaweka
mahusiano ya nchi zetu mbili
katika mashaka
makubwa.Serikali ya Israel
wakigundua hiki
mlichokifanya mtajiletea
matatizo makubwa ninyi na
taifa lenu.Nawahakikishia
kwamba hakuna
atakayeshiriki katika jambo
hili atakayebaki salama”
akasema Dr Yonathan
“Dr Yonathan naomba
ufahamu kwamba
tunachokifanya sisi ni
muendelezo wa kile
walichokianzisha
Israel.Walivamia ardhi yetu
wakaua na kumteka raia
wetu,tunachokitaka sisi ni
kumkomboa Raia wetu
ambaye walimteka hivyo huu
si uvamizi bali tunakwenda
kumchukua raia wetu ka
kutumia njia ile ile
waliyoitumia wao”akasema
Mathew
“Edger Kaka ni mtu
muhimu sana kwa nchi
yangu.Ni yeye ambaye
tunamtegemea atuonyeshe
mahala walipo wafadhili
wakuu wa vikundi vya ugaid
ambavyo vinaendelea kuua
waisrael”
“Tunajua umuhimu wake
kwa nchi yako lakini ukweli
unabaki pale pale kwamba
huyu bado ni raia wetu na
kama Israel inamuhitaji basi
wanatakiwa kufuata taratibu
kwa kuwasiliana na
mamlaka zetu husika.Edger
Kaka ni mtu muhimu sana
kwetu pia hivyo lazima
tumrejeshe nyumbani”
akasema Mathew
“Siwashauri mfanye hivi
jamani.Mtaibua jambo zito
amb……….”
“Dr Yonathan hauna
uwezo wowote wa kutuzuia
kufanya
chochote.Tunakwenda Kenya
kumchukua Edger Kaka na
kumrejesha nyumbani na
hakuna wa kutuzuia si wewe
wala taifa lako la
Israel.Ninataka utoe
ushirikiano kila pale
utakapotakiwa ufanye
hivyo.Umenielewa Dr
Yonathan? Akauliza Mathew
“Sawa nimekuelewa
lakini msije laumu huko
mbeleni kwamba
sikuwaonya” akasema Dr
Yonathan
Majadiliano yaliendelea
kisha Dr Yonathan
akaondoka zake.
“Nadhani hakuna tena
cha ziada kila kitu tayari
kimewekwa wazi ni wakati
wa kwenda kujiandaa kwa
safari” akasema Mathew
“Vipi kuhusu
silaha.Hatujui huko
tuendako tutakutana na
hatari gani hivyo lazima
tujihami
kw……………”akasema
Devotha lakini Mathew
akamkatisha
“Usihofu kuhusu
hilo.Tino atashughulikia kila
kitu na silaha zitapatikana”
akajibu Mathew.
“Kuna lingine unataka
kulifahamu?akauliza
“Mathew we have a
problem” akasema Devotha
“What problem?
“Rais aliniamini akanipa
idara niingoze lakini jana
nilifanya mambo
yaliyonifanya nikawa adui
yake mkubwa.Nilidukua
simu yake na vile vile
kusababisha mauaji
makubwa ya watu wa idara
ya niliyokuwa
naiongoza.Rais ametoa amri
popote pale nitakaponekana
nipigwe risasi.Itakuaje pale
atakaposikia kwamba
nimejumuishwa katika
operesheni hii?Sina hakika
kama atakubali niwepo”
“Usihofu kuhusu
Rais.Leave that to me I can
handle it.Kuna lingine”
akauliza Mathew
“Hakuna” akajibu
Devotha
“Kama hakuna basi
tumemaliza hapa
kinachofuata ni kwenda
kuanza maandalizi” akasema
Mathew wote wakatoka
“Devotha tunakwenda
nyumbani kwako kuchukua
kompyuta ya
Ruby.Inahitajika sana katika
operesheni hii ” akasema
Mathew
Kutoka Samawati beach
hotel walielekea moja kwa
moja hadi nyumbani kwa
Devotha.Gosu Gosu
akamtaka Mathew abaki
garini yeye akashuka na
kumfuata Devotha ndani.
“Gosu Gosu thank
you.Uliniokoa sana pale
ulipoingia mle
ndani.Nilimuona Mathew
machoni alikuwa
amedhamiria kuniua na
kama si wewe angenitoa
uhai.Yule mtu ni hatari
sana.Sikuwa nimetegemea
kabisa kama ningeweza
kumkuta mle
chumbani.Halafu namna
alivyoweza kunikamata na
kuniingiza mle chumbani
mpaka sasa ninajiuliza
alifanyaje kwani kufumba na
kufumbua nilijikuta nikiwa
ndani” akasema Devotha
“Don’t mess with him
again.Mathew ni mtu mzuri
lakini ni mbaya mno pale
unapomkorofisha” akasema
Gosu Gosu
“Hata sasa bado naona
hana imani na mimi.Nina
wasi wasi nini kitatokea
huko mbeleni”
“Usihofu.Unachotakiwa
kukifanya ni kufuata
maelekezo yake na kufanya
kile anachokuelekeza”
“Nitafanya hivyo”
akasema Devotha na
kumpatia Gosu Gosu ile
kompyuta ya Ruby
“Vipi kuhusu
Ruby,atanisamehe kweli kwa
kile nilichokifanya?akauliza
Devotha
“I don’t know.Kwa sasa
tujielekeze katika operesheni
yetu na hayo mengine
yatakuja baadae” akasema
Gosu Gosu akabaki
amesimama akimtazama
Devotha
“Mbona unaniangalia
hivyo?akauliza Devotha
“Nothing.Anza
kujiandaa.Kumbuka hili ni
jambo la siri kubwa
sana.Funga mdomo wako
usimwambie yeyote.We’re
watching you”akasema Gosu
Gosu na kuondoka
“Siku zote nimekuwa
nikiamini kwamba mimi ni
mmoja wa watu mahiri sana
katika mambo haya ya
upelelezi lakini leo
nimethibisha kwamba bado
kiwango changu ni kidogo
mno.Kuna watu ambao wako
juu mno katika taaluma
hii.Sikuwahi kuwaza kama
Mathew angeweza kugundua
siri yangu kubwa ambayo
sikutaka watu wa hapa
nchini waijue lakini tayari
imejulikana.Kikubwa hapa
ni kujaribu kujenga
mahusiano mazuri na
Mathew ili amani kati yangu
naye iwepo.Anaonekana ni
mtu mbaya na mkatili
anayeweza kutoa uhai wa
mtu kufumba na
kufumbua.Sitakiwi
kumfanyia masihara
kabisa.Mathew amekuwa
mwanaume wa kwanza
kumuogopa” akawaza
Devotha
NAIROBI – KENYA
Helkopta iliyowabeba
Olivia na Coletha ilianza
kushuka taratibu na kutua
katika sehemu maalum ya
kutulia helkpota iliyokuwa
na herufi H ndani ya jumba
moja kubwa la ghorofa tatu
lililokuwa na uwanja
mkubwa uliopandwa majani
mazuri yenye ukijani
uliokolea.Ndege na wanyama
wa aina mbali mbali kama
vile Farasi na Punda milia
walionekana kwa
mbali.Magari ya kifahari
yalikuwa yamejipanga na hii
ilikuwa ishara tosha kwamba
aliyekuwa akiishi ndani ya
jumba hili alikuwa ni mtu
tajiri sana.
Watu sita waliovalia suti
nzuri nyeusi wakaisogelea
helkopta ile na mlango
ukafunguliwa akashushwa
Olivia halafu Coletha
wakawachukua na
kuwapeleka ndani na kila
mmoja akawekwa katika
chumba chake.Fahad ambaye
naye alikuwamo katika ile
helkopta akashuka na
kuongozwa na mmoja wa
jamaa aliyevaa suti nyeusi
hadi ndani ya jumba lile
akapelekwa ghorofa ya
pili.Mtu mmoja aliyekuwa
ndani ya ofisi nzuri
akawakaribisha wakaingia.
“Fahad karibu sana
Nairobi.Nimefurahi
kukuona” akasema Yule
jamaa mnene
“Nimefurahi kukutana
nawe pia Rashid” akasema
Fahad na Rashid
akamchukua wakaenda
katika sebule nzuri
“Vipi safari yenu
haikuwa na tatizo lolote?
Akauliza Rashid
“Hakukuwa na tatizo
lolote tumesafiri salama
kabisa”
“Nashukuru kusikia
hivyo.Poleni kwa safari”
“Tunashukuru sana”
“Nilipokea maelekezo
kutoka kwa viongozi wa juu
kwamba kila kitu
kitaendeshwa kutokea hapa
na maandalizi yote
yamekwisha fanyika”
“Nilielekezwa hivyo mimi
pia.Kwa ujumla kila kitu
kinakwenda vyema.Rais wa
Tanzania anaendelea
kutekeleza kila
tutakachomuamuru na hivi
sasa anasubiri kwa hamu
kubwa tumuambie kitu gani
kingine tunachokihitaji ili
kumuachia mwanae.Kabla ya
kumwambia kwamba
tunamuhitaji Edger Kaka
tunatakiwa kwanza kumtesa
kihisia.Tutamuacha kwa
muda bila kumpigia simu ili
kuendelea kumpa hofu
zaidi.Hatuna cha kuhofia
kwani hakuna anayejua
kama Olivia na mtoto wa
Rais hawako tena
Tanzania.Lilikuwa ni wazo
zuri sana kuamua kuwaleta
huku Kenya.Kwa kuwa
hatuna haraka na Rais
tunachotakiwa kukifanya
kwa sasa ni kumuhoji
Olivia.Maelekezo
yaliyotolewa na mama
Habiba kuna wasiwasi
kwamba Olivia anatumiwa
na serikali ya Tanzania
kuchota siri zetu na kutekwa
kwake ulikuwa ni mpango
wa serikali baada ya kupata
taarifa za kutosha kuhusu
sisi hivyo wakaamua
kumteka Olivia kumficha
wakati wanaendelea
kujiandaa kutushughulikia”
akasema Fahad.
“Fahad naomba nikuulize
kitu kimoja samahani lakini”
“Uliza Rashid usihofu”
“Una hakika kweli Olivia
alikuwa anatumiwa na
serikali ya Tanzania?
“Sina uhakika sana na
hilo lakini linawezekana”
akajibu Fahad
“Binafsi ninaingiwa na
mashaka kwa sababu kama
kweli angekuwa anatumiwa
na serikali kupata taarifa
zetu kwa muda huu wote
tayari tungekwisha ona
hatua kadhaa zikichukuliwa
na serikali ya Tanzania
katika kuwatafuta lakini
mpaka sasa hakuna hatua
zozote zilizowahi
kuchukuliwa na serikali ya
Tanzania kupambana nanyi
hii ina maana kwamba
Serikali ya Tanzania hawana
uhakika au hawajui kama IS
wana mtandao wao
Tanzania” akasema Rashid
“Nadhani wanajua ndiyo
maana wakamteka Edger
Kaka na kuidanganya dunia
kwamba amefariki katika
ajali.Nina uhakika mkubwa
wanamfahamu Edger ni nani
na hivi sasa watakuwa
wanausaka mtandao
wake.Haya yote
tutayafahamu kwa kumuhoji
Olivia” akasema Fahad.
Rashid akamchukua
Fahad hadi katika chumba
ambacho kiliandaliwa
maalum kwa ajili ya
mahojiano.Kulikuwa na kiti
ambacho nyuma yake
kulikuwa na kitambaa cheusi
chenye maandishi meupe
yalioandikwa kwa lugha ya
kiarabu.Kulikuwa na taa nne
zenye mwangaza mkali vile
vile kulikuwa na kamera
tatu.
“Maandalizi mazuri
sana.Habiba anapaswa
kufuatilia mubashara
tunavyomuhoji Olivia”
akasemaFahad na Rashid
akachukua simu yake
akampigia Habiba Jawad
“Hallo Rashid” akasema
Habiba baada ya kupokea
simu
“Mama Habiba habari za
huko?
“Huku kwema habari za
Nairobi?
“Huku salama
kabisa.Nimekupigia
kukujulisha kwamba timu ya
Dar es salaam imekwisha
wasili hapa Nairobi muda
mfupi uliopita,wote wako
salama kabisa”
“Vizuri sana.Olivia na
Yule mtoto wa Rais nao wako
salama?akauliza Habiba
“Wote wako salama”
“Ahsante kwa taarifa
hizo Rashid.Naweza
kuzungumza na
Fahad?akauliza Habiba
“Ndiyo,huyu hapa
zungumza naye” akasema
Rashid na kumpatia simu
Fahad
“Mama Habiba”akasema
Fahad
“Fahad nakupeni
hongera nyingi kwa kazi
kubwa mliyoifanya vile vile
poleni kwa safari”
“Tunashukuru
mama.Tuliondoka Dar es
salaam salama tukaenda
hadi Pemba ambako
tuliwakuta wenzetu kutoka
Mombasa wanatusubiri
tukaingia katika boti na
safari ya kuja huku
ikaanza.Tunashukuru
tumefika salama kabisa”
“Baada ya kufika Kenya
nini mipango yenu?
“Kwa kuwa tumetoka nje
ya Tanzania hatuna cha
kuhofia tena hivyo tunataka
kumtesa kwanza Rais
kihisia.Hatutampigia simu
kwa haraka na kwa muda
huu tunataka kumfanyia
mahojiano Olivia kama
ulivyoelekeza” akasema
Fahad
“Vizuri sana.Itakuwa
vyema kufahamu kama kweli
alikuwa anatumiwa na
serikali ya Tanzania kuchota
siri zetu”
“Kila kitu kiko tayari
mama na tutakuunganisha
moja kwa moja ushuhudie
kile kinachoendelea hapa”
“Nitafurahi sana”
akasema Habiba na vijana
waliokuwa katika chumba
kingine kilichokuwa na
mitambo na kompyuta
kadhaa wakaelekezwa
kumuunganisha Habiba ili
aweze kushuhudia Olivia
akihojiwa.Baada ya kila kitu
kukamilika Fahad akaagiza
Olivia aletwe katika kile
chumba cha
mahojiano.Akawekwa katika
kiti na mikono ikafungwa
mfuko ukatolewa
kichwani.Alikuwa dhaifu
mwili wake ulikuwa
umevimba kutokana na
kupigwa na mateso makali
aliyoyapata kutoka kwa
akina Kaiza.Kamera
zikawashwa na Fahad
akachukua kiti akamsogelea
Olivia.
“Olivia pole
sana.Unajisikiaje
sasa?akauliza Fahad
“I’m fine” akajibu Olivia
kwa sauti ndogo
“Olivia unaweza
kufahamu hapa uko
wapi?akauliza Fahad Olivia
akatikisa kichwa ishara
kwamba hafahamu chochote
“Can you guess?akauliza
Fahad
“I can’t” akajibu Olivia
“Olivia japokuwa hali
yako bado dhaifu lakini kuna
mambo ambayo tunataka
kuyafahamu kutoka kwako
ndiyo maana uko hapa
kuhojiwa”
“Nini mnataka
kukifahamu? Akauliza Olivia
“Tunataka kufahamu
namna ulivyotekwa na kile
kilichotokea baada ya
kutekwa” Akauliza fahad.
“What is the meaning of
this?Kwa nini mnanirekodi?
Niko kwenye
hukumu?akauliza Olivia
“Olivia just answer the
question! Akasema Fahad.
“Nilitekwa wakati
ninarejea nyumbani kutokea
Kinshasa kuonana na Seif
Almuhsin.Walioniteka ni
idara ya serikali
inayojulikana kama idara ya
siri ya mambo ya ndani ya
nchi.Walipata taarifa kuwa
nimekwenda Kinshasa
kukutana na Seif na
wakaanza
kunifuatilia.Kikubwa
walichotaka kukifahamu
kutoka kwangu ni
mahusiano yangu na IS
kwani katika kompyuta
yangu walikuta barua pepe
nilizokuwa ninawasiliana na
Sayid Omar” akasema Olivia
“Hii idara ya siri ya
serikali walifahamuje
kuhusu wewe kukutana na
Seif Almushin?
“Idara ya usalama wa
taifa ya jamhuri ya
kidemokrasia ya Congo
walipewa taarifa kwamba
Almuhsin anakwenda nchini
Congo na wakaanza
kumfuatilia na kugundua
nilikuwa na mazungumzo
naye wakaitaarifu serikali ya
Tanzania na ndipo
wakajiandaa na kuniteka”
“Nini kiliendelea baada
ya kukuteka?akauliza Fahad
“Kama nilivyowaeleza
kwamba walitaka kufahamu
mahusiano yangu na IS na
kwa kuwa walikuta
mawasiliano yangu na Sayid
Omar waliamini lazima
nitakuwa na mahusiano
nao.Ninaye rafiki yangu
anaitwa Mathew Mulumbi
huyu alinipa namba Fulani
za siri nimpigie pale
nitakapokuwa na matatizo
na nikawapa namba hizo
wapige nikiwadanganya
kwamba ni namba za Sayid
Omar walipopiga namba hizo
mifumo yao yote ikazima”
“Mifumo yao
ikazima?Kivipi?
“Idara hii ina mifumo
yake ya mawasiliano ambayo
yote ilijifunga baada ya
kutumia simu yao kupiga
namba zile”
“Huyo Mathew ni nani?
“Ni mpenzi wangu”
“Anafanya kazi gani?
“Ni mfanya
biashara.Anao mfumo wqa
ulinzi kwa ajili ya familia
yake na mimi akaniunga na
mfumo huo”
“Endelea”
“Walinitaka nifungue
mfumo wao na mimi sikujua
namna ya kuufungua
nikawaambia wakitaka
niwafungulie mfumo wao
ninataka kuzungumza na
Rais wakakubali na kumleta
Rais,nikamueleza kwamba
mwanae amechomwa
sindano yenye virusi na
atakufa kama hatatimiza
kile
ninachokitaka.Nilimuweka
wazi ili mwanae apone
anapaswa kunipa taarifa zote
za mahala alipo Edger
Kaka.Rais alikana kufahamu
chochote kuhusiana na Edger
Kaka.Nilianza kupewa
mateso makali nikitakiwa
kueleza kila kitu kuhusiana
na mahusiano yangu na
IS.Wamenitesa sana lakini
sikufumbua mdomo wangu
kusema chochote hadi
niliporejea tena katika
mikono yenu.Ahsanteni kwa
kuniokoa” akasema Olivia
“Olivia nakupa pole sana
kwa mateso
uliyoyapata.Pamoja na hayo
kuna jambo nataka
kukueleza.Baada ya kutekwa
tumefanya uchunguzi wetu
na tumegundua kwamba huu
ulikuwa ni mchezo
umechezwa kati yako na
serikali ili ionekane
umetekwa lakini ukweli ni
kwamba wewe unatumiwa
na serikali katika
kutuchunguza na kuwapa
taarifa zetu” akasema Fahad
na mstuko mkubwa
ukaonekana usoni kwa Olivia
“Sijakuelewa hicho
ulichokisema Fahad”
“Olivia tumegundua
kwamba unashirikiana na
serikali na hata kutekwa
kwako ulikuwa ni mchezo
maalum ili kutuvuruga na
kuwapa serikali nafasi ya
kushughulikia taarifa zile
ulizowapa” akasema Fahad
“Are you crazy?Nani
kawapa habari hizo zisizo na
ukweli wowote?Kitu gani
kimewafanya muhisi
kwamba ninashirikiana na
serikali kuwahujumu?
Akauliza Olivia
“Olivia tunataka majibu
ni mambo gani ambayo
umewaeleza serikali kuhusu
sisi? Olivia hili si suala la
mchezo na kama hautakuwa
mkweli basi huu utakuwa ni
mwisho wako.Tuambie
ukweli wote na ninakuahidi
tutakusamehe lakini kama
utaendelea kuficha wakati
tunafahamu kila kitu
utajiweka katika mazingira
mabaya sana ” akasema
Fahad.Olivia akamuangalia
kwa macho yaliyojaa hasira
“Sikujua kama ninyi
watu mko namna hii”
akasema Devotha na kuvuta
pumzi ndefu
“Nilimsaidia mtu wenu
Edger Kaka alipotaka
kuuawa kwa sumu.Baadae
mkanifuata na kuniambia
Edger Kaka yuko hai na
mkanitaka niwasaidie
kufanya uchunguzi wa suala
hilo.Nilikubali kuacha kazi
yangu niliyokuwa naifanya
kwa ajili ya kuwasaidia
kuufahamu
ukweli.Mliniingiza katika
mtandao wenu bila mimi
kutaka lakini bado
niliendelea kushirikiana
nanyi na hadi ukweli
ukabainika kwamba Edger
yuko hai.Kama haitoshi
nimetengeneza hadi kirusi
ambacho ameambukizwa
mtoto wa Rais ambaye ni
sawa na mdogo wangu.Ni
moja ya jambo gumu sana
ambalo nimewahi kulifanya
katika maisha yangu
kumuambukiza Coletha
virusi vile lakini nimefanya
kwa ajili ya kuwasaidia
kumpata Edger Kaka.Pamoja
na hayo yote niliyowafanyia
bado mnasema nashirikiana
na serikali?Kama ningekuwa
nashirikiana na serikali
ningekubali kuteseka namna
hii?Nimeteswa mateso
makali,nimechomwa na
umeme na kila aina ya
mateso ili kutoa taarifa za
kuhusiana nanyi lakini
sikufumbua mdomo wangu
kusema chochote
nimevumilia haya yote kwa
ajili ya kuhakikisha Edger
Kaka anapatikana.Kwa haya
yote niliyoyafanya hivi
ndivyo mnavyonilipa?
Sikujua kama ninyi ni watu
msio na shukran kiasi hiki”
akasema Olivia akionekana
kukasirika sana
“Olivia nataka ufahamu
kwamba hakuna kitu kibaya
katika mtandao wetu kama
usaliti.Kila tunapogundua
msaliti ndani ya kundi letu
adhabu yake ni kukatwa
kichwa.Tunafahamu msaada
wako mkubwa uliotusaidia
lakini yote uliyoyafanya
yameharibiwa na huu usaliti
uliofanya na umegeuka adui
yetu.Lakini kwa kuuthamini
mchango wako kwetu
tunakupa nafasi ya kukiri
kosa lako na ukitueleza
ukweli tutakusamehe ila
ukiendelea kutudanganya
utatulazimisha tuendelee na
adhabu unayoistahili”
akasema Fahad
“Ninafahamu mambo
mengi kuhusu ninyi na kama
ningekuwa nashirikiana na
serikali kama mnavyodai
nyote msingekuwepo hapa
muda huu.Kama ningekuwa
msaliti msingeupata ukweli
kuhusu Edger Kaka lakini
kama mnaamini mimi ni
msaliti nawapa uhuru wa
kufanya kile
mkitakacho.Kama ni kuniua
I’m ready.Fikisheni salamu
zangu kwa Habiba Jawad
mwambieni ninashukuru
kwa malipo aliyonilipa baada
ya kuhangaika kumtafuta
mwanae” akasema Olivia
“Olivia tueleze ukweli
tafadhali.Nakuhakikishia
tutak…………….” Akasema
Fahad na Olivi akamkatisha.
“Niueni!! akasema Olivia
Fahad akaenda katika
pembe ya chumba akachukua
panga kali akamsogelea
Olivia
“Olivia nafasi yako ya
mwisho”
“Sina cha
kuwaeleza.Nimewasaidia
kwa kila mlichokihitaji lakini
mmeamua kunilipa kwa
namna hii.Kill me! Akasema
Olivia na kufumba
macho.Fahad akaliinua
panga
“Fahad stop.Hana
mashirikiano yoyote na
serikali.Imetosha mfungueni
mpelekeni akapumzike”
akasema Habiba na Fahad
akalishusha chini panga
alilokuwa amelishika.
“Open your eyes
Olivia.It’s over” akasema
Fahad na Olivia akafumbua
macho akashangaa baada ya
kumuona Fahad
akitabasamu.Mtu mmoja
akaenda kumfungua mikono
“Mmeahirisha
kuniua?akauliza Olivia
“Olivia lile lilikuwa ni
zoezi la kupima uaminifu
wako.Tumejiridhisha wewe
ni muaminifu”
“Mmenisikitisha sana
kwa kushindwa kuniamini
hata baada ya kuwafanyia
mambo
mengi.Nimesikitishwa sana”
akasema Olivia
“Olivia usihofu.Ni
utamaduni wetu kila pale
tunapofanikiwa kumkomboa
mwenzetu ambaye alikuwa
ametekwa kumfanyia
mahojiano kufahamu
kilichotokewa wakati akiwa
ametekwa.Kwa sasa
utakwenda kupumzika”
akasema Fahad na kuwataka
watu wawili waliokuwamo
mle ndani wamchukue Olivia
na kumpeleka katika
chumba chake
alichoandaliwa akapumzike
“Mama Habiba
umeshuhudia mwenyewe
mahojiano” akasema Fahad
baada ya Olivia kutolewa mle
chumbani
“Olivia hana
mashirikiano yoyote na
serikali.Endeleeni na
mipango mingine ya
kumtafuta Seif.Mtoto wa
Rais anaendeleaje?
“Anaendelea
vyema.Olivia alimtibu jana
kabla ya kuanza safari ya
kuja huku na sasa
anaendelea vizuri”
“Vizuri sana.Lini
umepanga kumpigia simu
Rais kumpa maelekezo
kuhusu Seif?
“Nitampigia simu
kesho.Siku ya leo
ninamuacha ateseke kwa
mawazo” akasema Fahad.
DAR ES SALAAM
Mathew na Gosu Gosu
waliwasili katika nyumba ya
Rais waliyopewa waweke
makazi ya muda.Aliposhuka
garini akamfuata Ruby
chumbani kwake na
kumkuta amekaa kitandani
“Ruby unaendeleaje?
“Maendeleo yangu ni
mazuri sana” akajibu Ruby
“Namshukuru sana
Mungu kwa maendelo haya
mazuri.Ninakuhitaji sana”
akasema Mathew
“Mathew uliniahidi
kunieleza kile
kinachoendelea”
“Nitakueleza Ruby lakini
kwanza naomba nikurejeshee
kompyuta yako ambayo
Devotha aliichukua”
“Oh Thank you
Mathew.Tell me you’ve killed
her ! akasema Ruby
“Kuna mambo mengi
yanaendelea Ruby
nitakueleza kila kitu”
akasema Mathew na kuanza
kumsimulia Ruby kile
kilichotokea katika usiku wa
jana.
Machozi yalimtiririka
Ruby baada ya kusikia
namna Mathew na Gosu
Gosu walivyohangaika
kuyaokoa maisha
yake.Mathew akashindwa
kuendelea akaanza
kumbembeleza Ruby
“Nyamaza kulia Ruby”
“Mathew mimi ni nani
hadi ukanifanyia haya?
Akauliza Ruby
“Ruby wewe ni mtu wa
muhimu sana kwangu na
ndiyo maana nilikuwa tayari
kufanya kila lililo ndani ya
uwezo wangu kuhakikisha
unapata matibabu”
“You killed for me
Mathew.Oh my God !
Nitakulipa nini kwa hiki
ulichonifanyia? Akauliza
Ruby
“Ruby toka
tulipofahamiana ni mimi
ambaye nimekuwa na deni
kubwa kwako na kwa mambo
ambayo umekuwa
unanifanyia mpaka leo sina
cha kukulipa.Nilichokifanya
ni kidogo sana ukilinganisha
na mambo ambayo umekuwa
unanifanyia.Ni mimi ndiye
mwenye deni kubwa kwako
ambalo hata nikitumia
utajiri wangu wote sintaweza
kulilipa”
“Mathew sifahamu
niseme nini kwa hiki
ulichonifanyia” akasema
Ruby na kuushika mkono wa
Mathew akaubusu.
“Naomba niendelee
kukueleza kile kilichotokea
jana usiku kwani bado
sijamaliza” akasema Mathew
“Endelea tafadhali”
akasema Ruby huku akifuta
machozi
“Baada ya kuhakikisha
umepata matibabu tulianza
kumsaka Devotha na kitu
cha kwanza tulichokigundua
alikuwa amewasiliana na Dr
Yonathan Cohen balozi wa
Israel hapa nchini na
wakaenda kukutana katika
ubalozi wa Israel.Baada ya
kuligundua hilo kiguu na
njia tukavamia makazi ya
balozi na kuwateka yeye na
mke wake ambaye yuko nasi
hapa.Balozi akatueleza
sababu ya kukutana na
Devotha usiku wa leo na
akatueleza kitu ambacho
hatukuwa
tunakifahamu.Kumbe
Devotha ni wakala wa
shirika la ujasusi la
Israel.Mossad wametuma
watu wao kuja kuandaa
operesheni ya kumtafuta
Olivia” Mathew akamueleza
Ruby kila kitu kuhusiana na
Devotha,Edger Kaka na
mipango ya Mossad
“Sikufikiria kama jambo
hili ni kubwa kiasi hiki”
akasema Ruby baada ya
Mathew kumaliza kumpa
maelezo ya kina kuhusiana
na kile walichokuwa
wamekigundua.
“Baada ya kugundua
hayo yote ikalazimu kwenda
kuonana na Rais” Mathew
akaendelea
“Jitihada zilifanywa
nikafanikiwa kukutana na
Rais nikamueleza mambo
haya yote na tofauti zetu za
awali zikamalizika
tukaungana na kuwa kitu
kimoja.Hivi sasa
tunawasiliana moja kwa
moja na Rais” akasema
Mathew
“Hilo ni jambo kubwa
sana umelifanya Mathew
hongera.Nini mlikipanga
baada ya kukutana na Rais?
“Kama utakumbuka jana
usiku lilifanyika shambulio
la kigaidi katika hospitali ya
Mtodora na shambulio hilo
lilimlenga mtoto wa Rais na
magaidi walifanikiwa
kumteka wakaondoka naye
kisha wakampigia simu Rais
wakamjulisha na kumtaka
awapatie Olivia.Rais hakuwa
na namna ya kufanya
akawapatia Olivia.Rais
aliniomba sana nimsaidie
kuwakomboa Olivia na
Coletha.Ili kuwakomboa
Olivia na Coletha lazima
kwanza kumpata Edger
Kaka ambaye anashikiliwa
katika ubalozi wa Israel
nchini Kenya.Kuna namna
moja tu ya kuweza kumpata
Edger Kaka nayo ni kuvamia
ubalozi huo na
kumchukua.Rais amekwisha
toa ruhusu jambo hilo
lifanyike na hivi sasa tuko
katika maandalizi ya awali
ya operesheni hiyo ya
kwenda kumuokoa Edger
Kaka.Ili tuweze kuingia
ndani ya ubalozi huo
tunahitaji kupata ramani ya
namna jengo lilivyo na
taarifa za kiusalama hivyo
basi tunatanguliza timu ya
watu watatu kwenda Nairobi
mchana huu kuanza
kuifanya kazi hiyo.Wakiwa
kule watakuwa
wakiwasiliana nasi huku
Tanzania kutujulisha kila
kinachoendelea hivyo
nakuhitaji sana katika
operesheni hiyo.Tunahitaji
kuwa na mawasiliano kati ya
ofisi ya Dar es salaam na
watu wa Nairobi” akasema
Mathew
“Mathew hakuna tatizo
katika hilo.Mimi niko zaidi
ya tayari” akasema Ruby
“Ahsante sana Ruby
nafahamu muda wowote uko
tayari lakini kuna tatizo
kidogo” akasema Mathew
“Kuna tatizo gani
Mathew? Akauliza Ruby
“Timu inayokwenda
Nairobi mchana huu ni Gosu
Gosu,rafiki yangu mwingine
anaitwa Tino na ……”
Mathew akasita
“Mbona unasita
Mathew?akauliza Ruby
“Ruby kuna jambo
limefanyika ambalo naamini
halitakupendeza lakini
imebidi lifanyike”
“Jambo gani hilo Mathew
nieleze tafadhali” akasema
Ruby
“Ili kuweza kupata
ramani ya jengo na taarifa
zote za ulinzi inatubidi
tupandikize mtu ndani ya
Mossad jambo ambalo ni
gumu na linahitaji muda
mrefu ambao sisi hatuna
hivyo tumeamua kumtumia
mtu ambaye tayari ana
ukaribu na Mossad ili asaidie
katika kupata taarifa hizo.”
Mathew akanyamaza kidogo
halafu akasema
“Tumemshirikisha pia
Devotha katika operesheni
hii”
Ruby akamtazama
Mathew kwa mshangao
mkubwa
“Mathew naomba
usinitanie tafadhali”
akasema Ruby
“Ruby haikuwa rahisi
kwangu kufanya maamuzi
haya niliyoyafanya lakini ni
kwa ajili ya operesheni hii”
akasema Mathew
“Mathew that witch shot
me three times.She’s
supposed to be in hell right
now.Unathubutuje
kumrejesha ashirikiane nasi
tena? Akauliza Ruby
“Ruby imelazimu iwe
hivyo kwani tunahitaji mtu
ambaye anaweza kuingia
ndani ya Mossad akatusaidia
kupata taarifa muhimu za
kutuwezesha kufanikisha
operesheni yetu.Hata mimi
nafsi yangu haitaki jambo
hili lakini imebidi iwe
hivyo.Nakuomba Ruby
ukubali Devotha ashirikiane
nasi na baada ya operesheni
kumalizika nitajua adhabu
ya kumpa lakini kwa sasa ni
mtu wa muhimu sana”
akasema Mathew.
“Mathew sina cha
kusema kwa sababu wewe
ndiye kiongozi na ndiye
mwenye kauli ya mwisho
kama umeamua
kumshirikisha mtu aliyetaka
kuniua katika timu yetu sina
cha kupinga lakini Mungu
atanilipia” akasema Ruby
“Ruby my dear do you
trust me?
“With all my life” akajibu
Ruby
“Ahsante kwa kuniamini
Ruby”
“Mathew nimekuwa
ninakuamini toka siku ya
kwanza nilipofahamiana
nawe”
“Ruby nakuomba
uniamini pia katika
hili.Niliumizwa na kitendo
alichokifanya Devotha na
adhabu niliyokuwa naifikiria
kichwani kwangu ni kumuua
lakini mwanamke huyu ana
maisha marefu kama paka
kwani nimejikuta sina
namna zaidi ya kukubali
kumtumia tena kutokana na
umuhimu wake lakini this
isn’t over yet.Mimi na yeye
tutamalizana baada ya
operesheni hii kumalizika”
akasema Mathew
“Mathew sina chochote
ninachoweza
kukupinga.Kauli yako ni ya
mwisho na lazima
niiheshimu hata kama moyo
wangu hautaki”akasema
Ruby na Mathew
akamtazama kisha akauliza
“Ruby kutakuwa na
tatizo lolote kufanya kazi na
Devotha?
Ruby akafikiri kidogo
halafu akasema
“Hakuna tatizo lolote.I
trust you”
“Thank you my Ruby”
akasema Mathew akambusu
Ruby katika paji la uso na
kutoka akamfuata Gosu
Gosu
“Nimezungumza na Ruby
kuhusu Devotha” akasema
Mathew
“Amesemaje?akauliza
Gosu Gosu akionekana kuwa
na shauku ya kutaka kujua
maamuzi ya Ruby
“Haikuwa rahisi
kumshawishi akubali
kufanya kazi tena na
Devotha lakini amekubali
Devotha ashiriki katika
operesheni hii na amekubali
kufanya naye kazi.Najua
amekubali kwa kuniridhisha
mimi ila moyoni bado ana
kinyongo”
“Ahsante sana kwa
kumshawishi Ruby.Nini
kinafuata?Umewasiliana na
Tino?akauliza Gosu Gosu
“Kabla ya kuwasiliana na
Tino natakiwa kwanza
kuwasiliana na Rais na
kumjulisha hatua tuliyofikia”
akasema Mathew na
kuchukua simu akampigia
Dr Evans
“Mathew nimelazimika
kusimamisha kikao kwa
muda ili kupokea simu yako
kwani ni ya muhimu sana
kwa sasa.Nini kinaendelea
huko?
“Mheshimiwa Rais
samahani kwa usumbufu
huu”akasema Mathew
“Mathew nimekupa
uhuru wa kupiga simu yangu
muda wowote ambao
utakuwa na jambo la
kuniambia usione kama ni
usumbufu tafadhali”
“Ahsante mheshimiwa
Rais kwa heshima
hiyo.Nimekupigia
kukujulisha kwamba mchana
huu timu ya watu watatu
itaondoka hapa Dar es
salaam kuelekea Nairobi kwa
ajili ya kuanza maandalizi ya
ile operesheni.Kila kitu
tayari kimewekwa sawa”
“Safi sana Mathew.Hilo
ni jambo zuri.Lini mmepanga
kufanya operesheni?
“Mheshimiwa Rais
operesheni inategemea na
uhodari wa timu yetu
inayokwenda Nairobi namna
watakavyotekeleza yale
tunayowatuma wakayafanye
yaani kutafuta ramani ya
jengo la ubalozi wa Israel
nchini Kenya na mahala
alipofichwa Edger.Kama
wakiweza kuyakamilisha
haya mchana huu basi hata
usiku wa leo tunaweza
kufanya operesheni
yetu”akasema Mathew
“Mathew kwa nini
usiongozane na hao jamaa
wanaokwenda Nairobi ili
kuhakikisha kwamba mambo
yanakwenda haraka na kwa
mafanikio?akauliza Rais
“Usihofu mheshimiwa
Rais watu ninaowatuma
huko ninawaamini
wanaweza wakaifanya kazi
kwa haraka na kwa
ufanisi.Hata hivyo
mawasiliano kati yetu ni
makubwa na nitakuwa
nikifuatilia kila kitu
wanachokifanya kule nikiwa
hapa hapa Dar es
salaam.Mheshimiwa Rais
kuna jambo nataka
ulifahamu pia kuhusu timu
ninayoituma Nairobi”
“Ndiyo nakusikiliza
Mathew” akasema Dr Evans
“Katika timu hiyo ya
watu watatu yupo pia
Devotha Adolph” akasema
Mathew na ukimya wa
sekunde kadhaa ukapita
“Mheshimiwa Rais”
akaita Mathew
“Nimestuka sana
nilipolisikia jina la
Devotha.Huyo mwanamke
sihitaji kabisa kumuona
mbele ya macho
yangu.Nilimuamini sana
lakini kwa aliyoyafanya
hastahili kuendelea kuwa hai
na sitaki ashiriki tena suala
lolote linalohusiana na nchi
yetu.Ni msaliti na atatuuza!
akasema Dr Evans kwa ukali
“Mheshimiwa Rais
nafahamu kila kitu kuhusu
Devotha na hata mimi
nilikuwa namtafuta mno
nimuadhibu kwa kitendo
alichokifanya cha kutaka
kumuua mmoja wa watu
wangu wa karibu lakini
mheshimiwa Rais kwa sasa
Devotha ana umuhimu
mkubwa sana katika
operesheni yetu.Ni yeye
ambaye tutamtanguliza
mbele kutafuta ramani ya
jengo la ubalozi tunalotaka
kuvamia.Ni kwa umuhimu
huo ndio maana nimeamua
kumjumuisha katika kikosi
hiki”
“Mathew I real don’t like
this ! akasema Dr Evans
“Nafahamu mheshimiwa
Rais na hata mimi sikutaka
lakini imenilazimu.Naomba
uniamini mheshimiwa Rais”
Dr Evans akafikiri
kidogo halafu akasema
“Mathew kama unaona
ana umuhimu wa kushiriki
katika operesheni hiyo sawa
mjumuishe lakini kwa sharti
moja” akasema Dr Evans na
kunyamaza kimya kwa
sekunde kadhaa
“Nakusikiliza
mheshimiwa Rais” akasema
Mathew
“Baada ya operesheni
kumalizika kill her !
Ilipita dakika moja ya
ukimya Dr Evans akasema
“Mathew umenisikia
nilichokwambia?
“Nimekuelewa
mheshimiwa Rais”
“Good.Akishamaliza kile
ambacho umemtuma
akifanye nataka auawe”
akasema Dr Evans
“Nitafanya hivyo
mheshimiwa Rais”
“Ahsante.Ninawatakia
kila la heri katika
maandalizi yenu kama kuna
chochote mtakihitaji msisite
kuniambia”
“Ahsante mheshimiwa
Rais kwa sasa ni hilo tu
nililotaka kukufahamisha”
“Keep me posted !
akasema Dr Evans na
kukata simu
“Rais
amesemaje?akauliza Gosu
Gosu.Mathew akavuta pumzi
ndefu na kusema
“Rais amekubali
tumjumuishe Devotha lakini
ameagiza baada ya kumaliza
kazi tuliyomtuma tumuue”
Gosu Gosu alistushwa na
maagizo yale akamtazama
Mathew kwa sekunde
kadhaa na kuuliza
“Mathew are you real
going to kill her?akauliza
Gosu Gosu
“I don’t know yet” akajibu
Mathew
“Mathew please don’t kill
her.She’s an asset.Kuna
mambo mengi ambayo
tutaendelea
kumuhitaji.Mathew hatuna
sababu ya kumuua Devotha
badala yake tunapaswa
kumsaidia kumuondoa
katika hatari hii ya
kuuawa.This is a win win
situation.Anatusaidia na sisi
tunapaswa kumsaidia”
akasema Gosu Gosu
“Gosu Gosu naomba
tusiliongelee suala hili kwa
sasa.Tujielekeze katika
safari ya Nairobi” akasema
Mathew na kumpigia simu
Tino ambaye alimjulisha
kwamba anakaribia kufika
pale nyumbani.
“Mathew wakati
tukimsubiri Tino nataka
tumalize lile suala la
Devotha” akasema Gosu
Gosu
“Gosu Gosu Rais
amekwisha toa maelekezo
ambayo hatuna budi
kuyafuata na isitoshe hata
mimi bado nina hasira naye
sana kwa alichomfanyia
Ruby”
“Mathew kama
unakubaliana na
alichokiagiza Rais kwamba
tumuue Devotha basi tufanye
hivyo kabla hajaenda
Nairobi.Haitakuwa busara
tumtume kazi atufanyie
halafu tumuue.Mathew
hatuna sababu ya kumuua
Devotha.Nakubali amefanya
kosa kubwa na hata mimi
sikufurahia kitendo
alichokifanya lakini Devotha
bado ana msaada mkubwa
kwetu.Atatusaidia mno”
akasema Gosu Gosu Mathew
akamkazia macho
“Gosu Gosu unaonekana
kumtetea sana
Devotha,why?Mathew
akauliza
“The truth is,I don’t want
her to die” akasema Gosu
Gosu na mlango ukagongwa
Gosu Gosu akaufungua
alikuwa ni Tino amerejea.
“Karibu Tino” akasema
Mathew.
“Ahsanteni
sana.Nimerejea na huko
nilikotoka nimefanikiwa
kupata tiketi tatu katika
ndege ya shirika la ndege la
Tanzania inayoondoka saa
saba mchana kuelekea
Nairobi.Nimekata daraja la
kwanza” akasema Tino
“Safi sana” akasema
Mathew
“Vipi kwa upande wenu
mambo yamekwenda
vizuri?Tino akauliza
“Kwa upande wetu kila
kitu kimekwenda
vyema.Tumekutana na balozi
na Devotha na mambo yote
yamewekwa sawa kilichobaki
kwa sasa ni kujiandaa kwa
safari ila kuna jambo moja
ambalo nataka utusaidie
Tino kama litakuwa ndani ya
uwezo wako”
“Jambo gani Mathew?
“Mkiwa Nairobi mtahitaji
vifaa vya mawasiliano
kuhusu hilo hakuna tatizo
kwani fedha zipo mtanunua
lakini zitahitajika silaha kwa
ajili ya kujilinda kabla ya
operesheni.Unaweza
ukatusaidia kwa hilo?
“Mathew usiwe na hofu
yoyote kuhusu silaha.Hilo ni
jambo dogo sana
kwangu.Ninao mtandao
mkubwa wa watu Afrika
Mashariki na Kenya ninao
watu wangu ambao
watanipatia hizo silaha”
“Good.Pamoja na silaha
kuna jambo lingine vile vile
ambalo ninataka ukiwa
Nairobi uanze
kulishughulikia.Siku
tutakayofanya operesheni
tutalazimika kukata umeme
eneo lote la karibu na ubalozi
wa Israel.Tunatakiwa
kuifanya operesheni yetu
gizani hivyo basi kwa kuwa
tayari unao mtandao wako
jijini Nairobi anza kulifanyia
kazi hilo suala” akasema
Mathew
“Hesabu hilo nalo
limekwisha.Mtandao wangu
unao watu wazito na hilo
suala nitalifanikisha”
akasema Tino.
“Sawa ndugu zangu
naona yale yote yalipangwa
kufanyika asubuhi ya leo
yamekamilika kinachofuata
kwa sasa ni kujiandaa kwa
ajili ya safari”
Mathew,Gosu Gosu na
Tino wakaingia katika gari la
Mathew wakaondoka
kuelekea nyumbani kwa
Mathew ambako Gosu Gosu
alikuwa ameacha sanduku
lake halafu wakaelekea
nyumbani kwa Tino naye
akachukua vitu vichache
alivyovihitaji wakatoka na
kuelekea nyumbani kwa
Devotha ambaye tayari
alikwisha jiandaa
wakamchukua na kuelekea
uwanja wa ndege
“Guys this is
it.Nawatakia kila la heri
katika safari yenu hii mfike
salama na mtekeleze jukumu
mlilotumwa.Ninawategemea
sana ndugu zangu na nchi
inawategemea
pia.Kumbukeni hamtarejea
tena Tanzania hadi
operesheni itakapokamilika
hakikisheni mnakuwa
salama” akasema Mathew na
kuwaaga akina Gosu Gosu
ambao waliingia ndani
sehemu ya kusubiri
ndege.Mathew hakuondoka
hadi pale alipohakikisha
ndege waliyopanda akina
Tino imepaa
“Mungu awatangulie
tutakutana Nairobi” Mathew
akasema kwa sauti ndogo
akawasha gari lake na
kuondoka akarejea katika
makazi yao ya muda moja
kwa moja akaelekea katika
chumba cha Ruby.
“Ruby akina Gosu Gosu
tayari wameondoka kuelekea
Nairobi.Tunahitaji
kuwasiliana nao pindi tu
wakifika hivyo basi
tunapaswa kuanza kuandaa
ofisi kwa ajili ya
mawasiliano.Dar es salaam
hadi Nairobi kwa ndege ni
mwendo wa saa moja na
nusu hivi hivyo maandalizi
yanatakiwa yaanze mara
moja” akasema
Mathew.Ruby akamtazama
akamshika mkono na
kusema
“Mathew moyo wangu
hauko tayari kufanya kazi na
mtu aliyetaka kuniua lakini
nitafanya kwa ajili yako.You
want to know why?akauliza
Ruby
“Ndiyo Ruby ningependa
kujua”akasema
Mathew.Ruby akamtazama
Mathew machoni akafumbua
midomo yake laini akasema
‘It’s because I love you
Mathew”
Mathew akatabasamu
kidogo halafu akasema
“I love you too Ruby”
“Mathew naelewa
unanipenda kama rafiki
yako,kama mtu wako wa
karibu lakini mimi ni tofauti
kidogo.Nakupenda Mathew
like I..ouh gosh I don’t know
how to say it” akasema Ruby
“Niambie Ruby chochote
unachotaka kuniambia”
akasema Mathew.Ilimlazimu
Ruby kuvuta pumzi halafu
akasema
“Mathew nilikupenda
sekunde ya kwanza
nilipokutia
machoni.Niliamini wewe
ndiye mwanaume pekee
ambaye ninastahili kuwa
naye maishani.Mathew I
know you have a wife and
beautiful kids na hiyo ndiyo
sababu iliyonifanya niishi na
mzigo huu mzito moyoni
mwangu kwa muda mrefu
lakini siwezi kuendelea tena
kubeba zigo
hili.Nimechungulia kaburi na
kwa hiki kilichonitokea ni
kama vile nimekumbushwa
kwamba maisha haya ni
mafupi sana na uhai
unaweza ukakutoka sekunde
yoyote ile hivyo tunatakiwa
kuyaishi maisha tuliyonayo
sasa.Hakuna anayeijua
kesho yake.Kama una kitu
cha kumwambia mtu
mwambie sasa na usisubiri
hadi kesho kwani hujui kama
utaiona hiyo kesho.Kwa
nafasi hii niliyoipata baada
ya kunusurika kifo ninataka
nikueleze Mathew kwamba
wewe ndiye mwanaume wa
maisha yangu.Nakuhitaji
Mathew katika dunia
yangu.Milango ya himaya
yangu nimekwisha ifungua
kwako muda mrefu sana ila
bado hujaingia.Mathew
nakutaka uwe mpenzi
wangu” akasema
Ruby.Mathew alibaki
anamtazama Ruby
akashindwa aseme nini
“Ruby sijui niseme nin…”
“Usiseme chochote
Mathew kwani nafahamu
utakachokisema na
kitanivunja moyo wangu
sana lakini naomba
unisikilize.Najua una mke
lakini niko tayari kuwa
mpenzi wakjo wa siri bila
mke wako kujua.Niko tayari
kuzaa nawe mtoto.Kama
uliweza kuwa na Olivia bila
mkeo kujua naomba uwe na
mimi pia.Sijali una
wanawake wangapi pembeni
ya mke wako lakini
ninachohitaji ni penzi lako
Mathew” akasema Ruby kwa
hisia kali na kwa mbali
macho yake yalilengwa
machozi.
“Look at me Mathew”
akasema
“I’m very pretty may be
than your wife and your
Olivia but….” Akashindwa
kuendelea akamwaga
machozi
“Ruby
nimekuelewa.Nyamaza
kulia.Nimekuelewa yote
uliyoniambia” akasema
Mathew
“Umenielewa?
“Ndiyo nimekuelewa
lakini ninaomba
tuyazungumze baada ya
operesheni yetu
kumalizika.Tushike suala
moja tulimalize kwanza
halafu tutaingia tena katika
suala lingine.Jambo hilo
linazungumzika”
“Mathew nataka
tulimalize suala hili hapa
hapa.Nina hofu kubwa baada
ya kunusurika kifo”
“Ruby wewe
unanifahamu mimi vizuri
pengine kuliko mtu yeyote,
nikisema tutalizungumza
jambo hili amini
hivyo.Nakuahidi Ruby mara
tu operesheni hii
itakapomalizika mimi na
wewe tutakwenda mahala
mbali na Dar es salaam
tukiwa peke yetu tupumzike
na tutazungumza mengi
likiwamo suala hili.”
akasema Mathew na kwa
mbali tabasamu likaonekana
usoni kwa Ruby.Mathew
akamsaidia kusimama
akamshika mkono
wakatembea hadi katika ofisi
akaketi kitini na kuanza
kumpa Mathew maelekezo ya
kufanya.
“Sikutegemea kabisa
kama Ruby angeweza
kunitaka niwe mpenzi
wake.Mimi na yeye
tunaheshimiana sana na
ninamchukulia kama mdogo
wangu lakini kumbe
mwenzangu amebeba mzigo
mzito moyoni mwake.Ngoja
kwanza nijielekeze katika
operesheni nzito na baadae
tutazungumza kwani hili si
jambo dogo”akawaza Mathew
akiendelea kuuganisha vifaa
huku akielekezwa na Ruby
aliyekuwa ameketi kitini
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 6
Ndege waliyopanda
akina Gosu Gosu ilitua
katika uwanja wa ndege wa
kimataifa wa Kilimanjaro na
kisha ikapaa kuendelea na
safari ya kulekea Nairobi
Kenya.Devotha aliyekuwa
amekaa upande wa dirishani
alionekana kutabasamu
muda wote
“You are always smilling”
Gosu Gosu aliyekuwa
amekaa pembeni ya Devotha
akaanzisha
maongezi.Devotha akageuka
na kumtazama Gosu Gosu
“Hivi ndivyo nilivyo.Kila
wakati sura yangu
inatabasamu hata nikifa
bado nitaendelea
kutabasamu” akasema
Devotha na kumfanya Gosu
Gosu naye atabasamu
“Nadra sana kukuona
ukitabasamu Papii” akasema
Devotha akitoa kicheko cha
chini chini
“Natabasamu kwa
sehemu muhimu tu na
nimeanza kutabasamu hivi
karibuni.Kabla ya hapo
sijawahi kuweka tabasamu
usoni pangu.Sira yangu
imekaa kikazi zaidi”
akasema Gosu Gosu
“Ngoja nikufundishe kitu
Papii,jifunze na jizoeshe
kutabasamu kila
wakati.Tabasamu linaficha
mengi na linaepusha
mengi.Tabasamu ni silaha
kubwa ya ushindi” akasema
Devotha na kutazama nje
akaendelea kutabasamu
“What a beautiful
country! Akasema halafu
mara tabasamu likapotea
usoni pake.Bado Gosu Gosu
alikuwa amegeuza shingo
yake akimuangalia
“Umeona nini?Mbona
tabasamu limepotea
ghafla?akauliza
“Kuna wazo limenijia, ni
vipi kama sintarudi tena
nyumbani?What if I die
there?akauliza Devotha
“That won’t happen.We’ll
all come home together.I’ll
protect you” akasema Gosu
Gosu kwa sauti ndogo ili
watu wasisikie maongezi
yao.Devotha akamtazama
akatabasamu tena
“Gosu Gosu you are a
killer but to me you are so
sweet.So soft.Why?akauliza
Devotha lakini Gosu Gosu
akajifanya kama vile
hajasikia alichoulizwa
“Umesemaje?
“Nilipokabwa na Mathew
ulikuja
ukaniokoa.Sikutegemea
kama ungesimama kunitetea
kwani ninyi ni
washirika.Kwa nini
ulinisaidia?Kwa nini
ulimzuia Mathew?Devotha
akauliza
“Hivyo ndivyo
nilivyo.Nina sura mbili.Kuna
wakati ninakuwa shetani na
kuna wakati ninakuwa
malaika” akajibu Gosu Gosu
na Devotha akatoa kicheko
kidogo.
“Wewe na Mathew ni
watu ambao ni vigumu sana
kuwaelewa.Mathew
anaonekana ni mkatili sana
lakini kuna wakati anakuwa
mpole.By the way where is
your family?
“Family?
“Ndiyo”
“Sina familia”akajibu
Gosu Gosu
“Huna familia?
“Ndiyo.Sina mke,sina
watoto sina mpenzi.Familia
yangu mimi ni Mathew na
Ruby hao ndio watu wangu
wa karibu wanaonijali na
ndio ndugu zangu”
“You and Ruby why you
worship Mathew so much
like he’s you God?akauliza
Devotha
“You don’t know him
yet.Once you know him well I
hope you’ll worship him as
well” akajibu Gosu
Gosu.Devotha akainamisha
kichwa kidogo akafikiri
halafu akauliza
“Mathew na Ruby ni
wapenzi?
“Sifahamu kama wana
mahusiano hayo kwani mimi
nimefahamiana nao tayari
wakiwa marafiki”
“Mke wa Mathew yuko
wapi?
“Mke wa Mathew anaishi
Ufaransa.Mbona unaonekana
kutaka kumfahamu sana
Mathew? Gosu Gosu akauliza
“Ndiyo ninataka
kumfahamu.Ni mtu ambaye
amenishangaza sana kwa
mambo anayoyafanya ndiyo
maana ninataka kumjua ni
mtu wa aina gani”akajibu
Devotha
“Mathew hapendi
kuchunguzwa so let’s not talk
about him.Vipi kuhusu wewe
una mume na watoto?
Akauliza Gosu Gosu na
muhudumu akapita na torori
lililojaa vinywaji Devotha
akachukua glasi ya mvinyo
unaotengenezwa Dodoma
akanywa funda moja halafu
akatabasamu
“Mvinyo bora kabisa huu
unaotengenezwa na zabibu
ya hapa hapa nyumbani”
akasema Devotha
“Devotha nilikuuliza
swali naomba unijibu”
“Sina mume wala watoto
na sijawahi kufikiria kuwa
na mume”
“Kwa nini?Gosu Gosu
akauliza
“Sitaki mume.Sitaki
kuwa chini ya
mwanaume.Ninao uwezo wa
kufanya yale yote
anayoyafanya mwanaume.I
can shoot and kill,I can give
men orders and they obey
hivyo sina haja ya kuwa na
mwanaume ambaye
ataniweka chini yake.I want
to control not to be controlled
you understand me?
Akauliza Devotha
“Nimekutana na
wanawake kama wewe vitani
ambao walikuwa na mawazo
kama yako lakini siku zote
mwanamke atabaki kuwa
chini ya mwanaume.Mathew
amenifanya nikakutana na
watu mbali mbali na mmoja
wao ni mchungaji Crintson
Davis ambaye amenisaidia
sana kunitoa katika dunia
niliyokuwepo na kuanza
kujifunza neno la
Mungu.Nitakutolea mifano
michache.Katika 1
Wakorinto 11:9 maandiko
yanasema " Wala
mwanamume hakuumbwa
kwa ajili ya mwanamke, bali
mwanamke kwa ajili ya
mwanamume." Tukirudi
katika kitabu cha mwanzao
2:18 Bwana Mungu akasema
si vyema huyo mtu awe peke
yake,nitamfanyia msaidizi
wa kufanana
naye”.Maandiko haya mawili
ni mfano tu kwamba siku
zote mwanamke atakuwa
chini ya mwanaume.Ukisema
kwamba hutaki kuwa chini
ya mwanaume unakwenda
kinyume na maandiko na
unamkosoa aliyekuumba
mwanamke” akasema Gosu
Gosu na Devotha
akatabasamu
“Gosu Gosu unaonekana
wewe bado u mchanga sana
katika maandiko.Biblia hiyo
hiyo imeonyesha nguvu
kubwa aliyonayo
mwanamke.Tukianzia na
hapo hapo ulipoishia.Mungu
alimuumba mwanamke
baada ya kuona kwamba
wajibu aliompa mwanaume
katu asingeweza kuutekeleza
ndipo akamleta
mwanamke.Mwanaume ni
dhaifu bila mwanamke na
mimi siwezi kuongozwa na
kiumbe dhaifu wakati
nimepewa nguvu kubwa.Si
nguvu ya misuli bali nguvu
ya ndani.Mwanamke ndiye
aliyeiharibu dunia kwa kula
tunda alilokatazwa na
Mungu.Unadhani kwa nini
shetani aliamua kumfuata
na kumshawishi mwanamke
kula tunda?Ni kwa sababu
aliifahamu nguvu yake
kwamba anao uwezo wa
kumfanya mwanaume afanye
kitu chochote.Sitaki kwenda
ndani zaidi lakini
mwanamke ni kiongozi wa
mwanaume.Atakaloliamua
mwanamke mwanaume
hawezi akalipinga.Hiyo ni
nguvu kubwa sana aliyopewa
mwanamke”
“Hizo ni dharau kwa
wanaume Devotha ! akasema
Gosu Gosu ambaye
hakupendezwa na maneno
yale ya Devotha
“Gosu Gosu wanaume
ninawaheshimu lakini si
kuwa chini yao na kuwaacha
wawe na maamuzi katika
kila jambo”
“Kwa maneno hayo
unataka kuniambia kwamba
wewe hautaolewa katika
maisha yako yote?
“Don’t you get it Papii?
Sitaki kuwa chini ya
mwanaume.Nikiolewa
nitakuwa chini ya
mwanaume ambaye atataka
kunitawala na mimi sitaki
kutawaliwa ninataka
nitawale.Kama nikimpata
mwanaume ambaye
atakubali kuwa chini yangu
nimtawale niwe na maamuzi
ya mwisho ndani ya nyumba
nitakuwa tayari kuolewa”
akasema Devotha
“Mwanaume wa aina
hiyo utasubiri sana.Siku zote
katika ndoa mwanaume
ndiye kichwa cha
nyumba.Ukitaka wewe kuwa
kichwa utasubiri sana na
yawezekana utaishi hivyo
kwa maisha yako yote”
“I don’t care.Hata kama
nikiishi mwenyewe kwa
maisha yangu yote hakuna
ubaya.Isitoshe mwili wangu
huu mzuri sitaki uanze
kuharibiwa kushikwa shikwa
hovyo kutumikishwa kingono
na mwishowe nianze
kuchujuka.Sitaki hilo”
akasema Devotha
“Ni hicho tu ndicho
kinakuogopesha
kutumikishwa na
mwanaume?
“Papii nimekwambia
ninataka kuwa mtawala na
si mtawaliwa.I wish
ningekuwa na….”akasema
Devotha na kunyamaza
“Ungekuwa na
nini?akauliza Gosu Gosu
“Ningekuwa na sehemu
za siri za mwanaume..”
“Ah ! don’t go there.Huko
unakotaka kuelekea si
kuzuri hata kidogo.Wewe ni
mwanamke na utabaki kuwa
mwanamke.Jikubali !
akasema Gosu Gosu kwa
sauti ya ukali kidogo halafu
kukawa kimya
“Gosu Gosu umechukia?
“Maneno ulioyasema
hayajanifurahisha mimi
kama mwanaume”
‘I’m sorry lakini huo ni
ukweli Papii.Sipendi
kutawaliwa ninataka
nitawale niwe na
sauti.Ninafikiria hata siku
moja niwe Rais wa nchi”
akasema Devotha na Gosu
Gosu akatoa kicheko kidogo
“Mbona unacheka Gosu
Gosu siwezi kuwa
Rais?Ninapenda sana
uongozi kuwa na sauti”
“Devotha nieleze ukweli
katika maisha yako hujawahi
kuwa na mwanaume?
“You’ve been so nice to
me hivyo nitakuwa mkweli
kwako.Nimewahi kuwa na
wanaume kadhaa kwa ajili
ya kujifurahisha tu lakini si
kwa ajili ya mapenzi lakini
katika wanaume wote ambao
nimetembea nao sijawahi
kufurahia hilo tendo hata
mara moja.Ninaona kama
vile ninakereka tu”
“Kutokana na uzuri wako
mwanaume ambaye unaweza
ukatoka naye ni yule
mwenye wadhifa au mwenye
pesa ambaye kwake pesa na
kazi ndivyo vipaumbele na
ndiyo maana wakashindwa
kukuridhisha na
wakasababisha utuone
wanaume wote hatuna
maana.You need to try with a
rough man like me,I swear
you’ll forget your name !
akasema Gosu Gosu na
kumfanya Devotha aangue
kicheko kikubwa hadi abiria
wengine wakageuka
kumtazama.
“Kitu gani
kimekufurahisha?akauliza
Gosu Gosu
“Umenifurahisha sana
Papii.You can’t afford me
hata kwa mfano.Mimi na
wewe hatuendani.Ni kama
mafuta na maji”akasema
Devotha
“Devotha I need to
sleep.Usiku mzima wa jana
sijalala naomba nitumie
dakika chache tulizonazo
kabla ya kufika Nairobi
nijipumzishe” akasema Gosu
Gosu na kufumba macho.
“Katika wanawake wote
wa hii dunia kwa nini moyo
wangu umemuangukia
Devotha? Ni mara ya kwanza
nimejikuta nikimpenda
mwanamke lakini
mwanamke mwenyewe
ambaye moyo wangu
umemuangukia ana utata
mkubwa ila sikati tamaa
nitahakikisha ninampata
Devotha.Mimi ni mpiganaji
nitapigana pia katika hili
hadi nihakikishe anatua
mikononi
mwangu.Kinachotakiwa
hapa ni kumbadili mtazamo
wake na kumfanya ahitaji
kupendwa” akawaza Gosu
Gosu
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 7
Ndege ya shirika la
ndege la Tanzania ilitua
katika uwanja wa ndege wa
Jomo Kenyatta jijini
Nairobi.Abiria walishuka na
miongoni mwao walikuwemo
Gosu Gosu,Tino na
Devotha.Gosu Gosu ndiye
aliyekuwa wa kwanza
kukamilisha taratibu za
uhamiaji, akawasubiri
wenzake nje na wote
walipokamilisha na kuingia
nchini Kenya wakachukua
taksi na kumuomba Dereva
awapeleke Sadena hoteli.Ni
moja kati ya hoteli kubwa ya
nyota tano jijini Nairobi.Tino
na Devotha walionekana
kulifahamu vyema jiji la
Nairobi tofauti na Gosu Gosu
ambaye alikuwa kimya
akitazama nje.
Sadena hoteli
walipokewa vizuri na
wahudumu.Gosu Gosu na
Tino wakachukua chumba
kimoja kikubwa na Devotha
akachukua chumba chake
peke yake.Wahudumu
wakawasindikika hadi katika
vyumba vyao.Baada ya
kuonyeshwa vyumba vyao
wote wakakutana na kuanza
kupanga mikakati.
“Tayari tumefika Nairobi
na hakuna kupoteza muda
tunaanza kazi.Devotha wewe
ndiye tunayekutegemea sana
katika vipi mipango yako?
akasema Gosu Gosu
“Mpango uko namna
hii,nitawasiliana na Avi
mkuu wa Mossad afrika
Mashariki na kupanga
kuonana naye hapa
hotelini.Zitafungwa kamera
katika chumba change na
mtakuwa mkifuatilia kile
kitakachokuwa kinaendelea
chumbani
kwangu.Namfahamu Avi ana
udhaifu mkubwa kwa
wanawake,nitampa
vishawishi ili tufanye
mapenzi.Wakati mimi
nikifanya naye mapenzi
mmoja ataingia ndani na
kupekua mavazi ya Avi
.Tunachokitafuta ni kadi
anayoitumia kuingilia ofisini
kwake.Tutachukua taarifa
zote za muhimu za kadi hiyo
na tutatengeneza kadi
ambayo itatusaidia kuingia
ndani ya ubalozi wakati wa
operesheni.Zoezi la kuchukua
taarifa za muhimu katika
hiyo kadi likimalizika kadi
itarudishwa na mlango
ugongwe mara mbili haraka
haraka nitajua kazi
imekalika na mimi nitaingia
katika awamu ya pili ambayo
nitamtaka Avi anipeleke
katika ubalozi wa Israel
nikaonane na Edger Kaka na
kujua mahala
alipo.Nitakuwa nimevaa
kamera ndogo ya siri ambayo
itawezesha ninyi kuipata
ramani kamili ya mahala
alipo Edger Kaka.Kama
mpango huu ukifanikiwa
basi tutakuwa tumerahisisha
sana kazi yetu” akasema
Devotha
“Ni mpango mzuri sana
tuombe ufanikiwe.Na kama
ikishindikana una plani
nyingine? Akauliza Gosu
Gosu na Devotha
akatabasamu
“Nina plani zaidi ya mia
moja kichwani msiwe na
wasiwasi” akasema Devotha
“Vizuri sasa.Kwa ajili ya
zoezi hilo tunahitaji kupata
vifaa muhimu vya
kutuwezesha
kulifanikisha.Nina watu
wangu hapa Nairobi ambao
watanisaidia kupata vifaa
mbali mbali
tutakavyovihitaji katika
zoezi hilo na vile vile
usisahau kuwajulisha watu
wa Dar es salaam kama
tumefika salama” akasema
Tino na kutoka akaenda
mapokezi kuomba huduma
ya gari.Hoteli hii ya Sadena
hutoa huduma ya usafiri kwa
wageni wake wanaotaka
kuzunguka sehemu mbali
mbali za jiji la Nairobi.Tino
analifahamu vyema jiji la
Nairobi hivyo hakuhitaji
dereva alipewa gari
akaondoka mwenyewe.
Baada ya Tino
kuondoka,Devotha akaenda
chumbani kwake akachukua
simu ambayo ni maalum kwa
mawasiliano na Mossad pale
anapokuwa nje ya Dar es
salaam akaiwasha na kupiga
namba Fulani akatakiwa
kutaja namba zake za
utambulisho akazitaja na
baada ya sekunde kadhaa
sauti ya mwanamke ikasema
“Karibu sana Devotha
jijini Nairobi.Nikusaidie nini
tafadhali?
“Ninataka kuzungumza
na mkurugenzi Avi
Abramson” akasema Devotha
na kutakiwa kusubiri
sekunde chache
aunganishwe.Zilipita
sekunde hamsini na sauti ya
kiume ikasikika
“Devotha habari
yako?Nimeshangaa
kuambiwa uko
Nairobi.Mbona umekuja bila
kutoa taarifa?
“Dr Yonathan Cohen
hajakujulisha kuhusu ujio
wangu?
“Hapana hajanipa taarifa
zozote kama unakuja Kenya”
“Dr Yonathan
anafahamu kuhusu safari
yangu ya dharura nchini
Kenya na nilitegemea
akujulishe” akasema
Devotha
“Hakijaharibika
kitu.Yawezekana ametingwa
na mambo mengi ndiyo
maana
hajanijulisha.Nikusaidie nini
Devotha?Uko hapa kwa
shughuli gani?
“Kikubwa kilichonileta
hapa ni kuonana nawe Avi”
“Unataka kuonana nami?
“Ndiyo ninataka kuonana
nawe.Nina mazungumzo ya
muhimu mno nawe” akasema
Devotha
“Haikuwezekana
kunipigia simu
tukazungumza hadi uamue
kuja mwenyewe
Nairobi?akauliza Avi
“Ndiyo Avi nimeamua
kuja mwenyewe kuzungumza
nawe ana kwa ana kwa kuwa
suala lenyewe ni kubwa na
hatuwezi kuzungumza
simuni” akasema Devotha
“Umefikia wapi hapa
Nairobi?
“Nimefikia Sadena hotel
chumba 204”
“Unataka tukutane wapi
na saa ngapi?akauliza Avi
“Nifuate hapa katika
chumba changu saa kumi na
moja za jioni kwa sasa
nahitaji kupumzika.Ukifika
mlangoni gonga mara moja
halafu subiri kidogo gonga
tena mara mbili halafu subiri
kidogo kisha gonga mara
tatu nitajua ni wewe”
“Sawa Devotha nitafika
hapo”
“Ahsante” akasema
Devotha na kukata simu
halafu akamfuata Gosu Gosu
“Kila kitu tayari.Avi
atafika hapa saa kumi na
moja za jioni naamini hadi
wakati huo maandalizi yote
yatakuwa yamekamilika”
akasema Devotha
wakaendelea na
mazungumzo mengine
Katika ubalozi wa
Israel,Avi Abramson mkuu
wa Mossad katika ukanda
wa afrika mashariki na kati
alibaki na maswali mengi
kichwani kwake baada ya
kumaliza kuzungumza na
Devotha.Kikubwa
kilichokula akili yake ni kile
kilichompeleka Devotha
Nairobi.Mara akainua mkono
wa simu ya mezani na
kumpigia Dr Yonathan jijini
Dar es salaam.Baada ya
kusalimiana Avi akauliza
“Dr Yonathan
nimekupigia kukujulisha
kwamba nimetoka
kuzungumza na Devotha
muda mfupi uliopita yuko
hapa Nairobi.Ulifahamu
kuhusu safari yake ya
Nairobi? “Utanisamehe
sana kwa kutokujulisha
mapema Avi.Ni kweli ninazo
taarifa zake.Aliondoka hapa
mchana wa leo akiwa na
Fishel na Ehud wakaelekea
Arusha kuna uchunguzi
wanakwenda kuufanya
lakini aliniambia kwamba
akifika Kilimanjaro
atawaacha akina Ehud
waelekee Arusha na yeye
ataunganisha na ndege hadi
Nairobi anataka kuonana
nawe halafu atarejea tena
Arusha kuendelea na
uchunguzi wanaoufanya na
akina Ehud”akasema Dr
Yonathan
“Alikueleza sababu ya
kunifuata Nairobi?akauliza
Avi
“Hapana hakunieleza
sababu yoyote lakini
anaonekana ana jambo
kubwa anataka kuzungumza
nawe.Nahisi ni kuhusiana na
suala la Olivia”
“Vipi kazi niliyowatuma
akina Fishel inakwendaje?
Akauliza Fishel
“Kila kitu kinakwenda
vyema na Devotha atakupa
maelezo ya kutosha kuhusu
suala hilo” akasema Dr
Yonathan
“Ahsante Dr Cohen
naamini nitafahamu mengi
pale nitakapokutana na
Devotha baadae”akasema
Avi na kuagana na Dr
Yonathan.
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 8
Tino alirejea hotelini
akiwa ameongozana na mtu
mwingine.Akamtambulisha
mtu Yule kwa akina Gosu
Gosu kuwa anaitwa Abdallah
ni mtaalamu wa masuala ya
mawasiliano.Mtu Yule
ambaye alionekana si
muongeaji sana alianza
kusaidiana na Tino kufunga
kamera katika chumba cha
Devotha.Walifunga kamera
nne ndani ya chumba kile
ambazo zote ziliunganishwa
na kompyuta iliyokuwemo
katika chumba cha akina
Gosu Gosu.Picha kutoka
chumbani kwa Devotha
zikaanza kuonekana.Wote
wakazihakiki na kufanya
marekebisho kidogo halafu
kila kitu kikakaa
sawa.Katika chumba cha
akina Gosu Gosu kulikuwa
na kompyuta tatu.Moja
iliunganishwa kamera na
nyingine mbili zilikuwa kwa
ajili ya kazi
nyingine.Abdallah baada ya
kumaliza kazi yake akaaga
na kuondoka Tino
akamsindikiza na baada ya
dakika chache akarejea
chumbani
“Abdallah ni mmoja wa
marafiki zangu walioko hapa
jijini Nairobi.Ni mtaalamu
sana wa mambo ya
mawasiliano.Kwa sasa ofisi
imekamilika na kinachofuata
ni kujiunganisha na Dar es
salaam ili nao waweze
kufuatilia kila
kinachoendelea hapa”
akasema Tino na kumpigia
simu Mathew
“Tino habari za Nairobi?
Umekwisha
rejea?Nilijulishwa na
Devotha ulikuwa umetoka
kidogo”
“Ndiyo nilikuwa
nimetoka kidogo nilikwenda
kufuatilia vifaa na tayari
tumekwisha tengeneza ofisi
kilichobaki ni kujiunga nanyi
huko ili muweze kufuatilia
kila kinachoendelea hapa”
akasema Tino kisha akaanza
kufuata maelekezo ya Ruby
na baada ya dakika chache
tayari wakawa wamejiunga
na akina Mathew Dar es
salaam.
“Good job guys.Mmekuwa
na mwanzo mzuri nawatakia
kila la heri pale
mtakapokuwa tayari
mtatujulisha” akasema
Mathew
 
SIRI
MTUNZI: PATRICK CK
PART 1 SEASON 8
EPISODE 9
Saa kumi na moja na
dakika ishirini na nane
mkurugenzi wa Mossad
ukanda wa Afrika Mashariki
Avi Abramson akawasili
Sadena hotel.Ndani ya gari
alikuwa na dereva pamoja na
mlinzi wake mmoja ambao
aliwataka wabaki garini yeye
akashuka na kuelekea ndani
ya hoteli akapanda lifti hadi
ghorofa ya tano akakitafuta
chumba 204 akagonga kama
alivyoelekezwa.Mlango
ukafunguliwa na Devotha
aliyekuwa amevaa gauni
jepesi ambalo liliweza
kuyaonyesha hadi mavaziya
ndani.Kwa sekunde kadhaa
Avi alibaki amesimama
mlangoni akimshangaa
Devotha.Hakuwa ametarajia
kumkuta akiwa katika hali
ile
“Avi karibu ndani ”
akasema Devotha
“Devotha..” akasema Avi
akionekana kuendelea
kumshangaa
“Samahani nilikuwa
ninajiandaa kwenda kuoga
sikutegemea kama ungeweza
kuja mida hii.Umewahi
sana”
“Tulikubaliana tukutane
saa kumi na moja jioni na
nilipotoka kazini nimekuja
moja kwa moja hapa”
akasema Avi
“Karibu naomba
unisubiri nikaoge
kwanza.Utatumia kinywaji
gani? Akauliza Devotha huku
akilitikisa umbo lake na
kuzidi kumpagawisha Avi
“Kitu chochote
ulichonacho humu ndani
nitatumia malaika wangu”
akasema Avi Devotha
akaenda katika kabati
akachukua chupa ya mvinyo
akaiweka mezani na
kumuwekea David katika
glasi.
“Devotha U mrembo
sana” akasema Avi akiwa na
tabasamu pana sana.Devotha
naye akatabasamu
“Devotha hakuna ubaya
wowote tukiendelea
kuzungumza ukiwa katika
mavazi hayo.Ninafurahi sana
kuliona umbo lako
zuri.Mungu amekujalia uzuri
wa kipekee
kabisa.Ninamshukuru na
kumsifu kwa uumbaji huu
uliotukuka” akasema Avi
akiwa katika tabasamu pana
sana
“Ouh Avi” akasema
Devotha akiilegeza sauti
yake na kuwa laini sana
“Kweli kabisa
Devotha.Uzuri wako si wa
kawaida” akasema Avi na
Devotha akabaki amesimama
akitabasamu
“Ahsante sana
Avi.Nisubiri dakika mbili
nikaoge” akasema Devotha
na kuanza kupiga hatua
kuelekea katika mlango wa
chumba cha kulala na mara
tu alipokishika kitasa
akageuka na kumtazama Avi
ambaye bado alikuwa
anamtazama kwa uchu.
“Ungependa kuoga nami
Avi?akauliza huku kidole
kimoja akiwa amekiweka
mdomoni.Avi akatabasamu
na kubabaika
“Ninakutania Avi”
akasema Devotha akitoa
kicheko kidogo
“Hakuna tatizo
Devotha.Kuna mtu yeyote
unayemtegemea hapa kuja
mida hii?akauliza Avi
“Hakuna
ninayemtegemea.Hapa
Nairobi nimekuja kuonana
nawe pekee sina miadi na
mtu mwingine” akasema
Devotha na Avi akasimama
akavua koti
“Basi hakuna tatizo
nitajumuika nawe.Hakuna
mwanaume anayeweza
kukataa ombi la kuoga na
malaika kama wewe”
akasema Avi huku akivua
shati haraka haraka na
kulitupa katika sofa
akaufungua mkanda wa
suruali lakini akasita halafu
akapiga hatua kuelekea
mlangoni akaufunga mlango
kwa funguo halafu akavua
suruali na kubakiwa na nguo
ya ndani
“Niko tayari malaika
wangu” akasema Avi na
kumfuata Devotha
bafuni.Devotha akafungua
mkanda wa ile nguo laini
aliyokuwa ameivaa akaiachia
ikaanguka chini akabaki
amevaa mavazi ya
ndani.Kitendo kile kilileta
vurugu ikulu kwa Avi
ambako kulichachamaa na
kufura kwa hasira.Devotha
huku akitabasamu akamtaka
Avi amsaidie kuifungua
sidiria yake kwa
nyuma.Wakati Avi
akimfungua akayagusisha
makalio yake kwa makusudi
ikulu kwa Avi.
“Kwisha habari
yake.Nikiwaambia viumbe
hawa ni wadhaifu
wanakasirika lakini huo ndio
ukweli angalia macho
yanavyomtoka Avi mwili
wote unamchemka kama
ningekuwa na nia ya
kumuua ningemtoa roho
yake sasa hivi” akawaza
Devotha halafu akamshika
mkono Avi wakaingia bafuni
wakakaa katika beseni
kubwa la kuogea.
“Tunahitaji mvinyo”
akasema Devotha akitaka
kuinuka
“Usiinuke Devotha
nielekeze nikachukue”
akasema Avi na kutoka
ndani ya maji akaenda
kuchukua chupa ya mvinyo
wakaendelea kuoga huku
wakipata mvinyo.Mkono wa
kulia wa Devotha ulikuwa
ukiisugua sugua ikulu ya Avi
ambaye alifumba macho kwa
raha alizohisi.Mara
akakumbuka kitu
“Devotha karibu sana
Nairobi.Nimefurahi kukuona
japo ujio wako umekuwa wa
ghafla sana”
“Hata mimi sikuwa
nimetarajia kama ningekuja
Nairobi lakini imenilazimu
kuja kwa dharura”
“Nini hasa sababu ya
kuja Nairobi?Kuna tatizo
gani?
“Usihofu Avi nitakueleza
kila kitu lakini kwanza tu…”
akasema Devotha huku
akiinuka na Avi akajua
alichokitaka
Devotha.Hakumpa nafasi na
kumaliza sentensi yake
akamkamata sawa sawa na
mtanange ukaanza bafuni.
Tino na Gosu Gosu
walikuwa wakishuhudia kila
kinachoendelea katika
chumba cha Devotha kupitia
kamera wakiwa chumbani
kwao.Akina Mathew Dar es
salaam nao pia walikuwa
wanashuhudia pia
kinachoendelea Nairobi
“Ni muda wa kuingia
kuichukua kadi” akaelekeza
Mathew baada ya kuona
Devotha na Avi wakiwa
wamezama mapenzini.Tino
akatoka ndani ya chumba
chao akatazama pande zote
kulikuwa kimya akaenda
katika mlango akaingiza vitu
Fulani katika kitasa akaanza
kukichokonoa na ndani ya
muda mfupi akafanikiwa
kufungua kitasa
akakinyonga na taratibu
akaingia ndani.Moja kwa
moja akaenda katika mavazi
ya Avi yaliyokuwa sofani
akalichukua koti akaanza
kulipekua na katika mfuko
wa ndani wa koti akaikuta
kadi waliyokuwa
wanaitafuta.
“Hiyo ndiyo kadi
tunayoitafuta” akasema
Ruby ambaye naye alikuwa
akishuhudia kila kitu akiwa
na Mathew Dar es
salaam.Taratibu Tino
akatoka ndani ya kile
chumba cha Devotha
akarejea katika chumba chao
“Good job Tino” akasema
Mathew
Katika kamera bado
mtanange ulikuwa
unaendelea bafuni.Devotha
aliendelea kumpeleka Avi
vilivyo.
Baada ya kuipata ile kadi
kazi ikaanza na usukani
akaushika Ruby akiwa Dar
es salaam.Tino akaanza
kufuata maelekezo aliyopewa
na Ruby akaingiza kadi ile
katika kifaa Fulani
kilichounganishwa na
kompyuta ambacho
kilimuwezesha Ruby kuweza
kupata taarifa alizozihitaji
kutoka katika ile kadi.Baada
ya dakika saba akamtaka
Tino aitoe kadi ile.
“Guys kazi yetu
tumeimaliza nimepata
taarifa zote ninazozihitaji
katika hiyo kadi sasa
mnaweza kuirejesha”
akasema Ruby.Tino
akichukua kadi ile na
kuirejesha katika chumba
cha Devotha,baada ya kutoka
akagonga mlango mara mbili
kama alivyokuwa
ameelekeza Devotha halafu
akaelekea chumbani
kwake.Akiwa bafuni Devotha
alisikia mlango ukigongwa
kama alivyokuwa
ameelekeza mara moja
akajua kazi imekwisha
“Avi
imetosha.Tutaendelea
baadae kama ukitaka”
akasema Devotha
“Devotha mbona
unaniacha kati
kati?Tuendelee malaika
wangu” akasema Avi huku
akitweta
“Usijali Avi tutaendelea
hata baadae lakini kwanza
nataka tuzungumze kile
kilichonileta hapa Nairobi”
akasema Devotha na kutoka
ndani ya lile beseni la kuogea
akajifuta maji.Avi alibaki
anashangaa lakini Devotha
akamtaka atoke ndani ya
maji
“Sawa Devotha
tuzungumze kile
kilichokuleta Kenya.Kuna
tatizo gani? Kwa nini
umetaka kuniona?akauliza
Avi huku akivaa mavazi yake
“Avi usiku wa jana
nilikutana na watu wako
wawili uliowatuma Tanzania
Fishel na Ehud.Walinieleza
kile kilichowaleta Tanzania
kwamba ni kuandaa
operesheni ya kumtafuta
Olivia ambaye ametekwa na
watu wasiojulikana na
mpaka sasa bado vyombo
vyote vinaendelea kumsaka
ikiwemo na idara yangu
lakini bado hatujampata.Ili
niweze kuwasaidia kuandaa
operesheni yao nilitaka
kwanza kufahamu sababu ya
Mossad kumtafuta
Olivia.Fishel na Ehud
walilazimika kunieleza
sababu ya kumtafuta
Olivia.Walinipa siri kubwa
ambayo sikuwa nikiifahamu
kuwa Edger Kaka ambaye
aliwahi kuwa mbunge wa
bunge la jamhuri ya
muungano wa Tanzani
ambaye sisi sote tunaamini
alifariki dunia katika
ajali,yuko hai” akasema
Devotha na sura ya Avi
ikaonyesha mshangao
mkubwa
“Najua hili ni suala la
siri kubwa lakini mimi kama
mtu wenu ambaye
mnanitumia katika masuala
yenu mbali mbali sikupaswa
kuwekwa gizani hadi
ninakuja kufahamu hivi
sasa”akasema Devotha
“Devotha hukupaswa
kufahamu jambo hili na hata
hao waliokueleza wamefanya
makosa makubwa mno
kukupa taarifa hizi za siri”
akasema Avi
“Avi tayari nimekwisha
fahamu siri hii na
usiwalaumu sana watu wako
kwani hawakuwa na namna
nyingine zaidi ya kunieleza
ukweli ili niwasaidie nami
nitawasaidia kumpata Olivia
na ndiyo maana nimekuja
hapa.Kikubwa kilichonileta
kwako ninataka kuonana na
Edger Kaka.Nataka
nizungumze naye” akasema
Devotha
“Hilo haliwezekani
Devotha.Edger yuko mahala
pa siri na wanaoruhusiwa
kuonana naye ni watu
wachache tena maalum
tu.Wewe hauko katika kundi
hilo la watu wanaoweza
kuonana na Edger
Kaka”akasema Avi
“Avi nafahamu Edger
anazo taarifa nyeti sana
mnazozitafuta na ili awape
taarifa hizo lazima mumpate
Olivia.Ili kumpata Olivia
lazima nifanye mahojiano na
Edger Kaka yeye anafahamu
mahala alipo
Olivia,anafahamu
waliomteka”
“Olivia ametekwa na
IS?akauliza Avi
“Tunahisi hivyo ndiyo
maana ninataka kuhojiana
naye.Edger anampenda
Olivia na lazima atanipa
ushirikiano wa kujua mahala
alipo.Avi naomba unipe
dakika tano tu nizungumze
na Edger na ninakuahidi
Olivia atapatikana” akasema
Devotha na Avi akazama
mawazoni huku akiendelea
kumtazama Devotha
“Avi nisingeweza kuja
hapa kama sina uhakika wa
hiki
ninachokuomba.Tafadhali
naomba unipe dakika tano tu
za kuzungumza na Edger
Kaka na ninakuhakikishia
zitakuwa na msaada
mkubwa sana” akasema
Devotha lakini Avi
alionekana kuwa na wasi
wasi na kumuangalia
Devotha kwa macho makali.
“Huyu jamaa tayari
ameonyesha wasiwasi.Kuna
kitu amekihisi kuhusu
Devotha.Guys we need to get
in there fast.Tukichelewa
Devotha atakuwa katika
hatari kubwa! akasema Gosu
Gosu
“Wait ! akasema Mathew
“Mathew Devotha yuko
katika hatar…”
“Ninasema subiri Gosu
Gosu.She knows what she’s
doing” akasema Mathew
“Devotha nataka
uniambie ukweli nani
aliyekupa taarifa za Edger
Kaka?akauliza Avi
“Nimekwambia Avi
taarifa hizo nimezipata
kutoka kwa watu
uliowatuma kwangu
niwasaidie kumpata Olivia
Fishel na Ehud”akajibu
Devotha
“Hapana si kweli.Fishel
na Ehud ni majasusi
wakubwa sana na
wanafahamu umuhimu wa
siri hii ambayo hata watu
wengi ndani ya Mossad
hawaifahamu na majasusi
wetu wamekula kiapo cha
kutokutoa siri zozote.Nataka
uniambie ukweli aliyekupa
taarifa hizi” akasema Avi
Devotha akawa kimya
akimtazama
“Nijibu Devotha,nani
amekupa siri hii? Akauliza
Avi
“Avi najua unawaamini
sana watu wako lakini ni
mimi ndiye niliyewafanya
hadi wakavunja kiapo chao
na kunipa siri hii kwani
sikuwa tayari kuwasaidia
kumpata Olivia kama
wasingenieleza sababu ya
kumtafuta.Kama ni lawama
mimi ndiye ninastahili.Avi
kwa nini usinipeleke mara
moja nikaonana na Edger
Kaka halafu tutakuja
kuendelea pale
tulipoishia?akasema Devotha
na kumfuata Avi akaanza
kuchezea maeneo ya ikulu
“Devotha una uhakika
kwamba Edger anaweza
kuwa na msaada katika
kumtafuta Olivia?akauliza
“Nisingeweza kuja hapa
Nairobi kama nisingekuwa
na uhakika Avi.Naomba
dakika tano tu na nitakuwa
na jibu mahala alipo
Olivia.Edger anafahamu kila
kitu” akasema Devotha
“Lakini Edger amekaa
ndani kwa miaka mitatu
sasa hafahamu chochote
kinachoendelea huko nje na
kikubwa zaidi hafahamu
chochote kuhusu kutekwa
kwa Olivia Themba”
akasema Avi
“Avi niamini
ninachokwambia.Nisingewez
a kupoteza nauli yangu
kutoka Dar es salaam kuja
hapa Nairobi kama
nisingekuwa na uhakika
kwamba Edger anaweza
akasaidia kupatikana kwa
Olivia” akasema Devotha
“Devotha vipi kuhusu
serikali yako,una hakika
hawataweza kugundua kama
tunamtafuta Olivia?
“Usihofu hawataweza
kufahamu chochote” akajibu
Devotha.Avi akamtazama
kwa makini halafu akasema
“Sawa nitakupa dakika
tano tu za kuzungumza naye
lakini hii ni siri kubwa na
ninaomba upate majibu ya
mahala alipo Olivia.Jambo
lingine ni kwamba hii ni siri
kubwa na asifahamu mtu
mwingine jambo
hili.Tukigundua kwamba
umetoa siri
tutakuua.Umenielewa?
akauliza Avi na kusimama
“Ahsante sana Avi”
akasema Devotha
“Tusipoteze muda twende
mara moja” akasema Avi
wakatoka mle ndani.Devotha
alikuwa amevaa suti ya
kijivu na kifuani upande wa
kushoto aliweka ua jekundu
ambalo kati kati yake
kulikuwa na kamera ndogo
ambayo ingewawezesha
wenzake kufuatilia kile
kinachoendelea ndani ya
ubalozi wa Israel
MPENZI MSOMAJI
- DEVOTHA
ATAFANIKIWA
KUONANA NA EDGER
KAKA?
- OPERESHENI YA
KUVAMIA UBALOZI
WA ISRAEL
ITAFINIKIWA?
- NINI HATIMA YA
OLIVIA NA COLETHA?
ENDELEA KUFUATILIA
SIMULIZI HII
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…